SSN We Are East, African Media.

Zaidi ya watu milioni moja mapema leo jumapili walijaa barabarani karibu na moja ya viwanja vikuu vya Madrid ili kuungan...
07/06/2026

Zaidi ya watu milioni moja mapema leo jumapili walijaa barabarani karibu na moja ya viwanja vikuu vya Madrid ili kuungana na Papa Leo kwa Misa ya nje, ambayo huenda likawa tukio kubwa zaidi la ziara yake ya wiki moja nchini Uhispania.
Leo amehimiza umati huo kuishi imani yao ya kikatoliki kwa kuwasaidia wengine katika mahubiri yake ya Misa.
Kadhalika Papa ameelezea matumaini mapema kwamba Madrid itasalia kuwa jiji la kukaribisha na kujumuisha, ambapo maisha ya kijamii yamechochewa na maadili ya kweli ya kibinadamu.
Ziara yake ya Juni 6-12 pia inajumuisha vituo vya Barcelona na Visiwa vya Canary, ambapo atakutana na wahamiaji ambao wamehatarisha maisha yao wakivuka huko kutoka Afrika Magharibi.

07/06/2026

Mwajiri Amnasa Yaya Akifanya Tukio La Ajabu Baada Ya Kumuagiza Amuandalie Chakula.

06/06/2026

Ni nini kinaendelea hapa?

06/06/2026

Una maoni gani mdau?

Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran Ali Khamenei, aliyeuawa katika shambulio la Marekani na Israeli mnamo Februari 28, atazi...
04/06/2026

Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran Ali Khamenei, aliyeuawa katika shambulio la Marekani na Israeli mnamo Februari 28, atazikwa katika mji wa kaskazini mashariki wa Mashhad, afisa mkuu wa manispaa alisema hapo jana ( Jumanne).

Mohammad-Amin Tavakkolizadeh, naibu wa meya wa Tehran wa masuala ya kijamii na kitamaduni, alisema Khamenei atazikwa katika kaburi takatifu la Imam Reza kulingana na wosia wake na mapendekezo ya familia, kulingana na shirika la habari la nusu rasmi la Fars.

Katika picha hizi, watu wanaonekana wakitembelea maonyesho ya michoro ya Vincent Willem van Gogh  yenye mada "Beyond Van...
04/06/2026

Katika picha hizi, watu wanaonekana wakitembelea maonyesho ya michoro ya Vincent Willem van Gogh yenye mada "Beyond Van Gogh: The Immersive Experience" huko Cairo, Misri, Juni 1, 2026. Vincent Willem van Gogh alikuwa mchoraji wa Kiholanzi wa Post-Impressionist ambaye ni miongoni mwa wasaani maarufu na wenye ushawishi mkubwa katika historia ya uchoraji ya Magharibi. Katika zaidi ya muongo mmoja aliweza kuchora michoro zipatazo 2,100, ikiwa ni pamoja na takriban michoro 860 ya mafuta, mingi ikiwa katika miaka miwili ya mwisho ya maisha yake.

Kundi la kwanza la wataalamu wa matibabu kutoka China kwa ajili ya kupambana na janga nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya ...
04/06/2026

Kundi la kwanza la wataalamu wa matibabu kutoka China kwa ajili ya kupambana na janga nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) liliwasili Jumanne mjini Kinshasa, mji mkuu wa nchi hiyo. Wataalamu hao watatoa msaada wa matibabu nchini humo kwa muda wa miezi mitatu ili kuunga mkono juhudi za kuzuia na kudhibiti mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.

Korea Kaskazini imezindua kiwanda kipya cha kuzalisha malighafi zinazotumika kutengeneza silaha za Nyuklia huku Kiongozi...
04/06/2026

Korea Kaskazini imezindua kiwanda kipya cha kuzalisha malighafi zinazotumika kutengeneza silaha za Nyuklia huku Kiongozi wa Nchi hiyo, Kim Jong Un akitangaza mpango wa kuimarisha uwezo wa Nyuklia wa Taifa hilo kwa kiwango kikubwa zaidi.

Katika taarifa iliyotolewa na Shirika rasmi la Habari la Korea Kaskazini (KCNA), limesema kiwanda hicho kinatumia teknolojia ya kisasa.

Hata hivyo, taarifa hiyo haikubainisha eneo kilipo au lini kilianza kufanya kazi kiwanda hicho. Picha zilizochapishwa na Vyombo vya Habari vya Serikali zimeonyesha ukumbi mkubwa wenye mashine za Centrifuge zinazodhaniwa kutumika kurutubisha urani kwa matumizi ya silaha za Nyuklia.

Baada ya kutembelea kiwanda hicho, Kim alifahamishwa kuhusu utendaji wake pamoja na mipango ya muda mrefu ya uzalishaji.

Akinukuliwa na KCNA, akisema kuna haja ya kuongeza uwezo wa kuzuia vitisho kupitia silaha za Nyuklia kutokana na kile alichokiita mashinikizo yanayoongozwa na Marekani na Korea Kusini.

Uzinduzi wa kiwanda hicho kunakuja wakati Korea Kaskazini ikiendelea kupanua na kuboresha silaha zake za Nyuklia licha ya vikwazo vya Kimataifa.

04/06/2026

Kapata ajali dada wa taifa,wengine wanamwita mbea wa taifa.
Toa pole zako hapo chini👇

04/06/2026

Rais Donald Trump,amfokea mwandishi wa habari wa CNN.

Address

Mbezi
Dar Es Salaam
11000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SSN posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share