Nipashe

Nipashe Nipashe - Mwanga wa Jamii - Most reliable Kiswahili newspaper in Tanzania. YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCsp4pNVOxIl6RzKIZwzsRfQ

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo...
17/01/2026

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.WhatsApp 0715086344

Januari 17, 2026

Vijana 5746 wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya Uanagenzi katika vyuo 47 hapa nchini kwa ajili ya kupata ujuzi utakaowa...
16/01/2026

Vijana 5746 wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya Uanagenzi katika vyuo 47 hapa nchini kwa ajili ya kupata ujuzi utakaowawezesha kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Vijana hao wamepata fursa hiyo ya kushiriki mafunzo hayo, baada ya ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano kutoa tangazo kwa umma kuhusu vijana kushiriki mafunzo ya ufundi stadi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Ajira na Mahusiano,Deus Sangu amesema vijana hao wanatakiwa kuripoti katika vyuo hivyo kuanzia Januari 19 ili kuanza masomo ya fani tofauti walizoomba.

"Vijana wote waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti katika vyuo hivyo kuanzia Januari 19 ili kuanza masomo ya fani mbali mbali walizoomba, zikiwemo za ubunifu " amesema Sangu.

Ametaja fani nyingine ambazo vijana hao watapata ujuzi ni zile za ushonaji nguo, ufundi bomba, uashi, useremala, uchomeleaji , uungaji vyuma, upakaji rangi, ufundi magari na mitambo, umeme wa majumbani na viwandani pamoja na fani nyingine.

Imeandikwa na Renatha Msungu, Dodoma

Soma zaidi kupitia www.ippmedia.com



16/01/2026

Wakati wa ujauzito elimu kiafya ni muhimu kwa kipindi hicho.

Mkunga Mbobezi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, Lidya Massae, anafafanua kuhusu dalili za hatari, kwa mjamzito.

Imeandaliwa na Christina Mwakangale

Zaidi ya wakazi milioni 1.2 wa wilaya za Mpwapwa na Kongwa mkoani Dodoma pamoja na Wilaya ya Kilolo na baadhi ya maeneo ...
16/01/2026

Zaidi ya wakazi milioni 1.2 wa wilaya za Mpwapwa na Kongwa mkoani Dodoma pamoja na Wilaya ya Kilolo na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Iringa wanatarajiwa kunufaika na upatikanaji wa umeme wa uhakika baada ya kukamilika kwa kituo cha kupooza na kusambaza umeme cha Mtera kilichojengwa kwa gharama ya Sh bilioni 9.2.

Mradi huo umejengwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Serikali za Sweden na Norway, ukiwa na lengo la kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara iliyokuwa ikiathiri shughuli za kiuchumi na huduma za kijamii katika maeneo hayo.

Akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho, Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kukamilika kwa mradi huo kutawezesha usambazaji wa umeme wa uhakika baada ya awali umeme kusafirishwa umbali mrefu kabla ya kuwafikia wananchi, hali iliyosababisha upungufu wa nguvu za umeme.

Amesema mradi huo unaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kukuza uchumi wa nchi kupitia uimarishaji wa miundombinu ya umeme, hususan katika maeneo ya vijijini.

Soma zaidi kupitia www.ippmedia.com

Imeandikwa na Rehema Matowo, Dodoma



16/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watu watano kwa tuhuma za kumuua Hamza Malingumu (20) katika eneo la Lukobe Manispaa ya Morogoro.

Polisi wamesema marehemu aliuawa baada ya kudhaniwa kuwa ni mwizi. Hata hivyo, mjomba wa marehemu, Ngwenje Mohamed, amesema kijana huyo alikuwa mgonjwa wa akili na alikuwa mgeni maeneo hayo akitokea Kilosa akidai alitoroka nyumbani majira ya saa tisa usiku bila mtu kujua alikokwenda.

"Kumbe walimwitia mwizi na watu kujitokeza na kumpiga hadi kupoteza fahamu,” amesema.

Amesema familia ilijaribu kumkimbiza hospitali, lakini alifariki dunia akiwa njiani. Polisi imesema uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea huku baadhi wakitiwa nguvuni kuhusiana na tukio hilo.

Imeandaliwa na Christina Haule na Idda Mushi, Morogoro



Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema hakuna tatizo kwa Serikali ya nchi hiyo kuzima mtandao kwa kuwa wao ndio waliout...
16/01/2026

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema hakuna tatizo kwa Serikali ya nchi hiyo kuzima mtandao kwa kuwa wao ndio walioutengeneza na hivyo pale wanapoona inafaa hawana budi kuuzima.

Amesema hayo katika mahojiano yake na chombo kimoja cha kimataifa wakati huu ambapo kura zinaendelea kuhesabiwa huku akielezwa kuongoza dhidi ya mpinzani wake Robert Kyagulanyi (BobiWine).

"Sisi ndio tulioujenga huo mtandao ambao wewe unauzungumzia kwahiyo kuuzima ni kwasababu ya kushughulika na wahalifu wanaotaka kutuharibia nchi" amesema Museveni.

Tume ya Uchaguzi Uganda inaendelea kupokea matokeo ya uchaguzi uliofanyika jana Alhamisi kutoka vituo mbali mbali vya kupiga kura ambapo matokeo ya awali yaliyotangazwa yanaonesha kuwa Museveni amepata asilimia 76.25 ya kura zilizohesabiwa kufikia sasa kulingana na hesabu kutoka karibu nusu ya vituo vya kupigia kura.

Chanzo: Mtandao



Serikali mkoani Morogoro imeongeza muda wa utambuzi wa miili ya marehemu waliopata ajali ya magari mawili kugongana uso ...
16/01/2026

Serikali mkoani Morogoro imeongeza muda wa utambuzi wa miili ya marehemu waliopata ajali ya magari mawili kugongana uso kwa uso na kuteketea kwa moto kwenye eneo la Maseyu mkoani Morogoro kutokana na miili miwili kati ya 10 kuendelea kubaki kwa siku 16 sasa katika chumba cha kuhifadhia maiti kwenye hospitali ya Rufaa (MRRH).

Kwa Mujibu wa Kaimu Ofisa Mahusiano wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Morogoro Scolastica Ndunga amesema serikali ya mkoa imeamua kuongeza muda kutokana na kuwa miili hiyo kuwa tayari imeshapitisha siku 14 ambazo zimewekwa kitaalamu kwa ajili ya miili yoyote kuzikwa na serikali, ili kusaidia ndugu kujitokeza kwa utambuzi wa miili ikiwa ni pamoja na kupimwa vinasaba (DNA) na kuruhusiwa kwenda kuzika.

"Ni kweli leo ni siku ya 16 tangu ajali hiyo itokee lakini miili miwili bado haijatambuliwa wala ndugu hawajajitokeza kutambua na tayari miili 8 imeshatambuliwa na kwenda kusitiriwa na ndugu zao baada ya kupima vinasaba, miili miwili iliyobaki ni ya jinsia ya kiume na Mkuu wa mkoa wa Morogoro Adam Malima ametoa agizo kuwa siku ziongezwe kwa ajili ya utambuzi wa miili hiyo". Amesema Scolastica.

Akizungumzia hali za majeruhi Scolastica amesema majeruhi mmoja anayejulikana kwa jina la Hadija Suleiman (23) kati ya majeruhi 23 wa ajali hiyo amebaki akipatiwa matibabu kwenye hospitali hiyo na kwamba anaendelea vizuri ambapo tayari ameshafanyiwa upasuaji wa mifupa kwa mara ya pili.

Ajali hiyo ilitokea Desemba 31 mwaka jana majira ya usiku katika kijiji cha Maseyu Kata ya Gwata mkoani Morogoro.

Imeandikwa na Christina Haule, Morogoro



16/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Doto Lubongeja, mkazi wa Kijiji cha Madundasi, Wilaya ya Mbarali, kwa tuhuma za kuwaua watoto watatu wa familia moja kwa kuwanyonga shingo.

Watoto hao ni Petro Amosi (8), Samu Amosi (6) na Nkamba Amosi (4), waliokuwa wakichunga ng’ombe eneo la jirani na nyumbani kwao.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Wilbert Siwa, amesema tukio hilo lilitokea Januari 15, 2026, ambapo mtuhumiwa aliwaua watoto hao na baadaye kuiba ng’ombe 15 waliokuwa wakichungwa.

Amesema baada ya tukio, mtuhumiwa alificha ng’ombe hao nyumbani kwa mjomba wake, Masoda K***a, Kijiji cha Madundasi “B”, na kufanikiwa kuwauza kwa shilingi milioni tano.

Polisi walifanya msako na kuwakamata watuhumiwa wawili hao, kurejesha ng’ombe wote 15 pamoja na fedha taslimu shilingi milioni tano.

“Uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha tukio kuwa ni tamaa ya kujipatia mali kwa njia isiyo halali, upelelezi unaendelea kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria, tunatoa wito kwa jamii kujiepusha na uhalifu na ukatili dhidi ya watoto,” amesema Kamanda Siwa.

Imeandikwa na Grace Mwakalinga



"Tumelipa gharama kubwa kwa mapambano haya ya kidemokrasia, tumepoteza baadhi ya mashujaa wetu wengi, tumeshuhudia kupot...
16/01/2026

"Tumelipa gharama kubwa kwa mapambano haya ya kidemokrasia, tumepoteza baadhi ya mashujaa wetu wengi, tumeshuhudia kupotea kwa makamanda wetu akina Ben Saanane, Dionis Kipanya, Deusdedith Soka na wengine."

"Hadi leo haijulikani wako wapi lakini pamoja na hayo yote CHADEMA haijafa badala yake imezidi kuimarika ni kwasababu tuna watu na tuna ujasiri wa kusema tutashinda kwani hakuna marefu yasiyokuwa na ncha kwahiyo iko siku tutashinda"-Amani Golugwa, Naibu Katibu Mkuu, CHADEMA Bara.



16/01/2026

Moto mkali umeibuka kwenye ghorofa moja lililopo maeneo ya Posta, Samora, Ilala jijini Dar es Salaam

VIDEO: GRACE MWAKALINGA



"Ulimwengu unahitaji kujua kilichoendelea Uganda kuanzia siku ya uchaguzi. Mtandao umezimwa. Kujazwa kwa kura nyingi kum...
16/01/2026

"Ulimwengu unahitaji kujua kilichoendelea Uganda kuanzia siku ya uchaguzi. Mtandao umezimwa. Kujazwa kwa kura nyingi kumeripotiwa kila mahali. Viongozi wetu, akiwemo Naibu Rais wa Kanda ya Magharibi, walikamatwa. Wengi wa mawakala wetu katika vituo vya kupigia kura na wasimamizi walitekwa nyara, na wengine wakafukuzwa katika vituo vya kupigia kura. Mashine za kielektroniki zimeshindwa kila mahali."-Mgombea Urais wa Uganda Robert Kyagulanyi (BobiWine).



Address

The Guardian Limited
Dar Es Salaam
31042,DSM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nipashe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nipashe:

Share