Azam TV

Azam TV Azam Media Ltd is a Tanzanian media company owned by the Bakhresa Group.

Under the AzamTV brand | Follow our other accounts AzamTV Burudani AzamSports Sinema Zetu HD

11/08/2025

Chama cha TLP kimekuwa chama cha tatu leo Agosti 11, 2025 kuchukua fomu za uteuzi kwa ajili ya kugombea Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Mgombea Urais wa chama hicho, Yustas Mbatina na mgombea mwenza Amana Suleiman Mzee wamekabidhiwa fomu hizo leo kwenye ofisi ya INEC jijini Dodoma.

Imeandaliwa na Nifa Omary
Mhariri

11/08/2025

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema mchakato wa maombi ya michango kwa wanachama na wasio wanachama wa CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu hautoathiri uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi.

Msikilize hapa.

Imeandaliwa na Alpha Jenifer
Mhariri

11/08/2025

Mwili wa hayati Job Ndugai umezikwa leo jijini Dodoma na hawa ni miongoni mwa waombolezaji walioguswa na msiba wake na hapa wanatoa maneno kuhusu Spika huyo mstaafu.

Imeandaliwa na Henry Masanja na Joyce Mwakalinga

Mhariri

11/08/2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinahitaji kupata Shilingi bilioni moja kwa ajili ya shughuli za kampeni kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na waandishi na wahariri wa habari, Katibu Mkuu wa CCM ambaye pia ni mgombea mwenza wa Urais, Dkt. Emmanuel Nchimbi ameviomba vyama shindani vya siasa kuichangia CCM sambamba na wanachama na wadau wengine.

Imeandaliwa na Nifa Omary

Mhariri

11/08/2025

Mtandao wa mashirika yasiyoya kiserikali mkoani Lindi, LANGO umeandaa mafunzo maalum kwa wadau mbalimbali wa sekta ya uchimbaji madini ili kutoa elimu ya haki na wajibu kwa kila mmoja ili kunusuru migogoro ambayo hujitokeza kwneye maeneo ya uchimbaji ikihusisha kampuni za uchimbaji na wananchi.

Imeandaliwa na Omari Mikoma

Mhariri

11/08/2025

Wataalamu wa kilimo nchini wamesema miongoni mwa sababu za zao la pamba kuendelea kukabiliw ana magonjwa sugu ni uelewa mdogo wa wakulima ambao hushindwa kufuata kikamilifu maelekezo ya matumizi ya viuatilifu hali inayochangia kuongezeka kwa usugu wa dawa kwa wadudu hao.

Imeandaliwa na Rehema Evance

Mhariri

LALIGA msimu wa 2025/2026 unaanza Ijumaa hii Agosti 15.Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama LALIGA mwezi mzima mb...
11/08/2025

LALIGA msimu wa 2025/2026 unaanza Ijumaa hii Agosti 15.

Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama LALIGA mwezi mzima mbashara kupitia AzamSports4HD.

11/08/2025

Mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha UMD,. Mwajuma Mirambo na mgombea mwenza Mashavu Alawi Haji wamekabidhiwa fomu za kuwania nafasi hiyo kwenye Uchaguzi Mkuu 2025 utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

UMD wamekabidhiwa fomu hizo katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).

Imeandaliwa na Alpha Jenifer

Mhariri

CHAN kuendelea leo kwa mechi za Kundi C.Saa 11:00 jioni, Afrika Kusini wakiwa na na alama moja kucheza na Guinea wenye a...
11/08/2025

CHAN kuendelea leo kwa mechi za Kundi C.

Saa 11:00 jioni, Afrika Kusini wakiwa na na alama moja kucheza na Guinea wenye alama tatu.

Saa 2:00 usiku, Wenyeji Uganda wakiwa na alama tatu kucheza na Niger ambao wamepoteza mchezo wao wa kwanza.

Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama mashindano haya mwanzo mwisho mbashara kupitia AzamSports1HD.

11/08/2025





11/08/2025

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha ADA - TADEA, Georges Gabriel Bussungu na mgombea mwenza Ally Makame wamechukua fomu za kugombea nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyioka Oktoba 29, 2025.

Bussungu na Makame wamekabidhiwa fomu hizo kwenye ofisi za INEC zilizopo jijini Dodoma.

Imeandaliwa na Alpha Jenifer
Mhariri

11/08/2025



Address

Tazara
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Azam TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Azam TV:

Share