Tanzatube

Tanzatube The fastest growing Online Media in Tanzania
with unique content ranging from Entertainment,
Sports, Hard news, Exclusive Interviews and
Documentaries

NEW JOB VACANCIES FROM OBAMA CHARITY FUND1. Community Outreach Manager (COM) - 7 Vacancies2. Monitoring, Evaluation and ...
03/11/2023

NEW JOB VACANCIES FROM OBAMA CHARITY FUND
1. Community Outreach Manager (COM) - 7 Vacancies
2. Monitoring, Evaluation and Learning Officers - 3 Vacancies)

3. Project Accountants (Maisha Project) - 5 Vacancies
4. District Focal Personnel (Maisha Project) - 23 Vacancies
5. Nurses and Midwives (Maisha Project) - 15 Vacancies
6. Data Analysts - 40 Vacancies

UNATAFUTA KAZI?AU UNAMATANGAZO YA KAZI? TEMBELEA HAPA UPOST BURE KABISAAAA
26/07/2022

UNATAFUTA KAZI?

AU UNAMATANGAZO YA KAZI? TEMBELEA HAPA UPOST BURE KABISAAAA

Ajira zote Tanzania kutoka serikalini, makampuni binafsi, NGO na mashirika ya kimataifa.

BREAKING NEWS : OTHMAN MASOUD ATEULIWA KUWA MAKAMU WA KWANZA WA RAISRais wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, amemteua Othuman M...
01/03/2021

BREAKING NEWS : OTHMAN MASOUD ATEULIWA KUWA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS

Rais wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, amemteua Othuman Masoud Othuman wa ACT-Wazalendo kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais visiwani humo, kuchukua nafasi ya Maalim Seif Sharif Hamad, aliyefariki dunia 17 Februari 2021.

Uteuzi wa Masoud umefanywa na Rais wa Zanzibar, Dkt Hussein Mwinyi baada ya mashauriano na chama cha ACT-Wazalendo. Masoud amewahi kuhudumu katika nafasi za ngazi za juu katika serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo mwanasheria Mkuu wa serikali.

DONALD TRUMP AIBUKA, AMKOSOA VIKALI BIDENKwa mara ya kwanza toka aondoke madarakani, Rais mstaafu wa Marekani Donald Tru...
01/03/2021

DONALD TRUMP AIBUKA, AMKOSOA VIKALI BIDEN

Kwa mara ya kwanza toka aondoke madarakani, Rais mstaafu wa Marekani Donald Trump amekosoa vikali sera za mrithi wake Joe Biden na kusema kuwa Marekani wametoka kuwa Taifa la Kwanza kwa sera nzuri na kuwa Taifa la MWISHO.

Trump ameyasema hayo kwenye mkutano wa (CPAC) uliofanyika Orlando akiwa anakiwakilisha chama cha Republican. Ukiachana na hayo Trump amedokeza kuwa hana mpango wa kuanzisha chama chake, kwani kitendo hicho kitazigawanya kura za Republican kitu ambacho hapendi, vilevile Trump amegusia kuwa na uwezekano wa kugombea tena 2024 k**a mambo yataenda sawa.

MBWA KUTUMIKA KUGUNDUA WAGONJWA WA COVID19MBWA waliofunzwa nchini Finland wana uwezo wa kugundua wagonjwa walio na maamb...
01/03/2021

MBWA KUTUMIKA KUGUNDUA WAGONJWA WA COVID19

MBWA waliofunzwa nchini Finland wana uwezo wa kugundua wagonjwa walio na maambukizi ya virusi vya corona (Covid-19).

Mbwa hao waliopewa mafunzo maalum wamekuwa wakitumika katika viwanja vya ndege nchini humo tangu Septemba, kudhibiti abiria kwa sababu ya Covid-19. Kulingana na matokeo ya awali, kiwango cha usahihi ni kati ya asilimia 95 na asilimia 100.

Baada ya ukaguzi wa Covid-19 ambao unafanyika ndani ya dakika moja, abiria huruhusiwa kuendelea na safari zao kwa kutegemea na matokeo ya vipimo vya mbwa hao.

Katika mchakato wa ukaguzi, abiria hufuta shingo zao kwa vitambaa vya kufyonza, kisha vitambaa hivyo huwekwa kwenye makopo ambapo baadaye mbwa huja kufanya ukaguzi kwa kunusa upande wa pili wa kuta za makopo hayo.

Ikiwa matokeo yanaonyesha kuwa na maambukizi, abiria hupelekwa kwenye kitengo cha huduma za afya katika uwanja wa ndege.

CHADWICK BOSEMAN ASHINDA TUZO YA MUIGIZAJI BORAChadwick Boseman alishinda tuzo yake ya kwanza ya Golden Globe katika fil...
01/03/2021

CHADWICK BOSEMAN ASHINDA TUZO YA MUIGIZAJI BORA

Chadwick Boseman alishinda tuzo yake ya kwanza ya Golden Globe katika filamu ambayo hakuishi kuiona.

Mjane wa nyota huyo ambaye alitamba kwenye filamu ya Black Panther, Taylor Simone Ledward, alikubali tuzo hiyo ya muigizaji bora kwa niaba ya muigizaji huyo , ambaye alifariki mwezi Agosti kutokana na saratani ya utumbo akiwa na umri wa miaka 43 – miezi mitatu kabla ya filamu kwa jina ‘’Ma Rainey’s Black Bottom’’ ambayo ndiyo imempa tuzo kuzinduliwa.

POLISI  WAUA  WAANDAMANAJI 18Polisi wamepiga risasi na kuwaua waandamanaji 18 nchini Myanmar, ofisi ya Umoja wa Kimataif...
01/03/2021

POLISI WAUA WAANDAMANAJI 18

Polisi wamepiga risasi na kuwaua waandamanaji 18 nchini Myanmar, ofisi ya Umoja wa Kimataifa ya kutetea haki imesema katika siku ambayo maandamano ya kupinga mapinduzi yamekumbwa na mauaji mabaya.

Vifo vimeripotiwa katika miji kadhaa ikiwemo Yangon, Dawei na Mandalay baada ya polisi kutumia risasi halisi na vitoa machozi.

Vikosi vya usalama vilianza msako uliokumbwa na vurugu siku ya Jumamosi baada ya wiki kadhaa za maandamano ya amani kupinga mapinduzi ya kijeshi ya Februari mosi.

Viongozi wa serikali, miongoni mwao Aung San Suu Kyi, waliondolewa madarakani na kuzuiliwa.

SABABU YA KIM NA KANYE KUTALIKIANA YATAJWASababu ya ndoa ya mastaa Kanye West na Kim Kardashian kuangukia pua imewekwa w...
01/03/2021

SABABU YA KIM NA KANYE KUTALIKIANA YATAJWA

Sababu ya ndoa ya mastaa Kanye West na Kim Kardashian kuangukia pua imewekwa wazi kwenye nyaraka za talaka ambayo mkewe Kim Kardashian ameomba kwa mumewe.

Katika nyaraka hizo, sababu kuu ambayo imeelezwa ni 'kutoelewana Mara kwa mara'. Mastaa hao walifunga ndoa miaka 7 iliyopita, na wana watoto wanne.

BABA AKE  YOUNG KILLER ALIA  ADAI MWANAYE ANAJUA AMEKUFA ...Baba mzazi wa msanii wa HipHop Young Killer, anayefahamika k...
01/03/2021

BABA AKE YOUNG KILLER ALIA ADAI MWANAYE ANAJUA AMEKUFA ...

Baba mzazi wa msanii wa HipHop Young Killer, anayefahamika kwa jina la Mzee Msodoki ambaye amesema chanzo cha kutokuwa sawa na mwanaye huyo ni mama yake kumwambia kwamba baba yake amefariki tangu utotoni.

Mzee Msodoki amesema mama Young Killer aliamua kumwambia hivyo mtoto wao kwa sababu aliumizwa na kitendo cha Mzee Msodoki kuukimbia ujauzito wa msanii huyo kabla hajazaliwa na kwenda kuishi nchini Congo DR.

"Mama Young Killer nilikuwa nakaa naye jirani kule Mwanza, wakati huo nilikuwa nafanya kazi Saloon, tukawa kwenye mahusiano ambayo yalidumu k**a miezi 6 na baadaye akaniambia ana ujauzito, sasa kwa wakati huo mimi nilikuwa sijajiandaa kulea na majukumu hivyo nikapata safari ya kwenda Congo nilivyorudi sikumkuta" ameeleza Mzee Msodoki

"Nimekuja kugundua k**a mtoto yupo na ameshakuwa mkubwa ila mama yake alishamwambia kwamba baba yake ameshakufa wakati mimi nipo, ndiyo maana hata yeye haamini k**a mimi ndiyo baba yake kweli" ameongeza

Mzee Msodoki amesema aliwahi kukutana na Young Killer na alimwambia k**a yeye ndiyo baba yake lakini alijibiwa kwamba hana shida lakini mpaka mama yake amdhibitishie.

Address

Seaview 17
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tanzatube posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tanzatube:

Share

Category