11/08/2025
Chama cha TLP kimekuwa chama cha tatu leo Agosti 11, 2025 kuchukua fomu za uteuzi kwa ajili ya kugombea Urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.
Mgombea Urais wa chama hicho, Yustas Mbatina na mgombea mwenza Amana Suleiman Mzee wamekabidhiwa fomu hizo leo kwenye ofisi ya INEC jijini Dodoma.
Imeandaliwa na Nifa Omary
Mhariri