Azam TV

Azam TV Azam Media Ltd is a Tanzanian media company owned by the Bakhresa Group.

Under the AzamTV brand | Follow our other accounts AzamTV Burudani AzamSports Sinema Zetu HD

03/10/2025

Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa daraja la Msangano lenye thamani ya shilingi bilioni tatu katika barabara ya Chindi–Msangano, Wilaya ya Momba, Songwe.

Daraja hilo litaunganisha Halmashauri ya Tunduma na Makao Makuu ya Wilaya ya Momba, pamoja na tarafa za Msangano na Kamsamba maarufu kwa kilimo cha mazao ya biashara.

Mradi unaotekelezwa na TARURA kupitia tozo ya mafuta ulianza Septemba 2023 na unatarajiwa kukamilika Desemba 2025. Hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 80 na zaidi ya shilingi bilioni 1.5 zimetumika.

✍ Joyce Lyanda
Mhariri

03/10/2025

Shirika la Kuendeleza Kilimo Hai nchini (Toam) na Wizara ya Kilimo wanatarajia kufanya mkutano wa nne wa kitaifa wa kilimo ikolojia hai, utakaoambatana na tafiti mbalimbali za sekta hiyo ambazo zinaonesha jinsi kilimo kinavyosaidia katika afya na uhifadhi wa mazingira.


✍Upendo Michael
Mhariri | John Mbalamwezi

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Zainab Khamis Shomari, amesema kuwa ucha...
03/10/2025

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT), Zainab Khamis Shomari, amesema kuwa uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu utakuwa mwepesi kwa chama hicho kutokana na maendeleo makubwa yaliyoletwa na Serikali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM katika Jimbo la Mtambwe, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba Zainab amesisitiza kuwa wananchi wanapaswa kuendelea kukiamini chama hicho, akieleza kuwa maendeleo makubwa katika sekta mbalimbali yamekuwa yakithibitisha uongozi bora wa CCM kwa wananchi.

Aidha, amewahimiza wananchi wa Jimbo la Mtambwe kuchagua viongozi wa CCM kwenye nafasi zote.


Mhariri | John Mbalamwezi

03/10/2025

Mgombea urais kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuendeleza sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi wilayani Karatu kwa kujenga minada, majosho, kununua boti za uvuvi pamoja na kuboresha mwalo wa Ziwa Eyasi ili kukuza uchumi wa kaya na taifa.

Akihutubia wananchi katika viwanja vya mnadani, Dkt. Samia alisema serikali yake imepanga kuongeza maeneo ya ufugaji kutoka ekari milioni 3.6 hadi milioni sita, kujenga machinjio ya kisasa.

Aidha, amebainisha kuwa Tanzania ipo kwenye mazungumzo na India ili kuhakikisha wakulima wa mbaazi na dengu wanapata bei nzuri ya mazao yao kwenye soko la dunia.


03/10/2025

Makamu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Modest Katonto, ameiasa jamii kushirikiana na viongozi wa dini katika kukabiliana na mmomonyoko wa maadili unaoendea kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Ametoa wito huo leo wakati wa maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 ya huduma ya upadri wa Padri Anselmo Kashatila, Paroko wa Parokia ya Chala, ambaye sasa ana umri wa miaka 77.


Mhariri | John Mbalamwezi

03/10/2025

Wakandarasi mkoani Katavi wametakiwa kuachana na visingizio na badala yake kuelekeza nguvu katika kuhakikisha miradi ya ujenzi wa meli kwenye Ziwa Tanganyika inakamilika kwa wakati.

Viongozi wa mkoa wamesisitiza kuwa ucheleweshaji wa miradi hiyo unakwamisha juhudi za serikali katika kukuza uchumi wa wananchi kupitia usafiri wa maji na biashara zinazotegemea Ziwa Tanganyika.


Mhariri | John Mbalamwezi

03/10/2025

Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) imeongeza muda wa udahili wa shahada ya kwanza katika programu ambazo bado zina nafasi kwa mwaka wa masomo 2025/2026. Hatua hiyo inalenga kutoa nafasi kwa wanafunzi ambao hawakufanikisha kutuma maombi kwenye dirisha la kwanza na la pili.

Kwa mujibu wa TCU, dirisha la udahili la awamu ya tatu litafunguliwa kuanzia Oktoba 6 -10 mwaka huu.


Mhariri |John Mbalamwezi

03/10/2025

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameahidi kuendeleza sekta ya utalii mkoani Arusha kwa kukarabati na kupanua viwanja vya ndege vya Lake Manyara wilayani Karatu na Waso, Ngorongoro.

Akihutubia wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika Karatu, Dkt. Samia amesema zaidi ya shilingi bilioni 88.5 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya kurukia ndege, jengo la abiria litakalohudumia watu 150 kwa wakati mmoja, pamoja na barabara ya lami kuelekea uwanja huo ili kurahisisha usafiri wa watalii.


03/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesema serikali inaendelea na mikakati ya kuongeza thamani ya zao la zabibu ili wakulima wanufaike zaidi.

Ameeleza kuwa mkoa huo tayari umepata kiwanda cha kuchakata na kuhifadhi zabibu, hatua itakayopunguza changamoto za masoko na kuongeza kipato kwa wakulima.


✍Alpha Jenipher
Mhariri | John Mbalamwezi

Makamu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Modest Katonto ameiasa jamii mkoani Rukwa kushirikiana na viong...
03/10/2025

Makamu wa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, Modest Katonto ameiasa jamii mkoani Rukwa kushirikiana na viongozi wa dini katika kukabiliana na changamoto ya mmomonyoko wa maadili.

Mabadiliko ya sayansi na teknolojia yachochea vipi mmomonyoko wa maadili katika jamii unayoishi? nini kifanyike? Tuandikie maoni yako na tutayasoma saa 7:00

03/10/2025

Kwa taarifa yako…nzi na funza wanaweza kukuinua kiuchumu…

Fuatilia simulizi ya Denis Kamanzi, mwanzilishi wa BIOAKEMI, ambaye aliona fursa kwenye ufugaji wa nzi-chuma na funza. Fursa hii imebadili muelekeo wa maisha yake, ikamwezesha kujiajiri na pia kuajiri vijana wengine.

Msikilize akifafanua namna nzi na funza walivyokuwa daraja la kumuinua kiuchumi.


✍Alpha Jenipher
Mhariri | John Mbalamwezi

03/10/2025

Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam iko mbioni kukamilisha jengo la ghorofa tano la shule ya kisasa ya Olympio ambalo linatarajiwa kuongeza udahili wa wanafunzi wa shule ya awali sambamba na maboresho ya ujifunzaji kutokana na miundombinu iliyowekwa.

Ujenzi huo umefikia asilimia 94 huku viongozi wa idara ya elimu msingi ukitoa pongezi kwa serikali na shukrani kwa Rais Samia kutokana na maboresho hayo makubwa.

Imeandaliwa na

Address

Tazara
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Azam TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Azam TV:

Share