28/11/2025
Mfumo wa kidijitali wa Tanzania Chamber Portal (TCP) umeendelea kuboresha biashara nchini, ukifanya iwe rahisi, haraka na wazi kwa wafanyabiashara.
Akizungumza jijini Mwanza ambako mafunzo ya mfumo huo yanaendelea kwa siku ya tatu mfululizo, Afisa TEHAMA wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Nelson Urio amesema mfumo huo unarahisisha huduma muhimu k**a usajili wa wanachama na kuripoti malalamiko kwa njia salama na haraka.
Ameongeza kuwa kuunganishwa kwa TCP na mifumo ya Serikali k**a TANeSW – Single Window kumepunguza muda wa kupata huduma na kuongeza uwazi, jambo linalosaidia mauzo ya nje na usafirishaji wa bidhaa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema TCP imefungua fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa mikoani kupata huduma kwa wakati, bila usumbufu.
Kwa ujumla, TCP inasaidia kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya kimataifa, kukuza mauzo ya nje, na kuimarisha biashara kidijitali nchini.