
24/09/2025
Vikosi vya Israel vimewauwa Wapalestina 15 hivi leo wakati viliposhambulia maeneo yaliyolenga nyumba na mahema huko Gaza.
Hayo yamesemwa na msemaji wa shirika la ulinzi wa kiraia katika eneo hilo alipozungumza na shirika la habari la AFP akisema mashambulio hayo ya Israel ni mwendelezo wa operesheni yake ya kijeshi ya angani na ardhini kwenye mji wa Gaza na ambayo imewalazimu maelfu ya watu kuondoka katika maeneo hayo yenye idadi kubwa ya watu.
Mhariri |