Koncept TV

Koncept TV Pata Habari za Hivi Punde/Kitaifa/Kimataifa/Biashara na Uchumi/Siasa, Michezo/Burudani/Teknolojia na Hamasa Whatsapp ; 0658123310



Like Page Upate Uhondo.

Pata Habari za Hivi Punde/Kitaifa/Kimataifa/Biashara na Uchumi/Siasa, Michezo/Burudani/Teknolojia na Hamasa


LIKE PAGE Kisha Tembelea Website Yetu Kupata UHONDO Zaidi

12/10/2025

Mwanaume mmoja huko Nigeria aneacha Mkewe apigwe na Mfanya kazi wake baada ya kuona Mfanyakazi amechoka kuonewa na Mwanamke huyo.

12/10/2025

Mdudu Hatari hasa kwa Wadudu wenzake wanaojaribu kumdhuri mfano Mijusi na wadudu wengine Wadogowadogo Mdudu huyu Bombadia Battler anatabia ya Kutoa sumu yenye Kemikali hatari na yenye Joto ambayo inaua wadudu wenzake.

11/10/2025

Marubani wa ndege moja hawapaswi kula chakula kinachoshabiliana wakati wa safari moja.

11/10/2025

Slot: ni miongoni mwa Wanyama wanaolala zaidi Duniani, wanalala kati ya saa 18 - 22 kwa siku. Chakula chao kikuu ni Majani ambayo hayana virutubisho vya kutosha na ni magumu kumeng’enywa.

11/10/2025

Katika Misitu mingi Afrika na hata Ulaya kuna hawa Ndege wa ajabu wanaoitwa Woodpecker wanaweza kudonoa Miti bila kuumia wala kuathirika Ubongo. Wanaweza kudonoa Mara 20 kwa Sekunde Moja tu.

HABARI:  Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Songea, Damian Dallu, ametangaza kutoweka kwa Padri Camillus Nikata...
10/10/2025

HABARI: Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Songea, Damian Dallu, ametangaza kutoweka kwa Padri Camillus Nikata, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (SAUT), Mwanza.

Katika taarifa yake iliyotolewa leo, Askofu Dallu amesema kuwa Padri Nikata haonekani wala hapatikani kwa simu. Askofu Dallu amesema padri alikuwa ametokea Dodoma kwenye mafundisho ya moyo ya mapadri wanaofundisha katika vyuo vikuu vya TEC, akiwa na mhadhiri mwenzake wa Jimbo.

Inaelezwa kuwa alipanga kusafiri kwenda Mwanza Oktoba 8, 2025 kwa basi la Super Feo, na tayari alikuwa amenunua tiketi kwa njia ya mtandao. Taarifa inazidi kueleza kuwa, walipoanza kuangalia Jumatano mchana, waligundua kuwa hakusafiri kwani mzigo wake ulikuwa bado umebaki katika chumba chake kilichofungwa, na ufunguo haukurudishwa kwa mtumishi wa nyumba ya mapadri.

Jitihada za kumtafuta kwa simu na kuulizia kwa watu waliokuwa naye hazikuzaa matunda, na alikosekana pia Mwanza, mahali alipokuwa amepanga kufika. Ofisi ya mabasi ya Super Feo ilithibitisha kuwa hakusafiri kwa basi hilo. Baada ya kushindikana kwa jitihada za kumtafuta Padri Nikata, Askofu Dallu amesema kuwa tayari wameshatoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ili msaada zaidi upatikane na kumtafuta padri huyo.

10/10/2025

Ndege hawa ni Muhimu sana kwa Wanyama Porini hasa wenye Majeraha.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia kijana aitwaye Piere Saimoni (20), mkazi wa Nzuguni B kwa tuhuma za kujihus...
10/10/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia kijana aitwaye Piere Saimoni (20), mkazi wa Nzuguni B kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ubakaji. Kijana huyo anatuhumiwa kuwabaka wanawake wanne wa Mtaa wa Nzuguni B Oktoba 5, 2025.

Baada ya kutokea tukio hilo, Polisi na wananchi wa mtaa huo walifanikiwa kumk**ata mtuhumiwa baada ya kufanyika msako maalumu. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mbinu ya kuingia kwa siri katika nyumba anamoishi mwanamke anayemlenga na kutekeleza kitendo hicho kwa kutumia vitisho vya kujeruhi.

Katika uchunguzi wa awali uliofanywa na Jeshi la Polisi, imebainika kuwa mtuhumiwa huyo anaishi katika nyumba moja na watu wengine 13. Mtuhumiwa atafikishwa mahak**ani mara tu taratibu za kisheria zitakapokamilika. Polisi Mkoa wa Dodoma inatoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu pamoja na kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi ili kudumisha amani na usalama katika jamii.

10/10/2025

Pangolin au Kaka kuona, Tamaduni nyingi huamini k**a ni Mnyama waajabu anayeweza kuitambua kesho. Mnyama huyu hupatika kwa nadra sana na wanasema ukimuona ni Bahati kwako/wewe unabahati. Wewe unaonaje?

Mgombea mteule wa nafasi ya udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Kata ya Ng’apa, Jimbo la Lindi Mjini, Ndugu...
30/09/2025

Mgombea mteule wa nafasi ya udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Kata ya Ng’apa, Jimbo la Lindi Mjini, Ndugu Issa Ngasha, amewaomba wananchi wa kata hiyo kuiamini CCM na kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Ng’apa katika uzinduzi rasmi wa kampeni uliofanyika Septemba 29, 2025, Ngasha amesema atatumia nafasi hiyo kufanya kazi kwa bidii katika kuhakikisha changamoto zinazowakabili wananchi wa kata hiyo zinatatuliwa.

Ngasha pia amewaomba wananchi waendelee kumuunga mkono Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya urais, Mohammed Utaly kwa nafasi ya ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini, pamoja na yeye mwenyewe kwa nafasi ya udiwani.

“Mimi ni kijana wenu mliyenilea. Tukishirikiana, nitapeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi kwa uaminifu na sitowaangusha ndugu zangu wa Ng’apa,” alisema.

Uzinduzi huo uliambatana na shamrashamra na hamasa kubwa kutoka kwa wanachama wa CCM na wakazi wa kata hiyo ambapo mgeni rasmi, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Wilaya ya Lindi Mjini, Ndugu Jamadin Mandoa, amewasihi wananchi kumuunga mkono Ngasha, akimwelezea k**a kiongozi mwenye maono, uaminifu na uzoefu wa kutosha.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARIVODACOM TANZANIA PLC PAMOJA NA CHAMA CHA GOFU TANZANIA WAUNGANA ILI KUUNGA MKONO MCHEZO WA ...
24/09/2025

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
VODACOM TANZANIA PLC PAMOJA NA CHAMA CHA GOFU TANZANIA WAUNGANA ILI KUUNGA MKONO MCHEZO WA GOFU NCHINI.
Dar es Salaam, 23 Septemba 2025: Vodacom Tanzania Plc kwa kushirikiana na Chama cha Gofu Tanzania, imejitokeza k**a mdhamini mkuu wa mashindano ya Vodacom Tanzania Open, yanayotarajia ushiriki wa wachezaji zaidi ya 150 wa gofu kutoka Tanzania na nchi za mashariki na kusini mwa Afrika
Ushirikiano huu ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuendeleza michezo ya gofu katika msimu wa tatu hapa jijini Dar es Salaam na visiwani Zanzibar. Vodacom ikiwa inaadhimisha miaka 25 inalenga kujikita k**a mtandao namba moja unaounga mkono mchezo wa gofu nchini Tanzania.
Tanzania Open si mashindano pekee, bali ni jukwaa la kuonesha vipaji, mshik**ano katika michezo na ubunifu wa kidijitali. Kupitia ubia huu, Vodacom inaleta mapinduzi katika mchezo wa gofu kwa kuunganisha urithi wa mchezo huu na teknolojia ya kisasa, huku ikikuza ushirikishwaji wa jamii na ujumuishi kwenye michezo.
Akizungumza katika uzinduzi wa mashindano haya, Mkuu wa idara ya masoko na uwezeshaji Vodacom Business, Joseph Sayi, alisema:
“Ushirikiano wetu na Tanzania Open unaonyesha dhamira ya Vodacom katika kukuza michezo nchini Tanzania huku tukionesha namna teknolojia inavyoweza kuboresha maisha ya wananchi hata kupitia michezo. Kuanzia huduma za mtandao hadi huduma za malipo kwa kutumia M-Pesa, tunahakikisha kila mmoja anapata uzoefu wa kipekee ndani na nje ya uwanja.”
Pia, mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania, Gilman Kasiga, alisema:
Mashindano ya Vodacom Tanzania Open 2025 ni tukio la kihistoria kwa mchezo wa gofu na kwa taifa letu. Kwa mwaka wa tatu mfululizo, Vodacom imeendelea kuwa bega kwa bega nasi k**a mdhamini mkuu, jambo linalodhihirisha dhamira yao ya kuendeleza michezo na kukuza vipaji nchini. K**a mashindano makuu ya Chama cha Gofu Tanzania, Vodacom Tanzania Open siyo tu jukwaa la kuonesha umahiri wa wachezaji wetu wa kulipwa na wale wa kiwango cha juu, bali pia ni chanzo cha hamasa na matumaini kwa kizazi kipya cha wachezaji.
Tunajivunia kuona vijana, wanawake, na wachezaji chipukizi wakishiriki kwa pamoja, jambo linaloashiria dhamira ya dhati ya TGU katika kukuza ushirikishwaji, maendeleo, na ukuaji endelevu wa mchezo huu. Kupitia ushirikiano wetu naVodacom, tunaonesha namna ambavyo gofu si mchezo pekee bali ni nyenzo ya kukuza utalii, uwekezaji, ajira na fursa nyingi za kijamii na kiuchumi nchini Tanzania. Mashindano haya ni ya ubora wa kimataifa, na tunawaalika wadau wote wa gofu pamoja na umma kushiriki nasi katika kusherehekea mchezo huu wa heshima na hadhi ya kipekee
Kwa kuhitimisha, Mkuu wa idara ya masoko na uwezeshajiVodacom Business, Joseph Sayi, alieleza:
“Vodacom Tanzania Open ni mfano halisi wa kuunganisha urithi wa michezo na ubunifu wa teknolojia ya kisasa. Sisi Vodacom tunajivunia kuwa sehemu ya mashindano haya.
”Ushirikiano kati ya Vodacom Tanzania na Chama cha Gofu Tanzania ni hatua kubwa katika kuimarisha nafasi ya Tanzania kwenye ramani ya gofu ya kikanda, huku ikisukuma mbele dhamira ya Vodacom ya jamii iliyounganishwa kidijitali.

24/09/2025

Darasa la Uongozi kutoka kwa Dr. Kelvin Mwita

Address

Mikocheni B, Malezi Bora , House No 30, Cocacola Road
Dar Es Salaam
00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Koncept TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share