Jitambueforums

Jitambueforums We believe Every young has unique Identity! We connect young talented and young at heart!,
BE POSTV. TUFUATILIE YOUTUBE CHANNEL YETU YA JITAMBUEFORUMS

Subscribe Our YouTube Channel "Jitambueforums" For more Young men's and women's' at heart Interview.

Hifadhi ya vyanzo vya maji na bahari ni muhimu kwa ustawi wa jamii, uchumi, na mazingira. Hapa kuna njia bora, rahisi, n...
25/01/2025

Hifadhi ya vyanzo vya maji na bahari ni muhimu kwa ustawi wa jamii, uchumi, na mazingira. Hapa kuna njia bora, rahisi, na zinazotekelezeka kwa kuhifadhi rasilimali hizi muhimu:

1.Kutumia kikamilifu mfumo wa taka: Watu na mashirika wanapaswa kuchakata taka na kupunguza plastiki zinazomwagwa baharini.
Kuanzisha vikundi vya usafi wa bahari na mito: Vijana na jamii wanaweza kushirikiana kufanya kampeni za mara kwa mara za kuondoa uchafu kwenye fukwe na mito.
Kutoa elimu kuhusu athari za uchafuzi: Shule, mashirika, na mitandao ya kijamii inaweza kutumika kufundisha madhara ya kutupa taka kiholela.

2. Kupanda miti kando ya mito: Miti husaidia kudhibiti mmomonyoko wa udongo unaoingia kwenye mito na bahari.
Kuzuia ukataji miti kiholela: Jamii zinapaswa kuelimishwa juu ya athari za ukataji miti na kupewa mbinu mbadala k**a matumizi ya nishati jadidifu.
Kuanzisha maeneo ya hifadhi: Hifadhi za kando ya mito na mabwawa zitasaidia kulinda mimea na wanyama wa majini.

3.Kuhakikisha sheria za uvuvi zinaheshimiwa: Serikali na asasi zisizo za kiserikali (NGOs) zisimamie matumizi endelevu ya bahari na kuhakikisha uvuvi haramu unakomeshwa.
Kuweka vikundi vya ulinzi wa mazingira: Vijana na viongozi wa jamii wawe walinzi wa bahari na mito kwa kushirikiana na mamlaka.

4.Kukuza utalii wa mazingira: Kufanya bahari kuwa kitovu cha utalii endelevu, k**a kupiga mbizi (diving) na safari za boti, huku ukilinda mazingira.
Kuwekeza katika ufugaji wa samaki wa kisasa: Hii itapunguza shinikizo la uvuvi wa kupindukia.
Kuhamasisha biashara za kijani: Vijana wahimizwe kuanzisha biashara k**a utengenezaji wa bidhaa kutoka kwa taka za plastiki zilizokusanywa.

5.Kuendesha semina za kijamii: Semina na warsha kuhusu hifadhi ya bahari na vyanzo vya maji zinaweza kufanyika vijijini na mijini.
Kuunda vikundi vya wanaharakati wa mazingira: Wananchi wawe mabalozi wa kulinda vyanzo vya maji kwa kuchukua hatua za kila siku, k**a kuacha kutumia kemikali zinazomwagika kwenye maji. Kuwapa mafunzo ya uvuvi endelevu na hifadhi ya mazalia ya samaki.

6. Kupanda miti zaidi: Miti ni ngao dhidi ya joto kali na mmomonyoko unaochangia kwa vyanzo vya maji n.k

Kadri Afya yako ya akili inavyoitajika kwako mwenyewe, ndivyo mazoezi pia yanavyoitaji kwako, Hapa ndipo umhimu wa Yoga ...
18/01/2025

Kadri Afya yako ya akili inavyoitajika kwako mwenyewe, ndivyo mazoezi pia yanavyoitaji kwako, Hapa ndipo umhimu wa Yoga unaonekana na ili kufahamu umhimu wake, hapo ndipo anaitajika katika Maisha yako.
Basi mpe nafasi katika maisha yako ili kuona tofauti katika ustawi wa akili yako na afya yako kwa ujumla

Simulizi ya Mafanikio ya William Kamkwamba: Kijana Kutoka Malawi.William Kamkwamba ni kijana kutoka Malawi, nchi yenye m...
03/01/2025

Simulizi ya Mafanikio ya William Kamkwamba: Kijana Kutoka Malawi.

William Kamkwamba ni kijana kutoka Malawi, nchi yenye mazingira sawa na Tanzania, ambaye alijipatia umaarufu kutokana na ubunifu wake wa kipekee. Alizaliwa mwaka 1987 katika kijiji cha Masitala, familia yake ikitegemea kilimo kwa maisha yao. Mwaka 2001, akiwa na umri wa miaka 14, Malawi ilikumbwa na ukame uliosababisha njaa kali, na familia ya William haikuwa na uwezo wa kumlipia ada ya shule.

Licha ya changamoto hizo, William hakuacha kujifunza. Alitembelea maktaba ya kijiji na kusoma vitabu vya sayansi, ambapo alijifunza kuhusu nishati ya upepo. Akitumia vifaa vya kutelekezwa k**a vipande vya baiskeli, miti, na vifaa vingine vya zamani, alitengeneza kinu cha upepo ambacho kiliweza kuzalisha umeme wa kuendesha vifaa vidogo na kupampu maji kwa ajili ya umwagiliaji.

Ubunifu wake ulileta mabadiliko makubwa katika kijiji chake, na habari zake zilisambaa kimataifa. Ambapo mwaka 2007 alipanda katika Jukwaa ta TEDx iliyofanyika Arusha, Tanzania, ikiwa ni mara yake ya kusafiri nje ya nchi yake, Alipata fursa ya kusoma katika shule za kimataifa na baadaye kuhitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dartmouth nchini Marekani. William ameandika kitabu kiitwacho "The Boy Who Harnessed the Wind," ambacho pia kimegeuzwa kuwa filamu inayopatika katika mtandao maarufu wa filamu wa NETFlIX akieleza safari yake ya kuvuka vikwazo na kufanikisha ndoto zake.

Mafunzo kutoka kwa William Kamkwamba:

Azma na Bidii:
Licha ya changamoto za kifamilia na kiuchumi, William alijitahidi kujielimisha na kuboresha maisha ya jamii yake.

Ubunifu na Ujasiriamali:
Kutumia rasilimali chache alizokuwa nazo, aliweza kutengeneza suluhisho la kudumu kwa tatizo la nishati na maji katika kijiji chake.

Kujifunza kwa Kujitegemea:
William alionyesha kuwa elimu haipatikani tu darasani; bidii na hamu ya kujifunza vinaweza kumwezesha mtu kufikia malengo yake hata katika mazingira magumu.

Simulizi ya William Kamkwamba inatufundisha kuwa, kwa kujituma na kutumia maarifa tunayopata, tunaweza kuboresha maisha yetu na ya jamii zetu, hata k**a tunakabiliwa na changamoto kubwa.
Unaweza kumfuatilia kupitia .kamkwamba

We wish you a happy new year 2025.New start while setting our new studio in Arusha
01/01/2025

We wish you a happy new year 2025.

New start while setting our new studio in Arusha

  "Pengine umewai kuliona neno na kulisikia neno hili mahali fulani... "AIRBNB" ,Hili neno maarufu sana hasa katika ulim...
16/07/2024


"Pengine umewai kuliona neno na kulisikia neno hili mahali fulani... "AIRBNB" ,Hili neno maarufu sana hasa katika ulimwengu wa sasa wa kizazi cha Gen Z.

Je unajua maana ya neno hili? ..

Kwa mjibu wa ChatGPT , neno Airbnb ni kifupisho cha neno "Air Bed and Breakfast"

Hili ni jukwaa la kimataifa ambalo linawezesha watu kutoa, kupata, na kukodisha makazi ya muda mfupi.

Jina "Airbnb ama "Air Bed and Breakfast," awali wakati linaamzishwa lengo kuu la mwanzishi wake lilikuwa ni kutoa fursa za kukodisha vitanda na huduma za kifungua kinywa kwa njia ya mtandao.

Leo hii, Airbnb imekuwa maarufu k**a njia ya kipekee ya kupata makazi mbadala kwa hoteli kwa njia rahisi na yenye urahisi kutumia.

Je ni neno gani la technology unatamani kujua maana yake?

Weka yako hapo chini...tutakuelemisha.. zaidi.

22/06/2024

Vijana wengi wanasingizia kukosa muda wa ziada na wengi wao wakitumia muda wanaopata kufanya mambo yasiyowanufaisha

Huyu ni Mkurugenzi mtendaji wa akieleza namna ambavyo kijana anaweza kutumia muda wa ziada.

Unaweza kushiriki kwa maoni yako kutuambia wewe k**a kijana unatumiane muda wako wa ziada?

Full video unaweza kuitizama YouTube channel yetu

"Ni vyema sana kuwekeza fedha kwenye ardhi, watu wengi wanaazima au kukopa fedha kwaajili ya kuwekeza kwenye vitu vinavy...
21/06/2024

"Ni vyema sana kuwekeza fedha kwenye ardhi, watu wengi wanaazima au kukopa fedha kwaajili ya kuwekeza kwenye vitu vinavyoshuka thamani k**a magari, hapo lazima uwe unaongeza gharama. Kwenye maisha si kwamba gari ni baya la hasha ila angalia linaenda kutatua nini? Hivyo tizama uwekezaji unaolipa."- UBA Managing Director Akiwa katika hafla ya kujengea uwezo vijana juu ya mada isemayo" youth financial literacy" inayoendelea katika ukumbi wa Aura Suit Iliyoandaliwa na

Sikiliza kwa makini hasa ujue namna ya kuishi na Mwanamke
24/05/2024

Sikiliza kwa makini hasa ujue namna ya kuishi na Mwanamke

Hivi karibu nchi Tanzania , tatizo la Afya ya akili limeibuka na kushamiri kwa kasi, mpaka kufikia Serikali kuliweka k**a moja ya kipa umbele cha kuangalia kwa sasa, lakini si kwamba dalili hazikuonyesha mapema, kwani moja ya sababu zinapelekea ta...

Hivi karibu nchi Tanzania , tatizo la Afya ya akili limeibuka na kushamiri kwa kasi, mpaka kufikia Serikali kuliweka k**...
18/05/2024

Hivi karibu nchi Tanzania , tatizo la Afya ya akili limeibuka na kushamiri kwa kasi, mpaka kufikia Serikali kuliweka k**a moja ya kipa umbele cha kuangalia kwa sasa, lakini si kwamba dalili hazikuonyesha mapema, kwani moja ya sababu zinapelekea tatizo hili kuwa kubwa ni NDOA, hasa zile za wazazi kuchagulia mabinti/ Vijana wenza wa maisha, lakini Tatizo hili linakuwa kubwa sana kwa wanawake ambao wengi wao waliingia kwenye ndoa kwa hiari ya jamii au wazazi, sasa basi, tumefanya mahojiano na MAsuma Somji ambaye ni mtanzania mwenye asili ambaye alipitia matatizo haya ya afya ya akili hasa kutokana na kulazimishwa kuingia kwenye ndoa na wazazi wake watanzania wenye asili ya KIINDI, ambaye kwasasa anafanya kazi ya kuelimisha jamii hasa wanawake na mabinti , juu ya afya ya akili (Mental Health) k**a Unapitia tatizo hili au k**a huko kwenye ndoa ama unapanga kuingia kwenye ndoa, kwa wanaume na wanawake, mabinti na vijana, hii ndio sehemu sahihi ya kupata ushauri.

Kwa sababu hakuna anayewesha kukusimulia matatizo haya vizuri ukaelewa zaidi ya mhanga wa tatzio usika. Tafadhali washirikishe na wenzio

Stream MENTAL HEALTH/AFYA YA AKILI, a podcast playlist by jitambue Radio, to discover new music on Audiomack.

18/05/2024

Audiomack is a youth-driven, artist-first music streaming platform that allows creators to share unlimited music and podcast content for free.

17/04/2024


17/04/2024

Una Muda gani tangu umefika hapa Dsm, Umekaa kweny huu mji , umejishughulisha, Uelezea maisha ya Dar es salaam k**a unavyoyaona kwa Sentensi moja? je ni Unakubaliana na huyu jamaa?

Address

Jitambueforums TV Makuburi Kwa Mbonde , Ubungo External House #17
Dar Es Salaam
0255

Telephone

+255785933880

Website

https://www.youtube.com/c/JitambueforumsTV/videos

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jitambueforums posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jitambueforums:

Share

Category