Azam TV

Azam TV Azam Media Ltd is a Tanzanian media company owned by the Bakhresa Group.

Under the AzamTV brand | Follow our other accounts

06/06/2026

Zaidi ya walimu 300 mkoani Manyara wameripotiwa kukosa kupandishwa madaraja mwaka huu kutokana na taarifa zao kutokuonekana katika mfumo wa kielektroniki, licha ya wengi wao kutimiza sifa na kuwa na ufaulu mzuri wa kitaaluma.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Manyara, Theophin Joseph amesema changamoto za mtandao zimekuwa zikikwamisha walimu kupata haki zao kwa wakati, ikiwemo kupandishwa madaraja, hali inayopunguza morali na ufanisi kazini.

Ameiomba serikali kuboresha huduma za mawasiliano kwa kuongeza minara ya simu na kuimarisha intaneti, pamoja na kurejesha kikokotoo cha asilimia 55 katika ukokotoaji wa mafao ya walimu, akieleza kuwa hali ya gharama za maisha imeendelea kupanda na kuathiri ustawi wa watumishi hao.

Helen Chikawe
Mhariri | John Mbalamwezi

Waumini wa dini ya Kiislamu nchini wamehimizwa kuanza mapema maandalizi ya ibada ya hija ya mwaka 2027, ili kuhakikisha ...
06/06/2026

Waumini wa dini ya Kiislamu nchini wamehimizwa kuanza mapema maandalizi ya ibada ya hija ya mwaka 2027, ili kuhakikisha wanakamilisha taratibu zote muhimu zinazohitajika kwa safari hiyo ya kiibada.

Miongoni mwa waratibu wa safari za hija na umra nchini, Abbas Bantulaki, amesema maandalizi ya mapema huwapa waumini fursa ya kujipanga kifedha, kupata nyaraka muhimu za usafiri na kufahamu mahitaji mbalimbali yanayohusiana na ibada hiyo.

Bantulaki ameeleza kuwa hija ni miongoni mwa nguzo za Uislamu kwa wale wenye uwezo, hivyo maandalizi ya kutosha husaidia kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza wakati wa mchakato wa usajili na safari yenyewe.

Aidha, waumini wametakiwa kutafuta taarifa sahihi kutoka kwa taasisi na waratibu wanaotambuliwa ili kupata mwongozo unaohitajika kuhusu masharti, ratiba na taratibu za safari za hija na umra, hatua inayoweza kusaidia kufanikisha utekelezaji wa ibada hiyo kwa utulivu na ufanisi.


Mhariri | John Mbalamwezi

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Lindi imewahukumu watu wawili vifungo vya muda mrefu gerezani katika kesi mbili tofauti...
06/06/2026

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Lindi imewahukumu watu wawili vifungo vya muda mrefu gerezani katika kesi mbili tofauti za ubakaji wa mtoto na umiliki haramu wa nyara za serikali, baada ya kupatikana na hatia ya makosa hayo.

Katika kesi ya ubakaji, mshtakiwa Hamis Rashid Mkon'gonda (55), amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani pamoja na kulipa fidia ya shilingi milioni moja baada ya kutiwa hatiani kwa kumbaka mtoto wa k**e mwenye umri wa miaka minne.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Lindi, Consolata Singano baada ya mahak**a kujiridhisha kuwa ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka ulithibitisha kosa hilo bila kuacha shaka yoyote.

Katika kesi nyingine, Michael Atanas Antoni (46), amehukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kumiliki vipande vitatu vya nyama ya mnyama aina ya ngiri bila kibali halali kutoka mamlaka husika.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Khalfan Omari Khalfan, huku pande wa Jamhuri ukiwakilishwa na Mwendesha Mashtaka wa Serikali Jordan Kyambo.

✍Omary Mikoma
Mhariri | John Mbalamwezi

06/06/2026

Mapema wiki hii ilizindua mashine ya kisasa ya kubebea na kuhamishia makasha (kontena) kwenye bandari yake kavu maarufu k**a Azam ICD.

Tazama video hii fupi ikieleza faida mbalimbali za mashine hiyo katika kutunza mazingira na kupunguza gharama za uendeshaji huku ikitoa ufanisi zaidi.

05/06/2026

Kampuni ya Said Salim Bakhresa (SSB) imeibuka mshindi wa tuzo sita katika Tuzo za Taifa za Ubora zilizoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) zikihusisha kampuni mbalimbali za uzalishaji na utoaji huduma kutoka sekta binafsi na umma. Tuzo hizo zimetolewa leo Juni 5 jijini Dar es Salaam.

Mhariri

05/06/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amehitimisha ziara yake ya kitaifa ya siku tatu nchini Urusi kwa kushiriki k**a mzungumzaji mkuu katika moja ya mikutano mikubwa na yenye ushawishi mkubwa duniani kuhusu masuala ya uchumi, yaani Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg.

Ziara hiyo, iliyojumuisha mazungumzo ya ngazi ya juu na Rais wa Urusi, Vladimir Putin, inatarajiwa kufungua fursa mpya za biashara, uwekezaji, ushirikiano katika sekta za nishati, madini na elimu kati ya Tanzania na Urusi.

Mwenzetu Hassan Mhelela, aliyeko St. Petersburg anasimulia katika taarifa yake.

Mhariri

05/06/2026

Tanzania imesema inaendelea kutekeleza mambo sita katika kuimarisha sekta ya Ajira, Kazi na Ustawi wa Wafanyakazi.

Maeneo hayo SITA yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu katika Mkutano Mkuu wa 114 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) leo Juni 5, 2026 jijini Geneva, Uswisi.

Msikilize hapa.

Mhariri

05/06/2026

Halmashauri ya wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro imeanza kufanya ukarabati wa lililokuwa jengo la Ikulu ya viongozi wa jadi wa kichaga maarufu k**a ‘Mangi’ ili litumike k**a makumbusho ya Malikale na urithi mwingine wa kitamaduni.

Wadau mbalimbali wamekutana kwenye jengo hili kujadili namna nzuri ya kuendesha makumbusho hayo akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Shadrack Mhagama, Mtafiti wa historia Dkt. Valency Silayo, Katibu wa Machifu mkoa wa Kilimanjaro, Joseph Msele na Agness Robert, Mkurugenzi wa Makumbusho Kanda ya Kaskazini.

Taarifa ya Enos Masanja.

Mhariri

Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo itaendelea kuimarisha ushirikiano katika kuharakisha mageuzi ya sekta ya...
05/06/2026

Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo itaendelea kuimarisha ushirikiano katika kuharakisha mageuzi ya sekta ya afya kupitia utaratibu wa pamoja wa kuandaa mipango mikakati, utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini chini ya mfumo wa Sector Wide Approach (SWAp) ambapo Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zilizofanikiwa kutekeleza mfumo huo kwa takribani miaka 26.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ametoa kauli hiyo wakati wa kikao maalumu cha Wadau wa Maendeleo wa Sekta ya Afya kilichofanyika jijini Dar es Salaam ambapo amesema ushirikiano huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha mifumo ya utoaji huduma za afya nchini na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya sekta hiyo.

Dkt. Shekalaghe ameeleza kuwa utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote (UHI) ni miongoni mwa mageuzi makubwa yanayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya kwa gharama nafuu.

Aidha, amebainisha umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi ili kufanikisha mageuzi hayo, huku akisisitiza haja ya kuongeza uzalishaji wa dawa ndani ya nchi ili kuimarisha upatikanaji wa dawa muhimu na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi.

Mhariri |

05/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linawashikilia watu 75 kwa tuhuma za kufanya vurugu, kuwajeruhi watumishi wa umma pamoja na kushiriki vitendo mbalimbali vya uhalifu katika Kijiji cha Sanjo, Kata ya Idukilo, Wilaya ya Kishapu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna MsaidiziMwandamizi wa Polisi SACP- Janeth Magomi amesema matukio hayo yalitokea kati ya Mei 28 na Juni mosi, 2026, wakati watumishi wa umma walipokuwa wakitekeleza majukumu yao katika eneo hilo.

Mhariri

Address

PLOT 57, 1, 13656 Nelson Mandela Road
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Azam TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Azam TV:

Share