06/03/2026
Hongera sana Maleo Stanley Lameck!
Tunayo furaha kubwa kukupongeza kwa kuchaguliwa rasmi kuwa Youth Representative – Africa Scout Region (2025–2028).
Ushindi huu si wa bahati, bali ni matokeo ya juhudi zako za muda mrefu, uvumilivu, na kutokukata tamaa. Umejaribu mara nyingi, ndani na nje ya nchi, bila kuchoka na bila kurudi nyuma. Leo hii, hatimaye umeweza na si tu katika ngazi ya taifa, bali katika ngazi ya Afrika nzima.
Hii ni heshima kubwa kwako binafsi, kwa Tanzania Scouts Association, na kwa vijana wote wa Tanzania. Umeonyesha kuwa kukata tamaa si sehemu ya safari ya mafanikio, na kwamba anayevumilia na kuamini anaweza kufika mbali.
Tunakuombea hekima, nguvu, na mafanikio mema katika kuwatumikia na kuwawakilisha vijana wa Afrika kwa uadilifu na weledi.
Hongera sana kwa ushindi huu mkubwa. Umetuheshimisha! 🌍⚜️🇹🇿