06/06/2026
Zaidi ya walimu 300 mkoani Manyara wameripotiwa kukosa kupandishwa madaraja mwaka huu kutokana na taarifa zao kutokuonekana katika mfumo wa kielektroniki, licha ya wengi wao kutimiza sifa na kuwa na ufaulu mzuri wa kitaaluma.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Manyara, Theophin Joseph amesema changamoto za mtandao zimekuwa zikikwamisha walimu kupata haki zao kwa wakati, ikiwemo kupandishwa madaraja, hali inayopunguza morali na ufanisi kazini.
Ameiomba serikali kuboresha huduma za mawasiliano kwa kuongeza minara ya simu na kuimarisha intaneti, pamoja na kurejesha kikokotoo cha asilimia 55 katika ukokotoaji wa mafao ya walimu, akieleza kuwa hali ya gharama za maisha imeendelea kupanda na kuathiri ustawi wa watumishi hao.
Helen Chikawe
Mhariri | John Mbalamwezi