Serengeti Media Centre

Serengeti Media Centre Official Serengeti Media Centre page | Follow Now | Media Activities and Production

Habari na Makala mbalimbali za Picha,Video na Sauti katika Nyanja za Kijamii,Siasa,Kiuchumi,Afya,Michezo na Burudani,Elimu na Matangazo.

Hongera Rosca | Serengeti Media Centre Picture
30/11/2025

Hongera Rosca | Serengeti Media Centre Picture

Na Serengeti Media Centre - MugumuTaasisi ya Nyansaho Foundation yenye makazi yake Mugumu Wilayani Serengeti Mkoa wa Mar...
28/11/2025

Na Serengeti Media Centre - Mugumu

Taasisi ya Nyansaho Foundation yenye makazi yake Mugumu Wilayani Serengeti Mkoa wa Mara imetumia kiasi cha Shilingi 41,100,000 kufadhili masomo ya wanafunzi 116 wa vyuo mbalimbali;- 47 wa Shahada, 59 Stashahada, 9 Astashahada na mmoja wa Kidato cha sita.

Masiko Mirama Katibu Tawala wa Wilaya ya Serengeti akikabidhi hundi kwa wanafunzi hao leo Novemba 28,2025 amewataka kusoma kwa bidii na kutambua thamani ya elimu katika maisha.

"Wengi wetu tumetoka katika familia za kawaida kupitia msaada huu utumike k**a chachu ya kufanya vizuri kitaaluma, mtakapofanya vyema mtamheshimisha Nyansaho kwa moyo wake wa majitoleo" amesema Masiko.

Modesta Mwema Mratibu wa Taasisi hiyo Kanda ya Ziwa akiongea kwa niaba ya Dk. Rhimo Nyansaho amesema "tunathamini jitihada kubwa za serikali katika kuboresha elimu nasi tumefanya kwa uwezo wetu tunatarajia mtafanya vizuri zaidi".

Modesta amesema wanafunzi hao watapewa pesa kwa mfumo wa kidijitali wa benki na kuwataka wazazi kuwaendeleza watoto wa k**e ili kuimarisha uwiano wa ufaulu kati yao na wa kiume katika masomo ya elimu ya juu.

Magari Igai mmoja wa wanufaika wa ufadhili huo amesema "namshukuru Nyansaho kwa kiasi kikubwa kanibeba nimepata pa kuanzia katika masomo yangu ya udakitari naahidi kufanya vyema".

27/11/2025
26/11/2025

Modesta Mwema Mratibu wa Taasisi ya Nyansaho Foundation Kanda ya Ziwa akipokea zawadi ya kofia maalumu kutoka kwa Clara ...
26/11/2025

Modesta Mwema Mratibu wa Taasisi ya Nyansaho Foundation Kanda ya Ziwa akipokea zawadi ya kofia maalumu kutoka kwa Clara Benard ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake katika kurasa zetu za Serengeti Media na Antomnatv Online.

Utaratibu huu utawafikia wadau wengine ikiwa ni sehemu ya kutambua jitihada zenu kwa kutembelea Chaneli yetu ya YouTube na kurasa zetu kila siku.

ELIAS KIGOCHA AUTENDEA HAKI MSAADA ALIOPATA KUTOKA NYANSAHO FOUNDATION Na Serengeti Media Centre - Mugumu.Elias Kigocha ...
25/11/2025

ELIAS KIGOCHA AUTENDEA HAKI MSAADA ALIOPATA KUTOKA NYANSAHO FOUNDATION

Na Serengeti Media Centre - Mugumu.

Elias Kigocha (Mangomba) Mkazi wa Mugumu Wilayani Serengeti Mkoani Mara ameithibitishia Taasisi ya Nyansaho Foundation kuwa hawakukosea kumpa msaada wa mashine ya umwagiliaji baada ya kuongeza uzalishaji kwenye shamba lake la matunda na mbogamboga.

Akikumbuka Oktoba 15,2025 alipopewa mashine hiyo yenye thamani ya Shilingi laki 6.5 Elias amesema imekuwa msaada mkubwa katika matumizi ya muda tofauti na awali alipokuwa akitumia ndoo kumwagilia mazao.

"Bustani hii ya Ekari 3 nilianzisha nikiwa pekee yangu, kutokana na ukubwa wa eneo na uzito wa kazi ilinilazimu kutafta wenzangu wawili huku tukitumia vifaa duni kufanya kazi" amesema Elias na kuongeza,

"Niliposikia habari za Nyansaho Foundation nilituma ombi langu waliponikubalia kunipa mashine niliwashirikisha wenzangu baada ya kuipata tukachagua kulima zao la Nyanya kwa kiwango kikubwa" amesema Elias,

Goodluck Mosha Mtaalamu wa kuendesha mashine hiyo amesema "awal ilituchukua muda wa saa 3 kumwagilizia tulishindwa kumudu shamba lote lakini sasa kwa saa moja tunaweza kumaliza eneo lote" amesema Goodluck.

Goodluck ameishukuru Nyansaho Foundation na kuwaomba kuendelea kuwashika mkono vijana wengine k**a walivyowafanyia kwao.

Modesta Mwema Mratibu wa Taasisi ya Nyansaho Foundation Kanda ya Ziwa amesema "nikupongeze Elias kwa namna ulivyoonesha uthubutu, kitendo hiki kinaipa taasisi nguvu ya kuwashika vijana, hii iwe chachu na kwa wengine" amesema Modesta.

Zaidi Tazama Youtube ya Serengeti Media Centre

Na Serengeti Media Centre Wadau wadau wa kurasa za Serengeti Media na Antomatv Online Sylvester Bija (Picha ya Kwanza Ku...
25/11/2025

Na Serengeti Media Centre

Wadau wadau wa kurasa za Serengeti Media na Antomatv Online Sylvester Bija (Picha ya Kwanza Kushoto) na Jumanne J4 wakipokea zawadi ya kofia maalumu kutoka kwa Clara Bernad ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wao.

Utaratibu huu utawafikia wadau wengine ikiwa ni sehemu ya kutambua jitihada zenu kwa kutembelea Chaneli yetu ya YouTube na kurasa zetu kila siku.

25/11/2025

24/11/2025

Na Serengeti Media CentreMdau wa muda mrefu wa kurasa za Serengeti Media Centre na Antomatv Online Babu Chile akitunikiw...
24/11/2025

Na Serengeti Media Centre

Mdau wa muda mrefu wa kurasa za Serengeti Media Centre na Antomatv Online Babu Chile akitunikiwa zawadi ya kofia maalumu na Clara Bernad kutokana na mchango wake katika kurasa hizo.

Utaratibu huu utawafikia wadau wengine ikiwa ni sehemu ya kutambua jitihada zenu kwa kutembelea Chaneli yetu ya YouTube na kurasa zetu kila siku.

Na Serengeti Media Centre.Ukimshangaa mbuni asiyepaa utamstaajabu ngwini, samaki asiyepaa mwenye uwezo wa kuogelea.Kawai...
24/11/2025

Na Serengeti Media Centre.

Ukimshangaa mbuni asiyepaa utamstaajabu ngwini, samaki asiyepaa mwenye uwezo wa kuogelea.

Kawaida ukimkuta mbuni ndani ya hifadhini anavyovimba akiwa amejichanganya na pundamilia na nyumbu wakitafuta malisho unaweza kujisahaulisha kuwa huyu ni ndege.

Watu wengi wamekuwa wakimuona mbuni k**a ndege wa kipekee na wa tofauti basi k**a unaisoma hii makala utaweza kuujua utofauti.

1. Muonekano

Mbuni ndiyo ndege mrefu, mkubwa na mzito zaidi duniani, anaweza kuwa na wastani wa kilo 50 k**a mbuzi lakini pia ana uzito sawa na kuku 20 na ndiyo sababu kuu kwanini mbuni hana uwezo wa kupaa.

Sasa utajiuliza, kwanini kuku ni mwepesi lakini hapai juu angani k**a kunguru? Naomba huo uwe mjadala wa siku nyingine.

2. Mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

Mbuni ana matumbo matatu na ni ndege pekee ambaye haja zake ndogo na kubwa hutoka tofauti, yani hazijichanganyi.

Mbuni ni mnyama mrefu kuliko wanyama wengine duniani. Ana vidole viwili tu vya miguuni.

3. Mbio na kasi

Mbuni ana uwezo wa kukimbia kwa kasi ya kilomita 70 kwa saa, kasi kubwa kuliko ndege yoyote yule. Hivyo safari yake ya Dar kwenda Bagamoyo inaweza kumchukua saa moja tu. Hatua yake moja ni sawa na hatua tano za binadamu.

4. Vidole

Tofauti na ndege wengine wenye vidole vinne ambapo vitatu huangalia mbele na kimoja nyuma, mbuni ana vidole viwili kwenye mguu wake mmoja, vyote vinaangalia mbele.

5. Kujihami

Kwenye hatari, silaha kubwa ya mbuni huwa ni mateke yake, hurusha mateke ya mbele yenye uwezo wa kuua wanyama wakali k**a fisi, chui hadi simba.

6. Tabia za misimu

Katika msimu wa masika mbuni hukaa peke yake au na mpenzi wake na katika msimu wa kiangazi, mbuni hukaa katika makundi ya mbuni wengi hadi 50 na hupenda kujichanganya na makundi ya swala na pundamilia.

Wakati mwingine ndege hao hujichanganya na wanyama wengine k**a pundamilia na swala.

7. Mapenzi yao ni ya kipekee

Katika hichi kitengo, mbuni ana utaratibu wa kipekee sana. Kwanza jogoo la mbuni hupiga mabawa yake k**a anataka kupaa ikiwa ni ishara kwamba anatafuta mwenza.

Akishapata mwenza, wanaanza kutafuta malisho na anahakikisha anampeleka sehemu ambapo hakuna wanyama wengine na wanaendelea kutafuta malisho hapo huku wakizoeana tabia.

Baadaye jogoo la mbuni huanza tena kupiga mabawa kwa nguvu zaidi na kuzunguka akiwa ameyashusha na akiwa anadonoa udongo, ambapo jike la mbuni likishaona hizo ishara basi huchuchumaa na kurusu kupandwa.

8. Yai la mbuni ni bonge la yai

Mbuni zaidi ya mmoja huweza kutaga mayai yao kwenye tundu moja na kila mbuni ana uwezo wa kutofautisha mayai yake na ya mbuni wengine.

Yai la mbuni lina uzito wa zaidi ya kilo 1 na ukubwa sawa na n**i. Yai la mbuni bwana, unaweza kulikaangia chipsi sahani k**a tano hivi.

9. Jike na dume wote huatamia mayai

Jike la mbuni ana rangi ya kijivu na huatamia mayai mchana kwa sababu rangi yake hufanana na mchanga hivyo ni ngumu kuonekana, huku jogoo la mbuni lenye rangi nyeusi hutamia mayai usiku kwa sababu ni ngumu kuonekana gizani. Mayai ya mbuni huchukua siku 35 mpaka 45 kutotolewa.

10. Jicho kubwa sana

Jicho la mbuni linalingana na yai la kuku. Jicho la mbuni ni kubwa kuliko ubungo wake. Hivyo ana uwezo mkubwa sana wa kuona mbali na kwenye giza.

Mbuni ni mnyama asiyeonekana kirahisi kwa sababu idadi yao imepungua sana hivyo kuwaona ni mpaka mbugani, kwenye hifadhi.

Ukitaka kumuona mbuni basi tufunge safari moja kwa moja mpaka kwenye hifadhi za taifa za Serengeti, Mikumi, Ruaha au Katavi. Pia ukitembelea maeneo ya uhifadhi k**a Selous na Ngorongoro utaweza pia kujionea mbuni.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Serengeti Media Centre posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Serengeti Media Centre:

Share