
10/10/2025
Katika mwendelezo wa kesi yake, Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu ameibua hoja mahak**ani kuhusu kitendo cha wageni wake kuzuiwa kuingia kusikiliza mwenendo wa kesi hiyo.
Akizungumza mbele ya jopo la majaji, Lissu amesema kuwa amepokea taarifa kwamba wageni wake wamezuiwa kuingia mahak**ani hadi watakapopata kibali kutoka Idara ya Uhamiaji, jambo ambalo amelieleza k**a ukiukwaji wa haki na ishara ya ukosefu wa uhuru wa mahak**a nchini.
“Naomba kukumbushia suala la wageni wangu waliozuiliwa kuingia mahak**ani. Nimeambiwa wameambiwa mpaka wapate kibali cha Idara ya Uhamiaji. Hawa ni wageni ambao wapo halali nchini, hivyo wataendelea kuwepo nchini labda wafukuzwe na uhamiaji. Tunataka dunia ijue k**a Tanzania kuna uhuru wa mahak**a au ni maneno tu. K**a kuna chombo kingine chenye mamlaka zaidi ya mahak**a hii, dunia inapaswa ijue. Jambo hili ni mtihani kwa mahak**a hii na kwa mahak**a ya Tanzania. Nitaendelea kusema, waheshimiwa majaji,” alisema Lissu.
Akijibu hoja hiyo, upande wa mahak**a ulieleza kuwa hadi kufikia jana, taarifa kutoka kwa Msajili wa Mahak**a zilionesha kuwa mgeni wa Lissu alitakiwa kuwasiliana na Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya kuthibitisha baadhi ya mambo, lakini aliahirisha hadi Jumatatu.
“Hadi kufikia jana tulipata taarifa kutoka kwa Msajili wa Mahak**a kwamba mgeni wako alitakiwa kuwasiliana na watu wa uhamiaji kwa ajili ya kuthibitisha vitu fulani fulani, lakini yeye alisema ataenda Jumatatu,” ilieleza mahak**a.
Lissu alisisitiza kuwa mgeni huyo ni wa kwake binafsi na si wa chama, hivyo ni yeye au ndugu zake pekee wanaoweza kumzungumzia.
“Huyo mgeni ni wa kwangu mimi, si mgeni wa chama, hivyo mimi au ndugu zangu ndiyo wanaoweza kumzungumzia maana ndio waliompokea,” alifafanua.
Majaji walihitimisha kwa kuelekeza ndugu wa Lissu kuwasiliana na Ofisi ya Msajili wa Mahak**a ili suala hilo lipatiwe ufumbuzi.
“Basi ndugu zako wawasialiane na ofisi ya Msajili wa Mahak**a ili hili jambo liishe,” walielekeza.
Kesi ya uhaini inayomkabili Tundu Lissu inaendelea leo mahak**a kuu, Masjala ndogo ya Dar es salaam.