Jamhuri Digital

Jamhuri Digital The official page of Jamhuri Media Company
Wanapoishia Wengine

01/06/2026

01/06/2026

😂😂

01/06/2026

😂😂😂

31/05/2026

Studio za mwanamuziki wa Tanzania, Barnaba Classic, zimeungua moto usiku wa kuamkia Juni 1, 2026 katika eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Barnaba amesema moto huo ulianza majira ya saa 2:30 usiku muda mfupi baada ya kurejea kutoka kwenye shoo ya Malkia wa Nguvu iliyofanyika Arusha.

Msanii huyo amesema studio zake za High Table Sound Entertainment zimeungua kabisa na kubaki majivu, licha ya kufanyiwa ukarabati mkubwa wiki mbili zilizopita kwa gharama kubwa.

“Moyo wangu unaumia, nimelia sana kwa uchungu na nimepoteza nguvu kabisa. Nasikitika kusema HQ yetu imekuwa majivu,” ameandika Barnaba.

Aidha, amemshukuru Mungu na kusema kuwa licha ya hasara kubwa aliyopata, yuko tayari kuanza upya, akieleza kuwa maisha huleta mafunzo na changamoto ambazo ni lazima zipokelewe kwa ujasiri. 🙏🏽🔥💔

29/05/2026

29/05/2026

Ng'ombe anayefanana na Trump anusurika kuchinjwa Eid Al adha

29/05/2026

29/05/2026
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Mu...
29/05/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, ambaye ni Mama wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, yaliyofanyika Kilimani, Chato mkoani Geita.

Akitoa salamu za rambirambi mara baada ya kumalizika kwa Ibada ya kumuombea Marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli, Makamu wa Rais amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameguswa na msiba huo na anatoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki na wote walioguswa na msiba huo.

Makamu wa Rais amewasihi Watanzania kumtumia marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli k**a kielelezo cha malezi ya watoto, malezi ya maadili na uzalendo kwa kuwafanya watoto kutanguliza maslahi ya Taifa mbele na kuwa tayari kutumikia Taifa kwa nafasi yeyote wanayopewa. Ameongeza kwamba namna bora ya kumuenzi marehemu Bi. Suzana Ngolo Magufuli ni kuiga mfano wa malezi bora na mema ya watoto.

Amesema msiba wa Bi. Suzana Ngolo Magufuli unafundisha kuwa alikuwa sehemu kuu ya malezi ya Hayati Rais Dkt. John Magufuli ambaye alitoa mchango mkubwa katika utumishi wa nchi yetu. Amesema kitendo cha wananchi wengi kutoa salamu za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii ni ishara ya Watanzania kuguswa na Maisha ya Hayati Magufuli ambaye alitumikia nchi kwa uzalendo wa hali ya juu.

Halikadhilika, Makamu wa Rais amemuelezea hayati Dkt. John Pombe Magufuli, k**a kiongozi aliyejitoa kutetea nchi pamoja na kuwa na utashi wa kujua wajibu wa kulea watu wengine na kuwafanya kuwa Viongozi wa Taifa baadaye. Ameongeza kwamba kujitoa na kufanya matendo mema kwaajili ya wengine ni matunda ya baadaye kwa mtu na familia yake.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya familia Bw. Simon Nyahinga amesema familia hiyo inamshukuru kwa dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upendo mkubwa, huruma, faraja na mchango wake mkubwa aliyouonesha wakati wa kuugua kwa Bi Suzana Magufuli.

29/05/2026

Na OWM - TAMISEMI, Kahama

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali haitomuongezea muda Mkandarasi M/s China Civil Engineering Construction Corporation wa kukamilisha miradi ya ujenzi wa barabara na mitaro katika Manispaa ya Kahama, inayotekelezwa kupitia Mradi wa Uendelezaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) kwani ubovu wa miundombinu ya barabara imekuwa ni kero ya muda mrefu kwa wananchi wa manispaa hiyo.

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Mei 27, 2026 Katika Manispaa ya Kahama wakati wa hafla ya Utiaji Saini wa Mkataba wa Umaliziaji wa Ujenzi wa Barabara na Mitaro kupitia Mradi wa TACTIC, iliyofanyika katika eneo la Phantom kwenye manispaa hiyo.

“Ninamueelekeza Mkandarasi Kampuni ya M/s China Civil Engineering Construction Corporation kumaliza ujenzi ndani ya muda ulioanishwa katika mkataba ambao wameusaini leo, hakutakuwa na nyongeza ya muda,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amemtaka Mtaalamu Mshauri kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama pamoja na TARURA katika kuhakikisha mikataba iliyosainiwa inatekelezwa kikamilifu na inakamilika ndani ya muda uliopangwa na kwa ubora uliokubalika ili thamani ya fedha ionekane.

Prof. Shemdoe ameanisha kuwa Mei 27, 2026 imekuwa ni siku yenye furaha kwani kitendo cha kusainiwa kwa mikataba hiyo kinasadifu nia ya dhati ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaboreshea miundombinu ya barabara wananchi wa Kahama, na kuongeza kuwa k**a lilivyo jina lake amekuwa ni suluhu ya changamoto iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa Manispaa ya Kahama.

“Tumeshuhudia utiaji saini wa mradi huu mkubwa wa zaidi ya Shilingi Bilioni 25 ambazo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia zitumike kujenga miundombinu ya barabara katika Manispaa ya Kahama, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2025 hivyo tunamshukuru sana na kumuahidi kwamba ofisi yangu itasasimamia kikamilifu utekelezaji wa mkataba huo,” amesema Prof. Shemdoe.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jamhuri Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jamhuri Digital:

Share

Category