Mwendokasi Media

Mwendokasi Media Kupitia picha tunaileta dunia kiganjani mwako,

Permanently closed.

Kwahuduma za matangazo, kupitia ukurasa wetu wa Facebook, Twitter, Instagram pamoja na YouTube, Tafadhali wasiliana nasi kwa nambari +255759269138 Karibu sana.

08/06/2026

Rais wa Jumuiya ya wanafunzi wa elimu ya Vyuo na Vyuo Vikuu Nchini TAHLISO Bw. Geofrey Kiliba amewataka Vijana wa Vyuo na Vyuo Vikuu Nchini kutambua nafasi zao katika jamii na namna ambavyo Taifa linawategemea katika ujenzi wa Taifa lao.

“Nchi yetu inatutegemea sana sisi Vijana, hatuwezi tukasahau na tukapuuzia uhalisia wa matumaini na mategemeo ya Taifa hili juu ya sisi Vijana. Wanatutegemea sisi vijana kwasababu kwanza tuna nguvu lakini pia kwasababu tuna maarifa. Wanatutumainia pia kwasababu sisi vijana tuna muda mrefu zaidi wa kuendelea kuichunga na kuiendeleza Nchi yetu.” Amesema.

Kiliba amebainisha hayo Juni 06, 2026 wakati akihutubia Bunge la serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar Es Salaam (DarTUso), akisisitiza pia umuhimu wa utulivu na busara katika kuyaendea mambo na kusema Mungu ndiye tumaini la maisha kwani yeye pia ndio hupanga mambo katika maisha ya binadamu.

Kiliba kadhalika amesisitiza umuhimu wa vijana hao kutokata tamaa na kujihusisha na makundi yasiyofaa kwenye jamii, akimtaka kila mmoja kutoogopa mustakabali wa kesho zao na badala yake kuhakikisha wanapambana katika kutimiza ndoto zao bila ya kukatishwa tamaa na changamoto mbalimbali zinazotokea katika maisha.


Hofu ya kuongezeka kwa mgogoro wa Mashariki ya Kati imeanza tena kutikisa soko la mafuta duniani baada ya mashambulizi m...
08/06/2026

Hofu ya kuongezeka kwa mgogoro wa Mashariki ya Kati imeanza tena kutikisa soko la mafuta duniani baada ya mashambulizi mapya kati ya Iran na Israel kusababisha bei za mafuta kupanda kwa zaidi ya asilimia 4 ndani ya siku moja.

Kupanda huko kunakuja siku chache baada ya bei za mafuta kufikia takribani dola 104 kwa p**a kufuatia hofu ya kuongezeka kwa mvutano katika Mlango wa Hormuz, njia muhimu inayopitisha sehemu kubwa ya mafuta yanayouzwa duniani.

Hata hivyo, dalili za mazungumzo na matumaini ya kupungua kwa mzozo huo zilisababisha bei kushuka hadi karibu dola 95 kwa p**a.

Lakini matumaini hayo yanaonekana kuyeyuka haraka baada ya mashambulizi mapya kuripotiwa, hali iliyorejesha hofu katika masoko ya nishati na kusukuma tena bei kuelekea dola 99 kwa p**a.

Wachambuzi wa sekta ya nishati wanaeleza kuwa kinacholisumbua zaidi soko kwa sasa si kiwango cha mafuta kilichopo duniani, bali hatima ya Mlango wa Hormuz ambao hupitisha karibu asilimia 20 ya mafuta yote yanayosafirishwa duniani kwa njia ya bahari.

Iwapo njia hiyo itaathirika au kukumbwa na vikwazo vya kiusalama, athari zake zinaweza kuonekana haraka katika bei za mafuta, gharama za usafirishaji na hatimaye bei za bidhaa mbalimbali duniani.

Kwa Tanzania na nchi nyingine zinazotegemea mafuta kutoka ukanda wa Ghuba ya Uajemi, hali hiyo inaendelea kufuatiliwa kwa karibu.

Wataalamu wanaonya kuwa vita vikidumu au kusambaa zaidi, shinikizo la bei za mafuta katika soko la dunia linaweza kuongezeka katika miezi ijayo.


08/06/2026

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Mara, Chacha Heche Mei 06, 2026 akiwa Rorya mkoani Mara amesema kwa sasa watu wanaogopana, wanashindwa hata kupeana misaada barabarani kwa sababu ya kuogopa kutekwa.

Aidha, Chacha Heche amesema wakosoaji wa Serikali wamekuwa wakikumbwa na kadhia ya kutekwa kwa kukosoa maovu yanayofanywa na watawala, “tukiyasema hayo ndugu zangu, tunaonekana maadui, tunapangiwa hukumu ya kuotoonekana, hata nguo isionekane”


08/06/2026

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh ameyasema hayo Juni 8, 2026 bungeni wakati akijibu Swali lililoulizwa na Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Salma Kikwete kuhusu mkakati wa Serikali juu ya malipo ya Walimu wanaojitolea.

Ikumbukwe Mei 13, 2026 Mdau wa JamiiForums.com aliandika kuwa “Walimu wa kujitolea Shule za Msingi, Sekondari - Morogoro waboreshewe maslahi, malipo hayaendani na hali halisi ya sasa”


08/06/2026

Aliyewahikuwa Mbunge wa CHADEMA Iringa mjini , Mchungaji Msigwa, ametoa ufafanuzi kuhusu kauli yake ya awali aliyosema kuwa “alipokuwa CHADEMA alikuwa mjinga”, kauli ambayo ilizua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii na miongoni mwa wadau wa siasa pindi alipohamia CCM na hivi sasa amerudi CHADEMA.


07/06/2026

Jumla ya ndoa 130 zimefungwa leo jijini Dar es Salaam katika hafla maalum ya ndoa iliyoandaliwa na Taasisi ya Al-Hikma chini ya uongozi wa Rais wa taasisi hiyo, Sheikh Shareef Abdulgadir. Hafla hiyo ilifanyika katika Wilaya ya Temeke na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, dini pamoja na wananchi.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, ambaye alisisitiza kuwa msingi wa maadili katika jamii huanzia ndani ya familia.

Akizungumza baada ya ibada hiyo, Katambi aliipongeza Taasisi ya Al-Hikma kwa kuandaa mpango huo wa kuwawezesha vijana kuingia katika ndoa kwa kufuata taratibu zote muhimu, ikiwemo mahojiano na uchunguzi wa kina wa wahusika, kugharamia mahari kwa baadhi ya vijana wa kiume pamoja na kutoa ushauri wa ndoa kwa wanandoa watarajiwa.

“Nitumie fursa hii kutoa pongezi zangu za dhati kwenu Taasisi ya Al-Hikma. Katika zama za sasa, changamoto ya mmomonyoko wa maadili kwa asilimia kubwa inachochewa na ongezeko la mahusiano yasiyo halali, migogoro ya kifamilia na mambo mahususi yanayowakabili vijana. Ndoa k**a hizi ni sehemu ya suluhisho,” alisema Katambi.


07/06/2026

Rais wa Jumuiya ya wanafunzi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Nchini Tanzania TAHLISO Bw. Geofrey Kiliba amesisitiza umuhimu wa kufanya uchaguzi kwa amani na upendo na kuepuka chaguzi kuwa sehemu ya vyanzo vya migogoro na makundi miongoni mwa wanafunzi ndani ya Vyuo na Vyuo Vikuu vilivyopo Nchini.

Kiliba amebainisha hayo Juni 06, 2026 wakati wa hotuba yake kwa Bunge la serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini Dar Es Salaam (DarTUso), akibainisha kuwa Mungu ndiye huamua ni nani awe kiongozi na kwa wakati gani.

“Mungu ndiye anayepanga nani awe kiongozi, anayeamua nani aongoze watu na kwa wakati gani ni yule aliyeumba watu. Sisi binadamu nafikiri malaika wanatucheka sana kwasababu Mungu anajua mwisho wetu, anajua kesho yetu ni ipi kwahiyo mipango mipango hii kwamba wewe unautaka urais, unaanza kuchorachora mipango, hakuna huo ni udanganyifu, hakuna bingwa wa uchaguzi na hata ikitokea umeshinda basi jua kuwa ulikuwa upande wa kile Mungu alichokipanga.” Amesema Kiliba.

Kiliba amesisitiza pia umuhimu wa mshik**ano na umoja miongoni mwa viongozi na wanafunzi kwa ujumla, akieleza kuwa ushirikiano ni msingi muhimu wa kufanikisha maendeleo ya wanafunzi na taasisi za elimu ya juu Nchini, akisisitiza pia kwamba kudumisha amani, utulivu na mazingira bora ya kujifunzia vyuoni ndio silaha muhimu katika ukuaji wa elimu.


07/06/2026

Vijana Mkoani Kilimanjaro wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa programu zake mbalimbali za kuwainua na kuwawezesha kiuchumi, ikiwemo mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kwa maelekezo ya kuweza kuwafikia na kuwanufaisha Vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Wakizungumza na mwandishi wetu wa habari leo Jumamosi Juni 07, 2026, wanakikundi wa Quality printing kutoka Kata ya Mawenzi, Wilayani Moshi,Mkoani Kilimanjaro wameeleza kuwa kupitia Mkopo walioupata wa Shilingi Milioni 123, wamesema mbali ya kunufaika kiuchumi, wamewezs pia kutoa ajira kwa vijana wenzao pamoja na kuisaidia jamii dhidi ya changamoto walizokuwa nazo.

“Kikundi chetu kilianza rasmi mwaka 2020 na usajili wa kudumu tukapata mwaka 2021. Sisi ni miongoni mwa kikundi tulichobahatika kupata mkopo wa serikali na mpaka sasa tumenufaika na mkopo katika awamu mbili, awamu ya kwanza ilikuwa 2022 ambapo tuliomba na kupewa milioni 18, kufikia 2023 tukafanikiwa kurejesha na baadae zoezi hilo lilisimama ili kuweka mambo sawa na baadae tukaomba tena na awamu hii kwasababu tulirejesha mkopo wa kwanza kwa mafanikio, tukafanikiwa kupata shilingi Milioni 105 mwaka 2025.” Amesema Ally Mohamed, Mwenyekiti wa kikundi cha Quality Printing.

Wanakikundi hao watano wameishukuru serikali kwa kujielekeza katika kutimiza ndoto za Vijana wengi Nchini pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa Vijana wa Kitanzania, kwani kupitia mikopp hiyo mbali ya uanzishwaji wa miradi mbalimbali kwa wana vikundi, ajira pia zimetolewa kwa wataalamu mbalimbali walioajiriwa kutekeleza majukumu katika vikundi hivyo kote Nchini.

Aidha kipo kikundi cha B5 Enteprises group, ambao kupitia mradi wa B5 Media waliwezeshwa mkopo wa shilingi Milioni 45,500,000 ambapo awali walilazimika kufanya kazi kwa mkataba wa muda mfupi usiokuwa na kipato cha uhakika wakimuahidi Rais Samia Suluhu Hassan kuwa watarejesha mkopo wao kwa uaminifu, wakisisitiza pia kuwa mabalozi wa kuhamasisha Vijana wengine kuitumia fursa hiyo ya mikopo ya Halmashauri ili kuweza kujiendeleza kiuchumi.


07/06/2026

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Faris Buruhani, ameendelea kuhamasisha vijana kujitokeza na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi kupitia Operesheni ya Vijana Daka Fursa na Samia (VIDAFUSA) awamu ya pili, ambayo imeanza rasmi katika Wilaya ya Ngara, Kata ya Ngara Mjini. Operesheni hiyo inalenga kuwafikia vijana katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera kwa kipindi cha siku 16 kupitia makongamano maalumu ya fursa.

Akizungumza katika mkutano huo, Faris amesema kuwa awamu ya pili ya VIDAFUSA imewakutanisha maafisa kutoka Benki za CRDB na NMB pamoja na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa halmashauri husika ili kutoa elimu kuhusu mikopo, uwekezaji na fursa nyingine za kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi. Amesisitiza kuwa lengo kuu ni kuwajengea vijana uwezo wa kutumia fursa zilizopo badala ya kusubiri ajira pekee.

Faris ameeleza kuwa operesheni hiyo inawakutanisha vijana wote bila kujali itikadi zao za kisiasa, kwa kuwa maendeleo ya vijana ni agenda ya pamoja inayohitaji ushirikiano wa kila mmoja. Amehimiza vijana wa Kagera kujitokeza kwa wingi katika makongamano hayo ili kupata elimu, taarifa na mwongozo utakaowasaidia kunufaika na fursa zinazotolewa na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na taasisi mbalimbali za kifedha.


06/06/2026

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amewataka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kushiriki mdahalo wa wazi wa kujadili masuala mbalimbali ya kisiasa.

Miongoni mwa viongozi aliowataja ni John Heche, Godbless Lema, Joseph Mbilinyi na Boniface Jacob (Bon Yai).

Kihongosi ametoa wito huo alipokuwa akizungumza na wananchi katika viwanja vya Kanisa Katoliki Ngaramtoni, wilayani Arumeru mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kukagua uhai wa chama, utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na kusikiliza kero za wananchi.


Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwendokasi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwendokasi Media:

Share