TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

Yaliyomo katika kurasa za mbele za magazeti leo Januari 17, 2026.
17/01/2026

Yaliyomo katika kurasa za mbele za magazeti leo Januari 17, 2026.

16/01/2026

Katika Hadubini Jumamosi hii utasikia visababishi vya ajali za barabarani hususani katika Barabara kuu ya kuingia Tanga. Ni kuanzia saa 12 jioni, kesho Jumamosi Januari 17, 2026 hapa TBC1, penye Ukweli na Uhakika.

16/01/2026

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, amewaonya baadhi ya wakuu wa shule wanaowarudisha wanafunzi nyumbani kwa kigezo cha kutokamilisha mahitaji k**a rimu na sare. Ameagiza wanafunzi wote wapokelewe bila masharti na kuendelea na masomo huku wazazi na walezi wakiendelea kukamilisha mahitaji hayo.

Sendiga ametoa onyo hilo leo Januari 16, wakati akitoa taarifa ya mwitikio wa wanafunzi wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza kuripoti shule. Amesema mkoa ulipanga kusajili wanafunzi 28,908 waliofaulu darasa la saba na kupangiwa shule za sekondari, lakini hadi sasa ni asilimia 25 pekee ya wanafunzi wa kidato cha kwanza walioripoti.

Kwa upande wa darasa la kwanza, amesema mkoa ulitarajia kusajili wanafunzi 65,970, lakini walioandikishwa hadi sasa ni 41,980 sawa na asilimia 69.

Kutokana na hali hiyo, Sendiga amesisitiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto shule hata k**a hawajakamilisha sare au kununua rimu, huku akiwaonya wakuu wa shule wanaokataa kuwapokea wanafunzi kwa vigezo hivyo.

Aidha, ameagiza wakuu wa wilaya kushirikiana na maafisa elimu pamoja na viongozi wa vijiji na mitaa kuhakikisha kila mwanafunzi aliyefaulu na kupangiwa shule anaripoti, na kubaini wenye changamoto ili mkoa uweze kuwasaidia.

16/01/2026

Wafanyakazi wa kiwanda cha kuzalisha bidhaa za ujenzi cha Rodhia kilichopo jijini Arusha wamegoma wakidai utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya kupewa nyongeza ya mshahara kuanzia mwezi Januari.

Baadhi ya wafanyakazi hao wamesema wamekuwa wakiuliza uongozi wa kiwanda kuhusu utekelezaji wa nyongeza hiyo, lakini hawajapata mrejesho wa kuridhisha. Wamedai pia kuwepo kwa changamoto nyingine zinazohusu maslahi na mazingira ya kazi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, kwa kushirikiana na viongozi wengine, ameomba pande zote kuvumilia huku akieleza kuwa majibu ya kina kuhusu madai hayo yatatolewa kesho Januari 17, kwa kuhusisha wadau wote muhimu.

Mamlaka zimeeleza kuwa juhudi zinaendelea ili mgogoro huo utatuliwe kwa njia ya mazungumzo na kurejesha utulivu pamoja na mwendelezo wa shughuli za uzalishaji.

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Dodoma Jiji dhidi ya Singida Black Stars umemalizika kwa sare ya 1-1 Dodoma Jiji, wenyeji wa m...
16/01/2026

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Dodoma Jiji dhidi ya Singida Black Stars umemalizika kwa sare ya 1-1

Dodoma Jiji, wenyeji wa mchezo huo walianza kupata bao dakika ya 83’ kupitia kwa Yasin Mgaza kwa mkwaju wa penalti na baadae dakika za jioooooniiiii Singida BS wakapata goli la kusawazisha kupitia kwa Marouf Tshakei kwa mkwaju wa penalti pia.

FT: Dodoma Jiji 1️⃣🆚1️⃣Singida Black Stars

⚽️ Yassin Mgaza 83’ (Pen)
⚽️Marouf Tshakei 90+4’ (Pen)

16/01/2026

Utoaji wa Huduma za Msaada wa Kisheria bado unaendelea kugusa maisha ya Watanzania wengi wenye kipato cha chini na wasio na uwezo wa kumudu gharama za mawakili.

Wizara ya Katiba na Sheria kupitia kliniki ya Msaada wa Kisheria imemfikia Mzee Jumanne Ngaiza anayeishi katika mtaa wa Unyankahe kata ya Mandewa Manispaa ya Singida.

Ngaiza aliwasilisha mgogoro wa ardhi uliomsumbua kwa muda mrefu kwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Homera kupitia kliniki ya msaada wa kisheria mkoani humo.

Baada ya kusikilizwa, timu ya Wataalamu wa Wizara na Manispaa ya Singida wakishirikiana na Ofisi ya mtaa walielekea katika eneo lililokuwa na mgogoro ili kupata uhalisia na kujiridhisha juu ya hoja zilizowasilishwa na mzee Jumanne kuhusu mgogoro huo wa ardhi.

Serikali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imetangaza kuwa vijana 5,746 wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya uanagenzi, yata...
16/01/2026

Serikali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imetangaza kuwa vijana 5,746 wamechaguliwa kujiunga na mafunzo ya uanagenzi, yatakayowawezesha kupata ujuzi wa vitendo na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi kwa kujiajiri au kuajiri wenzao.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, amesema mafunzo hayo yanadhaminiwa na Serikali kwa asilimia 100. Mafunzo yatafanyika katika vyuo 47 nchini yakihusisha fani za ubunifu wa mitindo na ushonaji nguo, ufundi bomba, uashi, useremala, uchomeleaji na uungaji vyuma, upakaji rangi, upishi, utengenezaji wa vipuri vya mitambo, ufundi magari, umeme wa majumbani na viwandani, huduma za hoteli na utalii, pamoja na ukataji madini na ufundi vyuma.

Aidha, Waziri Sangu amesema Serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukuza ujuzi wa vijana na kuhakikisha nguvu kazi inashindana katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi. Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa njia ya uanagenzi inalenga kuhakikisha vijana wanapata ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko, hivyo kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri kikamilifu.

HT’ |  Milango bado migumu dakika 45 za kwanza, Dodoma Jiji wakikipiga dhidi ya Singida Black Stars katika Dimba la Jamh...
16/01/2026

HT’ |

Milango bado migumu dakika 45 za kwanza, Dodoma Jiji wakikipiga dhidi ya Singida Black Stars katika Dimba la Jamhuri Dodoma.

Dodoma Jiji 0️⃣🆚0️⃣ Singida Black Stars.

Singida Black Stars imethibitisha kuwa beki wake wake wa kushoto, Nickson Kibabage, amehamia Simba SC kwa uhamisho wa bu...
16/01/2026

Singida Black Stars imethibitisha kuwa beki wake wake wa kushoto, Nickson Kibabage, amehamia Simba SC kwa uhamisho wa bure. Taarifa iliyotolewa na klabu leo imefafanua kuwa uongozi umekubali kumwachia mchezaji huyo kwa manufaa yake binafsi.

"Singida Black Stars inafahamisha umma kuwa imekubali maombi ya uongozi wa Simba SC kumruhusu Nickson Kibabage kujiunga na klabu hiyo. Baada ya majadiliano, uongozi umeamua kumtoa mchezaji huyo bila malipo," imesema taarifa ya klabu.

Aidha, klabu imesisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya falsafa ya kuendeleza vipaji vya wachezaji wazawa. Simba SC, inayoshiriki mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, inatoa fursa nzuri kwa Kibabage ambaye pia ni mchezaji wa Timu ya Taifa.

16/01/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda anatarajiwa kuwasilisha ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe wa kuthibitisha dhamira ya Tanzania kuwa moja ya nchi mwenyeji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027.

Akizungumza na waandishi wa habari Januari 16, 2026 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam, saa chache kabla ya kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya ujumbe huo, Makonda amesema kuwa, hatua hiyo ni matokeo ya juhudi kubwa za Serikali katika kuimarisha sekta ya michezo hususani miundombinu ya viwanja, usafiri, malazi na maandalizi ya kiufundi yanayokidhi viwango vya kimataifa.

Ameongeza kuwa, Tanzania kuwa mwenyeji wa AFCON 2027 itakuwa ni fursa adhimu ya kutangaza sekta ya utalii, kuimarisha diplomasia ya michezo, pamoja na kukuza uchumi kupitia ajira na biashara zitakazotokana na mashindano hayo.

Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, le...
16/01/2026

Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Januari 16, 2026, imekutana na wataalamu wa ustawi wa jamii na saikolojia katika Ukumbi wa Ngorongoro, uliopo katika ofisi za Benki Kuu ya Tanzania (BoT), jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, amesema lengo la kukutana na wataalamu hao ni kupata uelewa wa kina kuhusu madhara ya kisaikolojia na kijamii yaliyotokana na matukio ya wakati na baada ya uchaguzi huo.

Ameongeza kuwa wataalamu hao, kutoka taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali, pia wamejadili mapendekezo ya namna bora ya kuyashughulikia madhara hayo ili kurejesha ustawi wa jamii na kuimarisha mshik**ano wa kitaifa.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Januari 16, 2026, ameongoza kikao cha kimkakati kilichowakutanisha mawaziri, naib...
16/01/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Januari 16, 2026, ameongoza kikao cha kimkakati kilichowakutanisha mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wa kisekta, kilichofanyika ofisini kwake, Mlimwa, jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, viongozi hao wamejadili kwa kina changamoto za biashara kati ya Tanzania na Zambia, pamoja na hatua za kuboresha uratibu na ufanisi wa shughuli za kibiashara kati ya nchi hizo mbili.

Wizara zilizoshiriki kikao hicho ni pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Aidha, kikao hicho kimehudhuriwa pia na Wakuu wa Mikoa ya Mbeya, Songwe na Rukwa.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Share

Tanzanian Broadcasting Corporation

TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.