Nipashe

Nipashe Nipashe - Mwanga wa Jamii - Most reliable Kiswahili newspaper in Tanzania. YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCsp4pNVOxIl6RzKIZwzsRfQ

"Natambua pia yapo maeneo yenye changamoto kati ya wakulima na wafugaji ikiwemo Nanyumbu na maeneo mengine lakini tunaya...
26/09/2025

"Natambua pia yapo maeneo yenye changamoto kati ya wakulima na wafugaji ikiwemo Nanyumbu na maeneo mengine lakini tunayafanyia kazi na moja kati ya hatua tunazizichukua mkitupa ridhaa ndani ya miaka mitano ijayo ni pamoja na kuendelea kupima maeneo ya wafugaji kila tutakapopata eneo na nilisema tutatoka ekari Milioni tatu kwenda mpaka sita.

"Hiyo ni ili wafugaji wapate maeneo maalumu wakafuge kitaalamu na wakulima waendelee na kilimo chao," Dk. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM akizungumza na wananchi wa Mtwara Mjini leo.

Ameongeza akisema; "Mkitupa ridhaa na tunapoendelea mbele tutaendelea kutafuta masoko ya uhakika na sio tu kwa Korosho lakini kwa mazao yote tunayozalisha nchini ikiwemo ufuta na mbaazi na tutaendelea kuvutia wawekezaji kwaajili ya ujenzi wa viwanda vya kuchakata korosho katika Kongani ya viwanda iliyopo pale kijiji cha Maranje katika Wilaya ya Mtwara.

"Tutaendelea pia kusimamia kwa karibu vyama vya Ushirika ili kuondoa ubadhirifu wa fedha za washirika lakini pia ucheleweshaji wa malipo kwa wakulima. Tunavijenga viwe taasisi tunazoweza kuzitegemea katika uendeshaji wa kilimo chetu nchini. Katika hatua nyingine k**a mnavyojua tumeanzisha benki ya ushirika ili iweze kutoa huduma bora kwa vyama vya ushirika katika kuendeleza kilimo chetu," amesema Dk. Samia.

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.



Ukraine imeendeleza mashambulizi yake ya kimfumo dhidi ya sekta ya mafuta ya Urusi ikilenga kiwanda cha kusafisha mafuta...
26/09/2025

Ukraine imeendeleza mashambulizi yake ya kimfumo dhidi ya sekta ya mafuta ya Urusi ikilenga kiwanda cha kusafisha mafuta katika eneo la kusini, haya ni kwa mujibu wa mamlaka ya Urusi wakati ambapo inasubiri silaha zaidi kutoka kwa washirika wake ikiwamo Marekani.

Mamlaka hiyo ya Urusi katika eneo la Krasnodar, imeripoti kuzuka kwa moto mdogo kwenye kiwanda cha kusafisha mafuta cha Afipski na kusema sehemu za droni moja ziliangukia kiwanda hicho.

Wataalamu wanakadiria kuwa Urusi imepoteza takriban robo ya uwezo wake wa usindikaji kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya viwanda vya kusafisha mafuta, vituo vya mafuta na vya upakiaji. Hali hii imesababisha uhaba wa dizeli na petroli katika baadhi ya mikoa.

Chanzo: DW



Mgombea Urais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan amesema tangu kuanza kwa mpango wa serikali wa kutoa ruzuku za mbolea pamoj...
26/09/2025

Mgombea Urais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan amesema tangu kuanza kwa mpango wa serikali wa kutoa ruzuku za mbolea pamoja na pembejezo za Kilimo mwaka 2021/22, serikali imetumia takribani Sh. Bilioni 726 kwaajili ya kunufaisha wakulima wa Tanzania.

Akiomba kura kwa mamia ya wananchi wa Mtwara leo Septemba 26, 2025 Dk. Samia ameeleza dhamira yake ikiwa wananchi wataendelea kukipa ridhaa Chama Cha Mapinduzi ni kuendelea kuongeza kiwango hicho cha ruzuku ili kukuza uzalishaji na kuongeza tija kwa wakulima.

"Tunatumia Sh. Bilioni 152 kila mwaka fedha ambayo ingetoka mfukoni kwa mkulima lakini tumeibakisha mifukoni kwao na serikali tunagawa kwa ruzuku ya nusu bei na pembejeo nyingine ni bure kabisa k**a salfa, dawa za kuulia wadudu na blight na tunafanya hivyo kwasababu tumedhamiria kukuza kilimo na uzalishaji wa Korosho.

"Kwa hakika uzalishaji tumeuona ikiwemo kwenye zao la korosho kutoka tani 118, 811 mwaka 2020/21 zikiwa na thamani ya Sh. Bilioni 265 na leo mwaka 2024/25 tunazungumzia uzalishaji wa tani 330, 505 zikiuzwa Sh. Trilioni moja na Bilioni 900." amesema Dk. Samia.

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.



Mgombea urais kupitia Chama cha ADA TADEA, George Bussungu, amesema iwapo atachaguliwa, serikali yake itajenga mji maalu...
26/09/2025

Mgombea urais kupitia Chama cha ADA TADEA, George Bussungu, amesema iwapo atachaguliwa, serikali yake itajenga mji maalum wa teknolojia unaoitwa Bongo Technological City, ambapo vijana wenye vipaji kutoka mikoa yote watapelekwa kwenda kuvumbua na kuendeleza miradi mbalimbali ya kiteknolojia.

Akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Singida kwenye stendi ya zamani, Bussungu amesema:

“Mkitupa ridhaa tutajenga mji maalum wa teknolojia ambao tutauita Bongo Technological City, watoto wote vijana wote wenye bongo wenye akili nyingi watakuwa wanabebwa na kupelekwa kule wakavumbue mambo,” amesema.

Imeandikwa na Thobias Mwanakatwe,SINGIDA

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.

Address

The Guardian Limited
Dar Es Salaam
31042,DSM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nipashe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nipashe:

Share