17/08/2026
Hii nguvu tunayo weka sisi mashabiki kwenye kurumbana, kwa nini tusiweke kwenye kuijenga timu? 🤔 Ligi ndio kwanza imeanza, ila kila kukicha linazuka jipya. Sio kwa ubaya, lakini tukiendelea hivi hata mvuto tunapoteza.
Sisi wote tumekutanishwa na Simba ❤️🤍. Tuache malumbano yasiyo na tija, tuipambanie timu yetu. N.B: SISI NDIO MASHABIKI BORA! 🔥 Kwa nini tusiioneshe hiyo bora yetu kwa kuacha haya mambo ya kutupiana maneno?
TUWE SIMBA NGUVU MOJA, NA SIO KINGINEEEEE! 💪🏾❤️🤍