ITV Tanzania

ITV Tanzania Official Facebook account for ITV Tanzania
P.O.Box 4374, DAR ES SALAAM
Tel: 065 877 7144 , 07677771
(279)

ITV-Independent Television Ltd,
Mikocheni Light Industrial Area
P.O.Box 4374, Dar Es Salaam,
Tanzania. Tel:+255 22 2775914/6
E-mail:[email protected]

Tanzania · http://www.ippmedia.com

17/08/2026

🔴HABARI ZA SAA, SAA NNE NA DAKIKA 55 - AGOSTI 17, 2026

17/08/2026

:Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu leo Agosti 17, 2026 amefikishwa katika Mahakama Kuu, Masjala Ndogo Dar es Salaam , kwa ajili ya kuendelea na kesi ya uhaini inayomkabili, ambapo upande wa mashtaka unatarajiwa kuendelea na ushahidi wa shahidi wa 18.

‎Kesi hiyo iliahirishwa Agosti 14, 2026 baada ya shahidi huyo wa 18 kudaiwa kupata changamoto ya kiafya na kushindwa kufika mahakamani.

Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu mpya wa Facebook EXTRA>>>> https://www.facebook.com/share/1QMjXDHqGv/?mibextid=wwXIfr

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.

‎ ITVTanzania
‎Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania.

17/08/2026
 : Rais wa Marekani Donald Trump amesema mazoezi ya kijeshi ya nchi yake na Korea Kusini, yataanza rasmi baina ya mataif...
17/08/2026

: Rais wa Marekani Donald Trump amesema mazoezi ya kijeshi ya nchi yake na Korea Kusini, yataanza rasmi baina ya mataifa hayo.

Bw. Trump amesema kuwa Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ndiye aliyemfanya kufikia uamuzi huo. Aliyataja mazoezi hayo kuwa ya gharama kubwa na ya kichokozi, huku akigusia hatua ya Korea Kusini kukataa kujiunga na mazungumzo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran.

Mazoezi hayo yenye jina la Ulchi Freedom Shield hufanyika kila mwaka ili kujiandaa dhidi ya tishio la mashambulizi katika Rasi ya Korea.

Korea Kaskazini inaendelea kuimarisha silaha zake za nyuklia na wiki iliyopita ilifanya majaribio kadhaa ya makombora ya masafa marefu yaliopewa jina la ballistic missiles.

Katika ujumbe wake wa mitandao ya kijamii siku ya Jumapili, Trump alisema ilikuwa ni vigumu kuahirisha, mpango huo kwani Marekani na Korea Kusini zilikuwa zikitarajiwa kuanza mazoezi yao ya kila mwaka ya kijeshi Jumatatu.

Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu mpya wa Facebook EXTRA>>>> https://www.facebook.com/share/1QMjXDHqGv/?mibextid=wwXIfr

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.

‎ ITVTanzania
‎Follow .

 : Je utaratibu wa mgonjwa  kupata PF3 una tija kihuduma au utaratibu huu unaleta changamoto.?-Weka maoni yako- Saa Tisa...
17/08/2026

: Je utaratibu wa mgonjwa kupata PF3 una tija kihuduma au utaratibu huu unaleta changamoto.?

-Weka maoni yako
- Saa Tisa Alasiri

 : Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT-Wazalendo wamelaani kukamatwa kwa Wakili Peter Madeleka, huku viki...
17/08/2026

: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT-Wazalendo wamelaani kukamatwa kwa Wakili Peter Madeleka, huku vikitaka Jeshi la Polisi kumuachia huru bila masharti yoyote.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Agosti 13, 2026, Madeleka alikamatwa saa 9:30 Alasiri katika eneo la Mikocheni B, Wilaya ya Kinondoni, kwa tuhuma za kudharau amri ya Mahakama Kuu.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Wakili Madeleka anatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho Agosti 17, 2026, kuhusiana na tuhuma hizo.

Kwa nyakati tofauti, vyama hivyo vimesema mwenendo wa kutumia vyombo vya dola kuwabana watu wanaotoa maoni kuhusu masuala ya umma unaweza kujenga hofu miongoni mwa wananchi, kudhoofisha imani ya umma katika taasisi za haki na utawala wa sheria.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia, Agosti 16, 2026, chama hicho kinalitaka Jeshi la Polisi kumuachia huru Madeleka mara moja bila masharti yoyote.

“Chadema inalitaka Jeshi la Polisi kumuachia huru mara moja bila masharti yoyote. Pia, tunatoa wito kwa wadau wa haki za binadamu, wanasheria, vyombo vya habari na wananchi wote kuendelea kufuatilia kwa karibu suala hili na kuhakikisha haki za Wakili Madeleka zinalindwa,” amesema Rupia katika taarifa hiyo.

Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu mpya wa Facebook EXTRA>>>> https://www.facebook.com/share/1QMjXDHqGv/?mibextid=wwXIfr

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.

‎ ITVTanzania
‎Follow

17/08/2026

: Hali ya taharuki ilitanda katika Mji wa Homa Bay, huku baadhi ya shughuli za biashara na usafiri zikisitishwa kwa muda kabla ya mkutano wa kisiasa wa Linda Mwananchi katika eneo hilo.

Polisi wamewakamata watu kwa tuhuma za kupanga kuvuruga shughuli za kisiasa, hata hivyo mkutano huo uliendelea huku viongozi wa Linda Mwananchi wakikashifu jaribio la kuzuia mkutano.

Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu mpya wa Facebook EXTRA>>>> https://www.facebook.com/share/1QMjXDHqGv/?mibextid=wwXIfr

Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.

‎ ITVTanzania
‎Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania.

HECHE ALIVYOGEUKA "SHABAHA" YA CCM17Agosti2026
17/08/2026

HECHE ALIVYOGEUKA "SHABAHA" YA CCM

17Agosti2026

Kuondoa wanaolima kwenye maeneo ya hifadhi na vyanzo vya maji. Je, kuambatane na kuwajibisha viongozi wa maeneo hayo kwa...
17/08/2026

Kuondoa wanaolima kwenye maeneo ya hifadhi na vyanzo vya maji. Je, kuambatane na kuwajibisha viongozi wa maeneo hayo kwa kushindwa kulinda maeneo hayo yasivamiwe ?

16/08/2026

: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amesema uamuzi wa Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kuunda Tume na ndio utaratibu wa Sheria za Kikanda na Kimataifa ambapo ametoa mifano ya nchi mbalimbali zilivyounda tume za kuchunguza masuala yaliyotokea katika nchi zao.‎

Ameyasema hayo Kijiji cha Kangagani, Kaskazini Pemba wakati akimwakilisha Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuweka Jiwe la Msingi la Skuli ya Amali inayojengwa kwa Shilingi Bilioni 4.

‎Powered by

‎JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
‎-
‎Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.


‎Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania
‎Capitalradio Tanzania.

Address

Mikocheni
Dar Es Salaam
14111

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ITV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ITV Tanzania:

Shortcuts

Share