Mwendokasi Media

Mwendokasi Media Kupitia picha tunaileta dunia kiganjani mwako,

Permanently closed.

Kwahuduma za matangazo, kupitia ukurasa wetu wa Facebook, Twitter, Instagram pamoja na YouTube, Tafadhali wasiliana nasi kwa nambari +255759269138 Karibu sana.

25/10/2025

Kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 , 2025 , nchini Tanzania , wananchi wameendelea kuhimizwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kumchagua Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa upande wa Zanzibar.

Pia wamesisitizwa kutimiza wajibu wao k**a wananchi kwa kujitokeza na kupiga kura.


25/10/2025

Tanzania inapiga hatua kubwa kuelekea katika zama za usafiri wa kisasa na uchumi unaounganisha wananchi wote kutoka pwani hadi magharibi. Reli ya kisasa ya SGR ni alama ya uthubutu, dira sahihi na uongozi makini unaoleta matokeo yanayoonekana kwa kila Mtanzania.

Kupitia uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, serikali imewekeza kwenye miradi mikubwa ya kimkakati — ikiwemo SGR, nishati, elimu, na afya — ili kuhakikisha maendeleo hayabaki kwenye karatasi, bali yanaguswa na maisha ya watu.

Kasi hii ya maendeleo haiwezi kusimama! Chagua Dkt. Samia Suluhu Hassan na Chama Cha Mapinduzi (CCM) tarehe 29 Oktoba, ili tuendelee kujenga Tanzania yenye uchumi imara, miundombinu ya kisasa, na fursa sawa kwa wote.


25/10/2025

Mgombea Ubunge wa Arusha Mjini kupitia CCM, Paul Makonda, Oktoba 24, 2025, ametembelea Soko la Darajani lililopo Malindi, Zanzibar, ambapo amezungumza na wafanyabiashara na kutoa elimu ya namna sahihi ya kupiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Katika ziara hiyo, Makonda amehamasisha wananchi kumuunga mkono Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wa CCM, huku akisisitiza umuhimu wa amani na utulivu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.


25/10/2025

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amedai watu wanaochochea maandamano nchini wamelipwa fedha kwa lengo la kuvuruga amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Amesema hayo leo Jumamosi, Oktoba 25, 2025, wakati wa muendelezo wa kampeni zake katika Kata ya Unga Limited, ambapo amewataka wananchi kupuuza wito wa maandamano na kuendelea kulinda amani na mshik**ano kwa maslahi ya taifa.

Makonda amesema amepata taarifa kuwa mfadhili wa watu wanaochochea maandamano hayo ameishiwa fedha, jambo ambalo limepunguza kasi ya harakati hizo.

“Nimejaribu kuangalia hata wale wanaotangaza kuandamana, mfadhili wao ameishiwa fedha. Katika siku mbili hizi mtaona hata nguvu waliyo nayo imeyeyuka. Wenzetu wamekuwa wanaingiza pesa, na mtaona wengine wameanza kujenga nyumba na kununua magari waangalieni tu,” amesema Makonda


25/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko amesema utekelezaji wa mradi wa uendelezaji Miji Tanzania (TACTIC) kwenye Mji wa Mpanda utaleta mabadiliko chanya kwa wananchi wa Mji huo kwa kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji pamoja na kuboresha huduma za Kijamii na kiuchumi kwa wananchi.

Mhe. Mrindoko amebainisha hayo leo Jumamosi Oktoba 25, 2025, Mpanda Mjini mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa kuanza kwa mradi wa TACTIC kati ya Halmashauri ya Mpanda na Mkandarasi M/s Chonqing International Construction Corporation, mradi ukijumuisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa Kilomita 8.4 kwa kiwango cha lami, ujenzi wa jengo la usimamizi na ununuzi wa magari manne ya kusimamia utekelezaji wa mradi huo, Vyote vikitarajiwa kugharimu Shilingi Bilioni 21.9.

Kulingana na Mhe. Mrindoko barabara zitakazojengwa na mradi wa TACTIC ndani ya Manispaa ya Mpanda ni barabara za Mkumbo Junction- Nsemulwa health Center (Km1.68), Nsemulwa- Sokoine (Km1.23), barabara ya Kapufi (Mita 760), Sumri (Mita 460), Pinda (Mita 260), Fimbo ya Mnyonge (Mita 390), Fish Market (Mita330), Mpanda Hotel (Mita 760), Mikocheni Junction- White Girrafe (Km1.88) na Homeground yenye urefu wa Mita 730.

“Ni matumaini yangu kuwa mradi huu utakuwa chachu ya maendeleo na ustawi wa wananchi wa Mpanda na Mkoa wa Katavi kwa ujumla. Mradi huu utachochea biashara, kurahisisha shughuli za kiuchumi na Kijamii na zaidi kuuweka Mji wetu katika mandhari nzuri zaidi na kuzifanya barabara zetu zipitike muda wote.” Amesisitiza Mhe. Mrindoko.


25/10/2025

Kiongozi Mkuu wa Taasisi ya Twariqa Tanzania, Sheikh Said Hamis Migire, amesisitiza umuhimu wa Kila Mtanzania kuwajibika katika kudumisha amani na utulivu kabla, wakati wa upigaji wa kura na hata baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 akifananisha amani na yai ambalo likivunjika ni vigumu kulirejesha katika hali yake ya awali.

Akizungumza na waandishi wa habari pembezoni mwa dua maalumu ya kuombea amani iliyofanyika katika Zawia Kuu, Makao makuu ya taasisi hiyo jijini Arusha, na kuhudhuriwa na mamia ya waumini kutoka maeneo mbalimbali nchini, Sheikh Migire amesema ni muhimu kila Mtanzania kujiepusha na vurugu na viashiria vingine vyovyote vyenye kutishia tunu za Taifa, akihimiza kutafakati kabla ya kuchukua hatua yoyote inayoenda kinyume na tamaduni na ustaarabu.

“Amani ni k**a yai likivunjika ni ngumu sana kulirudisha. Tumeona mataifa mengi ya Afrika yaliyopoteza amani, na sasa wanajuta." Amesema.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Twariqa Taifa, Sheikh Haruna Hussen ametoa wito kwa viongozi wa dini nchini kuungana kwa pamoja katika maombi ya kuombea amani, akisisitiza kuwa jukumu la kulinda amani ni la kila Mtanzania.

“Na sisi k**a viongozi wa dini tunao wajibu wa kuhubiri amani usiku na mchana. Amani ni msingi wa taifa.
Tunawaomba Watanzania wasidanganyike bali tushike amani yetu kwa mikono miwili." Amesema Sheikh Haruna.


25/10/2025

Mgombea ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amemsifia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji bora wa mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR, akisema uwekezaji huo umeonyesha kwa vitendo ubora na umakini wa Serikali ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha wananchi wanasafiri kwa usalama na uhakika.

Makonda amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Arusha, akieleza kuwa hivi karibuni Reli ya SGR iliyokuwa ikisafiri kutoka Dar es Salaam kuelekea Dodoma ilipata hitilafu njiani kuelekea Morogoro, na baadhi ya watu kutangaza kwenye mitandao ya kijamii kwamba treni hiyo imepata ajali.

Hata hivyo, alisema kutokana na ubunifu na teknolojia ya kisasa iliyoekezwa na Serikali, ndani ya masaa mawili na nusu tu treni nyingine ya mchongoko ililetwa na kuendelea na safari, na hakuna abiria hata mmoja aliyeshindwa kufika Dodoma au Dar es Salaam kwa njia ya SGR.

“Huu ndio ushahidi wa uongozi makini wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Enzi za nyuma behewa moja likidondoka, treni ilikuwa inasimama siku kadhaa; mvua ikinyesha kidogo reli inateleza na abiria wanakwama porini. Leo hii, ndani ya muda mfupi tu, tatizo linatatuliwa na safari zinaendelea k**a kawaida,” alisema Makonda.

Makonda alisisitiza kuwa mafanikio hayo ni kielelezo cha Tanzania mpya yenye mifumo imara ya usafiri, inayotokana na dira ya maendeleo ya Rais Samia katika kuboresha miundombinu na huduma kwa wananchi.


25/10/2025

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania (JMAT) Mkoa wa Dodoma, Askofu Evance Chande, amewataka viongozi wa dini na wadau mbalimbali kutumia siku chache zilizosalia kuelekea uchaguzi mkuu kutoa elimu kwa makundi mbalimbali hasa vijana kuhusu umuhimu wa kudumisha amani.

Akizungumza leo Oktoba 25, 2025 jijini Dodoma katika kongamano la viongozi wa dini wa Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) kuliombea taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu, Askofu Chande amesema ni muhimu kuwaelimisha vijana kutotumika vibaya na kujingiza kwenye vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa nchi.

“Tukae na vijana tuwaambie kwamba sumu haionjwi. Unaweza ukasema nitaandamana vyovyote itakavyokuwa, bila kuelewa madhara yake. Tuwape elimu hawa vijana, wasije wakaitumbukiza nchi hii kwenye matatizo,” amesema Askofu Chande.


25/10/2025

Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Sheikh Mustafa Rajab, amesisitiza kuwa maandamano pekee yanayokubalika ni yale ya wananchi kuandamana kwenda kwenye vituo vya kupiga kura na kurejea nyumbani kwa amani, akiwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025.

Akizungumza leo Oktoba 25, 2025, jijini Dodoma, katika kongamano la viongozi wa dini wa Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) lililolenga kuliombea taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi, Sheikh Rajab aliwahimiza wananchi kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, kwa kuendeleza misingi ya amani na umoja wa kitaifa.

“Hakuna maandamano mengine isipokuwa yale ya wananchi kuandamana kwenda kwenye vituo vya kupiga kura na kurudi nyumbani. K**a viongozi wa dini, tunaendelea kuyahamasisha maandamano haya halali. Maandamano mengine hayapaswi kuungwa mkono na tuna wajibu wa kuyakemea,” Sheikh Mustafa Rajab.


25/10/2025

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Sheikh Issa Nassoro, amewataka viongozi wa dini nchini kuwa waaminifu na kutumia nafasi zao kwa ajili ya kuijenga jamii, si kuchochea taharuki au migogoro ya kisiasa. Amesema baadhi ya viongozi wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya udanganyifu, ikiwemo kujiteka wao wenyewe kwa maslahi binafsi jambo linalochafua taswira ya taasisi za kidini.

Akizungumza leo Oktoba 25, 2025, jijini Dodoma, katika kongamano la viongozi wa dini wa Kanda ya Kati (Dodoma na Singida) lililolenga kuliombea taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, Sheikh Nassoro amesema ni muhimu viongozi wa dini kujitathmini na kusema ukweli ili kulinda heshima na uadilifu wa taasisi zao.

“Viongozi wa dini tumekuwa chachu ya kuchochea baadhi ya mambo ya kisiasa yanayolalamikiwa nchini, ikiwemo suala la utekwaji wa watu. Ukweli ni kwamba baadhi yetu tumekuwa tukitumia nafasi hizi kujiteka sisi wenyewe kwa maslahi binafsi. Ni lazima tuambizane ukweli, maana ukweli siku zote humweka mtu huru,” amesema Sheikh Nassoro.

Ameongeza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikisababisha taharuki katika jamii, huku waumini wakihisi viongozi wao wametekwa, kumbe baadhi yao wameamua kuishi maisha tofauti kwa hiari yao binafsi.


25/10/2025

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Elico Foundation imekabidhi Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa soko la samaki na mtambo wa kukaushia dagaa wenye thamani ya shilingi milioni 129.98, unaoweza kukausha tani 3 hadi 5 kwa siku.
Akizindua mradi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Edwin Mhede amesema uwekezaji huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, za kuboresha uchakataji wa mazao ya uvuvi na kupunguza upotevu unaosababishwa na changamoto za hali ya hewa.
Mtambo huo utasaidia kuongeza ubora wa dagaa, thamani ya soko, na kipato cha wavuvi, huku ukitumia teknolojia rafiki kwa mazingira.


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipowa...
24/10/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alipowasili katika Uwanja wa Mnazi Mmoja Visiwani Zanzibar kwenye Mkutano Mkubwa wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu leo Oktoba 24, 2025.


Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwendokasi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwendokasi Media:

Share