ExtraPower Tv

ExtraPower Tv Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ExtraPower Tv, Digital creator, kinondoni, Dar es Salaam.

Nyota wa kimataifa wa Senegal, Sadio Mané, amemstusha ulimwengu wa soka kwa kutangaza kuwa mchezo wa fainali ya AFCON ut...
16/01/2026

Nyota wa kimataifa wa Senegal, Sadio Mané, amemstusha ulimwengu wa soka kwa kutangaza kuwa mchezo wa fainali ya AFCON utakaopigwa Jumapili dhidi ya wenyeji Morocco utakuwa wa mwisho kwake kushiriki mashindano hayo ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Mané ameweka wazi kuwa anatumaini kuiongoza Senegal kuibuka na ushindi na kutwaa taji hilo kwa mara nyingine ili kulipeleka jijini Dakar k**a zawadi ya mwisho kwa taifa lake kabla ya kuhitimisha safari yake kwenye mashindano hayo makubwa barani Afrika. Uamuzi huu wa Mané, mwenye umri wa miaka 33, unakuja baada ya kuisaidia timu yake kutinga fainali hiyo kwa kufunga bao la ushindi dhidi ya Misri katika nusu fainali.

​Kauli hiyo ya Mané imewagusa mashabiki wengi wa soka barani Afrika, ikizingatiwa mchango wake mkubwa kwa Taifa la Senegal na soka la Afrika kwa ujumla tangu alipoanza kushiriki michuano hiyo mwaka 2015.

Fainali hiyo itakayopigwa katika uwanja wa Prince Moulay Abdellah jijini Rabat sasa itakuwa ya kihistoria kwa Mané, huku mashabiki wa "Simba wa Teranga" wakitarajia kumuona akimaliza safari yake ya AFCON kwa furaha na ubingwa wa pili katika historia ya nchi hiyo.

Kustaafu huku kwa Mané kwenye AFCON kunamaanisha hatashiriki michuano ijayo ya mwaka 2027 itakayofanyika katika nchi za Afrika Mashariki (Kenya, Uganda, na Tanzania).

Imedhaminiwa na

Depu anawazidi nini Dube na Mzize? Huu hapa uchambuzi wa kina kutoka kwa Hans rafael
16/01/2026

Depu anawazidi nini Dube na Mzize? Huu hapa uchambuzi wa kina kutoka kwa Hans rafael

Mchambuzi wa soka Hans rafael amechambua kwa kina kuhusu uwezo wa Depu na utofauti wake na duba na mzinze

Klub ya Simba ipo hatua za mwisho kukamilisha usajli wa beki wa kati wa zamani wa Stellenbosch  Osmail Olivier Touré (28...
15/01/2026

Klub ya Simba ipo hatua za mwisho kukamilisha usajli wa beki wa kati wa zamani wa Stellenbosch Osmail Olivier Touré (28)

Simba wamemuandalia Toure mkataba wa miaka mitatu na tayari beki inasemekana yuko Tanzania kwa ajili ya kukamilisha taratibu za usajili. Hili ni pendekezo la kocha mkuu.

Imedhaminiwa na

Klub ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji raia wa Angola Laurindo Dilson Maria Aurélio (Depu) alizaliwa tarehe 8 January...
15/01/2026

Klub ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji raia wa Angola Laurindo Dilson Maria Aurélio (Depu) alizaliwa tarehe 8 January 2000. Huu ni usajili mwengine baada ya kumtambulisha Okelo.

Yanga wanaendelea kuboresha kikosi cha kwa kushusha vyuma vipya.

Imedhaminiwa na

15/01/2026

Kwa mujibu wa mchambuzi wa Soka jemedari Saidi, amesema "k**a hakutakuwa na umoja ndani ya klub ya simba ni ngumu sana kutoboa" maneno haya yanakuja baada ya mambo mengi ndani ya klub hiyo kuonekana hayaendi sawa. Mpaka sasa klub hiyo haijakamilisha usajili wa mcbezaji hata mmoja na ikisemekana kocha akiwakataa wachezaji wengi waliopo ndani ya klub hiyo.

Kutazama video kamili ingia kwenye ukurasa wetu wa youtube wa extrapower tv
Link https://youtu.be/-zxLC_Pk2nQ

Imedhaminiwa na Madodi istore

Ligi Kuu ya NBC inarejea Ijumaa ya Januari 16, 2026, Dodoma JIJI FC dhidi ya Singida BS.Jan 17, Azam FC Vs Coastal Union...
14/01/2026

Ligi Kuu ya NBC inarejea Ijumaa ya Januari 16, 2026, Dodoma JIJI FC dhidi ya Singida BS.
Jan 17, Azam FC Vs Coastal Union.
Jan 18, Simba SC Vs Mtibwa Sugar.
Jan 19, Yanga SC Vs Mashujaa FC.
Jan 20, Azam FC Vs Fountain Gate.
Jan 20, Singida BS Vs JKT Tanzania.

Powerd by

Rapa Country Wizzy anasema anajua watu wengi watamsifia siku ambayo hatakuwepo duniani kutokana na kipaji chake, uwezo w...
14/01/2026

Rapa Country Wizzy anasema anajua watu wengi watamsifia siku ambayo hatakuwepo duniani kutokana na kipaji chake, uwezo wake na aliyoyafanya kimuziki.

Kwenye post yake mpya ya Instagram Country Wizzy ameandika 👇

"Najua mtanisifia sana nikifa, basi kabla sija-dead wakubwa statement official video iko Youtube".

"Halafu niwaambie tu nina mzuka mwaka huu, Promota piga simu na ukipiga simu hakikisha wasanii wako wote waimbe, mi mwaka huu wote nataka niimbe Dakika 40/ 1 hour Hapo yani".

Pia Country Wizzy ameongeza kueleza kuwa ata-performe Live Band kila show ili kuweka heshima na thamani ipande hataki kuimba Dk 10 wala 30 ni saa 1 stejini.


Powerd by

Dili la uhamisho wa winga wa Teungueth FC anayetumia mguu wa kushoto Libasse Gueye (22) kutua katika klub ya Simba limek...
14/01/2026

Dili la uhamisho wa winga wa Teungueth FC anayetumia mguu wa kushoto Libasse Gueye (22) kutua katika klub ya Simba limekufa hii ni baada ya ofa ya $173,000 ilitumwa na simba kwenda Teunguueth fc kukataliwa.

Simba wameamua kuachana na dili hilo kwani hawana mpango wa kuongeza kiwango cha pesa kwa ajili ya kumpata nyota huyo.

powerd by

12/01/2026

K**a unaijua combinagion nyengine kali zaidi ya hii, itaje kwenye comment.


10/01/2026

K**a unatafuta movie ya kuangalia leo angalia hili tambala linaitwa Companion. Ni moja ya movie nzuri sana.

Klub ya TRA United imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Dennis Nkane kutoka Yanga. Nkane amejiunga na TRA baada y...
05/01/2026

Klub ya TRA United imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Dennis Nkane kutoka Yanga. Nkane amejiunga na TRA baada ya kukaa benchi kwa muda mrefu katika klub ya Yanga na sasa amea aende sehemu ambayo atacheza.


Address

Kinondoni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ExtraPower Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share