06/06/2026
Daktari Bingwa wa Macho, Majala Jafari Majara amesema kuwa kuvaa miwani kwa ajili ya urembo si jambo baya, kwani watu wengi huivaa ili kuboresha mwonekano wao na kuongeza mvuto. Hata hivyo, ameeleza kuwa baadhi ya watu hununua miwani hiyo kwa kuzingatia zaidi muonekano wake bila kujiridhisha kuhusu usalama na ubora wake.
Dkt. Majala amesisitiza umuhimu wa kupeleka miwani ya urembo kwa mtaalamu wa macho kwa ajili ya uchunguzi kabla ya kuitumia. Kulingana naye, hatua hiyo inaweza kusaidia kubaini k**a miwani hiyo ni salama kwa macho na inakidhi viwango vinavyohitajika vya matumizi.
Amefafanua kuwa baadhi ya miwani inayopatikana sokoni huenda ikawa ilitumika awali katika nchi nyingine na baadaye kuingia katika masoko ya Afrika. Kutokana na hali hiyo, ni muhimu kufahamu historia na ubora wa miwani hiyo ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kwa afya ya macho.
✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri | John Mbalamwezi
Mbaya