African Adventure

African Adventure Showcasing the timeless heritage of Africa
Culture | Foods | Lifestyles

  Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 26 kujeruhiwa kufuatia ajali kubwa iliyohusisha magari 56 kwenye Barabara ya Kan-...
27/12/2025

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 26 kujeruhiwa kufuatia ajali kubwa iliyohusisha magari 56 kwenye Barabara ya Kan-etsu Expressway mkoani Gunma, kaskazini magharibi mwa Tokyo, mapema leo Disemba 27.
Polisi walisema ajali ilianza baada ya kugongana kwa malori mawili mjini Minakami, hali iliyosababisha foleni ndefu. Moto ulizuka mwishoni mwa foleni na kuteketeza zaidi ya magari kumi, na ulizimwa baada ya saa saba.
Ajali hiyo ilitokea huku kukiwa na onyo la theluji nzito wakati wa likizo za mwisho wa mwaka mpya.
Written by

  Muigizaji Mario Rodriguez amemfungulia   kesi akimtuhumu kwa madai ya unyanyasaji wa kingono, akisema kulikuwa na vite...
27/12/2025

Muigizaji Mario Rodriguez amemfungulia kesi akimtuhumu kwa madai ya unyanyasaji wa kingono, akisema kulikuwa na vitendo visivyotakiwa kwa kipindi cha miaka kadhaa alipofanya kazi naye.
Perry amekanusha madai hayo Wakili wake amesema tuhuma hizo si za kweli na anaziita jaribio la kupata fedha.
, aliyewahi kuonekana kwa nafasi ndogo kwenye Boo! A Madea Halloween (2016), anadai fidia ya dola milioni 77.
Written by

  Baada ya kumtwanga Bondia kutoka nchini Nigeria, Mtanzania Bondia   alionekana akiwa amevalia T-shirt yenye picha ya R...
27/12/2025

Baada ya kumtwanga Bondia kutoka nchini Nigeria, Mtanzania Bondia alionekana akiwa amevalia T-shirt yenye picha ya Rais Samia na nyuma ikiwa na Picha ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lisu huku pembeni yake ikiwa na Nyundo ya Mahakama.

Unadhani kitendo hiki cha Mwakinyo kinabeba picha gani?

  Kwenye Ngoma Mpya ya   na   “LEO” ni Verse ya Nani Imekukosha Zaidi? Written by
26/12/2025

Kwenye Ngoma Mpya ya na “LEO” ni Verse ya Nani Imekukosha Zaidi?

Written by

  Jair Bolsonaro, mwenye umri wa 70, aliyekuwa Rais wa Brazil (2019–2022) na sasa akitumikia kifungo cha miaka 27 kwa ku...
26/12/2025

Jair Bolsonaro, mwenye umri wa 70, aliyekuwa Rais wa Brazil (2019–2022) na sasa akitumikia kifungo cha miaka 27 kwa kupanga njama ya mapinduzi baada ya kushindwa katika uchaguzi wa 2022 dhidi ya Luiz Inácio Lula da Silva, alienda hospitali kwani alikuwa akipata matatizo ya kiafya kutokana na ngiri.
Alipata idhini ya Mahakama Kuu ya Brazil (Supreme Court) kuondoka jela na kwenda Hospitali ya DF Star mjini Brasília kwa ajili ya upasuaji huo.
Written by

  Marekani imefanya shambulizi la anga dhidi ya wanamgambo wa Islamic State (ISIS) katika jimbo la Sokoto, kaskazini-mag...
26/12/2025

Marekani imefanya shambulizi la anga dhidi ya wanamgambo wa Islamic State (ISIS) katika jimbo la Sokoto, kaskazini-magharibi mwa Nigeria, kufuatia ombi la serikali ya Nigeria.
Rais Donald Trump amesema mashambulizi hayo yalilenga wanamgambo waliodaiwa kushambulia Wakristo. Jeshi la Marekani barani Afrika (AFRICOM) limesema wanamgambo wengi wameuawa katika operesheni iliyofanywa kwa ushirikiano na Nigeria.
Serikali ya Nigeria imeeleza kuwa makundi yenye silaha yanawalenga Waislamu na Wakristo, ikipinga madai ya mateso ya Wakristo pekee, lakini ikathibitisha kuendelea kushirikiana na Marekani katika masuala ya kiusalama.
Written by

  Mmetoboa?
24/12/2025

Mmetoboa?

24/12/2025

Zuchu amjibu shabiki kuhusu Marioo, Harmonize anakinukisha usiku huu, Whozu aibuka na mastaa kibao

  Mahakama Wilaya ya Momba mkoani Songwe imemhukumu Yaledi Sinkala (38) kifungo cha miaka 40 jela baada ya kupatikana na...
24/12/2025

Mahakama Wilaya ya Momba mkoani Songwe imemhukumu Yaledi Sinkala (38) kifungo cha miaka 40 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka ndugu yake wa damu mwenye changamoto ya afya ya akili. Sinkala alikamatwa na kufikishwa mahakamani Novemba 18, 2025.
Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi mkoani Songwe linawasaka watu watatu kwa tuhuma za kumshambulia na kumjeruhi Linus Boniface, mkazi wa Chang’ombe, Wilaya ya Songwe, wakidaiwa kufanya hivyo kwa madai ya kuiba bata. Taarifa hizo zimetolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, RPC Augustino Senga.
Written by

Address

Ngorongoro
Dar Es Salaam
1411

Telephone

+255767420674

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when African Adventure posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to African Adventure:

Share