Ahadun Ahad Studio

Ahadun Ahad Studio Ni media, iliodhamiria kukuletea elimu juu ya Imani yako, ukumbusho, mawaidha, pamoja na upambanuzi juu ya Uislam na waislam. Baki hapa ili ufaidike.

media hii ipo kwa ajili ya kukufahamisha Uislam nje, ndani.. Ahadun Ahad Studio,
Onja Ladha Ya Imaan.

اَلّٰهُمَّ أَعِنِّيْ عَلَىٰ ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ. Allāhumma aʿinni ʿala dhikrika wa shukrika wa ḥusn...
16/09/2024

اَلّٰهُمَّ أَعِنِّيْ عَلَىٰ ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ.

Allāhumma aʿinni ʿala dhikrika wa shukrika wa ḥusni ʿibādatik.

Ewe Allah, nisaidie kukukumbuka Wewe, kukushukuru Wewe, na kukuabudu Wewe kwa namna iliyo bora.

Muadh b. Imepokewa kutoka kwa Jabal (رضي الله عنه) kuwa Mtume wa Allah (ﷺ) alimshika mkono na akasema:

“Ewe Mu’adh, ninaapa kwa jina la Allah kwamba ninakupenda. Naapa kwa jina la Allah kwamba ninakupenda. Ewe Mu’adh, nakushauri:

Usikose kamwe kusema [hayo hapo juu] baada ya kila swala.

[Abu Dawud 1522]

Sadaka humpandisha mtoaji wake daraja la juu zaidi Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, amesema:  “Maisha haya ya dunia ...
08/09/2024

Sadaka humpandisha mtoaji wake daraja la juu zaidi

Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, amesema:

“Maisha haya ya dunia ni ya makundi manne ya watu: mtu ambaye Allah amempa mali na elimu, basi akamcha Mola wake Mlezi, akaweka mafungamano mazuri na ndugu zake kwa mali hii, na anazijua haki za Allah juu yake, hakika huyu ndiye katika kiwango bora…”

[At-Tirmithi]

Assalam alaykum warahmatullah..U hali gani ndugu?Huenda wewe ni miongoni mwa watu wanao struggle kuamka kusali Tahajjud....
30/08/2024

Assalam alaykum warahmatullah..

U hali gani ndugu?

Huenda wewe ni miongoni mwa watu wanao struggle kuamka kusali Tahajjud..

Umeset alarm, lakini wapi..🤦🏽‍♂️
Umejitahid ulale mapema, wapi wee..🤦🏽‍♂️
Ukamuomba hadi mtu akuamshe, ase kwan uliamka basi..😄

Ikiwa huyu ni wewe basi shuka nami nikueleze mambo 5 ya kufanya ili uweze kuamka usiku na kumuomba Allah..

1. Lala ukiwa twahara (wudhu), na utakapolala ukiwa na wudhu utapata Faida ya kuomba na malaika pindi utapopatwa na usingiz hadi utakapoamka na kutokana na hilo itakuwa rahisi kwako kuamka..

2. Weka Nia ya kuamka usiku kuswali, Na hakika penye Nia, Pana njia. Utakapokusudia kuamka usiku, itakuwa vyepesi kwako kuamka usiku na pia hata usipoamka utalipwa na Allah kwa Nia yako ya kuamka

3. Jitahidi Usile Sana usiku, Usile hadi ukashiba. Kumbuka shibe ni mwana malevya😄. Ukishiba sana utalewa na utashindwa kuamka usiku kuswali..

4. Ikiwa utapata nafasi mchana, pumzika kidogo lala. Ili kuupa mwili nguvu ya kuamka usiku..

5. Jiepushe na maradhi ya Moyo k**a vile chuki, hasadi, unafiki, kusengenya watu katika moyo wako, kuwadhania watu vibaya moyoni mwako, kuwasema watu vibaya moyoni mwako n.k.

Kwan ukiwa na tabia hizo moyo wako utakuwa mzito na utashindwa kuamka kuswali Tahajjud.

By the way, ikiwa unahitaji kujifunza zaidi na kupata ukumbusho na mawaidha kutoka kwangu kwa njia ya WhatsApp bonyeza hapo

https://bit.ly/3Mx7IPH

Al Akh. Mubaarak

يوم الجمعة Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira kuwa Mtume wa Allah (ﷺ) amesema: Aliyetawadha vizuri kisha akaja kwenye Swal...
29/08/2024

يوم الجمعة

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraira kuwa Mtume wa Allah (ﷺ) amesema:

Aliyetawadha vizuri kisha akaja kwenye Swalah ya Ijumaa, akasikiliza (mahubiri), akanyamaza, (madhambi yake) yote baina ya muda huo na Ijumaa ijayo yatasamehewa kwa ziada ya siku tatu.

[Sahih Muslim 857]

゚ ゚viralシ

Tetea heshima ya kaka/dada yako Muislamu: Amesema Mtume ﷺ: "Mwenye kulinda utukufu wa ndugu yake ALLAH atauepusha moto u...
24/08/2024

Tetea heshima ya kaka/dada yako Muislamu:

Amesema Mtume ﷺ:

"Mwenye kulinda utukufu wa ndugu yake ALLAH atauepusha moto usoni mwake Siku ya Kiyama."

[Sahih At-Tirmidhiy #1931]

Papaa Sedute Mpenda Amani, Hamisi Matimbwa, Azhad Said, Mwanaidy Hamadi, Emanuel Msafiri

✒ Allah Harudishi Mikono Iliyoinuliwa Mtupu 🤲🏻 Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: إن ا...
12/08/2024

✒ Allah Harudishi Mikono Iliyoinuliwa Mtupu 🤲🏻

Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

إن الله رحيم حيي كريم يستحي من عبده أن يرفع إليه يديه ثم لا يضع فيهما خيرا

“Hakika Allaah ni Mwingi wa Rehema, Mwenye haya, Mkarimu, Anafedheheka kwa mja Wake kunyanyua mikono yake Kwake kisha Haweki chochote cha Khayr (wema).”

● [مختصر صحيح الجامع الصغير ١٧٦٨ ، صححه الألباني]

✒ Malipo ya Maswahabah 50 (Allah Awawiye Radhi) Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kw...
09/08/2024

✒ Malipo ya Maswahabah 50 (Allah Awawiye Radhi)

Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

“Kwa hakika mbele yenu zipo siku za subira ambazo ndani yake kuifuata dini kikweli kweli itakuwa k**a KUSHIKA KAA LA MOTO, mwenye kutenda haki katika kipindi hicho atapata thawabu k**a WANAUME HAMSINI watendao k**a yeye.”

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa na Swahaba: “Ewe Mtume wa Allah ujira wa watu hamsini miongoni mwetu au wao?”, akajibu: “Bali malipo ya watu hamsini miongoni mwenu.”

● [صحيح الترغيب والترهيب ٣١٧٢ ، صححه الألباني]

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ahadun Ahad Studio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share