ITV Tanzania

ITV Tanzania ITV- Independent Television Limited (ITV) associate company of IPP Limited. Tel:+255 22 2775914/6
E-mail:[email protected]

Tanzania · http://www.ippmedia.com
(282)

ITV-Independent Television Ltd,
Mikocheni Light Industrial Area
P.O.Box 4374, Dar Es Salaam,
Tanzania.

16/01/2026

: “….. Bado huu ni mchakato endelevu n ani kwasababu ni kitu ambacho tunaendelea kujifunza ni kitu mtambuka matumizi sahihi ya mtandao…………” Yoabu Ndanzi – Mkurugenzi Transformation Network
‎Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.



‎.

16/01/2026

: “Dira sio tukio la kwamba unaamka asubuhi unawapigia watu simu, hii ni mipango ambayo. Unakuta jamii kwanza inakuwa na matarajio…..” Deodatus Balile – Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania
‎Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.



‎.

16/01/2026

🔴JIJI LETU KUTOKA DAR ES SALAAM: JANUARI 16, 2026

16/01/2026

🔴MCHEZO SUPA: BADILISHA JANUARI YAKO KWA BUKU TU..JANUARI 16, 2026

16/01/2026

🔴KIPIMAJOTO: DIRA YA 2050. JE INAFURSA ZIPI KWA VIJANA WA LEO?

16/01/2026

: Familia ya Bi. Pendo Sangiziro, mkazi wa Nyantorontoro Kata ya Nyankumbu Halmashauri na Manispaa ya Geita mkoani Geita wamelazimika kulala nje ya nyumba yao kwa siku nne mpaka sasa baada ya kuzuka kwa moto ambao chanzo chake hakijafahamika na kuunguza vitu mbalimbali, ndani ya nyumba yao kwa siku nne mfululizo hali iliyozua taharuki na kusababisha familia hiyo kuikimbia nyumba yao wakihofia kuteketea kwa moto.

Bi. Jasimini anasema moto huo umekuwa ukitokea ghafla na kuteketeza vitu na unapodhibitiwa na zima moto, unaibuka kesho yake na kuteketeza nyumba kila mara na hapa analiomba Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lifanye uchunguzi kujua chanzo cha moto huo.

Balozi wa eneo hilo pamoja majirani wanasema moto huo wa maajabu umeteketeza na nyumba zingine, katika eneo hilo kwa mtindo huo huo, hali inayotishia usalama wa wananchi wanaoishi katika mtaa huo.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Geita Mrakibu Hamisi Shabani Dawa, amesema uchunguzi wa matukio ya moto katika eneo hilo, umeanza ili kubaini chanzo cha kuteketea kwa nyumba na mali katika eneo hilo.

Powered by

JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


Follow

‎ : Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika sekta ya kilimo kupitia ushiriki wake katika Jukwaa l...
16/01/2026

‎ : Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wa Kimataifa katika sekta ya kilimo kupitia ushiriki wake katika Jukwaa la 18 la Kimataifa la Chakula na Kilimo (GFFA) linalofanyika mjini Berlin, Ujerumani.

‎Hayo yamebainika wakati Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, alipofanya mikutano ya pande mbili na Mawaziri wa Kilimo kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Pakistan, pamoja na taasisi za kimataifa za maendeleo ya kilimo.

‎Katika mazungumzo na Waziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula wa DRC, Mhe. Muhindo Nzangi Butondo, viongozi hao wamekubaliana kuanzisha makubaliano ya moja kwa moja ya kibiashara ili kuwezesha mazao ya kilimo ya Tanzania kuuzwa nchini Congo.

‎Baada ya kikao hicho, Mhe. Chongolo amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, na wataalam wa wizara hiyo kuhakikisha makubaliano hayo yanakamilika ndani ya wiki nne.

‎Mhe. Chongolo amekutana na Waziri wa Kilimo, Usalama wa Chakula na Utafiti wa Kitaifa wa Pakistan, Mhe. Rana Tanveer Hussain, na kujadiliana juu ya ushirikiano katika teknolojia za kilimo, usalama wa chakula na tafiti za pamoja.

‎Vilevile, amefanya mazungumzo na Dkt. Helmut Fluhrer, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Rain Maker ya Ujerumani, kuhusu uwekezaji na ubunifu katika teknolojia za kilimo.

‎Ujumbe wa Tanzania katika Jukwaa hilo unajumuisha Bw. Gerald Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo; Bw. Raymond Mndolwa, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC); Bw. Gungu Mohamed Mibavu, Mkurugenzi wa Masoko na Usalama wa Chakula; Bi. Irene Madeje Mlola, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko pamoja na Bi. Tagie Daisy Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Kilimo.

‎Powered by


‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow
‎.

 : DIRA YA 2050. JE INAFURSA ZIPI KWA VIJANA WA LEO?
16/01/2026

: DIRA YA 2050. JE INAFURSA ZIPI KWA VIJANA WA LEO?

16/01/2026

TAARIFA YA HABARI YA SAA MBILI USIKU JANUARI 16, 2026 -JENGO LA NSSSF LASHIKA MOTO DAR ES SALAAM

 : Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Seke Mabirika Sesila (45), mkazi wa Wilaya ya Magu, kwa tuhuma za kumuua ...
16/01/2026

: Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Seke Mabirika Sesila (45), mkazi wa Wilaya ya Magu, kwa tuhuma za kumuua mke wake, Rahel Samwel Mabina (39), kwa kumshambulia kwa ngumi na mateke.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Januari 15, 2026, kufuatia ugomvi wa kifamilia uliotokana na marehemu kudai fedha za matumizi kutoka kwa mume wake.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alimshambulia mke huyo, aliyekuwa na ujauzito wa miezi miwili, sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo tumboni, hali iliyosababisha apoteze nguvu na kufariki dunia papo hapo.

Marehemu Rahel alikuwa mke wa tatu wa mtuhumiwa na walikuwa wamejaliwa kupata mtoto mmoja katika maisha yao ya ndoa.

Jeshi la Polisi limelaani vikali kitendo hicho cha ukatili wa kijinsia na kutoa wito kwa wananchi kutumia mazungumzo kutatua migogoro ya kifamilia badala ya kutumia nguvu. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Magu kwa ajili ya uchunguzi, huku mtuhumiwa akisubiri kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

‎Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.



‎.

16/01/2026

Kwa haya na Mengine mengi usikose kuungana nasi ifikapo Saa mbili kamili usiku.
Unaweza pia kutazama Taarifa yetu ya Habari kupitia Youtube na Facebook
Usisahau Ku-Subscribe ili kupata Taarifa zetu za kila zinapotufikia

Address

Mikocheni
Dar Es Salaam
14111

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ITV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ITV Tanzania:

Share