Sikio la Jamii

Sikio la Jamii Uwanja rasmi wa habari mbalimbali za Kijamii,Uchumi &Biashara, Siasa na Burudani tembelea Ukarasa huu au Bog yetu.

16/11/2019
UTEUZI
12/09/2019

UTEUZI

11/09/2019
22/07/2019

Rais Magufuli Atoa Agizo Kero Ucheleweshaji Vibali NEMC Itatuliwe
Na: Frank Shija – MAELEZO
JPM: Rais John Pombe Magufuli metoa agizo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Goerge Simbachawene kushughulikia kero ya ucheleweshwaji wa vibali kwa wawekezaji ili kuendana na kasi ya uchumi wa viwanda.
Amelitaka Baraza la la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), kutochelewesha utoaji wa vibali kwa wawekezaji ili kuongeza ufanisi katika ukuaji wa uchumi wa viwanda.
“Pasiwe na ucheleweshwaji wa vibali vya NEMC kwa viwanda vyetu, sisi tunataka kuwa na viwanda vya kutosha na wawekezaji wasiwekewe vikwazo kwa visingizio vya NEMC, vibali hivi vitoke kwa sababu tunahitaji viwanda, ikiwezekana wawekeze kwanza vibali vya NEMC vitafuata baadae,”alisema Dkt. Magufuli.
Rais Magufuli amemtaka Simbachawene kusimamia kwa karibu suala hilo la ucheleweshwaji wa vibali vya Tathmini ya uharibifu wa Athari ya Mazingira vinavyotolewa na NEMC.
Rais Magufuli ameongeza kuwa fedha nyingi zinatolewa na wafadhili kwa ajili ya miradi ya mazingira lakini kumekuwa hakuna matokeo ya kuridhisha hivyo ametaka kuwepo usimamizi madhubuti wa rasilimali fedha inayoelekezwa katika miradi ya mazingira.
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amempongeza Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed Bashe kwa uchambuzi mzuri wa masuala ya kilimo aliokuwa anaufanya akiwa bungeni na kuongeza kuwa hiyo ndiyo sababu ameamua kumteua ili akayatekeleze kwa vitendo kwa ajili ya kukwamua kilimo.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), George Boniphace Simbachawene amesema kuwa shughuli zote za kiuchumi zinategemea sana mazingira hivyo atashirikiana na wataalamu wa wa ofisi yake kumshauri vyema Makamu wa Rais katika namna bora ya kutatua changamoto zitokanazo na uharibifu wa mazingira.
Ameongeza kuwa fedha zinazotajwa kuingia katika nchi kwa ajili ya mazingira ni nyingi lakini zimekuwa zinatumika zaidi katika masuala ya kiutawala badala ya kuelekezwa katika miradi ya kukabiliana na uharibifu wa mazingira.
“Nataka nikuhakikishie Mhe. Rais kuwa nitamsaidia Makamu wa Rais katika Ofisi yake, kwanza natambua lakini pili mimi kwa kushirikiana na wenzangu nitakaowakuta pamoja na walaalamu nitajitahidi kutoa mawazo yangu ili tuone ni namna gani tunaokoa mazingira,” alisema Simbachawene.
Akizungumzia masuala ya Muungano, Waziri Simbachawene amesema kuwa anafahamu kuwa msingi wa Muungano wetu siyo tu yaliyoandikwa katika Katiba na kufafanuliwa katika sheria bali ni wa kihistoria ambao unajengeka katika maelewano zaidi badala ya maandishi.
Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Mohamed Bashe amesema kuwa anafahamu changamoto zinazowakabili wakulima wa nchi hii hasa ukizingatia kuwa ndiyo sekta inayowagusa asilimia kati ya 60-70 ya watanzania wote, wengi wao ndiyo wanyonge ambao Rais Magufuli ndiye mtetezi wao.
Amesema kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kwa mamlaka atakayopewa kuhakikisha anamsaidia Mhe. Rais katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ili kukwamua sekta ya Kilimo nchini.
Hafla hii ya uapisho imefanyika kufuatia Mhe. Rais kufanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri kwa kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Januari Makamba na nafasi yake kuchukuliwa na Waziri George Simbachawene, huku Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Mhe. Innocent Bashungwa ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara..
Mwisho.

25/06/2019

LIVE: RAIS MAGUFULI AKIZINDUA GHALA NA MITAMBO YA KUCHAKATA GESI KIGAMBONI

Rais Magufuli Amfuta Machozi Mfanyabiashara Aliyezuiliwa Bidhaa Zake Tangu 2015• Aiagiza TRA kumlipa Fidia• Maofisa Wali...
07/06/2019

Rais Magufuli Amfuta Machozi Mfanyabiashara Aliyezuiliwa Bidhaa Zake Tangu 2015
• Aiagiza TRA kumlipa Fidia
• Maofisa Walihusika TRA Kuk**atwa, Kufunguliwa Mashtaka

Na Mwandishi Wetu-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kumlipa fidia mfanyabiashara ambaye bidhaa zake zilishikiliwa na Mamlaka hiyo tangu mwaka 2015 kinyume na taratibu.
Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo Juni 7, 2019 wakati akiongea na wafanyabiashara kutoka wilaya zote za Tanzania kwa lengo la kuangalia changamoto na fursa zilizopo katika kufanya biashara nchini.
Ametoa maagizo hayo baada ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa kuelezea namna alivyoingilia kati suala la mfanyabiashara huyo wa Kariakoo (jina lake halikujulikana mara moja) kurejeshewa bidhaa zake zilizokuwa zimezuiliwa baada ya mfanyabiashara huyo kukataa kutoa rushwa kwa Maafisa watatu wa TRA.
“Hao watatu wote Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU kawashike na uwaweke ndani halafu wapelekwe Mahak**ani, wakiwa Mahak**ani Kamishna Mkuu wa TRA uwe umewasimamisha kazi, lakini TRA mkapige hesabu ile biashara yake imekaa kwa miaka mitatu mkamlipe fidia,” Rais Magufuli alitoa maagizo.
Aidha, Rais amewataka wafanyabiashara kuiga mfano wa mfanyabiashara mwenzao aliyekataa kutoa rushwa na kuwaomba watoe ushirikiano katika kulipa kodi na pia Mamlaka ya Mapato kutomuonea mfanyabiashara katika kumkadiria kodi.
Waziri Mkuu alikuwa akielezea malalamiko aliyopata kutoka kwa wafanyabiashara hususani kodi kubwa na rushwa ambapo baadhi ya maofisa wamekuwa wakitumia vibaya majina ya viongozi kwa kusingizia kuwa ni maagizo kutoka juu.
Mheshimiwa Kassim Majaliwa alieleza kwamba aligundua matatizo hayo baada ya kutembelea eneo la biashara la Kariakoo jijini Dar es Salaam na kugundua mfanyabishara mmoja aliingia na bidhaa kutoka Zambia na kuwa na vibali vyote lakini alipofika Kimara alizuiliwa na kuomba rushwa lakini Mfanyabiashara huyo alikataa kutoa rushwa na TRA wakachukua bidhaa zake kupeleka bohari.
Kwa upande wake Waziri Mkuu amewataka wafanyabishara kuendelea kuwa na imani na Serikali ina haki na wajibu wa kuwalinda wafanyabishara kwa namna yeyote ile na ndio maana Serikali inachukua hatua mbalimbali ili kuweka mazingira bora kwa wafanyabishara.
Mheshimiwa Majaliwa alisema kuwa Serikali itahakikisha inajenga mazingira wezeshi nchini na pia itaimarisha biashara za mipakani na pia eneo la Kariakoo ambalo ndio soko kubwa ambapo wafanyabishara kutoka Malawi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekuwa wakichukua bidhaa Kariakoo.
Mkutano wa Rais na wafanyabiashara kutoka wilaya zote mchini uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam pia ulihudhuriwa na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi, Mawaziri, Makatibu Wakuu na baadhi ya Wakuu wa taasisi za Serikali na sekta binafsi.
-MWISHO-

16/05/2019

Kakunda Akanusha Profesa Kabudi Kuhusika na Mkataba wa Kampuni ya Indo Power Solution
Na: Mwandishi Wetu.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Joseph Kakunda amekanusha shutuma zilizotolewa kuhusu ushiriki wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania katika mchakato wa kumpata mzabuni wa ununuzi wa Korosho ambaye ni Kampuni ya Indo Power Solution ya nchini Kenya.
Waziri Kakunda amesema kuwa anashanga kuona Profesa Kabudi anatupiwa lawama kuwa ameingiza Serikali mkenge jambo ambalo si kweli kwani wahusika wakuu ni timu ya wataalam kutoa Ofisi ya Wizara ya Viwanda na Biashara na kwamba upatikanaji wa zabuni hiyo ulipitia mchakato yote halali kilichotoke ni Serikali kuvunja mkataba baada ya mzabuni kutotimiza masharti yaliyomtaka kulipa ndani ya siku 10 na hata alipoongezewa muda haikutimiza.
“Kumuweka mtu ambaye hana makosa yeyote kwenye suala hili na bahati mbaya sana maagazeti karibu yote yakawa yanaandika yakimlaumu kushauri vibaya Serikalijambo ambalo halina ukweli wowote, Kabudi ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria alikuwa mualikwa tu wa kushuhudia hafla ya utiwaji saini mkataba wa Makubaliano baina ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Kampuni ya Indo Power Solution,” Alisema Waziri Kakunda.
Kakunda alisema kuwa ni ajabu kwa kumlaumu mtu aliyealikwa na kuongeza kuwa timu ya wataalam iliyohusika inaongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa anayeshughulikia Viwanda hivyo kumuhusisha Profesa Kabudi ni jambo hili si sawa ni bora hata wangemuhusisha yeye kwa kuwa ndiye Waziri mwenye dhamana na Biashara.
Aidha Waziri Kakunda amesema kuwa ni vyema Watanzania wakaelewa na kutokubali kupotoshwa juu ya hatua iliyochukuliwa na Serikali kuvunja mkataba na Kampuni ya Indo Power Solution ya nchini Kenya iliyokuwa imepewa zabuni ya kununua Korosho tani 100 kwa kutofuata masharti ya mkataba.
Alisema kuwa mchakato wa Kuipatia zabuni Kampuni hiyo ulipitia njia mbalimbali zilizohusisha wataalam kutoka pande mbili na kujiridhisha kuwa Kampuni hiyo inavigezo vyote vya vya kupewa zabuni hiyo ya kununua Korosho nchini na kuongeza kuwa pamoja na kuwa imeshindwa kutimiza masharti ya mkataba uliopelekea Serikali kusitisha mkabata bado inabaki kuwa ni Kampuni halali.
Waziri Kakunda ametoa ufafanuzi huu kufuatia kauli iliyotolewa Bungeni jana na Mbunge wa Moshi Vijijini, Anthony Komu akimtuhumu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashari, Profesa Paramagamba Kabudi kuitia hasara Serikali kwa kumuhusisha na mkabata wa makubaliano ya ununuzi wa Korosho tani 100 na kampuni ya Indo Power Solution ya nchini Kenya ambayo baadae Serikali iliamua kusitisha mkataba wake baada ya Kampuni hiyo kutofuata masharti.
Mwisho.

13/05/2019
11/05/2019

Serikali Yasisitiza Marufuku ya Matumizi ya Mifuko ya Plastiki Ifikapo Juni Mosi
Na: Mwandishi Wetu, DODOMA.
Serikali yasisitiza marukufu ya matumizi ya mifuko ya plastiki ifikapo tarehe 1 Juni 2019 ipo palepale tofauti na inavyopotoshwa na baadhi ya watu wenye nia hovu ya kuleta mkanganyiko miongoni mwa jamii.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Balozi Joseph Sokoine alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari leo jijini Dodoma.
Alisema kuwa katazo hilo la kupiga marufuku mifuko ya plastiki ya aina zote lilitolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akihitimisha Hotuba yake ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
“Mtakumbuka kuwa tarehe 9 Aprili 2019 Serikali ilitoa Tamko la kusitisha matumizi ya Mifuko ya plastiki hapa nchini ifikapo Juni Mosi 2019, katazo hili linalenga kuepusha athari za kiafaya na mazingira zinazoendelea kujitokeza kutokana na matumizi ya mifuko hiyo” alisema Balozi Sokoine.
Balozi Sokoine amesema kuwa wananchi wanapaswa kuunga mkono jitihada hizo na si kubeza na kupotosha k**a ambavyo imetokea hivi karibuni kwa mtu kutumia video clip kwa kuisambaza mitandaoni kwa lengo la kupotosha umma.
“Nitumie fursa hii kuwakumbusha wananchi wote kuwa ifikapo tarehe 1 Juni 2019, Serikali itaendesha operesheni kabambe nchi nzima ya kusaka mifuko hii, ambayo itahusisha wadau mbalimbali vikiwemo Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Kamati za Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya, Mamlaka za Serikali za Mitaa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, TBS, TFDA, Ofisi ya Mashtaka, pamoja na Mamlaka za Viwanja vya Ndege,Bandari, Forodha, Uhmiaji, na Usafiri wa Nchi Kavu,”
Aliongeza kuwa katika kufanikisha zoezi hilo Serikali imeshafanya maandalizi mbalimbali ikiwemo kutunga kanuni zitakazo anza kutumika kuanzia tarehe 1 Juni, 2019 hivyo ametoa rai kwa watanzania wote kuzingatia maelekezo ya Serikali pamoja na matakwa ya Kanuni za kupiga marufuku matumizi na biashara ya mifuko ya plastiki nchini kwa mustakabali wa uhifadhi wa mazingira ya nchi yetu.
Mwisho.

05/04/2019

YALIYOJIRI BUNGENI LEO TAREHE 05/04/2019 WAKATI WA KIPINDI CHA MASWALI NA MAJIBU.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile.

ujumla sheria zilizopo zinajitosheleza kabisa kuwashughulikia wale wote wanao kutwa na hatia katika makosa ya ubakaji, kunajisi watoto wa kiume na wa k**e.

ya Makosa ya Jinai ya mwaka 1985 k**a ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, imeelekeza adhabu kali kwa yeyote atakayebainika kutenda kosa la kumdhalilisha mtoto au kumbaka mtoto ikiwemo kifungo cha miaka 30.

hivyo, imekuwa vigumu kuwatia hatiani wakosaji hasa wa ndani ya familia kwa kukosekana kwa ushahidi.

wao wanaogopa kutoa ushahidi kutokana na hofu ya kupoteza mmoja ya wanafamilia kutokana na adhabu ya kifungo cha maisha.

inajitahidi kuweka mikakati ya kusaidia kupunguza au kumaliza kabisa tatizo hili, lakini bila ushirikiano katika ngazi zote za familia, haitokuwa rahisi.

inatoa rai kwa jamii kutomaliza masuala ya kijinsia ndani ya familia na badala yake ushirikiane na Serikali ili Sheria ichukue mkondo wake.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Joseph Kakunda.

imeweka vipaumbele vitatu ambavyo, ndivyo tunavyoviwekea msisitizo wa uwekezaji kwenye Sekta ya Viwanda.

hivyo ni viwanda vya kusindika mazao ya kilimo ili kuongeza thamani sambamba na kulinda jasho la mkulima.

vya kutengeneza bidhaa za majumbani k**a vyakula, nguo, samani na bidhaa tegemezi kwenye sekta ya ujenzi k**a sementi na mabati ili kuharakisha ubora wa maisha na maendeleo.

cha tatu ni viwanda vinavyoajiri watu wengi kwa ajili ya kuhakikisha ajira kwa vijana.

la Muhogo ambalo ni maarufu kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi, Mtwara na Kigoma kwa sasa limepewa kipaumbele maalum Duniani.

na ukweli kwamba muhogo hausindikwi kutengeneza unga wa ugali, uji, biskuti au mkate peke yake bali unga wa Muhogo unatumika sana kwa sasa kwenye uunganishaji wa chuma, mbao, kutengeneza gundi na matumizi mengine mengi.

la muhogo Ulaya, Marekani na China ni kubwa sana kwa sasa. China peke yake inahitaji tani milioni mbili na nusu za muhogo kwa mwaka.

na ukweli huo, kasi ya ujenzi wa viwanda vya kusindikika muhogo ni kubwa, mwaka huu peke yake ukiacha viwanda Vitano vinavyonunua muhogo wa mkulima kwa sasa, viwanda vipya Viwili vitakuwa vimefunguliwa kabla ya Juni, 2019 kimoja Lindi na kingine Pwani.

Imeandaliwa na Idara ya Habari - MAELEZO.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sikio la Jamii posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sikio la Jamii:

Share