23/07/2025
Watu 125 wanatuhumiwa kuhusika na makosa mbalimbali wakiwemo wenye makosa ya kutumia dawa za kulevya na kusambaza,pamoja na wizi wa mali mbalimbali katika kipindi cha kuanzia mwezi juni 27,2025 hadi julai 22,2025 .
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akizungumza na vyombo vya habari leo Julai 23, 2025, amesema watuhumiwa hao walik**atwa wakati jeshi hilo likifanya operesheni iliyolenga kubaini na kuzuia uhalifu.
Amesema katika operesheni hizo, dawa za kulevya zilizok**atwa ni pamoja na bhangi gramu 2,261 mirungi kilo 29 pamoja na pombe ya moshi lita 142. bajaji moja ,runinga saba mbati 16, nondo vipande 17 vitanda vinne pikipiki mbili, redio nane na risasi moja ya silaha ndogo.
Aidha amesema jumla ya kesi 25 zimepata mafanikio ambapo kesi mbili za kulawiti wash*takiwa wawili wamehukumiwa kifungocha maisha jela, kesi mbili za kubaka, ambapo wash*takiwa wawili wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.