Halisi Media

Halisi Media Halisi Media Inakupatia Taarifa Mbalimbali Za Burudani,Sanaa na Michezo kutoka Kila pande Ulimwenguni
(3)

Mdm Media is a platform that provides a wide range of information, especially in Kiswahili and English, and highlights the lifestyle and aspirations of the people of Tanzania, Kenya, Burundi,Uganda,Congo DRC between the ages of 18 and 45. political issues and offers Opportunities for entrepreneurs to get more involved.

18/09/2025
18/09/2025

Mmiliki wa kampuni ya Meta, Mark Zuckerberg, ametambulisha miwani na bangili za kiteknolojia zitakazoweza kuchukua nafasi ya simu na kompyuta kwa matumizi mengi ya kila siku.

Bidhaa hizi zitaanza kuingia sokoni kuanzia Septemba 30, huku baadhi zikitarajiwa kutambulishwa rasmi Oktoba 21.
Bei yake inaanzia USD $3,636 (zaidi ya Milioni 9 za Kitanzania).

18/09/2025

"Natumai ujumbe huu utakupata vyema. Ninaandika ili kueleza wasiwasi wangu na kufadhaika kwangu kuhusu malipo ambayo bado hayajalipwa kwa utendakazi wangu wa hivi majuzi jijini Nairobi mnamo Agosti 30, 2025. Kulingana na makubaliano yetu na mawakala wako katika LEAP Creative Agency,

salio kamili la huduma zangu lililipwa baada ya kukamilisha tukio, lakini licha ya uvumilivu wangu na uelewa wa timu yangu, bado sijapokea malipo kamili. Timu yangu ya usimamizi imekuwa katika mawasiliano ya mara kwa mara na wanachama mbalimbali wa wakala wa LEAP akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wake, Bw. Roshan Soomarshun bila mafanikio. POP zinazodhaniwa zilitumwa ambazo baadaye hazikuweza kuthibitishwa, za kutiliwa shaka na kwa wazi hazikutumwa au kulipwa.

Nimeshikilia mwisho wangu wa makubaliano kwa kutoa utendakazi ambao nilijitolea kikamilifu ili kuhakikisha unakidhi viwango vya juu zaidi. Inasikitisha sana kupata kwamba kiwango sawa cha taaluma hakijapanuliwa kwa malipo linapokuja suala la kutimiza majukumu yako ya kifedha.

K**a msanii, ninatarajia kutendewa kwa heshima na haki ambayo msanii yeyote wa kitaalamu anastahili. Ucheleweshaji huu sio tu wa haki lakini pia haukubaliki kabisa. K**a msanii nilidondosha maonyesho niliyoweka awali ili niweze kushiriki onyesho la mwisho sitarajii kutendewa isivyo haki. Ni muhimu kwamba salio litatuliwe mara moja bila kucheleweshwa au kuahirishwa, vinginevyo, sitakuwa na chaguo ila kuchukua hatua zaidi kurejesha pesa zinazodaiwa.

Ninaamini utachukua hatua za haraka kutatua suala hili na kuheshimu masharti ya makubaliano yetu."

Ni maneno mazito aliyoyachapisha kupitia ukurasa wake wa instagram akidai malipo yake baada ya onesho lake pale Nairobi kwenye fainali za CHAN

18/09/2025

๐Ÿ“Š Matokeo ya Awali ya Uchaguzi Malawi ๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ผ

Ripoti za awali zinaonyesha kuwa Kiongozi wa Upinzani, Prof. Arthur Peter Mutharika, anaongoza katika maeneo kadhaa dhidi ya Rais wa sasa, Dkt. Lazarus Chakwera.

๐Ÿ”น Matokeo rasmi ya mwisho bado hayajatangazwa na Tume ya Uchaguzi.
๐Ÿ”น Matarajio ni kwamba mshindi wa urais lazima apate zaidi ya 50% ya kura, vinginevyo kutakuwa na duru ya pili ya uchaguzi.

โœจ Funzo la Maadili: Kweli si jambo la kawaida โ€” Rais aliyepo madarakani anaweza kuelekea kuondoshwa madarakani kwa nguvu ya kura za wananchi ๐Ÿค”.

18/09/2025

Mwanamitandao maarufu kutoka Nigeria na msanii wa Tanzania wanaendelea kuacha mashaka mitandaoni kuhusu ukaribu wao. Awali wengi walidhani ni utani au kiki, lakini matukio yanavyozidi kuonekana yanaashiria huenda kuna jambo zaidi.

Hivi karibuni, Phina alisafiri hadi Nigeria na kuonekana akifurahi kimahaba na Enioluwa katika maeneo mbalimbali. Leo tena jamaa huyo amepakia video na picha mpya wakionekana wakiwa na bashasha tele kana kwamba mapenzi yao yanazidi kushamiri.

Je, unaona huu ni utani wa kawaida au kweli kuna โ€œlove storyโ€ inayoendelea? ๐Ÿ˜…โค๏ธ

18/09/2025

Wataalamu wa Magari Mje Mtuambie โœ๏ธ

18/09/2025

Hakika Vita si lelemama! Picha ya kushoto alipiga wakati anaagwa kwenda vitani, picha ya kulia akipokewa baada ya kurejea kutoka vitani!

18/09/2025

Staa wa muziki kutoka nchi9ni Nigeria Tiwa savage amefunguka kile kilichotokea kwenye mahusiano yake ya nyuma na kueleza namna alivyonyanyaswa kwenye hayo mahusiano

โ€œNimekaa kimya kwa miaka miwili nikivumilia. Fikiria niko chumbani, njaa inanibana, sherehe inaendelea, siwezi kutoka kwa sababu hataki watu wajue kuhusu sisi,โ€ alisimulia kwa uchungu. Aliendelea kufichua kuwa hakuwa hata akiwekewa vitafunwa au maji wakati wa hali hizo, na visa hivyo vilitokea Nigeria, New York na Los Angeles.

Tiwa aliyasema hayo kupitia mahojiano na Joe Budden Podcast

18/09/2025

SAWA DADA TUSHAJUA K**A SIO YAKO BASI YAISHEE ๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi Media:

Share