UTVTZ

UTVTZ Kituo chako cha habari zilizochujwa na kuandaliwa kwa ustadi na umakini.

22/08/2025

Kituo cha kumbukumbu cha Dkt. David Livingstone kilichopo Ujiji, mkoani Kigoma, kimeendelea kuwa kivutio muhimu cha utalii wa kihistoria kutokana na mchango wa mmisionari huyo katika kupinga biashara ya utumwa barani Afrika katika karne ya 19.

Kupitia kituo cha kumbukumbu ya Dkt. Livingstone watalii wamekuwa wakizuru na kujifunza namna jitihada zake zilivyoweza kuibua mjadala mpana wa haki za binadamu na mabadiliko ya kijamii.

Ramadhani Mvungi ana undani zaidi


Imehaririwa na

22/08/2025

Jinamizi la matumizi ya dawa za kulevya kwa msanii wa Bongo Fleva, Rashid Makwiro anayefahamika zaidi kwa lakabu ya ‘Chid Benz’ linatajwa kufika tamati na kumuacha huru rapa huyo wa Hip Hop.

Mwenyewe anasimulia safari ngumu ya maisha iliyomfanya kutazamwa kwa jicho lisilopendeza lakini sasa anarejea katika jamii hiyo akiwa mtu wengine na mfano bora baada ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kumkamilishia tiba ya kuacha kutumia dawa za kulevya.


Mhariri |

22/08/2025

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka baadhi ya wafanyabiashara hususani wamiliki wa viwanda kutokukwepa kodi baada ya kubainika kuwa sekta hiyo ina wafanyabiahsara wasio waaminifu wanaokwepa jukumu hilo la kisheria.

Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda ametoa rai hiyo alipozungumza na waandishi wa habari pembezoni mwa mkutano uliowakutanisha na wakuu wa kampuni zilizo chini ya Taasisi ya Sekta binafsi Tanzania (TPSF).


Imehaririwa na

22/08/2025

Shirika la Ufuatiliaji Usalama wa Chakula (IPC) linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa (UN) imethibitisha uwepo wa njaa ya kiwango kikubwa zaidi katika jiji la Gaza kwa mara ya kwanza na kuongeza kuwa zaidi ya raia 500,000 wa Palestina wanakabiliwa na hali mbaya ya njaa, umaskini na vifo.

Taarifa ifuatayo inaeleza kwa kina.


Mhariri |

22/08/2025

Wafuatialiaji na wachambuzi wa siasa nchini wamesema wanatarajia mchujo wa CCM katika nafasi ya Ubunge na Uwakilishi utavinufaisha vyama vingine vya siasa kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinatarajiwa kutangaza majina ya wagombea wa Ubunge na Uwakilishi kufikia Jumamosi Agosti 23, 2025 ikitarajiwa miongoni mwa walioomba uteuzi katika chama hicho hawatopata nafasi kwasababu kila chama kinapaswa kusimamisha mgombea mmoja kwa kila jimbo.


Mhariri |

22/08/2025

Sasa hivi inapatikana kwenye 'platform' ya Android, iOS, Samsung TV, Web pamoja na iPad.

Pia sasa inakuwezesha kujiunga kupitia mitandao ya kijamii na kutengeneza 'profile' zaidi ya moja.


✍ Warda John
Mhariri |

22/08/2025

Wananchi wa Kata ya Migoli wilayani Iringa wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti wanyama wakali hususani viboko na mamba wanaopatikana katika Bwawa la Mtera, wakidai kuwa wamekuwa chanzo cha vifo vya mara kwa mara kwa wakazi wa eneo hilo.


Mhariri | John Mbalamwezi

22/08/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Mhandisi Antony Sanga, ametoa mwezi mmoja kukamilisha utatuzi wa migogoro ya ardhi na ugawaji wa hati katika viwanja 66 vilivyopo Mtaa wa Misitu, Kata ya Kivule, Jijini Dar es Salaam.

Zoezi hili lilitakiwa kukamilika wiki iliyopita, lakini kutokana na idadi kubwa ya wananchi kujitokeza, limelazimika kuongezewa muda.


Mhariri | John Mbalamwezi

22/08/2025

Katika kuimarisha mahusiano ya kibiashara na kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara katika maeneo ya mipakani, Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imeendelea na mazungumzo ya kirafiki na Zambia, yakilenga kutatua changamoto zisizo za kikodi katika mpaka wa Tunduma mkoani Songwe na kuchochea ukuaji wa uchumi pamoja na ustawi wa wananchi wa pande zote.


Mhariri | John Mbalamwezi

Wananchi wa Kata ya Migoli wilayani Iringa wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti wanyama wakali, hususan...
22/08/2025

Wananchi wa Kata ya Migoli wilayani Iringa wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kudhibiti wanyama wakali, hususan viboko na mamba wanaopatikana katika Bwawa la Mtera, wakieleza kuwa wamekuwa chanzo cha vifo vya mara kwa mara kwa wakazi wa eneo hilo.

Ombi hili la wananchi linakuja kufuatia watu wanne kuuawa na viboko mwezi Julai na Agosti mwaka huu.

Nini kifanyike kupunguza vifo vya binadamu vinavyosababishwa na wanyama? Tuandikie maoni yako na tutayasoma saa 7:00

22/08/2025

Maziwa ya mimea yamekuwa chaguo jipya kwa watu wengi wanaotafuta mbadala wa maziwa ya wanyama, hasa kwa sababu ya faida zake kiafya.

Yakitengenezwa kutokana na soya, korosho au nafaka, maziwa haya hubeba virutubisho muhimu k**a vitamini, madini na viambata vya asili vinavyosaidia kuimarisha kinga ya mwili.

Kwa mujibu wa mtaalamu wa lishe, Dkt. Leonard Rweyemamu viambata vya mimea vilivyomo kwenye maziwa haya huchangia kupunguza uvimbe mwilini, kusaidia usagaji chakula na hata kupunguza hatari ya kupata saratani kwa kuzuia ukuaji wa chembe hatarishi.


✍Nifa Omary
Mhariri | John Mbalamwezi

22/08/2025

Umewahi kuyaona au kutumia maziwa yanayotengenezwa kutokana na mimea k**a soya, karanga, mchele au n**i?

Mzalishaji wa maziwa hayo, Dkt. Leonard Rweyemamu, anaeleza kuwa maziwa haya yana faida nyingi kiafya kwa mtumiaji. Msikilize hapa.


✍Nifa Omary
Mhariri | John Mbalamwezi

Address

Mandela Road

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Tuesday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Wednesday 20:00 - 21:00
Thursday 09:00 - 17:00
20:00 - 21:00
Friday 06:00 - 21:00
Saturday 20:00 - 21:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UTVTZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UTVTZ:

Shortcuts

  • Address
  • Opening Hours
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share