UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

06/06/2026

Msikilize Jafari Mponda akisimulia tukio la raia mmoja wa Marekani aliyeilalamikia mahak**a, akieleza kutoridhishwa na chakula anachopatiwa akiwa maabusu…ambacho ni ugali na kabichi.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya

06/06/2026

Mshauri wa masuala ya biashara, Coach Godfrey amesema kuwa changamoto kubwa inayowakumba watu wengi wenye mitaji ya biashara ni uelewa mdogo wa biashara wanazozianzisha, jambo linalosababisha kushindwa kufanikiwa.

Amesema kuwa kabla ya kuanza biashara yoyote, ni muhimu kupata maarifa na uelewa wa kina wa namna biashara hiyo inavyofanyika ili kusaidia kuweka mipango madhubuti na kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya

06/06/2026

Daktari Bingwa wa Macho, Majala Jafari Majara amesema kuwa kuvaa miwani kwa ajili ya urembo si jambo baya, kwani watu wengi huivaa ili kuboresha mwonekano wao na kuongeza mvuto. Hata hivyo, ameeleza kuwa baadhi ya watu hununua miwani hiyo kwa kuzingatia zaidi muonekano wake bila kujiridhisha kuhusu usalama na ubora wake.

Dkt. Majala amesisitiza umuhimu wa kupeleka miwani ya urembo kwa mtaalamu wa macho kwa ajili ya uchunguzi kabla ya kuitumia. Kulingana naye, hatua hiyo inaweza kusaidia kubaini k**a miwani hiyo ni salama kwa macho na inakidhi viwango vinavyohitajika vya matumizi.

Amefafanua kuwa baadhi ya miwani inayopatikana sokoni huenda ikawa ilitumika awali katika nchi nyingine na baadaye kuingia katika masoko ya Afrika. Kutokana na hali hiyo, ni muhimu kufahamu historia na ubora wa miwani hiyo ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kwa afya ya macho.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya

06/06/2026

Afya njema hujengwa kwa kula lishe bora na kufanya mazoezi mara kwa mara. Mazoezi husaidia kuimarisha mwili, kuchoma mafuta yasiyohitajika, na kuboresha afya kwa ujumla.

Fanya mazoezi haya kuupa mwili wako mwonekano mzuri.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya

06/06/2026

Mfanyabiashara, Farida Mwinshehe anasema kuwa mafanikio ya biashara yanategemea uwezo wa mfanyabiashara kuelewa mazingira anayofanyia biashara.

Anasisitiza kuwa ni muhimu kufanya uchambuzi wa eneo husika ili kuhakikisha bidhaa au huduma zinazotolewa zinakidhi mahitaji na matarajio ya watu wa eneo hilo.

Ameeleza kuwa kufahamu aina ya wateja unaowalenga ni jambo muhimu kwani hukusaidia kupanga mikakati sahihi ya biashara na kuongeza nafasi ya kupata faida.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya

05/06/2026

Mchambuzi wa siasa za kimataifa, Ibrahim Rahbi, amesema Iran awali haikuwa imefahamu kikamilifu uwezo wa makombora yake hadi ilipoingia katika vita vya Twelve Days War dhidi ya Israel, hali iliyosababisha taifa hilo kuongeza juhudi za kuboresha na kuimarisha zaidi teknolojia yake ya kijeshi.

Rahbi pia amelishutumu Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kwa kushindwa kuchukua hatua dhidi ya uvunjwaji wa sheria za kimataifa zinazokataza kushambuliwa kwa vinu vya nyuklia, akidai kuwa Marekani na Israel zimekuwa zikilenga maeneo hayo bila kuadhibiwa licha ya kukiuka kanuni hizo.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi


05/06/2026

Tazama kionjo cha waigizaji wa tamthilia ya Kombolela, Tukae na Mashavu walipokuwa katika studio za

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi


05/06/2026

Mwigizaji wa tamthilia ya Kombolela, Tukae Kikala, amesema kuwa ujumbe unaogusa jamii moja kwa moja hupokelewa kwa haraka na kwa ufanisi zaidi, kwani husaidia kuwakumbusha watu na kuonesha uhalisia wa maisha yao ya kila siku.

Ameeleza kuwa sanaa yenye maudhui yanayogusa changamoto halisi za jamii ina uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko ya tabia na mitazamo, akibainisha kuwa moja ya vipande alivyoshiriki katika tamthilia hiyo kimechangia mabadiliko ya haraka katika jamii kutokana na kugusa moja kwa moja suala lililokuwa likiathiri maisha ya watu.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi


05/06/2026

Mwigizaji wa Tamthilia ya Kombolela, Tukae Kikala, ameonyesha kipaji chake kingine cha sanaa akiwa mgeni katika kipindi cha Morning Trumpet kinachoruka Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 4:00 kamili.

Mbali na umahiri wake wa uigizaji, Tukae amedhihirisha kuwa pia ni mwimbaji mahiri, hasa wa nyimbo za Kikongo.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi


05/06/2026

Mwandaaji wa tamthilia ya Kombolela, Abdul Usanga, amesema ubunifu alioutumia katika uchaguzi wa wahusika umechangia kufikisha ujumbe kwa ufanisi kwa kuwa majina na matendo ya wahusika yanaendana na tabia zinazojitokeza katika jamii.

Amesema sanaa inahitaji ubunifu mkubwa ili kuhakikisha ujumbe unaokusudiwa unawafikia walengwa na kupokelewa kwa namna inayowezesha jamii kujifunza kupitia maudhui yanayoandaliwa.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi


Address

Mandela Road
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Share