Dh4y tv

Dh4y tv subscribe YouTube channel yetu: https://youtube.com/?sub_confirmation=1 all news and updates we will bring to you immediate

25/07/2025

Maboresho ndani ya chama ni lazima kutokana na vitu hivi...

Aliyekuwa miongoni mwa mwagwiji wakubwa wa mieleka na kutamba sana katika tasnia ya WWE Hulk Hogan, amefariki dunia akiw...
24/07/2025

Aliyekuwa miongoni mwa mwagwiji wakubwa wa mieleka na kutamba sana katika tasnia ya WWE Hulk Hogan, amefariki dunia akiwa na miaka 71.

Hogan ambaye jina lake halisi ni Terry Gene Bollea anaripotiwa kufariki alfajiri ya leo nyumbani kwake Clearwater, Florida, nchini Marekani baada ya kupata msh*tuko wa moyo.

Polisi wa Clearwater wamesema alikimbizwa hospitalini lakini alitangazwa kufariki muda mfupi baadaye, WWE shirika kubwa la mieleka limetoa taarifa ya masikitiko makubwa na kumwelezea Hogan k**a sura ya zama za dhahabu katika mieleka aliyekuwa na mchango mkubwa na aliyeacha alama isiyofutika katika tasnia hiyo.

Katika maisha yake ya ulingo, Hogan alipata mataji mengi ya mieleka na pia alijikita katika filamu na vipindi vya televisheni, akiwahamasisha mashabiki wa michezo hii kote duniani.

KICHWA CHA HABARI: Gyokeres Atua London! Arsenal Yakamilisha Dili la Paundi Milioni 73 Kumnasa Mshambuliaji Huyo Hatari!...
24/07/2025

KICHWA CHA HABARI: Gyokeres Atua London! Arsenal Yakamilisha Dili la Paundi Milioni 73 Kumnasa Mshambuliaji Huyo Hatari!

🚨BREAKING Wawakilishi wa Victor Gyokeres tayari wako Uingereza kusaini mkataba na klabu ya Arsenal

Kila kitu kimekamilika Victor Gyokeres yuko tayari kwa Kusafiri kuelekea London kwa ajili ya Vipimo. ✈️

Makubaliano yaliyofikiwa ya pande zote mbili ni ada ya €63.5m nyongeza ya €10m. 🇸🇪 🔴🔐💰

  Viongozi wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) wamesema hawataunga mkono mipango yoyote ya kupanua matumizi ya tek...
23/07/2025

Viongozi wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA) wamesema hawataunga mkono mipango yoyote ya kupanua matumizi ya teknolojia ya VAR ili kujumuisha maamuzi yanayohusu mipira ya kona na utoaji wa kadi za njano za pili.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye vyombo vya shirikisho hilo, UEFA imesisitiza kuwa kuongeza mamlaka ya VAR katika maeneo hayo kutavuruga zaidi mtiririko wa mchezo na kuongeza mijadala isiyoisha kuhusu uamuzi wa waamuzi.

Hatua hii imepokelewa kwa shangwe na mashabiki wengi wa soka waliokuwa wakihofia kuwa VAR inaweza kuwa chanzo cha kuharibu ladha ya mchezo. "Naamini nazungumza kwa niaba ya wengi tunaposema, asante sana kwa uamuzi huu!" aliandika shabiki mmoja kwenye mitandao ya kijamii huku akiongeza emoji za kushangilia.

Kwa sasa, VAR inaruhusiwa kutumika katika maamuzi makuu manne tu: mabao, penalti, kadi nyekundu za moja kwa moja, na makosa ya kumtambua mchezaji aliyehusika.

UEFA inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuweka teknolojia k**a chombo cha kusaidia waamuzi, si kuchukua nafasi yao kabisa.

Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na Sporting Lisbon juu ya kumsajili mshambuliaji Victor Gyokeres kwa ada ya uhamis...
22/07/2025

Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na Sporting Lisbon juu ya kumsajili mshambuliaji Victor Gyokeres kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 63.5 na nyongeza ya milioni 10.

Gyökeres, 27, raia wa Sweden anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano utakaombakisha kwa Washika Mitutu hao mpaka Juni 2030.

  Chuo Kikuu Cha UDOM Chasitisha Udahili Wa Wanafunzi Program Tisa.....Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kimesitisha udahili ...
21/07/2025


Chuo Kikuu Cha UDOM Chasitisha Udahili Wa Wanafunzi Program Tisa.....

Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kimesitisha udahili wa wanafunzi katika programu tisa za shahada ya kwanza za ualimu kwa mwaka wa masomo 2025/2026, kikitaja sababu ya kufanya mashauriano na mamlaka za udhibiti.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika mitandao rasmi ya chuo hicho, programu zilizoathirika ni pamoja na Ualimu wa Sayansi, Saikolojia, Biashara, Sanaa, Mafunzo ya Habari na Mawasiliano, Elimu ya Watu Wazima na Maendeleo ya Jamii, Elimu ya Awali na Ushauri Nasaha, Utawala na Uongozi, pamoja na Mipango ya Sera na Usimamizi.

“Chuo kwa sasa kipo katika mashauriano na mamlaka husika ya udhibiti. Endapo kutatokea mabadiliko au taarifa mpya kuhusu tangazo hili, zitatolewa mara moja,” sehemu ya taarifa hiyo ilisomeka.

Kwa mjibu wa gazeti la "The Citizen", Makamu Mkuu wa Chuo cha Udom, Profesa Lughano Kusiluka amethibitisha kuwepo kwa mashauriano hayo, akisema chuo kiko kwenye majadiliano na wadau wote muhimu na kitaweka wazi taarifa kamili baada ya mchakato kukamilika.

“Hakuna haja ya kuwa na hofu. Tunafanya kazi kwa ukaribu na mdhibiti. Mara baada ya mazungumzo kukamilika, tutatoa mwongozo rasmi,” alisema.

Alipoulizwa kuhusu sababu ya kusitisha programu hizo, Profesa Kusiluka amekataa kueleza kwa undani, akisema ni mapema mno kutoa maelezo na akatoa wito kwa umma kuwa na subira..
https://youtu.be/BU4gkV9pDeA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeutaarifu umma wa Watanzania wote kuwa, kwa sasa kinatumia nembo maalum (QR Code) kuweza ku...
21/07/2025

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeutaarifu umma wa Watanzania wote kuwa, kwa sasa kinatumia nembo maalum (QR Code) kuweza kuhakiki na kuitambua taarifa rasmi inayotolewa na CCM ili kuzuia na kudhibiti uzushi, unaotolewa na watu wenye malengo ovu ya kupotosha na kuzua tafrani

Kwa mujibu wa taarifa ya leo Julai 21, 2025 iliyotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla uhakiki na uthibitisho huo unaweza kufanyika kwa 'ku-scan` nembo hiyo, ambapo mara moja itakupeleka kwenye taarifa halisi iliyopo kwenye vyanzo rasmi vya Chama hicho ikiwa ni pamoja na tovuti na kurasa za mitandao ya kijamii.

CPA, Makala amesema taarifa yoyote ya uongo, ambayo watu wenye malengo ovu wanakuwa wameitengeneza kwa ajili ya kuzua tafrani na kupotosha jamii, msomaji `aki-scan, hawezi kupelekwa, wala hawezi kuikuta, kwenye vyanzo rasmi vya chama, iwe tovuti au kurasa za mitandao ya kijamii ya CCM.

“Mfano mzuri ni taarifa iliyotengenezwa na kuzushwa jana tarehe 20/7/2025, ambayo tuliikanusha, msomaji `aki-scan` atapelekwa kwenye chanzo rasmi cha chama, lakini atakuta kichwa cha habari kisemacho "CCM YATOA RAMBIRAMBI KWA AJALI GARI IWAMBI, MBEYA." Jambo linalodhihirisha ilikuwa taarifa ya uongo.” — imeeleza taarifa hiyo.

“Chama Cha Mapinduzi kimetoa ufafanuzi huu ili kusaidia mtu yeyote akiamua kujiridisha iwapo taarifa anayoisoma imetolewa rasmi na CCM, anaweza kufanya hivyo kwa 'ku-scan` nembo hiyo (QR Code) na kupata uhakika. Lakini pia Chama kinapenda kuwaepusha Watanzania na walaji wote wa habari dhidi ya taarifa au habari za uongo.”.” — imeeleza taarifa hiyo.

21/07/2025

Tazama yaliyotokea leo wafuasi wanaodaiwa kuwa wa chama cha mapinduzi. Mkoa fulani wakifanya uharibifu.
Tukio k**a hili pia limejitokeza juzi huko Mkuranga la madai ya kuibiana kula za udiwani.
Tuilinde aman yetu ni muhimu sana k**a hujalizika na matokeo nenda kwenye ngazi husika kalalamike huko.
https://youtu.be/BU4gkV9pDeA full video tazama kwenye link hiyo

JE ACCOUNT ZA UFUFUO NA UZIMA ZIMEFUNGWA! hadi muda huu sasa (tarehe 20 Julai 2025):Hakuna taarifa rasmi iliyoripotiwa n...
20/07/2025

JE ACCOUNT ZA UFUFUO NA UZIMA ZIMEFUNGWA!
hadi muda huu sasa (tarehe 20 Julai 2025):
Hakuna taarifa rasmi iliyoripotiwa na vyombo vikubwa vya habari kuhusu kufungwa kwa akaunti za benki za kanisa la Askofu Gwajima. Inawezekana ni uvumi au habari ya kutungwa.
Mitandao mingi ya kijamii hueneza habari za uongo kwa nia ya kuvutia watazamaji (clickbait).

Usisambaze habari ambazo hazijathibitishwa rasmi – ni kinyume cha maadili na kunaweza kuleta madhara kwa wengine.

19/07/2025

Mtangazaji Aloyce apiga swali gumu, Mpolepole ajibu kisomi. Tazama hii video. Like comment na subscribe kwenye page yetu na Youtube

Address

Tandale
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dh4y tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dh4y tv:

Share