Digitaltvtz Update

Digitaltvtz Update Television & Radio Broadcasting 📻📺

Follow Us On YouTube Digitaltvtz Update 👇

https://youtube.com/-p5p?si=5C_v4m_ggmX-L-zF

17/01/2026

Polisi katika mji mkuu wa Uganda, Kampala, wametumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais. Waandamanaji hao pia walikuwa wamewasha moto barabarani, hatua iliyolazimu polisi kuzima mioto hiyo.

Tume ya Uchaguzi ya Uganda imetangaza matokeo ya awali yanayomuonesha Rais Yoweri Museveni ambaye amekuwa madarakani tangu 1986 akiongoza kwa zaidi ya asilimia 70 ya kura. Uchaguzi huo umechafuliwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo kuzimwa kwa intaneti nchini kote, ucheleweshaji wa upigaji kura katika baadhi ya vituo, pamoja na madai ya upinzani ya kujazwa kwa masanduku ya kura.

Cc

Tume ya Uchaguzi ya Uganda Leo January 17, imemtangaza Yoweri Museveni, mwenye umri wa Miaka 81, kuwa mshindi wa Uchaguz...
17/01/2026

Tume ya Uchaguzi ya Uganda Leo January 17, imemtangaza Yoweri Museveni, mwenye umri wa Miaka 81, kuwa mshindi wa Uchaguzi Mkuu wa Uganda uliofanyika Januari 15, 2026, akipata Asilimia 71.6 ya jumla ya kura halali zilizopigwa, na kuendeleza utawala wake zaidi ya miongo minne.

17/01/2026

🗣️Makamu mwenyekiti Wa Chama Cha ACT Wazalendo Tanzania Bara Isihaka Mchinjita

゚viralシviralシfypシ゚viralシalシ ♥️

17/01/2026

"Sisi tunaamini Maridhiano ni Mchakato, Unaohitaji Ujasiri, Muda na utayari wa Kusikilizana kwa kuheshimiana kwa pande zote na Mwisho ni kutekeleza yale mliyokubaliana kwa mustakabali mpana wa taifa letu" Dorothy Semu Kiongozi Wa Chama Cha Act Wazalendo



Powered by

16/01/2026

Alex Mufumbiro ambaye ni Naibu Msemaji wa chama kikuu cha upinzani cha National Unity Platform (NUP), ameshinda nafasi ya Ubunge wa Nakawa East katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Januari 15, 2026 (Jana) , ushindi ambao ameupata akiwa katika Gereza la Luzira Jijini Kampala tangu Septemba 2025.

Mufumbiro amepata Asilimia 78 ya kura katika nafasi hiyo, ambapo hakufanya kampeni wala hakushiriki katika mdahalo wowote wa hadhara.

Powered by

15/01/2026

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Muheshimiwa amefanya uhakiki wa Ugawaji wa Hekari 2 za Shamba Kwa Kila Kijana Wilayani humo.

Akiongoza tukio hilo katika Kijiji cha Kihesa Mh. Petro Magoti amewataka Vijana Wilayani humo kutumia fursa hiyo kwa Kuanzisha Kilimo cha biashara na chakula ili waweze kujiinua kiuchumi k**a vile Ufuta, mbazi,Maharage, Mahindi na Pamba

Tufuatilie YouTube, Instagram, Facebook

Powered by

14/01/2026

Mgongano wa kikatiba umejitokeza katika Mahak**a Kuu ya Zanzibar baada ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwasilisha pingamizi ikidai kuwa Mahak**a hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uchaguzi wa wabunge.

Kwa upande wa walalamikaji, mawakili wao wakiongozwa na Wakili Msomi Omar Said Shaaban walipinga pingamizi hilo wakieleza kuwa Mahak**a Kuu ya Zanzibar ina mamlaka kamili ya kikatiba kusikiliza mashauri hayo, ikiwemo yanayohusu Muungano. Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Mahak**a imeahirisha kesi hadi tarehe 27 Januari 2026 kwa ajili ya kutoa uamuzi juu ya pingamizi la kikatiba

Cc

14/01/2026

🎥 Aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Mheshimiwa George Simbachawene leo January 14 amekutana na Waziri Mteule Mh. Patrobas Katambi na kumkabidhi ofisi, Video kamili tufuatilie YouTube Link on Bio.

Powered by

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255788509024

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Digitaltvtz Update posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Digitaltvtz Update:

Share