Pavea News.

Pavea News. Kwa habari za ukweli na uhakika masaa 24.Fuatilia page hii au bofya link ifuatayo http.www.pavea1.blogspot.com

10/12/2017

*NUKUU ZA NDG. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI, MWENYEKITI WA CCM NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE MKUTANO MKUU WA 9 WA UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)*

Disemba 10, 2017.
Dodoma.

1. "Ni ukweli usiopingika kuwa, uhai na ustawi wa taifa lolote duniani ni vijana, hii inatokana na sababu moja vijana ni kundi kubwa" JPM

2. "Chama kinapokuwa na vijana wengi walio hamasika ndio usalama wa chama na taifa " JPM

3. "Napenda mfahamu ujana pekee haikufanyi uwe hazina ila ili uwe hazina inakupasa uwe mzalendo, muadilifu, nidhamu, utu, mchapakazi, mtii, mwenye kupenda kujielimisha na mwenye udhutu wakuleta fikra mpya na siyo kijana legelege".JPM

4. "Kijana ambaye ni mpenda rushwa, mwizi, fisadi, tapeli, mtumia madawa ya kulevya hana mchango wowote kwa taifa na hata kwa chama".JPM

5. "Uchaguzi huu ni muhimu sana kwa sababu Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) ni chombo muhimu sana katika chama". JPM

6. "Muelekeo wa Umoja wa Vijana tuliokuwa tunaujua, siyo muelekeo tulionao sasa".JPM

7. "Ni lazima wajumbe mlioko hapa mumtangulize Mungu mbele, na mtambue jukumu lenu kwa Vijana wote wa Tanzania".JPM

8. "Nitashangaa sana k**a leo mtaniletea Mwenyekiti aliyewahonga, kuwahonga ni kushusha thamani yenu, na ni dalili ya kuonesha hatokuwa kiongozi mzuri".JPM

9. "Mwenyekiti wa Vijana anayetakiwa ni mmoja tu, makabila ya watanzania ni zaidi ya 120 hamuwezi kuchagua kwa kabila na mkifanye hivyo hamtafanikiwa kupata kiongozi".JPM

10. "Mkachague viongozi waadilifu, wanyenyekevu, wachapakazi, wenye kuchukizwa na rushwa watawavusha. Ninyi muwaelekeze viongozi pakwenda siyo
wao wawaelekeze pakwenda".JPM

11. "Umoja wa Vijana limekuwa ni kundi la kuwazuia vijana wengine wasiingie, kila mwenye uwezo amekuwa akiwekewa vigingi vya kila aina". JPM

12. "Nawaomba Ndugu zangu vijana msitengeneze ukuta na vijana wenzenu taifa hili ni lenu wote". JPM

13. "Viongozi wakiwa wanyonge na wachini wanakuwa wanyonge zaidi, Vijana wa CCM niwaombe mjiamini mmekuwa wanyonge sana".JPM

14. "Ifike wakati viongozi wastaafu mrudi kwenye jumuia hii hata mfanye nao mikutano ya kuwahamasisha na kuwatia moyo". JPM

15. "Hii bodi ya Umoja wa Vijana iondoke bodi hii haitusaidii".JPM

16. "Viongozi mtakao wachagua na mliochaguliwa fanyeni tathimini ya mali za Umoja wa vijana ziwe kwenye daftari moja, hapo ndipo mtakuwa mnaweza kujitegemea". JPM

17. "UVCCM iwe sauti ya vijana, mtetezi wa vijana, kimbilio, chemchem ya fikra na chuo cha kuandaa vijana katika uongozi kwa chama na serikali "JPM

18."Chagueni wagombea wenye sifa na uwezo". JPM

19."Tuanzishe ukurasa upya wa Umoja wa Vijana nawapenda sana UVCCM nina wahitaji katika kuleta maendeleo ya Nchi yetu". JPM

20. "Na waahidi kila penye nafasi vijana hatutawasahau".JPM
21." Vijana muwe wenye kujenga hoja na msibweteke, anzisheni miradi tutawasaidia". JPM

22."Ukijituma watu watakuona tu".JPM

23. "Nataka Umoja wa Vijana wenye muelekeo wakushika dola".JPM

Imetolewa na,

IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM).

Tafadhali Hakikisha unasoma Gazeti lako Makini la JAMVI LA HABARI leo.*πŸ‘†πŸ‘‡πŸ‘†πŸ‘‡
31/10/2017

Tafadhali Hakikisha unasoma Gazeti lako Makini la JAMVI LA HABARI leo.*πŸ‘†πŸ‘‡πŸ‘†πŸ‘‡

30/10/2017

Tafadhali Hakikisha unasoma Gazeti lako Makini la JAMVI LA HABARI leo.*πŸ‘†πŸ‘‡πŸ‘†πŸ‘‡
30/10/2017

Tafadhali Hakikisha unasoma Gazeti lako Makini la JAMVI LA HABARI leo.*πŸ‘†πŸ‘‡πŸ‘†πŸ‘‡

Rais Magufuli amtumia ujumbe mfalme wa Oman.Rais John Magufuli leo Oktoba 18, 2017 amemtumia ujumbe Mfalme wa Oman Mtuku...
19/10/2017

Rais Magufuli amtumia ujumbe mfalme wa Oman.

Rais John Magufuli leo Oktoba 18, 2017 amemtumia ujumbe Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said na wawekezaji wengine wa Oman kuwa atafurahi kuona wanakuja kuwezeka nchini tena kwa haraka na kudai serikali itatoa ushirikiano.

Rais ametuma ujumbe huo kwa mfalme wa Oman kupitia kwa Waziri wa Mafuta na Gesi wa Oman Mhe. Dkt. Mohammed Hamad Al Rumhy aliyeongozana na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe. Salem Ben Nasser Al Ismaily na Naibu Waziri wa Utalii Mhe. Maitha Saif Majid, ambao walikua Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mfalme wa Oman Mtukufu Sayyid Qaboos bin Said Al Said amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa nchi hiyo ipo tayari kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuongeza uwekezaji katika viwanda, uzalishaji wa nishati, kuongeza thamani ya madini, kuendeleza sekta ya gesi na mafuta na kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo ili kukuza uchumi kwa kasi zaidi.

β€œMhe. Dkt. Mohamed naomba ukamwambie Mfalme kuwa namshukuru kwa ujumbe huu na namkaribisha sana Tanzania, nimefurahi kuona mpo tayari kushirikiana nasi kujenga viwanda, kuzalisha mazao na kuendeleza ukanda wa uwekezaji wa Bagamoyo, sisi tupo tayari hata leo, njooni tushirikiane kwa sababu nyinyi ni ndugu zetu na tutafanya uwekezaji kwa faida yetu sote” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ametaka Oman iongeze ushirikiano na Tanzania katika masuala ya utalii na usafiri wa anga, kuwekeza katika usindikaji wa nyama na uvuvi na ushirikiano katika kubadilishana wataalamu wa nyanja mbalimbali wakiwemo walimu wa lugha ya Kiswahili na Kiarabu.

Mbali na hilo Rais Magufuli amemshukuru Mfalme wa Oman kwa msaada kujenga visima vya maji 100 hapa nchini na amemuomba kuungana na Serikali katika safari yake ya kuhamia Dodoma kwa kujenga miundombinu itakayoweka kumbukumbu ya ushirikiano wa kidugu na kihistoria kati ya nchi hizi mbili.

WAZIRI MKUU AWAONYA MAWAZIRI.Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaonya mawaziri na kuwataka watumie madaraka yao kwa manufaa...
17/10/2017

WAZIRI MKUU AWAONYA MAWAZIRI.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaonya mawaziri na kuwataka watumie madaraka yao kwa manufaa ya Taifa na kamwe wasiyatumie k**a fursa ya kujitajirisha wao binafsi.

Kassim Majaliwa amesema hayo leo Oktoba 16, 2017 alipozungumza na baadhi ya Mawaziri, Manaibu na Makatibu Wakuu katika kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
Aidha Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli amesisitiza kwamba amewateua ili wafanye kazi na kamwe wasitumie madaraka waliyopewa kwa maslahi yao binafsi.

β€œMadaraka haya ya Uwaziri si fursa ya kujipatia utajiri, tunatakiwa tufanye kazi kwa weledi, uadilifu, bidii na uaminifu mkubwa ili kuondoa kero za wananchi kwa wakati.”

Waziri Mkuu amesema Mawaziri hao wanatakiwa wasimamie utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa Taifa wa miaka kuanzia mwaka 2016/2017 hadi 2020/2021. Pia utekelezaji wa ahadi zote zilizopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 pamoja na ahadi alizozitoa Rais Dkt Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi.

Hata hivyo Waziri Mkuu amewataka Mawaziri hao wakapunguze urasimu katika utekelezaji wa malengo ya Serikali kwa sababu wananchi wanahitaji kuhudumiwa kwa wakati
Mawaziri waliohudhuria kikao hicho ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI Bw. Suileiman Jaffo pamoja na Manaibu wake Bw. Joseph Kandege na Bw. George Kakunda, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi Ummy Mwalimu na Naibu wake Dkt. Faustine Ndungulile.

Wengine ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe na Naibu wake Bw. Jumaa Aweso, Waziri wa Viwanda na Biashara Bw. Charles Mwijabe na Naibu wake Mhandisi Stella Manyanya.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla na Naibu wake Bw. Josephat Hasunga, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako na Naibu wake Bw. William Ole Nasha, Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Bw. Abdallah Ulega pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara hizo.https://pavea1.blogspot.com/2017/10/waziri-mkuu-awaonya-mawaziri.html?m=1

Stephen Wasira asema kuwa, kuikosoa serikali sio jinai na kwamba ni wajibu wa Rais kuwasikiliza wananchi wake. https://t...
16/10/2017

Stephen Wasira asema kuwa, kuikosoa serikali sio jinai na kwamba ni wajibu wa Rais kuwasikiliza wananchi wake. https://t.co/PotElk5MwH

Mahak**a Kuu itaanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu, Elizabeth Michael maarufu k**a...
16/10/2017

Mahak**a Kuu itaanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya mauaji inayomkabili msanii wa filamu, Elizabeth Michael maarufu k**a Lulu Alhamisi. https://t.co/sn8Erju8XM

Address

TEMEKE
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pavea News. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share