Digitaltvtz Update

Digitaltvtz Update Television & Radio Broadcasting 📻📺

Follow Us On YouTube Digitaltvtz Update 👇

https://youtube.com/-p5p?si=5C_v4m_ggmX-L-zF

Siasa za Tanzania zinajenga umoja au zinachochea mgawanyiko?
13/06/2026

Siasa za Tanzania zinajenga umoja au zinachochea mgawanyiko?

Follow  Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza kusitisha mashambulizi mapya ya kijeshi yaliyokuwa yamepangwa kufanyi...
11/06/2026

Follow
Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza kusitisha mashambulizi mapya ya kijeshi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika dhidi ya Iran, akieleza kuwa hatua hiyo inalenga kutoa nafasi kwa mazungumzo ya amani yanayoendelea.

Kwa mujibu wa taarifa yake, majadiliano kati ya pande husika yamefikia ngazi ya juu ya uongozi wa Iran na yameidhinishwa, jambo ambalo limeongeza matumaini ya kupatikana kwa suluhisho la kidiplomasia badala ya kuendelea kwa mapigano.

Hata hivyo, Trump amesema hatua nyingine za shinikizo dhidi ya Iran zitaendelea kutumika hadi makubaliano ya mwisho yatakapokamilika.

Muungano wa Tanzania umefikisha miaka 64 , ukiwa nguzo ya umoja na mshikamano wa Taifa.Je, kizazi cha sasa kinauelewa vy...
11/06/2026

Muungano wa Tanzania umefikisha miaka 64 , ukiwa nguzo ya umoja na mshikamano wa Taifa.

Je, kizazi cha sasa kinauelewa vya kutosha? Na ni nini kifanyike ili kuudumisha na kuuimarisha kwa vizazi vijavyo?... Elimu ya Muungano inatosha? ... Vijana wanashiriki vya kutosha kuuenzi? .. Ni maboresho gani ungependekeza?

:::

10/06/2026

Watu Wanne Wakamatwa Kuhusiana na Mauaji ya Mfanyabiashara wa China Dar es Salaam

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watu wanne wanaodaiwa kuhusika katika mauaji ya mfanyabiashara raia wa China, Baozhang Ge.

Taarifa hiyo imethibitishwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro.
Kwa mujibu wa polisi, watuhumiwa hao walikamatwa katika maeneo mbalimbali nchini baada ya uchunguzi kubaini ushiriki wao katika tukio hilo. Aidha, polisi walifanikiwa kurejesha kiasi cha fedha kinachokadiriwa kufikia shilingi milioni tisa ambacho kinahusishwa na tukio hilo.
Marehemu Baozhang Ge alikuwa mmiliki wa kiwanda cha kuchakata makopo kilichopo Mabibo, Dar es Salaam. Alifariki dunia baada ya kuuawa Mei 16, 2026, huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

Jeshi la Polisi Tanzania limetoa taarifa kuhusu uchunguzi wa mauaji ya raia wa China, Bhaozan Li, yaliyotokea katika ene...
10/06/2026

Jeshi la Polisi Tanzania limetoa taarifa kuhusu uchunguzi wa mauaji ya raia wa China, Bhaozan Li, yaliyotokea katika eneo la Mabibo, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, uchunguzi wa kina ulioanza Mei 16, 2026 umewezesha kukamatwa kwa watuhumiwa wanne wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo.

Jeshi la Polisi limesema watuhumiwa hao walipanga njama ya kumvamia marehemu usiku, kumshambulia na kumuua baada ya kuiba kiasi cha shilingi milioni tisa kilichokuwa ndani ya kiwanda chake cha kuchakata chuma. Baada ya kutekeleza tukio hilo, watuhumiwa walitoroka na baadaye kukamatwa katika maeneo ya Namanga, Arusha na Mabibo, Dar es Salaam.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa uchunguzi unaendelea huku hatua za kisheria zikichukuliwa dhidi ya watuhumiwa hao.

10/06/2026

Chaumma haitumiki Kuvikosoa Vyama Vingine Vya Upinzani

Fuatilia Mahojiano haya na Aliyekuwa Mgombea Ubunge Wa Jimbo la Kilosa 2025 Kwa tiketi ya Chama Cha Ukombozi Wa Umma Mr David Chiduo Digitaltvtz Update

10/06/2026

Unakubaliana na kauli ya Super Julio Kocha Mkuu wa Mashujaa FC?

Powered by Afrimex Courier

Je, wewe unaenda na taifa gani mwaka huu? 👇😀 tuambie hapo tuungane Mapema Digitaltvtz Update Digitaltvtz Supporters 📻&📺 ...
09/06/2026

Je, wewe unaenda na taifa gani mwaka huu? 👇😀 tuambie hapo tuungane Mapema

Digitaltvtz Update Digitaltvtz Supporters 📻&📺

09/06/2026

Aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Kilosa Kwa tiketi ya Chama Cha Ukombozi Wa Umma na N/Mkurugenzi David Chiduo Akifafanua mchakato halali uliotumika kuwapata Wabunge wa Viti Maalumu Chaumma

Video Kamili ipo YouTube channel ya Digitaltvtz Update

Kwa Nini Vigogo wengi  Wanahama Vyama Katika Kipindi cha Uchaguzi?Wakati uchaguzi unapokaribia, mara nyingi tunaona wana...
08/06/2026

Kwa Nini Vigogo wengi Wanahama Vyama Katika Kipindi cha Uchaguzi?

Wakati uchaguzi unapokaribia, mara nyingi tunaona wanasiasa wakihama kutoka chama kimoja kwenda kingine, Wapo wanaosema ni haki yao ya kidemokrasia kuchagua wanapoona wanaweza kutimiza malengo yao, huku wengine wakiamini kuwa hatua hizo husukumwa zaidi na tamaa ya madaraka au nafasi za uongozi.

Je, kuhama chama wakati wa uchaguzi ni ishara ya kukua kwa demokrasia na uhuru wa kisiasa, au ni mkakati wa kutafuta madaraka na maslahi binafsi?
👇

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255788509024

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Digitaltvtz Update posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Digitaltvtz Update:

Share