ExtraPower Tv

ExtraPower Tv Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ExtraPower Tv, Digital creator, kinondoni, Dar es Salaam.

Ikiwa leo ni Alhamisi ngoja tukurudishe mpaka mwaka 1993, kwenye moja ya tukio ambalo liliwaacha wengi na mshangao. Kati...
09/10/2025

Ikiwa leo ni Alhamisi ngoja tukurudishe mpaka mwaka 1993, kwenye moja ya tukio ambalo liliwaacha wengi na mshangao. Katika kile kinachoweza kuwa moja ya uhalifu wa kipuuzi zaidi wa ubinafsi uliowahi kurekodiwa, mwanamume mmoja nchini India aliripotiwa kusababisha mafuriko yaliyofunika ekari 14,000-yote ili mke wake asiweze kurudi nyumbani na kukatiza sherehe yake ya kunywa pombe.

Kulingana na ripoti za eneo hilo, mwanamume huyo alikuwa akiandaa sherehe ya siku tatu nyumbani kwake na marafiki huku mkewe akiwa mbali na familia yake. Aliposikia kwamba anarudi mapema kuliko ilivyotarajiwa, aliogopa - sio kwa upendo, lakini kwa sababu hakutaka sherehe hiyo iishe.

Katika uamuzi wa kushangaza, alifungua lango la karibu la bwawa, akitoa mamilioni ya galoni za maji katika eneo jirani.
Mafuriko yaliyotokea yaliharibu mazao, yakawafanya mamia ya wanavijiji kuyahama makazi yao, na kusababisha hasara ya mamilioni. Wenye mamlaka walifuatilia udukuzi huo kwake kwa haraka kupitia uchunguzi na mashahidi wa ndani.

Alipoulizwa, inasemekana alikiri ukweli: "Nilitaka tu kuendelea na karamu." Hali yake ya kustaajabisha iligeuza msukumo wa ubinafsi kuwa janga la kimazingira na kibinadamu - ukumbusho mchungu wa jinsi vitendo vya kutojali vinaweza kubadilika zaidi ya raha ya kibinafsi.

Kocha mkuu wa JKT amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi September baada ya kumshinda kocha Gamondi, huku Goli kipa wa Ya...
05/10/2025

Kocha mkuu wa JKT amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi September baada ya kumshinda kocha Gamondi, huku Goli kipa wa Yanga Diarra akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi september.


Mtoto wa gwiji wa soka la Ufaransa Zinédine Zidane, Luca Zidane ambaye ni golikipa ameitwa kwa mara ya kwanza kwenye Tim...
04/10/2025

Mtoto wa gwiji wa soka la Ufaransa Zinédine Zidane, Luca Zidane ambaye ni golikipa ameitwa kwa mara ya kwanza kwenye Timu ya Taifa ya Algeria kwa ajili ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia 2026.

Luca ambaye aliwahi kuichezea Ufaransa kwenye ngazi za Vijana, alikamilisha mchakato wa kubadili uraia wa soka mwezi uliopita baada ya kuidhinishwa rasmi na FIFA na kuwa anastahili kuichezea Algeria kupitia urithi wa Baba yake kwani wazazi wa Zinédine Zidane walihamia Ufaransa wakitokea eneo la Kabylie Algeria.

Kocha Vladimir Petkovic amemjumuisha Luca miongoni mwa Makipa watatu kwa michezo muhimu ya mwisho dhidi ya Somalia na Uganda ambapo Algeria kwa sasa inaongoza kundi lake la kufuzu na inahitaji ushindi mmoja pekee kati ya michezo hiyo miwili ili kufuzu rasmi.

Klub ya Simba Sc imemtambulisha kocha wake mkuu raia wa Bulgaria DIMITAR PANTEV ambaye alikuwa anakinoa kikosi cha Gabor...
03/10/2025

Klub ya Simba Sc imemtambulisha kocha wake mkuu raia wa Bulgaria DIMITAR PANTEV ambaye alikuwa anakinoa kikosi cha Gaboren United.


Uongozi wa Azam FC imeiandikia barua bodi ya ligi TPLB ikilalamikia uamuzi mbovu kwenye mchezo wao dhidi ya JKT Tanzania...
02/10/2025

Uongozi wa Azam FC imeiandikia barua bodi ya ligi TPLB ikilalamikia uamuzi mbovu kwenye mchezo wao dhidi ya JKT Tanzania uliopigwa jana Oktoba 01, MEJA JENERALI ISAMUYO.

Azam FC barua yao imewasilishwa Ofisi ya Mtendaji Mkuu (CEO) wa Bodi ya Ligi leo asubuhi.

Timu ya Azam FC imefanya kwa mujibu wa Kanuni zinavyosema kuwa malalamiko yote yanapaswa kupelekwa sehemu husika kwa maandishi na sio kuzungumza sehemu ambazo sio sahihi.

Uongozi wa Azam FC una malalamiko matatu, tukio la Japhte Kitambala ambalo alivutwa jezi ndani ya BOX, Lusajo Mwaikenda kuchezewa rafu na Himid ambae alichezewa rafu na mlinzi wa mwisho ambae alistahili kuonyeshwa kadi nyekundu ila alionyeshwa kadi ya Njano.

Kocha Nasreddine Nabi yupo Jijini Dar es Salaam. Zipo taarifa huenda akatangazwa kuwa Kocha wa moja ya timu kubwa nchini...
30/09/2025

Kocha Nasreddine Nabi yupo Jijini Dar es Salaam. Zipo taarifa huenda akatangazwa kuwa Kocha wa moja ya timu kubwa nchini wakati wowote. Nabi amewasili nchini leo asubuhi tayari kwa kumalizana na moja ya timu hizo. Unadhani ni timu gani?


30/09/2025

"Tumewasikia mashabiki wa yanga wanapiga kelele, tupo kwenye mchakato wa tathimini" - Ally kamwe

Full video nimekuwekea katika youtube channel ya Extrapower,
Link https://youtu.be/XlbouZDfdPE

Mwanamume mmoja kutoka Kisumu Ndogo-Malindi amemkimbia mwanamke aliyekuwa amekuja katika hoteli moja kukutana nae.Inadai...
30/09/2025

Mwanamume mmoja kutoka Kisumu Ndogo-Malindi amemkimbia mwanamke aliyekuwa amekuja katika hoteli moja kukutana nae.
Inadaiwa jamaa alichukua maamuzi hayo baada mwanamke huyo kwenda hapo na watoto wake watano na kumuachia bili ya shilingi 8,200/= ambayo ni sawa na 155,781 ya Tanzania.

Address

Kinondoni
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ExtraPower Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share