UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Jeshi la Iran limesema litalinda miundombinu na mali ya umma, likiwataka Wairani kuzuia njama za adui huku mamlaka zikik...
11/01/2026

Jeshi la Iran limesema litalinda miundombinu na mali ya umma, likiwataka Wairani kuzuia njama za adui huku mamlaka zikikandamiza maandamano.

Taarifa ya jeshi la Iran imetolewa baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutoa onyo jipya kwa viongozi wa Iran siku ya Ijumaa, na baada ya Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio kutangaza kwamba "Marekani inawaunga mkono watu jasiri wa Iran."

Machafuko yameendelea usiku kucha huku vyombo vya habari vya serikali vikisema kuwa jengo la manispaa lilichomwa moto mjini Karaj, magharibi mwa Tehran, na kuwalaumu "wachochezi kwa ghasia".

Televisheni ya taifa imerusha picha za mazishi ya wanachama wa vikosi vya usalama ambao ilisema waliuawa wakati wa maandamano katika miji ya Shiraz, Qom na Hamedan.

Mhariri |

Leo ni kumbukizi ya kuzaliwa Mtangazaji wa    , ungana nasi kumtakia kheri ya kuzaliwa kwake.
11/01/2026

Leo ni kumbukizi ya kuzaliwa Mtangazaji wa , ungana nasi kumtakia kheri ya kuzaliwa kwake.

11/01/2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amewataka wataalamu na viongozi wa Halmashauri zote za mkoa huo kuwa wabunifu katika kuibua fursa mbalimbali za kiuchumi zitakazowawezesha vijana kujiajiri na kujipatia kipato.

Akizungumza wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), Mtanda amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana na kwa kiasi kikubwa kupunguza makundi ya uhalifu katika jamii.

Amesisitiza kuwa Halmashauri zina wajibu wa kubuni miradi itakayowashirikisha vijana moja kwa moja ili kuwajengea uwezo wa kiuchumi na kuchangia maendeleo ya mkoa wa Mwanza kwa ujumla.

Mhariri |

11/01/2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mazingira ya kujifunzia kwa kujenga skuli za kisasa zenye hadhi, viwango na ubora unaokidhi mahitaji ya elimu ya karne ya sasa.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipofungua Skuli mbili za Ghorofa za Ramadhan Haji Faki iliyopo Gamba, Mkoa wa Kaskazini Unguja, pamoja na Skuli ya Kifundi iliyopo Pemba.

Amesema ujenzi wa skuli hizo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuondokana na skuli za mabanda na badala yake kuwa na majengo ya kudumu yanayokidhi viwango vya kisasa vya elimu, jambo litakalosaidia kuongeza ufanisi wa ufundishaji na mafunzo.

Mhariri |

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia Wakimbizi limesema zaidi ya raia wa Kongo 50 waliokimbia vita mashariki mwa n...
11/01/2026

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia Wakimbizi limesema zaidi ya raia wa Kongo 50 waliokimbia vita mashariki mwa nchi yao wamekufa nchini Burundi.

Shirika hilo limesema kati ya jumla ya vifo 53 vilivyorekodiwa, watu 25 wamekufa kutokana na mlipuko wa kipindupindu, huku wengine sita wakifariki kutokana na upungufu wa damu na matatizo mengine yanayohusiana na utapiamlo.

Jean Jacques Purusi, gavana wa jimbo la Kivu Kusini ambapo Uvira iko, ameieleza hali inayowakabili raia wa Kongo waliokimbilia Burundi kuwa ni ya "taabu" na kwamba ni mgogoro uliosahaulika na jamii ya kimataifa. Burundi kwa upande wake haijatoa maoni juu ya taarifa hiyo.

Mhariri |

09/01/2026

Wananchi wa kijiji cha Ntinga, kata ya Msangano, wilayani Momba mkoani Songwe, wamelazimika kuyahama makazi yao na kutafuta hifadhi katika maeneo ya jirani kufuatia mafuriko ya maji yaliyovamia makazi yao baada ya mvua kubwa kunyesha usiku wa kuamkia leo katika wilaya za Ileje, Mbozi na Tunduma.

Inaelezwa kuwa mafuriko hayo yaliyoanza saa 9 usiku yamesababisha maji kuzingira makazi ya wananchi, kuharibu vyakula vilivyokuwa ndani ya nyumba na kuwaacha wakazi hao bila hifadhi ya kulala usiku, licha ya maji kuanza kupungua katika baadhi ya maeneo.

Diwani wa kata ya Msangano amesema kuwa kutokana na mafuriko hayo, wananchi wako katika hatari ya kukumbwa na magonjwa ya mlipuko, hivyo ametoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua za haraka za kiafya na kibinadamu ili kudhibiti athari zaidi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Momba, Elias Mwandobo, ametembelea kijiji hicho kujionea hali halisi na kueleza kuwa Serikali imeanza kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa wananchi. Aidha, amewataka wakazi hao kuwa watulivu, kushirikiana wao kwa wao wakati Serikali ikiendelea kufanya tathmini ya madhara yaliyojitokeza.

✍Joyce Lyanda
Mhariri |

09/01/2026

Je, watajipangaje uwanjani...???

Swali hili linajibiwa leo

Ni Singida BS vs Yanga SC ni leo saa 2:15 usiku LIVE

09/01/2026

Kwahiyo Mlandege aliifunga timu mbovu mwaka ule, si ndiyo...!!!???

Leo ni zamu ya Singida BS vs Yanga SC saa 2:15 usiku LIVE

Jeshi la Lebanon limesema limekamilisha awamu ya kwanza ya mpango wake wa kupokonya silaha kundi la Hezbollah kusini mwa...
09/01/2026

Jeshi la Lebanon limesema limekamilisha awamu ya kwanza ya mpango wake wa kupokonya silaha kundi la Hezbollah kusini mwa nchi hiyo, hatua ambayo Israel imeitaja kuwa ya matumaini.

Hatua hiyo inajiri chini ya shinikizo kubwa kutoka Marekani na hofu ya kuongezeka kwa mashambulio ya Israel.

Jeshi hilo limesema awamu ya kwanza imelenga eneo lililo kusini mwa Mto Litani, isipokuwa maeneo ambayo bado yanakaliwa na wanajeshi wa Israel karibu na mpaka.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, yuko nchini Lebanon kwa mazungumzo kuhusu kile anachokiita tishio la Israel katika eneo hilo., Huku Rais wa nchi hiyo, Joseph Aoun, akiunga mkono hatua za jeshi, akisema lengo ni kuhakikisha serikali pekee ndiyo yenye mamlaka ya kubeba silaha na kufanya maamuzi ya vita na amani.

Mhariri |

Jeshi la Syria limetangaza amri ya kutotoka ndani katika maeneo ya Sheikh Maqsoud na Ashrafieh na kuwataka wakazi wahame...
09/01/2026

Jeshi la Syria limetangaza amri ya kutotoka ndani katika maeneo ya Sheikh Maqsoud na Ashrafieh na kuwataka wakazi wahame mara moja, likisema litalenga maeneo yanayodaiwa kutumiwa na wapiganaji wa SDF.

Maelfu ya raia tayari wamekimbia makazi yao, huku vifo na majeruhi vikiripotiwa kuongezeka.

SDF imesema inapambana na makundi yanayoiunga mkono Syria karibu na kitongoji kinachokaliwa na Wasyria na kudai kuwa imewasababishia hasara kubwa.

Waziri Mkuu wa Serikali ya Kikurdi ya Iraq, Masrour Barzani, ameeleza wasiwasi wake kuhusu mashambulio dhidi ya vitongoji vya Wakurdi, akionya kuwa yanaweza kufikia kiwango cha maangamizi ya kikabila.

Mhariri |

09/01/2026

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imefanya operesheni mwishoni mwa Desemba 2025 na kufanikiwa kukamata kilogramu 9,689.833 za dawa za kulevya, pikipiki 11 na magari matatu, huku watuhumiwa 66 wakikamatwa kuhusiana na uhalifu huo.

Mhariri |

09/01/2026

: Tazama Ally Kamwe ‘alivyomwaga chozi’ baada ya Azam FC kuitoa Simba SC kwenye mchezo wa nusu fainali ya .

Hasheem Ibwe alikuwa na kazi ya kumtuliza.

FT: Azam FC 1-0 Simba SC (Lameck Lawi 73')

Leo ni Singida BS dhidi ya Yanga SC, saa 2:15 usiku LIVE

Address

1 Mandela Road
Dar Es Salaam
12301

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Share

Category