Watetezitv

Watetezitv WATETEZI TV is a Not-For-Profit online Tv under the Tanzania Human Rights Defenders Coalition(THRDC). Watetezi Tv operates in lieu of all applicable laws.

It will not be responsible to any subscriber who will post anything contrary to the applicable laws

Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Paul Christian Makonda kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akichukua n...
08/01/2026

Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Paul Christian Makonda kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo akichukua nafasi ya Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi.

Kabla ya uteuzi huu, Makonda alikuwa Naibu Waziri katika Wizara hiyo.

Rais Samia Suluhu Hassan Amemteua Patrobas Paschal Katambi  kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Kabla ya uteuzi huu, ...
08/01/2026

Rais Samia Suluhu Hassan Amemteua Patrobas Paschal Katambi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Kabla ya uteuzi huu, Katambi alikuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, anachukua nafasi ya Boniface George Simbachawene ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Uteuzi huo umefanyika leo Januari 8, 2026 k**a ulivyotolewa kwenye taarifa rasmi na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dk. Moses Kusiluka.

05/01/2026

Serikali imetaja Mkoa wa Morogoro kuwa miongoni mwa mikoa iliyoonesha kiwango cha juu cha ustaarabu na uzingatiaji wa sheria wakati wa maandamano ya Oktoba 29, 2025, baada ya kubainika kuwa hakuna tukio la vurugu wala mkazi yeyote wa mkoa huo aliyek**atwa.

Akizungumza leo Jumatatu, Januari 5, 2026, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani mjini Morogoro, Waziri wa Katiba na Sheria, Juma Homera, amesema kuwa tathmini iliyofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka imeonesha kuwa wananchi wa Morogoro waliendelea na shughuli zao za kila siku badala ya kushiriki katika maandamano yaliyoambatana na vurugu katika maeneo mengine.

Kwa mujibu wa Waziri Homera, hali hiyo ni matokeo ya uongozi na ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa Serikali, vyombo vya usalama na wananchi. Amemtaja Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, kuwa ni miongoni mwa viongozi waliofanikiwa kuimarisha mshik**ano na kuifanya Morogoro kuwa eneo salama na lenye utulivu.

Waziri ameongeza kuwa mazingira hayo ya amani yamechangia Serikali kuchukua uamuzi wa kupeleka huduma za Kliniki ya Msaada wa Kisheria mkoani Morogoro, kwa lengo la kuwafikia wananchi wanaohitaji msaada wa kisheria na kuendelea kukuza utawala wa sheria.

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, leo Jumatatu Januari 05, 2026, anatarajiwa kuongoza zoezi la utoaji...
05/01/2026

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera, leo Jumatatu Januari 05, 2026, anatarajiwa kuongoza zoezi la utoaji wa msaada wa kisheria bure mkoani Morogoro, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wananchi, sambamba na kuelekea siku 100 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tangu alipoingia madarakani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Katiba na Sheria, zoezi hilo linalenga kuwasaidia wananchi wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali za kisheria, ikiwemo migogoro ya ardhi, masuala ya mirathi, malezi na ulinzi wa watoto, upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa, pamoja na changamoto nyingine zinazohitaji ufumbuzi wa kisheria.

Huduma hizo zitatolewa kupitia kliniki maalum za msaada wa kisheria zitakazohusisha wataalamu wa sheria pamoja na taasisi zilizo chini ya Wizara. Wananchi watapatiwa elimu ya kisheria, ushauri wa kitaalamu, pamoja na mwongozo wa hatua za kuchukua kulingana na changamoto zao.

Aidha, mkutano wa pamoja wa kusikiliza na kushughulikia kero za wananchi unatarajiwa kufanyika katika Viwanja vya Stendi ya Zamani, Manispaa ya Morogoro, ambapo wananchi watapata fursa ya kuwasilisha hoja na changamoto zao moja kwa moja kwa wataalamu wa sheria na viongozi wa taasisi husika.

Mbali na utoaji wa huduma kwa wananchi, Dkt. Homera anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi katika taasisi za haki zilizopo mkoani Morogoro kwa lengo la kukagua utekelezaji wa majukumu yao, kusikiliza changamoto na kutoa maelekezo yatakayoboresha utoaji wa huduma za kisheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamtafuta mwanaume aitwaye Helakumi Kacheri kwa tuhuma za kumuua mkewe katika tukio l...
05/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamtafuta mwanaume aitwaye Helakumi Kacheri kwa tuhuma za kumuua mkewe katika tukio lililotokea Januari 4, 2026, katika Kitongoji cha Tindegala, Kata ya Singisa, Wilaya ya Morogoro.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mk**a, tukio hilo lilitokea wakati marehemu akiwa shambani pamoja na mtuhumiwa. Inadaiwa kuwa Helakumi Kacheri alimshambulia marehemu kwa kutumia silaha kali sehemu mbalimbali za mwili, akimtuhumu kuendeleza mahusiano ya karibu na mzazi mwenza wake wa awali. Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alitoroka eneo la tukio na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Katika taarifa hiyo, Jeshi la Polisi pia linachunguza matukio mengine mawili ya vifo yaliyotokea katika mkoa huo.

Tukio la kwanza liliripotiwa katika Kitongoji cha Isago, Kata ya Mgeta, ambapo Jesse Melumba (49), mkulima, alifariki dunia akiwa shambani. Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa huenda marehemu alikunywa sumu kwa bahati mbaya, baada ya kubainika kuwepo kwa mabaki ya dawa ya kilimo aina ya Banafos.

Tukio jingine lilitokea Januari 3, 2026, katika Kata ya Doma, Wilaya ya Kilosa, ambapo Ally Charles Dagaza (38) alifariki dunia baada ya kukanyagwa na tembo wakati akilinda miche ya nyanya na zao la pilipili.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limetoa wito kwa wananchi wote wenye taarifa zitakazosaidia kuk**atwa kwa Helakumi Kacheri kujitokeza na kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya mtuhumiwa.

Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, amewataka Watanzania kuutumia mwaka 2026 k**a fursa y...
03/01/2026

Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, amewataka Watanzania kuutumia mwaka 2026 k**a fursa ya kuliponya Taifa na kulirejesha kwenye misingi sahihi ya kikatiba, kisheria na kimaadili, akisisitiza kuwa amani ya kweli haiwezi kupatikana bila haki, uwajibikaji na ridhaa ya wananchi.

Akizungumza kupitia salamu zake za Mwaka Mpya wa 2026, Masoud amesema licha ya changamoto, majaribu na maafa yaliyoikumba nchi mwaka 2025, Watanzania wamefanikiwa kusimama, jambo linalotoa nafasi ya kutafakari kwa pamoja mustakabali wa Taifa.

Amesema utulivu uliopo haupaswi kuchukuliwa k**a ishara ya amani ya kudumu, bali k**a fursa ya kujenga Taifa lenye haki kwa dhamira ya dhati ya viongozi na wananchi. Amepongeza wananchi na wadau waliopaza sauti dhidi ya ufisadi na ukiukwaji wa Katiba na sheria, akibainisha kuwa vitendo hivyo vimeathiri uhai wa watu, mali za raia na hadhi ya Tanzania kimataifa.

Masoud amesisitiza kuwa mamlaka ya kuamua nani awaongoze Watanzania yapo mikononi mwa wananchi kwa mujibu wa Katiba, na kuonya kuwa hatua zozote zinazokwamisha haki hiyo ndizo chanzo cha kuvuruga amani ya Taifa. Amesema Taifa lisilowapa wananchi haki ya kuchagua na kuwawajibisha viongozi halina maendeleo ya kweli.

Akizungumzia Zanzibar, amesema busara ya wananchi kuchagua subira ilisaidia kuepusha maafa makubwa baada ya Uchaguzi wa Oktoba 2025. Ameeleza kuwa hatua za ACT Wazalendo zinalenga kutatua mzizi wa tatizo la uchaguzi kwa maslahi ya Zanzibar na Wazanzibari wote.

Amehitimisha kwa kuwashukuru wanachama wa ACT Wazalendo kwa mshik**ano wao na kuwatakia Watanzania wote Heri ya Mwaka Mpya wa 2026.

31/12/2025

’’Tumeondokewa na wapendwa wetu, tuendelee kuwaombea’’ – Rais,Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika salamu za mwaka mpya 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imejipanga katika mwaka 2026 kuimarisha u...
31/12/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali imejipanga katika mwaka 2026 kuimarisha umoja wa kitaifa, akirejea kile alichokiita mitihani ya mwaka 2025 iliyopitia Taifa katika nyakati ngumu zilizohitaji mshik**ano, uzalendo na uvumilivu wa hali ya juu.

Akizungumza leo Jumatano, Desemba 31, 2025, katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka kwa Taifa aliyotoa kutoka Ikulu Ndogo ya Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja, visiwani Zanzibar, Rais Samia amevishukuru vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na wananchi kwa kuendelea kudumisha amani na mshik**ano nchini.

Kuhusu ajenda ya umoja wa kitaifa, Rais Samia amesema tayari Serikali imeanza hatua za awali za kuunda Tume ya Maridhiano, akibainisha kuwa itashirikiana na wadau mbalimbali ili kufikia makubaliano kuhusu muundo wa tume hiyo, aina ya wajumbe, majukumu yao pamoja na muda wa utekelezaji wa kazi zake.

Aidha, amesisitiza kuwa kuelekea katika hatua hizo muhimu, Watanzania hawapaswi kuruhusu tofauti za kiitikadi au kimtazamo kuwagawa au kuwapotezea mwelekeo wa maendeleo na ustawi wa Taifa.

“Tofauti ni sehemu ya demokrasia, lakini hazipaswi kutumika kuligawa Taifa la Tanzania,” amesisitiza Rais Samia.

Mtume Bonifasi Mwamposa amesema kuwa moja ya matukio yaliyomhuzunisha zaidi mwaka 2025 ni vifo na vurugu zilizotokea wak...
31/12/2025

Mtume Bonifasi Mwamposa amesema kuwa moja ya matukio yaliyomhuzunisha zaidi mwaka 2025 ni vifo na vurugu zilizotokea wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Viwanja vya Kawe jijini Dar es Salaam, kuelekea Mkesha wa Vuka na Chako, Mtume Mwamposa amesema tukio hilo halikuwa la kufurahisha kwa Taifa, na liliacha majonzi makubwa miongoni mwa wananchi.

“Nilisikitika sana mwaka 2025 kutokana na yaliyotokea katika Taifa letu. Kuona watu wakipoteza maisha wakati wa Uchaguzi na kushuhudia vurugu si jambo la kufurahisha hata kidogo. Ni tukio lililonihuzunisha sana. Natoa pole kwa wananchi wote kwa dhati na kuwatia moyo kwa kuwaambia kuwa bado tumaini lipo,” amesema Mtume Mwamposa.

Ameongeza kuwa athari za tukio hilo hazikuishia kwa waliopata majeraha ya mwili pekee, bali pia ziliwaathiri wananchi wengi kisaikolojia, hali inayoonesha uzito wa madhara yaliyosababishwa na vurugu hizo.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Awali ya Saint Clemence, Clemence Mwandambo, mkazi wa Mt...
30/12/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Awali ya Saint Clemence, Clemence Mwandambo, mkazi wa Mtaa wa Uzunguni “A” jijini Mbeya, kwa tuhuma za kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo pamoja na kukashfu imani za dini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga, mtuhumiwa alik**atwa leo majira ya saa nne asubuhi katika eneo la Uzunguni, jijini Mbeya.

Inadaiwa kuwa Mwandambo alitumia akaunti zake za mitandao ya kijamii kuchapisha na kusambaza maudhui yanayodaiwa kukashfu imani za dini ya Kiislamu na Kikristo, pamoja na taarifa zinazodaiwa kuwa za uongo.

Kamanda Kuzaga amesema Jeshi la Polisi linaendelea na upelelezi wa kina ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo kabla ya kuchukua hatua zaidi za kisheria dhidi ya mtuhumiwa.

Aidha, kumbukumbu zinaonesha kuwa Mwandambo aliwahi kuk**atwa hapo awali kwa tuhuma zinazohusiana na matumizi ya mitandao ya kijamii, ambapo alishikiliwa kwa siku kadhaa kabla ya kuachiwa kwa mujibu wa taratibu za kisheria.

Kamanda Kuzaga ametoa wito kwa wananchi kutumia mitandao ya kijamii kwa kuzingatia sheria na maadili, pamoja na kuheshimu imani za watu wengine, akisisitiza kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watakaobainika kukiuka sheria.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia na kuendelea kumuhoji Fahima Twaibu (19), msaidizi wa kazi za nyumbani, kwa...
29/12/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia na kuendelea kumuhoji Fahima Twaibu (19), msaidizi wa kazi za nyumbani, kwa tuhuma za kutupa kichanga cha k**e kinachokadiriwa kuwa na umri wa takribani saa mbili tangu kuzaliwa.

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi, mtuhumiwa ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Balyehela, Wilaya ya Ilemela, anadaiwa kutekeleza tukio hilo alfajiri ya Desemba 25, 2025, saa 11:00.

Taarifa kwa umma iliyotolewa leo Jumatatu Desemba 29, 2025, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mutafungwa, imeeleza kuwa Fahima anadaiwa kutupa kichanga hicho muda mfupi baada ya kujifungua juu ya paa la nyumba inayomilikiwa na Emmanuel Muruli, fundi wa kuchomelea vyuma na mkazi wa Balyehela.

Kamanda Mutafungwa amesema askari polisi walifika eneo la tukio kwa haraka na kufanikiwa kuokoa maisha ya kichanga hicho kwa kushirikiana na maofisa ustawi wa jamii pamoja na wananchi wa eneo hilo. Mtoto huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa Sekou-Ture kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

“Uchunguzi wa tukio hili unaendelea na hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa, ikiwemo kufikishwa mahak**ani. Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ni kosa la jinai, na Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo,” amesema Kamanda Mutafungwa.

Jeshi la Polisi nchini limethibitisha kumk**ata Thadei Sabinus Kweka, mwenye hati ya kusafiria namba C23858350, mnamo ta...
29/12/2025

Jeshi la Polisi nchini limethibitisha kumk**ata Thadei Sabinus Kweka, mwenye hati ya kusafiria namba C23858350, mnamo tarehe 28 Desemba, 2025 majira ya usiku, katika mkoa wa Kilimanjaro.

Katika taarifa iliyotolewa leo Desemba 29, 2025, Jeshi la Polisi limesema kuwa mtuhumiwa huyo anakabiliwa na tuhuma mbalimbali za jinai, zikiwemo tuhuma za uchochezi, ambazo ni kinyume na sheria za nchi.

Jeshi hilo limeeleza kuwa taratibu za kisheria zinaendelea, ikiwemo kukamilisha ushahidi na kuchukua maelezo ya mtuhumiwa, ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa.

“Taratibu za kukamilisha ushahidi, ikiwemo kupata maelezo yake kuhusu tuhuma zinazomkabili, zinaendelea ili hatua nyingine za kisheria zifuatwe,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa ya Jeshi la Polisi imetolewa saa chache baada ya kusambaa kwa taarifa mitandaoni zikidai kuwa Thadei Kweka ametekwa nyara akiwa nyumbani kwao usiku wa kuamkia leo.

Address

P. O Box 105926
Dar Es Salaam
00225

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watetezitv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Watetezitv:

Share

Category