TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wamechangia fedha na kununua mashine ya kisasa ya kurud...
07/09/2026

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wamechangia fedha na kununua mashine ya kisasa ya kurudufu nyaraka (photocopy machine) kwa Shule ya Sekondari ya Sinde, Mbeya, ili kusaidia utayarishaji wa mitihani na kuondoa changamoto ya wanafunzi kufuata huduma hiyo nje ya shule.

Akikabidhi mashine hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Dkt. Godlove Mbwanji, amesema wameamua kuunga mkono sekta ya elimu kwa kuwa shule ndiko kunakotengenezwa wataalamu wa baadaye, wakiwemo madaktari na wauguzi. Mkuu wa Shule, Anatalia Valence Luwungo, ameshukuru msaada huo akisema utawanufaisha wanafunzi 1,196 na kuongeza ufanisi wa taaluma.

Wanafunzi Noel Sanga na Vanesa Kyando wamewashukuru watumishi hao, wakisema mashine hiyo itawachochea kuongeza bidii katika masomo na kuboresha ufaulu.

Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ametuma salamu za pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan, familia yake na Watanzania kufuatia ki...
07/09/2026

Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ametuma salamu za pole kwa Rais Samia Suluhu Hassan, familia yake na Watanzania kufuatia kifo cha mwenza wa Rais Samia, Hafidh Ameir Hassan.

Katika ujumbe wake, Kagame amesema Serikali na wananchi wa Rwanda wako pamoja na Rais Samia na Watanzania katika kipindi hiki cha maombolezo, huku wakiheshimu maisha na urithi wa Hafidh Ameir Hassan aliyefariki leo Septemba 7, 2026 na kuzikwa leo.

07/09/2026

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Riziki Pembe Juma, amesema kifo cha Hafidh Ameir Hassan, mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kimeacha pengo kubwa kwani alikuwa mlezi na mshauri katika sekta hiyo.

Akizungumza kufuatia msiba huo, Riziki amesema Hafidh alikuwa akitoa ushauri mara kwa mara katika sekta anayoisimamia, hivyo kuondoka kwake ni pigo kwao.

“Alikuwa mlezi kwa kweli na tumeondokewa. Allah amsamehe, Inshaallah, na sisi tuliobaki tuendelee kufuata nyayo zake,” amesema Riziki.

Hafidh Ameir Hassan amefariki dunia leo Septemba 7, 2026 na kuzikwa Kizimkazi, Zanzibar.

07/09/2026

Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo imesema Serikali inaendelea kufanya maboresho katika Stendi Kuu ya Mabasi ya Magufuli, ikiwemo kuboresha maeneo ya abiria kusubiria na kuweka mabango ya kuwaelekeza abiria mabasi wanayotakiwa kutumia kulingana na mikoa wanayokwenda.

Akizungumza wakati wa ziara maalumu ya kukagua stendi hiyo, Mstahiki Meya wa Ubungo, Laurence Mlaki, amesema wananchi wanapaswa kupuuza taarifa zinazotolewa na baadhi ya watu kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kupotosha umma kuhusu huduma zinazotolewa katika stendi hiyo.

Mlaki amesema maboresho yamefanyika katika maeneo mbalimbali, ikiwemo huduma za vyoo, ambapo stendi hiyo sasa ina zaidi ya matundu 140.

Amesema tangu kurejeshwa kwa huduma za mabasi kwenye stendi hiyo, mapato yameendelea kuimarika kutokana na kuongezeka kwa idadi ya mabasi yanayofanya safari kupitia stendi hiyo kila siku.

Kwa upande wake, Meneja wa Stendi hiyo, Isaac Kasebo, amewataka abiria kufuata taratibu na maelekezo ya watoa huduma, ikiwemo kukata tiketi mtandaoni au kufika katika ofisi husika ili kujiepusha na hatari ya kuibiwa.

Kasebo amesema operesheni ya kuwaondoa wapiga debe wasiotambulika kisheria inaendelea, huku hatua za kisheria zikichukuliwa dhidi yao.

FULL TIME⏰ | Alama tatu muhimu zimebaki kwa Azam FC , Namungo wakiondoka patupu.FT’ Azam FC 2️⃣🆚0️⃣ Namungo FC⚽️Mubiru⚽️...
07/09/2026

FULL TIME⏰ |

Alama tatu muhimu zimebaki kwa Azam FC , Namungo wakiondoka patupu.

FT’ Azam FC 2️⃣🆚0️⃣ Namungo FC

⚽️Mubiru
⚽️Sillah

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapi...
07/09/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali, vyama vya siasa na wananchi, wamefika nyumbani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kumpa pole kufuatia kifo cha mumewe, Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Maalim Hafidh Ameir Hassan amefariki dunia leo Septemba 7, 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mzena, Zanzibar, alipokuwa akipatiwa matibabu.

Viongozi hao wameungana na ndugu, jamaa na wananchi mbalimbali katika kipindi hiki cha maombolezo, wakimfariji Rais Samia na familia yake kufuatia msiba huo.

07/09/2026

Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imeongeza siku 14 za kuendelea kusikiliza kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, baada ya upande wa utetezi kushindwa kukamilisha uwasilishaji wa ushahidi wake.

Jaji Dunstan Ndunguru ametangaza kuongezwa kwa siku hizo huku shahidi wa nne wa utetezi, ambaye ni Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia, akitakiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kesho, Septemba 8, 2026.

Katika hatua hiyo, Jaji Ndunguru amezitaka pande zote mbili, Jamhuri na utetezi, kutumia vizuri siku hizo 14 ili kuhakikisha kesi hiyo haichukui muda mrefu zaidi, huku akizitaka kuepuka mambo yanayoweza kuongeza muda wa shauri.

Kwa upande wake, mshtakiwa Tundu Lissu amesema yeye pamoja na mashahidi wake watajitahidi kukamilisha ushahidi ndani ya muda uliotolewa, akisema muda huo pia utategemea muda ambao upande wa mashtaka utatumia katika kuwauliza mashahidi maswali ya dodoso (cross examination).

Upande wa Jamhuri umesema umepokea maelekezo ya Jaji na umeahidi kuyazingatia, hususan kujikita katika masuala yanayohusiana moja kwa moja na shauri hilo.

07/09/2026

Zaidi ya shilingi milioni 200 zinatarajiwa kukusanywa kupitia TPDC Marathon 2026 kwa ajili ya kugharamia matibabu ya watoto 100 wenye maradhi ya moyo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPDC, Derick Mosha, amesema marathon hiyo ni zaidi ya zoezi la maudhui, kwani inalenga kuchangia matibabu na kuwapa tabasamu watoto wanaosumbuliwa na maradhi ya moyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, amesema mahitaji ya huduma hiyo ni makubwa, akieleza kuwa takribani watoto 4,000 nchini wanahitaji matibabu ya moyo. Amesema kupitia marathon hiyo, pamoja na kusaidia matibabu, washiriki watapata fursa ya kufanya mazoezi na kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.

TPDC Marathon 2026 inatarajiwa kufanyika Novemba 21, 2026, ikihusisha mbio za kilomita 5, 10 na 21, huku ikibeba ujumbe wa “Hatua yako inaokoa maisha.”

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi; Waziri Mk...
07/09/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Deogratius Ndejembi, Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi; Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba na viongozi wengine mbalimbali wameshiriki maziko ya Hafidh Ameir Hassan, mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mazishi hayo yamefanyika Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, leo Septemba 7, 2026 ambapo pia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari pia wameshiriki.

Viongozi wastaafu waliohudhuria maziko hayo ni pamoja na Rais mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, na Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Aidha, maziko hayo pia yamehudhuriwa na viongozi wa Serikali, dini, vyama vya siasa, mahakama, bunge, vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na ndugu, jamaa, marafiki na waombolezaji kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Hafidh Ameir Hassan amefariki dunia leo Septemba 7, 2026 katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Zanzibar, alipokuwa akipatiwa matibabu.

HALFTIME ⏰ |NBCPLNi mapumziko Azam FC wakiwa mbele kwa bao moja huku Wauaji wa Kusini wakienda vyumbani vichwa chini HT’...
07/09/2026

HALFTIME ⏰ |NBCPL

Ni mapumziko Azam FC wakiwa mbele kwa bao moja huku Wauaji wa Kusini wakienda vyumbani vichwa chini

HT’ Azam FC 1️⃣🆚0️⃣ Namungo FC

⚽️Mubiru

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Shortcuts

Share