TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

Mfumo wa kidijitali wa Tanzania Chamber Portal (TCP) umeendelea kuboresha biashara nchini, ukifanya iwe rahisi, haraka n...
28/11/2025

Mfumo wa kidijitali wa Tanzania Chamber Portal (TCP) umeendelea kuboresha biashara nchini, ukifanya iwe rahisi, haraka na wazi kwa wafanyabiashara.

Akizungumza jijini Mwanza ambako mafunzo ya mfumo huo yanaendelea kwa siku ya tatu mfululizo, Afisa TEHAMA wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Nelson Urio amesema mfumo huo unarahisisha huduma muhimu k**a usajili wa wanachama na kuripoti malalamiko kwa njia salama na haraka.

Ameongeza kuwa kuunganishwa kwa TCP na mifumo ya Serikali k**a TANeSW – Single Window kumepunguza muda wa kupata huduma na kuongeza uwazi, jambo linalosaidia mauzo ya nje na usafirishaji wa bidhaa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema TCP imefungua fursa kubwa kwa wafanyabiashara wa mikoani kupata huduma kwa wakati, bila usumbufu.

Kwa ujumla, TCP inasaidia kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kwenye masoko ya kimataifa, kukuza mauzo ya nje, na kuimarisha biashara kidijitali nchini.

28/11/2025

Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, amewataka wadau wa sekta ya ujenzi nchini kuhakikisha wanatumia teknolojia za kisasa zinazozingatia utunzaji wa mazingira katika ujenzi wa miundombinu imara, endelevu na ya kisasa.

Akizungumza mkoani Dar es Salaam wakati wa hafla ya utoaji wa Tuzo za Afrika Mashariki za Sekta ya Ujenzi na Miundombinu, Dkt. Kiruswa amesema sekta ya ujenzi na miundombinu imeendelea kuwa mhimili muhimu wa uchumi kwa kuchochea ajira na kuimarisha sekta nyingine, ambapo katika mwaka wa fedha 2024/2025, madini ya viwandani yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni moja yaliuzwa kwa wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chemba ya Ujenzi, Pamela Shoo, amesema sekta ya ujenzi na miundombinu ni nguzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi, huku akiiomba Serikali kuongeza ushirikiano na wadau ili kuiwezesha sekta hiyo kwenda sambamba na kasi ya ukuaji wa teknolojia duniani.

Ijumaa Kareem.
28/11/2025

Ijumaa Kareem.

28/11/2025

Vijana changamkieni fursa za utalii wa ikolojia

Muhifadhi wa Msitu wa Mazingira Asilia wa Amani uliopo mkoa wa Tanga, Nanzia Shedura, ametoa wito kwa vijana nchini kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo kwenye sekta ya utalii, ikiwemo utalii wa ikolojia katika mkoa huo na maeneo mengine nchini, ili waweze kujiingizia kipato.

Ameeleza kuwa katika Hifadhi ya Msitu wa Amani wenye hekta zaidi ya 8,000, uliopo mkoani Tanga, vipo vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo utalii wa utamaduni na historia, utalii wa ndege, mapango ya Ambaoni, maporomoko ya maji, utalii wa wanyama watambaao n.k. Ameeleza kuwa aina zote hizi za utalii ni fursa nzuri kwa vijana, hivyo wanapaswa kuzichangamkia.

Kwa upande wake, mwongoza watalii wa Hifadhi ya Msitu wa Amani, Gabriel Ponera, ametaja utalii wa ndege wa msituni kuwa na uhaba wa nguvu kazi ya kuongoza watalii katika eneo hilo, huku akiwataka vijana kuchangamkia fursa hiyo kwa kuongeza ujuzi utakaowawezesha kuongoza utalii kwa ufanisi mkubwa.

Utalii wa ikolojia ni aina ya utalii ambao kivutio chake kikuu ni kuonyesha mandhari na hufanyika katika maeneo ya misitu au porini.

Yaliyomo katika kurasa za mbele za magazeti leo Novemba 28, 2025.
28/11/2025

Yaliyomo katika kurasa za mbele za magazeti leo Novemba 28, 2025.

27/11/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi ya Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete amekitaka Chuo cha Utumishi wa Umma kuhakikisha kinatoa mafunzo yatakayoendana na mipango ya serikali kufikia dira ya maendeleo ya Mwaka 2050.

Akizungumza na watendaji wa Chuo cha Utumishi wa Umma Jijini Dar es Salaam Waziri Kikwete amesisitiza kuwa chuo hicho kina wajibu wa kutoa mafunzo kwa wanaonza kazi lakini pia kutoa mafunzo endelevu wale waliopo kazini.

"Msingi mkubwa wa dira ya 2050 lazima tufanye tafakari ya kina ya wapi tunaelekea katika miaka 50 ijayo kwa kuweka mazingira mazuri ambayo watumishi wa umma wanakuwa wanaweza kujitofautisha na watu wengine."Amesema Kikwete

Ameongeza kuwa miongoni mwa majukumu ya chuo cha Utumishi wa Umma ni kuwarekebisha watumishi wa umma kufikia adhama ya serikali katika kuwahudumia wananchi.

Naye Mkuu na Ntendaji wa Chuo hicho Dkt.Ernest Mabonesho ameeleza kuwa kwa sasa Chuo hicho kimekamilisha jumla ya tafiti nane ikiwemo sababu ya kiwepo kwa migogoro miongoni mwa viongozi ambao ni wateule wa Rais katika ngazi ya serikali za mitaaa pamoja na masuala ya teknolojia na mabadiliko ya stadi na matumizi ya tehama katika kufanikisha utoaji huduma bora.

27/11/2025

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Nicodemus Mk**a, amewataka wawekezaji katika sekta ya ujenzi kutumia fursa zinazotolewa na mazingira wezeshi yanayoendelea kujengwa na serikali ili kuanzisha miradi yenye tija kwa maendeleo ya uchumi wa nchi.

Mk**a alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa uwasilishaji wa hati fungani ya kampuni ya Saruji ya Simba Cement, yenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 203.75, kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE). Alifafanua kuwa Mamlaka imeidhinisha utoaji wa hati fungani hiyo baada ya kampuni kukidhi vigezo vinavyokubalika kibiashara ndani na kimataifa.

Aidha, Mk**a amesema fedha zitakazopatikana kupitia hati fungani hiyo zitaleta mageuzi makubwa katika sekta ya ujenzi, hivyo kuchochea maendeleo ya watu na taifa kwa ujumla.

Emmanuel Nyalali, Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE, ameongeza kuwa Simba Cement imetumia njia rafiki na jumuishi kwa wadau katika kuongeza mitaji ya kuendesha miradi ya maendeleo. Amesisitiza kuwa mfano huu unaweza kuigwa na taasisi nyingine, sio tu kwa faida ya mtu binafsi, bali pia kwa maendeleo ya taifa.

Nyalali amefafanua kuwa fedha hizo pia zitasadia kupanua uwezo wa uzalishaji na kuongeza ufanisi wa kiutendaji, huku akipongeza ushirikiano kati ya wadau wote na taasisi zinazohusika kufanikisha zoezi hilo.

27/11/2025

Baadhi ya wanawake wa mikoa ya Dar es Salaam na Dodoma wamewaasa vijana kote nchini kutoshiriki matukio ya uvunjifu wa amani yanayopangwa kufanyika Disemba 9, 2025, badala yake, siku hiyo waadhimishe Siku ya Uhuru kwa kuitunza na kudumisha amani ya nchi.

Wanawake hao wametoa rai hiyo kwa nyakati tofauti, huku wakiwasihi vijana kuwa wasikivu na kutojihusisha na matukio ya uvunjifu wa amani yanayopangwa na wasiotakia mema Tanzania.

27/11/2025

Wazazi nchini wametakiwa kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kufuatilia malezi, makuzi na matunzo ya watoto wao ili kuwajengea msingi imara wa kimaadili hata watakapokuwa watu wazima, na kusaidia taifa kuwa na kizazi bora.

Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma, Novemba 27, 2025, na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi, wakati wa kikao na vikundi vya wajasiriamali katika kata ya Ihumwa.

Mahundi amesema ni muhimu wazazi na walezi kutambua kuwa malezi chanya ya watoto ndio msingi imara wa kimaadili katika vizazi vijavyo, hivyo wanapaswa kuzingatia wajibu wao ili kuboresha ustawi wa watoto.

Aidha, Waziri Mahundi amewasisitiza wajasiriamali kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo katika wizara yake pamoja na wizara nyingine, ili waweze kujikwamua kiuchumi na kukuza pato la taifa.

27/11/2025

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema ujenzi wa matanki 15 ya hifadhi ya mafuta Kigamboni utapunguza gharama za ushushaji na muda wa meli kusubiri kutoka siku 22 hadi 7, hivyo kuongeza ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam kikanda.

Amesema mradi umefikia asilimia 33.57 na unatarajiwa kukamilika Agosti 2026, huku Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) ikielekezwa kusimamia mkandarasi ili kuhakikisha ubora na kukamilisha kazi kwa wakati.

27/11/2025

Wadau mbalimbali wamejitokeza kumpongeza Miss Universe Tanzania, Naisae Yona, kwa kushinda tuzo ya Most Beautiful People alipokuwa kwenye mashindano ya Miss Universe nchini Thailand, katika bustani ya Bravo Coco jijini Dar es Salaam.

Aidha, kwa upande wake, muandaaji wa , , amemshukuru mama yake Naisae kwa kumwamini na kumwachia mwanae.

Wadau walioshiriki ni pamoja na Miss Grand Tanzania 2025, , na Miss Tanzania 2022, , pamoja na wengine wengi.

Wadau wengine ni Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Hyundai Tanzania, pamoja na Rushtrek Tours

Wadau wa mazingira mkoani Katavi wametoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti, k**a njia ya ku...
27/11/2025

Wadau wa mazingira mkoani Katavi wametoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti, k**a njia ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ikiwemo uhaba wa mvua na ongezeko la joto.

Wito huo umetolewa baada ya kushiriki kampeni ya upandaji miti ya TBC Mti wa Mama 27 ya Kijani, ambapo zaidi ya miti 300 imepandwa katika Shule ya Sekondari Nsimbo, mkoani humo.

Akizungumza baada ya kushiriki zoezi hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Jamila Yusuph, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi, ameipongeza TBC kwa kufikisha kampeni hiyo mkoani humo na kuwasihi wananchi kuendeleza utamaduni wa kupanda miti ili kulinda na kuhifadhi mazingira.

Kampeni ya Mti wa Mama 27 ya Kijani imelenga kutoa elimu na hamasa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira kupitia upandaji miti.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Share

Tanzanian Broadcasting Corporation

TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.