Wasafi TV

Wasafi TV Official page For Wasafitv Channel
(11)

08/08/2025

Mfahamu .rsa 🇿🇦 Aliyeshirikishwa na 🦁 Kwenye Wimbo Wa ‘Down’ Akielezea Maana Ya Mistari Yake Aliyoimba Kwa Lugha Ya Kizulu Katika Ngoma Hiyo.

“Lempile esiy’philayo…. (Isikoo)
Masfika Endaweni bathi (Yiboo)
Diamond Bathini ?🤷‍♂️ … bathi … Bathi Yizoo
Get Down Vele Ushayi … Ibiboo” 🎶

Mistari Hii inaeleza hali ya furaha na maisha ya starehe wanayoishi Kwasasa, Na Kila Wanapoingia sehemu K**a Club, watu huwapokea kwa shangwe Yani Furaha Wakisema (“Yiboo”, “Yizoo”), Huku Wakihamasisha watu kucheza kwa Vibe (“Ushayi Ibiboo”).🎶🔥

“Masfika Endaweni Bathi .. Yibo” - Wanapofika Mahali Au Eneo Fulani Wanakaribishwa Kwa Furaha Kwa Kuambiwa ‘Yiboo’.

“Diamond Bathini ?…. Bathi Yizooo”
Bathini? - “Wanasema Nini” ….. Yizoo (Noma San, Hatari …)

INGIA YOUTUBE KATIKA CHANNEL YETU YA ILI KUTAZAMA ZAIDI INTERVIEW HII.

07/08/2025

Zaidi ya wakulima 300 kutoka mkoa wa Morogoro wamenufaika na uwepo wa Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kinanunua miwa yao kwa ajili ya uzalishaji wa sukari yenye ubora wa hali ya juu.

Akizungumza katika Maonesho ya Wakulima (Nane Nane) yanayofanyika kitaifa jijini Dodoma, Afisa Uhusiano wa Kiwanda hicho, Clementina Patrick, amesema lengo la ushiriki wao katika maonesho hayo si tu kutambulisha bidhaa, bali ni kuwa karibu na wananchi kwa kuwapatia sukari bora inayozalishwa kwa kutumia mitambo ya kisasa.

“Uwepo wa kiwanda hiki umeleta mabadiliko makubwa kwa jamii, wakazi wa maeneo ya jirani, hususan wakulima wa miwa wana uhakika wa soko la mazao yao na hivyo kukuza uchumi wao,” amesema Clementina.

Kwa mujibu wa clementina, Kiwanda cha Mkulazi kinatoa sukari yenye ujazo tofauti tofauti kuanzia kilo moja, kilo 25 na hadi kilo 50, ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha wananchi wa kipato cha aina yoyote, wanapata bidhaa hiyo muhimu kwa matumizi ya nyumbani na matumizi mengine.

“Wananchi wanakaribishwa kutembelea banda letu Dodoma na Morogoro, tumeweka bei rafiki kwa kila aina ya kipato kwa lengo la kuhakikisha kila mtu anapata sukari bora ” ameongeza.

06/08/2025
22/07/2025

KAMPUNI ya Selcom kupitia Huduma yake ya kifedha ya kidigitali -Selcom Pesa imezindua kampeni ya Huduma ya Mabando ya Miamala, ijulikanayo k**a "Tumia Bando la miamala, k**a Bure,okoa gharama" ikiwa ni muendelezo wa dhamira yake ya kutoa Huduma za kifedha zenye gharama nafuu kwa watanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa kitengo Cha Masoko wa Selcom Shumbana Walwa amesema kampeni hiyo imekuja baada ya mafanikio ya kampeni ya kwanza ya 5 kwa jero iliyoanzisha ajenda ya upatikanaji wa Huduma nafuu Zaidi kwa Kila Mtanzania

Aidha ameeleza kwamba Mabando ya Miamala ya Selcom pesa ni ya kwanza Tanzania yakilera SULUHISHO jipya linalomwezesha watumiaji kufanya miamala kwa makato madogo kuliko huku wakijipangia matumizi Yao kwa ufanisu bila kutozwa ada ya Kila muamala.

Kampeni hiyo inalenga siyo tu kupunguza gharama kwa watumiaji Bali pia KUWAJENGEA tabia ya kupanga matumizi ya kifedha kwa unafuu Zaidi

20/07/2025

WAZIRI ULEGA ATUMIA SAA MBILI NA MTOTO MWENYE KIPAJI KUTIMIZA NDOTO ZAKE

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, leo ametumia zaidi ya saa mbili kuzungumza na kumtembeza mtoto mwenye kipaji kutoka Dodoma kwenye maeneo aliyotamani kuyaona jijini Dar es Salaam.

Wiki hii, picha mjongeo za mtoto huyo, Ridhiwani Asheri mwenye umri wa miaka 13 zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiionyesha uwezo wake mkubwa wa kubuni ujenzi wa barabara na madaraja akiwa kijijini kwao Kibaigwa, Dodoma.

Baada ya Ulega ambaye ana dhamana ya masuala ya ujenzi nchini kuona picha hizo, aliagiza wataalamu wa wizara yake kwenda kumwona na kuangalia namna ya kumsaidia.

Baada ya kumwona na kuzungumza na familia, waziri aliomba mkutano nao ili kuangalia namna bora ambayo serikali inaweza kufanikisha ndoto zake.

Baada ya mkutano wa jana katika ofisi ndogo za Wizara ya Ujenzi jijini Dar es Salaam, Ulega alisema serikali ya Tanzania ina historia, uwezo na dhamira ya kusaidia watoto wenye uwezo mkubwa kimaarifa kwa maslahi ya taifa.

Baada ya mazungumzo hayo Waziri Ulega ameahidi kumsaidia kijana huyo kuhakikisha anatimiza ndoto zake za kuwa Mhandisi mkubwa hapo baadaye.

Waziri Ulega amesema atakaa na Wizara ya Elimu kuona ni sehemu gani sahihi kijana huyo apelekwe ili kuweza kumsaidia kielimu hasa kwenye maswala ya ujenzi.

Pia Waziri Ulega amemtembeza mtoto huyo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ili aweze kujionea kwa macho yale ambayo alikuwa anayatengeneza akiwa nyumbani kwao kwa kuyaona tu kwenye TV.

Miongoni mwa maeneo hayo ni Daraja la Kijazi lililopo Ubungo, Daraja la Tanzanite na kituo cha Treni ya Mwendokasi (SGR) Posta

20/07/2025

Teknolojia huko Amerika, Ulaya na mataifa makubwa imefikia kiwango cha kutengeneza binadamu halisi kwa kutumia DNA pekee.

TAYARI SIMULIZI HII MPYA IPO YOUTUBE KATIKA CHANNEL YETU YA .

Cc.
Co-Producer
Graphics / VFX
Editor
Videographers &

19/07/2025

USHIRIKA VILLAGE YAWAKARIBISHA WADAU MBALIMBALI WA MAENDELEO, MASHIRIKA YOTE NCHINI NA NJE YA NCHI.
Fursa ya kipekee ya kushiriki kwenye Maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane 2025 imewadia!
Kuanzia tarehe 1 hadi 8 Agosti 2025, Dodoma, Kwenye Viwanja vya 8 8 (Nane Nane) jiunge na Ushirika Village Kupata eneo maalum lenye mabanda 100+ ya maonyesho kutoka kwa:

-Mashirika ya Ushirika na Kilimo
-Wadau wa Masoko na Mitaji
-Sekta ya Mifugo, Lishe, Chakula na Mashine
-Watoa Teknolojia, Ubunifu na Uwekezaji
-Wadau wa Madini,Uvuvi na Saccos
- Wadau wote mnakaribishwa kwenye Ushirika Village.

Onesha bidhaa zako, panua mtandao wa kibiashara, fikia wateja wapya na shiriki midahalo ya kitaalamu.

Nafasi ni chache! Wahi nafasi yako ya kushiriki leo!

Tupigie +255789856246
Barua pepe [email protected]

Ccfederation




19/07/2025

Usiruhusu kabisa Weekend yako kuwa kinyonge, mizigo hii hapa ya kibabe alafu mipyaaaaa. 🎬🍿🔥

Usikose kutazama kila siku ya Jumatatu Alhamisi na Jumamosi saa 07:45 jioni

Cc


13/07/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewahimiza wafanyabiashara wa kimataifa kuwahamasisha wawekezaji wengine kuja kuwekeza Tanzania ili kutumia fursa zilizopo katika sekta mbalimbali kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa ndani ya nchi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), Waziri Mkuu amesema Tanzania ina fursa nyingi katika kila sekta na ni wakati muafaka kwa wawekezaji kuzichanganua na kuzalisha bidhaa.

Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa kuendelea kutangaza maonesho ya Sabasaba ili kuvutia wafanyabiashara na wawekezaji ambao watajenga viwanda na kuongeza thamani ya rasilimali zilizopo nchini, na kuuza bidhaa kwenye masoko ya kimataifa.

Ameiagiza Wizara ya Viwanda na Biashara kushirikiana na wafanyabiashara ili kuelewa namna bora ya kutangaza fursa za uwekezaji nchini, kwa lengo la kukuza uchumi wa Taifa.

Aidha, Waziri Mkuu ameitaka
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) kutafuta masoko ya bidhaa za Tanzania nje ya nchi, ili kila mzalishaji aweze kufahamu mahitaji ya bidhaa yake kwenye nchi mbalimbali na ubora unaotakiwa katika soko husika.

✍️ 🎥

13/07/2025

📺: - Raul 🔥🔥

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wasafi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share