07/06/2026
Zaidi ya watu milioni moja mapema leo jumapili walijaa barabarani karibu na moja ya viwanja vikuu vya Madrid ili kuungana na Papa Leo kwa Misa ya nje, ambayo huenda likawa tukio kubwa zaidi la ziara yake ya wiki moja nchini Uhispania.
Leo amehimiza umati huo kuishi imani yao ya kikatoliki kwa kuwasaidia wengine katika mahubiri yake ya Misa.
Kadhalika Papa ameelezea matumaini mapema kwamba Madrid itasalia kuwa jiji la kukaribisha na kujumuisha, ambapo maisha ya kijamii yamechochewa na maadili ya kweli ya kibinadamu.
Ziara yake ya Juni 6-12 pia inajumuisha vituo vya Barcelona na Visiwa vya Canary, ambapo atakutana na wahamiaji ambao wamehatarisha maisha yao wakivuka huko kutoka Afrika Magharibi.