UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

03/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesema serikali inaendelea na mikakati ya kuongeza thamani ya zao la zabibu ili wakulima wanufaike zaidi.

Ameeleza kuwa mkoa huo tayari umepata kiwanda cha kuchakata na kuhifadhi zabibu, hatua itakayopunguza changamoto za masoko na kuongeza kipato kwa wakulima.


✍Alpha Jenipher
Mhariri | John Mbalamwezi

Makamu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Modest Katonto ameiasa jamii mkoani Rukwa kushirikiana na viong...
03/10/2025

Makamu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Modest Katonto ameiasa jamii mkoani Rukwa kushirikiana na viongozi wa dini katika kukabiliana na changamoto ya mmomonyoko wa maadili.

Mabadiliko ya sayansi na teknolojia yachochea vipi mmomonyoko wa maadili katika jamii unayoishi? nini kifanyike? Tuandikie maoni yako na tutayasoma saa 7:00

03/10/2025

Kwa taarifa yako…nzi na funza wanaweza kukuinua kiuchumu…

Fuatilia simulizi ya Denis Kamanzi, mwanzilishi wa BIOAKEMI, ambaye aliona fursa kwenye ufugaji wa nzi-chuma na funza. Fursa hii imebadili muelekeo wa maisha yake, ikamwezesha kujiajiri na pia kuajiri vijana wengine.

Msikilize akifafanua namna nzi na funza walivyokuwa daraja la kumuinua kiuchumi.


✍Alpha Jenipher
Mhariri | John Mbalamwezi

03/10/2025

Mapitio ya leo Oktoba 3, 2025 kwenye

02/10/2025

Shuhuda wa kifo cha mama anayekadiriwa kuwa na miaka 36 anayedaiwa kufariki dunia akiwa katika harakati za kutoa ujauzito mkoani Morogoro ambaye ni mtoto wa marehemu amesimulia ‘maumivu, mateso na machungu aliyopitia mama yake wakati wa dakika za mwisho za uhai wake’ huku akishuhudiwa na watoto wake wawili.

Mwandishi wetu Theresia Mwanga ametuandalia taarifa zaidi.


Mhariri |

02/10/2025

Ubora wa unga wa ngano unaozalishwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa umeendelea kuvutia mataifa mbalimbali duniani kupitia bidhaa zake zinazouzwa katika mataifa mengi ya Afrika.

Hayo yamebainishwa wakati wa ziara ya Wakufunzi na Wanafunzi kutoka Chuo cha Uk**anda na Unadhimu cha Zambia waliotembelea kiwanda hicho na kukiri kushuhudia uzalishaji mkubwa na wa hali ya juu sambamba na kupongeza fursa za ajira zilizozalishwa kupitia kiwanda hicho.

Taarifa hii ina undani zaidi.


Mhariri |

02/10/2025

Wakulima wa karafuu visiwani Zanzibar wameahidiwa soko la kimataifa la bidhaa zitokanazo na zao hilo iwapo watampa kura mgombea wa chama cha UDP, Salum Rashidi anayewania Urais wa Tanzania.

Mgombea huyo alikuwa akinadi sera zake katika viwanja vya Magirisi visiwani Zanzibar na kuongeza kuwa ataimarisha miundombinu ya zao la karafuu ili kukuza uchumi wa wananchi k**a anavyoripoti Naima Haji.


Mhariri |

02/10/2025

Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi kukamilisha mchakato wa kufufua mashamba ya maua ya Kiliflora Usariva, Arusha Blooms na Kiliflora Nduruma ambayo yalisitisha uzalishaji ikiwa ni sehemu ya kutumika kwa shughuli zingine ikiwemo programu za kilimo na kugawiwa kwa wananchi.

Ramadhani Mvungi ana undani wa taarifa hii.


Mhariri |

02/10/2025

Wakazi wa Iringa wanatarajiwa kunufaika na ujenzi wa viwanda vya usindikaji matunda na mazao ya chakula sambamba na kiwanda cha kutengeneza karatasi kupitia mazao ya misitu iwapo mgombea Urais wa chama cha NLD, Doyo Hassan Doyo atafanikiwa kushinda uchaguzi wa Oktoba mwaka huu.

Ahadi ya ujenzi huo imetolewa na mgombea huyo katika kampeni zake zilizofanyika leo mkoani humo na kushuhudiwa na Muhammad Nyaulingo.


Mhariri |

02/10/2025

Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameahidi kuondosha changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo ambayo bado kuna changamoto hiyo iwapo atafanikiwa kutetea kiti cha Urais wa Zanzibar.

Dkt. Mwinyi ni mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mtumwa Said anaeleza.


Mhariri |

02/10/2025

Mgombea wa Urais Coaster Kibonde wa Chama cha MAKINI ameahidi kuboresha sekta ya kilimo nchini ikiwemo kugawa bure pembejeo kwa wakulima nchini kwasababu sekta hiyo inahusisha wananchi wengi.

Taarifa ya Sammy Kisika kutoka Rukwa imeangazia kampeni za Kibonde.


Mhariri |

02/10/2025

Mgombea Urais wa Chama cha CHAUMMA, Salum Mwalim amewaahidi wapiga kura wa Kilosa mkoani Morogoro kuwa endapo atafanikiwa kushinda Uchaguzi Mkuu ataunda serikali ambayo itashughulikia changamoto za muda mrefu za wilaya hiyo bila kuwa na kizuizi katika kufanya maamuzi.

Taarifa zaidi na Emmanuel Kalemba


Mhariri |

Address

Mandela Road
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Share