03/02/2026
MAOMBI YA MFALME HEZEKIA - PART 1
Baada ya kufa kwake Mfalme Sulemani mwana wa Daudi, mwanaye Rehoboamu akatawala juu ya Israeli yote, hata hivyo hakwenda katika njia sahihi mbele za Mungu kwani aliacha shauri la wazee akafuata shauri la vijana.
Mpasuko ukatokea miongoni mwa kabila 12 za Israeli, Yeroboamu mwana wa Nebati akiongoza mgogoro huo kwa kutaka makabila ya Israeli yajitenge.
Mwisho kabisa, Yeroboamu akafanikiwa kuyashawishi makabila 10 ya Israeli kumfuata na kufanya Reheboamu kubaki na makabila mawili pekee yaani Yuda na Benjamini.
Makabila 10 yakaanzisha ufalme wa kaskazini ulioitwa, Ufalme wa Israeli katika mji wa Samaria huku makabila mawili yakabaki kusini, Yerusalemu ambapo ufalme wao uliitwa Ufalme wa Yuda.
Makabila ya kaskazini yakamwasi Mungu kwa kufuata ibada za sanamu kiasi cha kutokwenda Yerusalemu kumtolea Mungu dhabihu katika sikukuu za pasaka, uasi huu uliongozwa na Yeroboamu mwenyewe. Ikawa hivyo miaka mingi kiasi cha kwamba Mungu sasa akatuma manabii kuhubiri hukumu na ya kwamba watu warudi katika njia sahihi.
Eliya mtishibi alikuwa ndiye nabii wa kwanza kuhubiri toba katika nyumba ya mfalme Ahabu na mkewe Yezebeli, hata hivyo nyumba ya Israeli walizidi kurudi nyuma na kumuasi Mungu zaidi, maanabii k**a Elisha, Amosi na Hosea nabii wa mwisho walifuatia kuendeleza kile ambacho Eliya alikianza lakini bado hali ikawa ngumu.
Mungu mwenyewe akamwambia Hosea "Efraimu amejifungamanisha na sanamu, mwache" Hos 4:17, kwahio Mungu akawaacha kabila 10 maana waliukataa wokovu.
Katika enzi hizo palikuwa na falme mbili zenye nguvu, yaani Ashuru na Misri. Mfalme wa Ashuru alikusudia kutanua mipaka yake kwa kuzivamia falme jirani, mfalme wa Ashuru akaazimia kuivamia Israeli na katika mwaka 722 akaiangusha Israeli yote na kuwa mwisho wa makabila 10 za Israeli maana kwa Ashuru kwao kuua ilikuwa k**a mchezo.
...............