ExtraPower Tv

ExtraPower Tv Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ExtraPower Tv, Digital creator, kinondoni, Dar es Salaam.

Klub ya Azam fc imeanza kuboresha kikosi chake kwa kuwaongezea mikataba wachezaji wake Muhimu. Baada ya wiki iliyopita k...
08/06/2026

Klub ya Azam fc imeanza kuboresha kikosi chake kwa kuwaongezea mikataba wachezaji wake Muhimu. Baada ya wiki iliyopita kumuongezea mktaba kocha Ibenge, tayari wiki hii wamemsainisha mkataba mpya winga wa Idi seleman nado.

Nado ameongeza mkataba wa miaka miwili kuitumikia klub ya Azam fc, mkataba wa nado ulikuwa unaisha mwishoni mwa mwezi huu wa sita.
Kwa mujibu wa Taarifa za ndani ya Azam fc tayari CEO wa azam fc yupo mezani na wachezaji kadhaa ikiwemo fei toto katika mkakati wa kumuongezea mkataba mwengine.

Klub ya Azam fc inapambana kumbakisha kocha wake mkuu Florent Ibenge. Taarifa za ndani zinasema kocha Ibenge aliandika b...
29/05/2026

Klub ya Azam fc inapambana kumbakisha kocha wake mkuu Florent Ibenge. Taarifa za ndani zinasema kocha Ibenge aliandika barua ya kuomba kazi timu ya Taifa ya mali kutokana na kuchelewa kwa mazungumzo ya mkataba mpya.

Ibenge alisaini mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza miaka miwili endapo haya yakifanyika.
1. Akiingia makundi ✅
2. Akipata nafasi ya kucheza shirikisho✅
3. Kubeba kombe la FA (yupo nusu fainali)

Mazungumzo yakuongeza mkataba yalichelewa kuanza hivyo k**a management ya Ibenge ilazimika kuanza mchakato wa kumtafutia kazi mpya kocha ibenge ukaanza.
Ila mpaka kufikia jana usiku mazungumzo ya ya CEO wa Azam fc na kocha l ibenge yamefikia pazuri na ibenge amesema yupo tayari kubaki endapo mambo aliyoomba yakikubaliwa na kutimizwa.

Klub ya Yanga sc imetozwa faini ya shillingi millioni 30 kwa kosa la kutotumia vyumba vya kubadilishia nguo katika uwanj...
11/05/2026

Klub ya Yanga sc imetozwa faini ya shillingi millioni 30 kwa kosa la kutotumia vyumba vya kubadilishia nguo katika uwanja Mej isamuyo kwenye mchezo wa dabi zidi ya simba. Kamati ya saa 72 imetoa adhabu hiyo kwa kuzingatia kanuni ya 27:7 ya ligi kuu kuhusu vyombo vya maamuzi.

Pia k**ati higo ya saa 72 imempiga faini ya millioni moja meneja wa klub ya Yanga water harreson

24/04/2026

Eti striker anakosa gani hapo?

Iddi selemani Nado ataingia kwenye vitabu vya historia kuwa moja ya wachezaji ambao wamezigomea Simba na Yanga. Klub ya ...
24/04/2026

Iddi selemani Nado ataingia kwenye vitabu vya historia kuwa moja ya wachezaji ambao wamezigomea Simba na Yanga. Klub ya Simba iliweka kitita cha kiasi million 500 za kitanzania k**a pesa za usajili kwa lengo la kunasa sign ya Nado. Lakini Nado amekataa kiasi hicho cha fedha na akiwajibu wawakilishi wa Simba kuwa pesa hiyo anaweza kupewa na klub yake aliyopo na pia yupo na Amani na furaha.

Taarifa zinasema Nado ameipa nafasi ya kwanza klub yake aliyopo na mazungumzo yao yanaendelea vizuri, hivyo hana mpango wa kuondoka sehemu ambayo anathaminiwa. Ikumbukwe mkataba wa nado na azam fc unaisha mwisho mwa msimu huu.

Happy easter watu wa Mungu
05/04/2026

Happy easter watu wa Mungu

29/03/2026

Rais Paul Kagame alikutana na jamii ya Waislamu nchini Rwanda katika ukumbi wa BK Arena mjini Kigali.
​Katika mkutano huo wa maswali na majibu, mshiriki mmoja alimueleza Rais kuhusu changamoto ya kuondolewa kwa adhana ya alfajiri (asubuhi mapema) kwenye vipaza sauti, jambo ambalo liliathiri uwezo wa waumini kujua muda wa sala hiyo.

Tazama video kamili kwenye youtube channel ya extrapower tv.
https://youtu.be/tT0l_B7K6yI

Mambo yanazidi kupamba moto! Klabu ya Inter Miami imeanza rasmi mazungumzo ya kumsajili kiungo fundi, Casemiro, k**a mch...
29/03/2026

Mambo yanazidi kupamba moto! Klabu ya Inter Miami imeanza rasmi mazungumzo ya kumsajili kiungo fundi, Casemiro, k**a mchezaji huru msimu huu wa kiangazi! 🇺🇸🔥
​Hali ya mazungumzo ikoje mpaka sasa?
​✅ Mazungumzo yanaendelea na ofa ya kwanza imeshawasilishwa.
​🧠 Uamuzi wa mwisho upo mikononi mwa Casemiro, ambaye kwa sasa anaonekana kuvutiwa zaidi na kujiunga na ligi ya MLS.
​🐐 Casemiro anavutiwa na mradi wa Inter Miami, fursa ya kucheza tena na Lionel Messi pamoja na mastaa wengine, maisha ya jiji la Miami, na malengo makubwa ya klabu hiyo.
​Ushindani ni mkubwa!
Licha ya Inter Miami kupewa nafasi, Casemiro pia anawaniwa na klabu nyingine kutoka:
​🇪🇺 Ulaya
​🇸🇦 Saudi Arabia
​Je, unamuona Casemiro akitua Miami kuungana na Messi, Suarez, na Busquets? ✍️👇

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kuingia kambini tarehe 22 mwezi huu.
18/03/2026

Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kuingia kambini tarehe 22 mwezi huu.

Morocco imetangazwa kuwa mshindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 kufuatia uamuzi wa Bodi ya Rufaa ya Shirikisho la So...
18/03/2026

Morocco imetangazwa kuwa mshindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 kufuatia uamuzi wa Bodi ya Rufaa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Senegal, ambayo awali ilishinda mchezo wa fainali kwa 1-0 Januari 18, 2026 na kuwa mabingwa.

Senegal imevuliwa taji hilo kutokana na tukio lilotokea dakika 17 ya mchezo wakati wachezaji wa Senegal walipopinga penalti iliyotolewa kwa mwenyeji Morocco.

Bodi ya Rufaa ya CAF ilipokea maombi ya rufaa ya Shirikisho la Soka la Kifalme la Morocco (FRMF) na jana

Bodi ya Rufaa ya CAF iliamua kwamba kwa kutumia Kifungu cha 84 cha Kanuni za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), Timu ya Taifa ya Senegal imetangazwa kupoteza Mechi ya Mwisho ya Kombe la Mataifa ya Afrika la TotalEnergies (AFCON) Morocco 2025 ("Mechi"), Na sasa bingwa wa mashindano hayo atakuwa Morocco huku matokeo ya Mechi hiyo sasa yakirekodiwa Morocco 3-O senegal.

Mashindano hayo yaliandaliwa nchini Morocco, huku fainali ikifanyika Rabat.

Address

Kinondoni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ExtraPower Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share