Petro Mlungu

Petro Mlungu instgram.com@cheka_kidogo_tu

Nimepokea taarifa rasmi Kutoka kwa Wakili Emmanuel Ukashu ambaye baada ya kupata taafifa za kuk**atwa kwa wahusika na Ku...
20/05/2025

Nimepokea taarifa rasmi Kutoka kwa Wakili Emmanuel Ukashu ambaye baada ya kupata taafifa za kuk**atwa kwa wahusika na Kuombwa na Mawakili wao tusaidie jambo hili na Msisitizo wa Ombi kutoka kwa Rais wa LSK Adv.Faith Odhiambo

Nimepokea hivi punde taarifa toka kwa Wakili Emmanuel Ukashu zikithibitisha kuwa Bwana Boniface Mwangi, mwanahabari na mtetezi wa haki za binadamu kutoka Kenya, pamoja na Bi. Agatha Atuhaire, mwanahabari na wakili kutoka Uganda, ambao walikuwa wakishikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tangu tarehe 19 Mei 2025, wamefukuzwa na kurejeshwa katika nchi zao za asili.

Inadaiwa kuwa Bwana Mwangi alik**atwa kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo kwa ajili ya kuingia nchini, ambapo aliwasili Tanzania tarehe 18 Mei 2025.

Watu hao wawili wameondolewa nchini kwa kusindikizwa rasmi na maafisa wa Idara ya Uhamiaji ya Tanzania.

K**a marafiki wa haki za binadamu, utawala wa sheria na katiba katika ukanda wa Afrika Mashariki, tunayo dhamana ya kuendelea kushirikiana na mamlaka zetu kuhakikisha kuwa mikataba ya kikanda, katiba na sheria za kitaifa na kimataifa zinazolinda haki za binadamu, wanahabari na watetezi wa haki, zinazingatiwa ipasavyo ili kuimarisha misingi ya utawala wa sheria katika ukanda wetu.

Tunasihi umuhimu wa kuheshimu misingi iliyowekwa chini ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu, pamoja na nyaraka nyingine zinazotambulika kimataifa ili kuimarisha uwajibikaji, uwazi na utawala bora katika eneo letu.

Wakili B.A.K. Mwabukusi.
Rais wa Chama cha Wanasheria
Tanganyika.

KUENDELEA KUMSHIKILIA HON TUNDU LISSU TAIFA LITAPASUKA VIPANDE VIPANDE._________________________________________________...
19/05/2025

KUENDELEA KUMSHIKILIA HON TUNDU LISSU TAIFA LITAPASUKA VIPANDE VIPANDE.

_________________________________________________________________________

Kutoka kwenye Mahak**a ya Hakimu Mkazi
Kisutu, jijini Dar es Salaam leo, Jumatatu Mei
19.2025 kesi ya uhaini inayomkabili
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Taifa Wakili Tundu
Lissu ililetwa kwa ajili ya kutajwa, ambapo
upande wa Jamhuri umeieleza Mahak**a
kuwa upelelezi wa shauri hilo bado
haujakamilika.

Jamhuri imesema shauri hilo
linaendelea na uchunguzi chini ya mamlaka
za Kipolisi, na kwamba kwakuwa upelelezi
haujakamilika hivyo wanaiomba Mahak**a
kuhairisha kesi husika kwa siku 14 zaidi,
jambo ambalo limeonekana kupingwa vikali
na Mawakili wa utetezi

Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na
Mawakili waandamizi Mpale Mpoki, Dkt.
Rugemeleza Nshala na Peter waliwasilisha
maombi kadhaa Mahak**ani hapo, ambapo
miongoni mwake wameiomba Mahak**a
"kulazimisha' upande wa Jamhuri ueleze nini
hasa kinachokwamisha upelelezi kwa sababu mwanzo ilidaiwa Mahak**ani hapo kuwa ushahidi wote kuhusiana na shauri hilo upo mtandaoni

Jambo la pili walilowasilisha Mawakili wa
utetezi Mahak**ani hapo ni kwamba,
hawafurahishwi namna ambavyo mteja wao
anavyokuwa amezungukwa na maafisa wa
Jeshi la Magereza (askari), ambapo
wameishawishi Mahak**a kutoa amri ya
kuwaondoa askari wote 'wanaomlinda' Lissu
ndani ya chumba cha Mahak**a, kwakuwa
kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania 1977 Mahak**a
haimtambui mtuhumiwa k**a 'mkosaji na
kwamba kitendo cha mteja wao kuzungukwa
na askari wengi haikubaliki

Ukijibu hoja hizo, upande wa Jamhuri
umeieleza Mahak**a kuwa licha ya kwamba Katiba imeeleza hivyo, lakini haijatoa maelekezo ya aina gani ya ulinzi inahitajika kwa mtuhumiwa pindi anapokuwa ndani ya chumba cha Mahak**a, hivyo kaiomba Mahak**a kutupilia mbali maombi hayo nakwamba ikiwezekana wanaomba ulinzi huouongezwe

Mawakili hao wa serikali wameenda mbali
zaidi kwa kueleza kuwa suala la ulinzi lina
faida kwa mtuhumiwa mwenyewe,
Mahak**a na maafisa wa Mahak**a kwa
ujumla wake

Kesi ya uhaini inayomkabili Kiongozi wa Upinzani Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Wakili Msomi Mwandamizi Tundu A. M. Lissu imeahirishwa hadi June 2, 2025 kwa kile Jamhuri inachodai kuwa upelelezi haujakamilika.

Msimamo ni uleule

✌️

 : Mahak**a ya Hakimu mkazi Kisutu imeahirisha hadi Juni 2, 2025 kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Dem...
19/05/2025

: Mahak**a ya Hakimu mkazi Kisutu imeahirisha hadi Juni 2, 2025 kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, baada ya upande wa mashtaka kusema kuwa uchunguzi wa shauri hilo bado haujakamilika na kuiomba mahak**a kupanga tarehe nyingine.

Shauri la kesi hiyo ya uchunguzi wa Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu imetajwa leo Mei 19 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Godfrey Mhini.

Lissu anakabiliwa na kesi mbili tofauti za jinai katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Dar es Salaam, Kisutu, moja akikabiliwa na shtaka moja la uhaini na nyingine akikabiliwa na mashtaka matatu ya kuchapisha taarifa za uwongo mitandaoni.

Bodi imechoka sana😂😂😂😂
18/05/2025

Bodi imechoka sana😂😂😂😂

India vs Turkiye | Land Power Comparison 2025
18/05/2025

India vs Turkiye | Land Power Comparison 2025

🛎️ Akiwa nchini Urusi, Rais Kapteni Ibrahim Traoré alimlaumu Barack Obama, rais wa zamani wa Marekani, kwa kuisambaratis...
15/05/2025

🛎️ Akiwa nchini Urusi, Rais Kapteni Ibrahim Traoré alimlaumu Barack Obama, rais wa zamani wa Marekani, kwa kuisambaratisha Libya. Alisema kuwa hali mbaya ya Libya kwa sasa imesababishwa na Barack Obama, na akamkosoa Jenerali Langley kwa kutumia dhahabu ya taifa ili kujinufaisha binafsi.

🤴🏽 Kapteni Ibrahim Traoré alisema kuwa hakukuwa na hata gramu moja ya dhahabu aliyoikuta kwenye hazina ya Burkina Faso aliposhika madaraka. Sasa ameanza kukusanya dhahabu upya huku Marekani ikianza kuonyesha nia ya kumuingilia.

🗣️ Alisema: "Wao hutumia mtu mweusi kumkandamiza mwingine mweusi." Aliomba Jenerali Langley aombe msamaha kwa kauli alizotoa.

Traoré alihitimisha kwa kusema kuwa Burkina Faso ni taifa huru, na kwamba kila kitu kilichopo ni cha watu wa taifa hilo, hivyo hawahitaji usimamizi kutoka mataifa ya nje.

⚠️ Pia aliongeza: "Waafrika weusi wanadharauliwa, wanachukuliwa kuwa duni kuliko hata wanyama. Wapo waliogeuzwa kuwa mashoga wa kulazimishwa enzi za ukoloni. K**a mambo hayo yalitokea wakati wa ukoloni, fikiria k**a Wanazi wangekuwa wameshinda Vita ya Pili ya Dunia?"

Alisema: "Katika kupambana na madhalimu hatutaleta ubaguzi wowote, kwa sababu tuna vifaa vya kutosha; kinachokosekana ni kuwafundisha wanajeshi wetu wapate ujuzi wa kutosha. Silaha tulizonazo tangu enzi ya Thomas Sankara bado zinafaa! Iwapo zitakwisha, tutanunua nyingine kutoka kwa Urusi ambayo ina vya kutosha. Hao wanaofanya mashambulizi si raia wa Burkina Faso, bali ni watu wanaotumwa na madhalimu."

Baada ya juzi askofu mkuu wa kanisa la anglican church Tanzania kutoa tamko kuwa kuhairishwa kwa uchaguzi kutaleta macha...
15/05/2025

Baada ya juzi askofu mkuu wa kanisa la anglican church Tanzania kutoa tamko kuwa kuhairishwa kwa uchaguzi kutaleta machafu nilifadhaika sana ukizingatia ndie askofu wetu mkuu....

Leo nimefarijika sana baada ya kusikiliza hotuba ya askofu wa anglican jimbo la daresalam kwenye mazishi ya mtangazaji charles hilary

Askofu amekemea vitendo viovu vya kuteka kupoteza hata kuua baàdhi ya watu kuwa ni chukizo akupindisha maneno wala kuita nyeusi kuwa nyeupe alisimamia iliyo haki....

Hongera sana baba askofu.... binafsi nimetamani wakati ukifika wa baraza la Maaskofu kuchagua askofu mkuu kanisa liombe apatikane mtumishi sahihi anaeweza kusimama katika HAKI kwa kusema nyeupe ni nyeupe na nyeusi ni nyeusi

Mashabiki wa timu ya Soka ya Mbeya City FC wameingia uwanjani wakiwa  na mabango yenye picha ya Kada wa chama Cha Demokr...
11/05/2025

Mashabiki wa timu ya Soka ya Mbeya City FC wameingia uwanjani wakiwa na mabango yenye picha ya Kada wa chama Cha Demokrasia Maendeleo (CHADEMA) Mpaluka Said maarufu k**a Mdude Nyagali, ambaye alipotea Mei 2, 2025 baada ya kuvamiwa, kujeruhiwa na kuchukuliwa na watu wasio julikana ambapo mpaka sasa bado haifahamiki Alipo.

Mashabiki wa Mbeya City wameingia na mabango hayo katika mchezo wa ligi ya Champion Ship baina yao na Green Worries mchezo uliomalizika kwa City Kuibuka na ushindi wa bao 5-0 mchezo uliopigwa katika Dimba la Sokoine.

Anaandika Baba Askofu Kalikawe Lwakalinda Bagonza PhD..MWONGOZO WA KUHAMA CHAMAKatika msimu wa Ligi yoyote, huwa kuna wa...
10/05/2025

Anaandika Baba Askofu Kalikawe Lwakalinda Bagonza PhD..

MWONGOZO WA KUHAMA CHAMA

Katika msimu wa Ligi yoyote, huwa kuna wachezaji kuhama club zao. Hata kwenye siasa, dini na hata ndoa, imeanza kuzoeleka watu kuhama au kuachana. Napendekeza Mwongozo wa kuhama:

1. Unapohama, tueleze uzuri wa unakokwenda, si ubaya wa unakotoka. Tayari tunajua utokako ni kubaya ndiyo maana umeondoka.

2. Tueleze uzuri na ubaya wako, si uzuri na ubaya wa watu unaoachana nao. Mapenzi yana upofu wa kudumu. Mwenye neno “MAPINDUZI” katika jina lake, anamshtaki mwenye harufu tu ya jina la “UHAINI”.

3. Jitahidi kukumbuka kuwa unayemwacha aliwahi kuwa mwema kwako (Baby) mpaka mkazaa watoto. Kwa ajili ya watoto, songa mbele kimya kimya.

4. Ukiweza hamia uendako kimya kimya, tutakuona ukiwa huko. Ukitaka kurudi, rudi kimya kimya. Usipoahidi kitu hudaiwi chochote. Maneno mengi yanamtisha mpenzi mpya.

5. KUMBUKA: Hakuna chuki ya kudumu wala mahaba ya kudumu. Mahaba ya kutongozea siyo ya kutunzia ndoa. Unakimbia kikwapa na kuangukia kwenye shombo.

Ameandika Msanii Roma Mkatoliki."Nilichojifunza kwenye haya maisha, usitengeneze watu individually, bali tengeneza taasi...
10/05/2025

Ameandika Msanii Roma Mkatoliki.
"Nilichojifunza kwenye haya maisha, usitengeneze watu individually, bali tengeneza taasisi imara!! Ukitengeneza taasisi imara, basi hata wakiondoka watu wote likabaki jiwe, still taasisi inaweza isife ikasimama na ikaendelea kuaminika na kuwa na wafuasi loyal!! CDM iliwahi kuwa na miamba haswa kwenye politics zetu, Miamba ile ikaondoka na kwenda vyama vingine….CDM Still ilisimama. Covid 19 walivyoondoka wengi waliamini CDM imefika mwisho, Lakini bado Wafuasi wengi waliendelea kuwa na imani na ngome hii ya upinzani!! Hapo katikati waliondoka wengine wengi tu na kuisema vibaya CDM lakini bado imesimama!! Na sasa wanaondoka G55 Naamini CDM bado watasimama!! Watu hawako CDM kuwafata viongozi, ndiomaana viongozi wanaondoka watu wanabaki!! CDM imejinasibu k**a ndiyo taasisi imara ya upinzani nchini!! Mungu awabariki kwakweli, hata k**a msiposhika dola. Lakini uwepo wenu unatuponya mno mno mno kwa maana mnahubiri injili inayompendeza Mungu aliye hai!!"

Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo

Haya sasa wafia timu,.😂😂😂😂Semeni niliweke wapi hili mike,ili mpate kumwaga povu!? ......😂😂😂😂
07/11/2024

Haya sasa wafia timu,.😂😂😂😂
Semeni niliweke wapi hili mike,ili mpate kumwaga povu!? ......😂😂😂😂

BATTERY LOW 🤣🤣🤣🤣
04/11/2024

BATTERY LOW 🤣🤣🤣🤣

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Petro Mlungu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Petro Mlungu:

Share