
27/09/2025
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia kampeni yake ya kuhamasisha kupanda miti ya '27 ya Kijani' kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, leo Septemba 27, 2025 imepanda miti 200 katika Shule ya Sekondari ya Bombambili iliyopo mkoani humo.
Akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela kwenye upandaji wa miti hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashimu Komba amewashukuru wadau wote walioshiriki kufanyika kwa zoezi hilo wakiwemo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ambao wametoa miche ya miti 200 na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ambao wamechimba mashimo.
Komba amesema kwa kushirikiana na Shule ya Sekondari ya Bombambili, wataisimamia miti hiyo iliyopandwa leo, ili iweze kukua na kuleta tija iliyokusudiwa.
Kila ifikapo tarehe 27 ya kila mwezi, TBC huendesha kampeni ya kupanda miti nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za kuikijanisha Tanzania.
📸