30/06/2026
CHAMA CHA SALONIST TANZANIA (CCST) KUZINDULIWA RASMI LEO
Leo , Jumanne Juni 30, 2026, Chama cha Salonist Tanzania (CCST) kitazinduliwa rasmi hafla itakayofanyika katika ukumbi wa EACCL, Ubungo, huku kikitarajiwa kuwa mwanzo wa ukurasa mpya kwa tasnia ya urembo nchini.
Tamasha hili litakuwa na matukio mbalimbali ya kuvutia, fursa za kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuwakutanisha wadau wa tasnia ya urembo na utanashati kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Waandaaji wanasema hatua kwa hatua wamekuwa wakiliandaa tamasha hilo ili liwe la kihistoria kwa watoa huduma za urembo nchini. Miongoni mwa malengo yake ni kuweka viwango vya taaluma, kutambua na kuthamini vipaji, pamoja na kukitangaza rasmi Chama cha Salonist Tanzania (CCST) kwa wadau wa tasnia ya urembo na utanashati.
Ni muda wa Masalonist kusimama pamoja na kuandika historia mpya ya tasnia ya urembo Tanzania