Halisi TZ

Halisi TZ Life โ€ข vibes โ€ข moments
๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ ๐Ÿ‡ฐ๐Ÿ‡ช ๐Ÿ‡บ๐Ÿ‡ฌ ๐Ÿ‡จ๐Ÿ‡ฉ ๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ฎ ๐Ÿ‡ท๐Ÿ‡ผ political issues and offers Opportunities for entrepreneurs to get more involved.
(3)

Mdm Media is a platform that provides a wide range of information, especially in Kiswahili and English, and highlights the lifestyle and aspirations of the people of Tanzania, Kenya, Burundi,Uganda,Congo DRC between the ages of 18 and 45.

ALIYETELEKEZWA AKIWA ANAUGUA UVIMBE MKUBWA USONI SASA AANZA MAISHA MAPYABinti mwenye umri wa miaka 22, Eliet (Neema) Rwe...
04/06/2026

ALIYETELEKEZWA AKIWA ANAUGUA UVIMBE MKUBWA USONI SASA AANZA MAISHA MAPYA

Binti mwenye umri wa miaka 22, Eliet (Neema) Rwechungura kutoka Bukoba, amepewa nafasi mpya ya maisha baada ya kupitia safari ngumu ya ugonjwa, upweke na changamoto za kifedha zilizokuwa zikihatarisha maisha yake.
Eliet alipoteza wazazi wake akiwa na umri wa miaka mitatu tu na kulelewa na baba mdogo huko Ifakara. Hata hivyo, mwaka 2022 alipofikisha miaka 18, mlezi wake huyo alifariki dunia na kumlazimu kurejea Bukoba kuishi na bibi yake.
Baadaye alipata mwenza na kuhamia naye mkoani Shinyanga. Wakiwa huko, Eliet alianza kuugua uvimbe mkubwa kwenye shavu uliosambaa hadi sehemu ya shingo, hali iliyobadilisha muonekano wake na kuathiri afya yake kwa kiasi kikubwa. Katika kipindi kigumu zaidi, mwenza wake alimtelekeza na kumwacha akiwa hana msaada wala makazi.
Akiwa amekata tamaa hospitalini, muuguzi mmoja wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga aliguswa na hali yake na kuamua kumsaidia kwa gharama za vipimo. Matokeo yalibaini kuwa Eliet alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Ameloblastoma, uvimbe unaoshambulia mfupa wa taya na kusababisha uharibifu mkubwa wa uso.
Kutokana na hali yake, muuguzi huyo alimpa hifadhi na kushirikiana na madaktari wengine kuratibu matibabu yake. Baadaye alipatiwa rufaa kwenda Hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu ya kibingwa, lakini changamoto ya fedha ilikuwa kikwazo kikubwa.
Kupitia juhudi za taasisi ya GH Foundation na michango ya Watanzania wenye moyo wa huruma, Eliet alipata fedha za matibabu na kufanikiwa kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kuondoa uvimbe pamoja na sehemu ya mfupa wa taya iliyoathirika.
Kwa sasa, hali yake inaendelea kuimarika na anaendelea na huduma za kliniki chini ya uangalizi wa wataalamu. GH Foundation pia imemkatia bima ya afya ili kuhakikisha anapata huduma za ufuatiliaji hadi atakapopona kikamilifu.
Hadithi ya Eliet ni ushahidi wa nguvu ya utu, mshik**ano na huruma ya Watanzania katika kuokoa maisha ya wenye uhitaji. Mchango wa madaktari, wauguzi, wafadhili na wananchi mbalimbali umegeuka kuwa tumaini jipya kwa binti ambaye wakati mmoja alikuwa amekata tamaa ya kuishi.
Hakika, pale ambapo matumaini yalionekana kufifia, upendo wa binadamu umeandika historia mpya ya maisha yake. โค๏ธ๐Ÿ™๐Ÿฝ

MSANII ZAY B AFARIKI DUNIA Msanii mkongwe wa Hip Hop Tanzania, Zay B (Zaynab Lipangile), amefariki dunia alfajiri ya leo...
31/05/2026

MSANII ZAY B AFARIKI DUNIA

Msanii mkongwe wa Hip Hop Tanzania, Zay B (Zaynab Lipangile), amefariki dunia alfajiri ya leo nyumbani kwake Temeke, Dar es Salaam, baada ya kusumbuliwa na matatizo ya vidonda vya tumbo.

Zay B anakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika Bongo Hip Hop na Bongo Flava kupitia nyimbo k**a Gado, Monica na Ananitesa. Kifo chake kimeacha simanzi kubwa kwa wadau wa muziki na mashabiki nchini.

Mazishi yanatarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni katika makaburi ya Kinyerezi, Dar es Salaam.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

28/05/2026

Ndugu zetu Wakenya Mbona Hawatusifii Kwa Kufuzu Fainali ya AfconU17๐Ÿคทโ€โ™‚๏ธ๐Ÿค”

HISTORIA MPYA YAANDIKWA SERENGETI BOYS WAFUZU FAINALI YA AFCON U17 Timu ya Taifa ya Tanzania, Serengeti Boys, imeandika ...
28/05/2026

HISTORIA MPYA YAANDIKWA SERENGETI BOYS WAFUZU FAINALI YA AFCON U17

Timu ya Taifa ya Tanzania, Serengeti Boys, imeandika historia mpya kwenye soka la Afrika baada ya kufuzu hatua ya Fainali ya AFCON U17 ikiwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo.

Hii ni hatua kubwa ambayo haijawahi kufikiwa na timu yoyote ya vijana wa chini ya miaka 17 nchini, na inaonesha maendeleo makubwa ya soka la vijana Tanzania. Zaidi ya kufuzu Nusu Fainali, Serengeti Boys pia wameweka rekodi nyingine ya kihistoria kwa kukata tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia la U17, linalotarajiwa kufanyika nchini Qatar mwezi Novemba 2026.

27/05/2026

EID MUBARAK ๐Ÿ•Œ
Vipi unasherehekea EID Al ADHAA ukiwa mkoa gani na eneo gani โœ๏ธ

Huyu ni moja ya wasanii maarufu nchini Congo kipindi hicho je anaitwa nani?โœ๏ธ
26/05/2026

Huyu ni moja ya wasanii maarufu nchini Congo kipindi hicho je anaitwa nani?โœ๏ธ

Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha Xin Lin, Baozhang Ge (50) umechomwa moto leo hadi kuwa majivu katika eneo l...
24/05/2026

Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha Xin Lin, Baozhang Ge (50) umechomwa moto leo hadi kuwa majivu katika eneo la uchomaji Makumbusho Jijini Dar es salaam.

Baozhang Ge aliuawa usiku wa Mei 16, 2026 katika eneo la kiwanda chake Mabibo na wanaodaiwa kuwa ni Walinzi wake kisha kuondoka na kiasi cha fedha shilingi milioni 10.

Baada ya kukabidhiwa majivu ya Ge, mdogo wa marehemu Denis Jerry ameshukuru na kusema: โ€œAsanteni sanaโ€. Majivu ya Baozhang yatasafirishwa hadi China kwa ajili ya taratibu nyingine za kimazishi.

Mazishi ya Mchina aliyeuawa na Wamasai yamewaacha watu wengi wakiwa katika huzuni kubwa na majonzi mazito ๐Ÿ˜ข๐Ÿ•Š๏ธTukio hilo ...
23/05/2026

Mazishi ya Mchina aliyeuawa na Wamasai yamewaacha watu wengi wakiwa katika huzuni kubwa na majonzi mazito ๐Ÿ˜ข๐Ÿ•Š๏ธ

Tukio hilo limeibua simanzi kwa wengi kutokana na mazingira ya kifo chake pamoja na picha za maombolezo zilizoonekana wakati wa mazishi hayo. Watu mbalimbali wameendelea kutoa salamu za pole na kuombea familia pamoja na ndugu wa marehemu wapate nguvu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao. ๐Ÿ™๐Ÿ’”

Mtandao wa Facebook hautakuruhusu kuandika hivi๐Ÿ‘‰ @ [4:0] kwenye sehemu ya maoni (comment section); itatafsiriwa kuwa Mar...
23/05/2026

Mtandao wa Facebook hautakuruhusu kuandika hivi๐Ÿ‘‰ @ [4:0] kwenye sehemu ya maoni (comment section); itatafsiriwa kuwa Mark Zuckerberg mmiliki wa Mtandao huo.

Ijaribu uone ukiweza kuandika Nakupaa kongole.๐Ÿ˜ƒ๐Ÿ‘๐Ÿ’ช๐Ÿคณ

WANAKUJA KITAA KULINDA RAIAAskari wapya wa Jeshi la Polisi wakionesha vitendo vya ukak**avu wakati wa Sherehe za kufunga...
22/05/2026

WANAKUJA KITAA KULINDA RAIA

Askari wapya wa Jeshi la Polisi wakionesha vitendo vya ukak**avu wakati wa Sherehe za kufunga mafunzo ya Awali ya Askari Polisi Mei 22, 2026 Shule ya Polisi Tanzania -Moshi.

Askari hao wapya leo wamsikiliza nasaha na hotuba wakati wa Sherehe za kufunga Mafunzo ya Awali ya Askari Polisi Mei 22, 2026.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi TZ:

Share