
20/08/2025
Rais wa Kenya William Ruto ameunda jopo la pamoja linaloshirikisha idara na mashirika mbalimbali ili kupiga jeki vita dhidi ya ufisadi nchini humo.
Jopo kazi hilo linahusisha asasi na tume kumi zitakazofanya kazi pamoja kukomesha ufisadi nchini Kenya ili kuunda mustakabali mpya wa kukomesha vitendo vya rushwa.
Rais ruto ambaye amesafiri kuelekea Japan, amesema kuwa vita dhidi ya wizi na ufujaji wa mali ya umma sasa vitakuwa na adhabu kali na ya kesi za ufisadi kutatuliwa kwa haraka zaidi.
✍