16/01/2026
: Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika sekta ya kilimo kupitia ushiriki wake katika Jukwaa la 18 la Kimataifa la Chakula na Kilimo (GFFA) linalofanyika mjini Berlin, Ujerumani.
Hayo yamebainika wakati Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, alipofanya mikutano ya pande mbili na Mawaziri wa Kilimo kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Pakistan, pamoja na taasisi za kimataifa za maendeleo ya kilimo.
Katika mazungumzo na Waziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa DRC, Mhe. Muhindo Nzangi Butondo, viongozi hao wamekubaliana kuanzisha makubaliano ya moja kwa moja ya kibiashara ili kuwezesha mazao ya kilimo ya Tanzania kuuzwa nchini Congo.
Baada ya kikao hicho, Mhe. Chongolo amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, na wataalam wa wizara hiyo kuhakikisha makubaliano hayo yanakamilika ndani ya wiki nne.
Mhe. Chongolo amekutana na Waziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula na Utafiti wa Kitaifa wa Pakistan, Mhe. Rana Tanveer Hussain, na kujadiliana juu ya ushirikiano katika teknolojia za kilimo, usalama wa chakula na tafiti za pamoja.
Vilevile, amefanya mazungumzo na Dkt. Helmut Fluhrer, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Rain Maker ya Ujerumani, kuhusu uwekezaji na ubunifu katika teknolojia za kilimo.
Ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa hilo unajumuisha Bw. Gerald Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo; Bw. Raymond Mndolwa, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC); Bw. Gungu Mohamed Mibavu, Mkurugenzi wa Masoko na Usalama wa Chakula; Bi. Irene Madeje Mlola, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko pamoja na Bi. Tagie Daisy Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Kilimo.
Powered by
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
Follow
.