Azam TV

Azam TV Azam Media Ltd is a Tanzanian media company owned by the Bakhresa Group.

Under the AzamTV brand | Follow our other accounts AzamTV Burudani AzamSports Sinema Zetu HD

15/01/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, amezitaka wizara zinazohusika na ajira kusimamia kikamilifu sheria zinazozuia wageni kufanya kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania.

Dkt. Nchemba amesema hayo wakati wa kikao cha viongozi wa wizara za kisekta kuhusu ajira, Dkt. Nchemba amesema wageni wanapaswa kufanya kazi za kitaalamu pekee ambazo nchi ina uhaba wa wataalam.

Mhariri

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limemk**ata Denis Ogesa (28), raia wa Kenya na mkazi wa Nairobi, kwa tuhuma za kuvunja na...
15/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limemk**ata Denis Ogesa (28), raia wa Kenya na mkazi wa Nairobi, kwa tuhuma za kuvunja na kuiba katika tawi la Benki ya Azania lililopo mji wa Namanga, wilayani Longido.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, tukio hilo lilitokea Januari 14, 2026, saa 6:40 usiku, wakati mtuhumiwa akiwa anaendelea kutekeleza tukio hilo la kihalifu ndani ya benki hiyo ndipo alik**atwa na askari wa polisi.

Kamanda huyo amesema wakati wa kuk**atwa, mtuhumiwa alikutwa na fedha taslimu jumla ya shilingi za Tanzania 91,280,000 pamoja na shilingi za Kenya 288,700, fedha zinazodhaniwa kuwa ni sehemu ya mali iliyopatikana katika tukio hilo.

Mharirir

15/01/2026

Mapitio ya leo Januari 15, 2026 kwenye

14/01/2026

Ubunifu uliofanywa ndani ya Kilimanjaro IX unaifanya boti hiyo mpya ya Azam Marine kuwa ya kipekee zaidi.

Miongoni mwa ubunifu uliomo ni viti vya kisasa na picha za vivutio vya utalii wa Tanzania.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Azam Marine, Abubakar Azizi Salim anafafanua zaidi.

Mhariri

14/01/2026

Uzalishaji wa parachichi unaofanywa kwa kutumia mbegu ya kisasa aina ya HASS unaelezwa kubadilisha mtazamo wa kilimo cha zao hilo mkoani Kigoma.

Uzalishaji huo unaofanyika katika shamba la Kibondo Greem farm unatajwa kuwavutia wakulima wengi na inakadiriwa idadi ya wakulima wa zao hilo kuongezeka.

Mhariri

14/01/2026

Ndoto ya wakulima wa vijiji vya Ilemba, Sakalilo na Isanga mkoani Rukwa wanaotegemea skimu ya umwagiliaji kwa ajili ya kilimo huenda ikawa 'ndoto iliyopotea' baada ya miundombinu ya skimu hiyo kuanza kuharibiwa kutokana na mto unaopeleka maji kwenye skimu hiyo kupanuka na kuharibu kingo za skimu hiyo.

Mhariri

14/01/2026

Kiwango cha ukosefu wa ajira kidunia kinatajwa kufikia wastani wa asilimia 8.9 huku Tanzania kiwango hicho kikishuka kwa asilimia 0.2 na kufikia 8.7 kwa mwaka 2025.

Miongoni mwa hatua zinazoisaidia Tanzania ni ubunifu wa vijana wake kwenye kutengeneza ajira binafsi zilizo rasmi kwa njia zinazowawezesha kuendesha maisha yao na wanaowategemea.

Mhariri

14/01/2026

Mabadiliko ya tabianchi yameendelea kusababisha mvua zisizotabirika hali inayotishia kilimo na usalama wa chakula kwa ujumla wake huku waathirika wakubwa zaidi wakiwa wakulima.

Ripoti ya Faraja Samo inaangazia namna mabadiliko ya tabianchi yanavyogeuza mvua kuwa kitendawili hatarishi.

Mhariri

14/01/2026

Zaidi ya kaya 52 za wilayani Ruangwa mkoani Lindi zimekosa makazi kufuatia nyumba zao kuathiriwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo iliyonyesha kwa muda mfupi jana Januari, 13, 2026.

Kwa mujibu wa taarifa ya athari za mvua hizo, baadhi ya nyumba zimebomoka na nyingine zimeezuliwa mapaa.

Taarifa ya Omary Mikoma.

Mhariri

14/01/2026

Bi Julia anaeleza katika maisha yao ya ndoa imekuwa ni nyakati njema, huku mzee kimiti akiamini katika falsafa yake ya “ta te ti to tu “


Mhariri |

14/01/2026

Kiongozi mstaafu, Paul Kimiti na mkewe Julia Kimiti wanandoa waliounganishwa na upendo, wakishirikiana safari ya maisha kwa miaka mingi wakizeeka pamoja.


Mhariri |

14/01/2026

Mchambuzi wa masuala ya uchumi, Walter Nguma, amesema ukuaji wa uchumi wa taifa unategemea kwa kiasi kikubwa mzunguko wa fedha ndani ya mfumo rasmi wa kifedha, hali inayowezesha benki, watu binafsi na Serikali kupata rasilimali za kuendesha shughuli za maendeleo.

Amesema kuhifadhi fedha majumbani kunazuia mzunguko huo, jambo linalopunguza uwezo wa benki kukopesha wafanyabiashara na wawekezaji, hivyo kudhoofisha shughuli za uzalishaji na ajira.

Nguma amewashauri wafanyabiashara na watu wenye kipato kikubwa kuhifadhi fedha zao benki, ili zitumike k**a mtaji wa kukopesha wengine na kuendesha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

✍Ibrahim Kilumbo
Mhariri |

Address

Tazara
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Azam TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Azam TV:

Share