Wasafi TV

Wasafi TV Official page For Wasafitv Channel
(11)

28/10/2025

'ITEGAMATWI' YAFANYA ZIARA KUHIMIZA
WAKULIMA KUJITOKEZA KUPIGA KURA

Chama Cha msingi ITEGAMATWI kilichopo usoke wilaya ya urambo kimehitimisha ziara Yao ya nyumba Kwa nyumba na kuwahimiza wakulima wake na wananchi Kwa ujumla kutoka Kwa wingi kwenda kupiga kura tarehe Oktoba 29,2025

Wakisindikizwa na mwenyekiti wa tawi Hilo kupitia chama Cha mapinduzi ndugu Bakari m***a Isike na mwenyekiti wa chama hicho ndugu umaiya musoma.

27/10/2025

Who done more 👀 ⁉️ Let’s See
________________________________

- Nani Ana Mchango Mkubwa Zaidi Katika Ulimwengu Wa Hiphop ?

27/10/2025

Who Are You Listening To First ⁉️ 👀 🇺🇸
______________________________

Utaanza kumsikiliza Nani Hapa K**a Wote wakiachia album siku moja ?

Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, imetambua ra...
15/10/2025

Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, imetambua rasmi mchango wa waliowahi kuwa viongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa kuwatuza hati za shukrani, ikiwa ni heshima kwa uzalendo wao uliotukuka.

Akizungumza katika kilele cha mbio hizo zilizohitimishwa kitaifa Oktoba 14, 2025 katika Viwanja vya Sokoine jijini Mbeya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, alisema kuwa tukio hilo ni hatua ya kihistoria na heshima kwa wazee hao waliolitumikia taifa kwa moyo wa kizalendo.

Miongoni mwa waliotunukiwa hati za shukrani na mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, ni pamoja na Balozi Christopher Liundi (85) ,Meja Jenerali Mstaafu Zawadi Madawili (76) ,Mwanamke wa kwanza kuwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge mwaka 1975 akiwa na cheo cha Luteni, Jordan Rugimbana (59) Julius Tweneshe (62) na Meja Musa Ng’omambo

Kwa mujibu wa Ridhiwani Kikwete, tangu kuanzishwa kwa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 1964, jumla ya vijana 339 wamepata heshima ya kuukimbiza Mwenge katika kipindi cha miaka 61, wakiwa mstari wa mbele katika kueneza ujumbe wa mshik**ano, amani na maendeleo.

Katika hafla hiyo, Mkoa wa Pwani umetunukiwa cheti na kikombe maalumu kwa kuwa mwenyeji wa uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025.

Aidha, Halmashauri ya Chalinze iliibuka mshindi wa kwanza wa mbio hizo katika Kanda ya Nne, inayojumuisha mikoa ya Pwani, Lindi, Mtwara, Kigoma, Katavi na Rukwa.

Sherehe hizo pia zilipambwa na burudani mbalimbali, kauli mbiu za kitaifa, na tafakari juu ya mchango wa vijana katika kulijenga taifa kupitia dhana ya Mwenge wa Uhuru.

Dar es Salaam, Oktoba 15 2025 — Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025, kampuni ya kifedha OYA Micro-Credit T...
15/10/2025

Dar es Salaam, Oktoba 15 2025 — Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja 2025, kampuni ya kifedha OYA Micro-Credit Tanzania imeonesha upendo na kuthamini mchango wa wateja wanaojishughulisha k**a Mama Lishe,katika maeneo mbali mbali jijini Dar es Salaam kwa kuwazawadia bidhaa mbalimbali za chakula k**a ishara ya shukrani kwa mchango wao mkubwa katika kuinua uchumi wa jamii inayowazunguka

Tukio hilo lililofanyika Kinondoni na Ubungo jijini Dar es Salaam lilijumuisha zaidi ya Mama Lishe 100 walionufaika na OYA kupitia huduma zake za mikopo midogo midogo kwa wafanyabiashara. Walipewa zawadi za vyakula k**a unga, mafuta ya kupikia, maharage, mchele, sukari, na sabuni — vyote vikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zao za kila siku katika kutoa huduma ya chakula kwa maelfu ya Watanzania

Kupitia wiki hii ya huduma kwa wateja OYA imewaletea wateja wake huduma mpya ya Mikopo kwa watumishi na waajiriwa “SALARY LOAN” ambayo imeanza kutolewa rasmi na taasisi hii kuanzia Octoba hii

Kwa sasa watumishi na waajiriwa wote wanaweza kupata Mkopo huu KWA URAHISI na masharti nafuu kabisaa. OYA imejikita kutoa mikopo isiyo na dhamana na masharti nafuu.

12/10/2025

AJIRA 1,213 KWA WATU WENYE ULEMAVU NA MSAADA WA BILLION 16 KATIKA MIONGO MIWILI YA UONGOZI WA DK SAMIA

Takribani watu 1,213 wenye ulemavu wamepata fursa ya kuajiriwa katika taasisi mbalimbali za Serikali katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa awamu ya sita.

Ajira hizo zimepatikana katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, elimu, uhasibu, lishe, ustawi wa jamii pamoja na maendeleo ya jamii.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, wakati wa hafla ya mapokezi ya Tuzo ya Shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

Waziri Kikwete alisisitiza kuwa jitihada za Rais Samia zimeleta mabadiliko makubwa katika kuwasaidia na kuwapatia ajira watu wenye ulemavu.

Katika kipindi hicho cha miaka minne, Dk. Samia pia ameridhia kutoa ruzuku ya shilingi milioni 61 kwa kiwanda cha KCMC Moshi, Kilimanjaro, kuzalisha mafuta ya kinga ya saratani ya ngozi kwa watu wenye ualbino. Mafuta haya sasa yanagawiwa bure kupitia Bohari ya Dawa katika vituo vya afya nchini kote.

"Wizara imefanikiwa kufungua milango ya ajira kwa watu wenye ulemavu na kuwekeza zaidi ya shilingi bilioni 16.4 katika vikundi mbalimbali na mtu mmoja mmoja wenye ulemavu," amesema Waziri Ridhiwani Kikwete.

Tuzo hizo zilipokelewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa niaba ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan tarehe 11 Oktoba jijini Dar es Salaam, zikiwa ni ishara ya shukrani kutoka kwa watu wenye ulemavu kwa juhudi na msaada mkubwa uliofanywa katika kipindi cha uongozi wa Rais Samia.


Digital

09/10/2025
Baadhi Ya Nyimbo Zilizowasilishwa Katika Tuzo Za Grammy Kipengele Cha ‘Best African Music Performance. Ngoma 5 Tu Zinahi...
07/10/2025

Baadhi Ya Nyimbo Zilizowasilishwa Katika Tuzo Za Grammy Kipengele Cha ‘Best African Music Performance. Ngoma 5 Tu Zinahitaji Kuwania tuzo hizo katika kipengele hiki.

Wasanii Watakaowania Tuzo Hizi Watatangazwa Rasmi Novemba 7, 2025, Huku Halfa Ya Ugawaji Wa Tuzo Hizo Itafanyika February 1, 2026.

JE, Unadhani Ngoma Gani Itachaguliwa Kuwania Tuzo Hizo Katika Kipengele Hicho ?

✍️: ()

Oktoba 29, 2025  ☑️
07/10/2025

Oktoba 29, 2025 ☑️

Upo ushahidi madhubuti unaoonesha uwepo wa tija ya kupiga kura Katika uchaguzi Mkuu wa Tanzania licha ya uwepo wa mitaza...
05/10/2025

Upo ushahidi madhubuti unaoonesha uwepo wa tija ya kupiga kura Katika uchaguzi Mkuu wa Tanzania licha ya uwepo wa mitazamo na kauli mbalimbali kuwa kushiriki kwenye uchaguzi huo ni kupoteza muda tofauti na uhalisia ulivyo, uchaguzi ukitajwa k**a heshima, wajibu na silaha ya Kidemokrasia kote duniani.

"Kupiga kura ni haki ya Kikatiba, inayomuwezesha kila Mtanzania kushiriki katika maamuzi ya nchi kwa njia ya amani, kupitia kura wananchi huamua ni nani awaongoze katika nafasi za kisiasa k**a Rais, Wabunge na Madiwani na hii ni njia halali ya kushiriki katika ujenzi wa Taifa na kuhakikisha kuwa sauti ya mwananchi inasikika." Amesema Mchambuzi wa siasa Ally Said alipozungumza nasi.

Kulingana na Mchambuzi huyo, wananchi wanapojitokeza kwa wingi kupiga kura wana nafasi ya kuchagua Viongozi waadilifu na wenye uwezo wa kuwaletea maendeleo, kupitia kura matatizo ya huduma duni za jamii yanaweza kushughulikiwa, Kura ikiimarisha pia misingi ya demokrasia na utawala bora kwa kuwafanya walioko madarakani kuwajibika kwa wananchi kwa kujua kuwa wanaweza kuondolewa kwa kura ikiwa hawatatimiza wajibu na ahadi zao.

John James, Mwananchi wa Goba Jijini Dar Es salaam anasema anafahamu kuhusu haki yake ya kupiga kura, akihimiza umuhimu wa kuwachagua wale wanaojua shida za wananchi na wenye kujali mahitaji ya wananchi. Akieleza kuwa mabadiliko ha kweli yanapatikana kupitia kura na si vurugu, matusi, jazba ama maandamano ya kutaka kushinikiza mambo isivyo halali.

Ushiriki wa uchaguzi unatoa nafasi kwa wananchi kushiriki moja kwa moja katika maamuzi yanayogusa maisha yao ya kila siku ambapo Viongozi wanaochaguljwa kwa ushirikishwaji wa wananchi wanakuwa na uwezo wa kutengeneza mipango ya maendeleo inayokidhi mahitaji halisi ya eneo husika, wito ukitolewa kwa kila mwananchi mwenye sifa kujitokeza kupiga kura kwa amani, kuheshimu sheria za nchi ikiwa ni pamoja na kuepuka kuvunja sheria kwa kuhamasisha wananchi kutokupiga kura ama kulinda kura kwenye Vituo vya upigaji kura.

05/10/2025

Tanesco Saccos inatajwa kuwa ni msaada wa kuwainua kiuchumi wanachama wake katika nyanja mbalimbali hasa kiuchumi

akizungumza katika mkutano mkuu wa 57 wa mwaka Wilison Kingu Mwananchama na Mshiriki wa Tanesco Saccos ameridhishwa na huduma kwani imekuwa mkombozi kiuchumi na kuwafanya kuwa na maisha bora

Kwa upande wake Neema Martine Fransis mwanachama wa Saccos na mwakilishi kutoka mkoa wa Morogoro amewaomba wafanyakazi wenzake kujiunga kwani kimekuwa chama chenye msaada kwa wafanya kazi wote

Akitoa taarifa ya Bodi Omary Shabani ambaye ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya Saccos amesema chama kimeendelea kukua kwa upande wa hisa kwa mwaka 2023 huku hisa za wananchama zikiwa zaidi ya Bilion 10

Hata hivyo chama kimeendelea kutoa mikopo kwa wanachama wanaofikia 4031 ambapo thamani yake inafikia Bilion 27 kwa kipindi cha mwaka mmoja

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Tanesco ambaye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi katika mkutano huu Injinia Antony Mbushi naibu mkurugenzi mtendaji uzalishaji amesema Tanesco Saccos ni chama cha muhimu kwa sababu kinawasaidia wafanyakazi kupata mikopo na kujikumu katika maisha yao

02/10/2025

Address

Kanisani Road, Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wasafi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share