Nipashe

Nipashe Nipashe - Mwanga wa Jamii - Most reliable Kiswahili newspaper in Tanzania. YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCsp4pNVOxIl6RzKIZwzsRfQ

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amemsimamisha kazi Waziri wa Elimu ya juu Nobuhle Nkabane, baada ya mshirika mkuu ...
22/07/2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amemsimamisha kazi Waziri wa Elimu ya juu Nobuhle Nkabane, baada ya mshirika mkuu wa muungano wa chama chake kumtuhumu kwa utovu wa nidhamu.

Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi yake, kuondolewa kwa Nkabane kutoka wadhifa wake kunaweza kusaidia kupunguza mvutano kati ya chama cha Ramaphosa cha African National Congress (ANC) na Democratic Alliance (DA), vyama viwili vikubwa katika serikali ya mseto, kabla ya kura ya bajeti wiki hii.

Chama cha DA kinadai kuwa Nkabane amesaidia mhandisi uteuzi wa watu waliounganishwa na ANC kwenye bodi za mashirika ya kukuza ujuzi na alidanganya bunge kuficha hilo.

Nkabane amekanusha madai dhidi yake, kulingana na kituo cha televisheni cha ndani cha eNCA. Akisema katika taarifa kwamba imekuwa ni fursa nzuri kuhudumu katika nafasi yake.

Pia imeelezwa kuwa chama hicho kilizidisha ukosoaji wake dhidi ya waziri huyo baada ya Ramaphosa kumfukuza kazi naibu waziri wake wa biashara kwa kutopokea kibali cha rais kwa safari ya nje ya nchi, katika mzozo wa hivi karibuni kati ya vyama viwili vikuu vinavyoongoza.

Imeandikwa na Mwandishi Wetu



Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dk. Fred Msemwa (Kushoto) akutana na Mkuu wa Huduma wa Mfuko wa Ushirikiano...
22/07/2025

Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dk. Fred Msemwa (Kushoto) akutana na Mkuu wa Huduma wa Mfuko wa Ushirikiano na Udhamini wa Miradi wa Umoja wa Mataifa(UN), Dk. John Gilroy katika Ofisi za Umoja wa Mataifa, jijini New York.

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewasili nchini Belarus kuanza ziara ya kikazi nchini humo ambako amepokelewa na Naibu Waz...
22/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amewasili nchini Belarus kuanza ziara ya kikazi nchini humo ambako amepokelewa na Naibu Waziri Mkuu wa Beralus, Viktor Karankevich kwenye Uwanja wa Ndege wa Kinsk.

Katika ziara hiyo, Waziri Majaliwa ameambatana na Balozi wa Tanzania, Russia na Belarusi, Frederick Kibuta, Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Shariff Ali Shariff na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Cosato Chumi.

Imeandikwa na Mwandishi Wetu


Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Wilaya y...
22/07/2025

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Wilaya ya Wanging’ombe na Halmashauri ya Mji wa Makambako, mkoani Njombe, na kumuagiza mkandarasi Larsen & Toubro Limited kuongeza kasi ya utekelezaji kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama kwa wakati.https://www.ippmedia.com/nipashe/habari/kitaifa/read/waziri-aweso-amkalia-kooni-mkandarasi-mradi-wa-maji-wangingombe-2025-07-22-175528

22/07/2025

Taharuki imetanda kwa wakazi wa Mtaa wa Majengo B, Kata ya Kalobe, jijini Mbeya baada ya watu wasiojulikana kumuua kwa kumchoma moto Luth Mtawa (70), chanzo kikidaiwa kuwa ni migogoro ya ardhi.

Imeandikwa Na Nebart Msokwa

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.

 #𝐓𝐞𝐭𝐞𝐬𝐢 𝐳𝐚 𝐉𝐚𝐬𝐮𝐬𝐢 𝐥𝐚 𝐒𝐨𝐤𝐚: Timu ya Maghreb Fez ya Morocco imewasilisha ofa rasmi kwa Klabu ya Simba SC kwa lengo la kum...
22/07/2025

#𝐓𝐞𝐭𝐞𝐬𝐢 𝐳𝐚 𝐉𝐚𝐬𝐮𝐬𝐢 𝐥𝐚 𝐒𝐨𝐤𝐚: Timu ya Maghreb Fez ya Morocco imewasilisha ofa rasmi kwa Klabu ya Simba SC kwa lengo la kumsajili mshambuliaji hatari wa timu hiyo, Lionel Ateba.

Kocha mkuu wa timu hiyo, Pablo Franco Martin, amemweka Ateba kwenye orodha ya wachezaji anaowahitaji kwa msimu ujao, akivutiwa na kiwango bora alichokionyesha akiwa na Wekundu wa Msimbazi.

Ateba alikuwa na kiwango bora katika Ligi Kuu Tanzania Bara, na mchango wake kwenye kikosi cha Simba umevutia macho ya vilabu kadhaa barani Afrika na nje ya mipaka.

𝗜𝗺𝗲𝗮𝗻𝗱𝗮𝗹𝗶𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗝𝗮𝘀𝘂𝘀𝗶 𝗹𝗮 𝗦𝗼𝗸𝗮, 𝗛𝗮𝗹𝗳𝗮𝗻 𝗖𝗵𝘂𝘀𝗶

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.

Mapigano mapya yameibuka tena katika eneo la Kivu Kusini kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na waasi wa M23 ...
22/07/2025

Mapigano mapya yameibuka tena katika eneo la Kivu Kusini kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na waasi wa M23 ikiwa ni siku mbili pekee zimepite baada ya kusainiwa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa pande zote mbili, hali ambayo imeibua sintofahamu.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani, katika eneo la Uvira na Rurambo, milio ya risasi na mizinga imekuwa ikisikika kwa nyakati tofauti tangu usiku wa kuamkia juzi hali iliyowalazimu mamia ya wakazi kuyahama makazi yao na kutafuta hifadhi maeneo ya milimani karibu na mpaka wa Burundi.

Aline Mbusa, mama wa watoto watatu mkazi wa Rurambo aliyekimbilia eneo la Lemera amesema “Hatukutegemea k**a mapigano yangerudi haraka namna hii. Tulidhani baada ya Doha, hatimaye tungeweza kulala kwa amani.”

Hata hivyo, makubaliano ya Doha yalilenga kufungua njia ya mazungumzo ya kina, usitishwaji wa uhasama, na kuandaa mazingira ya kuwarejesha wakimbizi waliokimbia machafuko ya miezi ya nyuma.

Imeandikwa na Mwandishi Wetu





Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nipashe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nipashe:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share