UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

01/12/2025

Ritha Erasto (29) anaendelea kuvunja ukuta wa vikwazo vilivyomzuia kitaaluma miaka iliyopita, huku safari yake sasa ikifungua mjadala mpana juu ya nafasi ya mifumo mbadala ya elimu na namna mifumo hiyo inavyoweza kuwainua wasichana waliopoteza mwelekeo katika mfumo rasmi wa elimu.

Ungana na Faraja Sendegeya katika Makala ya Ufunguo akiangazia mafanikio ya Ritha kupitia mifumo mbadala ya kielimu na kuibua mjadala juu ya nafasi yake kwa sasa.


Mhariri |

01/12/2025

Baadhi ya wazee katika kijiji cha Nyijundu, Wilaya ya Nyang’hwale, mkoani Geita wamejitokeza leo Disemba mosi 2025 kupima maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani na kujenga uelewa wa kupima afya mara kwa mara.

Wakizungumza na mwandishi wa mkoani humo, wazee hao wamesema kilichowasukuma kujitokeza ni kutokana na jukumu kubwa walilonalo la kusimamia familia zao, ambapo wamekua wakiwahudumia wagonjwa nyumbani, hivyo ni vyema wafahamu hali ya afya zao.


Mhariri |

01/12/2025

Serikali imesema itawafutia hadhi ya ukimbizi, wakimbizi 238,956 wanaoishi nchini baada ya nchi zao kurejea kwenye hali ya amani, ambapo awali zilikumbwa na machafuko.

Kauli hiyo ya serikali imetajwa leo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene kwenye mkutano maalum wa Tanzania, Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) na kueleza kuwa miongoni mwa wakimbizi hao ni Warundi 152,019, Wakongo 86,256 na kutoka mataifa mengine ni 681.


Mhariri |

01/12/2025

Mafuriko na maporomoko ya ardhi yaliyozikumba nchi nne za bara la Asia yamesababisha vifo vya takriban watu 1150, huku idadi hiyo ikiendelea kuongezeka kadri siku zinavyosonga tangu mvua kubwa zianze kunyesha wiki iliyopita.

Athari hizo zimesababishwa na vimbunga Senyar na Ditwah, ikielezwa kuwa nusu ya waliokufa maji wameripotiwa nchini Indonesia, ambako kuna madhara makubwa zaidi ikilinganishwa na mataifa mengine ya Sri Lanka, Thailand na Malaysia.


Mhariri |

Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshikilia askari magereza mwenye umri wa miaka 31 (jina limehifadhiwa kwa sababu za...
01/12/2025

Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshikilia askari magereza mwenye umri wa miaka 31 (jina limehifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi) kwa tuhuma za kumuua mke wake aliyetambulika kwa jina la Betia Oscar Chacha (25), mkazi wa Bugweto kwa kumkata na kitu kinachodhaniwa kuwa chenye ncha kali katika maeneo mbalimbali ya mwili na kumsababisha kifo.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, SACP Janeth Magomi amesema mtuhumiwa amek**atwa na mwili wa marehemu umehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu.


✍ Kasisi Costa
Mhariri |

01/12/2025

Ni kosa kisheria kupekua simu ya mume au mke wako, mwanasheria wetu anaelezea kwa undani.

01/12/2025

Hali ya sintofahamu imeendelea kukumba makaburi ya Dodoma, yaliyopo Mtaa wa Mageuzi, Manispaa ya Shinyanga kufuatia kuibuka kwa wizi wa vyuma vilivyotumika kujengea makaburi.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mageuzi, Vitalis Mugisha amesema tukio hilo limebainika baada ya baadhi ya ndugu wa marehemu kutoa malalamiko kuwa vyuma vilivyowekwa kwenye makaburi ya jamaa zao vimekuwa vikiibwa na huenda vinauzwa k**a chuma chakavu.


Mhariri | John Mbalamwezi

01/12/2025

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati, imeanza mikakati ya kuhakikisha matumizi ya nguvu ya nyuklia yanakuwa na manufaa, hasa katika uzalishaji wa nishati ya umeme nchini.


Mhariri | John Mbalamwezi

01/12/2025

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itahakikisha inaongeza bajeti katika kusimamia utoaji wa huduma za afya kwa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi, ili kuimarisha upatikanaji wa huduma hizo kwa uhakika.

Hayo yamebainishwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdullah, kisiwani Unguja, wakati wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani.


Mhariri | John Mbalamwezi

01/12/2025

Katika kukabiliana na uhaba wa chakula mashuleni, walimu wa shule ya sekondari Kihamili, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma, wameanzisha mabwawa ya samaki ili kuongeza lishe kwa wanafunzi na pia kuongeza kipato cha shule.

Walimu hao wanasema mradi huo pia umechangia kupunguza utoro wa wanafunzi, ambao awali walikimbia shuleni kwa sababu ya kula maharage kila siku.


Mhariri | John Mbalamwezi

01/12/2025

Fuatilia simulizi ya Job Nisilu na Mariam Lugenge, waliodumu katika ndoa kwa zaidi ya miaka 40. Wakati wa maisha yao pamoja, wameshuhudia milima na mabonde ya changamoto, huku wakijaribu kudumisha upendo na mshik**ano katika familia.

Hata hivyo, maisha yao yamepitia mtihani mkubwa baada ya kugundulika kuwa mmoja wao ameambukizwa virusi vya ukimwi (VVU).


Mhariri | John Mbalamwezi

Shirika la Afya Duniani linaeleza kuwa, baada ya miongo kadhaa ya maendeleo, vita dhidi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) sasa ...
01/12/2025

Shirika la Afya Duniani linaeleza kuwa, baada ya miongo kadhaa ya maendeleo, vita dhidi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) sasa ipo njia panda kutokana na ukweli kwamba huduma za kuokoa maisha zimetatizwa, na jumuiya nyingi zinakabiliwa na udhaifu mkubwa kufuatia kusimamishwa kwa ufadhili wa baadhi ya shughuli za kupambana na ugonjwa huo.

Unashauri hatua gani zichukuliwe ili kuimarisha mapambano dhidi ya VVU?

Address

Mandela Road
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Share