07/06/2026
Leo, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Zanzibar Suleiman Mujuni Baitan ameshiriki k**a mShereheshaji katika Kongamano na Mkutano Mkuu wa 26 wa Chama cha Wanasheria Zanzibar, ZLS, uliofanyika Golden Tulip Zanzibar Airport Hotel.
Kongamano hili limewakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za sheria na haki, jumuiya ya wanasheria, wadau wa maendeleo pamoja na asasi za kiraia kujadili nafasi ya taaluma ya sheria katika kuimarisha utawala wa sheria, ufanisi wa mahak**a na upatikanaji wa haki kwa wananchi.
Kaulimbiu ya mwaka huu, “Kukumbatia Mabadiliko ya Kidijitali kwa ajili ya Upatikanaji wa Haki kwa Ufanisi na Urahisi Zanzibar,” imeweka msisitizo kwenye matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma za haki, kuongeza ufanisi wa mifumo ya mahak**a, kurahisisha utoaji wa huduma za kisheria na kupanua upatikanaji wa haki kwa wananchi.
Kwa THRDC Zanzibar, ushiriki huu ni sehemu ya kuendeleza ushirikiano wa kimkakati kati ya asasi za kiraia, jumuiya ya wanasheria na taasisi za haki katika kulinda haki za binadamu, kuimarisha utawala wa sheria na kujenga mazingira salama kwa watetezi wa haki za binadamu.
LegalProfession DigitalJustice HumanRightsDefender