TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

30/07/2025

Mchambuzi wa masuala ya siasa, Paternus Niyegira, amesema kuna somo la kujifunza kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), hasa katika kipindi cha uchaguzi.

“Cha kujifunza kwenye CCM ni ule umoja na mshikamano linapokuja suala la uchaguzi. Tumeona vyama vingine uchaguzi ukifika wanafarakana, na hata baada ya uchaguzi mfarakano unaendelea,” amesema Niyegira.

Alikuwa akizungumza katika mahojiano kwenye kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Julai 31, 2025.

Ameongeza kuwa CCM imekuwa na neema ya kuelewa kwamba hata wakitofautiana ndani kwa ndani, huungana kwa haraka hasa pale wanapoona hatari ya kupoteza madaraka.

“Wanapokuwa kwenye uchaguzi, hata wakikosana au wakianza kuwa na wasiwasi kwamba wanaweza kupoteza madaraka, huamua kushikamana,” amesema Niyegira.

Leo ni kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Ally Mwinyimwaka, afisa usafirishaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).Tun...
30/07/2025

Leo ni kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Ally Mwinyimwaka, afisa usafirishaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Tunamtakia maisha marefu.

Kikosi cha Simba SC kimeondoka leo alfajiri Julai 30,2025 kuelekea nchini Misri, kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya (...
30/07/2025

Kikosi cha Simba SC kimeondoka leo alfajiri Julai 30,2025 kuelekea nchini Misri, kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya (Pre-Season).

Simba, chini ya Kocha Fadlu Davids wataweka kambi nchini Misri ikiwa ni maandalizi ya msimu huo mpya kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na mashindano ya Kimataifa.

Che Malone Fondoh hatakuwa sehemu ya kikosi hicho, kwani klabu hiyo imetangaza rasmi kuachana naye.

30/07/2025

Katika kipindi cha Mizani wiki hii, tutakuwa na Stephen Wasira, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, ambapo tutajadili hali ya kisiasa nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Tafadhali usikose kufuatilia kipindi hiki kitakachorushwa mbashara, kikiongozwa na Dkt. Ayub Rioba Chacha.

Ni Jumatano, Julai 30,2025 kuanzia saa 3:00 usiku, na marudio ni siku ya Alhamisi, Julai 31,2025.

TAFAKURI ANGAVU YA EZEKIEL SIMBEYE
30/07/2025

TAFAKURI ANGAVU YA EZEKIEL SIMBEYE

Maoni yako yatasomwa kwenye kipindi cha Jambo Tanzania
30/07/2025

Maoni yako yatasomwa kwenye kipindi cha Jambo Tanzania

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni miongoni mwawaliopita mchujo wa kwanza na hivyo kupata rid...
29/07/2025

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
ni miongoni mwa
waliopita mchujo wa kwanza na hivyo kupata ridhaa ya
kuingia mchujo mwingine wa kura za maoni.

Klabu ya Simba imetangaza rasmi kumsajili  Rushine De Reuck (29) akitokea Mamelodi Sundowns. Rushine alikuwa anaitumikia...
29/07/2025

Klabu ya Simba imetangaza rasmi kumsajili Rushine De Reuck (29) akitokea Mamelodi Sundowns. Rushine alikuwa anaitumikia Maccabi Petah Tikva kwa mkopo.

Rushine anamudu kucheza nafasi tatu uwanjani: mlinzi wa kati, mlinzi wa kulia na kiungo mkabaji.

Huu unakuwa usajili wa kwanza kwa Mnyama Simba kuuweka hadharani.

29/07/2025
29/07/2025

Kupitia Programu ya BOOST, Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha imepokea Sh. bilioni 2.071 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu ya awali na msingi, hatua iliyochochea mafanikio makubwa ya kimkakati.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Zainabu Makwinya, amesema kati ya fedha hizo, Sh. milioni 332 zinatumika kujenga shule ya msingi katika eneo la shule ya sekondari, ikiwa ni utekelezaji wa Sera ya Elimu ya lazima ya miaka 10 nchini kote.

“Shule hii si tu kwamba itakuwa ya mfano, bali inawakilisha taswira ya elimu na ujuzi unaohitajika katika Karne ya 21 na kufungua fursa kwa kizazi kijacho,” amesema Makwinya.

Amesisitiza kuwa Serikali imedhamiria kuboresha miundombinu ya kimkakati ili kuwawezesha vijana kupata maarifa na stadi za kujiajiri na kuajiriwa katika nyanja mbalimbali kitaifa na kimataifa.

29/07/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, amezitaka hospitali zote za umma kutekeleza kikamilifu maelekezo ya Serikali, ikiwemo kuhakikisha huduma inatolewa kwanza bila kigezo cha fedha. Amesisitiza kuwa ni marufuku hospitali kuzuia miili ya marehemu kwa sababu ya deni la gharama za matibabu.

Akizungumza Julai 29, 2025, wakati wa ziara katika hospitali za rufaa za mikoa jijini Dar es Salaam, Dkt. Shekalaghe amesema si busara wala utu kwa hospitali ya umma kuzuia huduma au mwili wa marehemu kwa sababu ya ukosefu wa fedha, kwani lengo kuu la Serikali ni kutoa huduma, si kukusanya fedha.

“Hakuna mwananchi anayepaswa kunyimwa huduma kwa sababu ya kukosa fedha, hayo si malengo ya Serikali. Mwananchi asiye na uwezo wa kifedha atachunguzwa, na akikidhi vigezo, atasaidiwa,” amesema.

Aidha, amesisitiza kuwa hospitali lazima zifuate muongozo wa Serikali unaowataka waganga wafawidhi kuhakikisha kuwa miili ya marehemu haizuiwi. “Wapeni mwili ndugu zake ili waende kumzika… si vyema, si busara kuzuia mwili kwa sababu ya fedha,” amesisitiza.

29/07/2025

Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri wamehimizwa kuonesha mabadiliko chanya katika usimamizi wa elimu baada ya kushiriki mafunzo ya siku tatu yanayoendelea Chuo cha ADEM, Bagamoyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Elimu, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Emmanuel Shindika amesema mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia Programu ya BOOST kuimarisha utawala bora katika shule za msingi.

“Serikali na wadau wake wametoa rasilimali nyingi kuwezesha mafunzo haya. Mna wajibu wa kubadilika na kuwa viongozi wa mfano,” alisema Dkt. Shindika.

Aliongeza kuwa hadi sasa, Walimu Wakuu 17,794 wa shule za msingi za Serikali na maafisa elimu kata kutoka mikoa 12 wamepatiwa mafunzo ya aina hiyo.

Dkt. Shindika pia ameishukuru Wizara ya Elimu na ADEM kwa uratibu wa mafunzo, huku akiwataka washiriki kuwa mabalozi wa mabadiliko ya kweli kwenye sekta ya elimu.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share

Tanzanian Broadcasting Corporation

TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.