Halisi Media

Halisi Media Halisi Media Inakupatia Taarifa Mbalimbali Za Burudani,Sanaa na Michezo kutoka Kila pande Ulimwenguni
(4)

Mdm Media is a platform that provides a wide range of information, especially in Kiswahili and English, and highlights the lifestyle and aspirations of the people of Tanzania, Kenya, Burundi,Uganda,Congo DRC between the ages of 18 and 45. political issues and offers Opportunities for entrepreneurs to get more involved.

22/07/2025

"Elon Musk Azindua Mgahawa wa Tesla Unaoendeshwa na Maroboti – Je, Hii Ni Hatari kwa Ajira?" 😳

Elon Musk amezindua mgahawa wa chakula cha jioni wa Tesla. Kwenye mgahawa huo, maroboti yake yanayojulikana k**a Tesla Optimus ndiyo yanayowahudumia wateja wanaoingia. Maroboti haya ni rafiki sana na yanaweza kufanya kazi saa 24 bila kuchoka. Pia yana uvumilivu na yanaweza kupiga picha na wateja endapo watapenda.

Ingawa hii ni jambo la kuvutia sana, pia linaathiri ajira. Kazi ambayo ingeweza kufanywa na watu wengi sasa inafanywa na roboti. Roboti linaweza kufanya kazi saa 24 bila kuchoka, lakini binadamu lazima atachoka.

Funzo la Maadili: Hongera Elon, lakini tafadhali asituchukulie kazi zetu.

22/07/2025

Staa wa muziki wa Bongo Harmonize amewasha moto mitandaoni baada ya kushare video kupitia Insta Story akidokeza ujio wa albamu yake mpya ya sita mwaka huu!

Katika ujumbe huo, Konde Boy amejinasibu kuwa safari hii haichezi bongo tu muziki wake ni wa kimataifa kabisa, na albamu hiyo inalenga moja kwa moja tuzo za Grammy

“It’s a World Music Album – Grammy Level Only!” 🎤🌍

Upo tayari kwa hili kubwa kutoka kwa Konde Gang?

22/07/2025
Gusa Kati kati Acha comment yako✍️
22/07/2025

Gusa Kati kati Acha comment yako✍️

Alimtabiria dogo Paten miezi miwili tu kwenye game... kumbe mwenyewe hakuivuka hata siku mbili kazini! 😅
Life huwa halina script bro — ni scene moja tu, unageuziwa camera 📸

Ulimtazama dogo Paten kwa jicho la mashaka, ukamsahau Mungu hutoa timing ya ajabu.
Leo una pause, yeye anasonga — hivyo ndivyo maisha yalivyo.

FUNZO 📌
Usimsemee mwisho wa mtu kwa sauti ya juu hujui mwanzo wako utasikika kwa kimya kikubwa.”
Maisha hubadilika haraka. Leo ni wao, kesho ni wewe. 🙏

22/07/2025
22/07/2025

Ni ajabu sana jinsi watoto wanavyokua haraka!
Emmanuella wa jana sasa amekuwa binti mkubwa. 👧🏽✨

Kwa sasa ni miongoni mwa watoto maarufu barani Afrika,
na ameweza kuwaburudisha watu wazima na watoto kwa kipaji chake cha kipekee. 🎬🌍

Heshima kubwa kwa Mark Angel kwa kugundua na kukuza kipaji hiki. 🙌🏽
Tunakutakia maisha marefu yenye furaha na mafanikio zaidi, Emmanuella! 💖🎂

22/07/2025

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Gigy Money ameweka picha mpya iliyoambatana na ujumbe ulioibua gumzo mitandaoni

“Haya wanaume wasio oa mke ndio huyo anapita 😅 (Nipe nafasi nikupende 🥰❤️)”

Kauli hiyo imewaacha mashabiki na maswali kibao je, kuna dalili ya kutibuana na mpenzi wake wa muda mrefu? Au ni kiki tu?

KITAELEWEKA😂

22/07/2025

Staa wa Bongofleva Zuchu amefunguka kwa hisia kali kupitia Insta Story yake, akieleza kuwa licha ya kupenda kuandika muziki, mara nyingi hulazimika kujibeba mwenyewe bila msaada wowote.

“Kuandika muziki wangu mwenyewe ni k**a tiba, lakini pia ni ngumu kwa sababu sina msaada… ni mimi na producer tu, nawaza kila kitu mwenyewe,” amesema Zuchu

Je, wasanii wengine wana changamoto k**a hizi pia? 😓🎶

22/07/2025

Kundi La Muziki Nchini La Wametangaza Rasmi Kubadili Jina Lao Kutoka ‘Navy Kenzo’ Hadi ‘Aika & Nareel’.

Kupitia Ukurasa Wao Wa Instagram Wamethibitisha Hilo Kwa Kutoa Taarifa Iliyosomeka; 👇

“KUBADILI JINA KUTOKA NAVY KENZO KUITWA “AIKA & NAHREEL”

Tangu mwanzo wa safari yetu ya muziki, mmekuwa nasi mkitupa moyo, nguvu, na mapenzi yasiyoisha.

Leo tunatangaza rasmi kwamba jina letu la kisanii “Navy Kenzo” linafika mwisho wake, na tunaanza ukurasa mpya tukitwa: Aika & Nahreel.

Hatubadili kiini cha muziki wetu, bali tunaufanya uwe wa karibu zaidi, halisi zaidi, na wa kweli kwetu k**a wasanii na watu binafsi.

Kwa wote mlioamini katika sisi, mkashika mikono yetu na kutembea nasi, tunawashukuru kwa dhati.

Upendo wenu ndiyo umetufikisha hapa. Na upendo wenu huo huo ndio unatusukuma katika sura hii mpya.

Yours Truly,
Aika & Nahreel” - Navy Kenzo

22/07/2025
22/07/2025

📢 NAFASI ZA AJIRA MJINI FM 92.5 DAR ES SALAAM 📢

Baada ya kusimamishwa kwa watangazaji wa kipindi cha kufuatia sakata la Dogo Paten, sasa MJINI FM wanatangaza nafasi mpya za kazi kwa watangazaji wapya! 🎙️🔥

Wanakaribisha:

✅ Watangazaji waliopitia vyuo vya habari kutoka Bara na Zanzibar (Cheti lazima kitambuliwe na Bodi ya Ithibati)
✅ Pia, k**a una kipaji cha utangazaji lakini hujapata nafasi ya kusoma – fursa hii ni yako pia utapelekwa chuo ili upate chetikinachotambuliwanaBodiyaIthibati! 🌟

🎯 SIFA ZINAZOTAKIWA:
📌 Cheti kinachotambulika na Bodi ya Ithibati
📌 wenye Kipaji cha utangazaji – Tuma video fupi kupitia WhatsApp: 0716 925 925

🎓 BONUS: Ukichaguliwa na huna elimu ya habari, MJINI FM itagharamia masomo yako ya Uandishi wa Habari! 👏🏾📚

📩 Tuma maombi yako sasa kupitia barua pepe:
👉🏽 [email protected]

⏳ Usikose nafasi hii ya KIPEKEE ya kuanza safari yako ya redio!

Funzo la Maisha: Wote mtakaopata kazi mshahara wenu wa kwanza msisahau kumpa fungu Dogo Paten

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Media:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share