UTVTZ

UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

20/07/2025

Wanawake zaidi ya 500 mkoani Morogoro wamepatiwa mafunzo ya ujasiriamali kupitia programu ya Academy for Women Entrepreneurs (AWE), ambayo yatawasaidia wanawake hao kuongeza fursa za biashara, kuhimili ushindani na kusimamia biashara zao.

Theresia Mwanga
Mhariri | _jm

20/07/2025

Rais wa taasisi ya Kalamu Education Foundation, Mohamed Kamilagwa ameshauri serikali na mashirika binafsi kutilia mkazo elimu jumuishi kwa watu wenye ulemavu, ili kukuza uwezo wao katika suala zima la elimu na kuwaondoa katika hali duni ili waweze kujikwamua kimaisha kwa kusoma kile wanachoamini wanaweza kufanya.


Mhariri|

19/07/2025

Katika dunia ya leo, kuna mambo mengi ya kushangaza, mengine hufurahisha, mengine huhuzunisha, lakini yapo pia yanayoacha maswali yasiyo na majibu ya haraka.

Katika Kijiji cha Chibe, Manispaa ya Shinyanga kuna kisima cha ajabu kilichopo juu ya mwamba mkubwa… kimekuwepo juu ya mwamba huo kwa miaka mingi bila kukauka.


Mhariri | John Mbalamwezi

19/07/2025

Viongozi na wafanyakazi wa kampuni ya Azam Media Ltd wamejumuika jijini Dar es Salaam leo kusherehekea ushindi wao wa kuwa kituo bora kwa maudhui katika tuzo za Samia Kalamu zilizoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA).

Katika tukio hilo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Patrick Kahemele amesema wameamua kutumia fedha za zawadi waliyopewa kwa kula na kunywa pamoja na wafanyakazi wote.


Mhariri | John Mbalamwezi

19/07/2025

Katika kukabiliana na upungufu wa chakula na mabadiliko ya tabianchi, wakulima wa zao la mtama kutoka wilaya sita za mkoa wa Dodoma wameanza kunufaika na mradi himilivu wa kilimo cha mtama kwa kuanzisha kilimo mbadala cha mbogamboga na matunda kwa njia ya umwagiliaji.

Mradi huo pia umelenga kuongeza uhakika wa kipato kwenye kaya za wakulima, hasa kina mama baada ya wakulima kuvuna mtama wakati wakisubiri msimu mpya wa kilimo kuanza.


Mhariri | John Mbalamwezi

Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mabaraza ya...
19/07/2025

Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mabaraza ya Habari Duniani (WAPC) na pia Makamu Mwenyekiti wa Mabaraza ya Habari ya Afrika Mashariki (EAPC).

Akitoa pongezi kufuatia uchaguzi huo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile amesema uchaguzi huu si tu ni heshima kwa Sungura binafsi, bali ni uthibitisho wa mchango mkubwa wa Tanzania katika uendelezaji wa taaluma ya habari duniani.

“TEF inatambua juhudi na uongozi mahiri wa Sungura uliosaidia kujenga misingi ya ushirikiano wa kikanda na kimataifa kupitia jukwaa la Mtandao wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika (NIMCA), na sasa amepanda kwenda WAPC. Tunathamini mchango wake katika kukuza mazingira wezeshi kwa uhuru wa habari, uwajibikaji na weledi katika sekta ya habari,” amesema Balile katika barua ya pongezi.


Mhariri | John Mbalamwezi

19/07/2025

Makamu wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church (AICT), Zakayo Bugota ameiomba serikali kuongeza mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya kati ili kuwawezesha kufikia ndoto zao.

Akizungumza na wanafunzi na wahitimu wa chuo cha AICT Shinyanga, Askofu Bugota alisema hali ngumu ya kiuchumi imekuwa kikwazo kikubwa kwa vijana wengi kutimiza malengo yao kielimu.


✍Kasisi Kosta
Mhariri | John Mbalamwezi

19/07/2025

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Geita imewataka mawakala wa huduma za fedha kujiepusha na utakatishaji wa fedha zinazotokana na takrima, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.

Akizungumza na watoa huduma hao kutoka kampuni mbalimbali za mawasiliano, Mkuu wa TAKUKURU mkoani humo, James Ruge amesema baadhi ya mawakala wamekuwa wakihusika kwa kujua au kutokujua katika utakatishaji wa fedha haramu, hali inayochochea vitendo vya rushwa.


✍Ester Sumira
Mhariri | John Mbalamwezi

19/07/2025

"Kwenye maisha sio mambo yote muhimu ni ya lazima lakini mambo yote ya lazima muhimu".

Unakubaliana na mtazamo huu? Msikilize mshauri wa saikolojia, Geofrey Mwamnyanyi akielezea mambo hayo.

✍Juliana James
Mhariri |

19/07/2025

Kwanini mara nyingi ukipanga miadi na wanawake, wao kuchelewa ni jambo la kawaida?

Msikilize mdau wa kijamii, Beatrice Michelle akielezea sababu hizo.

✍Juliana James
Mhariri |

19/07/2025

Una marafiki au ndugu wanaotoa 'visingizio' wanaposhindwa kutimiza yale mliohaidiana?

Huwa wanatoa sababu zipi?

✍Juliana James
Mhariri |

19/07/2025

Je, mdau wa huwa unafanya vitu kwa wakati unaotakiwa? Unadhani kwanini baadhi ya watu hupenda kufanya vitu "dakika za mwisho", sababu ni nini hasa?

Msikilize mdau wa masuala ya kijamii, Beatrice Michelle akifafanua zaidi kuhusu tabia hiyo.

✍Juliana James
Mhariri |

Address


Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Shortcuts

  • Address
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share