Chakushangaza

Chakushangaza Njoo tukujuze TUJUZANE

HISTORIA YA DR JOHN THORBURN WILLIAMSON NA MGODI WAKE WA ALMASI MWADUI  3.Aliamua kuuita mgodi wake jina la Mwadui jina ...
06/01/2026

HISTORIA YA DR JOHN THORBURN WILLIAMSON NA MGODI WAKE WA ALMASI MWADUI 3.

Aliamua kuuita mgodi wake jina la Mwadui jina la mtemi aliyemkaribisha, alikuwa anaitwa Ng'wadubhi. Jina la Ng'wadubhi lilimshinda kulitamka ndipo akaita
Mwadui.

Alipoona amekusanya almasi za kutosha ndipo. alipoenda kuuza kwenye soko la dunia na kuja
na mitambo ya kisasa. Alifanya utafiti na kugundua kuwa Mwadui ilikuwa na mkandawa "kimberlite "wenye hifadhi nyingi ya almasi. Ikiwa na ukubwa wa hakari 146, mkanda huu ni wa pili kwa ukubwa Duniani baada ya ule wa Mgodi wa Camafuca uliopo Angola.

Dr. Williamson mwaka 1946 alie kuchumbia katika familia ya kifalme huko Wingereza akitaka kumuoa Princess Margaret, akaambiwa huwezi kuoa kwenye familia yetu wewe ni masikini. Akajaribu kuwashawishi kuwa yeye ni tajiri anamilili mgodi wa almasi huko Tanganyika lakini akatoswa.

Alitoa zawadi ya Almasi yenye rangi ya PINK yenye uzito wa kareti 54.5 kwenye harusi ya Princess Elizabeth na Prince Philip mwaka 1947. Unaambiwa almasi hiyo ipo mpaka leo kwenye jumba la kifalme la Uingereza imewekwa pambo kwenye kofia ya Malkia, ilishachongwa ikabaki kareti 23.6. Mwaka1948 akafunga mkataba na serikali ya kikoloni ya Waingereza wa miaka 100 ( yaani 1948-2048. )

MAISHA NDANI YA MJI WA MWADUI.

Dr. Williamson akautengeneza mji mdogo wa Mwadui na kuwa moja kati ya miji bora sana kusini mwa jangwa la Sahara (MwaduiTownship). Kufikia mwaka 1947, Dr Williamson alikuwa amejenga nyumba bora za wafanyakazi, hospital ya kisasa, shule za msingi tatu, mbili za wafanyakazi wa kiafrika na moja ya wafanyakazi wa kizungu ambayo ndio ilikuwa moja ya "English Medium School" ya kwanza Tanganyika. Akajenga chuo cha Ufundi wa aina zote ndani ya mgodi kwa ajili ya watoto wa wafanyakazi, chuo cha
kilimo na shule ya upili.

Huko kwao waliita "School Near The Equator". Ilikuwa shule bora na ya kisasa. Dr Williamson akajenga uwanja wa ndege wa kisasa ndani ya mgodi mwaka 1948 akanunua ndege mbili za mwanzo aina ya Dakota DC3 na Cessna 180 wakati huo hata serikali ya Kikoloni ya Muingereza ikiwa haina wazo la ndege, wakati serikali ya Tanganyika ikiwa haina uhakika wa
uwanja wandege kupokea ndege kubwa aina ya Dakota DC4.

Dr Williamson alikuwa tayari na uwanja huo, ambapo wageni toka London Uingereza, ndege zilitua Malta, Khartoum-Sudani na baadae Nairobi (Wakati huo ukiitwa Embakasi Airport) na baadae kuchukuliwa na ndege moja kwa. moja mpaka Mwadui Shinyanga, ambapo Serikali ya Kikolonii likuwa na afisa mmoja wa uhamiaji. Dr Williamson alijenga kanisa na msikiti bora na wakisasa kwa ajili ya wafanyakazi
wake.

Wakatihuo, usafiri pekee wa watumishi wa serikali ya Kikoloni ilikuwa ni meli maarufu ya"The Braimer Castro" iliyokuwa inatoka Ulaya mpaka Mombasa. Yeye Dr Williamson na wafanyakazialioajili walikuwa wanapanda ndege kupitia Embakasi na baadae Mwadui. Williamson akajenga "Power House" yenye uwezo wa kuzalisha 900kw kwa mitambo ya diesel
na 750kw kwa Gas Turbine na hivyo kuwa na umeme wa uhakika kuliko hata mji wa Dar Es Salaam.

Dr Williamson alijenga "SailingClub", yaani Club inayoning'inia katika bwawa alilichimba eneo la Songwa. Hii ndio ilikuwa Club pekee inayoning'inia Kusini mwa Jangwa la Sahara. May 2 mwaka 1955, Gazeti Kongwela "The Cairns Post" (Est.1882) liliandika juu ya uwepo wa bwawa la Songwa, Mwadui-Shinyanga, Tanganyika. Gazeti hilo la Australia lilielezea bwawa la Songwa k**a moja kati ya "Artificial dam" kubwa zaidi duniani, lenye uwezo wa kuchukua "two thousands million gallons of water". Mradi ambao hata serikali ya mkoloni iliushangaa.

Notes;
Hiyo picha ni Dr. Williamson akiwa na Kijana Bundala wakiwa katika harakati za kuitafuta almasi.

ITAENDELEA

Credit: Njile Nkuba Sitta

HISTORIA YA DR. JOHN THORBURN WILLIAMSON NA MGODI WAKE WA ALMASI MWADUI  2Hali hiyo ilimuweka njia panda kwani vifaa vya...
03/01/2026

HISTORIA YA DR. JOHN THORBURN WILLIAMSON NA MGODI WAKE WA ALMASI MWADUI 2

Hali hiyo ilimuweka njia panda kwani vifaa vyake vilikuwa vinahitaji matengenezo nawafanyakazi wake walikiwa wakimdai mshahara. Aliamua kupunguza wafanyakazi na kuamua kumalizia mchanga wake ili afungashe vilago aondokezake.

Wakati wanamalizia kuuosha mchanga huo alipata vipande viwili vya almasi vichafu kimoja kikiwana uzito wa kareti 30, almasi hiyo ilimpanguvu ya kuendelea na kazi.

Mnamo mwezi wa February 1938 alisafiri mpaka mwabuki wilaya ya misungwi na alikaa huko kwa miezi kazaaakitafuta almasi, alipata lakini hazikuwa nyingi. Aliamua kurudi kizumbi kwenye mgodi wake na kuendelea na kazi, alifanya kazi bila kupata chochote kwa muda wa mwaka mmoja.

Mwaka 1939 mwezi wa 10 akiwa amekata tamaa ya kupata almasi, kijana wake Bundala yeye alikuwa anaendelea kuwasimamia wafanyakazi waliokuwa wakiosha mchanga. Williamson akiwa amelala
kwenye hema lake aliletewa na Bundala kipande cha Almasi kizuri sana chenye uzito wa kareti mbili.
Dr Williamson alifurahi sana na kumpa Bundala zawadi ya pesa.

Bundala alimuomba Williamson ruhusa azipeleke pesa zake nyumbani kwao katika kijiji cha Luhumbo (kwa sasa Mwadui ), Williamson alimkubalia kijana wake. Williamson alipatamatumaini tena ya kupata mkanda wa almasi maana aliamini kuwa lazima kuna sehemu karibuambayo mlipuko wa volcano ulipolipuka na kuzitoa hizo almasi.

Tarehe 6 mwezi wa 3 mwaka 1940 Bundala akiwa anatoka kijijini kwao kurudi kizumbi aliona vipande vinne vya almasi, ikiwemo ya rangi nyeusi pembezoni mwa mto akavichukua na kumpelekea boss wake Dr. Williamson. Dr Williamson alipoziona alichaganyiwa kwa furaha na maana alimasi hizo zilikuwa nzuri sana moja ikiwa na uzito wa carat 38. Akamwambia
Bundala ampeleke alipozichukilia, Bundala akiwa ameongozana na James na Dr. Williamson walifika sehemu ile na kuchimba kashimo kadogo wakatoa mchanga walipoosha walipata almasi nyingi sana.

Williamson alifurahi Sana na ndipo ndoto yake ya kuupata mlipuko wa volcano ikatimia. Alihamisha kambi yake kutoka kizumbi na kuileta Luhumbo na aliweka kambi chini ya Mbuyu, ( Mpaka leo Nembo Ya Mgodi Ni Mbuyu) kipindi hicho mtemi aliyekuwa anatawala hilo eneo alikuwa anaitwa NG'WADUBHI na eneo lake lilikuwa linajulikana kuwa BHUTEMI BHONG'WADUBHI. Dr. Williamson aliongea na mtemi akamruhusu kuanza kazi ya kuchimba almasi na alimuomba mtemi awahamishe wanakijiji waliokuwa wanakaa eneo hilo.
Eneo ulipo mgodi wa mwadui kilikuwa na vijiji vinane ambavyo ni ITUGUTU, NGW'ABHUKANGW'A, NGW'AGAGALA, ISHIDA, IBHELAMBASA, JINAMELI, LUHUMBO na GABHONDO. Mtemi pamoja na wananchi wake wakahama na kumwachia hilo eneo.

Mtemi akajengewa makazi mapya kijiji cha Utemini japo kipindi wanahamia walihama na jina lao la Luhumbo, baadae likapotea ikawa utemini wakimanisha kwa mtemi.

Dr. Williamson alifanya kazi kwa miaka kazaa wakiwa wanachimba watu na kusomba mchanga kupeleka
kwenye k**ashine kadogo alikokuwa nako. Mwaka 1942 alienda Dar Es Salaam kusajili kampuni yake na aliisajili kwa jina la Williamson Diamond Ltd. Ikiwa na mtaji wa €20,000 na ikiwa na hisa 400 yeye akamiliki hisa 299 na akampa kaka yake anayejulikana kwa jina la Percy hisa 100 na rafiki yake Bwana Iqbal Chand Chopra akampa hisa 1. Huyu Mr Chopra ndiyo aliyemsaidi mambo ya kisheria kipindi anaenda kusajili kampuni yake.

Aliamua kuuita mgodi wake jina la Mwadui jina la mtemi aliye mkaribisha, kwa kisukuma alikuwa
anaitwa Ng'wadubhi. Jina la Ng'wadubhi lilimshinda kulitamka ndipo akaita Mwadui.

Notes:
Mpaka hapo tumeona mvumbuzi wa mgodi ni kijana wa Kisukuma Bundala lakini kwenye mgawanyo wa hisa hakupewa hata nusu hisa, na habari yake inaishia hapo hakuandikwa tena kwenye hii stori.

Wazee wetu huwa wanatusimulia alipewa ajira ya kudumu mgodini hapo na kujengewa nyumba na kununuliwa Ng'ombe wengi sana.

ITAENDELEA

Credit: Njile Nkuba Sitta

HISTORIA YA DR. JOHN THOBURN WILLIAMSON   1John Thoburn Williamson alizaliwa huko Montfort, Quebec mnamo tarehe 10 Febru...
01/01/2026

HISTORIA YA DR. JOHN THOBURN WILLIAMSON 1

John Thoburn Williamson alizaliwa huko Montfort, Quebec mnamo tarehe 10 Februari 1907, ni wapili kuzaliwa kati ya watoto wanne kwenye familia yao. Baba yake, Bertie J Williamson,alikuwa ni Mscotland ambaye alikuwa amehamia Canada kutokae Ireland. Mama yake, Rose C Boyd alikuwa Mfaransa.

Mnamo mwaka 1919 Familia hiyo ilihama kutoka Montfort na kuhamia Montreal ambapo John alienda shule ya upili ya Macdonald huko Ste Annede Bellevue. Kutoka hapo aliingia Chuo Kikuu cha Mc Gill mnamo 1925 ambapo alisoma sheria. lakini baadae
aliamua kubadili masomo na kusoma jiografia.

Alipata shahada ya BA mnamo 1928, Shahada ya Uzamili ya Sayansi mnamo 1930 na Shahada ya Uzamivu mnamo 1933. Profesa wake wa zamani wa Jiolojia, Dk Richard Graham, alialikwa Johannesburg kukagua ardhi ambayo kampuni ya De Beers walita kakufanya uchunguzi. Williamson aliongozana na Dk Graham na kutoa hotuba fupi katika Chuo Kikuu cha Witwatersrand.

Baada ya hapo John T. Williamson alialikwa kujiunga na kampuni ndogo ya De Beers Consolidines Mines, k**a mtaalam wa jiolojia ambapo alikubali.
Kampuni hiyo ilikuwa ikifanya utafiti wa shaba katika nchi ya Rhodesia ya kaskazini mashariki, (Zimbabwe)
Dr Williamson aliwafuata wakurungezi wa De Beers na kuwaomba wamdhamini akafanye utafiti wa madini ya almasi katika nchi ya Tanganyika lakini walimkatalia na akaamua kujiuzulu kufanya kazi katika kampuni hiyo.

Dr Williamson aliamua kujiunga na Kampuniya Tanganyika Gold and Diamond Development
mnamo1935, akifanyakazi chini ya mtaalam wao mkuu wa jiolojia, Hank Le Tendresse, Mmarekani ambaye alimkubali Sana John Thoburn Williamson, Hata hivyo hakulidhika kufanyakazi Na kampuni hiyo. Mnamo Mei 1936 Dr Williamson alisafiri kwenda Mwanza kumtafuta Wakili mwenye asili ya Asia aliyekuwa anasheshimika sana, Bw Iqbal Chand Chopra KC. Walikutana tarehe 16 Mei1936.

Bwana Iqbal anasem,"Dr John Thoburn Williamson, aliletewa ndani ya chumba cha ofisi yangu akiwa na shati nyeupe na suruali ya khaki alitaka nimsaidie mambo ya kisheria ili aweze kufanya kazi yake ya utafiti wamadini ya almasi, na alihitaji kufadhiliwa pia."

Mnamo mwaka 1937 Kampuni ya Tanganyika Goldand Diamond Development ilisitisha shughuli za utafiti na kuanzia hapo Dr Williamson akawa huru kufanya kazi peke yake. Bwana Chopra aliungana na Dr Williamson na wakaanza kazi ya utafiti wa almasi. Waliaza utafiti pembezoni mwa Ziwa Victoria na Mikoa ya Magharibi bila mafanikio yoyote.

Alivumilia huko msituni na wavulana wawili wa aminifu wa Kiafrika, Bundala na James. Dr Williamson alikuwa ameweka kambi katika kijiji cha Kizumbi (mkoa wa shinyanga) na alikuwa anazunguka huku na huko akifanya utafiti wake na kisha kurudi kambini kwake. Na hakuwa na mtaji wa kutosha ilifikia hatua akabakiwa na dolla100 tu.

Hali hiyo ilimuweka njia panda kwani vifaa vyake vilikuwa vinahitaji matengenezo na wafanyakazi wake walikiwa wanamdai mshahara. Aliamua kupunguza wafanyakazi na kuamua kumalizia mchanga wake ili afungashe vilago aondoke zake. Wakati wanamalizia kuuosha mchanga huo alipata vipande viwili vya almasi vichafu kimoja kikiwa na uzito wa kareti 30, almasi hiyo ilimpa nguvu ya kuendelea na kazi.

ITAENDELEA

Credit: Njile Nkuta Sitta

Wangapi Mnamkumbuka Silas Mayunga?MBABE WA VITA YA KAGERALUTENI JENERALI SILAS MAYUNGA (MTI MKAVU) – R.I.PItakumbukwa ku...
31/12/2025

Wangapi Mnamkumbuka Silas Mayunga?
MBABE WA VITA YA KAGERA
LUTENI JENERALI SILAS MAYUNGA (MTI MKAVU) – R.I.P
Itakumbukwa kuwa tarehe Novemba 1, 1978, majeshi ya aliyekuwa Rais wa Uganda, Idi Amin, yalivamia Mkoa wa Kagera. Uvamizi huo ulimlazimu Hayati Mwalimu Julius Nyerere kutoa kauli ya kihistoria kabla hata vita kuanza, akiashiria ushindi kwa kusema:
> “Sababu ya kumpiga tunayo, nia ya kumpiga tunayo, na uwezo wa kumpiga tunao.”
Kauli hii haikuhitaji silaha pekee k**a risasi, mizinga au makombora ili isimamiwe, bali ilihitaji mashujaa wa kweli wa mstari wa mbele vitani.
Miongoni mwa mashujaa hao ni Luteni Jenerali Silas Mayunga, pamoja na wapiganaji wengine wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Watanzania kwa ujumla waliotoa mchango wao kwa hali na mali, hata kufikisha ng’ombe na kuku kwa ajili ya kuwalisha wapiganaji waliokuwa uwanjani.
Akiwa mstari wa mbele vitani, Luteni Jenerali Mayunga na wenzake walishika hatamu za mapambano kikamilifu. Kazi yao ilikuwa moja tu kufa au kupona kwa ajili ya kulinda hadhi na heshima ya Tanzania, na pia heshima ya wapenda haki duniani kote.
Ni kupitia Vita ya Kagera ndipo jina la Luteni Jenerali Mayunga lilipoanza kujulikana zaidi ndani ya JWTZ na hata kwa Jeshi la Uganda. Vita hiyo ilimthibitisha wazi kuwa alikuwa mpiganaji jasiri wa aina yake, hasa akiwa mstari wa mbele.
Safari yake ya kijeshi ilimfikisha katika nchi mbalimbali, ikiwemo Israel na Canada. Alihitimu mafunzo ya kijeshi tarehe Julai 26, 1963 nchini Israel, na miaka kumi baadaye (1973) alihitimu Kozi ya Unadhimu na Uk**anda wa Jeshi nchini Canada. Aidha, alihitimu Kozi ya Uk**anda wa Juu wa Jeshi mwaka 1974.
Tarehe Juni 21, 1995, Luteni Jenerali Mayunga aliweka rekodi binafsi baada ya kupandishwa cheo cha juu jeshini kuwa Luteni Jenerali, na miezi sita baadaye, tarehe Desemba 31, 1995, alistaafu rasmi utumishi wa jeshi.
Katika uongozi wake, Mayunga amewahi kuwa Mkurugenzi wa Mafunzo Makao Makuu ya Jeshi, Kamanda wa Brigedi ya 202 Tabora, na Kamanda wa Divisheni za 20 na 30 za JWTZ.
Huwezi kuizungumzia Operesheni Chakaza wakati wa vita dhidi ya majeshi ya Idi Amin bila kumtaja Luteni Jenerali Mayunga. Katika operesheni hiyo, alikuwa Kamanda wa Brigedi ya 206, akiongoza mapambano kwa uhodari mkubwa.
Ndani ya Jeshi la Uganda, jina la Mayunga lina historia ya kipekee. Aliwahi kuwa Kamanda wa Kikosi Maalumu cha JWTZ nchini Uganda kati ya mwaka 1979 hadi 1980.
Mbali na majukumu ya kijeshi, Mayunga pia alihudumu katika nafasi za kiraia na kidiplomasia. Aliwahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida (1977–1978), Balozi wa Tanzania nchini Nigeria (1989–1998), na baadaye Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuanzia 1998 hadi 2002, alipostaafu.
Luteni Jenerali Silas Mayunga alifariki dunia tarehe Agosti 5, 2011, nchini India. Hakufariki kwa risasi, mizinga wala milipuko k**a ilivyokuwa ikihofiwa na familia yake alipokuwa vitani, bali alifariki akiwa kitandani wakati wa matibabu.
Ewe Kamanda Mayunga, tunakulilia na tunasikitika kwa kifo chako, lakini pia tunajivunia kwa kutimiza wajibu wako kwa Tanzania na kwa dunia.
Kwa kila kijana wa Kitanzania, huu ni ujumbe: hakikisha unaacha alama muhimu Tanzania na duniani, ili kuwafundisha na kuwaongoza watakaoendelea kuishi baada ya wewe kuondoka duniani.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu ibariki Afrika.
Kwa msaada wa kumbukumbu za JWTZ.

HISTORIA KATIKA PICHA.Kwenye picha hii kuna watu Wanne.Hao wanaume WeusiMmoja ni Susi Na mwingine ni Chuma Wakiwa Nchini...
27/12/2025

HISTORIA KATIKA PICHA.
Kwenye picha hii kuna watu Wanne.
Hao wanaume Weusi
Mmoja ni Susi Na mwingine ni Chuma Wakiwa Nchini Uingereza Kwenye Mazishi ya Dr.Livingstone.

Chuma na Susi ndio Waafrika Pekee waliobeba Mwili wa Dr.Livingstone, kutoka Chitambo nchini
Zambia alikofia Mpaka Bagamoyo ambapo Huko mwili wa Dr.Livingstone ulisafirishwa Kwenda
Nchini Uingereza miaka ya 1873. Hapo walipo ni nchini Uingereza, ambapo Chuma na Susi
walialikwa Kwenye Mazishi ya Dr.Livingstone huko Nchini Uingereza.

Huyo Mwanamke na Mwanaume waliopo ukutani ni Watoto wa Dr. Livingstone. Na Huyo
Mwanamke kuna mtoto wake mmoja (Mjukuu wa Dr. Livingstone) alikuja nchini Tanzania miaka ya 2012. Na kutembelea sehemu zote ambazo Dr. Livingstone
alitembelea.

Na huyo mwanaume mzungu aliyekaa chini ni mchungaji. Na ukiangalia kwa chini, unaweza kuona ngozi ya Simba imetandikwa hapo. Hiyo ngozi ya Simba ilikuwa moja ya Zawadi waliobeba Susi na
Chuma kutoka huku Afrika.

Na pia Baadhi ya Sehemu za Mwili wa Dr.Livingstone ziliachwa baadhi ya Sehemu ambazo Dr.Livingstone alipata Kukaa. Kwa mfano Huko Tabora kwenye makumbusho ya Kwihala Kuna
nywele za Dr. livingstone.

Shirati-Musoma.Mtawala Mjerumani katika kudumisha utawala wake alileta askari Wanubi kutoka Sudan na Wazulu toka Msumbij...
24/12/2025

Shirati-Musoma.

Mtawala Mjerumani katika kudumisha utawala wake alileta askari Wanubi kutoka Sudan na Wazulu toka Msumbiji hili kuwakabili akina Abushiri,Mkwawa na hata vita ya majimaji.

Baadaye akaanzisha kambi kubwa Shirati-Musoma.

Huko akakutana na Wakurya,akaona hawa wana damu ya kijeshi.

Ndio ukawa mwanzo wa wakurya kuwa wengi jeshini.

Pichani wote ni askari wa Kikurya.

HASHIM MSHAM MPULA MPOTO BABA YAKE ALI MSHAM Picha hiyo hapo chini ni moja kati ya picha 11 Ali Msham alizowaachia wanae...
24/12/2025

HASHIM MSHAM MPULA MPOTO BABA YAKE ALI MSHAM

Picha hiyo hapo chini ni moja kati ya picha 11 Ali Msham alizowaachia wanae kabla ya kufariki dunia mwaka wa 2002.

Katika picha hiyo ya mwaka 1955 kulia katika picha ya kwanza ni Ali Msham, Hashim Mpula Mpoto (baba yake Ali Msham) Ali Msham, Julius Nyerere na huyo mwanamke aliyeshika saa ni Bi. Khadija bint Feruzi, hao wengine sijapata majina yao.

Katika picha ya pili wa kwanza ni Mzee Hashim Mpula Mpoto.

Nyumba ya Bi. Khadija bint Feruzi ambae katika picha kashika saa ya ukutani ipo Mtaa wa Kionga si mbali na kwangu na nilibahatika kufahamiana na mwanae marehemu Athumani Juma Kassanda aliyezaliwa mwaka wa 1943 na tulijenga urafiki mkubwa katika muda mfupi sana.

Nimepokea mengi katika historia ya Tawi la TANU la Ali Msham kutoka kwake kwani lilikuwa jirani na nyumbani kwao yeye akiwa mtoto wa kiasi cha miaka 11 wakati TANU inaundwa New Street na Tawi la TANU la Ali Msham linafungulia jirani na kwao mama yake akiwa mmoja wa wanachama wa mwanzo wa tawi hilo.

Hii picha ilikuwa siku Tawi la TANU la Ali Msham lilipomwalika Julius Nyerere, Rais wa TANU aje kwenye TANU wamkabidhi meza na viti vitatu kwa ajili ya ofisi yake pale New Street (Lumumba Avenue).

Kiti alichokalia Mwalimu Nyerere kilikuwa kiti kilichokuwa kinazunguka na ukikitazama utakiona hivyo katika umbo lake.

Kiti hiki Abdallah Omari Likonda, mtoto wa dada yake Ali Msham na mjukuu wa Mzee Hashim Msham Mpula Mpoto ameeleza kilitengenezwa na Said Msham mdogo wake Ali Msham.

Hii si picha ya kawaida.

Picha yoyote ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiwa na wazalendo wapigania uhuru wa Tanganyika kamwe haiwezi kuwa picha ya kawaida si kwake Mwalimu wala kwa wale ambao wamo katika picha hiyo.

Maktaba imebahatika kukusanya picha mfano wa hii na In Shaa Allah nitakuwa naziweka hapa na kueleza historia inayobebwa na picha hizo.

UNAWAKUMBUKA HAWA?Stella Situmbi, Gabriel Yotam, Deogratius Kiduduye, Sandu George Mpanda a.k.a Kid Boy, Isaack Muyenjwa...
21/12/2025

UNAWAKUMBUKA HAWA?
Stella Situmbi, Gabriel Yotam, Deogratius Kiduduye, Sandu George Mpanda a.k.a Kid Boy, Isaack Muyenjwa Gamba, Alex Ngusa a.k.a Mwana Ngusa...Lamaaaa, Godwin Gondwe,Paul Mabuga,Mukhsin Mambo, Rosemary Mkangara,Rahabu Fungo/Fred,Fred Fidelis a.k.a Fredwaa,Samadu Hassan Maduhu,James Range, Agrippina Cosmas, Prince Baina Kamukulu,Steve Moyo Mchonge,Deo Kaji Makomba, Beatrice Rabach,Mkamiti Juma/Kibayasa, Ahmed Ally,Ramadhani Ngoda,Yahaya Hassan,Juma Ahmed Baragaza,Wambura Mtani, Glory Robinson, Angelo Mwoleka,, Raymond Nyamwihula,Razaro Matarange, Jacob Usungu a.k.a Young Millionaire, Rebecca Mlesi,....Kurwijira,Dotto Bulendu.,Sky Walker (jina kamili limenitoka), Bernard James akiwa dogo tu, Gabriel Zakaria, Peter Omary,Abdallah Tilata eebwanaeee ilikua hatari sana kwa hivi vichwa.

Pichani ni Marehem ISAAC MUYENJWA GAMBA alifariki 2018

STAR TV na RFA walibahatika kuwa na Watangazaji mahiri enzi zile, mmoja wapo ni SAUDA MWILIMA, Enzi hizo, Sauda Mwilima,...
20/12/2025

STAR TV na RFA walibahatika kuwa na Watangazaji mahiri enzi zile, mmoja wapo ni SAUDA MWILIMA,

Enzi hizo, Sauda Mwilima, Rahabu Fred, Glory Robinson, Prince Baina Mamukuru, Fred Fidelis, Yusuph Magasha, Wambura Mtani, Kid Bway, Sky walker, Zuber Musabaha, Baruwan Muhuza, Deokaji Makomba a.k.a "DK THE SIMPLE MAN", Gabriel Zakaria.... Daaah kitambo sana... WAHENGA karibuni.

WILBERT KLERRU (1929 - 1970): MKUU WA MKOA MSOMI ALIYEUAWA NA MKULIMA WA IRINGA!Wilbert Klerru alizaliwa yapata mwaka 19...
20/12/2025

WILBERT KLERRU (1929 - 1970): MKUU WA MKOA MSOMI ALIYEUAWA NA MKULIMA WA IRINGA!

Wilbert Klerru alizaliwa yapata mwaka 1929 na kupata elimu ya awali nchini Tanganyika. Baadaye alitunukiwa Shahada ya Uzamivu katika Sayansi ya Siasa (Doctorate in Political Science) katika Chuo Kikuu kimojawapo nchini Marekani mwaka 1962 na kurejea Tanganyika.

Baada ya hapo, Dkt. Klerru alianzia kazi za Siasa katika Makao Makuu ya TANU jijini Dar es Salaam akiwa Katibu Mwenezi (Publicity Secretary) wa TANU. Baada ya Katibu Mkuu wa TANU, Mheshimiwa Oscar Kambona kukimbilia kuishi uhamishoni nchini Uingereza mwaka 1967, Dkt. Klerru akachukua majukumu ya Katibu Mkuu wa TANU katika kipindi muhimu cha Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na Azimio la Arusha. Baadaye, Dkt. Kleruu alitumwa katika Mkoa wa Mtwara kusimamia utekelezaji wa Siasa ya Vijiji vya Ujamaa. Baada ya ufanisi mkubwa ulioonekana Mtwara ndani ya kipindi kifupi, Dkt. Kleruu alitumwa Iringa kuwa Mkuu wa Mkoa huo kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa uanzishwaji wa Vijiji vya Ujamaa na Mashamba ya Ujamaa.

Imeelezwa kuwa tarehe 25 Desemba 1970, Dkt. Kleruu aliwaruhusu dereva wake na wasaidizi wake kuendelea kusherekea Siku Kuu ya Krisimasi na yeye mwenyewe akaamua kuendesha gari la Ofisi hadi eneo la Isimani ambako alikwenda kutembelea na kukagua Vijiji kadhaa vya Ujamaa katika eneo lile. Akiwa njiani kurudi nyumbani kwake alipita katika Kijiji cha Mkungugu ambako alisimama kukagua maendeleo ya Mashamba ya Ujamaa.

Akiwa katika Kijiji cha Mkungugu, Dkt. Klerruu alimkuta mkulima mmoja maarufu na tajiri akilima katika shamba lake kubwa kwa kutumia trekta. Mkulima huyu aliitwa Said Abdullah Mwamwindi aliyekuwa na umri wa miaka 28. Inasemekana kuwa Dkt. Klerru alimuuliza Mwamindi kuwa ataendelea hadi lini na kilimo cha ubinafsi pasipo kujiunga na mfumo wa uzalishaji wa Mashamba ya Ujamaa?

Inasemekana Mwamwindi alimjibu Dkt. Klerruu kuwa ingawa alikuwa anaheshimu kanuni za Ujamaa, lakini ingelimgharimu sana yeye binafsi endapo angelitelekeza familia yake ya watu 9 na kulitoa shamba lake kwenye Shamba la Ujamaa. Dkt. Klerru inasemekana alimjibu Mwamwindi kuwa matatizo yake binafsi yasingeliweza kuruhusiwa kuwa kikwazo kwa mapinduzi ya kijamaa ambayo yalikuwa yakienea katika nchi nzima. Muda mfupi baadaye, mwili wa Dkt. Klerru ulikutwa karibu na mlango wa gari lake.

Hivyo ndivyo alivyouawa Dkt. Wilbert Klerru akiwa na umri wa miaka 39 tu akiwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa. Aliuawa na mkulima aliyeitwa Said Abdullah Mwamwindi kwa kupigwa risasi na mkulima huyo siku ya Krisimasi katika Kijiji cha Mkungugu, Isimani kilichopo yapata kilomita 26 hivi kutoka Iringa mjini.

Wiki mbili baada ya mauaji yale, watu 23 walik**atwa na kuwekwa ndani kuhusiana na mauaji akiwemo Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) wa Iringa. Uchunguzi wa Kimahak**a (judicial inquiry) ulianza mara moja kuchunguza mauaji ya Dkt. Klerru.

Kumbukumbu pekee iliyobaki kuhusiana na Dkt. Klerru ni Chuo cha Ualimu kilichopo Iringa ambacho kimepewa jina la Klerruu. Vijana wengi hawaijui vizuri historia ya nchi hii kwa mapana yake. Makala hii imeandikwa hapa ili iwe k**a tone la maji katika historia pana ya nchi.

Je, ni jambo gani limekushangaza, kukuhuzunisha au kukutia moyo kuhusu maisha mafupi ya Dkt. Wilbert Klerru?

NB: Source: The Story of Julius Nyerere

Unavikumbuka viayu hivi?Unakumbuka wapi uliviona na ulivivaa ukiwa mkoa gani?Mlikua mnaviitaje huko kwenu?
19/12/2025

Unavikumbuka viayu hivi?
Unakumbuka wapi uliviona na ulivivaa ukiwa mkoa gani?
Mlikua mnaviitaje huko kwenu?

  Mwadui 1959.Almasi inachambuliwa na mkono mmoja tu-huo mwingine umeshonewa uniform vidole havitokezi kabisa.Sasa k**a ...
18/12/2025


Mwadui 1959.

Almasi inachambuliwa na mkono mmoja tu-huo mwingine umeshonewa uniform vidole havitokezi kabisa.

Sasa k**a waweza kuiba kwa kutumia mkono mmoja sawa!!

Address

Tabata
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chakushangaza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Chakushangaza:

Share