Mwendokasi Media

Mwendokasi Media Kupitia picha tunaileta dunia kiganjani mwako,

Permanently closed.

Kwahuduma za matangazo, kupitia ukurasa wetu wa Facebook, Twitter, Instagram pamoja na YouTube, Tafadhali wasiliana nasi kwa nambari +255759269138 Karibu sana.

11/09/2026

Mwanachama wa CHADEMA na Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano, Odero Charles Odero, ametoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia msiba wa kuondokewa na mume wake, huku akimuombea marehemu apumzike mahali pema.

Odero amewataka viongozi wa CHADEMA kutumia kipindi hiki cha msiba kufika na kutoa pole kwa Rais Samia na familia yake, akisisitiza kuwa misiba ni sehemu inayowaunganisha watu na kuwawezesha kusahau tofauti zao.

Amesema kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, ya kuwataka viongozi na wafuasi wa chama hicho kufikisha salamu zake za pole kwa Rais Samia na familia yake inaonesha uungwana, ubinadamu na moyo wa maridhiano.

Odero amekumbusha pia kuwa Rais Samia aliwahi kutuma salamu za pole kwa CHADEMA wakati wa msiba wa mmoja wa waanzilishi wa chama hicho, Edwin Mtei. Hivyo, amewataka viongozi wengine wa CHADEMA, wakiwemo waliopo Zanzibar, kutumia nafasi hiyo kufika na kuhani msiba.


11/09/2026

Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Dkt. Lameck Karanga, amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni kwamba aliamuru kufyekwa kwa migomba na miwa ya wananchi wa Kijiji cha Oldeani, Kata ya Endabash, akisema ofisi yake haikutoa agizo hilo.

Dkt. Karanga amesema mgogoro wa eneo hilo umeanza tangu mwaka 2017, kabla hajawa Mkuu wa Wilaya, na kwamba wananchi hao wamekuwa wakielekezwa mara kadhaa kuondoka katika eneo linalodaiwa kuwa la mwekezaji Kongoni Estate.

Amesema mamlaka mbalimbali, ikiwemo uongozi wa wilaya na wataalamu wa kilimo, ziliwahi kuwafikia wananchi hao na kuwaomba kuondoka, akieleza pia kuwa eneo hilo linahusisha vyanzo vya maji.

Kwa mujibu wa Dkt. Karanga, mwekezaji baadaye alifikisha suala hilo mahak**ani na wananchi kupewa notisi za kuondoka kupitia court broker. Hata hivyo, amesema yeye alikutana na pande zote na kuwataka wananchi wapewe muda wa kuondoka kwa amani.

“Yaliyotokea siyo maagizo ya Mkuu wa Wilaya. Mimi kwanza nimeona kwenye social media. Mimi sikuagiza watu kwenda pale,” amesema.

Aidha, Dkt. Karanga amekanusha madai kwamba wananchi hao walipigwa viboko kwa maagizo yake, akisema ofisi yake wala Jeshi la Polisi hawakuhusika na tukio hilo.

Ametoa wito kwa wananchi kutovamia maeneo ya watu wala kujichukulia sheria mkononi, huku akiwataka waandishi wa habari kusikiliza pande zote kabla ya kuripoti kuhusu migogoro ya aina hiyo.


Serikali inapanga kuanzisha vituo vya data vya akili bandia (AI) huku nchi ikijiandaa kwa matumizi mapana ya teknolojia ...
11/09/2026

Serikali inapanga kuanzisha vituo vya data vya akili bandia (AI) huku nchi ikijiandaa kwa matumizi mapana ya teknolojia hiyo katika sekta muhimu za uchumi

Akizungumza katika mahojiano maalum na Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) kando ya Mkutano wa Mawaziri wa Ushirikiano wa Kiuchumi wa Korea na Afrika (KOAFEC) wa 2026 huko Seoul, Korea Kusini, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bi. Angela Kairuki, amesema alisema Tanzania tayari inatathmini miundombinu inayohitajika kusaidia maendeleo ya AI.

“Tayari tuna umeme safi na upatikanaji wa kutosha wa maji. Haya ni miongoni mwa mahitaji muhimu ya kujenga vituo vya data nchini. Tunajiandaa kuanzisha vituo vya data vya AI ili tuweze kujiandaa vyema,” alisema.

Mkutano huo unaambatana na miaka 20 ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea na Afrika na hutoa jukwaa la majadiliano kuhusu uwekezaji, ufadhili wa maendeleo, uvumbuzi wa kiteknolojia na uhusiano imara zaidi wa kiuchumi.

Korea Kusini iliahidi katika Mkutano wa Korea na Afrika wa 2024 kuongeza maradufu msaada wake rasmi wa maendeleo kwa Afrika hadi dola bilioni 10 za Marekani ifikapo mwaka 2030, pamoja na dola bilioni 14 za Marekani katika ufadhili wa mauzo ya nje ili kusaidia makampuni ya Korea yanayopanua biashara na uwekezaji kote barani.


Watoto 25 walifariki baada ya moto kuzuka katika shule moja mjini Bukavu, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokraia ya Kongo ...
11/09/2026

Watoto 25 walifariki baada ya moto kuzuka katika shule moja mjini Bukavu, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokraia ya Kongo siku ya Alhamisi asubihi.

Idadi ya vifo hadi sasa ni 27, Wanafunzi walifariki dunia walipokuwa wakijaribu kukimbia moto ulienea katika shule mbili katika mtaa wa Kadutu, mtaa wenye watu wengi unaotazama mji,huku hali hiyo inaendana na siku chache zilizopita, soko kuu la Kadutu pia liliteketea.

Moto huo ulizuka siku ya Alhamisi asubuhi, Septemba 10, yapata saa 3:00 asubuhi. Kulingana na mashahidi, moto huo ulianzia katika nyumba kadhaa na kuenea hadi katika majengo mawili ya shule katika eneo la Bagira wakati watoto wakiwa darasani.

Katikati ya kifusi, Nsimire Rushuda, mama wa watoto wanne anayesoma katika moja ya shule hizo, anajaribu kutafuta watoto zake wawili. Anasema “Watoto wangu wawili wamejeruhiwa, na sijawaona wengine wawili bado. Bado nina matumaini; nitawapata kwa sababu hawakuwa miongoni mwa waliopelekwa hospitalini. Zaidi ya hayo, kila kitu kiliungua. Hatujui tutalala wapi,”.

Hata hivyo majanga k**a haya hutokea mara kwa mara katika miji ya DRC, ambayo kwa kiasi kikubwa haina vifaa vya kuzima moto, na mara nyingi husababishwa na nafasi ndogo kati ya majengo na miunganisho haramu kwenye gridi ya umeme.


Watoto 25 walifariki baada ya moto kuzuka katika shule moja mjini Bukavu, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokraia ya Kongo ...
11/09/2026

Watoto 25 walifariki baada ya moto kuzuka katika shule moja mjini Bukavu, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokraia ya Kongo siku ya Alhamisi asubihi.

Idadi ya vifo hadi sasa ni 27, Wanafunzi walifariki dunia walipokuwa wakijaribu kukimbia moto ulienea katika shule mbili katika mtaa wa Kadutu, mtaa wenye watu wengi unaotazama mji,huku hali hiyo inaendana na siku chache zilizopita, soko kuu la Kadutu pia liliteketea.

Moto huo ulizuka siku ya Alhamisi asubuhi, Septemba 10, yapata saa 3:00 asubuhi. Kulingana na mashahidi, moto huo ulianzia katika nyumba kadhaa na kuenea hadi katika majengo mawili ya shule katika eneo la Bagira wakati watoto wakiwa darasani.

Katikati ya kifusi, Nsimire Rushuda, mama wa watoto wanne anayesoma katika moja ya shule hizo, anajaribu kutafuta watoto zake wawili. Anasema “Watoto wangu wawili wamejeruhiwa, na sijawaona wengine wawili bado. Bado nina matumaini; nitawapata kwa sababu hawakuwa miongoni mwa waliopelekwa hospitalini. Zaidi ya hayo, kila kitu kiliungua. Hatujui tutalala wapi,”.

Hata hivyo majanga k**a haya hutokea mara kwa mara katika miji ya DRC, ambayo kwa kiasi kikubwa haina vifaa vya kuzima moto, na mara nyingi husababishwa na nafasi ndogo kati ya majengo na miunganisho haramu kwenye gridi ya umeme.


Ukraine imetangaza kwamba watu watano wameuawa na wengine 67 kujeruhiwa baada ya droni ya Urusi kushambulia kituo cha un...
11/09/2026

Ukraine imetangaza kwamba watu watano wameuawa na wengine 67 kujeruhiwa baada ya droni ya Urusi kushambulia kituo cha ununuzi katika mji wa Pavlograd, katika mkoa wa Dnipropetrovsk.

Waziri wa Mambo ya Ndani, Ivan Vihefsky, amesema maduka na magari yalishambuliwa mchana kweupe, “wakati barabara zilikuwa zimejaa watu.”

Vyombo vya habari vya Ukraine viliripoti kwamba vituo vingine viwili vya ununuzi katika miji ya Zaporizhzhia na Sumy vililengwa na mashambulizi ya anga ya Urusi mapema wiki hii.

Urusi ilikuwa imetangaza kwamba droni ya majini ya Ukraine ilishambulia mji wa mapumziko wa Sochi Jumatano usiku, na kusababisha watu 28 kujeruhiwa.

Aidha, watu wengine watatu waliripotiwa kuuawa katika mashambulizi mengine yaliyofanywa na Ukraine.

Vita vimekuwa vikiendelea kwa nguvu kati ya Urusi na Ukraine tangu Rais wa Urusi, Vladimir Putin, alipoanzisha uvamizi zaidi ya miaka minne na nusu iliyopita.

Juhudi mpya za kuleta amani zilizoongozwa na wajumbe wa Rais wa Marekani, Donald Trump, mwishoni mwa wiki zinaonekana kuwa zimeleta matokeo machache tu, kufuatia mazungumzo yao na Putin mjini Moscow na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, mjini Kyiv.


10/09/2026

Mtafiti wa masuala ya Akili Mnemba, Jacob Coxon, amezishutumu vikali kampuni kubwa za Marekani zinazotengeneza teknolojia hiyo, akidai zinaendesha mbio za kutengeneza mifumo ya AI yenye uwezo wa kujiboresha bila kuzingatia vya kutosha hatari zinazoweza kuikabili dunia.

Coxon, ambaye hivi karibuni ameondoka katika kampuni ya Anthropic, amesema kampuni hiyo pamoja na OpenAI zinaelekea kwenye uundaji wa kile kinachoitwa “superintelligence” mifumo yenye uwezo unaoweza kuzidi akili ya binadamu huku akionya kuwa teknolojia hiyo inaweza kuwa tishio kubwa kwa maisha ya binadamu.

Je, AI inaweza kufikia hatua ya kuwa na uwezo unaozidi ule wa binadamu na hata kuwa tishio kwa wanadamu?


10/09/2026

Zaidi ya washiriki 3,000 kutoka mataifa mbalimbali wamekusanyika jijini Arusha kuhudhuria Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Huduma za Afya ya Msingi unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Wadau wa utalii Arusha wamepongeza juhudi za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza utalii wa mikutano (MICE), wakisema mikutano mikubwa inaongeza idadi ya wageni na kuchochea fursa za kiuchumi na kibiashara.

Wamesema ongezeko la mikutano ya kimataifa linaendelea kuwanufaisha wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali, huku likichangia ukuaji wa uchumi kuanzia ngazi ya chini hadi kitaifa.

Mahak**a Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imemkatalia Tundu Lissu kuwaita Rais Samia Suluhu Hassan, Dkt. Phillip Mpang...
10/09/2026

Mahak**a Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imemkatalia Tundu Lissu kuwaita Rais Samia Suluhu Hassan, Dkt. Phillip Mpango, Kassim Majaliwa na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kuwa mashahidi katika kesi yake ya uhaini.

Hata hivyo, Mahak**a imeridhia Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Camilius Wambura, Mkuu wa Majeshi (CDF) Jacob Mkunda na DCI Ramadhani Kingai kuitwa kuwa mashahidi wa Lissu.

Uamuzi huo umetolewa leo Septemba 10, 2026 na Jaji Dunstan Ndunguru, akiongoza jopo la majaji watatu linalosikiliza kesi hiyo.


Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwendokasi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwendokasi Media:

Shortcuts

Share