Charlii Media

Charlii Media Tunaandaa na kutengeneza Filamu, Matangazo na Graphics Designs. kwa mawasiliano zaidi, piga simu na

05/06/2026

SAFARICOM, KCB NA NMB ZAONGOZA MFUKO WA UWEKEZAJI WA SOKO LA HISA, AFRIKA MASHARIKI

Wawekezaji wa Afrika Mashariki wanaendelea kuweka dau kubwa kwenye sekta ya benki na mawasiliano, huku kampuni ya simu ya Kenya, Safaricom, ikiongoza orodha ya uwekezaji mkubwa zaidi katika mfuko wa hisa wa kikanda (ETF) kwa asilimia 18.8 ya mali zote za mfuko.

Kwenye takwimu hizo zilizotoka tarehe 29 Mei, inaonesha benki ya KCB ikifuatia, kwa asilimia 14.99 na NMB Bank kwa asilimia 10.69.

Takwimu hizo zinaonyesha wawekezaji wanaendelea kuvutiwa na kampuni zinazotengeneza faida thabiti, kulipa gawio na kuwa na nafasi kubwa katika uchumi wa Afrika Mashariki.

Safaricom imeendelea kuimarika baada ya kutangaza faida ya zaidi ya TShs trilioni 1.8 (KES bilioni 100) na gawio kubwa zaidi katika historia yake, hatua iliyoongeza imani ya wawekezaji katika hisa hiyo.

Kwa upande wa benki, KCB, NMB, CRDB na taasisi nyingine za kifedha zimebeba karibu nusu ya uwekezaji wote wa mfuko huo, ishara kuwa wawekezaji wanaamini ukuaji wa huduma za kifedha na mikopo katika ukanda huu bado una nafasi kubwa ya kimaendeleo.
Kenya inaongoza kwa asilimia 49.29 ya uwekezaji wote wa mfuko, huku Tanzania ikifuata kwa asilimia 35.58. Uganda ina asilimia 10.17 na Rwanda asilimia 4.96.

Sekta ya benki pekee imechukua asilimia 43.79 ya uwekezaji wote, ikifuatiwa na mawasiliano kwa asilimia 27.91.

04/06/2026

*MRADI WA MTO MKUJU-RUVUMA KUCHANGIA ASILIMIA 4 YA URANI DUNIANI*

✅️ Urani ya Tanzania Kulenga Nishati Safi, Siyo Silaha za Nyuklia

✅️ Mradi Kutoa Zaidi ya Ajira 1,000 za Moja kwa Moja

📍Namtumbo, Ruvuma-

Mradi wa Urani wa Mto Mkuju uliopo Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma unatarajiwa kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa madini ya urani duniani, huku ukikadiriwa kuchangia takribani asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani mara utakapofikia hatua ya uzalishaji.

Akizungumza kuhusu maendeleo ya mradi huo mapema wiki hii, Meneja wa Mradi wa Mto Mkuju, Beria Vorster, alisema maandalizi ya utekelezaji wa mradi yanaendelea kwa kasi na kwamba mradi huo una umuhimu mkubwa katika kukidhi mahitaji ya nishati safi duniani.

“Mradi wa Mto Mkuju ni miongoni mwa miradi mikubwa ya urani barani Afrika. Uzalishaji utakapoanza, unatarajiwa kuchangia takribani asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani, jambo ambalo litaiweka Tanzania katika nafasi muhimu kwenye soko la kimataifa la madini hayo,” alisema Vorster.

Kwa mujibu wa Shirika la World Nuclear Association (WNA), mwaka 2024 uzalishaji wa urani duniani uliongozwa na Kazakhstan kwa asilimia 39, ikifuatiwa na Canada kwa asilimia 24 na Namibia kwa asilimia 12. Uzbekistan ilichangia takribani asilimia 7, huku Urusi ikichangia kati ya asilimia 4 hadi 5 ya uzalishaji wa dunia. Hivyo, makadirio ya Mradi wa Mto Mkuju kuchangia asilimia 4 ya uzalishaji wa urani duniani yanaweza kuiweka Tanzania miongoni mwa nchi 10 zinazoongoza kwa uzalishaji wa urani duniani mara mradi huo utakapoanza uzalishaji wa kibiashara.

Alifafanua kuwa urani itakayozalishwa nchini Tanzania haitahusishwa kwa namna yoyote na utengenezaji wa silaha za nyuklia, bali itatumika kuzalisha nishati safi inayotumika katika vituo vya kuzalisha umeme wa nyuklia duniani.

Vorster alisema Tanzania ni mwanachama wa Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (Treaty on the Non-Proliferation of Nuclear Weapons - NPT), hali inayoweka misingi madhubuti ya kuhakikisha matumizi ya madini ya urani yanazingatia malengo ya amani na maendeleo endelevu.

“Urani kutoka Tanzania itatumika katika uzalishaji wa nishati s

04/06/2026

ITALIA YAONYESHA SILAHA MPYA YA KUPAMBANA NA DRONI HADHARANI

ROME — Italia imeonyesha kwa mara ya kwanza hadharani mfumo wake mpya wa ulinzi wa anga wa Skynex, mfumo wa silaha maalum ulioundwa kukabiliana na tishio linaloongezeka la droni katika vita vya kisasa.

Mfumo huo ulionyeshwa wakati wa gwaride la maadhimisho ya miaka 80 ya Jamhuri ya Italia lililofanyika Juni 2 mjini Rome.

Hatua hiyo imeifanya Italia kuwa nchi ya kwanza ndani ya muungano wa NATO kuingiza rasmi mfumo wa Skynex katika matumizi ya kawaida ya kijeshi. Taarifa za mtengenezaji wa mfumo huo, zinaonyesha Italia ilipokea betri yake ya kwanza ya majaribio mwishoni mwa mwaka 2025.

Tofauti na mifumo mingi ya ulinzi inayotegemea makombora ghali, Skynex hutumia kanuni ya milimita 35 inayoweza kufyatua hadi risasi 1,000 kwa dakika.

Mfumo huo umetengenezwa mahsusi kuangusha droni, ndege zisizo na rubani na silaha ndogo za kuruka kwa gharama ndogo zaidi kuliko kutumia makombora ya kawaida.

Katika migogoro ya hivi karibuni k**a vita vya Ukraine na Russia, droni za bei nafuu zimekuwa zikitumika kwa kiwango kikubwa kushambulia malengo ya kijeshi na miundombinu muhimu.

Changamoto kubwa kwa majeshi mengi imekuwa kutumia makombora yenye thamani ya mamia ya maelfu au hata mamilioni ya dola kuangusha droni ambazo ni za bei nafuu.

Mfumo huo hutumia risasi maalum zinazofunguka angani na kutengeneza wingu la vipande vidogo vya chuma vinavyoweza kuharibu droni kabla hazijafika kwenye eneo husika.

Mfumo huo pia una radar inayoweza kufuatilia malengo ya angani kwa umbali wa hadi kilomita 50 na kuunganisha taarifa zote kwa wakati mmoja kwa kituo cha udhibiti.

Wachambuzi wa masuala ya ulinzi wanasema kuonekana kwa Skynex kwenye gwaride la taifa si tukio la kawaida la maonesho ya kijeshi.

Ni ishara kwamba mataifa ya Ulaya yanaanza kuhamisha nguvu zaidi kwenye vita vya teknolojia, hasa ulinzi dhidi ya droni, ambazo zimebadili kabisa sura ya vita vya karne ya 21.

Kwa lugha rahisi: wakati zamani majeshi yalikuwa yanajiandaa zaidi kupambana na ndege za kivita, leo yanawekeza zaidi katika namna ya kusimamisha droni ndogo zinazoweza kusababisha uharibifu mkubwa kwa gharama ndogo sana.

04/06/2026

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA ZA WILAYA KUIMARISHA UCHUMI: MSIGWA

wa Barabara za Mji wa Serikali-Mtumba Wafikia 95%

Mwanza

Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini kwa kupunguza barabara za changarawe na kujenga barabara za lami katika wilaya mbalimbali, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kuinuka kiuchumi kupitia shughuli za usafirishaji.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alipokuwa akizungumza na Maofisa Uhusiano na Mawasiliano Serikalini wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) unaoendelea jijini Mwanza.

Msigwa amesema maofisa Mawasiliano wanapaswa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kwa kuwa miradi hiyo ni ya manufaa kwa wananchi wenyewe.

“Sisi ndiyo tunaobeba taswira ya Serikali. Tunapaswa kuwaonesha wananchi fursa zilizopo kutokana na uwekezaji mkubwa wa miundombinu unaofanywa na Serikali,” amesema.

Ameongeza kuwa Serikali imejenga barabara za mzunguko zenye urefu wa kilomita 56 katika Mji wa Serikali wa Mtumba jijini Dodoma ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 95 kukamilika.

Aidha, amesema Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara nyingine za mzunguko zinazounganisha Chamwino na maeneo mbalimbali jijini Dodoma kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari na kuboresha huduma za usafiri.

03/06/2026

*RAS MHINTE : AFCON 2027 IWE AJENDA YA KUDUMU KWENYE VIKAO VYENU VYA TAASISI NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA*

-Asisitiza utoaji wa huduma bora kwa wananchi

-Ataka changamoto zilizopo kutatuliwa mara Moja kwa maslahi mapana ya wananchi

-Aagiza uwasilishwaji wa taarifa mapema kwa sektetarieti ya Mkoa sambamba na upangaji wa tarehe ya vikao hivyo

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndg. Abdul R. Mhinte amezitaka Taasisi na Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Mkoa huo kuhakikisha Kila wanapokuwa na vikao katika maeneo yao ya kazi suala la AFCON 2027 lijadiliwe ili kupanga namna ya kulifanikisha suala hilo kisekta

RAS Mhinte ameyasema hayo katika kikao Cha Robo ya Tatu ya Mwaka 2025/2026 cha Sektetarieti ya Mkoa na Taasisi za Umma kilichofanyika tarehe 2 Juni, 2026 na kile Cha Sektetarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kilichofanyika tarehe 3 Juni, 2026 katika ukumbi wa Shamba Hall uliopo maeneo ya Shangwe Kibada katika Manispaa ya Kigamboni

Hata hivyo Katibu Tawala huyo amesisistiza utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwani ndio lengo hasa la kikao hicho na kupelekea kufanya Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Salama

Aidhaa, RAS Mhinte amezitaka changamoto zilizopo kutatuliwa mara Moja kwa maslahi mapana ya wananchi ambapo aliyataja mambo k**a ya migogoro ya Ardhi, uwepo wa Foleni, changamoto ya mfumo wa upatikanaji wa tiketi za SGR, uwepo wa makontena jangwani, uvamizi wa maeneo ya wazi ni mojawapo ya changamoto zinazopaswa kutatuliwa na kutoa majibu chanya kwa wananchi

Vile vile Katibu Tawala ameagiza uwasilishwaji wa taarifa kwa Sektetarieti ya Mkoa mapema ili sektetarieti iweze kuzipitia na kufanya masahihisho inapohitajika sambamba na kupangwa tarehe ya vikao hivyo mapema ili kuwawezesha Wajumbe kufahamu muda na eneo la kikao

Kwa upande wao Wakurugenzi wa Mamla za Serikali za Mitaa, Viongozi wa Taasisi mbalimbali katika Mkoa wa Dar es Salaam wamepongeza uwepo wa vikao hivyo kwani vinafanya Mawasiliano yao kuwa karibu na kurahisisha utendaji wao wa kazi unaopelekea kutoa huduma bora kwa wananchi

03/06/2026

*VIONGOZI OFISI YA MAKAMU WA RAIS WAIPONGEZA TFS KWA JUHUDI ZA UHIFADHI WA MAZINGIRA*

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Richard Muyungi, na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Mazingira, Balozi Baraka Luvanda, wameipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa mchango wake katika uhifadhi wa mazingira, usimamizi wa misitu na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Viongozi hao walitoa pongezi hizo leo baada ya kutembelea banda la TFS katika Maonesho ya Wiki ya Mazingira yanayoendelea kwenye Viwanja vya Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, ambapo walijionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na wakala huo katika usimamizi wa rasilimali za misitu, uzalishaji wa miche ya miti, utalii wa ikolojia pamoja na ufugaji nyuki.

Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Dkt. Muyungi alisema kazi inayofanywa na TFS ina mchango mkubwa katika kulinda mazingira na kuhakikisha rasilimali za misitu zinatumika kwa njia endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

“Tunatambua mchango mkubwa unaotolewa na TFS katika uhifadhi wa mazingira na usimamizi wa misitu yetu. Kazi hizi ni muhimu kwa ustawi wa mazingira, uchumi na maisha ya wananchi kwa ujumla. Tunawapongeza kwa juhudi zao na kwa kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira,” alisema.

Alibainisha kuwa hatua za uhifadhi wa misitu na uhamasishaji wa upandaji miti zina mchango muhimu katika kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kulinda vyanzo vya maji vinavyotegemewa na wananchi.

Katika ziara hiyo, viongozi hao walipata maelezo kuhusu majukumu ya TFS katika kulinda misitu ya taifa, kuimarisha bioanuwai, kuendeleza utalii wa ikolojia na kusimamia shughuli za ufugaji nyuki ambazo zimeendelea kuwa chanzo cha kipato kwa jamii zinazozunguka maeneo ya misitu.

Kwa upande wake, Balozi Luvanda alisema ameridhishwa na hatua zinazochukuliwa na TFS katika kuendeleza sekta ya ufugaji nyuki na kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na nyuki, akieleza kuwa shughuli hiyo ina manufaa makubwa kiuchumi na kimazingira.

Alisema ufugaji nyuki ni miongoni mwa shughuli zinazochangia uhifadhi wa misitu kwa kuwa unahitaji mazingira salama na ende

03/06/2026

SERENGETI BOYS WAIWEKA TANZANIA KWENYE RAMANI YA AFRIKA

Na Mwandishi wetu

Serengeti Boys wamekosa kombe la Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 baada ya kufungwa kwa penalti 4-2 na Senegal kwenye fainali ya AFCON U17 iliyochezwa Rabat, Morocco.

Kiungo Issa Chole alitangazwa Mchezaji Bora wa Mashindano, huku Dismas Athanasi Elieneza akitwaa tuzo ya Mfungaji Bora.

Madogo wameiheshimisha vyema nchi kwa kushinda tuzo ya Fair Play kutokana na nidhamu nzuri waliyoinyesha uwanjani.

Mafanikio hayo yanaifanya Tanzania kuondoka na tuzo tatu kubwa za mashindano, jambo linaloonyesha ukuaji wa soka la vijana nchini.

Kufika fainali pia kumewapa Serengeti Boys tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia la FIFA U17 litakalofanyika Qatar mwaka huuhuu wa 2026.

Ingawa kombe limekwenda Senegal, Tanzania imeondoka na uthibitisho kwamba kizazi kipya cha soka kinaweza kushindana na timu bora kabisa Afrika.

03/06/2026

SERENGETI BOYS WAIWEKA TANZANIA KWENYE RAMANI YA AFRIKA

Na Mwandishi wetu

Serengeti Boys wamekosa kombe la Afrika kwa vijana chini ya miaka 17 baada ya kufungwa kwa penalti 4-2 na Senegal kwenye fainali ya AFCON U17 iliyochezwa Rabat, Morocco.

Tanzania ilianza mchezo kwa kasi na kupata bao la mapema dakika ya saba kupitia Hamis Chenga, kabla ya Senegal kusawazisha dakika ya 64 kupitia Ibrahima Dione.

Baada ya sare ya 1-1 ndani ya dakika 90, mchezo uliamuliwa kwa mikwaju ya penalti ambapo Senegal walikuwa makini zaidi na kutwaa ubingwa wao wa pili wa mashindano hayo.

Licha ya kukosa kombe, Serengeti Boys wameondoka Morocco wakiwa moja ya timu zilizong'ara zaidi kwenye michuano hiyo.

Kiungo Issa Chole alitangazwa Mchezaji Bora wa Mashindano, huku Dismas Athanasi Elieneza akitwaa tuzo ya Mfungaji Bora.

Madogo wameiheshimisha vyema nchi kwa kushinda tuzo ya Fair Play kutokana na nidhamu nzuri waliyoinyesha uwanjani.

Mafanikio hayo yanaifanya Tanzania kuondoka na tuzo tatu kubwa za mashindano, jambo linaloonyesha ukuaji wa soka la vijana nchini.

Kufika fainali pia kumewapa Serengeti Boys tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia la FIFA U17 litakalofanyika Qatar mwaka huuhuu wa 2026.

Ingawa kombe limekwenda Senegal, Tanzania imeondoka na uthibitisho kwamba kizazi kipya cha soka kinaweza kushindana na timu bora kabisa Afrika.

29/05/2026

CANADA YASHUSHA LEOPARD TANKS LATVIA, NATO YAONGEZA PRESHA ULAYA MASHARIKI

Canada na washirika wake wa NATO wameendelea kufanya mazoezi makubwa ya kijeshi nchini Latvia huku mizinga ya kisasa aina ya Leopard 2 ikionekana kwenye operesheni mbalimbali za kivita.

Mazoezi hayo yamefanyika katika kambi ya kijeshi ya Ādaži karibu na upande wa mashariki wa NATO.

Vikosi kutoka Canada, Ufaransa, Poland, Sweden na mataifa mengine ya NATO vilishiriki.

Wanajeshi wa infantry walifanya mazoezi ya kusonga vitani huku wakilindwa na Leopard 2 tanks zinazotajwa kuwa miongoni mwa mizinga yenye nguvu zaidi duniani.

Kulikuwa pia na mazoezi halisi ya silaha za moto, mpangilio halisi wa kupambana vitani, na mazoezi ya mapigano ya mazingira halisi ya vita kwa msaada wa akili unde.

NATO imesema mazoezi hayo yanalenga kuongeza utayari wa kombat na kuhakikisha vikosi vya washirika vinaweza kufanya operesheni za pamoja kwa haraka wakati wa dharura.

Canada imeendelea kuwa moja ya nchi zinazoongoza vikosi vya NATO nchini Latvia kupitia operesheni ya “Operation REASSURANCE”.

Mwaka 2023, Canada ilitangaza rasmi kupeleka Leopard 2 tanks Latvia k**a sehemu ya kuongeza ulinzi wa NATO karibu na Russia.

Mazoezi hayo yanakuja huku mvutano wa kiusalama Ulaya Mashariki ukiendelea tangu kuanza kwa vita vya Ukraine.

Kwa sasa Latvia imekuwa moja ya maeneo muhimu zaidi ya NATO barani Ulaya kutokana na ukaribu wake na Russia na Belarus.

28/05/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili Chato Mkoani Geita, ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Magufuli ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yatakayofanyika tarehe 29 Mei 2026 Wilayani Chato.

Makamu wa Rais amepokelewa katika Uwanja wa Ndege Geita, Wilayani Chato, Mapokezi yaliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martin Shigela, Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na Viongozi mbalimbali Waandamizi.

Pia Makamu wa Rais, amefika nyumbani kwa marehemu, Kilimani Chato kusaini kitabu cha maombolezo pamoja na kuwafariji wafiwa kufuatia msiba huo.

Address

Mji Mwema, Kigamboni
Dar Es Salaam
15114

Telephone

+255782171802

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Charlii Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Charlii Media:

Share