UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Zaidi ya waathirika 500 wamethibitishwa kuugua maradhi ya Ebola katika mlipuko unaoendelea kuenea katika Afrika ya Kati,...
07/06/2026

Zaidi ya waathirika 500 wamethibitishwa kuugua maradhi ya Ebola katika mlipuko unaoendelea kuenea katika Afrika ya Kati, kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa Juni 6, huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu ukubwa unaoongezeka wa janga hilo.

Katika taarifa ya kila siku kuhusu hali ya mlipuko huo, WHO imeripoti watu 452 kuugua maradhi hayo na vifo 82, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ambako mlipuko huo ulitangazwa wiki tatu zilizopita.

Nchini Uganda, shirika hilo limeripoti watu 19 kuugua maradhi hayo, vikiwemo vifo viwili.

Maafisa wa Afya wameonya kuwa bila hatua madhubuti za afya ya umma, mlipuko wa sasa unaweza kufikia kiwango cha janga la Ebola la Afrika Magharibi la mwaka 2014, ambalo liliua Zaidi ya watu 11,000.

✍️ Alinda Kato

06/06/2026
Wakati Serikali ikihimiza utekelezaji wa miradi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, imeelezwa mtazamo hasi w...
06/06/2026

Wakati Serikali ikihimiza utekelezaji wa miradi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, imeelezwa mtazamo hasi wa baadhi ya wananchi kuhusu mfumo huo ni miongoni mwa changamoto zinazokwamisha miradi hiyo nchini.

Hayo yamebainishwa na Mhadhiri Idara ya Usimamizi wa Biashara na Menejimenti Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), ambaye ameeleza historia ya Tanzania imechangia hisia kuhusu baadhi ya miradi ya ubia inaweza kuwa na sura ya unyonyaji.

Amesema katika kipindi ambacho nchi inafanya mageuzi ya kiuchumi kuelekea uchumi wa soko, bado kuna wananchi wanaoutazama ushiriki wa sekta binafsi kwa tahadhari, jambo linaloathiri namna wanavyoupokea na kuunga mkono utekelezaji wa miradi ya ubia.

Kwa mujibu wa Dkt Aman, hali hiyo inaonesha umuhimu wa kuelimisha umma ili kubadili mtazamo kuhusu nafasi ya sekta binafsi katika kuchochea maendeleo ya taifa kupitia ushirikiano na Serikali.

Mhariri |

06/06/2026

Una chaneli ya YouTube na kila mara huwa unawaomba watu wa “subscribe”? K**a ndiyo, basi leo anakuletea neno la Kiswahili fasaha ambalo wengi hawalitumii, ilhali ndilo sahihi zaidi.

Tazama video hii kujua neno hilo, na baada ya hapo tuambie umewahi kulisikia na ulikuww unalijua?

Endelea kusikiliza UFM 107.3 Dar es Salaam na kufuatilia kurasa zetu za mitandao ya kijamii ili uendelee kupata taarifa zaidi. UFM Sisi ni wewe.



✍🏽 jackline_mgina

Unakumbuka picha hii ilikuwa fainali ya mwaka gani za Kombe la Dunia?
06/06/2026

Unakumbuka picha hii ilikuwa fainali ya mwaka gani za Kombe la Dunia?

06/06/2026

“Ronaldo apate, asipate kombe la dunia tupo naeee.” .chemical_tz

Endelea kusikiliza UFM 107.3 Dar es Salaam na kufuatilia kurasa zetu za mitandao ya kijamii ili uendelee kupata taarifa zaidi. UFM Sisi ni wewe.

Katika kipindi cha   wiki hii… Utamsikia Mwanamke wa nguvu, mama anayeng’ara katika mitandao ya kijamii akiitendea haki ...
06/06/2026

Katika kipindi cha wiki hii… Utamsikia Mwanamke wa nguvu, mama anayeng’ara katika mitandao ya kijamii akiitendea haki sanaa ya uchekeshaji akipambana na kuitumia teknolojia kufanya shughuli zake.

Mwanamke huyu jasiri na mwenye uthubutu wa viwango vya juu, Conchester Ishengili (Mama Mawigi).

Atafunguka mengi katika kipindi cha . Ni Jumapili kuanzia saa 8:00 mchana - 9:00 Alasiri hapa hapa UFMRadio.

Usikose

Mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kati ya Mexico na Afrika Kusini inatazamiwa kuwa moja ya matukio ya liv...
05/06/2026

Mechi ya ufunguzi ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 kati ya Mexico na Afrika Kusini inatazamiwa kuwa moja ya matukio ya live yatakayotazamwa zaidi.

FIFA inatarajia mechi hiyo ya ufunguzi kuvutia zaidi ya watazamaji bilioni 1.5 kote ulimwenguni, idadi ambayo itazidi idadi ya watazamaji wa Super Bowl sambamba na baadhi ya matukio makubwa zaidi ya kimataifa katika historia.

Mtanange huo unaunganisha mataifa mawili yenye mapenzi makubwa ya mpira wa miguu, huku michuano hiyo yenyewe ikisubiriwa kwa hamu, ikishirikisha timu 48 na jumla ya mechi 104.

Endelea kusikiliza UFM 107.3 Dar es Salaam na kufuatilia kurasa zetu za mitandao ya kijamii ili uendelee kupata taarifa zaidi. UFM Sisi ni wewe.



✍🏽 jackline_mgina

05/06/2026

Simba na Yanga na wote wapo kwenye nafasi ya ubingwa wa taji la CRDB Confederation Cup, kutokana na michezo iliyopo mbele yao.

Endelea kusikiliza UFM 107.3 Dar es Salaam na kufuatilia kurasa zetu za mitandao ya kijamii ili uendelee kupata taarifa zaidi. UFM Sisi ni wewe.

05/06/2026

part 11

Address

1 Mandela Road
Dar Es Salaam
12301

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Share

Category