Nipashe

Nipashe Nipashe - Mwanga wa Jamii - Most reliable Kiswahili newspaper in Tanzania. YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCsp4pNVOxIl6RzKIZwzsRfQ

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo...
10/06/2026

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.WhatsApp 0715086344

Juni 11, 2026

‎Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha, ameupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa hatua ...
10/06/2026

‎Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha, ameupongeza Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kwa hatua yake ya kutoa mafunzo kwa waajiri, huku akiwataka washiriki kuhakikisha elimu hiyo inaleta tija na kukata mzizi wa urasimu kwa wastaafu katika maeneo yao ya kazi.
‎
‎
‎Macha ametoa pongezi na msisitizo huo mjini Bariadi Juni 10, 2026, wakati akifungua semina maalum ya waajiri iliyoandaliwa na PSSSF, iliyolenga kuwajengea uwezo maafisa wanaoshughulikia masuala ya wanachama mkoa wa Simiyu ili kuboresha utoaji wa huduma.
‎
‎Akizungumza juu ya maboresho ya huduma, Mkuu wa Mkoa alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye mifumo ya kidigitali na kusisitiza kuwa maafisa hao wanapaswa kutumia teknolojia hiyo kwa weledi ili kuondoa visingizio vinavyokwamisha na kuchelewesha huduma kwa wastaafu.
‎
‎
‎Ili kuhakikisha watumishi wanapata haki zao kwa wakati pindi wanapostaafu bila usumbufu.
‎
‎
‎Macha aliwaagiza waajiri wote mkoani Simiyu kuhakikisha kuwa michango ya watumishi inawasilishwa kwa wakati ili kuzuia changamoto ya mapengo ya michango.
‎
‎
‎Mkuu huyo wa mkoa alitoa onyo kwa watumishi wanaobadili majina kiholela wanapokaribia kustaafu, akibainisha kuwa jambo hilo linarudisha nyuma michakato ya kiserikali na kuongeza ugumu na kuleta ulazima wa kuwepo viapo vya ziada.
‎
‎
‎Katika kuunga mkono hitaji la kuwa na utendaji wenye tija na uadilifu, Mkuu wa Mkoa aliwakumbusha washiriki kuwa uzee haukwepeki, na kwamba maandalizi ya kustaafu salama yanategemea jinsi wanavyowatendea haki wastaafu wa sasa.
‎
‎
‎"Nawaasa washiriki kuachana kabisa na vitendo vya rushwa, hasa kwa hawa wazee ambao haki wanayoitafuta ni kwa ajili ya kuweza kujikimu na maisha yao yaliyosalia. Rushwa ya namna hii haiwezi kuwaacha salama wale walioipokea," alionya.
‎
‎
‎Kwa upande wake, Meneja wa PSSSF Mkoa wa Simiyu, Salumu Miraji, alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa utayari wake wa kuunga mkono juhudi za Mfuko na kufungua semina hiyo, huku akibainisha kuwa washiriki watapata elimu ya kina itakayowawezesha kuwaongezea ufanisi zaidi katika kuwahudumia wanachama na wastaafu.
‎
‎Miraji alisisitiza kuwa mafunzo hayo yatawafanya maafisa hao kuwa mabalozi wazuri wa PSSSF katika maeneo yao ya kazi, jambo ambalo litarahisisha utatuzi wa changamoto za wanachama na kusogeza huduma bora karibu zaidi na watumishi na wastaafu wa mkoa huo.
‎
‎Imeandikwa| Mwandishi Wetu
‎
‎Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.
‎
‎
‎

10/06/2026

‎Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) linaendelea kuratibu mashindano ya ujuzi na ubobezi katika fani mbalimbali za ufundi stadi, yakilenga kuibua vipaji na kuandaa vijana watakaoiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kikanda na kimataifa.
‎
‎Akizungumza wakati wa mashindano ya ubunifu wa ushonaji wa mavazi yaliyofanyika katika Chuo cha Anna Collection Academy jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora wa NACTVET, Joffrey Oleke, amesema mashindano hayo yalianza katika ngazi ya vyuo kabla ya kuendelea katika hatua za kanda na baadaye taifa.
‎
‎Amesema Tanzania inatarajia kushiriki mashindano ya ubunifu na ubobezi katika fani tisa tofauti, ambapo washindi wa ngazi za kanda watashindana katika hatua ya taifa kabla ya kuchaguliwa kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kimataifa.
‎
‎Katika mashindano ya Kanda ya Dar es Salaam ya ubunifu wa ushonaji wa mavazi, washiriki tisa kutoka vyuo mbalimbali walionyesha umahiri wao katika kubuni, kukata na kushona mavazi kwa kuzingatia viwango vya kimataifa.
‎
‎Mdhibiti Ubora Mkuu wa NACTVET Kanda ya Mashariki, Nicholaus Moshi, amesema mashindano hayo ni jukwaa muhimu la kukuza ubunifu, kuibua vipaji na kuwajengea vijana uwezo wa kushindana katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi.
‎
‎
‎Imeandikwa| Mwandishi Wetu
‎
‎Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi 📞+255 745 -700 710 au 0677- 020 701 kwa maelezo zaidi.
‎
‎

Wadau wa elimu nchini wamesisitiza umuhimu wa uongozi wa kimkakati katika kuimarisha utendaji wa taasisi za umma na kufa...
10/06/2026

Wadau wa elimu nchini wamesisitiza umuhimu wa uongozi wa kimkakati katika kuimarisha utendaji wa taasisi za umma na kufanikisha malengo ya maendeleo ya sekta ya elimu.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu, Dk. Maulid Maulid ameyasema hayo leo walati akifungua mafunzo ya uongozi wa kimkakati kwa viongozi wa shule za sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, yakiwakutanisha washiriki 44 wakiwemo Wakuu wa Shule za Sekondari 22 na makamu wakuu 22.

Mafunzo hayo yanatolewa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu kwa kushirikiana na African Centre for School Leadership (ACSL).

“Uongozi wa kimkakati ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha taasisi za umma zinafikia malengo yake kwa ufanisi. Viongozi wanapaswa kuwa na uwezo wa kutazama mbele, kupanga kwa weledi na kusimamia rasilimali zilizopo ili kuleta matokeo chanya kwa taasisi wanazoziongoza,” amesema Dk. Maulid.

Aidha, ameeleza kuwa mafunzo hayo yanatekelezwa kwa kutumia mfumo wa kisasa wa ufundishaji unaowapa washiriki fursa ya kujifunza kwa vitendo, kubadilishana uzoefu na kupata maarifa yatakayowawezesha kukabiliana na changamoto za kiuongozi katika mazingira yao ya kazi.

“Mafunzo haya yanaendeshwa kwa mfumo wa kisasa utakaohakikisha kunakuwa na mawasiliano ya mara kwa mara, lengo kuu likiwa ni kutoa nafasi kwa washiriki kutoa mrejesho kwa wazeshaji kuhusiana na maendeleo ya utekelezaji wa mada. Tunatarajia washiriki wote watatumia kikamilifu fursa hii kujifunza na kujijengea uwezo zaidi,” amesema.

Kadhalika, Mtendaji Mkuu huyo amebainisha kuwa washiriki watakaofanya vizuri katika mafunzo hayo watatambuliwa na kutunukiwa vyeti, hatua inayolenga kuongeza motisha na kuhamasisha ushiriki wenye tija katika mchakato mzima wa kujifunza.

Sambamba na hilo, Dk. Maulid amesisitiza umuhimu wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa maarifa na ujuzi unaotolewa katika mafunzo hayo, akieleza kuwa mafanikio ya programu hiyo yatapimwa kupitia mabadiliko chanya yatakayoonekana katika usimamizi na utendaji wa shule husika.

Imeandikwa na Mwandishi Wetu

Tembelea http://epaper.ippmedia.com kusoma gazeti lako au wasiliana nasi +255 745-700 710 au 0677-020 701 kwa maelezo zaidi.


Address

The Guardian Limited
Dar Es Salaam
31042,DSM

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nipashe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nipashe:

Share