Koncept TV

Koncept TV Pata Habari za Hivi Punde/Kitaifa/Kimataifa/Biashara na Uchumi/Siasa, Michezo/Burudani/Teknolojia na Hamasa Whatsapp ; 0658123310



Like Page Upate Uhondo.

Pata Habari za Hivi Punde/Kitaifa/Kimataifa/Biashara na Uchumi/Siasa, Michezo/Burudani/Teknolojia na Hamasa


LIKE PAGE Kisha Tembelea Website Yetu Kupata UHONDO Zaidi

25/10/2025

HB kwenye Pencil inamaana gani ??

24/10/2025

Pangolin / Kaka Kuona anaijua kesho kabla haijafika Pangolin ana Ulimi Mrefu kuliko Mwili wake Pangolin chakula chake ni Sisimizi na Mchwa Pangolin hawezi kuliwa na mnyama yoyote Wanajamiiana vipi hawa?

HABARI: Mchezaji nguli Duniani Lionel Messi raia wa Argentina amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba wa miaka mitatu n...
24/10/2025

HABARI: Mchezaji nguli Duniani Lionel Messi raia wa Argentina amefikia makubaliano ya kuongeza mkataba wa miaka mitatu na klabu yake ya Inter Miami inayoshiriki ligi kuu ya Marekani.

Mkataba huo wa miaka mitatu uliofungwa baada ya makubaliano ya mdomo tangu wiki iliyopita, Messi atatia saini ya kuendelea kusalia klabuni hapo hadi mwaka 2028.

HABARI:Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameidhinisha tarehe 29 Oktoba 2025 kuwa s...
24/10/2025

HABARI:Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameidhinisha tarehe 29 Oktoba 2025 kuwa siku ya mapumziko ya kitaifa, ili kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika zoezi la kupiga kura.

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 24, 2025 na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, ikieleza kuwa Rais ametumia mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Sikukuu za Kitaifa, Sura ya 35.

“Kama inavyofahamika, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza siku ya Jumatano, tarehe 29 Oktoba 2025, kuwa siku ya kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2025,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Aidha, hatua hiyo imelenga kuwawezesha wananchi wote wenye sifa stahiki — wakiwemo Watumishi wa Umma na Wafanyakazi wa sekta binafsi — kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura bila vikwazo vya kikazi.

Taarifa hiyo imehitimisha kwa kusisitiza kuwa tangazo hilo ni sehemu ya dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wote wanashiriki ipasavyo katika mchakato wa kidemokrasia wa kuwachagua viongozi wao kwa amani na utulivu.

23/10/2025

Sababu za macho ya Paka kuwaka wakati wa usiku.

HABARI; Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa taarifa kwa umma kuhusu ajali iliyohusisha treni ya Mwendokasi (EMU) iliy...
23/10/2025

HABARI; Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa taarifa kwa umma kuhusu ajali iliyohusisha treni ya Mwendokasi (EMU) iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma leo majira ya saa 2:00 asubuhi katika eneo la Ruvu, mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TRC, ajali hiyo imesababishwa na hitilafu za kiutendaji ambazo zilisababisha mabehewa matatu ya treni hiyo kuacha njia. Hata hivyo, shirika hilo limethibitisha kuwa hakuna vifo vilivyoripotiwa kufikia sasa.

Timu ya wataalamu ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TRC, vyombo vya ulinzi na usalama, na menejimenti ya shirika hilo, inaendelea kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo.

TRC imewahakikishia wananchi kuwa huduma za reli zitaendelea kurejeshwa haraka mara baada ya ukaguzi na matengenezo kukamilika. Aidha, shirika hilo limeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na tukio hilo, na limewataka abiria na wananchi kwa ujumla kuendelea kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea.

HABARI: Pwani, Oktoba 23, 2025 — Treni ya Mwendokasi (SGR) inayomilikiwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) imepata ajali...
23/10/2025

HABARI: Pwani, Oktoba 23, 2025 — Treni ya Mwendokasi (SGR) inayomilikiwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC) imepata ajali leo asubuhi katika eneo la Ruvu, mkoani Pwani, ikiwa katika safari yake kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, treni hiyo ilihama kwenye reli (kuondoka njia) katika mazingira ambayo bado hayajafahamika. Mpaka sasa, taarifa kamili kuhusu chanzo cha ajali na iwapo kuna majeruhi au madhara mengine hazijatolewa rasmi.

22/10/2025

Kima | Lemur anatabia ya kujipa Mzuka mwilini kwa kula wadudu wenye asumu k**a hawa

22/10/2025

Kabila la Dani Maarufu kwa Kukata Vidole vya Ndugu wa Marehemu. Dani ni kabila linalopatikana huko Papua Indonesia, endapi ndugu atafariki basi Mama au Shangazi lazima akatwe kidole kimoja kuashiria Uchungu au maumivu ya Mpendwa wake.

HABARI:Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy, ameanza kutumikia kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana ...
21/10/2025

HABARI:Rais wa zamani wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy, ameanza kutumikia kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kula njama ya kufadhili kampeni yake ya urais kwa fedha kutoka kwa kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi.

Sarkozy, ambaye aliongoza Ufaransa kati ya mwaka 2007 hadi 2012, alianza kutumikia adhabu hiyo katika Gereza la La Santé, lililopo eneo la Montparnasse, kusini mwa Mto Seine jijini Paris. Amewekwa katika chumba cha peke yake chenye ukubwa wa takribani mita za mraba tisa (9), ikiwa ni sehemu ya mpango maalum wa usalama binafsi kwa wafungwa wenye hadhi ya juu.

Zaidi ya watu 100 walikusanyika nje ya gereza hilo kuonyesha mshik**ano na kumuunga mkono Sarkozy, kufuatia wito uliotolewa na mwanawe Louis (28). Wakati huo huo, mwanawe mwingine Pierre aliwataka wafuasi wa familia hiyo kutuma ujumbe wa upendo pekee, akisema, “Hakuna kingine, tafadhali.”

Sarkozy, mwenye umri wa miaka 70, aliwasili gerezani saa 3:40 asubuhi kwa saa za Paris chini ya ulinzi mkali. Licha ya hali hiyo, ameendelea kusisitiza kuwa hana hatia, akidai kesi dhidi yake inachochewa kisiasa.

Amesema hataki kupewa upendeleo wowote akiwa gerezani, ingawa amewekwa katika sehemu ya kujitegemea kwa sababu za kiusalama, kutokana na uwepo wa wafungwa wengi waliotiwa hatiani kwa makosa ya uuzaji wa dawa za kulevya na ugaidi katika gereza hilo maarufu lililojengwa karne ya 19.

21/10/2025

Huyu Ndege anapatikana zaidi Katika Bara la America ya Kaskazini Anauwezo wa kuzaliana/kutaga bila kujamiiana Je Kiumbe gani mwingine ana maajabu k**a Ndege huyu Tuque.

HABARI:Sanae Takaichi, amechaguliwa rasmi kuwa Waziri Mkuu mpya wa Japan, na kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo...
21/10/2025

HABARI:Sanae Takaichi, amechaguliwa rasmi kuwa Waziri Mkuu mpya wa Japan, na kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo katika historia ya nchi hiyo, akichukua nafasi ya Shigeru lshiba aliyejiuzulu pamoja na Baraza lake la Mawaziri.

Takaichi, mwenye umri wa miaka 64 na kiongozi wa Chama cha Liberal Democratic Party (LDP), anaunda serikali ya wachache baada ya chama chake kupoteza udhibiti kamili wa Bunge. Anajulikana kwa msimamo wa kihafidhina, ikiwemo kupinga ndoa za jinsia moja na mageuzi ya kijinsia, huku akiahidi kuimarisha uchumi kupitia sera za upanuzi wa matumizi ya umma na kupunguza kodi. Wachambuzi wanasema uteuzi wake ni mkakati wa kisiasa wa LDP kupunguza ushawishi wa vyama vya mrengo wa kulia k**a Japan Innovation Party (Ishin no Kai).

Serikali yake inatarajiwa kujikita katika kukabili mfumuko wa bei, gharama kubwa za maisha, na kuimarisha nafasi ya Japan kimataifa. Takaichi, ambaye amevutiwa na sera za aliyekuwa Waziri Mkuu Margaret Thatcher, anaingia madarakani wakati taifa likikabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi na kisiasa, hatua yake ikitafsiriwa k**a mwanzo mpya kwa siasa za Japan.

Address

Mikocheni B, Malezi Bora , House No 30, Cocacola Road
Dar Es Salaam
00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Koncept TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share