ITV Tanzania

ITV Tanzania Official Facebook account for ITV Tanzania
P.O.Box 4374, DAR ES SALAAM
Tel: 065 877 7144 , 07677771
(279)

ITV-Independent Television Ltd,
Mikocheni Light Industrial Area
P.O.Box 4374, Dar Es Salaam,
Tanzania. Tel:+255 22 2775914/6
E-mail:[email protected]

Tanzania · http://www.ippmedia.com

 : Marius Borg Hoiby, mtoto wa miaka 29 wa Malkia Mette-Marit wa Norway, amepatikana na hatia ya makosa mawili ya ubakaj...
15/06/2026

: Marius Borg Hoiby, mtoto wa miaka 29 wa Malkia Mette-Marit wa Norway, amepatikana na hatia ya makosa mawili ya ubakaji na kuhukumiwa kifungo cha miaka minne jela.

Majaji watatu katika chumba cha Mahak**a nambari 250 katika Mahak**a ya Wilaya ya Oslo walimsamehe makosa mengine mawili ya ubakaji, lakini wakamkuta na hatia ya makosa mengine mengi ambayo alikuwa ameshtakiwa.
Høiby hakuwepo mahak**ani wakati wa uamuzi huo, lakini alijiunga na kikao hicho kwa njia ya video.

Waendesha mashtaka walikuwa wametaka Høiby apewe kifungo cha miaka saba na miezi saba jela. Mawakili wake wa utetezi walikuwa wametaka kifungo kiwe chini ya miezi 18 na wanaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Mama yake Marius Borg Høiby aliolewa katika familia ya kifalme alipokuwa na umri wa miaka minne, na ingawa alikulia katika familia hiyo, yeye mwenyewe si miongoni mwa familia ya kifalme.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow

MWANA WA MFALME NORWAY JELA MIAKA MIWILI KWA UBAKAJI : Marius Borg Hoiby, mtoto wa miaka 29 wa Malkia Mette-Marit wa Nor...
15/06/2026

MWANA WA MFALME NORWAY JELA MIAKA MIWILI KWA UBAKAJI

: Marius Borg Hoiby, mtoto wa miaka 29 wa Malkia Mette-Marit wa Norway, amepatikana na hatia ya makosa mawili ya ubakaji na kuhukumiwa kifungo cha miaka minne jela.

Majaji watatu katika chumba cha Mahak**a nambari 250 katika Mahak**a ya Wilaya ya Oslo walimsamehe makosa mengine mawili ya ubakaji, lakini wakamkuta na hatia ya makosa mengine mengi ambayo alikuwa ameshtakiwa.
Høiby hakuwepo mahak**ani wakati wa uamuzi huo, lakini alijiunga na kikao hicho kwa njia ya video.

Waendesha mashtaka walikuwa wametaka Høiby apewe kifungo cha miaka saba na miezi saba jela. Mawakili wake wa utetezi walikuwa wametaka kifungo kiwe chini ya miezi 18 na wanaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Mama yake Marius Borg Høiby aliolewa katika familia ya kifalme alipokuwa na umri wa miaka minne, na ingawa alikulia katika familia hiyo, yeye mwenyewe si miongoni mwa familia ya kifalme.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania
‎Capitalradio Tanzania

 :Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amewasihi vijana kuwa wabunifu kutumia rasilimali n...
15/06/2026

:Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amewasihi vijana kuwa wabunifu kutumia rasilimali na vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kunufaika na Michuano ya Kombe la Mataifa ya .Afrika (AFCON) 2027 k**a sehemu ya kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Chande amesema hayo mkoani Manyara alipotembelea eneo la chemchemi maji moto, kutembea kwenye daraja la kamba refu zaidi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati lililojengwa kwa kufuata uoto wa asili wa eneo la Hifadhi ya Taifa ya Lake Manyara na kupata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha akisistiza vijana hao kutumia ipasavyo fursa zilizopo kwenye utalii kupitia michuano hiyo.

“Nitoe mwito kwa vijana wetu, wajitoe waende kufanya kazi, wachangamkie fursa hii, hata k**a ni wasanii waoneshe vipaji vyao ninaamini kabisa tuna vijana wenye uelewa na ubunifu mkubwa sana kwa hiyo watumie ubunifu wao kupitia fursa hii ya AFCON ili wanufaike kiuchumi wakati na baada ya michuano hiyo kutamatika,” alisema Mhe. Chande.

Amesema Wizara inaendelea kuweka mikakati mbalimbali ikiwepo kutumia Mabalozi wa Tanzania kwenye nchini marafiki, Michuano ya Kombe la Dunia 2026 inayoendelea nchini Mexico, Marekani na Canada, Mikutano ya Kimataifa na Kikanda, kutoa elimu kwa waongoza watalii na wapagazi, kutumia vipindi vya runinga, wanamichezo na wasanii maarufu ulimwenguni k**a sehemu ya kutangaza vivutio vilivyopo nchini kwa lengo la kupata wengi zaidi wakati wa michuano hiyo.

Aidha, Mhe. Chande amewahimiza vijana hao kuwa mabalozi wazuri katika taifa kwa kufikisha ujumbe kwa vijana juu ya suala muhimu la uhifadhi wa rasilimali na vivutio vya asili vilivyopo nchini kutengeneza maudhui ya uhifadhi na utalii sambamba na kujenga tabia ya kufanya tafiti za wanyamapori walio hatarini kutoweka ikiwemo Faru hali itakayowasaidia kuwaongezea maarifa na kulisaidia taifa.

Katika hatua nyingine Mhe. Chande ameilekeza Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania (TAWA) kusimamia vyema chanzo cha Chemi Chemi Maji Moto kilichopo kando ya Ziwa Manyara kwa kujenga uzio na kukitangaza vyema ili kuvutia wageni wengi kipindi cha michuano hiyo jambo ambalo litasaidia kuongeza chachu ya mazao mapya ya vivutio vya utalii kufikia lengo la Serikali la kufikisha watalii milioni 8 ifikapo 2030.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow

15/06/2026
15/06/2026
 : Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano ya Jun...
15/06/2026

: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano ya Juni 17, 2026, itakuwa siku ya mapumziko kwa Zanzibar ili kuukaribisha Mwaka Mpya wa Kiislamu 1448 Hijria.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa tamko hilo leo, Juni 15, 2026, Ikulu Zanzibar, ikiwa ni utekelezaji wa uamuzi wa Serikali wa kuutambua Mwaka Mpya wa Kiislamu kuwa miongoni mwa siku muhimu Zanzibar.

Amesema siku hiyo itatoa fursa kwa wananchi, hususan waumini wa dini ya Kiislamu, kuukaribisha mwaka mpya kwa ibada, dua, na matendo mema, pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kuijaalia Zanzibar na Tanzania kwa ujumla amani, umoja na ustawi.

Alhaj Dkt. Mwinyi amewataka wananchi kuutumia mwaka mpya huo kujitathmini, kuimarisha uchamungu, kusaidiana na kuendeleza maadili mema yanayojenga familia na Taifa lenye mshik**ano.

Aidha, amezitaka taasisi za Serikali, taasisi binafsi, waajiri na wananchi wote kuzingatia tangazo hilo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.

Rais Dkt. Mwinyi amewatakia Waislamu na wananchi wote heri ya Mwaka Mpya wa Kiislamu 1448 Hijria, akimuomba Mwenyezi Mungu aufanye kuwa mwaka wa kheri, amani, afya njema na maendeleo kwa wote.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow
‎.

15/06/2026

🔴HABARI ZA SAA, SAA NNE NA DAKIKA 55- JUNI 15, 2026

15/06/2026

: Waumini wa Kanisa la Kilutheri Afrika Mashariki Moshono jijini Arusha wamepata na taharuki baada ya kukuta watu wanaodaiwa kuwa dalali wa Mahak**a wakiwa wametoa vitu vyote vilivyomo ndani ya Kanisa hilo huku wakiendelea na ujenzi wa uzio kuzunguka eneo hilo kwa madai kuwa mtu aliyetoa eneo hilo siyo mali yake kitendo kilichozua malumbano makali kurushia maneno kushikana na kuangushana chini kati ya dalali Mkandarasi wa ujenzi huo na familia inayodaiwa kumiliki kiwanja hicho ambao ni sehemu ya viongozi wa Kanisa hilo.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow

15/06/2026

: Waumini wa Kanisa la Kilutheri Afrika Mashariki Moshono jijini Arusha wamepata na taharuki baada ya kukuta watu wanaodaiwa kuwa dalali wa Mahak**a wakiwa wametoa vitu vyote vilivyomo ndani ya Kanisa hilo huku wakiendelea na ujenzi wa uzio kuzunguka eneo hilo kwa madai kuwa mtu aliyetoa eneo hilo siyo mali yake kitendo kilichozua malumbano makali kurushia maneno kushikana na kuangushana chini kati ya dalali Mkandarasi wa ujenzi huo na familia inayodaiwa kumiliki kiwanja hicho ambao ni sehemu ya viongozi wa Kanisa hilo.

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania
‎Capitalradio Tanzania

Address

Mikocheni
Dar Es Salaam
14111

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ITV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ITV Tanzania:

Share