22/07/2025
KAMPUNI ya Selcom kupitia Huduma yake ya kifedha ya kidigitali -Selcom Pesa imezindua kampeni ya Huduma ya Mabando ya Miamala, ijulikanayo k**a "Tumia Bando la miamala, k**a Bure,okoa gharama" ikiwa ni muendelezo wa dhamira yake ya kutoa Huduma za kifedha zenye gharama nafuu kwa watanzania.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa kitengo Cha Masoko wa Selcom Shumbana Walwa amesema kampeni hiyo imekuja baada ya mafanikio ya kampeni ya kwanza ya 5 kwa jero iliyoanzisha ajenda ya upatikanaji wa Huduma nafuu Zaidi kwa Kila Mtanzania
Aidha ameeleza kwamba Mabando ya Miamala ya Selcom pesa ni ya kwanza Tanzania yakilera SULUHISHO jipya linalomwezesha watumiaji kufanya miamala kwa makato madogo kuliko huku wakijipangia matumizi Yao kwa ufanisu bila kutozwa ada ya Kila muamala.
Kampeni hiyo inalenga siyo tu kupunguza gharama kwa watumiaji Bali pia KUWAJENGEA tabia ya kupanga matumizi ya kifedha kwa unafuu Zaidi