Harakati Media

Harakati Media Kwa habari za kitaifa, kimataifa, biashara, afya, kijamii, michezo na brudani...

14/04/2026

DKT, NCHEMBA - Kila mtanzania awe Mdau wa Amani

13/04/2026

KAMISHNA BADRU ATAKA MWENDO MDUNDO.

“Mnapovaa vyeo vya kijeshi, mnapaswa kuonesha dhamira ya dhati ya kutumikia na kulinda Hifadhi ya Ngorongoro na rasilimali zilizopo, ni muhimu kuelewa kwamba vyeo hivi vinakuja na majukumu makubwa ambayo yanahitaji mjitume na kuwajibika kwa kuzingatia maadili, nidhamu, bidii, na uaminifu katika majukumu yenu ili kuhakikisha kwa pamoja tunashirikiana kulinda rasilimali zetu, kuzihifadhi na kukuza utalii ili tutekeleze dira ya taifa ya 2050 kwa vitendo” amesisitiza kamishna Badru.

KUSAMEHEANA NI MSINGI WA TAIFA IMARA 🇹🇿Mchambuzi wa masuala ya siasa na diplomasia, Dkt. Dennis Muchunguzi, ametoa wito ...
13/04/2026

KUSAMEHEANA NI MSINGI WA TAIFA IMARA 🇹🇿

Mchambuzi wa masuala ya siasa na diplomasia, Dkt. Dennis Muchunguzi, ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuwa watulivu na wenye subira wakati wakisubiri ripoti ya Tume huru inayochunguza matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu.

Amesisitiza kuwa hadi sasa hakuna anayejua yaliyomo kwenye ripoti hiyo, hivyo ni muhimu kuepuka upotoshaji na badala yake kuheshimu mchakato unaoendelea kwa kuzingatia hadidu za rejea za Tume hiyo.

Katika kusisitiza mshik**ano wa kitaifa, Muchunguzi ameikumbusha jamii juu ya umuhimu wa falsafa ya 4R — maridhiano, ustahimilivu, mabadiliko na kujenga upya — akieleza kuwa kusameheana na kujisahihisha ni nguzo muhimu za kudumisha amani, umoja na maendeleo ya taifa.

Ameongeza kuwa, licha ya matukio ya Oktoba 29, 2025 kubaki katika historia, ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha hayajirudii kwa kuishi misingi ya upendo, uvumilivu na mshik**ano.

✨ Taifa imara hujengwa na watu wenye moyo wa kusamehe na kujenga upya.

Maendeleo

SANGU ATOA WITO KULINDA TUNU ZA TAIFA 🇹🇿Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, ame...
12/04/2026

SANGU ATOA WITO KULINDA TUNU ZA TAIFA 🇹🇿

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, ametoa rai kwa taasisi na viongozi wa dini nchini kushirikiana na Serikali katika kulinda na kudumisha tunu za Taifa.

Akizungumza mkoani Rukwa, Sangu alisisitiza kuwa amani, upendo, mshik**ano na umoja wa kitaifa ni msingi mkuu wa maendeleo ya kweli ya Tanzania.

Katika harambee ya ujenzi wa Kanisa la Parokia ya Mt. Fransisco wa Asizi, iliyofanyika Aprili 12, 2026, na kumwakilisha Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, zaidi ya Tsh milioni 53 zilichangwa. Waziri Mkuu alichangia Tsh milioni 20 kuonesha umuhimu wa mchango wa taasisi za dini katika maendeleo ya jamii.

Sangu pia alibainisha kuwa Serikali ya Samia Suluhu Hassan inaendelea kushirikisha viongozi wa dini katika mipango mikubwa ya kitaifa ikiwemo Dira ya Maendeleo 2050, akisisitiza kuwa wao ni nguzo muhimu katika kujenga maadili na uzalendo kwa vijana.

Kwa upande wake, Padri Didas Nandi alisema Kanisa litaendelea kuwa kiungo kati ya wananchi na Serikali kwa kuhamasisha amani, mshik**ano na maendeleo endelevu.

Vijana wamehimizwa kuendelea kulinda amani, umoja na mshik**ano nchini k**a msingi wa mafanikio yao binafsi na ya Taifa ...
12/04/2026

Vijana wamehimizwa kuendelea kulinda amani, umoja na mshik**ano nchini k**a msingi wa mafanikio yao binafsi na ya Taifa 🇹🇿

Mjasiriamali wa ufundi wa fenicha, Jerry Mushi, amesema kuwa amani na utulivu ni nguzo muhimu zinazowezesha vijana kutimiza ndoto zao, kukuza uchumi na kuleta ustawi wa jamii. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli.

🗣️ “Hatutaweza kufanya kazi k**a nchi haina utulivu. Tuilinde amani yetu kwa gharama yoyote ili ndoto zetu zitimie,” — amesema.

Aidha, amewahimiza vijana kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo na kujikita katika uzalishaji mali ili kujenga maisha bora na Taifa imara zaidi.

12/04/2026

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA DKT NCHIMBI KONGAMANO LA VIJANA KATIKA KUMBUKIZI YA KUZALIWA BABA WA TAIFA HAYATI MWL. J.K NYERERE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametoa wito kwa vijana kusimama imara na kulinda umoja, kujenga uadilifu, kutumia elimu na ubunifu katika kukuza maendeleo ya nchi ili kuweza kumuenzi Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere kwa vitendo.

Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Kongamano la Vijana katika Kumbukizi ya Miaka 104 ya Kuzaliwaa Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, lililofanyika Ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma, leo tarehe 11 Aprili 2026. Amesema ni muhimu kwa vijana kutambua wajibu wa msingi wa kizazi hiki, kwa kuhakakikisha wanafanya kila jitihada kuimarisha misingi ya kujitegemea kiuchumi, kiakili na kimaamuzi ili kuijenga nchi.

12/04/2026

Ziara ya Elimu Ngorongoro–Lengai 🌍✨

Leo, tarehe 11 Aprili 2026, watumishi wa Benki Kuu ya Tanzania tawi la Arusha walipata fursa ya kipekee kutembelea Makumbusho ya Urithi ya Ngorongoro–Lengai (Urithi Museum) kwa ajili ya kujifunza na kupanua maarifa yao.

Katika ziara hiyo, walijionea historia ya dunia kwa mamilioni ya miaka iliyopita na mabadiliko yake hadi ilivyo sasa. Pia walipata ufahamu wa kina kuhusu maumbile ya kipekee ya ukanda wa Bonde la Ufa pamoja na mwamba wa kale wenye umri wa takribani miaka milioni tatu unaopatikana katika hifadhi ya Jiolojia ya Ngorongoro–Lengai.

Aidha, wageni hao walijifunza na kuthamini urithi wa tamaduni za makabila ya Wahadzabe, Wairaqw, Wadatoga na Wamasai—utajiri mkubwa wa utamaduni wa Tanzania.

Karibu ujionee mwenyewe hazina hii ya kipekee ya elimu, historia na utamaduni!

Jiolojia Utamaduni

MAMA LISHE : AMANI NA UTULIVU NI NGUZO YA MAENDELEO YA TAIFAWazazi na walezi wametakiwa kutambua kuwa amani na utulivu n...
11/04/2026

MAMA LISHE : AMANI NA UTULIVU NI NGUZO YA MAENDELEO YA TAIFA

Wazazi na walezi wametakiwa kutambua kuwa amani na utulivu ni msingi muhimu wa maendeleo ya taifa, huku chimbuko la amani likianzia katika ngazi ya familia.

Akizungumza katika mahojiano maalum, Bi. Yusra Ismail, mama lishe, amesema kuwa malezi bora ya watoto yana mchango mkubwa katika kujenga taifa lenye amani na mshik**ano. Alisisitiza kuwa wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto maadili ya upendo, heshima na utulivu tangu wakiwa wadogo.

“Bila amani ndani ya familia, ni vigumu kufikia maendeleo ya kweli katika jamii,” alisema Bi. Yusra.

Ameongeza kuwa amani huunganisha familia na jamii na kuchochea maendeleo endelevu, hivyo kuwataka wananchi kuitunza na kuiendeleza.
“Ndugu zangu, tuilinde amani yetu. Amani huleta watu pamoja na kuchochea maendeleo ya taifa,” alisisitiza.

Aidha, amebainisha kuwa taifa lenye amani hupata heshima kimataifa na kuimarisha mazingira ya maendeleo na ustawi wa wananchi wake.

Amani ndio Muhimili wa Mafanikio Katika Michezo 🇹🇿Amani na michezo ni vitu vinavyokwenda pamoja Bila utulivu, vipaji hav...
11/04/2026

Amani ndio Muhimili wa Mafanikio Katika Michezo 🇹🇿

Amani na michezo ni vitu vinavyokwenda pamoja Bila utulivu, vipaji haviwezi kung’ara… lakini kwa amani, kila mwanamichezo hupata nafasi ya kuonyesha uwezo wake 💪⚽🏃‍♂️

Mwanariadha mashuhuri Filbert Bayi anasisitiza, Hakuna maendeleo ya michezo bila amani, Michezo hujenga umoja, urafiki na heshima, Ni chanzo cha ajira na mshik**ano wa kimataifa 🌍

Kupitia michezo, watu wa tamaduni tofauti hukutana, hushindana kwa heshima, na kujenga kuaminiana

Hata kimataifa, michezo imekuwa daraja la amani ikiunganisha mataifa yaliyowahi kuwa na migogoro 🤲

Kuendeleza michezo = Kuimarisha amaniKuimarisha amani = Kujenga taifa imara 🇹🇿

🎯 Tuendelee kuwekeza kwa vijana kupitia michezoKwa sababu AMANI + MICHEZO = MAFANIKIO

Vijana SportsForPeace Inspiration

Amani ni Jukumu Letu Sote!Wananchi wamehimizwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kulinda amani na utulivu...
10/04/2026

Amani ni Jukumu Letu Sote!

Wananchi wamehimizwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama ili kulinda amani na utulivu wa nchi 🇹🇿. Ushirikiano huu ni muhimu katika kuzuia uhalifu na kuhakikisha hatua zinachukuliwa mapema.

Akizungumza Tabata Twiga, Dar es Salaam, Jonas Lugayana alisisitiza umuhimu wa kutoa taarifa sahihi kwa wakati, akibainisha kuwa usalama wa taifa unaanza na mwananchi mmoja mmoja.

Pia, wananchi wameaswa kutumia mitandao ya kijamii kwa uwajibikaji—kuepuka kusambaza taarifa za uongo au zenye kuleta taharuki, na badala yake kueneza ujumbe wa umoja na mshik**ano.

Waandishi wa habari nao wamekumbushwa kuzingatia maadili ya taaluma kwa kutoa taarifa zenye kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa amani.

Akikumbusha yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, Lugayana alieleza kuwa vurugu zilisababisha hofu na kuathiri shughuli za kijamii na kiuchumi.

Vijana, hasa Gen Z, wametakiwa kutumia fursa ya amani kujiletea maendeleo kupitia sekta k**a kilimo na ufugaji.

Amani si jambo la kawaida—ni tunu ya kulindwa na kila mmoja wetu kwa maendeleo ya sasa na vizazi vijavyo.

05/04/2026

TANESCO tulipokea mwaliko kupitia Mtandao kutoka kwa Anisa ambaye ni content creator yeye content zake nyingi huonekana akipika nasi bila ajizi tukaitikia na tukaalikika! 🔥🔥🔥

Kutoka keki ya futari hadi pilau la Pasaka, tukapika pamoja kwa umeme na tukamzawadia jiko linalotumia umeme kidogo.

Furaha yake ilisema yote…

Pasaka hii pika kwa umeme!

03/04/2026

EAC YAWEKA MGUU CHINI USHIRIKISHWAJI WA WANAWAKE KATIKA AMANI, ULINZI NA USALAMA

Mkutano wa 13 wa Pamoja wa Mabaraza ya Kisekta ya Mawaziri wa Ushirikiano katika Ulinzi, Amani na Usalama na Baraza la Kisekta la Uratibu wa Sera za Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) umehitimishwa leo jijini Nairobi, Kenya na kuweka bayana vipaumbele vya Jumuiya katika Mabaraza hayo.

Ushirikishwaji wa Wanawake katika masuala ya amani, ulinzi na usalama ni kati ya ajenda zilizojadiliwa na kufanyiwa maamuzi ambapo Jumuiya imepitisha Mpango Mkakati wa kwenda sambamba na wanawake katika ulingo huo. Ajenda hiyo pia ni Utekelezaji wa Azimio la Baraza la Usalama la 1325 (UNSCR 1325) la Umoja wa Mataifa.

EAC pia imejadili kuanzishwa kwa mfumo jumuishi wa tahadhari za mapema katika masuala ya ulinzi, usalama na majanga (EAC Early Warning System). Aidha, katika kuhakikisha Mfumo wa Jumuiya wa uzuiaji na utatuzi wa migogoro unakuwa na tija, mkutano huu umepitisha Mpango Mkakati wa Ushirishwaji wa Asasi zisizo za kiserikali ili kutekeleza msingi wa ujumuishwaji wa wananchi katika shughuli za kikanda.

Mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti, Makamu wa Kwanza wa Waziri Mkuu na Waziri wa Masuala ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Rebecca Kadaga kutoka Jamhuri ya Uganda umesisitiza umuhimu wa kuharakisha utekelezaji wa uamuzi na maelekezo yanayotolewa na Mabaraza hayo na kuratibu vyema sera za mambo ya nje ili kukabiliana na changamoto zinazoibuka za usalama na mabadiliko ya kisiasa duniani.

Ajenda zilizojadiliwa zinaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 huku Tanzania ikiwa tayari imeanza utekelezaji wa ndani wa ajenda hizo ikiwemo kuwa na viongozi mahiri na shupavu wanawake katika sekta za ulinzi na usalama.

Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobass Katambi (Mb), akiambatana na Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Faraji Mnyepe, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia Masuala ya Afrika Mashariki Balozi Said Shaib M***a na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, na Dkt. Maduhu Kazi.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Harakati Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share