Numeric Digital

Numeric Digital Welcome to Numeric Digital! Your ultimate destination for dynamic and diverse content that delves into the heart of national and international news.

At Numeric Digital, we strive to bring you insightful stories.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kutegemea kupata umeme wa uhakika baad...
05/04/2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kutegemea kupata umeme wa uhakika baada ya Mradi wa kufua umeme kutoka Bwawa la Julius Nyerere uliokuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na Watanzania kukamilika rasmi.

Waziri Biteko ameyasema hayo leo April 5, 2025 baada ya kutembelea Mradi huo akiwa ameambatana na Mawaziri ambao ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mha. Hamadi Masauni.

Amesema hivi sasa mitambo yote tisa inafanya kazi ambapo amefafanua kuwa kukamilika kwa Mradi huo kumechangiwa na maono ya Rais wa Awamu ya Sita Mhe. Dokta Samia Suluhu Hassan ambaye aliupokea Mradi ukiwa katika asilimia 33 ya utekelezaji wake na ndani ya kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake ameweza kuukamilisha Mradi.

Katika hatua nyingine Mhe Dkt Doto Biiteko amelishukuru Shirika la umeme Tanzania TANESCO kwa utekelezaji wa Mradi kwa kiwango cha kimataifa na kumpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Mha. Gissima Nyamo-Hanga kwa usimamizi na jitihada zake katika kusimamia miradi mbalimbali ya umeme.

Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere umegharimu zaidi ya Shilingi Trilioni 6.5 ambapo mpaka sasa serikali imeshalipa zaidi ya asilimia 99.5.

05/04/2025

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Jengo la Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahak**a pamoja na Nyumba za Makazi ya Majaji Jijini, Dodoma, tarehe 05 Aprili, 2025.

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Jengo la Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahak**a ...
05/04/2025

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Jengo la Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania, Tume ya Utumishi wa Mahak**a pamoja na Nyumba za Makazi ya Majaji Jijini, Dodoma, tarehe 05 Aprili, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Aprili 5, 2025, amezindua rasmi jengo la Makao Makuu ya...
05/04/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Aprili 5, 2025, amezindua rasmi jengo la Makao Makuu ya Mahak**a ya Tanzania jijini Dodoma.

Jengo hilo limeweka rekodi k**a jengo la sita kwa ukubwa duniani miongoni mwa majengo ya Mahak**a na la kwanza barani Afrika.

Jengo hilo lenye ghorofa tisa na ukubwa wa mita za mraba 63,244, limejengwa kwa asilimia 100 kwa fedha za ndani ambapo jumla ya Shilingi bilioni 129.7 zimetumika katika ujenzi wake.

Mbali na jengo hilo kuu, Rais Samia pia amezindua miradi mingine miwili ya Mahak**a ikiwemo jengo la utumishi wa Mahak**a pamoja na nyumba 48 za makazi ya majaji – hatua inayolenga kuboresha ustawi wa watumishi wa chombo hicho cha haki.

Jengo hilo la Makao Makuu ya Mahak**a linajumuisha matawi matatu makuu ya Mahak**a nchini – Mahak**a ya Upeo, Mahak**a ya Rufani na Mahak**a Kuu – huku ofisi za utawala zikiwa zimejengwa katikati ya muundo huo wa kisasa.

Katika kuendana na mageuzi ya kiteknolojia, jengo hilo lina mifumo ya kisasa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) inayojumuisha matumizi ya akili unde (AI), maroboti ya kuwaongoza wageni, pamoja na eneo maalum la kutua helikopta, likiwa limetengenezwa kwa kudumu kwa zaidi ya miaka 100.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry Silaa Jerry William Silaa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya...
03/04/2025

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Jerry Silaa Jerry William Silaa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA, Bw. Kundwe Moses Mwasaga, leo Aprili 03, 2025 wameshiriki katika kikao cha mawaziri kuhusu matumizi ya Akili Unde ambacho kimefanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kigali jijini Kigali, nchini Rwanda.

Kikao hicho kimeratibiwa na Taasisi ya Tony Blair (Tony Blair Institute for Global Change - TBI) ambacho kimejikita katika kubainishi namna Akili Unde inavyoweza kutumika na inavyotumika katika maeneo mbalimbali na kuleta ufanisi katika Sekta ya Umma barani Afrika.

Kikao hicho ni sehemu ya Mkutano wa Kimataifa wa Akili Unde Barani Afrika unaondelea nchini Rwanda kuanzia Aprili 3-4, 2025.

Mtendaji Mkuu wa Mahak**a, Profesa Elisante Ole, anaongea na waandishi wa habari leo, tarehe 3 Aprili 2025, jijini Dodom...
03/04/2025

Mtendaji Mkuu wa Mahak**a, Profesa Elisante Ole, anaongea na waandishi wa habari leo, tarehe 3 Aprili 2025, jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa majengo mapya ya Mahak**a.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi, tarehe 5 Aprili 2025, na Mgeni Rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tufuatilie Mubashara kupitia Youtube channel yetu https://youtube.com/live/upoVsmHVfgw?feature=share

Mtendaji Mkuu wa Mahak**a, Profesa Elisante Ole Gabriel, anaongea na waandishi wa habari leo, tarehe 3 Aprili 2025, jiji...
02/04/2025

Mtendaji Mkuu wa Mahak**a, Profesa Elisante Ole Gabriel, anaongea na waandishi wa habari leo, tarehe 3 Aprili 2025, jijini Dodoma kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa majengo mapya ya Mahak**a.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi, tarehe 5 Aprili 2025, na Mgeni Rasmi atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Follow Our Channels:youtube.com/ | x.com/numerictz  |  Instagram.com/numericpress  | facebook.com/numericDigital
26/03/2025

Follow Our Channels:
youtube.com/ | x.com/numerictz | Instagram.com/numericpress | facebook.com/numericDigital

You can also follow on Instagram to see more.
26/03/2025

You can also follow on Instagram to see more.

Address

Dar Es Salaam
0255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Numeric Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Numeric Digital:

Share