Gazeti la Championi

Gazeti la Championi Sports Newspaper

RASMI✅️Michail Antonio ameondoka rasmi West Ham United baada ya kumaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu uliopita. Baada...
07/08/2025

RASMI✅️Michail Antonio ameondoka rasmi West Ham United baada ya kumaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu uliopita.

Baada ya miaka 10 ya huduma ya kipekee, klabu imethibitisha kuwa Antonio hatasaini mkataba mpya k**a mchezaji wa kikosi cha kwanza.

West Ham wamemshukuru rasmi kwa huduma yake bora na uaminifu kwa miaka yote aliyehudumu klabuni hapo.

Source: West Ham United

Mateo Kovacić anawindwa vikali na klabu moja kutoka nchini Saudia Arabia klabu ambayo haijaweka wazi.Ripoti zinadai kuwa...
07/08/2025

Mateo Kovacić anawindwa vikali na klabu moja kutoka nchini Saudia Arabia klabu ambayo haijaweka wazi.

Ripoti zinadai kuwa Mateo hajavutiwa na kuhamia Saudia na malengo yake ni kusalia City kwani anaamini yupo kwenye mipango ya kocha Pep Guardiola kuelekea msimu ujao.

[via Fabrizio Romano ]

Polisi wameitwa katika kituo cha mazoezi cha Chelsea Cobham kufuatia kutoweka kwa vifaa vya kamera vyenye thamani ya pau...
07/08/2025

Polisi wameitwa katika kituo cha mazoezi cha Chelsea Cobham kufuatia kutoweka kwa vifaa vya kamera vyenye thamani ya pauni £30,000 (takribani Tsh milioni 100).

Kwa sasa haijajulikana k**a ni wizi wa ndani au nje, lakini uchunguzi umeanza mara moja. Ripoti zaidi itatolea hivi karibuni.

Via. Author

🗣️ Saúl Ñíguez kuhusu João Félix:"Ana kila sifa za kuwa mchezaji wa ajabu, lakini haijalishi una kipaji kiasi gani ila  ...
03/08/2025

🗣️ Saúl Ñíguez kuhusu João Félix:

"Ana kila sifa za kuwa mchezaji wa ajabu, lakini haijalishi una kipaji kiasi gani ila k**a hufanyi kazi kwa bidii, haitasaidia chochote.

Wengi wetu tumewahi kujaribu kumsaidia João, lakini k**a mtu hataki mwenyewe".

Kauli hii inaonekana k**a lawama ya moja kwa moja kwa João Félix kuhusu kutokujituma, licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kiufundi.

[Transfer News Insider ]

Beki wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell anaamini ujio wa Viktor Gyökeres hautoshi kuipa Arsenal makombe hivyo wanapaswa ...
27/07/2025

Beki wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell anaamini ujio wa Viktor Gyökeres hautoshi kuipa Arsenal makombe hivyo wanapaswa kuongeza mshambuliaji mwingine.

“Huwezi kumtegemea mshambuliaji mmoja tu. Akiumia, timu inadorora. Unahitaji washambuliaji wawili mmoja mkuu na mwingine wa daraja la juu k**a msaidizi. Wanaweza kucheza wote au mmoja aanze na mwingine abadili mchezo kutokea benchi.

“Ni vizuri pia kuwa na mshambuliaji mzoefu ambaye anaweza kuingia dakika 20 za mwisho na kubadili matokeo. Huyo wa pili akichaguliwa vizuri, anaweza kuleta ushindi.”

The Sun

🟢JUST!!    Klabu ya Arsenal sasa imewekeza nguvu  kwenye dili la kumsajili  Eberechi Eze kutoka klabu ya   Crystal Palac...
27/07/2025

🟢JUST!!

Klabu ya Arsenal sasa imewekeza nguvu kwenye dili la kumsajili Eberechi Eze kutoka klabu ya Crystal Palace na wapo tayari kutuma ofa rasmi.

Inaripotiwa kuwa Eze ameshakubaliana mkataba wa mpaka 2030 kwa sasa ni suala la vilabu kufikia muafaka kwenye makubaliano ili Eze ahamie The Gunners.

Via.Enoch Arthur

Kipa wa Nigeria, Maduka Okoye, ambaye anachezea klabu ya Udinese ya Serie A, amefungiwa kujihusisha soka kwa muda wa  mi...
23/07/2025

Kipa wa Nigeria, Maduka Okoye, ambaye anachezea klabu ya Udinese ya Serie A, amefungiwa kujihusisha soka kwa muda wa miezi 2 kwa kosa la kujihusisha na ubashiri mchezoni (Betting).

Tukio lilitokea Machi 11, 2024, katika mechi dhidi ya Lazio, ambapo Okoye alifanya juu chini ili apewe kadi ya njano kwa makusudi baada ya kufanya makubaliano na rafiki yake ambaye alikuwa ameweka mkeka.

Rafiki huyo aliweka dau maalum kuhusu kadi hiyo na alishinda zaidi ya euro 120,000 baada ya dau lake kuzidishwa kulingana na odd iloyowekwa na mkeka ukatiki.

[Punch Nigeria | Football Italia]

Klabu ya Arsenal imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya AC Milan na kushinda bao 1-0 Leo mchana.Bao pekee katika mchezo hu...
23/07/2025

Klabu ya Arsenal imecheza mchezo wa kirafiki dhidi ya AC Milan na kushinda bao 1-0 Leo mchana.

Bao pekee katika mchezo huo limefungwa na Bukayo Saka, huu ni mchezo wa kwanza wa Arsenal kwenye maandalizi ya msimu mpya.

Licha ya ushindi huo timu zote mbili zilikubaliana kupiga mikwaju ya penati na Arsenal ikapoteza 5-6.

LUIS DIAZ: “Nilipokuwa mdogo, nilikuwa na jezi ya Argentina, na niliwaambia marafiki zangu kuwa Messi alinipa, na wakani...
23/07/2025

LUIS DIAZ: “Nilipokuwa mdogo, nilikuwa na jezi ya Argentina, na niliwaambia marafiki zangu kuwa Messi alinipa, na wakaniamini. Nilipokutana naye nilimwomba jezi yake na kumweleza kisa. Aliniambia, ‘Niletee jezi hiyo ili niitie sahihi na kugeuza uwongo kuwa ukweli, na sasa utakuwa na wa kweli.’ Pia aliniomba jezi yangu. Nilipompa, alisema kwa mzaha, ‘Waambie marafiki zako kwamba Messi aliomba jezi yako.’ Alikuwa mnyenyekevu sana na mwenye haya. Amekuwa role model wangu siku zote.”

Ni mchezaji gani bora wa Africa msimu huu kati ya Mo Salah, Achraf Hakimi na Omar Marmoush?Wesley Sneijder: "Mohamed Sal...
23/07/2025

Ni mchezaji gani bora wa Africa msimu huu kati ya Mo Salah, Achraf Hakimi na Omar Marmoush?

Wesley Sneijder: "Mohamed Salah. Wachezaji wote watatu wameonyesha kiwango bora msimu huu. Lakini Salah alikuwa na mwendelezo mzuri wa kiwango na kiwango bora zaidi alichoonyesha ndicho kinafanya Salah kuwa mchezaji bora wa Africa msimu huu."

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gazeti la Championi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Gazeti la Championi:

Share