Nipashe

Nipashe Nipashe - Mwanga wa Jamii - Most reliable Kiswahili newspaper in Tanzania. YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCsp4pNVOxIl6RzKIZwzsRfQ

27/11/2025

Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan, anatoa msukumo mkubwa kuhakikisha umeme unawafikia wananchi kote nchini kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Kauli hiyo ameitoa leo Novemba 27, 2025, wakati wa ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma, ambapo ametaka kuona kazi inakamilika kwa wakati na viwango vinavyotakiwa.

Amesema Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ya uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme kwa ufanisi mkubwa, hatua inayoliwezesha taifa kusonga mbele katika kujenga mfumo madhubuti wa upatikanaji wa nishati ya umeme.

Ndejembi amebainisha kuwa mradi huo mkubwa unatekelezwa kwa fedha za ndani, na hadi kukamilika kwake utagharimu takribani shilingi bilioni 556.

“Niwaagize TANESCO kuendelea kumsimamia Mkandarasi kuhakikisha kazi inakamilika kulingana na ratiba. Hatutaki kufika mwisho wa utekelezaji na kukuta mradi umekabidhiwa bila kukamilika,” amesisitiza Waziri Ndejembi.

Imeandikwa| Mwandishi Wetu

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), imetoa mashine mbili kutunzia watoto wanaozaliwa kabla ya mu...
27/11/2025

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), imetoa mashine mbili kutunzia watoto wanaozaliwa kabla ya muda wao ili kusaidia kukabiliana na changamoto hiyo nchini.

Imeelezwa kuwa mashine hizo zinasaidia ukuaji wa watoto hao kwa kuwaongezea joto, na kwamba zimekabidhiwa kwa General Hospital inayotajwa kupokea takribani watoto njiti 60 kila mwezi.

Akizungumza jana Dodoma wakati wa kupokea mashine hiyo Mganga Mfawidhi wa Hospitality hiyo Dk. Erenest Ibenzi, alisema “Tunaishkuru sana TAKUKURU kwa kuleta mashine huzo nao wamekuwa ni sehemu ya familia ya hospitali kutokana na kushirikiana nao katika mambo mbalimbali ya kitabibu.”

Amesema pamoja na kuzidi idadi ya kupokea watoto hao, lakini hospitality hiyo inafanya kadri ya uwezo wao kuhakikisha watoto hao wanakuwa sawa.

Naye, Mkurugenzi wa TAKUKURU Francis Chalamila amesema mashine hiyo ni ya nane kukabidhi katika hospitali ya mkoa kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaozaliwa njiti katika maeneo mbalimbali.

Amesema wameamua kushirikiana na hospitali mbalimbali na kutoa mchango wao baada ya kufanya utafiti na kuona kuna uhaba wa mashine hizo.

Amesema lengo ni kusaidia hospitali zote za mikoa nchini na kwamba gharama zinazotumika kununulia mashine hizo, ni fedha ambazo zinachangwa na watumishi wa taasisi hiyo.

Imeandikwa|Renatha Msungu, Dodoma

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.


Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime, ametoa wito kwa vyombo vya habari nchini kuhakikisha vinaandika na kuripoti ta...
27/11/2025

Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime, ametoa wito kwa vyombo vya habari nchini kuhakikisha vinaandika na kuripoti taarifa kutoka katika vyanzo sahihi na vya kuaminika, ili kuepusha kuzua taharuki katika jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma katika kikao cha siku moja kilichoandaliwa na Misa Tanzania, Misime amesema kumekuwa na ongezeko la taarifa zisizo na uhakika kusambazwa kupitia baadhi ya majukwaa na mitandao ya kijamii hali inayoweza kuhatarisha usalama na amani nchini.

“Wajibu wa chombo cha habari ni kuelimisha, kuhabarisha na kujenga jamii badala ya kusambaza taarifa zinazoibua hofu isiyo ya lazima,” amesema.

Aidha, Misime ameeleza kuwa mara nyingi taarifa zinazokosa uthibitisho zimekuwa zikitumiwa vibaya na watu wenye nia ya kupotosha au kuleta misukosuko, hivyo kuviomba vyombo vya habari kufanya uchambuzi na uhakiki wa kina kabla ya kuchapisha au kurusha taarifa yoyote.

Pia amewahimiza kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi na taasisi nyingine za serikali ili kuongeza uaminifu kwa wananchi na kupunguza mkanganyiko, huku akitoa wito kwa wananchi kuwa makini na taarifa wanazozisambaza, kwakuwa kila mtu ana jukumu la kulinda amani na utulivu wa taifa.

Imeandikwa na Shabani Njia, Dodoma

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.


Address

The Guardian Limited
Dar Es Salaam
31042,DSM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nipashe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nipashe:

Share