Gospel Kitaa

Gospel Kitaa Kwa utukufu wa Mungu, tunakuletea habari zinazohusiana na Ukristo Tanzania na ulimwenguni kote kwa ujumla. Ungana nasi kupitia pia Youtube na Blog.

JOYOUS CELEBRATION KUREJEA KWA KISHINDO MWEZI MAY Kundi la Joyous Celebration la Afrika ya Kusini linatarajiwa kuanza ku...
09/03/2026

JOYOUS CELEBRATION KUREJEA KWA KISHINDO MWEZI MAY

Kundi la Joyous Celebration la Afrika ya Kusini linatarajiwa kuanza kusherehekea miaka 30 tangu kuanzishwa kwake mwezi May mwaka huu kwa kufanya maonyesho ya siku 4 mfululizo kwa Mara ya kwanza.
Joyous ambao wamekuwa wakisuasua toka mkataba wake na kampuni ya simu ya MTN kumalizika miaka 5 iliyopita. Imekuwa ikiandamwa na na suala zima la uendeshaji baada ya waasisi wake Jabu na Mthunzi kuomba kujitoa katika kundi hilo mapema mwaka 2021 lakini mwenzao Dkt. Lindelani alipinga wazo hilo na kutaka kuachiwa jukumu la uendeshaji. Hata hivyo hivi karibuni Jabu alimshutumu Dkt Mkhize kwa ubadhirifu wa pesa kitu ambacho alikipinga na kutaka masuala yote ya pesa kuanzia mwanzo mpaka 2021 aulizwe Jabu kwakuwa ndiye aliyekuwa anasimamia.
Mthunzi Namba amekuwa akionekana kwenye kundi lingine la injili la Spirit of Praise ambako amekuwa akialikwa K**a mgeni maalumu.

Joyous watafanya maonyesho manne kuanzia tarehe 30/04 katika ukumbi wa Joburg theatre huku kukiwa na tetesi kwamba watatumia maonyesho hayo kurekodi album yao ya 29 maana hawajaweza kurekodi kwa miaka takribani miwili kutokana na tatizo la uendeshaji wa kundi hilo ambalo limekuwa chachu ya makundi mengi ya uimbaji barani Afrika ikiwemo Tanzania. Aidha litatangaza tarehe nyingine ya ziara zao nchini humo wiki hii

HILLSONG WORSHIP YAREJEA BAADA YA KIMYA CHA MUDA MREFUKundi maarufu la Hillsong Worship kutoka katika kanisa la Hillsong...
08/03/2026

HILLSONG WORSHIP YAREJEA BAADA YA KIMYA CHA MUDA MREFU

Kundi maarufu la Hillsong Worship kutoka katika kanisa la Hillsong lenye makao makuu Sydney Australia limeanza kutoa nyimbo mpya baada ya kimya cha muda mrefu kufuatia kashfa mbaya iliyowakumba baadhi ya viongozi wa juu wa kanisa hilo na kusababisha baadhi ya makanisa yao nchi mbalimbali ikiwemo Marekani kufungwa au kujiondoa chini ya mwamvuli wa kanisa hilo. Baadhi ya nyimbo ambazo zinapatikana YouTube ni Pamoja na Good news, Only Jesus na Great I AM. Hata hivyo bado haijajulikana k**a waimbaji wake nyota k**a Brooke, Morgan na Taya k**a bado wapo kwenye kundi hilo…

JE UNAJUA?Neema Gospel Choir wametoa wimbo mwingine wa tatu uitwao Umenibamba kutoka katika album yao mpya yenye nyimbo ...
07/03/2026

JE UNAJUA?

Neema Gospel Choir wametoa wimbo mwingine wa tatu uitwao Umenibamba kutoka katika album yao mpya yenye nyimbo zaidi ya 20 iitwayo Grace Unlimited waliyoirekodi mubashara mwezi November 2025 katika viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam. Nyimbo nyingine walizotoa ni pamoja na Umenipendelea, Ngiyabonga nasasa wanakwambia Umenibamba… nenda YouTube Ubarikiwe zaidi.

“Si kwa ujanja wangu, si kwa akili zangu… Neema yako imenibeba.”Umenibamba is a vibrant praise declaration of God’s grace, faithfulness, and sufficiency. The...

Mazishi ya mwimbaji wa zamani wa kundi la Soweto Gospel Choir la Afrika ya Kusini, Thembisa Khuzwayo yamefanyika hii leo...
07/03/2026

Mazishi ya mwimbaji wa zamani wa kundi la Soweto Gospel Choir la Afrika ya Kusini, Thembisa Khuzwayo yamefanyika hii leo katika makaburi ya Slovoville huko jijini Johannesburg. Thembisa alifariki dunia mapema wiki hii nchini humo. Licha ya kuimbia kundi la Soweto, Thembisa pia amewahi kuwa mchezaji wa step kwa waimbaji mbalimbali akiwemo Yvonne Chakachaka pia alikuwa ni kati ya waimbaji wa mwanzo wa Soweto akiwemo Sipokazi Nxumalo ambaye pia alifariki takribani miaka 3 iliyopita. Pumzika Thembisa

“Humwaga aibu juu ya hao wakuu, Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu. Huvumbua mambo ya siri tokea gizani, Na hicho kilicho...
28/10/2025

“Humwaga aibu juu ya hao wakuu, Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu. Huvumbua mambo ya siri tokea gizani, Na hicho kilicho giza tupu huleta mwangani.”
‭‭Ayu‬ ‭12‬:‭21‬-‭22‬ ‭SUV‬‬
https://bible.com/bible/164/job.12.21-22.SUV

““He pours contempt on princes and nobles And loosens the belt of the strong [disabling them]. “He uncovers mysteries [that are difficult to grasp and understand] out of the darkness And brings black gloom and the shadow of death into light.”
‭‭Job‬ ‭12‬:‭21‬-‭22‬ ‭AMP‬‬
https://bible.com/bible/1588/job.12.21-22.AMP

“puts mighty kings to shame, and takes away their power. God turns darkness to light;”
‭‭Job‬ ‭12‬:‭21‬-‭22‬ ‭CEV‬‬
https://bible.com/bible/392/job.12.21-22.CEV

*⛷️OSAC Night-YADAH Worship🔥*👌🏼Weekendi yenye Utukufu💥💡 *Sept 30,2022* Kuanzia Saa 3:30 Usiku, Utakuwa ni Mkesha wa *HAT...
17/09/2022

*⛷️OSAC Night-YADAH Worship🔥*

👌🏼Weekendi yenye Utukufu💥

💡 *Sept 30,2022* Kuanzia Saa 3:30 Usiku, Utakuwa ni Mkesha wa *HATUA MOJA MBELE NA YESU*, Yaani OSAC Night

▪️Usiku ambao tutakuwa na Mwalimu & Mwandishi *Emmanuel Makwaya*
Spiritual Family, Vijana wa KKKT Forest,BVC na Mwabudu Gwakisa Mwakilema, bila kusahau tutacheka na Mc Mtoto wa Mungu(Mc Mangula)

&
🙌🏾 *October 02,2022* Kuanzia Saa 3 alasiri, Tutakuwa TUNAINUA MIKONO YETU KWA BWANA, katika ibada Mahususi ya *YADAH Worship* kuashiria kuwa Tunahitaji Msaada wa Bwana kwa mwezi wa 10; Jumapili hii tutakuwa na Kwaya bora kabisa ya *WAKUMBUKENI YATIMA* Sambamba na BVC, Gwakisa Mwalimema na Mc Mangula tena!

✍️Ni Kujifunza, Kusifu, Kuabudu, Kuomba, Kula, Kucheka, Kufurahi na kupiga hatua ya Maisha!

📍Mahali ni pale pale, Mafichoni mwa Mapenzi yake * CHAPEL*
Upendo Hostels, Block T, Jijini Mbeya.

👏🏻KARIBU SANA NA K**A UKIKOSA KUJA, BASI USIACHE KUTUOMBEA NA KUSHIRIKI KWA SADAKA YAKO YA HIARI
🎫Lipa No. M-pesa(Kutoka Mitandao yote)
*5018851*
SADAKA EAGLES CHAPEL

Baraka za BWANA Yesu ziwe nawe!


30/06/2022

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gospel Kitaa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Gospel Kitaa:

Share