02/05/2026
*MINAKI MEDIA*
*JUKWAA JIPYA LA WATU WENYE ULEMAVU KUZINDULIWA*
*Dar es Salaam* – Taasisi ya Mwalimu Blasio Foundation imetangaza kuzindua jukwaa maalum kwa watu wenye ulemavu nchini.
Jukwaa linalenga kufungua fursa za elimu, uchumi na michezo, na kuhakikisha sauti za watu wenye ulemavu zinasikika.
Mkurugenzi wa Taasisi hiyo amesema, “Ulemavu si kikwazo. Jukwaa hili ni daraja la fursa.”
Uzinduzi rasmi unatarajiwa kufanyika hivi karibuni Dar es Salaam.
*Minaki Media*
*Mei 2, 2026*