Gazeti la Championi

Gazeti la Championi Sports Newspaper

‘Siku ya kwanza Pogba kupiga tizi Juve tulicheka sana’KIUNGO wa zamani wa Juventus, Andrea Pirlo amesema kuwa siku ya kw...
02/10/2025

‘Siku ya kwanza Pogba kupiga tizi Juve tulicheka sana’
KIUNGO wa zamani wa Juventus, Andrea Pirlo amesema kuwa siku ya kwanza Paul Pogba kufanya mazoezi na kikosi hicho mwaka 2012 walicheka sana kwa kuwa Manchester United walipoteza mchezaji mzuri.

Andrea Pirlo: “Siku ya kwanza Pogba alipofanya mazoezi nasi pale Juve, sote tulicheka. Je, Manchester United inawezaje kumwacha mchezaji k**a huyo kuondoka bure ili ajiunge nasi?

“Buffon alikuja kwangu akicheka na kusema ‘Wamemwacha aende bure?’”

Ílkay Gündogan amesimulia tukio la kwenye mchezo wao dhidi ya Porto alipokuwa Barcelona:Anasema "Msimu uliopita dhidi ya...
02/10/2025

Ílkay Gündogan amesimulia tukio la kwenye mchezo wao dhidi ya Porto alipokuwa Barcelona:

Anasema "Msimu uliopita dhidi ya Porto, kwenye tukio la Kona ilionekana Kuna mchezaji mmoja hakuwepo uwanjani.

"Baadaye, niligundua Lamine alikuwa amekwenda chooni wakati wa mechi na makocha hawakufanya mabadiliko kwenye nafasi yake.”

Mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or 2025 anatarajiwa kutangazwa leo Jumatatu Septemba 22,2025.Ni katika sherehe zitakazofanyi...
22/09/2025

Mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or 2025 anatarajiwa kutangazwa leo Jumatatu Septemba 22,2025.

Ni katika sherehe zitakazofanyikia kwenye ukumbi wa Théâtre du Chatelet jijini Paris, Ufaransa, ambapo kati ya majina 30 kwenye orodha kwa upande wa Wanaume na wanawake Mshindi atatangazwa.

Miongoni mwa majina yaliyo mstari wa mbele kwa upande wa Wanaume ni Washambuliaji Ousmane Dembélé wa Paris Saint-Germain na Lamine Yamal wa FC Barcelona.

Rúben Amorim: "Sitobadilisha falsafa yangu. K**a INEOS wanataka kubadilisha falsafa hii, basi wanatakiwa kubadilisha na ...
15/09/2025

Rúben Amorim: "Sitobadilisha falsafa yangu. K**a INEOS wanataka kubadilisha falsafa hii, basi wanatakiwa kubadilisha na kocha pia. Tutacheza kwa njia ile ninayoiamini mpaka pale nitakapotaka kubadilisha.

"Project yetu ni ya muda mrefu, kwa hiyo tunatakiwa kurekebisha matatizo yaliyopo..kiukweli, tungefunga angalau magoli mawili leo na tungezuia magoli tuliyoruhusu kufungwa. Mechi iliamuliwa kwa makosa madogo madogo. Manchester City walikuwa na uwezo wa kutumia nafasi walizopata lakini sisi tulishindwa kutumia nafasi zetu.

"Tupo katika hatua ya kitu fulani ili kujaribu kushindana tena dhidi ya hizi timu. Siendi kujilinda mwenyewe, lakini tunatakiwa kufanya vitu bora. Tunatengeneza kitu fulani, lakini bila shaka, tunahitaji kushinda.

"Tunafanya vizuri lakini matokeo hayaonyeshi hili. Nakumbuka klabu yangu ya zamani (Sporting CP), tuliwafunga Manchester City 4-1 bila kuwa na muongozi ule ule au nafasi zile zile k**a tulizozipata leo. Tulikuwa na nafasi nzuri za kufunga magoli.

"K**a ukiangalia magoli, tulikuwa na uwezo wa kuzuia hayo magoli. Huu ndio ulikuwa utofauti mkubwa. Tunatakiwa kufanya vitu bora zaidi, hususani goli la pili. Tulifungwa magoli ambayo tungeweza kuyazuia.

'Sijamuona mchezaji kwenye timu yangu ambaye hajatoa kila kitu uwanjani. Walipambana lakini mengine yote ni juu yangu. Muda mwingine, nachukia pindi ninapoiangalia timu yangu na kuhisi kwamba tunatakiwa kukimbia zaidi, lakini sikuwa na hii hisia leo kwa sababu tulikimbia zaidi."

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Kylian Mbappe msimu huu ana jambo lake kwani kila mechi anayoingia dimbani lazima aweke kam...
14/09/2025

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Kylian Mbappe msimu huu ana jambo lake kwani kila mechi anayoingia dimbani lazima aweke kambani.

Mbappe amefunga mabao manne kwenye michezo minne ya Laliga jambo linaloonesha utayari wake wa kutaka kutetea kiatu cha ufungaji bora.

Mbali na kufunga staa huyo wa Ufaransa amekuwa kwenye kiwango bora akionekana kuimarika katika maeneo mengi kiwanjani na ni miongoni mwa wachezaji wa Real Madrid waliotumika dakika nyingi zaidi msimu huu.

✍️ Spotileo

Kiungo wa Hungary na klabu ya Liverpool FC Dominik Szoboszlai baada ya mchezo kumalizika dhidi ya Portugal 🇵🇹, alimfata ...
11/09/2025

Kiungo wa Hungary na klabu ya Liverpool FC Dominik Szoboszlai baada ya mchezo kumalizika dhidi ya Portugal 🇵🇹, alimfata Cristiano Ronaldo akitaka kubadilishana nae jezi.

Bahati mbaya alikuta kashawahiwa na wengine wanayoitaka zaidi, kwahiyo ikabidi ampatie Cristiano Ronaldo jezi yake ya Hungary halafu Ronaldo akamuahidi mwezi ujao atampa yake baada ya mechi ya marudiano kumalizika nchini Portugal.

Kwahiyo jezi ya Ronaldo kwenye mchezo ujao tayari Iko booked na Dominik Szoboszlai.

BREAKING 🔴: Klabu ya Chelsea FC imeshtakiwa kwa kukiuka kanuni 74 za FA, ikiwemo:Kanuni za Mawakala wa Soka za FA ambazo...
11/09/2025

BREAKING 🔴: Klabu ya Chelsea FC imeshtakiwa kwa kukiuka kanuni 74 za FA, ikiwemo:

Kanuni za Mawakala wa Soka za FA ambazo ni (Kanuni J1 na C2),

Kanuni za FA kuhusu Kufanya Kazi na Wawakilishi (Kanuni A2 na A3),

Kanuni za Uwekezaji wa Watu wa Tatu katika Wachezaji za FA (Kanuni A1 na B3)

Mashtaka hayo yanahusu utovu wa nidhamu ambao unadaiwa kutokea kati ya mwaka 2009 na 2022, na hasa kati ya misimu ya 2010/11 pamoja na 2015/16.

Chelsea wamepewa siku 8 hadi tarehe 19 Septemba 2025 kujibu mashtaka haya.

Source: [ The Sun Football ]

  FT: Fulham 1-1 Man United
24/08/2025



FT: Fulham 1-1 Man United

Aliyekuwa golikipa wa PSG Gigio Donnarumma amekubaliana masharti binafsi na Manchester City.Hata hivyo, dili hili litaka...
24/08/2025

Aliyekuwa golikipa wa PSG Gigio Donnarumma amekubaliana masharti binafsi na Manchester City.

Hata hivyo, dili hili litakamilika endapo Éderson ataondoka msimu huu, ambapo kwa sasa Galatasaray bado wanaendelea na mazungumzo ya kumsajili kipa huyo wa Kibrazil.

Source:Fabrizio

Klabu ya AC Milan imefuta mpango wa kumsajili Victor Boniface mara baada ya kufeli katika zoezi la vipimo vya kukamilish...
24/08/2025

Klabu ya AC Milan imefuta mpango wa kumsajili Victor Boniface mara baada ya kufeli katika zoezi la vipimo vya kukamilisha usajili wake wa kujiunga na AC Milan kutokea Bayer04 Leverkusen.

Kipimo kimebaini mchezaji huyo ana jeraha ambalo litamuweka nje kwa kipindi kirefu kiasi, kwahiyo AC Milan hawapo tayari kununua mchezaji ambaye ana jeraha kwasasa.

Mchezaji huyo raia wa Nigeria mwenye miaka 24, anatarajia kurejea Leverkusen leo kuendelea na majukumu mengine kikosini hapo. 2025

Klabu ya Arsenal imemtambulisha mchezaji wake mpya Eberechi Eze akitokea Crystal Palace.Eze alikuwa mbioni kujiunga na T...
23/08/2025

Klabu ya Arsenal imemtambulisha mchezaji wake mpya Eberechi Eze akitokea Crystal Palace.

Eze alikuwa mbioni kujiunga na Tottenham lakini mambo yalibadilika mwishoni baada ya Arsenal kuonesha uhitaji na Eze akasema ndio kwa Arsenal.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gazeti la Championi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Gazeti la Championi:

Share