TBConline

TBConline Ukurasa rasmi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC). Verified

Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia kampeni yake ya kuhamasisha kupanda miti ya '27 ya Kijani' kwa kushirikiana...
27/09/2025

Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia kampeni yake ya kuhamasisha kupanda miti ya '27 ya Kijani' kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, leo Septemba 27, 2025 imepanda miti 200 katika Shule ya Sekondari ya Bombambili iliyopo mkoani humo.

Akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela kwenye upandaji wa miti hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashimu Komba amewashukuru wadau wote walioshiriki kufanyika kwa zoezi hilo wakiwemo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ambao wametoa miche ya miti 200 na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ambao wamechimba mashimo.

Komba amesema kwa kushirikiana na Shule ya Sekondari ya Bombambili, wataisimamia miti hiyo iliyopandwa leo, ili iweze kukua na kuleta tija iliyokusudiwa.

Kila ifikapo tarehe 27 ya kila mwezi, TBC huendesha kampeni ya kupanda miti nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za kuikijanisha Tanzania.

📸

27/09/2025

Serikali imeanza kuboresha mradi wa maji wa chanzo cha Kapripoint kilicho katika Ziwa Victoria jijini Mwanza, lengo likiwa ni kuhakikisha huduma ya maji safi na salama inapatikana kwa saa 24 kila siku.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amesema hayo wakati akikagua upatikanaji wa huduma ya maji jijini Mwanza baada ya kukamilika matengenezo ya mtambo wa kusukuma maji uliopata hitilafu katika mradi wa maji wa Butimba.

Mtanda amesema mahitaji ya maji kwa jiji la Mwanza ni lita milioni 180 kwa siku, wakati uzalishaji wa sasa ni lita milioni 138. Maboresho ya mradi wa Kapripoint yataongeza uzalishaji kutoka lita milioni 90 hadi lita milioni 130 kwa siku, jambo litakalosaidia kupunguza uhaba wa maji katika jiji hilo la miamba.

RC Mtanda ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, pamoja na wataalamu kutoka Wizara ya Maji makao makuu na wale wa Mwanza.

27/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere, amewataka wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi na mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, zitakazofanyika kuanzia kk kesho Septemba 28 hadi Oktoba 1, 2025 katika halmashauri zote za mkoa huo.

Mwenge wa Uhuru mkoani Rukwa unategemea kukimbizwa kwa umbali wa kilomita 653.1, ambapo utafanya ukaguzi, kuweka mawe ya msingi, na kuzindua miradi 34 yenye thamani ya shilingi bilioni 55.3. Kaulimbiu ya mwaka huu ni: "Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.”

Aidha, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu na hamasa kwa wananchi juu ya mapambano dhidi ya changamoto mbalimbali ikiwemo UKIMWI, malaria, rushwa, dawa za kulevya, na changamoto za lishe.

Mkuu wa Mkoa amesisitiza mshik**ano, utulivu, na ushirikiano k**a nyenzo muhimu za kuendeleza maendeleo ya Mkoa wa Rukwa na taifa kwa ujumla.

27/09/2025

Futa Delete Kabisa

27/09/2025

Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mgodi wa Buckreef, Isack Bisansaba, amesema mgodi huo ambao Serikali ni sehemu ya umiliki wake unaendeshwa na Watanzania wazawa kwa asilimia 100 na hivyo ajira zaidi ya 200 za kudumu zilizopo katika mgodi huo zinashikiliwa na Watanzania.

Akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwenye kipindi maalumu kilichofanyika mgodini hapo mkoani Geita, Bisansaba amesema ajira hizo za kudumu zimetolewa kwa Watanzania kutoka maeneo mbalimbali nchini, huku ajira zaidi ya 300 za muda mfupi zikitolewa pia kwa wananchi wa vijiji vilivyo karibu na mgodi huo.

Bisansaba amesema mbali na kutoa ajira kwa wazawa, uwepo wa mgodi huo umeleta manufaa kwa jamii kwani katika kutekeleza sera ya kurejesha kwa jamii, wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali zinazonufaisha kijamii ya eneo la mgodi huo.

“Kwa miaka minne mfululizo tangu tulipoanza kufanya kazi rasmi mwaka 2021, tumekuwa tukitenga fedha kwa ajili ya miradi ya kijamii. Kila mwaka tumekuwa tukitenga zaidi ya shilingi milioni 400 na kujikita zaidi katika sekta ya afya kwa kujenga baadhi ya hospitali na maabara katika kata zinazotuzunguka, pamoja na sekta ya elimu kwa kununua madawati na kusambaza maji katika vijiji jirani,” amesema Bisansaba.

27/09/2025

Kaimu Mkurugenzi wa Michezo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Kanali Penina Igwe, amesema ushindi wa Bingwa wa Dunia wa Marathon, Sajini Taji Alphonce Simbu, ni ushindi wa jeshi na taifa kwa ujumla, na umeongeza ari kubwa kwa wanamichezo jeshini.

Akizungumza katika Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Septemba 27, 2025, Luteni Kanali Igwe amesema ushindi huo ni chachu kwa wanamichezo wote, si wanariadha pekee, kuongeza jitihada na kujituma ili kufanikisha mafanikio makubwa k**a aliyoyapata Simbu.

Amefafanua kuwa JWTZ lina mikakati ya muda mfupi, wa kati na wa muda mrefu katika kukuza michezo, ikiwemo kutumia nafasi za ajira jeshini kuwapokea wanamichezo wenye vipaji maalumu k**a Simbu, ambao huunganishwa na timu mbalimbali za michezo ndani ya jeshi.

Aidha, Igwe ameongeza kuwa jeshi limewekeza pia kwenye shule zake kuanzia ngazi ya msingi hadi sekondari, kwa lengo la kufuatilia na kukuza vipaji vya vijana ili kuviendeleza katika michezo.

27/09/2025

Bingwa wa Dunia wa Marathon, Sajini Taji Alphonce Simbu, amesema ushindi wake ni uthibitisho kuwa mchezaji yeyote wa Tanzania anaweza kushinda mashindano ya kimataifa endapo ataweka juhudi, nidhamu na kuwa mwaminifu kwa ndoto zake.

Akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Septemba 27, 2025, Simbu alieleza kuwa Rais wa Tanzania mara nyingi amekuwa akisisitiza kiu ya kuona michezo ya nchi ikifika mbali zaidi. Anasema motisha hiyo imekuwa chanzo cha hamasa kwa wachezaji, hususan katika mpira wa miguu, na imewapa nguvu ya kuongeza bidii.

Sajini-taji Alphonce Simbu alishinda mbio hizo Septemba 15, 2025 nchini Japan, baada ya kutumia muda wa saa 2:09:48 katika mashindano ya riadha ya dunia, na kuiweka Tanzania katika ramani ya michezo ya kimataifa.

27/09/2025

Bingwa wa Dunia wa Marathon, Sajini-taji Alphonce Simbu, amesema ushindi alioupata katika mashindano ya dunia yaliyofanyika Septemba 15, 2025 nchini Japan, ulitokana na mbinu na kasi aliyoitumia katika hatua za mwisho za mbio hizo.

Akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Septemba 27, 2025, Simbu alieleza kuwa kila mkimbiaji huingia uwanjani akiwa na mikakati yake, hali inayofanya ushindani kuwa mkubwa na wenye changamoto kubwa.

Aidha, alibainisha kuwa teknolojia ya chip aliyovaa ilithibitisha muda wake rasmi. Simbu alimaliza mbio hizo kwa muda wa saa 2:09:48, na kuipa Tanzania heshima kubwa katika mashindano ya riadha ya dunia.

Sabato Njema
27/09/2025

Sabato Njema

Maoni yako yatasomwa kwenye kipindi cha Jambo Wikiendi
27/09/2025

Maoni yako yatasomwa kwenye kipindi cha Jambo Wikiendi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, amesisitiza umuhimu wa amani na mageuzi ya kimata...
26/09/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, amesisitiza umuhimu wa amani na mageuzi ya kimataifa alipohutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jijini New York.

Amesema kuibuka upya kwa ukiukwaji wa sheria za kimataifa na matumizi ya nguvu kupita kiasi kunapelekea ukatili kwa watoto, wanawake, wazee na wagonjwa katika maeneo yenye migogoro.

Ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuishughulikia haraka changamoto zinazohusiana na unyonyaji wa rasilimali za Afrika, matumizi mabaya ya nguvu za kijeshi, ongezeko la bajeti za silaha na kushindwa kwa mataifa yenye nguvu kukomesha umwagaji damu. Amesema hatua hizo zinazuia maendeleo endelevu na ustawi wa binadamu.

Makamu wa Rais pia amepongeza juhudi za Katibu Mkuu wa UN, viongozi wa dunia na mashirika yanayoshirikiana katika upatanishi wa migogoro, hususani Mashariki mwa DRC, Sudan, Urusi, Ukraine, na Mashariki ya Kati. Amehimiza ushirikishwaji wa wanawake katika kutafuta amani, huku akisisitiza mchango wa Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kukuza nafasi za wanawake, amani na usalama kikanda na kimataifa.

Dkt. Mpango amesema Tanzania imejitolea katika utekelezaji wa SDG’s 2030, ikiwa imefanikisha asilimia 60 ya malengo, ikiwemo kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, kuongeza upatikanaji wa maji safi, na kuunganisha vijiji vingi kwenye mtandao wa umeme.

Amehimiza pia jumuiya ya kimataifa kuimarisha jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, ikiwemo kutekeleza ahadi za COP30, kuchangia Loss and Damage Fund, na kuongeza ufadhili wa masharti nafuu.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TBConline posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TBConline:

Share

Tanzanian Broadcasting Corporation

TBC is your news, entertainment, music fashion website. We provide you with the latest breaking news and videos straight from the entertainment industry.