Serengeti Media Centre

Serengeti Media Centre Official Serengeti Media Centre page | Follow Now | Media Activities and Production

Habari na Makala mbalimbali za Picha,Video na Sauti katika Nyanja za Kijamii,Siasa,Kiuchumi,Afya,Michezo na Burudani,Elimu na Matangazo.

Butiama - MaraMkuu wa Wilaya ya Butiama Thecla Mkuchika akiangalia bidhaa za wajasiriamali waliotumia fursa ya maadhimis...
13/09/2025

Butiama - Mara

Mkuu wa Wilaya ya Butiama Thecla Mkuchika akiangalia bidhaa za wajasiriamali waliotumia fursa ya maadhimisho ya Siku ya Mara (Mara Day) kuonesha bidhaa zao leo Septemba 13,2025.

Maadhimisho hayo ya 14 yenye kaulimbiu isemayo "Hifadhi Mto Mara Linda Uhai" uadhimishwa kila mwaka kwa awamu moja nchini Tanzania na Kenya ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa nchi hizo mbili kutokana na mwingiliano wa wageni wa mataifa hayo.

HONGERA Mr & Mrs Mbalageti | Serengeti Media Centre Picture.
13/09/2025

HONGERA Mr & Mrs Mbalageti | Serengeti Media Centre Picture.

Na Serengeti Media Centre - Serengeti.Mgombea ubunge Jimbo la Serengeti kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mary Daniel ak...
12/09/2025

Na Serengeti Media Centre - Serengeti.

Mgombea ubunge Jimbo la Serengeti kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Mary Daniel akiongozwa na M/Kiti wa UVCCM Taifa Ali Kawaida amefungua kampeni huku akitaja vipaumbele vyake muhimu ambavyo ni barabara na uwanja wa ndege.

Mary akiongea na wananchi wa Serengeti waliojiTokeza kumsikililiza leo Septemba 12,2025 amesema akipata ridhaa ya miaka 5 atahakikisha anasemea kero ya ukosefu wa miundombinu ya barabara hususani za lami zinazounganisha jimbo hilo na wilaya nyingine.

"Tunatambua wazi bado miundombinu ipo chini kwa kushirikiana na serikali nitasukuma mambo hayo ili njia ya Tarime - Mugumu visa Nyamongo na Natta-Sanzatte ziweze kukamilika" amesema Mary

Mary amesema "kuhusu uwanja wa ndege tayari hatua za awali zimeanza na atakapopata ridhaa ni kwenda kukamilisha hatua zinazofuata kwa kuwa jambo lenyewe limeshawekwa kwenye ilani ya 2025-2030".

Ali Kawaida M/kiti wa UVCCM Taifa ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wananchi kujitokeza kupiga kura Oktoba 29.

Zaidi Tazama YouTube Yetu

TERRE ET FAUNE NA KRC WASAIDIA MIZINGA YA NYUKI JAMII KWA AJILI YA KUKUZA UCHUMI NA KUDHIBITI TEMBO WAVAMIZI.NA SMC -LON...
12/09/2025

TERRE ET FAUNE NA KRC WASAIDIA MIZINGA YA NYUKI JAMII KWA AJILI YA KUKUZA UCHUMI NA KUDHIBITI TEMBO WAVAMIZI.

NA SMC -LONGIDO.

Shirika lisilo la kiserikali la Kilimanjaro Resource Centre (KRC) kwa ufadhili wa shirika laTerre et Faune la nchini Uswisi wametoa mizinga 100 kwa vikundi vya ufugaji nyuki katika kijiji cha Lerang’wa Tarafa ya Enduimet wilayani Longido, mkoa Arusha, ili kukabiliana uharibifu wa mashamba na vifo vinavyosababishwa na Tembo.

Kijiji hicho ni miongoni mwa vijiji vitano, vinavyopakana na hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro, hifadhi ya Amboseli ya nchini Kenya na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Enduimet na vinatekeleza Mradi wa kuhifadhi na kurejesha ustawi wa maeneo ya mifumo ikolojia yaliyo hatarini kuathiriwa Kilimanjaro Magharibi na Longido (REPROTECT).

Akizungumza katika zoezi la kukabidhi Mizinga hiyo, lililotanguliwa na mafunzo ya wanavikundi na viongozi wa vijiji hivyo, Mkurugenzi wa shirika la KRC, Dr Gerubin Liberath Msaki alisema mizinga hiyo itatumika k**a uzio katika mashamba lakini pia k**a sehemu ya mradi wa wananchi kujiingiza fedha baada ya kuuza asali na mazao yake.

Dr Msaki alisema kupitia mradi huo wanatarajia pia kujenga uwezo wa jamii juu ya Shughuli za Ujasiriamali za uzalishaji Mali, ufugaji wa kisasa, kushirikiana jamii ili kukuza shughuli za utalii wa kitamaduni-ikolojia katika vijijini hivyo vitano na watu zaidi ya 15,000 wanatarajiwa kunufaika.

“Katika mradi huu pia tunatarajia kupanda miti, na kuendeleza jamii katika ufugaji wa nyuki wa kibiashara,kuwa na kilimo cha kisasa ili kuboresha maisha ya jamii katika Tarafa ya Enduimet”alisema

Dr. Msaki alisema vijiji vingine vilivyopo katika mradi huo ni Kitendeni, Irkaswa, Kamwanga na Olmolog ambapo Katika mwaka wa Kwanza mradi umeanza katika Kijiji cha lerangwa k**a sehemu ya majaribio ya mradi (Pilot project) na baadae kuendelea katika vijiji vingine vya mradi katika mwaka wa pili na wa tatu.

Akikabidhi mizinga hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Longido, Jacob Lyimo aliwataka wananchi wa vijiji vitano, ambao wapo katika mradi huo, kutumia mradi huo kuboresha maisha yao lakini pia kukabiliana na migogoro baina yao na wanyamapori.

Lyimo ambaye ni mkuu wa kitengo cha Maliasili na Mazingira katika halmashauri ya Longido, alisema halmashauri k**a mshirika wa mradi huo, itatoa ushirikiano kuhakikisha unaleta manufaa kwa jamii lakini pia kufatilia hatua zote za utekelezwaji wa mradi huo.

“Leo tunakabidhi mizinga hii mtumie vizuri katika ufugaji wa nyuki kisasa kwani licha ya kudhibiti tembo lakini pia mnapata asali ambayo mtauza na kupata fedha za kuboresha maisha yenu”alisema.

Akitoa mafunzo ya kukabiliana na Wanyama wakali hasa Tembo, kwa wananchi wa vijiji hivyo Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori nchini (TAWIRI) Revocatus Meney alisema matumizi ya mizinga ya nyuki ndio njia bora zaidi kudhibiti uvamizi wa Tembo.

Alisema adui mkubwa wa Tembo ni nyuki, hivyo wananchi hao sasa watakuwa na uwezo wa kufuga nyuki na kupata asali lakini pia kudhibiti makundi ya tembo kuvamia mashamba yao na nyumba zao.

Hata hivyo, alieleza tabia mbali mbali za tembo kabla ya kufanya uvamizi na kusababisha uharibifu na vifo na kuwataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinaadamu ikiwepo kilimo na ujenzi katika maeneo ya mapito ya Wanyama hao.

“Hivi sasa kuna wilaya 91 Tanzania zinakabiliwa na migogoro ya Tembo lakini chanzo kikubwa ni wananchi kuongeza shughuli za kibinaadamu katika maeneo ya asili ya wanyamapori, lakini pia kulima mazao yanayovutia wanyamapori pembezoni mwa hifadhi, mapori ya akiba na hifadhi ya jamii za wanyamapori” alisema.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Lerang’wa Isaya Lembuya na mmoja wa wanakindi cha ufugaji, Obedi Mollel walishukuru wafadhili wa mradi huo, ambao unakwenda kuboresha maisha yao na kuahidi kusimamia mradi huo ili ulete mafanikio.

Lembuya alisema serikali ya Kijiji chake, itatoa ushirikiano kwa mradi huo, kwani kwa miaka mingi wamekuwa na migogoro ya Tembo kuvamia mashamba yao na kufanya uharibifu mkubwa lakini sasa wanaamini Suluhu inapatikana.

Mradi huu wa miaka mitatu unafadhiliwa na shirika la Terre et Faune kutoka nchini Uswisi na kutekelezwa na KRC na unashirikisha TAWIRI ,TFS na halmashauri ya Longido.

MAMBO MAZURI YANAPIKWA YATAKUJIA HIVI KARIBUNI Endelea Kuwa Nasi
11/09/2025

MAMBO MAZURI YANAPIKWA YATAKUJIA HIVI KARIBUNI

Endelea Kuwa Nasi

04/09/2025

04/09/2025

K**a ulikosa kushiriki msimu wa sita wa mbio ya Anti-Poaching Run inayofanyika hifadhini katika mapori ya akiba ya Ikoro...
04/09/2025

K**a ulikosa kushiriki msimu wa sita wa mbio ya Anti-Poaching Run inayofanyika hifadhini katika mapori ya akiba ya Ikorongo na Grumeti eneo la Fort - Ikoma, hivi ndivyo ilivyokuwa.

Jiandae kwa msimu ujao mwaka kesho

Maliasili Yazidi Kung’ara Mwanza, Yaitandika timu ya Netball ya Katiba na Sheria 38–8 SHIMIWI 2025 Na John Bera – Mwanza...
03/09/2025

Maliasili Yazidi Kung’ara Mwanza, Yaitandika timu ya Netball ya Katiba na Sheria 38–8 SHIMIWI 2025

Na John Bera – Mwanza

Timu ya netiboli ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeendelea kuonesha ubabe kwenye Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) kwa kuichapa kwa kishindo Wizara ya Katiba na Sheria kwa mabao 38–8, katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza.

Timu hiyo ilianza kwa kasi na kutawala mchezo kutoka mwanzo hadi dakika ya mwisho, ikionesha uelewano mzuri, umakini mkubwa na nidhamu ya hali ya juu uwanjani. Ushindi huo umeiweka Maliasili katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye hatua za mtoano.

Kocha wa timu hiyo, Bi. Rehema Kapela, amesema ushindi huo si wa bahati nasibu, bali ni matokeo ya maandalizi ya muda mrefu na ari ya wachezaji wake waliodhamiria kuweka historia mwaka huu.

“Tumekuwa tukifanya mazoezi kwa bidii na leo tumeona matokeo. Wachezaji wameonesha kujituma, umoja na uthabiti. Tuna malengo makubwa, na huu ni mwanzo mzuri kwetu,” alisema Kocha Kapela.

Mchezaji wa timu hiyo, Julia Kepha, ambaye aling’ara katika mchezo huo kwa kucheza kwa kiwango cha juu katika safu ya ulinzi, amesema walijiandaa kisaikolojia na kimwili kuhakikisha wanapata ushindi.

“Ushindi huu umetokana na kazi ya pamoja. Kila mmoja alitimiza majukumu yake. Tuliingia uwanjani tukiwa na malengo, na tulihakikisha tunayatimiza kwa vitendo,” alisema Julia.

Kwa upande wake, Kaimu Mratibu wa Timu ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. George Rwezaura, amechukua fursa hiyo kuipongeza timu kwa ushindi huo wa kuvutia na kuahidi kuwa wataendelea kushirikiana na benchi la ufundi kuhakikisha timu inasonga mbele zaidi.

Wadau wa maendeleo Deogratias Chacha na Dk. Rhimo Nyansaho wameshirikiana na wakazi wa Kata ya Ring'wani kuchanga zaidi ...
02/09/2025

Wadau wa maendeleo Deogratias Chacha na Dk. Rhimo Nyansaho wameshirikiana na wakazi wa Kata ya Ring'wani kuchanga zaidi ya Sh 19Mil kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi Kenyana.

Deogratias na Dk Rhimo wamechangia bati 400 wananchi na wadau wengine wakichangia bati 100 sambamba na kiasi cha zaidi ya Mil 19, Saruji mifuko 255, Tofari 15000 na Misumari 30Kg.

Wakazi hao wamechukua hatua hiyo kutokana na jengo la sasa kuchakaa na kuiomba serikali kuwaongezea askari ikiwemo wa k**e katika eneo hilo.

Zaidi Tazama YouTube Yetu Hapa
>>>>> https://www.youtube.com/watch?v=6UL0GqMs4u8

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Serengeti Media Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Serengeti Media Centre:

Share