
14/07/2025
Marcus Rashford amekataa ofa ya kusajiliwa ya pesa nyingi kutoka moja ya klabu ya Saudia ikidaiwa moyo wake uko Barcelona.
Mchezaji huyo wa Manchester United anaripotiwa kugomea ofa ya pauni milioni 34 kutoka kwa klabu moja ya Saudi Pro League, Kwa mujibu wa chombo cha habari cha Hispania, Mundo Deportivo.
Rashford, 26, anasemekana kusitasita kuhamia Nou Camp, huku Barca wakiaminika kuwa tayari kumnasa winga huyo iwe kwa mkopo au kwa mkataba wa kudumu.