ExtraPower Tv

ExtraPower Tv Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ExtraPower Tv, Digital creator, Kinondoni.

Klub ya ya Mtibwa sugar imemsajili Beki Edward Charles Manyama baada ya kuachana na Singida Black Stars. Manyama ambae a...
24/07/2025

Klub ya ya Mtibwa sugar imemsajili Beki Edward Charles Manyama baada ya kuachana na Singida Black Stars. Manyama ambae amekuwa na wakati mgumu akiwa kwenye Klabu ya Singida Black Stars mbele ya Walinzi waliokuwepo katika Kikosi hicho.


Simba wamewasilisha offa kwa beki wa kushoto (Leftback) wa APR ya Rwanda 🇷🇼 Claude Niyomugabo (26). Taarifa zinasema Wak...
24/07/2025

Simba wamewasilisha offa kwa beki wa kushoto (Leftback) wa APR ya Rwanda 🇷🇼 Claude Niyomugabo (26). Taarifa zinasema Wakala wa mchezaji huyo amesema mchezaji wake amekubali ofa hiyo na kwasasa kilichobaki ni makubaliano ya klabu na klabu (APR & Simba) kwani Claude Niyomugabo, amebakiza mkataba wa mwaka mmoja na timu yake.

Real Madrid wako tayari kutoa pauni milioni 100 kwa kiungo wa Manchester City na Hispania Rodri, 29 (Sun).Winga wa Manch...
24/07/2025

Real Madrid wako tayari kutoa pauni milioni 100 kwa kiungo wa Manchester City na Hispania Rodri, 29 (Sun).

Winga wa Manchester City na England Jack Grealish, 29, ni mmoja wa wachezaji kadhaa wa upande wa kushoto wanaofuatiliwa na Napoli (Corriere dello Sport).

Javi Guerra amekataa ofa ya kurefusha mkataba wake na Valencia, huku Manchester United ikiripotiwa kumfuatilia kiungo huyo wa Hispania mwenye umri wa miaka 22 (Marca).

Tottenham wanamfuatilia kwa karibu Kobbie Mainoo, huku kiungo huyo wa Manchester United bado hajafikia makubaliano ya kurefusha mkataba wake wa muda mrefu, ambao unamalizika mwaka 2027 (tbrfootball.com).

Afisa habari wa Yanga Ali kamwe amefunguka na kuweka wazi, baada ya kuulizwa kuwa ni usajili wa mchezaji gani kwake ndio...
24/07/2025

Afisa habari wa Yanga Ali kamwe amefunguka na kuweka wazi, baada ya kuulizwa kuwa ni usajili wa mchezaji gani kwake ndio unabaki kuwa bora toka awe msemaji wa Yanga, Ali kamwe aksema, "Usajili bora kwangu toka nimeingia Yanga niwa Maxi Nzengeli aliingia nchi hii akiwa hajulikani na mtu yoyote na Maxi hakunihitaji Mimi (Ally Kamwe) nimpigie promo Maxi alijipigia promo yeye mwenyewe kwenye mechi na Kaizer Chiefs aliejitambulisha mwenyewe kuwa Mimi ndio Maxi na watu wakajua kweli huyu ni Bora, Lakini Maxi amekuwa tofauti na Wakongo wote, jamaa ni mtu wa kawaida anamjua Mungu wake, anamuheshimu anafanya Ibada anafanya kazi yake na anaheshimu watu wote"

Ali kamwe aliendelea kwa kusema, "Maxi kimpira Kuna story Moja watu wengi hawajawahi kuijua, tulicheza mechi Moja ya ligi mkoani alafu Maxi akatolewa nje (Substitution) alivyotolewa alikasirika kweli, akaenda vyumbani akakiamsha sana bonge Moja la mtiti kwanini anatolewa alijiona ni k**a Mbuzi wa kafara kila mechi dakika ya hamsini na kitu lazima aitwe hata k**a hakosei lazima aitwe benchi"

Watu wengi huudhika baada ya kusikia harufu ya pindi mtu akijamba. Lakini wengi wao hawajui faida ya ushuzi au faida ya ...
23/07/2025

Watu wengi huudhika baada ya kusikia harufu ya pindi mtu akijamba. Lakini wengi wao hawajui faida ya ushuzi au faida ya kujamba. Wanasayansi nchini uingereza wamesema kuwa ushuzi ni kinga dhidi ya saratani kwa sababu ndani ya ushuzi kuna gesi aina ya hydrogen sulfide ambayo hupunguza uwezekano Wa mtu kupata saratani. Wanasayansi hao wamesema kuwa kiafya kwa siku mtu anatakiwa kujamba mara 14 mapak mara 23.

Umejamba mara ngapi mpaka muda huu?


Klub ya Azam fc imepokea ofa nono kutoka klub ya Independiente Santa Fe kutoka colombia, ofa  yenye thamani ya dola 115,...
23/07/2025

Klub ya Azam fc imepokea ofa nono kutoka klub ya Independiente Santa Fe kutoka colombia, ofa yenye thamani ya dola 115,000 sawa na Tsh.298,930,193.85 kwa Mshambuliaji wao raia wa Colombia Jhonier Blanco lakini ofa hiyo imekataliwa mara moja na Azam FC asubuhi ya leo. Taarifa kutoka ndani ya Azam fc zinasema kuwa kocha ibenge ndio ataamua ni nani wa kuuza na nani wa kuacha pale atakapokutana na wachezaji wote pindi pre season itakapoanza.

Independiente santa fe wamepewa taarifa kuhusiana na hilo.

Hizi ndio takwimu za Steve Ebuela, Raia wa Dr Congo.Nafasi anayocheza ni Mlinzi wa kulia.Anaweza kutumia miguu yote kwa ...
23/07/2025

Hizi ndio takwimu za Steve Ebuela, Raia wa Dr Congo.
Nafasi anayocheza ni Mlinzi wa kulia.
Anaweza kutumia miguu yote kwa usahihi.
Ana Umri wa Miaka 24.

TAKWIMU ZA EBUELA AKIWA NA AL HILAL KATIKA CAF CHAMPIONS LEAGUE:

Takwimu za Jumla.
Amecheza michezo-8
Jumla ya dakika alizocheza ni 720
Hajafunga
Haja assist

Takwimu za Kiulinzi
Amepata Clean sheets 2.
Hana kadi ya njano wala nyekundu
Amenyang'anya mipira mara 18
Amekatiza mashambulizi ya wapinzani mara 10
Amezui mashuti ya wapinzi mara 2
Ameshinda mipira ya Juu ya kugombania mara 5.

Takwimu za kushambulia
Amepiga key pass 8
Amefanikiwa kukokota Mipira mara 11
Amepiga Mashuti 7 huku 2 yakilenga lango.

Watu 125 wanatuhumiwa kuhusika na makosa mbalimbali wakiwemo wenye makosa ya kutumia dawa za kulevya na kusambaza,pamoja...
23/07/2025

Watu 125 wanatuhumiwa kuhusika na makosa mbalimbali wakiwemo wenye makosa ya kutumia dawa za kulevya na kusambaza,pamoja na wizi wa mali mbalimbali katika kipindi cha kuanzia mwezi juni 27,2025 hadi julai 22,2025 .

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akizungumza na vyombo vya habari leo Julai 23, 2025, amesema watuhumiwa hao walik**atwa wakati jeshi hilo likifanya operesheni iliyolenga kubaini na kuzuia uhalifu.

Amesema katika operesheni hizo, dawa za kulevya zilizok**atwa ni pamoja na bhangi gramu 2,261 mirungi kilo 29 pamoja na pombe ya moshi lita 142. bajaji moja ,runinga saba mbati 16, nondo vipande 17 vitanda vinne pikipiki mbili, redio nane na risasi moja ya silaha ndogo.

Aidha amesema jumla ya kesi 25 zimepata mafanikio ambapo kesi mbili za kulawiti wash*takiwa wawili wamehukumiwa kifungocha maisha jela, kesi mbili za kubaka, ambapo wash*takiwa wawili wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela.

Viongozi wa klub ya Coastal Union wapo katika maongezi na kocha Zuberi katwila kwa lengo la kwenda kukinoa kikosi cha wa...
23/07/2025

Viongozi wa klub ya Coastal Union wapo katika maongezi na kocha Zuberi katwila kwa lengo la kwenda kukinoa kikosi cha wagosi wa kaya. Taarifa zinasema klub hiyo mpaka sasa imesitisha zoezi la usajili mpaka pale kocha hoyo atakapotia wino na kutoa mapendezo yake ya anahitaji mchezaji gani asajiliwe.


Kocha Miguel Gamond amependekeza jina la Jonas Mkude kwa viongozi wa Singida Black stars kumsajili katika dirisha hili k...
23/07/2025

Kocha Miguel Gamond amependekeza jina la Jonas Mkude kwa viongozi wa Singida Black stars kumsajili katika dirisha hili kubwa la usajili. Gamondi anamhitani mkude kuongeza uzoefu katika sehemu ya kiungo ya klub hiyo.

Mkunde kwasasa ni mchezaji huru baada ya kuamaliza makataba wake na klub ya Yanga sc.

Klabu ya Azam FC imeanza mazungumzo na Klabu ya Singida Black Stars ili kupata saini ya Mlinzi wa Kushoto wa Klabu hiyo,...
23/07/2025

Klabu ya Azam FC imeanza mazungumzo na Klabu ya Singida Black Stars ili kupata saini ya Mlinzi wa Kushoto wa Klabu hiyo, Ibrahim Imoro, ambae amekuwa na Kiwango bora sana kwenye Kikosi hicho.

Siku kadha zilizopita Kocha mkuu wa Klabu hiyo aliwaambiwa viongozi wa Klabu hiyo Kuwa anahitaji Mlinzi mwenye uwezo mkubwa katika eneo la Ulinzi wa Kushoto ambaye atakwenda kupambania namba na Pascal Msindo na pendekezo limedondoka Kwa Mlinzi Ibrahim Imoro, ambae bado ni kijana mdogo mwenye uwezo mkubwa sana akiwa katika kiwanja. Ikumbukwe imoro aliwahi kufanya kazi na ibenge.

Mlinzi huyo amewahi kuitumikia Klabu ya Al Hilal Omdurman ya Sudan kabla hajajiunga na Klabu ya Singida Black Stars.

Winga wa Real Madrid na Brazil Rodrygo, 24, ni mmoja wa nyota wa kumrithi Luis Diaz huko Liverpool iwapo winga huyo wa C...
23/07/2025

Winga wa Real Madrid na Brazil Rodrygo, 24, ni mmoja wa nyota wa kumrithi Luis Diaz huko Liverpool iwapo winga huyo wa Colombia mwenye umri wa miaka 28 ataondoka Anfield (Florian Plettenberg).

Mshambuliaji wa Sweden Alexander Isak, 25, anataka pauni 300,000 kwa wiki kusaini mkataba mpya Newcastle (Talksport).

Granit Xhaka amekubaliana masharti na Sunderland, huku klabu hiyo sasa ikiwa kwenye mazungumzo na Bayer Leverkusen kuhusu ada ya kiungo huyo wa Uswisi mwenye umri wa miaka 32 (Times).

Atletico Madrid wameanza mazungumzo na Chelsea kuhusu mpango wa kumsajili Renato Veiga, huku Blues wakidai takriban pauni milioni 35 kumuachia beki huyo wa kati wa Ureno mwenye umri wa miaka 21 (Fabrizio Romano).

Address

Kinondoni

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ExtraPower Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share