Chakushangaza

Chakushangaza Njoo tukujuze TUJUZANE

  Ipi kati ya hizi umewahi kuitumia?Ulikua wapi na mwaka gani?Tukio gani unalikumbuka kuhusu hizi pesa, mimi nakumbuka e...
07/06/2026


Ipi kati ya hizi umewahi kuitumia?
Ulikua wapi na mwaka gani?
Tukio gani unalikumbuka kuhusu hizi pesa, mimi nakumbuka enzi hizo sikukuu napewa shilingi ishirini nakula na chenchi inabaki 20 😁😁
Tuambie

USIONDOKE BILA KUNIFOLLOW UNAWEZA USIONE TENA PAGE HII ♥️

Pichani Anaitwa George Parrott Jambazi Sugu Sana Huko Wyoming US. Baada ya Kuk**atwa na Wananchi Wenye Hasira Kali Mwaka...
06/06/2026

Pichani Anaitwa George Parrott Jambazi Sugu Sana Huko Wyoming US. Baada ya Kuk**atwa na Wananchi Wenye Hasira Kali Mwaka 1880 Alipigwa Hadi Kifo, Wahuni Wakamchuna Ngozi na Kutengenezea Viatu. Wengine Walilifanya Fuvu Lake Kuwa Kibakuli cha Kuwekea Majivu ya Misokoto.Parrott alizaliwa Montbéliard Ufaransa, haijulikani alifikaje US wala alifika lini lakini kinachojulikana ni kwamba aliishi katika mji wa Wyoming huko Marekani katika miaka ya mwishoni mwa 1800, jina lake maarufu lilikuwa ni Big Nose George.

Parrott alikuwa jambazi mkubwa ambaye aliripotiwa kwa mara ya kwanza kwenye magazeti mwaka 1878 huko US baada ya kujaribu kuiteka treni katika reli ya Union Pacific Railroad na kupora mali, jaribio ambalo lilifeli.

Jaribio hili ilimfanya Parrott kuwa mhalifu sugu, na viongozi wa Wilaya ya Wyoming Kapteni Robert Woodville na rafiki yake mpelelezi wa kibinafsi Henry Vincent walijitwika jukumu la kumsaka Parrott na kumfikisha mahak**ani.

Baada ya kumfuatilia kwa muda wa miezi kadhaa walipafikia mahali alipokuwa akipatumia Parrott kujificha yeye na genge lake karibu na millima ya Elk Wyoming, mojawapo ya majimbo ya eneo la milimani magharibi mwa US.

Lakini Parrott alikuwa chonjo, aligundua ujio wa watu hao wawili hivyo yeye na genge lake wakawavizia na kuwaua kwa risasi na kisha kubadili mahali pao pa kujificha.

Haikuchukua muda, miili ya meya na mchunguzi huyo mwingine ilipatikana, na zawadi ya $10,000 iliwekwa mezani kwa mtu yeyote atakaekileta kichwa cha Parrott, na baadaye kitita kiliongezwa hadi $20,000.

Baada ya kona nyingi hatimaye Parrott na mwenzake walik**atwa kwa urahisi mwaka 1880 na kufikishwa mahak**ani ambako alihukumiwa kifo katika gereza Rollins, lakini wakati hukumu hiyo inaandaliwa kutekelezwa jamaa akatoroka.

Inaonekana kwamba tukio hili la kutoroka liliwakasirisha mno watu, wakaingia kila kona kumsaka Parrott mpaka wakamk**ata, hapo sasa ni k**a ilikuwa sherehe kwao, Jamaa alipewa kila aina ya kipigo na kufa mbele ya umati

Baada ya kifo chake march 22, 1881 hakuna aliyejitokeza kudai mwili wake, ndipo kiongozi mmoja kwa jina la Osborn aliichuna ngozi yake na kwenda kwa mafundi viatu akitaka wamtengenezee viatu.

Inaelezwa kuwa kila mmoja pia alijigawia sehemu ya mwili wa jamaa iliyokua imebaki kwa kadri alivyotaka, na historia inaelezaa kuwa fuvu lake pia watu walilifanya kuwa kibakuli cha kuwekea majivu ya misokoto, kudadeq. Vitu hivi vyote vipo katika makumbusho mjini humo hadi leo.
USIONDOKE BILA KUNIFOLLOW UNAWEZA USIONE TENA PAGE HII ♥️

 PIERLUIGI COLLINA MWAMUZI ALIYETAWALA SOKA LA DUNIA KWA MUONGO MMOJAKati ya mwaka 1995 na 2005, kulikuwa na jina moja a...
06/06/2026


PIERLUIGI COLLINA MWAMUZI ALIYETAWALA SOKA LA DUNIA KWA MUONGO MMOJA
Kati ya mwaka 1995 na 2005, kulikuwa na jina moja ambalo lilionekana mara kwa mara katika mechi kubwa zaidi za soka duniani. Kuanzia fainali za Kombe la Dunia, Michezo ya Olimpiki, Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) hadi Kombe la UEFA, Pierluigi Collina alikuwa mwamuzi aliyeaminiwa kusimamia mechi zenye presha kubwa zaidi. Kwa muonekano wake wa kipekee wenye kipara na macho makali, Collina alijijengea heshima kubwa kwa uwezo wake wa kudhibiti wachezaji nyota, migogoro ya uwanjani na mazingira yenye ushindani mkali bila kuyumba.

Umahiri wake ulitambuliwa rasmi mwaka 2011 alipoingizwa katika Ukumbi wa Umaarufu wa Soka la Italia (Italian Football Hall of Fame). Heshima hiyo ilionekana kuwa ya kipekee zaidi kutokana na ukweli kwamba aliingizwa kabla ya baadhi ya magwiji wakubwa wa soka la Italia k**a Paolo Maldini na Dino Zoff, ambao waliingizwa mwaka uliofuata. Hali hiyo ilionyesha jinsi mchango wake katika mchezo wa soka ulivyothaminiwa, licha ya kuwa hakuwa mchezaji bali mwamuzi.

Labda maelezo bora zaidi kuhusu ubora wa Collina yalitolewa na mwamuzi mwenzake, Graham Poll, wakati wa maandalizi ya Kombe la Dunia la mwaka 2002. Poll alisimulia kuwa Collina aliwachambulia kwa kina timu zote mbili, akieleza namna walivyocheza, wachezaji wenye hasira, maeneo yanayoweza kusababisha migogoro na hata matarajio ya kila mwamuzi msaidizi ndani ya mechi. Kila jambo lilikuwa limepangwa kwa umakini wa hali ya juu, na cha kushangaza zaidi ni kwamba utabiri wake ulikuwa sahihi. Ndiyo maana hadi leo Pierluigi Collina anaendelea kutajwa k**a mmoja wa waamuzi bora na wenye ushawishi mkubwa zaidi katika historia ya soka duniani. ⚽🏆

06/06/2026

GAMBOSH PART 11
IMESIMULIWA NA ZABRON C MWITA

Mwaka 1981 Mama wa Kijerumani Marianne Bachmeier Aliingia na Bastola Kortini na Kumtwanga Risasi Saba Mtuhumiwa Aliyekua...
06/06/2026

Mwaka 1981 Mama wa Kijerumani Marianne Bachmeier Aliingia na Bastola Kortini na Kumtwanga Risasi Saba Mtuhumiwa Aliyekua Amembaka Binti Yake Mdogo wa Miaka 7 Hadi Kufa. NI Baada ya M'bakaji Huyo Kuiambia Mahak**a Kuwa Eti Yeye Ndiye Alitongozwa na Binti Huyo Mdogo.
M'bakaji huyo ni Klaus Grabowski, mwenye umri wa miaka 35 mmiliki wa duka la nyama, mtoto Anna Bachmeier mwenye umri wa miaka 7 tuu alikuwa anaenda kucheza na paka wake mbele ya duka lake hilo, ndipo Mei 5, 1980 akamteka nyara na kumfungia nyumbani kwake akimbaka hadi kifo.

Baada ya kumaliza ubakaji wake, Klaus alimfunga mtoto Anna kwemye box na kwenda kumtupa nyuma ya bank moja mjini humo kabla ya kudakwa na dola.

Kwa mujibu wa taarifa ni kwamba bwana Klaus alikuwa amefungwa jela mara kadhaa katika miaka ya nyuma kwa makosa hayo hayo ya unyanyasaji wa kingono kwa mabinti, kwahivyo hio haikua mara ya kwanza.

Marianne aliyekuwa mmiliki wa mgahawa aliiambia mahak**a kwamba alikuwa amechukizwa mno na maneno ya mhalifu huyo eti kwamba binti yake Anna wa umri wa miaka 7 ndio aliyekua amemtongoza jamaa huyo, ndio maana akaamua kumuulia mbali.

Aliingia na bunduki katika chumba cha mahak**a huko Lübeck Germany wakati kesi inaendelea mwaka 1981 na kumpiga mshtakiwa risasi saba na kufa papo hapo.

Machi 1983 Marianne alihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani kwa mashtaka hayo ya kuuwa pamoja na kumiliki silaha kinyume cha sheria, lakini aliachiliwa huru baada ya miaka mitatu kutokana na utiifu wake katika mid wote akiwa gerezani.

Marianne alifariki mwaka 1996 kutokana na saratani akiwa na umri wa miaka 46 na kuzikwa katika kaburi lile lile alilozikwa binti yake miaka 16 iliyopita.
USIONDOKE BILA KUNIFOLLOW UNAWEZA USIONE TENA PAGE HII ♥️

  Mwaka 1984 Utajiri Binafsi wa Rais wa Zaire Mobutu Sese Seko Ulikuwa Mkubwa Kuliko Deni la Nchi. Utajiri Wake Ulikadir...
06/06/2026


Mwaka 1984 Utajiri Binafsi wa Rais wa Zaire Mobutu Sese Seko Ulikuwa Mkubwa Kuliko Deni la Nchi. Utajiri Wake Ulikadiriwa Kuwa Dola bilioni 5 Huku Deni la Taifa Likitajwa Kufika Dola Bilioni 4. Mshahara Wake Rasmi Ulikuwa 17% ya Bajeti. Aliwahi Kununua Concorde Matumizi yake Binafsi.Concorde ni ndege ya mwendo kasi inayoweza kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 2,100 kwa lisaa tuu, inaweza kuruka kutoka Dar es Salaam mpaka Lubumbashi Congo DR ndani ya dakika 60. Mwandishi wa habari mmoja wa kigeni alipomuuliza kuhusu uhalali wake wa kununua ndege hiyo, alijibu, “fikiria kuhusu muda ninaookoa.

Mobutu alikuwa rais wa nchi hiyo kuanzia mwaka 1965 hadi mwaka 1997. Alifariki miezi minne tuu akiwa na miaka 66 nchini Morocco alikokimbilia baada ya kuondolewa madarakani kinguvu mwaka 1997, Mobutu aliifanya Zaire k**a mali yake binafsi, na raia wake k**a mifugo yake.

Usichokijua ni kwamba Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Waziri wa Ulinzi wa Rwanda Paul Kagame (ambaye kwasasa ni rais) wakishirikiana na kijana mdogo mpiganaji wa Congo Joseph Kabila, ndio watu waliokuwa mstaari wa mbele kuongoza majeshi ili kumuondoa Mobutu madarakani, na walifanikiwa.

Sababu kubwa ya viongozi hao kulivalia njuga swala hili ni kwamba mwaka 1996 Mobutu alikuwa ametoa tangazo kuwa raia wote wa nje hasa wale wa makabila ya kutoka Rwanda na Uganda waondoke haraka nchini humo, lasivvyo ukikutwa tuu ni kifo, na ni kweli jamaa hakua anatania.

Mobutu aliyeiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 32 mfululizo alioa wanawake wawili mapacha ambao ni Bobi Ladawa na pacha wake Kosia Ladawa.
USIONDOKE BILA KUNIFOLLOW UNAWEZA USIONE TENA PAGE HII ♥️

CHAKUSHANGAZAKombe la Dunia 1994 Marekani, Mashindano Yaliyokuwa na Umaarufu Mkubwa Lakini Yaliandamwa na Matukio ya Kus...
06/06/2026

CHAKUSHANGAZA
Kombe la Dunia 1994 Marekani, Mashindano Yaliyokuwa na Umaarufu Mkubwa Lakini Yaliandamwa na Matukio ya Kushangaza na Kusikitisha

Kombe la Dunia la FIFA mwaka 1994 nchini Marekani linakumbukwa k**a moja ya mashindano makubwa zaidi katika historia ya soka. Hadi leo, ndilo Kombe la Dunia lililohudhuriwa na watazamaji wengi zaidi viwanjani, likivutia zaidi ya mashabiki milioni 3.5 katika mechi 52 zilizochezwa.

Hata hivyo, nyuma ya mafanikio hayo kulikuwa na matukio mengi ya kushangaza, ya kutatanisha na hata ya kusikitisha yaliyolifanya kuwa moja ya mashindano yanayozungumziwa sana katika historia ya mchezo wa miguu.

Miongoni mwa matukio yaliyotikisa dunia ni kifo cha mchezaji wa Colombia, Andrés Escobar. Katika mechi dhidi ya Marekani tarehe 22 Juni 1994, Escobar alijifunga bao la kujifunga kwa bahati mbaya lililochangia Colombia kufungwa mabao 2-1 na hatimaye kutolewa mapema kwenye mashindano hayo.

Wakati huo, Colombia ilikuwa ikipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri, huku kiasi kikubwa cha fedha kikiwa kimewekwa kwenye k**ari na makundi ya uhalifu nchini humo. Baada ya kurejea nyumbani mjini Medellín, Escobar alipigwa risasi na kuuawa tarehe 2 Julai 1994 akiwa na umri wa miaka 27. Kifo chake kilishtua dunia nzima ya soka na kubaki kuwa moja ya matukio ya kusikitisha zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Kombe la Dunia.

Mbali na hilo, siku ya ufunguzi wa mashindano hayo kulikua na tukio jingine lililovuta hisia za Wamarekani. Wakati mechi za Kombe la Dunia zikianza, matangazo mengi ya televisheni yalikatishwa ili kuonyesha moja kwa moja msako maarufu wa gari jeupe aina ya Ford Bronco lililokuwa limembeba nyota wa zamani wa NFL, O.J. Simpson, aliyekuwa akitafutwa na polisi kufuatia tuhuma za mauaji. Tukio hilo liliangaliwa na mamilioni ya watu na kuwa moja ya tukio maarufu zaidi katika historia ya televisheni ya Marekani.

Katika sherehe za ufunguzi, mwimbaji mashuhuri Whitney Houston alionekana pamoja na gwiji wa soka duniani Pelé, jambo lililoongeza hadhi ya mashindano hayo na kuvutia macho ya dunia nzima kuelekea Marekani.

Tukio jingine ambalo bado linakumbukwa ni lile la mwanamfalme wa mitindo na filamu, Diana Ross, ambaye alipewa nafasi ya kupiga penalti ya mfano katika sherehe za ufunguzi. Penalti hiyo ilikusudiwa kuonyesha jambo maalumu ambapo goli lingegawanyika katikati baada ya mpira kuingia. Hata hivyo, Diana Ross alikosa penalti hiyo akiwa karibu kabisa na goli, lakini tukio la goli kugawanyika lilitokea k**a ilivyopangwa, jambo lililosababisha tukio hilo kuwa moja ya matukio ya kuchekesha na ya kukumbukwa katika historia ya Kombe la Dunia.

Licha ya matukio hayo yote, Kombe la Dunia la 1994 lilifanikiwa sana. Brazil ilitwaa ubingwa kwa mara ya nne baada ya kuifunga Italia kwa mikwaju ya penalti katika fainali iliyochezwa mjini Pasadena, California. Ilikuwa pia fainali ya kwanza katika historia ya Kombe la Dunia kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti.

Miaka mingi baadaye, mashindano hayo yanaendelea kukumbukwa kwa sababu mbili kuu: mafanikio yake makubwa ya kuvutia mashabiki wengi zaidi kuwahi kushuhudia Kombe la Dunia viwanjani, na mfululizo wa matukio ya ajabu yaliyoifanya Dunia ya 1994 kuwa mojawapo ya mashindano yasiyosahaulika katika historia ya soka.

Pumzika kwa amani, Andrés Escobar. Jina lake litaendelea kukumbukwa k**a kumbukumbu ya upande wa huzuni uliogusa mashabiki wa soka duniani kote. Ama hakika duniani tunapita tuu na kila kitu kitabakia

USIONDOKE BILA KUNIFOLLOW UNAWEZA USIONE TENA PAGE HII ♥️

  Kushoto Mwenye Tai ni Sylvester Stallone(Rambo) akiwa na baba yake Frank Stallone Sr na mdogo wake Frank Stallone .Mov...
05/06/2026


Kushoto Mwenye Tai ni Sylvester Stallone(Rambo) akiwa na baba yake Frank Stallone Sr na mdogo wake Frank Stallone .
Movie gani ya RAMBO unaikumbuka?

  WALIOTOKELEZEA.Chama cha Tanganyika African Union (TANU) ambacho kilipigania Uhuru wa Tanganyika na mwishowe kuchangia...
05/06/2026


WALIOTOKELEZEA.

Chama cha Tanganyika African Union (TANU) ambacho kilipigania Uhuru wa Tanganyika na mwishowe kuchangia Muungano wa Nchi hiyo na Zanzibar na kuzaliwa kwa Nchi ya Tanzania kilikuwa chama Madhubuti chenye Matawi Mpaka Nje ya Nchi (nadhani hata huu Utaratibu wa Vyama kuwa na Matawi Nje ya Nchi uliasisiwa nao).

Pichani ni Baadhi ya Watanzania ambao walikuwa Wanachama wa Chama cha Tanu Tawi la London Nchini Uingereza, Picha hii ilipigwa Tarehe 9 Mei, 1959 ikiwaonyesha Wanachama hao wa Tanu ambao wengineo baadaye walikuja kushika Uongozi wa nafasi mbalimbali Nchini.
Kutoka Kulia Mstari wa Mbele waliosima ni Mzee Mark Bomani (Ameshika nafasi Mbalimbali ikiwemo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali), Jesse Kiritta (Amewahi kuwa Mwanasheria wa Serikali kabla ya Baadaye kujihusisha na Biashara Binafsi), Marehemu Emmanuel Bomani (wa Chama cha Ushirika cha Victoria kule Mwanza), Juma Mawalla ( alijikita zaidi Mkaoni Kilimanjaro na Arusha, tunadhani ndiye baba wa Mwanasheria Nyalla Mawalla wa Mawalla Advocates), na Mzee Oscar Salathiel Kambona (Mwanafunzi wa Sheria wakati huo, Katibu Mkuu wa Tanu na pia ameshika Nafasi Mbalimbali za Uwaziri Nchi.

Picha ni Kwa Hisani Kubwa ya Mzee Jesse Kiritta.

CHAKUSHANGAZATANZANIA ILIWAHI KUFANYA MAANDAMANO MAKUBWA KUPINGA VIMINI MWAKA 1973K**a ulikuwa hujui kuwa Tanzania iliwa...
05/06/2026

CHAKUSHANGAZA
TANZANIA ILIWAHI KUFANYA MAANDAMANO MAKUBWA KUPINGA VIMINI MWAKA 1973
K**a ulikuwa hujui kuwa Tanzania iliwahi kufanya maandamano makubwa kupinga vimini na mavazi yaliyotajwa kuwa hayafai, basi historia hii inaweza kukushangaza.

Mnamo tarehe 7 Septemba 1973, jijini Dar es Salaam kulifanyika maandamano makubwa ya wananchi yaliyolenga kupinga uvaaji wa nguo fupi maarufu k**a vimini pamoja na mavazi mengine yaliyotazamwa kuwa yanakiuka maadili ya jamii ya Kitanzania.

Maandamano hayo yaliandaliwa na makundi mbalimbali ya vijana, wanachama wa TANU na mashirika mengine ya kijamii. Yalianzia katika maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam na kuishia katika Makao Makuu ya TANU yaliyokuwa Mtaa wa Lumumba.

Maandamano hayo yalipokelewa na Waziri Mkuu wa wakati huo, Rashidi Mfaume Kawawa, pamoja na viongozi wengine wa serikali. Baada ya maandamano, mkutano mkubwa wa hadhara ulifanyika katika Makao Makuu ya TANU ambapo washiriki walieleza sababu zao za kupinga mavazi hayo.

Wakati huo, viongozi wengi waliamini kuwa kuenea kwa vimini na mavazi mengine mafupi kulikuwa ishara ya mmomonyoko wa maadili, utamaduni na nidhamu ya jamii. Serikali ikaweka tarehe 1 Oktoba 1973 kuwa mwisho wa kuvaa vimini nchini, huku ikitangaza kuwa msako dhidi ya watakaokiuka agizo hilo ungeanza rasmi baada ya tarehe hiyo.

Katika baadhi ya maeneo ya nchi, hatua zilianza kuchukuliwa hata kabla ya tarehe hiyo kufika. Mkoa wa Mwanza ulikuwa miongoni mwa maeneo yaliyoanza kampeni za kupinga mavazi hayo mapema. Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) nao uliunga mkono kampeni hiyo kwa kutoa mihadhara mashuleni na katika mikutano ya hadhara kuhusu mavazi yaliyotajwa kuwa yanafaa kwa mujibu wa maadili ya wakati huo.

Kampeni hiyo ilikuwa sehemu ya mazingira mapana ya siasa za Ujamaa na Kujitegemea chini ya uongozi wa Mwalimu Julius Nyerere, ambapo nidhamu, utu na maadili ya jamii yalisisitizwa sana katika maisha ya kila siku.

Hata hivyo, kampeni hiyo ilikosolewa na baadhi ya wanaharakati na mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu ambao waliona kuwa hatua hizo zilikiuka uhuru wa mtu binafsi wa kuchagua mavazi. Kadiri miaka ilivyopita, msimamo huo ulilegezwa na hatimaye kampeni hiyo ikapoteza nguvu, huku wananchi wakiendelea kuwa na uhuru mkubwa zaidi wa kuchagua mavazi yao.

VISA VINGINE VINAVYOFANANA NA HIKI DUNIANI
Uganda (1973)
Katika kipindi cha utawala wa Rais Idi Amin, wanawake walikatazwa kuvaa vimini katika maeneo mengi ya umma. Serikali ilidai kuwa mavazi hayo yalikuwa yanaenda kinyume na maadili ya Kiafrika. Kampeni hiyo ilidumu kwa miaka kadhaa lakini haikudumu baada ya mabadiliko ya kisiasa nchini humo.

Malawi (1965–1994)
Chini ya utawala wa Rais Hastings Kamuzu Banda, wanawake walikatazwa kuvaa suruali, vimini na mavazi mengine yaliyotazamwa kuwa ya Kimagharibi. Sheria hizo zilianza kulegezwa baada ya kuingia kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1994.

Iran (Baada ya 1979)
Baada ya Mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979, serikali ilianzisha sheria kali kuhusu mavazi ya wanawake. Hijabu ikawa ya lazima katika maeneo ya umma. Sheria hizo zinaendelea kuwepo hadi leo, ingawa zimekuwa zikizua maandamano na mijadala mara kwa mara.

Sudan (1991)
Sheria za maadili ya umma zilianza kutumika zikidhibiti aina za mavazi ya wanawake na tabia za kijamii. Sheria hizo zilipingwa kwa miaka mingi na baadhi yake zilifutwa baada ya mabadiliko ya kisiasa mwaka 2019.

India – Mumbai (2005)
Makundi kadhaa ya kijamii yaliendesha kampeni za kupinga mavazi mafupi kwa madai ya kulinda maadili ya kitamaduni. Hata hivyo serikali haikuweka marufuku rasmi, na kampeni hizo ziliishia katika mijadala ya kijamii na kisiasa.

Afghanistan (1996–2001)
Wakati wa utawala wa kwanza wa Taliban, wanawake walitakiwa kuvaa burqa na kufuata masharti makali ya mavazi. Baada ya kuondolewa madarakani mwaka 2001 sheria hizo zililegezwa, lakini baadhi yake zilirudi baada ya Taliban kurejea madarakani mwaka 2021.
DISCLAIMER:
Picha hizi zimewekwa kwa madhumuni ya mitindo, burudani na kuonyesha mavazi ya kisasa (fashion). Hazina nia ya kuudhi, kudhalilisha au kuhamasisha tabia yoyote isiyofaa. Heshima kwa watu wote imezingatiwa. Endapo mtu yeyote atahisi tofauti, tunaomba apokee radhi zetu za dhati.

Address

Tabata
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chakushangaza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Chakushangaza:

Share