Watetezitv

Watetezitv WATETEZI TV is a Not-For-Profit online Tv under the Tanzania Human Rights Defenders Coalition(THRDC). Watetezi Tv operates in lieu of all applicable laws.

It will not be responsible to any subscriber who will post anything contrary to the applicable laws

Katika mwendelezo wa kesi yake, Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu ameibua hoja mahak...
10/10/2025

Katika mwendelezo wa kesi yake, Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu ameibua hoja mahak**ani kuhusu kitendo cha wageni wake kuzuiwa kuingia kusikiliza mwenendo wa kesi hiyo.

Akizungumza mbele ya jopo la majaji, Lissu amesema kuwa amepokea taarifa kwamba wageni wake wamezuiwa kuingia mahak**ani hadi watakapopata kibali kutoka Idara ya Uhamiaji, jambo ambalo amelieleza k**a ukiukwaji wa haki na ishara ya ukosefu wa uhuru wa mahak**a nchini.

“Naomba kukumbushia suala la wageni wangu waliozuiliwa kuingia mahak**ani. Nimeambiwa wameambiwa mpaka wapate kibali cha Idara ya Uhamiaji. Hawa ni wageni ambao wapo halali nchini, hivyo wataendelea kuwepo nchini labda wafukuzwe na uhamiaji. Tunataka dunia ijue k**a Tanzania kuna uhuru wa mahak**a au ni maneno tu. K**a kuna chombo kingine chenye mamlaka zaidi ya mahak**a hii, dunia inapaswa ijue. Jambo hili ni mtihani kwa mahak**a hii na kwa mahak**a ya Tanzania. Nitaendelea kusema, waheshimiwa majaji,” alisema Lissu.

Akijibu hoja hiyo, upande wa mahak**a ulieleza kuwa hadi kufikia jana, taarifa kutoka kwa Msajili wa Mahak**a zilionesha kuwa mgeni wa Lissu alitakiwa kuwasiliana na Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya kuthibitisha baadhi ya mambo, lakini aliahirisha hadi Jumatatu.

“Hadi kufikia jana tulipata taarifa kutoka kwa Msajili wa Mahak**a kwamba mgeni wako alitakiwa kuwasiliana na watu wa uhamiaji kwa ajili ya kuthibitisha vitu fulani fulani, lakini yeye alisema ataenda Jumatatu,” ilieleza mahak**a.

Lissu alisisitiza kuwa mgeni huyo ni wa kwake binafsi na si wa chama, hivyo ni yeye au ndugu zake pekee wanaoweza kumzungumzia.

“Huyo mgeni ni wa kwangu mimi, si mgeni wa chama, hivyo mimi au ndugu zangu ndiyo wanaoweza kumzungumzia maana ndio waliompokea,” alifafanua.

Majaji walihitimisha kwa kuelekeza ndugu wa Lissu kuwasiliana na Ofisi ya Msajili wa Mahak**a ili suala hilo lipatiwe ufumbuzi.

“Basi ndugu zako wawasialiane na ofisi ya Msajili wa Mahak**a ili hili jambo liishe,” walielekeza.

Kesi ya uhaini inayomkabili Tundu Lissu inaendelea leo mahak**a kuu, Masjala ndogo ya Dar es salaam.

10/10/2025

VIDEO: Wakili kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Paul Kisabo pamoja na viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiwemo Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara, John Heche, na Naibu Katibu Bara, Amani Golugwa, wamewasili katika Mahak**a Kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Dar es salaam kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji wa mwenendo wa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu.

Kesi hiyo, ambayo inaendelea kusikilizwa kwa mfululizo mbele ya jopo la Majaji watatu likiongozwa na Jaji Danstan Ndunguru, imepangwa kusikilizwa leo ambapo mshtakiwa Tundu Lissu, anayejitetea mwenyewe, ameanza kumuuliza maswali ya dodoso (cross-examination) shahidi wa pili wa Jamhuri, Inspekta wa Jeshi la Polisi John Kaaya.

09/10/2025

Mama mzazi wa mwanasiasa na aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, Bi Anna Mary, amewasili katika Mahak**a Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam kufuatilia kesi ya dharura iliyofunguliwa baada ya madai ya kutekwa kwa mwanawe alfajiri ya Oktoba 6, 2025.

Wakili wa Polepole, Peter Kibatala, ameiomba Mahak**a iingilie kati mara moja, akidai kuwa Polepole alitekwa nyumbani kwake Ununio, Kinondoni, na watu wasiojulikana wanaoshukiwa kuwa askari wa Jeshi la Polisi. Kibatala amesema Polepole hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote na familia inaamini anashikiliwa katika eneo lisilojulikana.

Katika maombi hayo, Kibatala ameitaka Mahak**a itoe amri ya kumfikisha Polepole mahak**ani ama mamlaka husika kueleze alipo. Kesi hiyo inasikilizwa mbele ya Jaji Salma Maghimbi, huku wajibu maombi wakiwa ni IGP, DPP, AG, RPC na RCO wa Dar es Salaam.

Bi Anna Mary, akiwa na huzuni na wasiwasi, alionekana akiingia mahak**ani na hakutaka kuzungumza na wanahabari.

Baadhi ya Wananchi, wanaharakati wamejitokeza kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo, wakitoa wito kwa serikali kutoa taarifa rasmi juu ya aliko Polepole. Wengine wameitaka Mahak**a kuhakikisha haki inapatikana kwa haraka, wakisema vitendo vya watu kutoweka katika mazingira ya kutatanisha vinapaswa kukomeshwa mara moja.

Tukio hili limezua mjadala mkubwa mitandaoni, wengi wakionyesha masikitiko na hofu juu ya hali ya usalama wa viongozi wa kisiasa na wanaharakati nchini. Wengine wametumia mitandao ya kijamii kuomba mamlaka kuhakikisha Polepole anapatikana akiwa salama.

Kesi hiyo imepewa kipaumbele maalum kutokana na uzito wa madai yaliyowasilishwa, huku Jaji Maghimbi akitarajiwa kutoa maamuzi ya awali baada ya kusikiliza hoja za pande zote.

Watanzania wengi wanaendelea kufuatilia kwa karibu tukio hili, wakitarajia kuona hatua za kisheria zikichukuliwa ili kurejesha imani ya wananchi kwa vyombo vya usalama na utawala wa sheria.

09/10/2025

Leo ni siku ya nne ya usikilizwaji wa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mheshimiwa Tundu Lissu, katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam. Usikilizwaji wa kesi hiyo umeanza huku Lissu akilalamikia hatua ya kuzuiwa kwa baadhi ya watu kuingia ndani ya ukumbi wa mahak**a kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa ushahidi, Lissu alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha kuwa maagizo ya mahak**a ya kuruhusu watu kuingia hayatekelezwi ipasavyo, jambo linaloashiria kuwa wapo watu wenye nguvu kuliko mahak**a yenyewe. Amesema hatua hiyo inashusha hadhi na heshima ya chombo hicho cha utoaji haki.

“Mimi sitaacha kulizungumza jambo hili kwa sababu halipo sawa kisheria. Watu wanapaswa kuruhusiwa kufuatilia mwenendo wa kesi hii k**a mahak**a ilivyoagiza,” alisema Lissu.

Kufuatia hoja hiyo, Jaji Dunstan Ndunguru ambaye anaongoza jopo la majaji wanaosikiliza kesi hiyo, alisema kuwa usikilizwaji wa kesi uendelee na akabainisha kuwa atalitolea ufafanuzi suala hilo baadaye.

Baada ya maelezo hayo, upande wa mashtaka uliendelea na mchakato wa kumuhoji shahidi wa kwanza wa Jamhuri, George Bagyemu, ambaye ni Naibu Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Kamishna Msaidizi wa Polisi. Leo, upande wa mashtaka unaendelea kumuuliza shahidi huyo maswali ya msawazisho ili kufafanua hoja mbalimbali zilizojitokeza wakati alipokuwa akihojiwa na upande wa utetezi.

Kwa mujibu wa hati ya wito wa kesi, usikilizwaji huo umepangwa kuendelea mfululizo kuanzia Oktoba 6 hadi Oktoba 24, 2025.

Tundu Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalohusiana na kauli alizozitoa kuhusu kuzuiwa kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, leo amehitimisha kumhoji shahidi wa kwanza wa up...
08/10/2025

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, leo amehitimisha kumhoji shahidi wa kwanza wa upande wa Jamhuri, kufuatia ushahidi alioutoa mahak**ani tarehe 6 Oktoba 2025.

Kesi hiyo, inayosikilizwa katika Mahak**a Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imeahirishwa hadi kesho Oktoba 9, 2025, saa tatu asubuhi, ambapo upande wa mashtaka unatarajiwa kuendelea kumuuliza shahidi huyo maswali ya msawazisho ili kufafanua hoja zilizojitokeza wakati wa maswali ya mshtakiwa.

Baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Lissu amerudishwa rumande kutokana na shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana. Hadi sasa ametimiza siku 183 tangu alipok**atwa Aprili 9, 2025.

Kwa mujibu wa hati ya wito wa mahak**a, usikilizaji wa kesi hiyo umepangwa kufanyika mfululizo kuanzia Oktoba 6 hadi Oktoba 24, 2025.

Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini, kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalotokana na maneno anayodaiwa kuyatoa kuhusu kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Baada ya kusambaa kwa taarifa mitandaoni kuhusu kutoweka kwa Rogers Yohana Ludovick (miaka 34), mkazi wa Kata ya Dumila,...
08/10/2025

Baada ya kusambaa kwa taarifa mitandaoni kuhusu kutoweka kwa Rogers Yohana Ludovick (miaka 34), mkazi wa Kata ya Dumila, wilayani Kilosa mkoani Morogoro, Jeshi la Polisi limesema limeanza uchunguzi wa kufuatilia tukio hilo na litatoa taarifa rasmi mara uchunguzi utakapokamilika.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi mkoani Morogoro iliyotolewa leo, Oktoba 8, 2025, tukio hilo linadaiwa kutokea Oktoba 7, 2025 majira ya mchana, ambapo inadaiwa kuwa Rogers alichukuliwa na watu watatu kutoka katika duka lake la miamala ya fedha na kuondoka naye kusikojulikana.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi unaendelea, huku likihimiza yeyote mwenye taarifa zinazoweza kusaidia kubaini ukweli wa tukio hilo kuwasilisha taarifa hizo ili ziweze kufanyiwa kazi.

Shirika la kimataifa la haki za binadamu, Amnesty International,  limetoa tamko dhidi ya serikali ya Tanzania likiitaka ...
08/10/2025

Shirika la kimataifa la haki za binadamu, Amnesty International, limetoa tamko dhidi ya serikali ya Tanzania likiitaka kutoa maelezo ya wazi kuhusu madai ya kutoweka kwa Humphrey Polepole, aliyewahi kuwa balozi wa Tanzania na anayejulikana kwa ukosoaji wake dhidi ya serikali.

Kwa mujibu wa taarifa ya Amnesty International, Polepole aliripotiwa kupotea mnamo Oktoba 6, baada ya tukio la uvamizi lililofanyika nyumbani kwake jijini Dar es Salaam. Familia yake ilipofika eneo la tukio, ilikuta mlango wa nyumba umevunjwa, nyaya za umeme zimekatwa, na mabaki ya damu yakionyesha dalili za mapambano makali kabla ya kutoweka kwake.

Mkurugenzi wa Kanda wa Amnesty International kwa Afrika Mashariki na Kusini, Tigere Chagutah, ameitaka serikali kuchukua hatua za haraka kuhakikisha Polepole anapatikana akiwa salama, pamoja na kufanya uchunguzi huru na wa wazi kuhusu tukio hilo.

“Tunatoa wito kwa serikali ya Tanzania kuhakikisha usalama wa Polepole na kuonyesha uwazi katika uchunguzi huu,” amesema Chagutah.

Amnesty International imesisitiza kuwa tukio hili linaibua wasiwasi mkubwa juu ya usalama wa wakosoaji wa serikali na hali ya haki za binadamu nchini Tanzania, ikitaka mamlaka kuhakikisha tukio k**a hilo halijirudii tena.

Wakili Peter Kibatala ameiomba Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam, iingilie kati kwa dharura kuhu...
08/10/2025

Wakili Peter Kibatala ameiomba Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam, iingilie kati kwa dharura kuhusu kupotea kwa mwanasiasa Humphrey Polepole.

Maombi hayo yamewasilishwa Oktoba 7, 2025, chini ya hati ya dharura, yakielekezwa dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Afisa Upelelezi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, pamoja na K**anda wa Polisi wa Kanda hiyo.

Kupitia maombi hayo, Kibatala anaiomba Mahak**a kutoa amri kwa mamlaka husika kuhakikisha Polepole anafikishwa mahak**ani au, k**a sivyo, kueleza hadharani ni wapi alipo tangu alipotekwa.

Kwa mujibu wa hati hiyo, Polepole alidaiwa kuchukuliwa alfajiri ya Jumatatu, Oktoba 6, 2025, nyumbani kwake eneo la Ununio, Kinondoni, na watu wanaoaminika kuwa askari wa Jeshi la Polisi. Tangu wakati huo, hajawahi kuonekana tena, wala kufikishwa mahak**ani kujibu tuhuma zozote.

Wakili Kibatala amesema kitendo hicho kinavunja haki za msingi za kikatiba, hasa uhuru wa mtu binafsi, na kuongeza kuwa familia na umma kwa ujumla wana haki ya kujua hali ya Polepole, afya yake, na iwapo bado yupo hai.

Kutokana na uzito na uharaka wa jambo hilo, Kibatala ameiomba Mahak**a isikilize maombi hayo haraka iwezekanavyo, akisisitiza kuwa ni suala nyeti linalogusa moja kwa moja haki za binadamu.

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imekataa ombi lililowasilishwa na mshtakiwa Tundu Lissu la kut...
07/10/2025

Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imekataa ombi lililowasilishwa na mshtakiwa Tundu Lissu la kutaka maelezo ya maandishi ya shahidi wa upande wa Jamhuri, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) George Wilbert Bagyemu, yakubaliwe k**a kielelezo katika kesi ya uhaini inayomkabili. Mahak**a imesema ombi hilo halikufuata utaratibu wa kisheria.

Uamuzi huo umetolewa wakati kesi hiyo ikiendelea kwa siku ya pili ya ushahidi wa ACP Bagyemu, ambaye ni Naibu Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) Kanda Maalum ya Dar es Salaam. Lissu, akiwa anamuuliza maswali ya dodoso shahidi huyo, aliomba maelezo yake ya maandishi yakubaliwe na mahak**a k**a kielelezo cha upande wa utetezi, ombi ambalo shahidi mwenyewe aliridhia.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulipinga ombi hilo kwa maelezo kuwa liliwasilishwa kinyume na taratibu, wakirejelea hukumu mbalimbali za Mahak**a ya Rufani ambazo zimefafanua masharti ya kupokea vielelezo vya aina hiyo.

Mawakili wa serikali walisisitiza kuwa, hata k**a shahidi amekubali, bado mahak**a inapaswa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, hivyo ombi la Lissu halina msingi wa kisheria.

Baada ya hoja hizo, Lissu alikiri kuwa kuna mapungufu katika uwasilishaji wa ombi hilo na kuomba kuruhusiwa kuanza upya kwa kufuata utaratibu sahihi. Hata hivyo, upande wa Jamhuri ulipinga hoja hiyo, ukibainisha kuwa kisheria haiwezekani kurudia hatua hiyo baada ya ombi kuwasilishwa kimakosa.

Akisoma uamuzi wa Mahak**a, Jaji Dunstan Ndunguru, akisaidiana na Majaji James Karayemana na Ferdinand Kiwonde, alisema Mahak**a inakubaliana na hoja za upande wa Jamhuri na hivyo inakataa ombi la Lissu, hasa ikizingatiwa kuwa mshtakiwa mwenyewe alikubali kuwa hakufuata taratibu sahihi.

Baada ya uamuzi huo, Lissu aliendelea na maswali ya dodoso kwa shahidi huyo wa Jamhuri, huku kesi ikiendelea kusikilizwa mbele ya jopo la majaji watatu wa Mahak**a Kuu.

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)  umelaani vikali utekwaji wa  Balozi Humphrey Polepole, mwanasi...
07/10/2025

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umelaani vikali utekwaji wa Balozi Humphrey Polepole, mwanasiasa na mkosoaji wa serikali, aliyechukuliwa na watu wasiojulikana usiku wa Oktoba 6, 2025 jijini Dar es Salaam na umetoa wito kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuingilia kati na kusaidia kupatikana kwa Polepole akiwa salama.

Polepole ambaye ni mwanachama wa CCM, aliyehudumu k**a Katibu wa Itikadi na Uenezi, Mbunge aliyeteuliwa, na Balozi wa Tanzania nchini Malawi na Cuba. Pia amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo na Musoma, Kwa wiki kadhaa, amekuwa mkosoaji wa wazi wa serikali, na kitendo hiki kinaibua hofu kubwa kuhusu usalama wake na mustakabali wa uhuru wa kujieleza nchini.

Kwa mujibu wa tamko lililotolewa leo Oktoba 07,2027, THRDC imesema tukio hili ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na shambulio dhidi ya demokrasia na uhuru wa kujieleza.

Kati ya mwaka 2024 na 2025, THRDC imerekodi zaidi ya matukio 100 ya utekaji na kupotezwa kwa wanaharakati na wanasiasa, mengi yakiwa hayajachunguzwa mpaka sasa.

"Kutokana na mwenendo huu wa utekaji na kupotezwa kwa raia, tunamshauri Rais Samia kusaini na kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kulinda Watu Dhidi ya Utekaji, pamoja na Mkataba wa Kupinga Mateso na Adhabu za Kikatili, Kinyama au Kudhalilisha"

THRDC imetoa wito kwa serikali na vyombo vya dola kutekeleza wajibu wao wa kulinda usalama wa raia wote na kuhakikisha wahusika wanawajibishwa kisheria, Pia inatoa wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati haraka, kuhakikisha Polepole anaokolewa akiwa salama, na kuanzisha chombo maalum cha kitaifa cha kupokea malalamiko dhidi ya vyombo vya usalama.

Aidha, THRDC inatoa rai kwa jumuiya ya kimataifa, vyombo vya habari na wananchi wote kusimama pamoja kulaani vitendo hivi vya ukiukwaji wa haki za binadamu.

Jeshi la Polisi nchini limesema limeanza uchunguzi rasmi kuhusu tuhuma zilizotolewa na Augustino Polepole kwamba ndugu y...
07/10/2025

Jeshi la Polisi nchini limesema limeanza uchunguzi rasmi kuhusu tuhuma zilizotolewa na Augustino Polepole kwamba ndugu yake, Humphrey Polepole, ametekwa. Taarifa hiyo imetolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi kutoka Makao David Misime, ikieleza kuwa jalada la uchunguzi lilifunguliwa mara baada ya taarifa hizo kutolewa jana, Oktoba 6, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Jeshi la Polisi limesema limeanza kukusanya taarifa mbalimbali zinazohusiana na madai hayo na linaendelea kumtafuta Augustino Polepole ili kutoa maelezo ya kina pamoja na ushahidi wa tuhuma alizozitoa, hasa kuhusu madai kwamba afisa wa Jeshi la Polisi alihusika katika tukio hilo la utekaji.

Polisi pia wameeleza kuwa wanataka kuthibitisha iwapo Humphrey Polepole alikuwa mkazi au mpangaji wa nyumba inayodaiwa kuwa tukio hilo lilitokea, k**a ilivyoelezwa na Augustino kupitia mitandao ya kijamii.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuwa watulivu na kuepuka kusambaza taarifa zisizothibitishwa, huku likiahidi kutoa mrejesho kwa umma mara uchunguzi utakapokamilika.

Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho katika...
06/10/2025

Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi kesho katika Mahak**a Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.

Kuahirishwa huko kumetokea baada ya Lissu kuanza kumuuliza maswali shahidi wa kwanza wa Jamhuri, ACP George Wilbert, ambaye ni Naibu Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam (RCO). Kesho, Lissu anatarajiwa kuendelea na mchakato huo wa kumhoji shahidi huyo.

Lissu anakabiliwa na shtaka moja la uhaini, kinyume na Kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalohusishwa na maneno anayodaiwa kuyatoa kuhusu kuzuia kufanyika kwa uchaguzi mkuu ujao.

Mahak**a itaendelea kusikiliza ushahidi na hoja za pande zote kesho.

Address

P. O Box 105926
Dar Es Salaam
00225

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watetezitv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Watetezitv:

Share

Category