Watetezitv

Watetezitv WATETEZI TV is a Not-For-Profit online Tv under the Tanzania Human Rights Defenders Coalition(THRDC). Watetezi Tv operates in lieu of all applicable laws.

It will not be responsible to any subscriber who will post anything contrary to the applicable laws

Leo, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Zanzibar   Suleiman Mujuni Baitan ameshiriki k**a mShereheshaji ...
07/06/2026

Leo, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Zanzibar Suleiman Mujuni Baitan ameshiriki k**a mShereheshaji katika Kongamano na Mkutano Mkuu wa 26 wa Chama cha Wanasheria Zanzibar, ZLS, uliofanyika Golden Tulip Zanzibar Airport Hotel.

Kongamano hili limewakutanisha viongozi wa Serikali, taasisi za sheria na haki, jumuiya ya wanasheria, wadau wa maendeleo pamoja na asasi za kiraia kujadili nafasi ya taaluma ya sheria katika kuimarisha utawala wa sheria, ufanisi wa mahak**a na upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Kaulimbiu ya mwaka huu, “Kukumbatia Mabadiliko ya Kidijitali kwa ajili ya Upatikanaji wa Haki kwa Ufanisi na Urahisi Zanzibar,” imeweka msisitizo kwenye matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma za haki, kuongeza ufanisi wa mifumo ya mahak**a, kurahisisha utoaji wa huduma za kisheria na kupanua upatikanaji wa haki kwa wananchi.

Kwa THRDC Zanzibar, ushiriki huu ni sehemu ya kuendeleza ushirikiano wa kimkakati kati ya asasi za kiraia, jumuiya ya wanasheria na taasisi za haki katika kulinda haki za binadamu, kuimarisha utawala wa sheria na kujenga mazingira salama kwa watetezi wa haki za binadamu.

LegalProfession DigitalJustice HumanRightsDefender

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Pemba kimetangaza kumfukuza uanachama Ndugu Said Issa Mohammed baad...
07/06/2026

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Pemba kimetangaza kumfukuza uanachama Ndugu Said Issa Mohammed baada ya kubainika kuwa amekiuka Katiba, Kanuni na Miongozo ya Chama.

Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha dharura cha Kamati Tendaji ya Kanda ya Pemba kilichofanyika tarehe 6 Juni 2026 katika Ukumbi wa Pride ya Zamani, Chake Chake, Pemba. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Kanda, Mheshimiwa Omar Nassor, kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za Chama.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Kanda, Abdulla Hassan, ajenda kuu ya kikao hicho ilikuwa kujadili suala la nidhamu linalomhusu Said Issa Mohammed. Kamati ilipokea na kujadili taarifa iliyowasilishwa mbele yake na kufanya tathmini kwa kuzingatia masharti ya Katiba, Kanuni na Miongozo ya CHADEMA.

Baada ya kujiridhisha kuwa Ndugu Said Issa Mohammed amekiuka misingi na taratibu za Chama, Kamati Tendaji ya Kanda ya Pemba iliazimia kumfukuza uanachama wa CHADEMA kuanzia tarehe 6 Juni 2026.

Kutokana na uamuzi huo, CHADEMA Kanda ya Pemba imeutaarifu umma na wanachama wake kwamba kuanzia tarehe hiyo, Said Issa Mohammed si mwanachama wa Chama na hatambuliki tena k**a kiongozi au mwakilishi wa CHADEMA katika ngazi yoyote.

Chama kimesisitiza kuwa kauli, matendo au shughuli zozote atakazozifanya baada ya tarehe ya kufukuzwa kwake zitakuwa za kwake binafsi na hazitahusishwa kwa namna yoyote na CHADEMA.

Taarifa hiyo imetolewa leo, Jumapili tarehe 7 Juni 2026, na Katibu wa Kanda ya Pemba, Abdulla Hassan.

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, ameagiza kufutwa mara moja kwa makundi yot...
07/06/2026

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, ameagiza kufutwa mara moja kwa makundi yote ya WhatsApp yanayotumiwa kuchochea migogoro na migawanyiko ndani ya chama, akisisitiza kuwa CCM haiwezi kuendeshwa kupitia malumbano ya mitandaoni.

Wasira ametoa agizo hilo mjini Moshi baada ya mwanachama mmoja kueleza kuwepo kwa makundi mbalimbali ya WhatsApp ambayo baadhi ya wanachama wamekuwa wakiyatumia kurushiana maneno makali, kueneza migogoro na wakati mwingine kuwakashifu viongozi wa chama.

Akizungumza katika mkutano huo, Wasira amesema tofauti za maoni na mijadala ya ndani ya chama zinapaswa kujadiliwa kupitia vikao rasmi vinavyoongozwa na Katiba na Kanuni za CCM, badala ya kufanyika kwenye mitandao ya kijamii ambayo inaweza kusababisha taharuki na kudhoofisha mshik**ano wa wanachama.

“Makundi hayo yafutwe. Ndani ya chama chetu kuna mambo ya siri yanayopaswa kujadiliwa katika vikao husika. Kuyajadili kwenye makundi ya WhatsApp ni matumizi mabaya ya teknolojia,” amesema Wasira.

Kufuatia agizo hilo, baadhi ya wasimamizi wa makundi mbalimbali ya WhatsApp mkoani Kilimanjaro, yakiwemo Moshi ya Moto, Moshi Kwanza Group na Moshi ya Maendeleo, wameanza kuyafunga makundi hayo huku wakisubiri maelekezo zaidi kutoka kwa viongozi wa chama.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha nidhamu, mshik**ano na utunzaji wa siri za chama kuelekea utekelezaji wa shughuli zake za kisiasa na kiutawala.

Mahak**a ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu imeiamuru Serikali ya Tanzania kufanya marekebisho katika Kanuni ya Adhab...
06/06/2026

Mahak**a ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu imeiamuru Serikali ya Tanzania kufanya marekebisho katika Kanuni ya Adhabu kwa kuondoa adhabu ya kifo ya lazima kwa watu wanaopatikana na hatia ya mauaji pamoja na kuacha matumizi ya kunyonga k**a njia ya kutekeleza adhabu hiyo.

Uamuzi huo unaigusa moja kwa moja Kanuni ya Adhabu ya Tanzania, hususan Kifungu cha 197, ambacho kwa sasa kinaelekeza adhabu moja tu kwa kosa la mauaji, adhabu ya kifo kwa kunyongwa, bila kumpa jaji mamlaka ya kuzingatia adhabu mbadala kulingana na mazingira ya kila kesi.

Mahak**a imeeleza kuwa adhabu ya kifo ya lazima inakiuka haki za msingi za binadamu, ikiwemo haki ya kuishi inayolindwa na Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu, ambao Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizouridhia.

Hukumu hiyo ilitolewa Juni 5, 2026 na jopo la majaji wanane wa Mahak**a ya Afrika wakiongozwa na Rais wa Mahak**a hiyo, Blaise Tchikaya, pamoja na Makamu wa Rais, Chafika Bensaoula.

Maamuzi hayo yametokana na mashauri matatu tofauti yaliyowasilishwa mahak**ani na wafungwa saba waliokuwa wamehukumiwa adhabu ya kifo kwa makosa ya mauaji na kusubiri utekelezaji wa hukumu hiyo katika magereza mbalimbali nchini Tanzania.

Katika maombi yao, wafungwa hao walidai kuwa Serikali ya Tanzania ilikiuka haki zao za msingi zinazotambuliwa chini ya Mkataba wa Afrika, ikiwemo haki ya kuishi, haki ya utu wa binadamu, haki ya kusikilizwa kwa haki, haki ya kupata uwakilishi wa kisheria na haki ya kusikilizwa kwa mashauri yao ndani ya muda unaofaa.

Mahak**a imeagiza Tanzania kuchukua hatua za kisheria na kisera kurekebisha sheria husika ili kuendana na viwango vya haki za binadamu vinavyotambuliwa kimataifa na kikanda.

Watetezi wa haki za binadamu Jackson Martine Kabalo na Joseph Chaviruka Mrindoko, maarufu k**a “Wachokonozi”, wameachiwa...
06/06/2026

Watetezi wa haki za binadamu Jackson Martine Kabalo na Joseph Chaviruka Mrindoko, maarufu k**a “Wachokonozi”, wameachiwa huru na Mahak**a ya Wilaya ya Arumeru baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuendelea na ushahidi katika Shauri la Jinai Na. 000017735/2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) leo Juni 6,2026, shauri hilo lilikuwa limepangwa kusikilizwa Mei 26, 27 na 28 mwaka 2026 pamoja na Juni 4 na 5 mwaka huohuo. Katika tarehe hizo zote, upande wa Jamhuri uliwasilisha shahidi mmoja pekee mnamo Mei 26, ambaye alikuwa shahidi wa saba wa upande wa mashtaka.

THRDC imeeleza kuwa katika siku zilizofuata za usikilizwaji wa kesi hiyo, upande wa mashtaka haukuwa na mashahidi wa kuendelea kutoa ushahidi wala haukutoa sababu za msingi kueleza kutokuwepo kwao. Hali hiyo ilisababisha shauri kushindwa kuendelea k**a ilivyokuwa imepangwa na Mahak**a.

Mahak**a ilibainisha kuwa tayari ilikuwa imetoa maelekezo ya kuhakikisha kesi hiyo inasikilizwa kwa wakati kutokana na muda mrefu uliokuwa umepita tangu kufunguliwa kwake. Aidha, ilisisitiza umuhimu wa kutenda haki bila ucheleweshaji usio wa lazima kwa mujibu wa misingi ya sheria.

Kutokana na kushindwa kwa upande wa mashtaka kuendelea na ushahidi, Mahak**a ya Wilaya ya Arumeru iliamuru wash*takiwa waachiwe huru chini ya Kifungu cha 242(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20, Marejeo ya Mwaka 2023.

Kesi hiyo ilianzia katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Arusha k**a Shauri la Jinai Na. 15727/2025. Julai 27, 2025, upande wa Jamhuri uliomba kuondolewa kwa shauri hilo kwa maelezo kuwa haukuwa tayari kuendelea nalo, na Mahak**a ikaamuru wash*takiwa waachiwe huru. Hata hivyo, siku hiyo hiyo walik**atwa tena na kufikishwa Mahak**a ya Wilaya ya Arumeru wakikabiliwa na mashtaka yale yale.

Mashtaka yaliyokuwa yanawakabili ni kutoa taarifa za uongo mtandaoni na kufanya shughuli za utoaji wa maudhui mtandaoni bila leseni. Katika kipindi chote cha kesi hiyo, walitetewa na mawakili wa THRDC, Simon Mbwambo na Ally Mhyellah.

05/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limewak**ata watu 75 katika Kata ya Idukilo, Wilaya ya Kishapu, kwa tuhuma za kuhusika katika vitendo vya vurugu na kuwashambulia viongozi wa serikali waliokuwa wakitekeleza majukumu yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Juni 5, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi, amesema hatua hiyo imechukuliwa kufuatia matukio ya uvunjifu wa amani yaliyoripotiwa katika kata hiyo.

Kwa mujibu wa Magomi, watuhumiwa wanadaiwa kuwazuia viongozi na watumishi wa umma kutekeleza majukumu yao kwa madai ya kutoridhishwa na matokeo ya uchaguzi wa udiwani yaliyotangazwa baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.

Amesema baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakisisitiza kuwa mgombea wa ACT-Wazalendo ndiye aliyeshinda uchaguzi huo, licha ya matokeo rasmi kumtangaza mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi.

Kamanda Magomi amesema tukio kubwa lilitokea Mei 28, 2026 katika Kijiji cha Sanjo, ambapo Mtendaji wa Kata, Masende Msele, Afisa Maendeleo ya Jamii, Rozi Shao, pamoja na viongozi wengine wa kijiji walishambuliwa walipokuwa wakitekeleza zoezi la kuandikisha kaya zenye uhitaji kwa ajili ya mpango wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

“Watuhumiwa waliwashambulia viongozi hao, kuwajeruhi na kuharibu baadhi ya nyaraka zilizokuwa zikitumika katika zoezi hilo. Baada ya tukio walisisitiza kuwa hawataki viongozi wa serikali kufanya kazi katika kata hiyo,” amesema Magomi.

Ameongeza kuwa hali hiyo imeathiri utoaji wa huduma za serikali katika eneo hilo, ambapo baadhi ya watumishi wamesitisha shughuli zao huku wengine wakidaiwa kujiuzulu kutokana na hofu ya usalama wao.

Kamanda Magomi amesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea na kwamba Jeshi la Polisi halitavumilia vitendo vya uvunjifu wa amani, mashambulizi dhidi ya watumishi wa umma wala jaribio lolote la kuzuia utekelezaji wa shughuli za serikali.

Aidha, amewataka wananchi kufuata sheria na taratibu zilizowekwa katika kutatua migogoro na kutokuchukua sheria mkononi.

Mratibu wa THRDC Zanzibar  pamoja na Mkurugenzi wa ZAFELA  wamekuwa wenyeji wa kikao kazi cha Mradi wa SCATZ, unaofadhil...
05/06/2026

Mratibu wa THRDC Zanzibar pamoja na Mkurugenzi wa ZAFELA wamekuwa wenyeji wa kikao kazi cha Mradi wa SCATZ, unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya.

Kikao hicho kimewashirikisha Wakurugenzi kutoka Chama cha Mawakili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALS) na Jumuiya ya Mawakili wa Afrika (PALU), pamoja na Mratibu wa Kitaifa wa THRDC na timu ya watendaji wataalamu wanaotekeleza mradi huo.

Majadiliano yalilenga kuangalia mwenendo wa utekelezaji wa mradi, kuimarisha uratibu kati aya asasi za kiraia na vyama vya mawakili, pamoja na kuweka mikakati ya pamoja ya kukuza utawala wa sheria, uwajibikaji wa taasisi, ulinzi wa haki za binadamu na nafasi ya kiraia Tanzania Bara na Zanzibar.

Kupitia SCATZ, THRDC Zanzibar, ZAFELA, EALS, PALU na wadau wengine wanaendelea kujenga ushirikiano wa kimkakati katika kutumia taaluma ya sheria na kazi za asasi za kiraia k**a nyenzo muhimu za kulinda haki, kuimarisha uwajibikaji na kuchangia mifumo bora ya haki kwa wananchi.

Accountability Zanzibar

Mratibu wa  Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania Zanzibar (THRDC Zanzibar) , ameshiriki  Kongamano la Uwekez...
05/06/2026

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania Zanzibar (THRDC Zanzibar) , ameshiriki Kongamano la Uwekezaji Zanzibar 2026 (Investment Summit 2026) jukwaa muhimu linalokutanisha Serikali, sekta binafsi, wawekezaji, taasisi za maendeleo na wadau wa kijamii kujadili mustakabali wa ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.

Ushiriki huu unaakisi umuhimu wa kuunganisha ajenda ya uwekezaji na misingi ya haki za binadamu, utawala bora na uwajibikaji wa kibiashara. Sekta binafsi ina nafasi kubwa katika kukuza uchumi, ajira na ubunifu, lakini ukuaji huo unapaswa kwenda sambamba na kuheshimu haki za wafanyakazi, haki za jamii, mazingira, usawa wa kijinsia, ushirikishwaji wa vijana na watu wenye ulemavu, pamoja na uwazi katika maamuzi ya maendeleo.

Asasi za kiraia zina mchango muhimu katika kuhakikisha uwekezaji unakuwa jumuishi, wenye tija kwa wananchi, na unaozingatia wajibu wa biashara kuheshimu haki za binadamu. Ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na asasi za kiraia ni msingi wa kujenga mazingira ya uwekezaji yanayoaminika, salama na yanayolinda maslahi ya umma.

THRDC Zanzibar itaendelea kushiriki katika mijadala ya kitaifa inayolenga kuimarisha maendeleo, uwekezaji wenye uwajibikaji na ulinzi wa haki za binadamu katika Zanzibar.

ZanzibarDevelopment

Dunia leo inaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, inayofanyika kila mwaka Juni 5, ikiwa na kaulimbiu isemayo “Inspired b...
05/06/2026

Dunia leo inaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, inayofanyika kila mwaka Juni 5, ikiwa na kaulimbiu isemayo “Inspired by Nature. For Climate. For Our Future” (Tuhamasishwe na Asili. Kwa Ajili ya Hali ya Hewa. Kwa Mustakabali Wetu). Kaulimbiu hiyo inalenga kuhamasisha jamii kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kutumia suluhisho zinazotokana na asili pamoja na kulinda mifumo ya ikolojia kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. 

Akizungumza leo Juni 5,2026 katika maadhimisho hayo, Mratibu wa Dawati la Mazingira wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Mazingira Walio Mstari wa Mbele (NET-FEHRD) , Agness Godfrey , amesema mustakabali wa dunia unategemea maamuzi yanayofanywa na jamii kwa sasa.

“Mustakabali wetu unategemea uchaguzi tunaoufanya leo. Tuiruhusu asili ituhamasishe kuchukua hatua za ujasiri kwa ajili ya hali ya hewa, kulinda bioanuwai na kujenga dunia ya kijani kwa manufaa ya kila mtu,” amesema Agness.

Ameeleza kuwa changamoto za mabadiliko ya tabianchi, uharibifu wa mazingira na kupungua kwa bioanuwai zinaendelea kuathiri maisha ya watu duniani kote, hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha juhudi za uhifadhi wa misitu, vyanzo vya maji na mifumo mingine ya asili inayochangia ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi.

Kaulimbiu ya mwaka huu inaweka msisitizo katika kutambua mchango wa asili k**a sehemu muhimu ya suluhisho za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kujenga jamii endelevu. 

Siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa kila mwaka chini ya uratibu wa Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP) na imeendelea kuwa jukwaa kubwa la kimataifa la kuhamasisha ulinzi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali za asili. 

Jeshi la Polisi Wilaya ya Mufindi linamshikilia mwalimu mlezi wa Shule ya Sekondari Bukimau pamoja na wanafunzi tisa kwa...
05/06/2026

Jeshi la Polisi Wilaya ya Mufindi linamshikilia mwalimu mlezi wa Shule ya Sekondari Bukimau pamoja na wanafunzi tisa kwa ajili ya mahojiano kufuatia tukio la kuuawa kwa mwanafunzi mmoja wa shule hiyo iliyopo Kata ya Bumilayinga, Halmashauri ya Mji wa Mafinga.

Mwanafunzi aliyefariki dunia ametambulika kuwa ni Kojak Ungele (19), mwanafunzi wa kidato cha nne. Inadaiwa kuwa alifariki usiku wa kuamkia Juni 1, 2026, baada ya kushambuliwa na wanafunzi wenzake kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa mashine ya kunyolea nywele pamoja na redio.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, baada ya tukio hilo Kojak alikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Nyororo kwa ajili ya matibabu. Hata hivyo, alifariki dunia kabla ya kufikishwa katika kituo hicho.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo huku mwalimu mlezi na wanafunzi tisa wakishikiliwa ili kusaidia kukamilisha uchunguzi.

Akizungumza kwa masikitiko, baba mzazi wa marehemu, Emily Ungele, amesema familia bado haijaridhishwa na maelezo yaliyotolewa kuhusu mazingira ya kifo cha mtoto wao.

“Familia bado haijaridhishwa na maelezo tuliyopatiwa kuhusu mazingira ya kifo cha mtoto wetu. Bado kuna maswali mengi yanayohitaji majibu,” amesema.

Address

P. O Box 105926
Dar Es Salaam
00225

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watetezitv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Watetezitv:

Share

Category