Digitaltvtz Update

Digitaltvtz Update Television & Radio Broadcasting 📻📺

Follow Us On YouTube Digitaltvtz Update 👇

https://youtube.com/-p5p?si=5C_v4m_ggmX-L-zF

08/10/2025

Mahakama Kuu ya Tanzania Masijala Ndogo ya Dar es salaam imepanga Oktoba 9, 2025 kusikiliza maombi ya Wakili Peter Kibatala juu ya madai ya kutekwa kwa Mwanasiasa Humphrey Polepole.

Wakili Kibatala aliwasilisha maombi hayo chini ya hati ya dharura, Oktoba 7, 2025 akiiomba mahakama itoe amri ya Polepole afikishwe mahakamani ama mamlaka husika ziseme yupo wapi.

Kwa mujibu wa hati iliyosajiliwa baada ya kupokelewa kwa maombi hayo imepewa namba 24514 ya mwaka 2025 na imepangwa kusikilizwa mbele ya Jaji Salma Maghimbi, ambapo katika maombi yake, Kibatala ameiomba Mahakama iingilie kati mara moja akidai kuwa Polepole alitekwa nyara alfajiri ya Jumatatu, Oktoba 6, 2025, kutoka katika makazi yake yaliyoko eneo la Ununio, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam na watu wasiojulikana wanaoshukiwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi la Tanzania.

Katika hati hiyo ya dharura Wakili Kibatala ameieleza Mahakama kuwa Polepole hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote la jinai katika Mahakama yoyote, na kwamba kwa sasa inaaminika anashikiliwa katika eneo lisilojulikana na maafisa wa Jeshi la Polisi.

Maombi hayo yamewasilishwa dhidi ya wajibu Maombi watano akiwemo Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Afisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalum ya Dar es Salaam (RCO) na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar

Digitaltvtz Update

07/10/2025

Mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameyasema hayo leo katika Wilaya ya Sengerema Jijini Mwanza na Kusisitiza kua "tutaiheahimisha nchi yetu tukiwa na amani, tukifanya uchaguzi bila matatizo, vurugu au zogo.

Tutaiheahimisha nchi yetu tukizingatia sheria zetu, tukiitafuta haki na kila mtu akapata haki yake"

Video Kamili ipo YouTube Channel yetu ya Digitaltvtz Update

07/10/2025

Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Antipas Lissu, inaendelea katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam ambapo kwa sasa, imeahirishwa kwa muda na inatarajia kuendelea tena Alasili hii.

Kilichojiri, Lissu ameendelea kumuuliza maswali dodosi (cross examination) shahidi wa Jamhuri ACP George Wilbert ambaye alianza kutoa ushahidi wake hapo jana.

Digitaltvtz Update

07/10/2025

Mgombea Ubunge wa CUF jimbo la Kakonko, Damas Filbert amemuunga mkono mgombea wa jimbo hilo kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Olaf Kaboboye.

Tukio hilo lilifanyika wakati wa mkutano wa kampeni wa mgombea ubunge wa ACT Wazalendo uliofanyika katika kata ya Katanga, Oktoba 06, 2025

Damas alisema uamuzi wake huo unatokana na wote wawili kuwa na dhamira moja ya kuwatetea wananchi wa chini na ili hilo lifanikiwe ni muhimu kudhibiti mgawanyiko wa kura za wananchi

Digitaltvtz Update

06/10/2025

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema linafuatilia taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu kutekwa kwa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole na kwamba limekuwa likimsubiri afike katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai.

Mapema hii leo zilienea taarifa mbalimbali katika mitandao ya kijamii na zilizothibitishwa na familia ya Polepole kwamba ndugu yao ametekwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake.

Digitaltvtz Update

゚viralシviralシfypシ゚viralシalシ

06/10/2025

Mgombea Urais aliyeteuliwa na Chama cha ACT-Wazalendo Bw. Luhaga mpina tayari amefika Mahakama Kuu Masjala Kuu Dodoma kusikiliza shauri Lake walilolifungua pamoja na Chama cha ACT- Wazalendo wakipinga kuondolewa katika mchakato wa kugombea nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi huu Oktoba, 2025

06/10/2025

Hali ya mvutano imetokea baina ya mawakili wa Jamhuri na baadhi ya mawakili wa upande wa Lissu pamoja wafuasi wa Chadema wakigombea sehemu ya kukaa katika ukumbi wa Mahakama kuu baada ya Jaji kutoa mapumziko ya dakika 30 ,ndipo imetokea hali hiyo ya yakutoelewana na kuanza kutupiana maneno.

Ndani ya ukumbi huo Leo ni tofauti na siku nyengine ambazo kesi hiyo imekua ikiendelea,ambapo wafuasi na wafuatiliaji ni wachache, wengi wakiwa ni mawakili wa Jamhuri na waupande wa Lissu na baadhi ya maofisa wa Mahakama huku wanachama na viongozi wa Chadema Wakiwa ni wachache tofauti na hapo awali.

06/10/2025

Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa, bado linaendelea kumsubiri Ndg. Humphrey Polepole aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai huku pia likikiri kuona taarifa ya kutekwa kwake na wameanza uchunguzi.

“Ndg. Humphrey Polepole alitumiwa barua ya wito kwa mujibu wa Sheria za nchi aripoti katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ili atoe
maelezo kuhusiana na tuhuma mbalimbali alizozitoa kupitia Mitandao ya Kijamii làkini hadi leo hajatekeleza maelekezo hayo kwa mujibu wa Sheria.
“Jeshi la Polisi limeona taarifa zinazosambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii na ndugu zake kuwa ametekwa, tayari tumeanza kufanyia kazi taarifa husika ili kupata ukweli wake”- imeeleza taarifa ya Jeshi la Polisi

Digitaltvtz Update

06/10/2025

Jopo la Mawakili wa Jamhuriwakiongozwa na Wakili Mkuu Nassoro Katuga walivyowasili Mahakamani leo hii, Juma tatu Oktoba 6, 2025

Endelea kua karibu na kwa taarifa zaidi

06/10/2025

Kutokea hapa Mahakama Kuu masjala ndogo ya Dar es salaam, Leo kesi inayomkabili Mwenyekiti Wa Chama Cha Demokrasia Na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu inaendelea na Digitaltvtz Update ipo hapa kukujuza kile kinachoendelea Mahakamani muda huu.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255788509024

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Digitaltvtz Update posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Digitaltvtz Update:

Share