Tanzania mpya

Tanzania mpya Habari za uchunguzi, siasa, jamii, burudani na michezo

09/03/2025
11/12/2024

Naomba msikielewe kichwa cha habari vibaya maana yake ni kwamba wachezaji wengi walioonekana kushindwa Simba wamesaini Jangwani.

Nani anafuata?.

Kutangaza kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kukupa matokeo mazuri kukuza na kuboresha biashara yako, k**a utaelewa viz...
27/05/2024

Kutangaza kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kukupa matokeo mazuri kukuza na kuboresha biashara yako, k**a utaelewa vizuri jinsi ya kutangaza kwenye mitandao hiyo, iii kuweza kupata matokeo mazuri.

Baadhi ya watu wamekuwa wakitangaza kwenye mitandao ya Facebook na Instagram, kwa ku-post picha kutegemea kupata wateja wengi, matokeo yake wengi wao wanaambulia patupu watu huishia ku-like na ku-comment bila kununua bidhaa au huduma wanazotoa.

Kuna sababu nyingi sana zinazochangia kushindwa kupata matokeo mazuri unapotangaza kwenye mitandao ya kijamii,

Lakini moja ya sababu kubwa ni kutangaza bidhaa au huduma badala ya kutangaza suluhisho la changamoto za walengwa wako.

Kadilo Online tumekuandalia mafunzo ya bure kabisa ya jinsi ya kuuza bidhaa au huduma mtandaoni na kufanya matangazo facebook na instagram kupata wateja wengi.

Kupata mafunzo hayo bure bofya link ya group letu la whatsapp hapo chini au tuma ujumbe kwa namba ya whatsapp ifuatayo kujiunga bure kabisa.

Ni mimi ninayejali mafanikio yako
Mkurugenzi Kadilo Online
0713685823
https://chat.whatsapp.com/IWYo4wsIxi52UmbFCkb3pz

K**a wewe ni mwanamke, dada, binti unayekwenda na wakati, unayesuka mitindo ya nywele ya kisasa k**a Notlea na Yebo yebo...
21/05/2024

K**a wewe ni mwanamke, dada, binti unayekwenda na wakati, unayesuka mitindo ya nywele ya kisasa k**a Notlea na Yebo yebo au unatamani kusuka mitindo mipya ya kisasa,
Basi soma kwa makini ujumbe huu mpaka mwisho unaweza kuwa suluhisho la kile unachotamani k**a mwanamke,
Shamyney Beauty Salon ni wataalam wa kusuka nywele mitindo ya aina yote
Wanakusaidia kujua bure kabisa jinsi ya kutambua siri iliyojificha ya kusuka mitindo mipya ya kisasa, kujua zaidi tuma ujumbe kwenye namba ya whatsapp ifutatayo au bofya link hapo chini kujinga na group la whatsapp kujifunza zaidi.
Fanya hivyo mara moja kabla group halijaa
Shamyney Beauty Salon
Wataalam wa urembo na ususi
0786801047
https://chat.whatsapp.com/JhUnGaJzhYb5GxMtyVeKSO

K**a wewe ni mjasiliamali unahangaika kutangaza biashara yako mtandaoni, unatamani kupata wateja wengi, unatumia gharama...
19/05/2024

K**a wewe ni mjasiliamali unahangaika kutangaza biashara yako mtandaoni, unatamani kupata wateja wengi, unatumia gharama kubwa kutangaza facebook na Instagram lakini hupati matokeo mazuri, unatamani kufanya matangazo Facebook na Instagram lakini huna akaunti za mitandao ya kijamii.

K**a majibu ya maswali hayo ni ndio
Basi soma ujumbe huu kwa makini mpaka mwisho pengine hujawahi kusikia na unaweza kuwa ndio suluhisho la changamoto zako zote. ulizonazo kwa sasa kupata wateja mtandaoni

Kadilo online tunakusaidia kutangaza biashara yako facebook na instagram bila kuwa na akaunti, tunakupa garantii ya kupata wateja mtandaoni kutangaza facebook na Instagram .

Kujua zaidi nimekuandalia mafunzo ya bure kabisa ya jinsi ya kutangza bidhaa mtandaoni, jinsi ya kutangaza Facebook na Instagram kwa gharama nafuu na kupata matokeo mazuri.

Kupata mafunzo hayo bure kabisa kupitia group la Whatsapp tuma ujumbe au bofya link hapo chini kujiunga na group na kufurahia mafunzo hayo
Tuma ujumbe saaa hivi kabla group halijaa
Ni mimi ninayejali mafanikio yako
Kadilo online
Mkurugenzi
0713685823
https://chat.whatsapp.com/HjT12yHXoiPCULzB8K2Smz

Jerry William Silaa alizaliwa Februari 9, mwaka 1982, akipata bahati ya kuzaliwa katika familia ya rubani wa ndege 'Capt...
18/05/2024

Jerry William Silaa alizaliwa Februari 9, mwaka 1982, akipata bahati ya kuzaliwa katika familia ya rubani wa ndege 'Captain' Wiliam Slaa, aliyefariki kwenye ajali ya ndege iliyochukua pia uhai wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratius Filikunjombe.

Mhe. Slaa ni mwanasiasa, ambaye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, alimteua Agosti 30, na kuapishwa Septemba Mosi mwaka jana kuwa Waziri wa Aridhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Baada ya siku 100 za utendaji wake kwenye wizara hiyo Mhe. Slaa, alifanya kikao na Makamishina wa Ardhi Wasaidizi mikoa yote Tanzania Bara kutathmini siku 100 za uongozi wake tangu ameanza kuiongoza wizara hiyo.

Siku 100 za utendaji kazi wa Mhe.Jerry Slaa alifanya tathimini kutengeneza mpango wa kutekeleza maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutatua matatizo ya migogoro ya ardhi na kuwahudumia wananchi wa taifa hili.

Ndani ya utendaji wake akiwa Waziri wa ardhi Mhe. Slaa ameweza kufanya mambo makubwa ambayo yalihitaji ujasiri mkubwa, ambayo hayakuweza kufanywa kwa miaka mingi ikiwepo mpango wake wa kuanzisha kile alichokiita kliniki ya changamoto za ardhi.

Katika kile kinachoelezwa kuwa Mhe.Slaa ameweza na atakuwa msaada na mtaji mkubwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuonesha kuwa kiongozi anayesimamia ipasavyo haki na sera za chama chake na maagizo ya Mhe. Rais Samia.

Mhe. Slaa akionesha kuwa yuko katika kutetea maslahi na haki za wananchi wangonge wa taifa hili, alikataa kujiita kuwa yeye ni mtoto wa maskini ili kuwaziba midomo wale mafisadi wanaohisi kuwa wanaweza kutumia mwanya huu kumuhongo ili apindishe haki.

Mhe. Slaa ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga, hivi karibuni, alikataa rushwa ya Tsh milioni 300 kutoka kwa tajiri mmoja aliyejenga kituo cha Mafuta Kinyume cha utaratibu pale Mikocheni.

Mhe. Slaa alidhihirisha ukomavu na utendaji wenye ujasili baada ya kuchukua maamuzi magumu ya kusimamia nyumba ya ghorofa moja iliyokuwa kwenye eneo la kiwanja no. 484 Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Slaa alisimamia zoezi la ubomoaji wa nyumba hiyo, inayodaiwa mmiliki wake hakuwa na nyaraka za umiliki wa eneo hilo na pia hakua na kibali cha kujenga hapo na kwamba alivamia eneo hilo ambalo linamilikiwa na Bi. Naomi Raymond ambaye anadaiwa kulipigania eneo hilo kwa takribani miaka 20 sasa.

Sakata la mgogoro huo limedumu kwa takribani miaka 20, ambapo limepita katika ngazi mbalimbali za Serikali na Mahak**a na hatimaye kutolewa uamuzi na waziri Jerry Slaa kwa muda mfupi wa uongozi wake kwenye wizara hiyo.

Kabla ya kuanza majukumu yake ya kazi katika wizara hiyo Mhe. Jerry Slaa alitaka ushirikiano kutoka kwa watumishi wa wizara hiyo kwa kuweka vipambele vyake vikiwemo kutekeleza maagizo ya Rais Samia kuhusu kuondoa changamoto za ardhi nchini.

Katika kuendeleza utendaji wenye kasi kutatua changamoto za ardhi, Mhe. Slaa aliwahi kutoa siku saba kupatikana suluhu ya changamoto za urasimishaji makazi holela wa makazi katika mkoa wa Dar es Salaam.

Agizo la Waziri Slaa lilfuatia kwa mkoa wa Dar es Salaam kuwa moja ya mikoa yenye malalamiko mengi ya urasimishaji makazi holela zoezi ambalo lilianza mwaka jana na kutarajiwa kukamilika mwaka huo.

Mhe. Slaa alitoa tamko hilo Oktoba 4, mwaka jana
alipokutana na uongozi wa mkoa wa Dar es Salaam na watendaji wa sekta ya ardhi kujadili utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa upande wa sekta ya ardhi.

Pamoja na hatua iliyokuwa imefikiwa kwenye urasimishaji, utekelezaji wa programu ya urasimishaji wa ardhi mkoa wa Dar es Salaa, Slaa aliziona changamoto mbalimbali ikiwemo makampuni yaliyopewa kazi hiyo kushindwa kukamilisha kwa wakati huku wananchi wakikosa imani kwa makampuni na kuacha kuhangia gharama za utekelezaji kazi hiyo na kusababisha zoezi hilo kukwama katika maeneo mengi.

Kwa mujibu wa Waziri Silaa, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amemteua na kumuamini afanye kazi ya ardhi na yeye ameamua kufanya hivyo ili kupunguza k**a siyo kuondoa kabisa kero za ardhi nchini.

Tunamuomba Mungu ampe afya njema waziri Slaa ili aweze kuendelea na kasi ya utendaji ambayo watanzania wanahitaji kuondokana na kero nyingi zilizoko kwenye sekta ya ardhi.

Kupata taarifa za uchunguzi, uchambuzi, siasa, uchumi, jamii, utamaduni na michezo bofya link hapo chini

https://www.tanzaniampya.co.tz/

K**a wewe ni mfanyakazi, mfanyabiashara, mtumishi wa umma, kijana au mtu yeyote unayemiliki mbwa nyumbani kwako.Unataman...
14/05/2024

K**a wewe ni mfanyakazi, mfanyabiashara, mtumishi wa umma, kijana au mtu yeyote unayemiliki mbwa nyumbani kwako.

Unatamani kuwa na mbwa mkali, anayetii amri, a guard dog mbwa mlinzi mwenye mafunzo basi soma ujumbe huu mpaka mwisho huenda ukawa ni suluhisho la kile unachotamani ambacho hujawahi kusikia.

Muddy Madog, Dog trainer anakusaidia kufundisha mbwa, anayekusaida kutambua tatizo la tabia ya mbwa wako, anayekufundisha njia za kufundisha mbwa wako, kutengeneza mazingira mazuri ya kumfundisha mbwa wako.

Muddy Madogo anakusaidia bure kabisa kumpa mbwa wako chanjo za minyoo, vitamini na mkanda kwa ajili ya mbwa wako bure kabisa.

Kujua zaidi tuma ujumbe kwa namba ya whatsapp ifuatayo au piga simu atakushauri bure kabisa jinsi ya kumfanya mbwa wako kuwa mkali na obidience kutii amri.

Muddy Madog Trainer
0715911169

NA MWANDISHI WETUMfanyabiashara maarufu wa vitenge maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam, amekuwa akifanya biashara bi...
11/05/2024

NA MWANDISHI WETU

Mfanyabiashara maarufu wa vitenge maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam, amekuwa akifanya biashara bila kulipa kodi kwa kuwa analindwa na aliyekuwa Kamishina wa kodi Mamlaka ya Mapato Nchini TRA ambaye ana mahusiano naye ya kimapenzi.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa Tanzania Mpya, hivi karibuni mfanyabishara huyo alik**atwa na maafisa wa TRA, maeneo ya Sokota Temeke jijini Dar es Salaam kwenye ghala (Godown) na mzigo wa vitenge na bidhaa zingine ambazo ziliingizwa kimagendo.

Godown hili ambalo lilikuwa halina leseni mzigo ulik**atwa na Maafisa TRA, akidaiwa kuingiza vitenge kwa magendo na kukwepesha kulipa kodi, lakini maafisa wa TRA hawakuweza kumchukulia hatua zozote.

Habari zinadaiwa kuwa mfanyabishara huyo kwa kuwa amekuwa akikingiwa kifua na kamishina wa kodi, maafisa waliohusika kuk**ata mzigo huo maeneo ya Sokota walihamishwa vitengo vya kazi.

Mfanyabiashara huyo ambaye anaingiza bidhaa kutoka nje na kukwepesha kulipa kodi, amekuwa na mahusiano na kamishina wa TRA kwa muda mrefu ambaye amekuwa akimsaidia kukwepesha kulipa mabilioni ya kodi za serikali.

Baadhi ya Maafisa wa TRA ambao hawakupenda kutaja majina yao, wameliambia gazeti hili kuwa wanapofika kufanya ukaguzi kwa mfanyabiashara huyo hushindwa kufanya hivyo kutokana na Kamishina huyo kumkingia kifua mfanyabiashara huyo.

Gazeti hili linaendelea kufanya uchunguzi zaidi kwa kina kuhusu taarifa hii kabla ya kuweka hadharani majini ya kamishina huyo na mfanyabishara huyo.

Kupata taarifa za uchunguzi, uchambuzi, siasa, utamaduni na michezo bofya link hapo chini

https://www.tanzaniampya.co.tz/kigogo-tra-amkingia-kifua-hawara-kukwepa-kodi/

NA MWANDISHI WETUMfanyabiashara maarufu ambaye ni miongoni mwa wakurugenzi wa kampuni ya GSM, jijini Dar es Salaam, kati...
09/05/2024

NA MWANDISHI WETU

Mfanyabiashara maarufu ambaye ni miongoni mwa wakurugenzi wa kampuni ya GSM, jijini Dar es Salaam, katika hali ya kushangaza anatumia gari ya kisasa aina ya Land Cruiser SAHARA yenye namba za usajili wa miradi ya serikali.

Mfanyabiashara huyo maarufu kwa jina la Salaah Mohamed, anatumia gari namba za usajili DFPA 3794 ambazo zinapaswa kutumiwa na watumishi kwenye miradi ya serikali.

Hata uchunguzi wa Tanzania umebaini kuwa namba hasomeki kwenye usajili wa namba za miradi ya serikali.

Wachambuzi wa mambo wanasema hiyo ni k**a kuidharau serikali kwa mtu binafsi kutumia gari zenye namba ya serikali.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambaye alitaka kuthibitisha uhalali wa mfanyabishara kutumia magari ya serikali, Salaah alisema kwa jeuri kuwa hawezi kuzungumza na mwandishi wa habari kwa kuwa ni raia wa kawaida.

“Ungenionesha kitambulisho k**a wewe ni askari polisi, au usalama wa taifa TICS au Mkurugenzi wa makosa ya jinai, Ramadhani Kingai ningeweza kukujibu, lakini wewe ni raia tu k**a mimi” alisema.

Alisema kuwa anangekuwa anafanya makosa angekuwa ameshak**atwa kwa kuwa viongozi wanaiona inatembea kila siku.

Kwa mujibu wa maafisa wa TRA ambao hawakupendwa kutaja majina yao walisema gari hiyo namba hizo hazisomeke kwenye mfumo wa usajili wa magari TRA.

Walisema kuwa inawezekana gari hiyo ikawa imesajiliwa kwa namba zingine lakini amezitoa na kuweka namba za serikali, kwa sababu anazozijua yeye.

Mwezi uliopita zilik**atwa gari za wafanyabiashara aina ya Land Cruiser zikiwa zimepachikwa na za serikali zikiwa zimepakia wahamiaji haramu wa kutoka Ethiopi wakiwa wanasafirishwa kwenda nje

Kupata taarifa k**a hizi za uchunguzi uchambuzi siasa na kijamii utamaduni na michezo bofya link hapo chini

https://www.tanzaniampya.co.tz/mabilionea-wa-gsm-waanza-kuidharau-serikari-ya-mama-samia/

07/05/2024

NA MWANDISHI WETU

Mtumishi wa Wakala wa Barabara Nchini, TANROAD, Injiania wa Mkoani Lindi (jina tunalihifadhi) anadaiwa kumiliki mali za kutisha, Tanzania Mpya limebaini.

Mfanyakazi huyo ambaye anamiliki majumba mengi ya ghorofa moja ya kupangisha jijini Dar es Salaa, anadaiwa utajiri huu ameupata kwa muda mfupi na haufahamiki kwenye Tume ya Maadili ya Watumishi wa Umma.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa Tanzania Mpya injinia huyo anamiliki majumba zaidi 16 kwenye uzio mmoja huko maeneo ya Madale na njia panda ya Goba na majengo mengi uwanja wa Nike.

Hata hivyo, anadaiwa kumiliki baa kubwa ya kisasa mkoa wa Lindi mali ambazo haziendani na kipato chake halisi.

Taarifa zinadai kuwa injinia huyo ambaye ni kiongozi wa TANROAD mkoa wa Lindi anafanya biashara ya kupangisha nyumba bila kulipa kodi ya mapato na kuwa na leseni ya biashara ya kupangisha majengo (Real Estate Business)

Akizungumza na Tanzania mpya kwa njia ya simu kutoka Lindi kiongozi huyo alikanusha kuwa hamiliki majumba hayo, lakini alikiri kuwa anayatambua na kuwa anamsimamia mali za mtu mwingine ndio mwenye miradi hiyo.

Alipoulizwa kuwa k**a utajiri huo Tume ya Madili ya Watumishi wa Umma 'ame-declare' na k**a wanafahamu alishindwa kuthibitisha.

"Mimi sikufahamu nashindwa kueleza lolote kwa sababu sikujui ni vyema tukakuana tukafahamiana na shindwa kuzungumza lolote kwenye simu k**a unaweza kuja huku au usubiri mwisho wa mwenzi ntakuja Dar es Salaam" alisema injinia huyo.

Hata hivyo baada ya mwisho wa mwezi Injiania huyo alitafutwa na mwandishi wa habari hizi hakuweza kupatikana kwa kuwa simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa.

Gazeti hili linaendelea kufuatilia kumtafuta kufutilia umiliki wa nyumba hizo na tutaweka wazi majina ya kiongozi huyo.

kiwanda cha mifuko cha lalamikiwa kutiririsha maji machafu na kuhatarisha afya za watu
07/05/2024

kiwanda cha mifuko cha lalamikiwa kutiririsha maji machafu na kuhatarisha afya za watu

Kiwanda cha kutengeneza mifuko cha lalamikiwa kutiririsha maji taka na mazingira machafu maeneo DAR

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzania mpya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category