Spotibez

Spotibez LIKE page yetu ili usipitwe na habari mpya za soka kutoka Ligi mbalimbali barani Ulaya na hapa Bongo.

LIKE page yetu ya Spotibez ili usipitwe na habari mpya za soka kutoka Ligi mbalimbali barani Ulaya na hapa Bongo.

Mashindano makubwa ya soka ya Afrika kuhamishwa kutoka mwanzo wa mwaka hadi miezi ya Juni na Julai, na idadi ya timu zit...
19/07/2017

Mashindano makubwa ya soka ya Afrika kuhamishwa kutoka mwanzo wa mwaka hadi miezi ya Juni na Julai, na idadi ya timu zitaongezeka kutoka 16 hadi 24.

Mapendekezo hayo ya kuhamisha michuano ya mataifa ya Afrika yalifanyika katika mkutano wa siku mbili Jumanne na Jumatano huko Rabat, Morocco, ulioandaliwa na Shirikisho la Soka la Afrika.

Rais mpya wa CAF Ahmad, aliyemng'oa Issa Hayatou mwezi Machi , aliahidi mabadiliko kwenye michuano ya mataifa ya Afrika katika kampeni zake za uchaguzi.
Mabadiliko hayo yakifanyika yatawasaidia kwa kiwango kikubwa wachezaji wanaocheza ligi mbalimbali nje ya bara la Afrika hususa katika bara la ulaya, ambao kwa ratiba ya michuano hiyo sasa wanalazimika kuondoka wakati ligi zikiendelea.Jambo hilo limekuwa likiviathiri vilabu vyao kwa kiasi kikubwa na pia hata timu za taifa pia.

Antonio Conte amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuendelea kuwanoa mabingwa wa EPL, Chelsea. Katika mkataba huo   mpya ...
18/07/2017

Antonio Conte amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuendelea kuwanoa mabingwa wa EPL, Chelsea. Katika mkataba huo mpya Conte atakuwa akipokea £ 9m, na kumfanya kuwa kocha anayelipwa zaidi katika historia ya Chelsea.

Kieran Trippier nae amesaini mkataba mpya wa miaka mitano kuendelea kuitumikia Tottenham.Ndani ya mkataba huo utakaokwisha 2022, Trippier atakuwa akipokea karibu £ 70,000 kwa wiki.Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kuziba pengo la Kyle Walker aliyekwenda Manchester City.

DONE DEAL.Chelsea imethibitisha kumsajili kiungo  Tiemoue Bakayoko kutoka Monaco kwa mkataba wa miaka mitano.Bakayoko al...
15/07/2017

DONE DEAL.
Chelsea imethibitisha kumsajili kiungo Tiemoue Bakayoko kutoka Monaco kwa mkataba wa miaka mitano.
Bakayoko aliyekabidhiwa Jezi namba 14 amesajiliwa kwa dau la ada ya £ 40m. Bakayoko, mwenye umri wa miaka 22, anakuwa mchezaji wa tatu kuelekea Stamford Bridge akitanguliwa na W***y Caballero na Antonio Rudiger. Antonio Conte anajaribu kuimarisha kikosi chake akijiandaa kurudi kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.

DONE DEAL.Barcelona wamekamilisha usajili wa beki wa kulia  raia  wa  ureno kutoka Benfica, Nelson Semedo(23) kwa dau  l...
14/07/2017

DONE DEAL.
Barcelona wamekamilisha usajili wa beki wa kulia raia wa ureno kutoka Benfica, Nelson Semedo(23) kwa dau la £30m.
Nelson Semedo anayetarajiwa kuziba pengo lililoachwa na Dani Alves amesaini mkataba wa miaka mitano.
Je atafanikiwa kuvaa viatu vya Alves?

Picha za matukio mbali mbali yaliyotokea Leo katika ibada ya mwisho ya Bradley Lowery. Ibada hiyo ilifanyika katika kani...
14/07/2017

Picha za matukio mbali mbali yaliyotokea Leo katika ibada ya mwisho ya Bradley Lowery. Ibada hiyo ilifanyika katika kanisa la St Joseph's na kuhudhuriwa na watu mbali mbali akiwepo rafiki mkubwa na Bradley , Jermain Defoe na pia walikuwepo David Moyes , Lee Cattermole , John O'Shea kocha wa Sunderland Robbie Stockdale, manager Simon Grayson, kipa wa Sunderland Vito Mannone, Jimmy Montgomery,Bobby Moncur na Graeme Sharp.

R.I.P BRADLEY LOWERYS

Done deal.Tottenham wamefikia makubaliano na Manchester city juu ya Kyle Andrew Walker. Walker amesaini mkataba wa miaka...
14/07/2017

Done deal.
Tottenham wamefikia makubaliano na Manchester city juu ya
Kyle Andrew Walker. Walker amesaini mkataba wa miaka mitano wa kuitumikia Man City kwa dau la £45M pamoja na nyongeza ya £5M itakayofanya jumla kuwa £50M.

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 04/06/2017Mshambuliaji wa Spain na Chelsea Diego Costa, 28, anataka kuondoka Stamford Br...
04/07/2017

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 04/06/2017

Mshambuliaji wa Spain na Chelsea Diego Costa, 28, anataka kuondoka Stamford Bridge kwa wakati anaotaka yeye, na jambo hilo linachelewesha hatua ya Chelsea kumsajili Romelu Lukaku, 24, kutoka Everton (Chanzo Daily Mirror).

Antonio Conte anataka Chelsea watoe hata paundi milioni 100 kumsajili Romelu Lukaku, k**a Everton wanataka kiasi hicho ili kumuuza (Chanzo The Telegraph).

Mshambuliaji kutoka Argentina Lionel Messi, 30, atasaini mkataba mpya Barcelona mara tu atakaporejea kutoka kwenye fungate yake baadaye mwezi huu (Chanzo Goal).

Paris Saint-Germain wanajiandaa kupanda dau jipya la kumtaka mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, na wamewasiliana na wawakilishi wa mchezaji huyo (Chanzo L’Equipe).

Arsenal wanapanga kutoa paundi milioni 70 kuwasajili viungo wawili kutoka Sporting Lisbon ya Ureno, William Carvahlo, 25, na Gelson Martins, 22 (Chanzo A Bola).

Arsene Wenger atakutana na Alexis Sanchez, 28, na Hector Bellerin, 22, wiki hii kujaribu kuwashawishi wasiondoke Emirates (Chanzo The Sun).

Everton wana uhakika wa kumrejesha Goodison Park Wayne Rooney, 31, kutoka Manchester United msimu huu (Chanzo TalkSport).

West Ham United wanataka kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Javier Hernandez “Chicharito” , 29, kutoka Bayer Leverkusen (Chanzo Telegraph).

Liverpool wanapanga kutoa euro milioni 12 kumsajili kipa wa Sevilla Sergio Rico (Chanzo ABC Sevilla).
Chelsea wameonesha dalili kuwa wapo tayari kutoa paundi milioni 60 kumsajili beki wa kushoto Alex Sandro kutoka Juventus (Chanzo Telegraph).

Barcelona wanaongoza katika mbio za kumsajili beki wa Juventus Leonardo Bonucci. Chelsea wanataka kumsajili beki huyo, lakini yeye angependa kwenda Barcelona (Chanzo Daily Mirror).

Inter Milan wanataka kupanda dau la kumtaka mshambuliaji wa PSG Angel di Maria (Tuttosport).
Kipa wa zamani wa Arsenal Jens Lehmann anatarajia kurejea Emirates k**a mmoja wa makocha wa kikosi cha kwanza (Chanzo Guardian).

Gianluigi Donnarumma amekataa kuhamia Paris-Saint-Germain na amekubali kusaini mkataba mpya kusalia AC Milan (Chanzo Sky Sport Italia).

Kiungo wa zamani wa Manchester United Ravel Morrison, 24, amefanya mazoezi na Birmingham City, akitaka kuhamia klabu hiyo kutoka Lazio (Chanzo Daily Mirror).

Southampton wanataka kukamilisha usajili wa paundi milioni 8.75 wa mshambuliaji Yann Karamoh, 18, ambaye ana mzozo na klabu yake ya Caen ya Ufaransa (Chanzo Sun).

Meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone ameanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu mkataba mpya utakaompeleka hadi mwaka 2020 (Chanzo AS).

Meneja wa Manchester United Jose Mpurinho anakasirishwa na hatua ya klabu hiyo kutosajili wachezaji zaidi ya Victor Lindelof, 22, peke yake mpaka sasa (Chanzo Daily Mirror).

Jose Mourinho anataka mshambuliaji Alvaro Morata, 24, kutoka Real Madrid na kiungo Nemanja Matic, 28, kutoka Chelsea wajiunge na kikosi chake kabla ya Jumapili watakapoanza safari ya Marekani ya mechi za maandalizi (Chanzo Daily Star).

Real Madrid ‘wamekomaa’ na Alvaro Morata hadi Manchester United watakapotoa paundi milioni 79 (Chanzo Marca).

Kiungo kutoka Guinea Naby Keita, 22, anataka kuhamia Liverpool, lakini klabu yake RB Leipzig inataka paundi milioni 70 (Chanzo Daily Mirror).

Crystal Palace wameshindwa kulipa paundi milioni 30 wanazotaka Liverpool kwa ajili ya beki wa kati Mamadou Sakho, 27 (Chanzo Guardian).

Manchester United wanajiandaa kupanda dau kumsajili beki Marc Bartra, 26, kutoka Borussia Dortmund (Chanzo Manchester Evening News).

Newcastle bado hawajafanikiwa kumsajili kipa Pepe Reina, 34, kwa kuwa Napoli hawajapata mtu wa kuziba nafasi yake (Chanzo Newcastle Chronicle).

Leicester City wamefanya mazungumzo ya awali na Sevilla kuhusu usajili wa kiungo Vicente Iborra (Chanzo Sky Sports).

Kipa Wojciech Szczesny amerejea Arsenal kutoka Roma alipokuwa kwa mkopo kwa miaka mwili (Chanzo Instagram)

Tafadhari Gonga “SHARE” ili habari hizi ziwafikie na wadau wengine wapenda soka.

Tetesi nyingine kesho panapo majaaliwa, "LIKE" page yetu ya Spotibez ili habari hizi ziwe zinakufikia moja kwa moja kila zinapotoka, One Love!
https://www.facebook.com/Spotibez

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 03/06/2017Arsenal wako karibuni kutangaza usajili wa winga wa Leicester na Algeria Riyad...
03/07/2017

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 03/06/2017

Arsenal wako karibuni kutangaza usajili wa winga wa Leicester na Algeria Riyad Mahrez, 26. (Chanzo Calciomercato - kwa Kiitaliano)

The Gunners wanaweza kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Ufaransa Alexandre Lacazette, 26, ndani ya masaa 48 yajayo, kwa mujibu wa rais wa Lyon Jean-Michel Aulas. (Chanzo Le Progress kupitia Standard Standard)

Paris St-Germain imetuma maombi kumtaka kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho, huku Liverpool ikitaja euro milioni 100 (paundi milioni 87) k**a thamani ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Chanzo Daily Mirror)

Chelsea inamatumaini ya kufanikiwa katika usajili wa beki wa kushoto wa Brazil Alex Sandro, 26, huku mazungumzo yakipangwa kufanyika na Juventus siku ya leo Jumatatu. (Chanzo Daily Telegraph)

Antonio Conte anakabiliwa na upinzani katika kupata wachezaji wanaosakwa na Chelsea. Manchester City wanamtaka beki wa kati wa Roma Antonio Rudiger, 24. Barcelona wanamtaka beki wa kati wa Juventus Leonardo Bonucci, 30, na Juventus wamejaribu pia kumshawishi Sandro kusaini mkataba mpya. (Chanzo Daily Mirror)

Jurgen Klopp ameiambia Liverpool iongeza kasi katika kumfuatilia kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22, ambaye anatarajiwa kufanya mazungumzo na klabu yake ya Ujerumani wiki hii juu ya mustakabari wake. (Chanzo Times)

Aliyekuwa nahodha wa England na Chelsea John Terry, 36, anatarajiwa kutangazwa k**a mchezaji mpya wa Aston Villa siku ya leo Jumatatu. (Chanzo Daily Telegraph)

Kocha mkuu wa Monaco Leonardo Jardim anamatumaini ya kumbakisha mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 18, lakini amekili kuwa wachezaji wengi huenda wakaondoka msimu huu. (Chanzo RMC kupitia Sky Sports)

Chelsea wametuma maombi kwa Real Madrid kumtaka beki Danilo, 25. (Chanzo Marca kupitia Daily Express)

Beki wa Brazil anayesakwa na Manchester City, Marquinhos, 23, amesaini mkataba mpya wa muda mrefu na Paris St-Germain. (Chanzo Independent)

KALI YA ZILIZOVUMA SIKU YA JUMAPILI

Arsenal wanajiandaa kutoa dau la paundi milioni 125 kwa mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, ili kujaribu kuwapiku Real Madrid. (Chanzo Mirror)

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amemuambia Alexis Sanchez, 28, kuwa hatojiunga na Manchester City msimu huu (Chanzo Mail on Sunday).

Everton wanapanga kutoa paundi milioni 20 kumsajili mshambuliaji wa Arsnenal Olivier Giroud, 30 (Chanzo The Sun).

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola, yuko tayari kumruhusu kipa Joe Hart , 30, kuhamia kwa mahasimu wao Manchester United (Chanzo Sunday Express).

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp huenda akuzuia kumruhusu Daniel Sturridge kuondoka - kwa sababu itakuwa ni gharama kubwa sana kupata mbadala wa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Chanzo Sunday Mirror)

Mshambuliaji Diego Costa, 28, yuko karibuni kujiunga na Atletico Madrid kutoka Chelsea - lakini hataweza kucheza mpaka ifike Januari. (Chanzo AS, kupitia barua pepe Jumapili)

Tafadhari Gonga “SHARE” ili habari hizi ziwafikie na wadau wengine wapenda soka.

Tetesi nyingine kesho panapo majaaliwa, "LIKE" page yetu ya Spotibez ili habari hizi ziwe zinakufikia moja kwa moja kila zinapotoka, One Love!
https://www.facebook.com/Spotibez

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 01/07/2017Chelsea wanalenga kukamilisha uhamisho wa paundi milioni 125 kwa wachezaji wat...
01/07/2017

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 01/07/2017

Chelsea wanalenga kukamilisha uhamisho wa paundi milioni 125 kwa wachezaji watatu, Kiungo wa Monaco mwenye umri wa miaka 22, Tiemoue Bakayoko, beki wa Roma, Antonio Rudiger, 24, na beki wa kushoto wa Juventus Alex Sandro, 26, ambaye huenda akasajiliwa kwa paundi milioni 60. (Chanzo Daily Telegraph)

The Blues wanafikiria pia kumchukua beki wa kushoto wa Porto Alex Telles, 24, Ikiwa watamkosa Sandro, ambaye anasakwa pia na Paris St-Germain. (Chanzo Sun)

Arsenal wanakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Lyon Alexandre Lacazette, 26. Usajili wa Lacazette unatarajiwa kuvunja rekodi ya Arsenal ya paundi milioni 42.4 walizotoa kumsajili Mesut Ozil kutoka Real Madrid mwaka 2013 (Chanzo BBC Sport).

Mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, amewaambia jamaa zake amefanya maamuzi na anataka kujiunga na Manchester United na kwamba swala hilo “limeshapita”. (Chanzo Daily Express)

Neneja wa zamani wa Hispania na Real Madrid Vicente del Bosque ameitaka madrid imbakishe Morata. (Chanzo Daily Express)

Manchester United itajaribu kumsajili golikipa wa City Joe Hart, 30, ikiwa David de Gea, 26, atajiunga na Real Madrid. (Chanzo Sun)

Manchester United bado hawajafanikiwa kumpata Ivan Perisic, 28, na mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia amemwambia wakala wake kulazimisha uhamisho wake kwenda Uingereza (Chanzo Goal).

Leicester City wako tayari kusubiria dau la Ben Gibson wa Middlesbrough lishuke kwa sababu wanaamini bei ya paundi milioni 25 iliyotajwa kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 iko juu sana. (Chanzo Leicester Mercury)

Kiungo wa Chelsea Nathaniel Chalobah, 22, anasita kusaini mkataba mpya mpaka atakapohakikishiwa kuwa atapata namba katika kikosi cha kwanza Stamford Bridge (Chanzo Independent).

West Ham wanataka kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Javier Hernandez, 29, ambaye alijiunga na Bayer Leverkusen mwaka 2015 (Chanzo Bild).

Borussia Dortmund wametangaza kusajili wachezaji wanne Maximilian Philipp, Dan-Axel Zagadou, Omer Toprak na Mahmoud Dahoud.

Bosi wa Manchester United Jose Mourinho amempa kipaumbele kiungo wa Chelsea Nemanja Matic, 28, kwa kuwa kiungo wa Monaco Fabinho, 23, yuko karibuni kujiunga na Paris St-Germain. (Chanzo Manchester Evening News)

Jose Mourinho amekasirishwa na kasi ndogo ya Manchester United ya usajili, kwa kuwa mpaka sasa wamesajili mchezaji mmoja tu mwenye ‘jina’ (Chanzo The Sun)

KALI YA ZILIZOVUMA SIKU YA IJUMAA

Mesut Ozil amelipia tena chumba maalum cha kutazamia mpira (executive box) ndani ya uwanja wa Emirates - akionyesha dalili kuwa ataendelea kubakia Arsenal. (Chanzo The Sun)

Mchezaji wa Chelsea Pedro anasema hajawahi kuona mshambuliaji Diego Costa, 28, akigombana na meneja Antonio Conte – hata hivyo mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania anatarajiwa kuondoka Stamford Bridge. (Chanzo Daily Mirror)

Tafadhari Gonga “SHARE” ili zisambae zaidi na kwa wadau wengine wapenda soka.

Tetesi nyingine kesho panapo majaaliwa, "LIKE" page yetu ya Spotibez ili habari hizi ziwe zinakufikia moja kwa moja kila zinapotoka, One Love!
https://www.facebook.com/Spotibez

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 30/06/2017Liverpool wako tayari kupanda dau kwa kiungo wa RB Leipzig anayetajwa kuwa na ...
30/06/2017

TETESI KUTOKA BARANI ULAYA TAR. 30/06/2017

Liverpool wako tayari kupanda dau kwa kiungo wa RB Leipzig anayetajwa kuwa na thamani ya paundi milioni 70 Naby Keita, 22. (Chanzo Mirror)

Majogoo hao wa Jiji wanamatumaini ya kuwapata kwa pamoja kiungo huyo wa kimataifa wa Guniea na kiungo wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Chanzo Liverpool Echo)

Everton watakamilisha usajili wa mshambuliaji wa Malaga Sandro, 21, wiki ijayo. Everton walifikia dau la mchezaji huyo na tayari alisha pass vipimo vya matibabu lakini klabu ya Hispania haitaki kumruhusu hadi mkataba wake utakapoisha tarehe 3 Julai. (Chanzo Liverpool Echo)

Manchester United haitamuuza Ander Herrera kwa Barcelona msimu huu wa majira ya joto, licha ya ripoti kudai klabu hiyo ya Hispania itazingatia kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ikiwa itashindwa kumpata kiungo mwenzake Marco Verratti, mwenye umri wa miaka 24, kutoka Paris St-Germain. (Chanzo Independent)

Chelsea inataka kumsajili beki wa Roma Kostas Manolas. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alikaribia kuhamia Zenit St Petersburg kwa paundi milioni 26 lakini amesimama ili kuangali nafasi nyingine. (Chanzo London Evening Standard)

Bosi wa Blues Antonio Conte anazidi kupata wasiwasi juu ya utendaji wa klabu katika soko la usajili. (Chanzo Star)

Southampton wanamtaka mshambuliaji wa Manchester City, Kelechi Iheanacho, 20, ambaye anatajwa kuwa na thamani ya paundi milioni 25. (Chanzo Sun)

Kocha wa Watford Marco Silva anataka kumsajili Kieran Gibbs kutoka Arsenal. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 amehusishwa pia na Liverpool. (Chanzo Mirror)
Monaco haitarajii kumuuza Thomas Lemar msimu huu wa majira ya joto na wamekwisha waambia Arsenal na Tottenham, kuwa winga huyo mwenye umri wa miaka 21, hayuko sokoni. (Chanzo Independent)

Mtoto wa Zinedine Zidane, Enzo ameondoka Real Madrid kwenda kujiunga na Alaves. Mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 22, amesaini mkataba wa miaka mitatu baada ya kushindwa kupata nafasi ya uhakika katika timu inayosimamiwa na baba yake. (Chanzo FourFourTwo)

Mtendaji mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis anasema klabu hiyo itafanya usajili zaidi msimu huu. (Chanzo Star)

Mwenyekiti wa West Ham, Daudi Dhahabu amekanusha taarifa za klabu hiyo kumfukuzia mchezaji wa Arsenal Jack Wilshere, mwenye umri wa miaka 25, na anasema klabu hiyo inatafuta washambuliaji wawili wapya wenye uzoefu na Premier League. (Chanzo Talksport)

NA WAKATI HUO HUO…

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amepost picha ya akiwa amebeba watoto wake mapacha. “Nina furaha sana kuweza kubeba wapenzi hawa wapya wawili wa maisha yangu,” aliandika mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32.

Wachezaji wa Barcelona wa zamani na wa sasa wameanza kuwasili nchini Argentina kwa ajili ya harusi ya Lionel Messi. Mshambuliaji huyo wa Barca amewaalika wachezaji k**a Cesc Fabregas, Samuel Eto'o na Carles Puyol. (Chanzo Mail)

Klabu moja nchini Nigeria imewatimua wachezaji 27 kwa kucheza “chini ya matarajio”. (Chanzo The Nation)

KALI YA ZILIZOVUMA SIKU YA ALHAMISI

Real Madrid wametuma maombi kuhusu kumsajili golikipa wa Chelsea Thibaut Courtois, 25, kwa mujibu wa wakala wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji. (Chanzo Sport kupitia Evening Standard)

Mchezaji wa Monaco na Ufaransa Tiemoue Bakayoko, 22, anazidi kukaribia kukamilisha uhamisho wake wa paundi milioni 35 kwenda Chelsea baada ya kufanyiwa vipimo vya afya na mabingwa hao wa Premier League. (Chanzo Daily Mirror)

Tafadhari Gonga “SHARE” ili zisambae zaidi na kwa wadau wengine wapenda soka.

Tetesi nyingine kesho panapo majaaliwa, "LIKE" page yetu ya Spotibez ili habari hizi ziwe zinakufikia moja kwa moja kila zinapotoka, One Love!
https://www.facebook.com/Spotibez

Spotibez inawatakia waislamu wote
26/06/2017

Spotibez inawatakia waislamu wote

Victor Mugubi Wanyama anatimiza miaka 26 Leo.Happy birthday Victor Wanyama
25/06/2017

Victor Mugubi Wanyama anatimiza miaka 26 Leo.
Happy birthday Victor Wanyama

Address

Tanzania Commission For Science And Technology Ali Hassan Mwinyi Road, Kijitonyama COSTECH (Sayansi-building) Ground Floor P. O. Box 4302
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Spotibez posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share