28/02/2026
Mchekeshaji Kicheche ametumia ukurasa wake wa instagram kumuaga mke wake na kumuahidi kuwa hatoweza kufanya uzinz! kwenye safari yake ya Congo.
''LEO NASAFIRI KUELEKEA KWENYE ZIARA YANGU YA CONGO. Ila safari ya awamu hii ni tofauti kabisa na zile zilizopita.
Mala zote nishazoeaga kabla ya kufanya show huwa napiga kwanza show na mitulinga hotelini kisha ndo ikafanye show jukwaani hapa wasanii wa muziki washanelewa
Lakini safari hii ni tofauti.
Kwa heshima ya hali aliyokuwa nayo mke wangu , na kwa heshima ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani,
NAAHIDI hadharani kwamba kwa kipindi chote nitakachokuwa Congo, sitofanya uzinzi wa aina yoyote ile.
Najua si jambo rahisi — hasa ukizingatia uzinzi upo damuni. Lakini heshima ya mke wangu ni kubwa kuliko tamaa zangu. Heshima ya mwezi huu ni kubwa kuliko udhaifu wangu.
Nitajikaza. Na namuomba sana Mungu anipe nguvu ya kulitimiza hili, kwa sababu kwangu si jambo dogo wala rahisi.
Na ili kuweka wazi dhamira yangu, nitawaruhusu watu wangu wa karibu wanichukulie video muda wowote, saa yoyote, bila mipaka.
Video zote nitaziweka kwenye page yangu. Nafanya hivi kujipa challenge — nijithibitishe mwenyewe:
Je, nina uwezo wa kukaa muda mrefu bila kufanya uasherati au la''Ameandika-Kicheche