TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa mira...
06/06/2026

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeeleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam, ikisisitiza kuwa miradi hiyo inaonesha matumizi mazuri ya mapato ya ndani katika kuhudumia wananchi.

Kamati hiyo, ikiongozwa na Mwenyekiti wake Florent Kyombo, imekagua miradi minne ikiwemo ujenzi wa Shule ya Msingi Kibasila yenye thamani ya shilingi bilioni 4.4 na Shule ya Sekondari Kibondemaji inayojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 7.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Kyombo amesema Kamati imevutiwa na matumizi ya majengo ya ghorofa ambayo yamesaidia kuongeza nafasi ya madarasa katika maeneo yenye uhaba wa ardhi mijini, hasa Jiji la Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Tumaini Nagu amesema maelekezo na ushauri wa Kamati umepokelewa na utekelezaji wake utaimarishwa ili kuhakikisha miradi inawanufaisha wananchi zaidi.

Tanzania imeialika Belarus kushiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane 2026 kwa kuleta bidhaa na teknolojia za k...
06/06/2026

Tanzania imeialika Belarus kushiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane 2026 kwa kuleta bidhaa na teknolojia za kisasa za kilimo, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kiteknolojia kati ya nchi hizo.

Mwaliko huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli, wakati wa mazungumzo na Waziri wa Kilimo wa Belarus, Yury Gorlov, yaliyofanyika Juni 6, 2026 kufuatia utekelezaji wa Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) iliyosainiwa Julai 2025.

Viongozi hao pia wamejadili fursa za biashara ya mazao ya kilimo, ambapo Tanzania imeeleza utayari wa kuuza mazao mbalimbali yakiwemo kahawa, korosho, chai, parachichi na viungo katika soko la Belarus.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, ameiagiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (...
06/06/2026

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir, ameiagiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kukitambua rasmi Kituo Maalumu cha Mafunzo (Center of Excellence) cha Kampuni ya Superdoll, hatua itakayosaidia kukuza ujuzi na kuongeza uzoefu wa kazi kwa vijana wa Tanzania.

Naibu Waziri amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na taasisi za elimu katika kuwaandaa vijana kwa soko la ajira kupitia mafunzo yanayozingatia mahitaji halisi ya sasa.

Ametoa rai hiyo Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake katika Kiwanda cha Superdoll, ambapo amehimiza utoaji wa elimu inayojikita katika ujuzi na umahiri ili kuwajengea wahitimu uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi na kuendana na mahitaji ya sekta za uzalishaji.

Ameeleza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa vyuo 65 vya VETA na kuboresha vingine 12, hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa mafunzo ya ufundi stadi na kuwawezesha vijana kupata ujuzi unaohitajika katika uchumi unaobadilika.

Aidha, amezihimiza taasisi na wadau wengine kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kufungua milango ya mafunzo ya vitendo kwa vijana na wakufunzi ili kupunguza pengo kati ya maarifa ya darasani na ujuzi unaohitajika sokoni.

Vilevile, ameitaka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kuharakisha utiaji saini wa makubaliano na Kampuni ya Superdoll ili kuimarisha zaidi mafunzo ya vitendo kwa vijana.

Kwa upande wake, Meneja wa Superdoll, Ibrahim Ali, amesema kampuni hiyo imekuwa ikishirikiana kwa karibu na taasisi za elimu hususan VETA, ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa mafundi wake, huku takribani asilimia 80 ya mafundi wake wakiwa wahitimu wa VETA. Amesema pia kampuni hiyo imepokea vijana 20 kwa ajili ya tawi lake la Dodoma.

06/06/2026

Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Jawadu Mohamed, amesema chama hicho kimejipanga kuhakikisha wananchi wote wa Mkoa wa Dodoma wanapata huduma ya maji safi na salama ifikapo mwaka 2030, sambamba na utekelezaji wa Ilani ya CCM inayolenga kufikisha huduma hiyo kwa asilimia 100.

Jawadu amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maji mkoani Dodoma, ambapo ameeleza kuwa Serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan inaendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya maji ili kumaliza kabisa changamoto ya mgao, ukatikaji wa huduma na upatikanaji hafifu wa maji katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Amesisitiza Dodoma k**a Makao Makuu ya nchi haiwezi kuendelea kukabiliwa na changamoto za maji, akieleza kuwa juhudi zinazoendelea kupitia miradi ya visima vikubwa na miundombinu mingine ya maji zinalenga kufanya tatizo hilo kuwa historia, hivyo CCM inaamini kuwa maendeleo ya makao makuu ya nchi lazima yaendane na upatikanaji wa huduma bora za msingi ikiwemo maji.

Kwa mujibu wa Jawadu, CCM imeahidi kufikisha huduma ya maji safi na salama katika vijiji 702 ndani ya kipindi cha miaka mitano, huku akibainisha kuwa hadi sasa vijiji 448 tayari vimefikiwa na huduma hiyo.

Amesema visima vikubwa vinavyoendelea kujengwa vitakuwa suluhisho la kudumu kwa maeneo mengi ya Mkoa wa Dodoma na kuongeza upatikanaji wa maji kwa wananchi.

Aidha, amewataka wananchi kuendelea kuiunga mkono Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akisema CCM imejikita katika siasa za maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Amesema chama hicho kimeazimia kuhakikisha ahadi zote zilizomo kwenye Ilani yake zinatimizwa na kwamba ifikapo mwaka 2030 hakuna mwananchi wa Dodoma atakayebaki na malalamiko kuhusu huduma ya maji safi na salama.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amesema atawasilisha katika mene...
06/06/2026

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amesema atawasilisha katika menejimenti ya wizara yake wazo la kuanzishwa utaratibu wa kukusanya na kuhifadhi machapisho ya wanawake ili kuhamasisha wanawake wengi zaidi kuandika vitabu.

Dkt. Gwajima amesema anatamani kitabu cha Tawasifu cha Queen Mlozi kisajiliwe kuwa chapisho la kwanza katika mpango huo wakati wa uongozi wake ili kiwe chachu ya kuibuka kwa machapisho mengine mengi kutoka kwa wanawake wenye uzoefu katika nyanja mbalimbali za maisha na uongozi.

Akizungumza leo Juni 6, 2026 jijini Dodoma katika hafla ya uzinduzi wa Tawasifu ya Queen Mlozi, aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Mjumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Dkt. Gwajima amesema ni muhimu wanawake kuacha alama kupitia maandishi yanayoweza kutumiwa k**a rejea kwa wengine.

Amesema machapisho hayo yatawasaidia wanawake wenye ndoto za kuwa viongozi kupata fursa ya kujifunza moja kwa moja kutoka kwa waliowatangulia badala ya kutegemea simulizi pekee.

Kwa mujibu wa Waziri Gwajima, vitabu hivyo vitakuwa hazina ya maarifa na uzoefu kuhusu changamoto, fursa na safari ya kufikia nafasi za uongozi.

📸✍🏽

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima, amezindua kitabu cha Tawasifu k...
06/06/2026

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima, amezindua kitabu cha Tawasifu kiitwacho Nimeweza kilichoandikwa na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na Mjumbe wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC), Queen Mlozi.

Uzinduzi huo umefanyika leo Juni 6, 2026 jijini Dodoma ambapo Dkt. Gwajima alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali, marafiki na wadau wa maendeleo ya wanawake.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Gwajima amesema kitabu hicho ni nyenzo muhimu ya kujifunza kutokana na uzoefu wa mwandishi wake, huku kikitoa hamasa kwa wanawake na wasichana kujitambua, kujiamini na kufikia malengo yao ya maisha.

Tawasifu ya Nimeweza imelenga kuzungumza na wanawake wa rika zote kwa kubeba simulizi, ushuhuda na uzoefu wa maisha ya mwandishi wake, ambaye ameamua kutumia safari yake ya maisha k**a chachu ya kuhamasisha wengine kukabiliana na changamoto na kufikia mafanikio.

Kitabu hicho kinamwelezea Queen Mlozi k**a mwanamke aliyedhamiria kuwa kioo cha jamii kwa kushiriki uzoefu wake katika nyanja mbalimbali za maisha, uongozi na maendeleo ya wanawake.

📸✍🏽

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amesema ujasiri na umahiri wa ka...
06/06/2026

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima amesema ujasiri na umahiri wa kazi wa Queen Mlozi ulimfanya yeye pamoja na wengine kutamani kupewa nafasi za uongozi serikalini.

Dkt. Gwajima amesema alimfahamu Queen Mlozi walipokuwa wakifanya kazi pamoja mkoani Singida, ambapo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida na alikuwa akijitokeza kwa ujasiri kutoa hoja na kutetea masuala mbalimbali kwenye vikao vya viongozi.

Amesema namna Queen Mlozi alivyokuwa akizungumza na kushughulikia majukumu yake iliwapa hamasa wengine kuamini kuwa wanaweza pia kupewa nafasi za uongozi na kutumikia wananchi.

“Lililonivutia mimi hadi nikasema nije, Mwalimu Queen Mwashinga Mlozi ni dada yangu nimetoka nae kwenye utumishi Singida, alikuwa DC wa Wilaya ya Singida, enzi hizo alikuwa akikaa kwenye vikao akizungumza unasema mashalaaah mbona mimi siteuliwi?, unapata ule moyo wa kwenda mbele…,”

“Tulikuwa tukikaa pale enzi hizo Mkuu wa Mkoa akiwa Paseko Kone eehhee alikuwa anachapa kazi, sasa hoja zikimwagwa hapo mnaanza kutazamana nani ataongea, sasa nilikuwa namuona huyu mama ni jasiri anaongea na sisi tunabebwa tunatetewa humo humo,” amesema Dkt. Gwajima.

Ameeleza hayo leo Juni 6, 2026 jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Taasisi ya Queen Mlozi, ambapo alikuwa mgeni rasmi.

📸✍🏽

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe amewataka walimu nchini kuongeza ubunifu na kutu...
06/06/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe amewataka walimu nchini kuongeza ubunifu na kutumia mbinu za kisasa katika ufundishaji ili kuimarisha ubora wa elimu na kuwawezesha wanafunzi kukabiliana na changamoto za dunia ya sasa.

Profesa Shemdoe ametoa wito huo Juni 6, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo kwa washindi wa Shindano la Taifa la Stadi za Ufundishaji kwa walimu wa elimu ya awali, msingi na sekondari.

Amesema Serikali itaendelea kuthamini mchango wa walimu kwa kuboresha mazingira ya kazi na kutoa motisha mbalimbali ili kuwawezesha kufundisha na kujifunza kwa ufanisi zaidi.

Katika hatua nyingine, ameelekeza walimu 35 walioibuka washindi wa shindano hilo kupatiwa viwanja karibu na maeneo yao ya kazi k**a sehemu ya kutambua na kuthamini juhudi zao katika sekta ya elimu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET), Dkt. Aneth Komba amesema shindano la mwaka 2026 limehusisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara na linalenga kuimarisha umahiri wa walimu katika ufundishaji wa stadi mbalimbali.

Dkt. Komba ameeleza kuwa walimu 3,153 walijisajili kushiriki, 1,263 wakapakia video za ufundishaji kwa ajili ya tathmini, huku 232 zikifika katika hatua ya mwisho ya kitaifa.

06/06/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeanza kutumia teknolojia ya akili unde (AI) katika kufuatilia hali za wagonjwa kwa wakati halisi, hatua inayotajwa kuongeza usalama wa wagonjwa na kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini.

Akizungumza kuhusu matumizi ya mfumo huo wa kisasa, Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Redemptha Matindi, amesema teknolojia hiyo imeleta mapinduzi katika ufuatiliaji wa wagonjwa kwa kuwawezesha wauguzi kupata taarifa muhimu za afya bila kulazimika kufika kitandani kila wakati.

Amesema kupitia monita maalumu zilizounganishwa na mfumo wa AI, wahudumu wa afya wanaweza kufuatilia mapigo ya moyo, shinikizo la damu, kiwango cha oksijeni mwilini pamoja na joto la mwili wa mgonjwa kwa wakati halisi.

Matindi ameongeza kuwa matumizi ya teknolojia hiyo yanasaidia kubaini mabadiliko ya hali ya mgonjwa mapema, hivyo kuongeza kasi ya utoaji wa huduma na kupunguza hatari zinazoweza kujitokeza wakati wa matibabu.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dorothy Gwajima amesema changamoto nyingi anazokutana...
06/06/2026

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dorothy Gwajima amesema changamoto nyingi anazokutana nazo katika utekelezaji wa majukumu ya wizara yake zinatokana na kudhoofika kwa taasisi ya familia, hali ambayo imeendelea kujitokeza katika jamii ya sasa.

Dkt. Gwajima amesema msingi wa changamoto hizo huanza tangu hatua za awali za ujenzi wa familia, ikiwemo uchaguzi wa mwenza, maandalizi ya maisha ya pamoja, uwekaji wa misingi ya uendeshaji wa familia, umiliki na matumizi ya mali pamoja na makubaliano kuhusu uzazi na malezi ya watoto.

Amesisitiza kuwa maeneo hayo yakipuuzwa huathiri uimara wa familia na ustawi wa jamii kwa ujumla.

Akizungumza leo Juni 6, 2026 jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Taasisi ya Queen Mlozi, ambapo alikuwa mgeni rasmi, Dkt. Gwajima amesema jamii inapaswa kurejea katika misingi bora ya familia ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii zinazoendelea kujitokeza.

Ameeleza kuwa kitabu hicho kinatoa mafunzo muhimu kuhusu ujenzi wa familia imara, na kuwahimiza, wazazi hususan wanawake wenye majukumu ya uongozi, kusoma kazi hiyo ili kupata maarifa yatakayowasaidia kusawazisha wajibu wa kazi na familia. Amebainiaha kuwa uzoefu uliobebwa na mwandishi unaweza kuwa mwongozo kwa wengi katika kujenga familia zenye misingi thabiti.

Aidha, Dkt. Gwajima amesema mwandishi wa kitabu hicho, Queen Mlozi, amegusia masuala mbalimbali yanayotoa funzo kuwa ustawi wa jamii unaweza kupatikana endapo wananchi watazingatia misingi bora ya maisha, malezi na mahusiano, mambo yaliyoainishwa vizuri katika kitabu hicho.

📸✍🏽

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Share