Dofu Sports

Dofu Sports Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Dofu Sports, Media/News Company, Dar es Salaam.
(17)

Klabu ya Simba Sc Sports Imepangwa kundi D ya Ligi ya Mabingwa Afrika  2025/26.ESPERANCE SPORTIVE DE TUNISSIMBA SCOATLET...
03/11/2025

Klabu ya Simba Sc Sports Imepangwa kundi D ya Ligi ya Mabingwa Afrika 2025/26.

ESPERANCE SPORTIVE DE TUNIS

SIMBA SC

OATLETICO PETROLEOS

STADE MALIEN

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

kiwango anachokionyesha Mchezaji Elie Mpanzu kimekuwa kibaya hasa katika mechi ya leo. Amesema.. "Kila mwana-Simba aliku...
26/10/2025

kiwango anachokionyesha Mchezaji Elie Mpanzu kimekuwa kibaya hasa katika mechi ya leo.

Amesema.. "Kila mwana-Simba alikuwa na matumaini makubwa na Mpanzu msimu huu,na hii ni baada ya kuonyesha ishara za kuwa mchezaji muhimu msimu uliopita.

Msimu huu watu walitegemea moto,magoli na kiwango bora kutoka kwake kwani tayari ameizoea ligi ya Bongo na mazingira yote ila kila kukicha kiwango chake kinazidi kushuka.

leo ndo alikuwa mchezaji mbovu kiwanjani,alipoteza mipira mingi kizembe na hukuona nini cha ziada anafanya.

Haraka sana anatakiwa kuangalia kiwango chake na kurudi kwenye njia bora."

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Mshambuliaji wa Klabu ya Yanga, Prince Dube, anaripotiwa kuwa katika mawazo mazito ya kustaafu soka, kwa mujibu wa taari...
26/10/2025

Mshambuliaji wa Klabu ya Yanga, Prince Dube, anaripotiwa kuwa katika mawazo mazito ya kustaafu soka,

kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa rafiki yake wa karibu.
Chanzo hicho kimeeleza kuwa Dube amekuwa akipitia kipindi
kigumu ndani na nje ya uwanja, huku kasi yake ya kupoteza
ubora ikionekana wazi katika mechi kadhaa zilizopita.

Inadaiwa kuwa nyota huyo kutoka Zimbabwe amefikia hatua ya kuhisi kuwa amerogwa, jambo lililoongeza zaidi msongo wa mawazo kwake. Dube, ambaye amewahi kuwa miongoni mwa washambuliaji
hatari katika Ligi Kuu Tanzania Bara, amekuwa akikosa kujiamini, na mara kadhaa kuonekana mwenye huzuni.

Hadi sasa, uongozi wa Yanga haujatoa tamko rasmi, lakini
taarifa zinaeleza kuwa baadhi ya viongozi wanajaribu kumshawishi mchezaji huyo abadili mawazo na kuendelea
kupigania nafasi yake.

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

AZAM FC ilikuwa inazishuhudia timu nyingine zikitinga makundi tena wakitumia uwanja wao wa Azam Complex, lakini sasa baa...
26/10/2025

AZAM FC ilikuwa inazishuhudia timu nyingine zikitinga makundi tena wakitumia uwanja wao wa Azam Complex, lakini sasa baada ya miaka 21 tangu kuanzishwa kwa klabu hiyo, ikafanikiwa kubadilisha heshima yao kwa kukata tiketi hiyo ya kwenda hatua ya juu baada ya zile mechi za mtoano.

Huu ukiwa ni msimu wake wa 11 kushiriki tangu kuanzishwa
kwa klabu hiyo mwaka 2004, Azam ilikwama mara 10, safari hii imetoboa.

Azam iliyoanza kushiriki michuano ya CAF mwaka 2013,
ilikuwa haijawahi kucheza makundi ambapo mara mbili
imeshiriki Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 2015 na 2024-2025, zote imeishia hatua ya avwali. Kwa upande wa Kombe la Shirikisho Afrika kabla ya msimu huu kufuzu makundi, huko nyuma imewahi kujitahidi na kufika hatua ya pili.

Rekodi zinaonyesha katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam mara ya kwanza ilishiriki mwaka 2013 na kuishia hatua ya
kwanza, kisha 2014 (hatua ya awali), 2016 (hatua ya pili), 2017
(hatua ya kwanza), 2019-2020 (hatua ya kwanza), 2021-2022
(hatua ya pili), 2022-2023 (hatua ya pili), 2023-2024 (hatua ya kwanza

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

"Kocha Pantev anataka akikupa nafasi ufanye kitu cha tofautina hicho ndicho kila mchezaji anakipigania, haijalishi ni mu...
26/10/2025

"Kocha Pantev anataka akikupa nafasi ufanye kitu cha tofauti
na hicho ndicho kila mchezaji anakipigania, haijalishi ni muda kiasi gani anakupa. "K**a sio kufunga basi anataka ushiriki kutoa hata asisti

ilitimu ipate kitu tofauti, unajua tuna timu nzuri ambayo
kuendelea kushinda itaongeza morali na kuongeza kiu kufikia malengo yetu." "Ushindani wa namba uliopo kwa sasa ni mkali kwani kila mmoja anataka kuonyesha kiwango chake

kwa kocha kwamba anastahili kucheza hasa hizi mechi za kimataifa"

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Klabu ya Singida Black Stars imeandika historia mpya baada ya kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (CA...
25/10/2025

Klabu ya Singida Black Stars imeandika historia mpya baada ya kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup) kwa mara ya
kwanza tangu kuanzishwa kwake.

Hii inakuja baada ya ushindi wa jumla wa mabao 4-2 dhidi ya
Flambeau du Centre ya Burundi katika hatua ya pili ya michuano hiyo. Kwa ushindi huo, Singida Black Stars wanaungana na Azam FC kupeperusha bendera ya Tanzania katika hatua ya makundi ya michuano ya CAF.

FT: Singida Black Stars 3-1 Flambeau du Centre
(Agg. 4-2)
55' Muaku
67 CIlatous
72' Idrissa

O26' David Irishura

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Klabu ya Young Africans imetangaza kumteua aliyekuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Angola, Pedro Gonçalves kuwa kocha mkuu m...
25/10/2025

Klabu ya Young Africans imetangaza kumteua aliyekuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Angola, Pedro Gonçalves kuwa kocha mkuu mpya klabuni hapo akichukua mikoba ya Roman Folz aliyetupiwa virago.

Gonçalves (49) raia wa Ureno amewahi pia kufanya kazi k**a kocha wa kikosi cha vijana wa klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno.

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

RAIS wa klabu ya Yanga Sc, Eng Hersi Said amefichua kuwa usiku wa leo klabu hiyo itamtambulisha kochamkuu mpya akimtaja ...
25/10/2025

RAIS wa klabu ya Yanga Sc, Eng Hersi Said amefichua kuwa usiku wa leo klabu hiyo itamtambulisha kocha
mkuu mpya akimtaja k**a kocha bora kutoka Ulaya ambaye
anatarajiwa kuchukua mikoba ya Roman Folz aliyetupiwa virago Eng. Hersi amesema hayo baada ya Yanga Sc kutinga hatua ya makundi ya Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika kufuatia ushindi wa jumla wa 2-1 dhidi ya Silver Strikers Fc ya Malawi.

"Tumefanya maamuzi sahihi na usiku wa leo Yanga Sc
itatambulisha kocha bora kutoka Ulaya tutatambulisha kocha
mwenye Ubora, Experience Kubwa, kocha atakayetuvusha
kwenye mashindano haya kwenda hatua inayofuata"
"Habari hii Nzuri inakuja kwenu wananchi na leo
tutamtambulisha usiku huu k**a Zawadi kwenu kwa kutuunga
mkono"--Eng. Hersi Said

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

"Yanga wameshinda lakini mwamuzi amewabeba Yanga kwenye matukio mawili muhimu ambayo pengine Silver striker wangepata ma...
25/10/2025

"Yanga wameshinda lakini mwamuzi amewabeba Yanga kwenye matukio mawili muhimu ambayo pengine Silver striker wangepata magoli na kufuzu group stage

Tukio la kwanza ni la goli ambalo wamefunga na mwamuzi akalikataa wakati hakukuwa na madhambi ya aina yoyote ambayo waliyafanya

Tukio la pili Silver striker walikuwa wanaenda kushambulia Dickson Job akiuzui mpira kwa mkono lakini mwamuzi akashindwa kupuliza filimbi wakati Job alishika ule mpira kwenye eneo ambalo Silver wangeweza kunufaika kwa namna moja ama nyingine, Yanga wamefuzu lakini Silver Striker wameonewa"

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Young Africans wamemuajiri kocha wa zamani wa vilabu vya Sporting Lisbon,De Agosto na timu ya taifa ya Angola,Pedro Vald...
25/10/2025

Young Africans wamemuajiri kocha wa zamani wa vilabu vya Sporting Lisbon,De Agosto na timu ya taifa ya Angola,Pedro Valdemar Soares Gonçalves (49).

K**a nilivyoripoti jana kwamba Pira Ureno linakuja Jangwani,now nathibitisha kwamba Pedro Valdemar Soares Gonçalves ni kocha mpya wa Yanga

Ikumbukwe kocha huyo aliifikisha Angola hatua ya robo fainali kwenye Afcon iliyopita. Nini maoni yako

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Akizungumza na moja ya chombo cha habari leo, Afisa habari wa Yanga SC, Ali Kamwe ameonyeshwa kuilaumu klabu ya Simba SC...
25/10/2025

Akizungumza na moja ya chombo cha habari leo, Afisa habari wa Yanga SC, Ali Kamwe ameonyeshwa kuilaumu klabu ya Simba SC kwa kuwageuka.

"Tulikubaliana mwanzo kwamba linapokuja swala la kimataifa timu zote bila ya kujali uhasimu wetu tuwe kitu kimoja".

Jambo la kushangaza ni kwamba wenzetu wameamua kujitangaza wazi wazi kwamba hawatusapoti, na hawapo pamoja na sisi kinyume na makubaliano yetu".

Tulikubaliana msimu uliomalizika chini ya ushauri wa Raisi Karia kwamba tupeane sapoti kwenye mechi za nje, kitu ambacho wameshindwa kukifanya hadi sasa".

Na sisi hatuna budi, kwa kuwa wao wameamua kutukataa na siku zote ukikataliwa kubali kukataliwa".

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

"Sisi ni timu ndogo kwao lakini tulionesha uwezo wetu"Kocha wa Nsingizini Hotspurs, Mandla David Ohogi amesemapamoja na ...
25/10/2025

"Sisi ni timu ndogo kwao lakini tulionesha uwezo wetu"
Kocha wa Nsingizini Hotspurs, Mandla David Ohogi amesema
pamoja na kufungwa magoli 3-0 nyumbani kwao, lakini
waliwaonesha uwezo wapinzani wao Simba na walilitambua hilo. Kocha huyo anasema wamekuja kupambana kuubadili ubao

wa magoli na kuifanya nchi yao ijisikie faraja japo wanajua kuwa jambo hilo sio jepesi. Qhogi anasema wanajua kutakuwa na mashabiki wengi wakiihanikiza Simba, lakini wao hawatotoa fursa ya kufungwa goli la mapema na jambo hilo litawapa matumaini.

Kocha huyo ameongeza kuwa wanajua Simba inashika nafasi
ya tano Afrika na ipo kwenye kinyang'anyiro cha kuisaka Klabu
Bora va Mwaka Afrika

Kwa taarifa za kimichezo na makala maalumu Follow Instagram Link https://www.instagram.com/dofusports?

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dofu Sports posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

DIRECTOR DOFU

K2GA VIP WAZEE TUFUMUE KITU KIPYA