TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

22/07/2025

Simulizi kuhusu kiungo wa Taifa Stars, Mudathir Yahaya "Muda"

Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC wamethibitisha kumsajili winga Offen Chikola (26), raia wa Tan...
22/07/2025

Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC wamethibitisha kumsajili winga Offen Chikola (26), raia wa Tanzania, akitokea Klabu ya Tabora United.

"Left Footer Magician is now Green & Yellow" wameandika Yanga kupitia akaunti rasmi ya klabu hiyo

Chikola anaungana Moussa Balla Conte ambaye tayari amesajiliwa na klabu hiyo

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Mohamed Omar, ameipongeza Taasisi ya Elimu Tan...
22/07/2025

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Mohamed Omar, ameipongeza Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa jitihada zake katika kukuza sekta ya elimu, hususan kupitia mifumo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) inayochochea ujifunzaji na ufundishaji nchini.

Dkt. Hussein ametoa pongezi hizo leo, Julai 22, 2025, alipotembelea ofisi za TET zilizopo Mikocheni, Jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujionea shughuli za taasisi hiyo na kupokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dkt. Aneth Komba, pamoja na wajumbe wa menejimenti ya taasisi hiyo.

“Nimefurahishwa na utendaji wa TET, hasa katika eneo la mifumo ya TEHAMA ambayo imewezesha kuwafikia walimu karibu nchi nzima,” amesema Dkt. Hussein.

Katika hatua nyingine, amesifu maboresho ya mitaala inayotekelezwa na TET, akisema kuwa mabadiliko hayo yanaongeza uwezo wa wanafunzi kujiajiri, hasa kupitia mkondo wa Amali unaompa mwanafunzi nafasi ya kuchagua fani anayopenda kuisomea baada ya kumaliza darasa la sita.

Aidha, Dkt. Hussein ameitaka TET kuandaa mtaala utakaochangia katika kukabiliana na changamoto ya taka ngumu, ambayo imekuwa kero kubwa katika miji mikuu k**a Dar es Salaam, Arusha, Mbeya na Mwanza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dkt. Aneth Komba, amesema taasisi yake iko tayari kutekeleza maelekezo hayo, ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti katika maeneo yenye upungufu wa walimu na vifaa vya TEHAMA, ili yapewe kipaumbele katika awamu zijazo za utekelezaji.

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imeanza mashindano ya CECAFA ya Mataifa Matatu kwa ushindi baada ya kuilaza Ugan...
22/07/2025

Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, imeanza mashindano ya CECAFA ya Mataifa Matatu kwa ushindi baada ya kuilaza Uganda, The Cranes, bao 1-0 katika Dimba la Black Rhinos, Karatu, Tanzania.

Bao la Taifa Stars limefungwa dakika ya 14 na Iddy Seleman Nado, ambalo lilitosha kuwapa Stars alama tatu muhimu dhidi ya Uganda, kwenye michuano maalumu ya CECAFA inayoendelea mkoani Arusha, Tanzania.

Mashindano hayo, yanayoshirikisha mataifa ya Tanzania, Uganda na Senegal, ni sehemu ya maandalizi ya michuano ya CHAN 2024, inayotarajiwa kuanza Agosti 2, 2025.

Ikumbukwe kuwa Kenya imejitoa kwenye michuano hiyo kufuatia pendekezo la Kocha Mkuu wa Harambee Stars, Benedict McCarthy.

Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na klabu ya Sporting CP ya dili la kumsajili mshambuliaji Viktor Gyokeres kwa dau ...
22/07/2025

Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na klabu ya Sporting CP ya dili la kumsajili mshambuliaji Viktor Gyokeres kwa dau la Euro Milioni 63.5 (Fixed) pamoja na ongezeko la Euro Milioni 10 baadae (add ons) kufanya package nzima kuwa Euro Milioni 73.5

Gyökeres, 27, raia wa Sweden anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano utakaombakisha kwa Washika Mitutu hao mpaka Juni 2030.

22/07/2025

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametaja vigezo vya kupewa ufadhili wa Samia Scholarship kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha sita na kupata alama za juu za ufaulu zinazowapa sifa ya kuingia katika mpango huo.

Amesema ili kujaza maombi kwenye tovuti ya Wizara ya Elimu, mwanafunzi anatakiwa kuwasilisha ombi la kusoma masomo ya Sayansi, TEHAMA, Hisabati, Uhandisi au Elimu ya Tiba.

Aidha, Prof. Mkenda amesema atakayetamani kusoma nje ya masomo hayo atalazimika kufuata utaratibu mwingine, k**a vile kuomba mkopo wa elimu ya juu.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere, amewataka wananchi kushirikiana na uongozi wa shule katika kutunza miu...
22/07/2025

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere, amewataka wananchi kushirikiana na uongozi wa shule katika kutunza miundombinu ya shule ili iendelee kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo na kuwa sehemu ya maendeleo ya Tanzania.

Makongoro etoa kauli hiyo Julai 22, 2025, wakati wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali, ikiwemo Shule Mpya ya Msingi Pwela, iliyopo Kitongoji cha Pwela, Kijiji cha Nambogo, Kata ya Milanzi. Katika ziara hiyo, amesifu juhudi za Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kwa kukamilisha ujenzi wa shule hiyo kwa zaidi ya shilingi milioni 130 kutoka mapato ya ndani ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga, Upendo Mangali, amesema mradi huo ni sehemu ya mkakati wa halmashauri kuboresha huduma ya elimu kwa kuisogeza karibu na wananchi, hususan wa maeneo ya pembezoni.

Wananchi wa Pwela wamesema wamepokea shule hiyo kwa furaha, wakieleza kuwa sasa watoto wao watapata elimu bora kwa urahisi na umbali mfupi.

Katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa pia amekagua miradi mingine ya maendeleo, ikiwemo ukamilishaji wa bwalo la chakula la Shule ya Sekondari Kizwite, ujenzi wa nyumba za walimu Shule ya Sekondari Mazoezi, jengo la wazazi katika Hospitali ya Isofu, Kituo cha Afya Senga, pamoja na maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege Sumbawanga.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amehani  msiba wa Baba Mzazi wa mwanasiasa mkongwe, William Nge...
22/07/2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amehani msiba wa Baba Mzazi wa mwanasiasa mkongwe, William Ngeleja, Mzee Mganga Ngeleja aliyefariki dunia Julai, 16, 2025 na kuzikwa jana (Julai 21, 2025) Kijijini kwake Bitoto, Wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza.

William Mganga Ngeleja aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Sengerema (2005-2020) kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Pia aliwahi kushika nafasi ya Waziri wa Nishati na Madini kati ya mwaka 2008 na 2012 katika Serikali ya Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo Julai 22, 2025, ameendelea na ziara yake rasmi nchini Belarus kwa kutembelea maeneo muh...
22/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo Julai 22, 2025, ameendelea na ziara yake rasmi nchini Belarus kwa kutembelea maeneo muhimu ya uzalishaji na ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na taifa hilo rafiki.

Akiwa katika mji wa Minsk, Waziri Mkuu ametembelea kiwanda cha Belmedpreparaty, ambacho ni maarufu kwa utengenezaji wa dawa za binadamu, na kiwanda cha Minsk Tractor Plant kinachozalisha matrekta na mitambo ya kisasa ya zana za kilimo.

Ujumbe wa Tanzania umejionea teknolojia ya hali ya juu inayotumika katika viwanda hivyo, jambo linalofungua milango ya ushirikiano wa kibiashara na kiufundi baina ya mataifa haya mawili, hususan katika sekta za afya na kilimo.

Katika ziara hiyo, Waziri Mkuu ameambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Cosato Chumi, pamoja na viongozi wengine wa Serikali.

Aidha, Majaliwa ameweka shada la maua katika mnara wa mashujaa wa Jamhuri ya Belarus, k**a ishara ya heshima kwa historia na ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Belarus.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuimarisha diplomasia ya kiuchumi, kuboresha huduma za afya, na kuinua tija katika sekta ya kilimo kupitia teknolojia za kisasa.

Serikali imesema kuwa mafunzo ya uimarishaji wa mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Burundi yanalenga kujenga uelewa ...
22/07/2025

Serikali imesema kuwa mafunzo ya uimarishaji wa mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Burundi yanalenga kujenga uelewa wa pamoja kati ya wataalamu wa nchi hizo mbili.

Kauli hiyo imetolewa leo, Julai 22, 2025, jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga, alipofungua mafunzo ya siku tano kuhusu uimarishaji wa mpaka huo.

Kwa mujibu wa Mhandisi Sanga, mafunzo hayo yataharakisha utekelezaji wa kazi ya uimarishaji wa mpaka wa kimataifa kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Burundi.

Amesema kuwa baada ya mafunzo haya, kazi ya uimarishaji mpaka itakamilika kwa wakati, huku akisisitiza kuwa mipaka ya kimataifa ipo, na kazi ya uimarishaji hufanyika pale panapotokea uharibifu wa mipaka hiyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Hamdouny Mansoor, amesema kuwa nchi hizo mbili zilikubaliana katika kikao chao kujenga uelewa wa pamoja kwa kukutana eneo moja, kupata mafunzo na baadaye kwenda uwandani kuimarisha mpaka.

Kwa mujibu wa Mansoor, mafunzo hayo yatajikita kwenye maeneo makuu manne: uwekaji vipimo, uwekaji alama katika ramani, masuala ya mikataba, na upigaji picha za anga utakaowezesha kutafsiri mpaka kwa kutumia teknolojia ya picha za anga.

22/07/2025

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema bajeti ya ufadhili wa Samia Scholarship kwa mwaka huu 2025/2026 imeruhusu wanafunzi 1,051 waliomaliza kidato cha sita kupata ufadhili wa kuendelea na masomo ya juu zaidi katika sayansi, hisabati na tiba kupitia ufadhili huo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo, Julai 22, 2025, katika ofisi za wizara hiyo, Prof. Mkenda amesema Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni tano ili kutoa ufadhili huo kwa wale watakaokuwa na vigezo, na kwamba wanafunzi watakaopata fursa hiyo ni wale ambao wamesoma masomo ya sayansi na wamepata alama za juu za ufaulu (Division 1).

Aidha, Prof. Mkenda amesema kipindi cha nyuma ufadhili huo ulikuwa ukitolewa kwa wanafunzi 650 pekee, ila hivi sasa Serikali ya Awamu ya Sita imeiongezea wizara hiyo bajeti, ndiyo sababu idadi imeongezeka na inaweza kuchukua wanafunzi 1,051.

Ongezeko la idadi ya laini za simu kwa ajili ya mashine kwa mashine (M2M)Laini za simu zilizosajiliwa kwa ajili ya mawas...
22/07/2025

Ongezeko la idadi ya laini za simu kwa ajili ya mashine kwa mashine (M2M)

Laini za simu zilizosajiliwa kwa ajili ya mawasiliano ya M2M zimeongezeka kwa laini 33,028 kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2025 yaani kutoka laini milioni 1.05 Machi 2025 hadi kufikia laini milioni 1.08 Juni 2025.

Kwa mujibu wa ripoti ya takwimu ya sekta ya mawasiliano ya Juni 2025, ongezeko hilo ni sawa na asilimia 3.1 na kwamba idadi ya laini za simu nchini imeongezeka hadi kufikia milioni 92.7.

Ongezeko la laini za simu linachochea ukuaji wa shughuli za kibiashara na kuwezesha maendeleo katika matumizi ya teknolojia katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Tembelea tovuti ya TCRA (www.tcra.go.tz), au kupitia kiunganisho https://bit.ly/44tXbii ilikupitia ripoti kamili ya takwimu ya sekta ya Mawasiliano (Aprili - Juni 2025).

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share

Tanzanian Broadcasting Corporation

TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.