Mwendokasi Media

Mwendokasi Media Kupitia picha tunaileta dunia kiganjani mwako,

Permanently closed.

Kwahuduma za matangazo, kupitia ukurasa wetu wa Facebook, Twitter, Instagram pamoja na YouTube, Tafadhali wasiliana nasi kwa nambari +255759269138 Karibu sana.

Jeshi la Polisi nchini limesema si kila taarifa ya utekaji au kupotea kwa mtu inayoripotiwa ina uhusiano wa moja kwa moj...
01/09/2025

Jeshi la Polisi nchini limesema si kila taarifa ya utekaji au kupotea kwa mtu inayoripotiwa ina uhusiano wa moja kwa moja na vitendo vya uhalifu.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, amesema baada ya uchungu*i wa kina, imebainika kuwa baadhi ya matukio yamesababishwa na sababu binafsi au mambo ya kijamii ikiwemo wivu wa kimapenzi, imani za kishirikina, migogoro ya mali, kisasi, na hata visa vya watu kujiteka wenyewe.

“Polisi wataendelea kuchunguza kwa makini kila taarifa inayotolewa ili ukweli ujulikane na hatua stahiki zichukuliwe. Wananchi wanapaswa kuepuka kutumia hila au kujichukulia sheria mikononi, badala yake washirikiane na vyombo vya dola kusuluhisha matatizo yao,” amesema DCP Misime.

Hata hivyo, mjadala unaendelea miongoni mwa wananchi, hususan ndugu na jamaa za waliotekwa au kupotea bila kupatikana hadi leo, k**a vile Deus Soka, Mdude Nyagali, Ally Kibao, Sativa, Roma Mkatoliki na wengine, wakijiuliza iwapo kauli hizo za polisi zinaweza kuleta faraja kwao.


01/09/2025

Naibu Katibu Mkuu wa Kampeni ya Mama Asemewe, inayoratibiwa na wasomi wa vyuo na vyuo vikuu nchini, Bw. Gerald Mandago, amesema kuwa vijana wameamua kumuunga mkono Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, k**a ishara ya kuthamini maendeleo na sera zenye tija zinazotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita.

“Tumeamua kumuunga mkono Mheshimiwa Rais, na ukweli ni kwamba mikutano yake imekuwa ikijaza vijana wa vyuo na wananchi wengi. Ni matarajio yangu kuwa kupitia uchagu*i huu, vijana kwa pamoja tutamuheshimisha Mheshimiwa Rais, huku uchagu*i ukiendelea kwa amani na utulivu,” alisema Mandago.

Ameongeza pia kuwa wananchi hawapaswi kubagua mikutano ya kampeni, badala yake wahudhurie yote, wachuje hoja za kisiasa na kuepuka maneno ya chuki au matusi ambayo yanaweza kuathiri mshik**ano wa kitaifa.


01/09/2025

Jeshi la Polisi nchini limekanusha vikali uvumi ulioenea mitandaoni ukidaiwa kupatikana kwa kontena lililosheheni silaha katika Bandari ya Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Septemba 1, 2025 jijini Dodoma, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna Msaidizi wa Polisi (DCP) David Misime, amesema taarifa hizo hazina ukweli wowote na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki isiyo ya lazima.

DCP Misime amewahakikishia wananchi kuwa hali ya usalama nchini ni shwari na mipaka yote inalindwa kikamilifu. Amewataka wananchi kutumia mitandao ya kijamii kwa njia sahihi, kuepuka kusambaza taarifa zisizothibitishwa na kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa sahihi na kwa wakati.

Taarifa hizo za uongo zilianza kusambaa baada ya mtumiaji maarufu wa mitandao ya kijamii, Mange Kimambi, kudai kupitia kurasa zake kuwa silaha za kivita na magari ya kifahari yameingizwa nchini kwa siri, jambo lililoibua sintofahamu kubwa mitandaoni.


Simanzi na mshangao vimetanda katika Shule ya Msingi na Sekondari ya Narok Adventist baada ya mwanafunzi wa darasa la ti...
01/09/2025

Simanzi na mshangao vimetanda katika Shule ya Msingi na Sekondari ya Narok Adventist baada ya mwanafunzi wa darasa la tisa mwenye umri wa miaka 14 kupatikana amefariki dunia ndani ya bweni katika mazingira ya kutatanisha.

Taarifa zinaeleza kuwa kijana huyo alikutwa akiwa anatokwa na damu nyingi kutokana na jeraha kubwa shingoni. Alikimbizwa kwa dharura katika Hospitali ya Rufaa ya Narok, ambako alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu.

Uchungu*i wa awali unaonesha kuwa huenda mwanafunzi huyo alishambuliwa nje ya bweni kabla ya kuingia ndani, kwani mabaki ya damu yaligunduliwa katika maeneo ya jirani na bweni hilo. Polisi tayari wamemk**ata mtu mmoja anayedaiwa kuhusika na tukio hilo kwa ajili ya kusaidia katika uchungu*i.

Baada ya taarifa za kifo hicho kusambaa, wakazi wenye hasira walivamia shule hiyo na kuchoma bweni moja, hali iliyosababisha taharuki kubwa. Kufuatia vurugu hizo, shule imefungwa kwa muda usiojulikana huku mamlaka zikihangaika kurejesha utulivu na kuhakikisha familia ya marehemu inapokea haki.


Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama cha Mapindu*i (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema chama hicho kitaendelea ...
01/09/2025

Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama cha Mapindu*i (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema chama hicho kitaendelea kuwakaribisha viongozi na wanachama wa upinzani wenye uwezo mkubwa wa hoja na fikra za maendeleo ili kushirikiana katika kuijenga nchi.

Akizungumza katika moja ya mikutano ya kampeni, Dkt. Nchimbi alisema:

“Wale wote ambao wapo kwenye vyama vingine na wana uwezo mkubwa wa kujenga hoja na kutafakari maendeleo, tutawak**ata mmoja mmoja tuwalete CCM washirikiane kujenga nchi. Haiwezekani ukae na mtu mwenye akili na uwezo mkubwa huko upinzani halafu unamwachia. Ni lazima tumrudishe ili asaidie chama chetu kuendeleza Taifa.”

Aliongeza kuwa CCM itaendelea kuwa nyumba ya watu wote wenye dhamira ya dhati ya kuendeleza maendeleo ya Watanzania bila kujali walikotoka kisiasa.


Mkutano na Waandishi wa Habari uliopangwa kufanywa leo, Septemba 1, 2025 na mwanasiasa Luhaga Mpina, umeahirishwa ghafla...
01/09/2025

Mkutano na Waandishi wa Habari uliopangwa kufanywa leo, Septemba 1, 2025 na mwanasiasa Luhaga Mpina, umeahirishwa ghafla kutokana na dharura ambazo hazijafafanuliwa.

Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa ACT-Wazalendo, Abdallah Khamis, imesema:
“Tunaomba radhi kwa usumbufu uliotokana na mabadiliko haya. Tutawataarifu mara tu tutakapokuwa tayari.”

Hadi sasa, haijafahamika ni lini mkutano huo utapangwa upya.


Tume ya Uchagu*i (INEC) imekubali jumla ya rufaa nne na kutupilia mbali rufaa tisa zilizowasilishwa na wagombea waliokuw...
01/09/2025

Tume ya Uchagu*i (INEC) imekubali jumla ya rufaa nne na kutupilia mbali rufaa tisa zilizowasilishwa na wagombea waliokuwa wakipinga maamu*i ya wasimamizi wa uchagu*i katika maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza jijini Dodoma jana, Agosti 31, 2025, Mkurugenzi wa Uchagu*i wa INEC, Ramadhani Kailima, alisema miongoni mwa rufaa zilizokubaliwa, mbili ni za ubunge na mbili ni za udiwani. Aidha, kati ya zilizokataliwa, sita ni za ubunge na tatu ni za udiwani.

Kwa upande wa ubunge, waliopata ushindi wa rufaa ni Ezekiel Gabriel Katabi, mgombea wa Chama cha CHAUMMA Jimbo la Muhambwe, na Athuman Issah Henku wa CUF Jimbo la Ikungi Mashariki. Ushindi huo unamaanisha kuwa wagombea hao wataendelea rasmi na harakati za kampeni katika majimbo yao.

Hata hivyo, wagombea wa ubunge ambao rufaa zao zimekataliwa ni pamoja na:
• Msowoya Gelard Goodluck (ACT-Wazalendo – Kilombero),
• Innocent Gabriel Siriwa (ADC – Kibamba),
• David January Mhanga (CHAUMMA – Mkuranga), na
• Christina Gasper Mbise (ADC – Ubungo).

Kwa upande wa udiwani, INEC imekubali rufaa mbili na kukataa tatu.

Kailima alisisitiza kuwa maamu*i hayo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha uchagu*i mkuu unafanyika kwa uwazi, haki na kwa mujibu wa sheria za nchi.

“Tunaendelea kusimamia mchakato huu kwa misingi ya Katiba na sheria, ili wagombea wote wapate haki sawa,” alisema.


01/09/2025

Agosti 31, 2025 – Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba na mwanachama wa CCM, Humphrey Polepole, amemshambulia vikali mfanyabiashara na mwanasiasa Rostam Aziz akihusiana na bei ya gesi nchini.

Polepole amesema kuwa wakati nchini Cuba mtungi wa gesi wa kilo 15 unauzwa kwa takribani shilingi 2,000 za Kitanzania, hapa Tanzania mtungi wa ukubwa huo huo unauzwa shilingi 60,000, jambo alilolieleza kuwa ni unyonyaji mkubwa kwa wananchi.

“Nyie hapa Tanzania mnapigwa. Haiwezekani Cuba hawana gesi, mitungi yao wanatoa nje lakini bei ipo chini. Sasa nyinyi mna gesi, lakini mtungi wa kilo 15 unauzwa shilingi 60,000. Nyumbani kwangu ni marufuku mtungi wa Taifa Gesi kuingia,” alisema Polepole.

Akiendelea kuzungumzia sakata hilo, Polepole hakusita pia kuibua hoja za kisiasa, akidai kuwa upinzani nchini umebanwa kiasi cha kushindwa kushiriki kikamilifu katika chagu*i.


Mashabiki wa soka nchini wanaendelea kujadili nani kati ya watani wa jadi, Simba SC na Yanga SC, ameteka hisia za mashab...
31/08/2025

Mashabiki wa soka nchini wanaendelea kujadili nani kati ya watani wa jadi, Simba SC na Yanga SC, ameteka hisia za mashabiki kwa jezi mpya za nyumbani kwa msimu wa 2025/26.

Klabu zote mbili tayari zimezindua jezi zao, huku kila upande ukijinasibu kwamba umetengeneza u*i mkali zaidi. Jezi ya Simba imepewa maoni chanya kutokana na ubunifu wa rangi nyekundu yenye mguso wa kisasa, wakati Yanga wao wamekuja na muonekano wa kijani na manjano ulioongezewa nakshi za kiutamaduni, jambo lililowavutia mashabiki wengi.

Mitandaoni mjadala umepamba moto, kila shabiki akisifia na kutetea timu yake. Wapo wanaosema Yanga wameibuka na muonekano wa kipekee, huku wengine wakiamini Simba wamefanya mapindu*i makubwa ya kisanaa kwenye u*i wao.

Mpaka sasa, bado haijabainika wazi nani kapiga bao mwenzake, kwani mashabiki wanagawanyika kwa mitazamo. Hata hivyo, jambo moja limekuwa dhahiri: msimu huu, mashindano si uwanjani tu, bali pia kwenye mavazi ya nyumbani.

Funguka tujue nani kampiga bao mwenzake ?


31/08/2025

Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole,akizungumza kupitia kwenye ukurasa wake Wa Facebook.


Siku ya tarehe 30 Agosti 2025, wakati wa kampeni za mgombea wa CCM, Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika eneo la Mtumb...
31/08/2025

Siku ya tarehe 30 Agosti 2025, wakati wa kampeni za mgombea wa CCM, Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika eneo la Mtumbatu, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, wananchi waliomba maji safi na salama. Mgombea Dkt. Samia aliwaahidi kuwachimbia kisima cha maji ndani ya siku mbili.

Leo, 31 Agosti 2025, utekelezaji wa ahadi hiyo umeanza rasmi. Wataalamu kutoka Wizara ya Maji, Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu pamoja na Ruwasa wamefika eneo la Mtumbatu asubuhi na wameanza kupima miamba na baada ya hapo kazi ya kuchimba kisima kirefu kwa ajili ya kuhudumia wananchi wa eneo hilo itaanza mara moja .

Pichani: Walaamu Kutoka Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu wakitekeleza agizo la mgombea wa CCM Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Israel imetangaza kuwa msemaji mashuhuri wa Hamas, Abu Obeida, ameuliwa katika shambulizi lake, wakati operesheni kubwa ...
31/08/2025

Israel imetangaza kuwa msemaji mashuhuri wa Hamas, Abu Obeida, ameuliwa katika shambulizi lake, wakati operesheni kubwa ya kijeshi ikiendelea mjini Gaza City. Waziri wa Ulinzi Israel Katz amethibitisha taarifa hizo.

Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz, amethibitisha Jumapili kwamba msemaji wa muda mrefu wa kijeshi wa Hamas, Abu Obeida, ameuliwa katika shambulizi la anga mjini Gaza. Kupitia ujumbe aliouandika kwenye X, Katz aliwapongeza wanajeshi wa Israel na idara ya usalama wa ndani, Shin Bet, kwa “utekelezaji bora bila kasoro.”

Abu Obeida, ambaye jina lake halisi ni Hudaifa al-Kahlut kwa mujibu wa jeshi la Israel, alikuwa sauti kuu ya kitengo cha kijeshi cha Hamas, Qassam Brigades. Alijulikana kwa kujifunika uso kwa kitambaa cha rangi nyekundu na kuzungumza kupitia video na sauti zilizotolewa na Hamas.

Hamas, kwa upande wake, haijatoa tamko rasmi kuthibitisha kifo chake. Baadhi ya viongozi wake wameyataja madai haya kuwa ni “vita vya kisaikolojia” vinavyolenga kudhoofisha ari ya wapiganaji na raia wanaoendelea kukabiliana na mashambulizi.

Hospitali za Gaza zimeripoti kwamba angalau watu 43 wameuawa katika mashambulizi ya Israel tangu Jumamosi, wengi wao wakiwa raia waliokimbilia maeneo yanayodhaniwa kuwa salama. Mashirika ya kibinadamu yanasema idadi hiyo huenda ikaongezeka kutokana na ugumu wa kufika maeneo yaliyoathirika.


Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwendokasi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwendokasi Media:

Share