UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

17/01/2026

Kabila nyingi za Afrika zimekuwa na mila na desturi zake ambazo zimekuwa utambulisho wa jamii nyingi za bara hilo.

Miongoni mwa tamaduni ya kale ni ‘Jando na Unyago’ kwa makabila ya Tanzania likiwemo kabila la Makonde ambalo wenyeji wake huitwa ‘Wamakonde’.

Hata hivyo kunadaiwa kuwepo kwa dalili za kupotea kwa ‘Jando na Unyago’ katika kabila hilo hali iliyomsukuma mwandishi wetu, John Kasembe kufuatilia.

Mhariri

17/01/2026

Ngoma ya Kiduwo ya kabila la Wahehe imejizolea umaarufu mkoani Iringa ikiwa inachezwa katika sherehe, misiba na mapokezi maalumu ya viongozi na mashujaa.

Muhammad Nyaulingo amewatembelea wenyeji wa mkoa huo na kutaka kufahamu zaidi asili, inavyochezwa na umuhimu wa ngoma hiyo kwa jamii.

Mhariri

17/01/2026

Unajua kuwa kuna aina ya kobe ambayo ni tofauti na ile uliyoizoea?

Karibu umuone ‘kobe chapati’ ambaye amekuwa kivutio kingine cha utalii nchini.

Undani kuhusu kobe huyu unaletwa na Hellen Kawiche.

Mhariri

17/01/2026

Chama cha madaktari wa ugonjwa wa kisukari nchini umesema hatari ya vifo vitokanavyo na magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo ugonjwa huo imeongezeka na sasa duniani imefikia asilimia 75 huku pia ulemavu wa kudumu ukiwa ni sehemu ya athari za ugonjwa huo.

Chama hicho kimeendelea kufanya kiliniki ya ugonjwa huo sambamba na kuwasisitiza wananchi kujikinga zaidi kwa maradhi hayo.

Taarifa ya Esterbella Malisa.

Mhariri

17/01/2026

Kumekuwa na changamoto nyingi za majengo kwenye maeneo tunayoishi kutokana na kutokufanyiwa ukarabati kwa muda mrefu, Msanifu majengo, Osman S Mbarouk kutoka kampuni ya Majengo Grid Intarnational amesema kuwa, ukarabati wa majengo ni kitu cha muhimu sana na nikitu ambacho unatakiwa kushirikisha wataalam sahihi ili kuondoa changamoto hiyo na kuepusha gharama zisizo za lazima.

17/01/2026

Ikiwa leo ni siku ya ushauri elekezi duniani, Dr. Catherine Kahabuka, Mshauri mwelekezi (mentor) amabye pia ni (Career Advancement Coach) ametuambia kuwa, ushauri elekezi (mentorship) kwa kiasi kikubwa huwa inahusishwa na kukuza fani na kuingiza kipato na kumsaidia mtu kupiga hatua na kumfanya awe mwenye uwezo wa kutambua jambo alilojifunza kwa utaalamu zaidi.

17/01/2026

K**a ulishwahi kuhisi umecheleweshewa kupokea mzigo wako ambao uliagiza mahali popote pale basi hujawahi kucheleweshewa, huko nchini Libya jijini Tripoli mfanyabiashara wa simu amepokea mzigo huo wa simu alioagiza tangu mwaka 2010, ambapo hadi sasa ni miaka 16 tangu aagize bidhaa hizo kutokana na mzigo huokuzuiliwa kwa muda mrefu.

✍Roland John
Mhariri |

17/01/2026

Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amewataka watumishi wa umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida Fund k**a njia ya kujipatia uhuru wa kifedha kabla na baada ya kustaafu.

Akifungua mkutano mkuu wa tatu wa mfuko huo jijini Dar es Salaam, Ridhiwani amesema bado hajaridhishwa na watumishi 12,000 pekee waliowekeza, na akahimiza uongozi wa Faida Fund kubuni mikakati zaidi ya kuwavutia wawekezaji wengi ili kuongeza tija na ustawi wa watumishi nchini.

17/01/2026

Ukistaajabu ya Musa utayona ya Firauni, leo kwenye mikasa ya Dafrao huko nchini Marekani Jonathan Gerlack mwenye umri wa miaka 34, amejikuta matatani baada ya kushikiliwa na vyombo vya dola akish*takiwa kwa makosa zaidi ya 300
ikiwemo kuiba mafuvu 100 ya vichwa vya watu, viungo mbali mbali vya binadamu pamoja na vito vya thamani vilivyo ibiwa katika makaburi ya Mount Moriah jijini Philadelphia.

✍Roland John
Mhariri |

17/01/2026

Tazama mazoezi ya leo yanayohusu namna tofauti ya kunyoosha viungo na kupunguza uzito yanayoongozwa na mwalimu Eric, ambayo yanayoweza kufanywa na rika tofauti kwa watu wazima na wazee, mazoezi hayo husaidia kuweka viungo vya mwili imara na kupunguza uzito.

16/01/2026

Wahitimu wanne wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wamefanikiwa kubuni gari inayotumia umeme baada ya kusukumwa na udadisi wa kutatua changamoto za usafiri hususani upande wa uchafuzi wa mazingira na unafuu wa gharama.

Joseph Mpangala ameafuatilia ubunifu huo.

Mhariri

16/01/2026

Wakala wa Umeme Vijijini (REA) umefanikiwa kuzindua kituo cha kupoza umeme cha Mtera kinachotarajiwa kuwanufaisha wakazi wa Iringa na maeneo ya jirani.

Sambamba na hilo serikali imewahimiza wananchi kulinda miundombinu ya umeme nchini.

Joyce Mwakalinga ameandaa taarifa ifuatayo.

Mhariri

Address

Mandela Road
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Share