B24 Newz Tz

B24 Newz Tz B24 Newz ni ukurasa ambao unatumika kukupasha taarifa mbalimbali kuhusu matukio yanayojiri duniani bila upendeleo wowote

09/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA KWANZA

DIWANI LWAKOMEZI AMSHUKRU DKT RWEIKIZA KWA KUMWAMINI MIAKA 10 K**A KATIBU WAKE.

Diwani wa kata ya Kaibanja Mhe,Jasson Lwankomezi amemshukru mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza kwa kumwamini na kufanya nae kazi k**a katibu wake kwa kipindi cha miaka kumi.

Mhe,Lwankomezi ametoa shukrani hizo katika Mkutano wa hadhara wa Dkt Rweikiza wa kuwashukru wananchi waliompigia kura za ushindi uliofanyika kijiji Nyakigando kata Kaibanja

Mbali na kushukru Mhe,Lwankomezi amebainisha kuwa yupo tayari kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Katibu mpya alieaminiwa kwa kipindi hiki.

09/01/2026

šŸŽ„Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza akizungumza na wananchi wa kijiji Nyakigando kata Kaibanja amewashukru kwa kumpigia kura za kishindo huku akiwahakikishia kuwa miradi ya maendeleo iliyopo katika Ilani ya chama itatekelezeka hatua kwa hatua.

Kijiji cha Nyakigando kimekuwa cha pili kwenye vijiji vilivyopiga kura nyingi kwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi CCM katika uchaguzi mkuu wa 2025 na kujinyakulia shilingi milioni nne.

Tofauti na Nyakigando kijiji ambacho kimepata shilingi milioni nne, vijiji vingine vinne navyo vimetimiziwa ahadi ambavyo ni Kijiji Kiziru kata Karabagaine ambacho kimepata shilingi milioni moja,kijiji Kishogo kata Kishogo kimepata shilingi milioni moja,Kijiji Bundaza kimepata shilingi milioni moja na Kijiji Bwizanduru kata Maruku shilingi milioni moja.




08/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA KWANZA

IZIMBYA WAMSHUKRU DKT RWEIKIZA KWA KUTAMBUA MCHANGO WAO KWENYE USHINDI WAKE,YEYE AWAAHIDI MAKUBWA.

Wananchi wa kata ya Izimbya wamemshukru Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza kwa kutambua mchango wao baada ya kalizika kwa uchaguzi mkuu 2025 uliompa kura za kishindo.

Diwani wa kata hiyo Venant Tryphone amesema kuwa,Dkt Rweikiza amefika kuwashukru hivyo watampa tena.

Dkt Rweikiza akizungumza na wananchi hao ,amewashukru kwa kumpigia kura za kishindo huku akiwaahadi kumalizia ujenzi wa kiliniki ya Butulage ndani ya mwaka huu.

Ameongeza kuwa atatoa mchango wa shilingi Milioni tano kwenye ujenzi wa Zahanati ya Izimbya ndani ya miezi michache ijayo.

Dkt Rweikiza akiwa katika ziara yake ya shukrani ametimiza ahadi yake kwa vijiji vinne ambapo ametoa shilingi milioni nne.

Vijiji ambavyo jana vimetimiziwa ahadi ni Kijiji Izimbya kata Izimbya ambacho kimepokea shilingi milioni moja,Kijiji Mishenye kata Butelankuzi shilingi milioni moja,Kijiji Kagondo kata Mikoni shilingi milioni moja na Kijiji Buguruka kata Kanyangereko




08/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA PILI

Ndg,Deocles Byabato amebainisha kuwa wakati wa uchaguzi chama kilizuia wagombea kutoa ahadi kwa hofu ya kushindwa kuzitimiza lakini Dkt Rweikiza aliwahakikishia kuwa ahadi ya kutoa zawadi kwa vijiji imo ndani ya uwezo wake na ataitimiza mara baada ya uchaguzi.

07/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA KWANZA

WANANCHI KIJIJI KAGARAMA WAMSHUKRU DKT RWEIKIZA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Kagarama wamemshukru Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza kwa utekelezaji wa miradi ya Maendeleo

Hata hivyo wananchi hao wamemuomba kushughulikia suala changamoto ya uchakavu wa madarasa katika shule zilizopo katika kata hiyo pamoja na ufungaji wa pamu ya umeme katika kisima cha maji kinachohudumia kijiji Kagarama.

07/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA PILI

DKT RWEIKIZA AENDELEA KUUWASHA MOTO JIMBONI,ZIARA YAKE YAINGIA SIKU YA TATU

Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza amewaahidi wananchi wa kijiji Kagarama kata Ruhunga kuwa changamoto ya uchakavu wa shule atazifanyia kazi kwani hata mwaka jana kuna shule nyingi ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Bukoba zimefanyiwa ukarabati.

Ameongeza kuwa atatoa mchango wa shilingi milioni kumi kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa nyumba ya Mganga katika Zahanati ya Kihumulo.

Hata hivyo Dkt Rweikiza amefanya mikutano katika kata nne na kuwashukru kwa kumchagua kwa kura nyingi katika uchaguzi mkuu 2025 ambapo ametimiza ahadi yake ya kutoa zawadi kwa vijiji vilivyoongoza kwa kupiga kura nyingi kwa wagombea wa CCM ambao ni Rais,Mbunge na Diwani.

Vijiji ambavyo vimepata zawadi ni kijiji cha Kagarama kata Ruhunga ambacho kimepata shilingi milioni moja,Kijiji cha Kyaitoke kata Kyaitoke kimepata shilingi milioni moja,kijiji cha Mugajwale kata Mugajwale shilingi milioni moja na kijiji cha Kyansozi kata Maruku shilingi milioni moja.

WANANCHI KIJIJI KAGARAMA WAMSHUKRU DKT RWEIKIZA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.Baadhi ya wananchi katika kijiji ...
07/01/2026

WANANCHI KIJIJI KAGARAMA WAMSHUKRU DKT RWEIKIZA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO.

Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Kagarama wamemshukru Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza kwa utekelezaji wa miradi ya Maendeleo

Hata hivyo wananchi hao wamemuomba kushughulikia suala changamoto ya uchakavu wa madarasa katika shule zilizopo katika kata hiyo pamoja na ufungaji wa pamu ya umeme katika kisima cha maji kinachohudumia kijiji Kagarama.

Dkt Rweikiza amewaahidi wananchi hao kuwa changamoto hizo atazifanyia kazi kwani hata mwaka jana kuna shule nyingi ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Bukoba zimefanyiwa ukarabati.

Ameongeza kuwa atatoa mchango wa shilingi milioni kumi kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa nyumba ya Mganga katika Zahanati ya Kihumulo.

Hata hivyo Dkt Rweikiza amefanya mikutano katika kata nne na kuwashukru kwa kumchagua kwa kura nyingi katika uchaguzi mkuu 2025 ambapo ametimiza ahadi yake ya kutoa zawadi kwa vijiji vilivyoongoza kwa kupiga kura nyingi kwa wagombea wa CCM ambao ni Rais,Mbunge na Diwani.

Vijiji ambavyo vimepata zawadi ni kijiji cha Kagarama kata Ruhunga ambacho kimepata shilingi milioni moja,Kijiji cha Kyaitoke kata Kyaitoke kimepata shilingi milioni moja,kijiji cha Mugajwale kata Mugajwale shilingi milioni moja na kijiji cha Kyansozi kata Maruku shilingi milioni moja.




07/01/2026

šŸŽ„Wazazi pelekeni watoto shule hata k**a hawana sare-Mhe,Erasto Siima Mkuu wa Wilaya ya Bukoba

07/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA PILI

Mwenyekiti na wananchi wa kijiji Musira kata Katoro wakito kilio chao kwa Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza baada ya mtu mmoja kuzuia na kupinga ujenzi wa mradi wa maji

07/01/2026

šŸŽ„SEHEMU YA KWANZA

SERIKALI HAIWEZI KUTUMIA KODI ZA WANANCHI KUJENGA MRADI ALAFU USIWASAIDIE WANANCHI-DKT JASSON RWEIKIZA

Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza amewaahidi wananchi wa kijiji Musira kata Katoro kufuatilia mgogoro unaokwamisha wananchi kuanza kupata huduma ya maji licha ya kutumia fedha za serikali.

Dkt Rweikiza ametoa ahadi hiyo alikuwa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wa hadhara huku akisikitishwa na kitendo cha serikali kujenga mradi wa maji kwa gharama kubwa alafu usiwasaidie walengwa.

Amebainisha kuwa anakwenda kulishughulikia suala hilo ili wananchi waanze kupata huduma ya maji k**a dhamira ya serikali ilivyo.

Ameongeza kuwa atainunulia tank la maji shule ya Msingi Musira ambayo imefanyiwa ukarabati kwa shilingi milioni 90.

Katika hatua nyingine Dkt Rweikiza akiwa kijiji Kashozi amefafanua kuwa atakarabati chumba cha darasa katika shule ya Msingi Kashozi kilichoharibika.

Katika ziara ya Dkt Rweikiza ambayo imeingia siku ya pili ameendelea kutimiza ahadi yake kwa vijiji ambavyo viliongoza kwa kupiga kura nyingi kwa wagomnea wa CCM ambao ni Rais,Mbunge na Diwani ambapo kwa jana kijiji cha Kyamulaile kimepata shilingi milioni mbili,Kijiji cha Ngarama kata Katoro kimepata shilingi milioni moja,kijiji cha Musira kata Katoro shilingi milioni moja,kijiji cha Kashozi kata Nyakato shilingi milioni moja na kijiji cha Kishanje kata Kishanje shilingi milioni moja.



SERIKALI HAIWEZI KUTUMIA KODI ZA WANANCHI KUJENGA MRADI ALAFU USIWASAIDIE WANANCHI-DKT JASSON RWEIKIZAMbunge wa Jimbo la...
06/01/2026

SERIKALI HAIWEZI KUTUMIA KODI ZA WANANCHI KUJENGA MRADI ALAFU USIWASAIDIE WANANCHI-DKT JASSON RWEIKIZA

Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Dkt Jasson Rweikiza amewaahidi wananchi wa kijiji Musira kata Katoro kufuatilia mgogoro unaokwamisha wananchi kuanza kupata huduma ya maji licha ya kutumia fedha za serikali.

Dkt Rweikiza ametoa ahadi hiyo alikuwa akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mkutano wa hadhara huku akisikitishwa na kitendo cha serikali kujenga mradi wa maji kwa gharama kubwa alafu usiwasaidie walengwa.

Amebainisha kuwa anakwenda kulishughulikia suala hilo ili wananchi waanze kupata huduma ya maji k**a dhamira ya serikali ilivyo.

Ameongeza kuwa atainunulia tank la maji shule ya Msingi Musira ambayo imefanyiwa ukarabati kwa shilingi milioni 90.

Katika hatua nyingine Dkt Rweikiza akiwa kijiji Kashozi amefafanua kuwa atakarabati chumba cha darasa katika shule ya Msingi Kashozi kilichoharibika.

Katika ziara ya Dkt Rweikiza ambayo imeingia siku ya pili ameendelea kutimiza ahadi yake kwa vijiji ambavyo viliongoza kwa kupiga kura nyingi kwa wagomnea wa CCM ambao ni Rais,Mbunge na Diwani ambapo kwa jana kijiji cha Kyamulaile kimepata shilingi milioni mbili,Kijiji cha Ngarama kata Katoro kimepata shilingi milioni moja,kijiji cha Musira kata Katoro shilingi milioni moja,kijiji cha Kashozi kata Nyakato shilingi milioni moja na kijiji cha Kishanje kata Kishanje shilingi milioni moja.



06/01/2026

šŸŽ„Baadhi ya wananchi wameonesha kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Jimbo la Bukoba Vijijiniāœļø

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when B24 Newz Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to B24 Newz Tz:

Share