UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Vikosi vya Israel vimewauwa Wapalestina 15 hivi leo wakati viliposhambulia maeneo yaliyolenga nyumba na mahema huko Gaza...
24/09/2025

Vikosi vya Israel vimewauwa Wapalestina 15 hivi leo wakati viliposhambulia maeneo yaliyolenga nyumba na mahema huko Gaza.

Hayo yamesemwa na msemaji wa shirika la ulinzi wa kiraia katika eneo hilo alipozungumza na shirika la habari la AFP akisema mashambulio hayo ya Israel ni mwendelezo wa operesheni yake ya kijeshi ya angani na ardhini kwenye mji wa Gaza na ambayo imewalazimu maelfu ya watu kuondoka katika maeneo hayo yenye idadi kubwa ya watu.

Mhariri |

24/09/2025

Meddie Kagere akieleza sababu ya yeye kupendelea kufunga jicho moja anapofunga goli.

Ni sehemu ya mahojiano maalum aliyiyafanya na


24/09/2025

''Kazi kubwa ya mchezaji ambaye ni mshambuliaji ni kufunga goli'' Sehemu ya maneno ya Meddie Kagere, aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Simba akizungumza katika mahojiano maalum na .


24/09/2025

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Dkt Hussein Ali Mwinyi,serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya soko la asili la Chakechake ili libakie na uasili wake, huku ikipanga kujenga soko jipya la kisasa.

Dkt Mwinyi amebainisha hayo wakati akizungumza na wafanyabishara wa soko la Chakechake mkoa wa kusini ikiwa ni muendelezo wa kampeni zake za kuomba kura katika maeneo mbalimbali amesema serikali itaendela kuweka uwiano Sawa baina ya kisiwa cha unguja na kisiwa cha Pemba katika utekelezaji wa maendeleo.

✍ Mtumwa Saidi
Mhariri:

24/09/2025

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Makongoro Nyerere amewaasa vijana wahitimu wa mafunzo ya awali ya JKT katika Kikosi cha Luwa mkoani Rukwa kutumia vizuri mitandao ya kijamii ili kuepuka kujiingiza kwenye vitendo vibaya vya mmomonyoko wa maadili katika jamii na Taifa lao.

Taarifa ya Sammy Kisika inaeleza zaidi.
Mhariri |

Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Septemba 24, 2025 ametembelea na kuweka sh...
24/09/2025

Mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Septemba 24, 2025 ametembelea na kuweka shada la maua kwenye kaburi la aliyekuwa Rais wa wwamu ya tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, katika kijiji cha Lupaso, wilayani Masasi, mkoani Mtwara.

Dkt. Samia amemuelezea hayati Mkapa k**a kiongozi wa mfano ambaye alileta mageuzi makubwa ya kisiasa na kiuchumi nchini, hususan kupitia sera za uwazi, uwajibikaji na diplomasia zilizoisaidia Tanzania kupiga hatua kimaendeleo.

Aidha, amesisitiza kuwa historia ya Taifa haiwezi kukamilika bila kumtaja Mzee Mkapa kutokana na mchango wake mkubwa katika kuimarisha taasisi za kitaifa na kusimamia miradi yenye manufaa kwa wananchi.

Hayati Benjamin William Mkapa aliongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 na alifariki dunia Julai 23, 2020.


24/09/2025

Tazama utani wa msemaji wa Issa Liponda kwa Msemaji wa Ahmed Ally kuhusu Kocha.

Mhariri |

24/09/2025

Kocha wa Fountain Gate Denis Kitambi amesema wachezaji wake wamejiandaa vizuri kuhakika wanaondoka na ushindi mbele ya wapinzani wao Simba katika mchezo utakaopigwa kesho katika dimba la Benjamin Mkapa.

Mechi itakuwa live

Mhariri |

24/09/2025

Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema wachezaji wake wamejiandaa kwa kuhakikisha wanaondoka na alama tatu kwenye mchezo wao dhidi ya Fountain Gate utakaopigwa kesho katika dimba la Benjamin Mkapa.

Ameeleza hayo leo kwenye mkutano wa waandishi wa habari wakizungumzia maandalizi ya mchezo huo.

Mechi itakuwa live

Mhariri |

24/09/2025

‘’Mechi hii tunaitumia k**a kuwakaribisha rasmi wachezaji wetu wapya tuliowasajili’’ Sehemu ya maneno ya Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo wao dhidi ya Fountain Gate utakaopigwa kesho katika dimba la Benjamin Mkapa.

Mhariri |

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Kansela wa Jamhu...
24/09/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Kansela wa Jamhuri ya Austria Christian Stocker, mazungumzo yaliyofanyika pembezoni mwa Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani.

Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha maeneo mbalimbali ya ushirikiano baina ya Tanzania na Austria.

Dkt. Mpango yuko nchini Marekani kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Mhariri |

24/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amefika katika eneo la Msasani jijini Dar es Salaam nyumbani kwa mwanamke mjane ambaye amedai kuvamiwa na kuondolewa nyumbani kwake kwa nguvu.

Tukio hilo linajiri baada ya siku moja kuonekana video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii akionekina mwanamke huyo akiondoshwa katika nyumba aliyokuwa akiishi ikidaiwa kwamba aliyemuondosha ni mtu aliyekuwa akimdai marehemu mume wake.

Sikiliza maagizo ya Mkuu wa Mkoa Chalamila.

Mhariri |

Address

1 Mandela Road
Dar Es Salaam
12301

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Share

Category