Jamhuri Digital

Jamhuri Digital The official page of Jamhuri Media Company
Wanapoishia Wengine

Na Berensi ChinaTabora: Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo mkoani Tabora wamepinga uamuzi wa Mkuu wa Wilaya hiy...
03/08/2026

Na Berensi China

Tabora: Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo mkoani Tabora wamepinga uamuzi wa Mkuu wa Wilaya hiyo, Hamisi Mkanachi, wa kuwasimamisha kazi viongozi wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Uyumbu, wakidai hatua hiyo haikuzingatia haki na imeathiri utendaji wa jumuiya hiyo.

Hoja hiyo iliibuliwa katika kikao cha Kamati ya Uchumi na baadaye kuwasilishwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Julai 30 na 31, 2026, chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri, Athumani Mwiniko.

Baada ya kujadili taarifa ya kusimamishwa kwa viongozi hao, madiwani walieleza kutoridhishwa na uamuzi huo, wakidai ulifanyika bila kufuata utaratibu unaostahili.

Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Uyumbu, Gabriel Mkandala, alisema viongozi hao wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa ufanisi tangu walipochaguliwa na kwamba hakuna sababu za msingi za kuwaondoa madarakani.

«"Sisi k**a madiwani tunapingana na uamuzi wa Mkuu wa Wilaya. Viongozi hawa wamekuwa wakifanya kazi vizuri tangu walipochaguliwa na jumuiya imekuwa ikifanya kazi vizuri. Hatuwezi kukubali kuona jumuiya ikivurugwa. Tunahitaji Kamati ya Uchumi na Fedha ifike eneo husika kujionea kinachoendelea," alisema Mkandala.»

Hoja hiyo iliungwa mkono na Diwani wa Kata ya Kasisi, ambaye alitaka kusimamishwa kwa viongozi hao kufutwe ili warejee kazini na kuendelea na shughuli za jumuiya k**a ilivyokuwa awali.

Kwa mujibu wa baadhi ya madiwani, chanzo cha mgogoro huo kinadaiwa kuwa ni hatua ya viongozi hao kuk**ata magunia ya mkaa na magogo yanayodaiwa kuhusishwa na mtu mwenye ushawishi mkubwa, madai ambayo hayajathibitishwa rasmi.

Aidha, ilielezwa kuwa viongozi hao walisafiri kwenda mkoani Manyara kwa ajili ya mafunzo ya kujifunza utendaji wa jumuiya nyingine ya hifadhi ya wanyamapori. Inadaiwa kuwa Mkuu wa Wilaya hakuridhia safari hiyo, na waliporejea walikuta wamesimamishwa kazi kuanzia Julai 7, 2026, bila kupewa barua rasmi. Baadaye, Julai 21, 2026, alitangaza uongozi mpya.

03/08/2026
NIRC YATANGAZA NEEMA KWA WAKULIMA NANE NANE📍NIRC: DodomaSerikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), inaendelea...
03/08/2026

NIRC YATANGAZA NEEMA KWA WAKULIMA NANE NANE

📍NIRC: Dodoma

Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), inaendelea na utekelezaji wa Mkakati mkubwa wa kuimarisha kilimo cha Umwagiliaji
nchini kwa kuzindua miradi mipya zaidi ya 30 katika mwaka wa fedha 2026/27, huku ikitarajia kuajiri maelfu ya vijana kupitia uchimbaji wa visima na usimamizi wa miundombinu ya Umwagiliaji.

Pia inalenga kuongeza uzalishaji wa mazao na kufanikisha azma ya sekta ya kilimo kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Dr. John Malecela, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa amesema kwa kipindi cha miaka michache ya utekelezaji wa majukumu yake, tume imefanikiwa kuwa na wakandarasi 146 wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Umwagiliaji, huku miradi 634 ikiwa katika hatua za usanifu.

Amesema lengo ni kuhakikisha mkulima anakuwa na uwezo wa kuzalisha kwa tija na kuacha kutegemea mvua.

“Tume inatarajia kuanza zoezi kubwa la kugawa pampu za maji katika mikoa saba nchini, ambapo zoezi hili litaanza rasmi mkoani Katavi ifikapo tarehe 11,”amesema

Katika mpango huo, jumla ya pampu za kawaida (surface pumps) 1,000 zitatolewa ili kuwasaidia wakulima wa mbogamboga na matunda kuvuta maji kwa urahisi kutoka kwenye mito na mabonde, jambo ambalo litafanyika kwa njia salama isiyoharibu mazingira.

Sambamba na hilo, zaidi ya pampu 1,000 za kisasa zinazotumia nishati ya jua (solar pumps) zimenunuliwa maalum kwa ajili ya wakulima wa zao la parachichi.

“Wakulima hawa mara nyingi hukumbana na changamoto ya miinuko na mabonde inayokwamisha mifumo ya kawaida ya Umwagiliaji, hivyo pampu hizi ni mkombozi wao mkuu.

03/08/2026

MHESHIMU ALIYE JUU YAKO - DKT. BITEKO

“ Siri moja mheshimu aliye juu yako hatak**a unaona umemzidi akili. “

03/08/2026

NISHATI NI CHACHU YA KILIMO, UCHUMI NA MAENDELEO YA VIJIJINI – MHA. SAIDY

*📌Awakaribisha wananchi na wadau kutembelea banda la REA katika Maonesho ya Nane Nane 2026*

📍DODOMA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, amewakaribisha wananchi na wadau kutoka sekta mbalimbali kutembelea Banda la REA katika Maonesho ya Nane Nane 2026 yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma, ili kujionea mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini na kupata elimu kuhusu huduma zinazotolewa na Wakala.

Akizungumza kuhusu maonesho hayo, Mha. Saidy amesema REA inaendelea kutekeleza miradi ya umeme vijijini na nishati safi ya kupikia kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa nishati zote kwa wananchi ili kuchochea shughuli za uzalishaji, kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi nchini.

Ameeleza kuwa upatikanaji wa nishati bora umeendelea kuwa chachu ya maendeleo kwa kuwezesha matumizi ya teknolojia za kisasa katika kilimo, ikiwemo umwagiliaji, uchakataji na uhifadhi wa mazao, pamoja na kukuza biashara na viwanda vidogo vijijini. Hali hiyo imechangia kuongeza tija, kipato cha wakulima na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Mha. Saidy amesisitiza kuwa Banda la REA ni fursa muhimu kwa wananchi na wadau kupata elimu kuhusu utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini, kufahamu mafanikio yaliyopatikana na kuelewa mchango wa nishati katika kuimarisha maendeleo ya wananchi hususan waishio vijijini ili kuitekeleza kivitendo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

UmemeVijijini NishatiSafiYaKupikia

Mabanda ya NMB Yavuta Mawaziri na Maelfu ya Wananchi  Nane NaneMabanda ya Benki ya NMB yanaendelea kuwa miongoni mwa viv...
02/08/2026

Mabanda ya NMB Yavuta Mawaziri na Maelfu ya Wananchi Nane Nane

Mabanda ya Benki ya NMB yanaendelea kuwa miongoni mwa vivutio vikuu katika Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea katika kanda mbalimbali nchini, huku mawaziri, viongozi wa Serikali na maelfu ya wananchi wakitembelea kujionea suluhisho za kifedha zinazowezesha kilimo, mifugo, uvuvi na biashara.

Dodoma: Waziri wa Fedha, Balozi Khamis M***a Omar, na Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde, wakitembelea banda la Benki ya NMB wakati wa Maonesho ya Nane Nane yanayoendelea jijini Dodoma.

Morogoro: Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, akimsikiliza Meneja Mahusiano wa Benki ya NMB Kanda ya Kati kutoka Idara ya Kilimo na Biashara, Miastela Magoma, alipokuwa akipata maelezo kuhusu huduma za benki hiyo alipotembelea banda la NMB kwenye Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, mkoani Morogoro.

Mwanza: Meneja Mahusiano wa Biashara kwa Serikali wa Benki ya NMB, Humphrey Kaaya (kushoto), akitoa maelezo kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza kuhusu fursa za upatikanaji wa mikopo ya matrekta na suluhisho za kifedha zinazowezesha ununuzi wa zana za kisasa za kilimo, wakati wa Maonesho ya Nane Nane yanayofanyika katika Viwanja vya Nyamhongolo, mkoani Mwanza.

NMB ni mdhamini wa Maonesho ya Nane Nane 2026, ikiwa sehemu ya dhamira yake ya kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi na kuwawezesha wakulima, wafugaji, wavuvi na wajasiriamali kuongeza tija na kukuza uchumi kupitia huduma zinazokidhi mahitaji yao.

02/08/2026

🥤 Kwa nini uchague ORIJIN?

ORIJIN ni kinywaji kipya kilichotengenezwa kwa mchanganyiko wa mitishamba, matunda na viambato vya asili k**a vile kola nut, prune, maganda ya chungwa chungu na wormwood, vinavyoipa ladha ya kipekee na uzoefu tofauti wa unywaji.

Kwa mujibu wa watengenezaji wake, ORIJIN imebuniwa kwa kuzingatia ubora wa viambato vya asili ili kuwapa watumiaji chaguo lenye ladha ya kipekee.

Beverages HerbalBlend

Waziri Mkuu Apongeza NMB kwa Kusogeza Huduma za Kifedha VijijiniDodoma: Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameipongeza Ben...
01/08/2026

Waziri Mkuu Apongeza NMB kwa Kusogeza Huduma za Kifedha Vijijini

Dodoma: Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi kupitia matumizi ya teknolojia na utekelezaji wa mkakati wa Rural Banking, akisema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na kupunguza gharama za miamala ya kifedha nchini.

Akimkaribisha Waziri Mkuu katika banda la NMB kwenye Maonesho ya Nanenane, Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali wa benki hiyo, Bi. Vicky Bishubo, alisema NMB imeendelea kuwekeza kwa nguvu katika sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji, ambapo hadi sasa benki hiyo imetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi trilioni 2.3 kwa sekta hizo.

Alieleza kuwa NMB pia imeanzisha huduma zinazowawezesha vijana kupata mikopo ya hadi Shilingi milioni mbili kupitia teknolojia, bila hitaji la dhamana wala kufika tawi la benki, hatua inayolenga kuongeza ujumuishaji wa kifedha kwa makundi mbalimbali ya wananchi.

Bi. Bishubo aliongeza kuwa kupitia mpango wa Rural Banking, benki hiyo imeendelea kupeleka huduma za kifedha katika masoko, minada ya mifugo na maeneo mengine ya biashara vijijini ili kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

Mbali na huduma za kifedha, NMB inaendelea kutoa elimu ya fedha kupitia programu ya NMB Kijiji Day, pamoja na kushirikiana na vyuo vikuu nchini kuwajengea vijana ujuzi unaohitajika katika uchumi unaozingatia teknolojia, ubunifu na ujasiriamali.

Kwa mujibu wa Waziri Mkuu, juhudi za taasisi za kifedha k**a NMB zinachangia kuimarisha maendeleo ya uchumi wa wananchi na kuongeza fursa za ukuaji wa sekta za uzalishaji nchini.

01/08/2026
01/08/2026

NMB Yaendelea Kuimarisha Kilimo Kupitia Ushirikiano wa Nanenane.

Benki ya NMB imekabidhi hundi ya udhamini kwa Wizara ya Kilimo kwa ajili ya Maonesho ya Nanenane 2026, ikiendeleza ushirikiano wake wa muda mrefu na Serikali katika kukuza sekta ya kilimo.

Makabidhiano yaliyofanyika jana jioni jijini Dodoma yamefikisha jumla ya udhamini wa NMB katika maonesho hayo hadi Sh572 milioni ndani ya miaka minane mfululizo, yakionyesha dhamira ya benki hiyo katika kusaidia maendeleo ya wakulima, wafugaji na wavuvi.

Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Janeth Shango, alisema Nanenane ni jukwaa muhimu la kuwafikisha wazalishaji kwenye maarifa, teknolojia na huduma za kifedha zinazoongeza tija na kufungua fursa mpya za biashara.

Waziri wa Kilimo Daniel Chongolo aliipongeza NMB kwa kuendelea kuwa karibu na wakulima na kuitaka benki hiyo kuendeleza ushirikiano huo ili kuwafikia Watanzania wengi zaidi kupitia elimu, teknolojia na huduma za kifedha.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jamhuri Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jamhuri Digital:

Shortcuts

Share

Category