UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Mwanaharakati mashuhuri wa kutetea haki za binadamu nchini Kenya Boniface Mwangi ameshtakiwa kwa kumiliki risasi kinyume...
21/07/2025

Mwanaharakati mashuhuri wa kutetea haki za binadamu nchini Kenya Boniface Mwangi ameshtakiwa kwa kumiliki risasi kinyume cha sheria baada ya kutuhumiwa kuwa na dhima katika maandamano mabaya dhidi ya serikali.

Polisi ilimk**ata Mwangi, mwenye umri wa miaka 42, wiki iliyopita na kusema wamepata ushahidi kutoka nyumbani kwake, ikiwa ni pamoja na mabomu ya kutoa machozi ambayo bado hayajatumika, simu mbili za mkononi, kompyuta na vijitabu kadhaa vya kutunza kumbukumbu.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahak**a ya Rufani, Jacobs Mwambegele leo amefungua mafunzo kwa wa...
21/07/2025

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahak**a ya Rufani, Jacobs Mwambegele leo amefungua mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu kwa tarehe itakayotangazwa na Tume.

Jaji Mwambegele amewataka watendaji hao kutoa taarifa mapema kwa vyama vya siasa kuhusu utaratibu wa kuwaapisha mawakala.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kwenye mikoa mbalimbali nchini kwa siku tatu na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo.

Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu mbili ambapo awamu hii ya pili inahusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi, Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.

Shirikisho la Mpira nchini Kenya limetoa taarifa ikieleza Harambee Stars imejiondoa katika michuano ya CECAFA.Taarifa il...
21/07/2025

Shirikisho la Mpira nchini Kenya limetoa taarifa ikieleza Harambee Stars imejiondoa katika michuano ya CECAFA.

Taarifa iliyotolewa leo na shirikisho hilo imeeleza uamuzi huo umetokana na ushauri na mapendekezo yaliyotolewa na benchi la ufundi la timu hiyo likiongozwa na kocha mkuu Benni McCarthy.



Waziri Mkuu wa China Li Qiang ametangaza kuanza kwa ujenzi wa bwawa kubwa zaidi la kuzalisha umeme duniani, kwenye uking...
21/07/2025

Waziri Mkuu wa China Li Qiang ametangaza kuanza kwa ujenzi wa bwawa kubwa zaidi la kuzalisha umeme duniani, kwenye ukingo wa mashariki wa Tibet, kwa gharama inayokadiriwa dola bilioni 170.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Xinhua, bwawa hilo litakalokuwa na vituo vitano vya kufua umeme litazalisha kilowati bilioni 300 za umeme kila mwaka, sawa na kiasi cha umeme kilichotumiwa na Uingereza yote mwaka jana.

India na Bangladesh tayari zimeibua wasiwasi juu ya uwezekano wa athari za bwawa hilo kwa mamilioni ya watu chini ya mto, huku mashirika yasiyo ya kiserikali yakionya juu ya hatari kwa mazingira.

21/07/2025

Kampuni ya Azam Marine imeibuka mshindi wa Tuzo ya Usafirishaji Bora kwa vyombo vya baharini katika Tuzo za Usafiri na Ukarimu Afrika Mashariki za mwaka 2025, zinazotolewa na Taasisi ya Corporate Solution World Wide (CSW).

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni za Bakhresa, Rehema Salim amesema kampuni itaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi kwa gharama nafuu ikiwa ni sehemu ya dhamira yao ya kuboresha sekta ya usafiri wa baharini.

21/07/2025

Jeshi la Polisi Mkoani Tabora limethibitisha kutokea kwa kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka mitatu Ramin Sahbdad mkazi wa kata ya Mpela Manispaa ya Tabora ambapo mwili wake umekutwa ukielea juu ya maji ya kisima kilichopo maeneo ya nyumbani kwao jana Julai 20, 2025.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Polisi Mkoani humo Richard Abwao wakati akizungumza na waandishi wa habari.

21/07/2025

"Kwa umri wake bado ana uwezo wa kucheza misimu mitatu, minne" Sehemu ya maneno ya Mchambuzi wa michezo ndani ya ikiwa ni baada ya Simba kumuaga rasmi nahodha huyo ambaye ameitumikia klabu hiyo kwa zaidi ya miaka 10.

Imeandaliwa na

21/07/2025

"Yanga wana dira inayoeleweka, na ndio sababu unaona usajili wao" Mchambuzi wa michezo akizungumza ndani ya hasa kipindi hiki ambazo klabu mbalimbali nchini zinafanya usajili kuelekea msimu ujao wa ligi kuu.



21/07/2025

“Ukiwauliza mashabiki wengi kuhusu simba mpya, asilimia kubwa watasema hawaioni” Mchambuzi wa michezo akichambua kupitia hasa kupitia mabadiliko ambayo yanafanywa na klabu ya Simba SC kwa ajili ya msimu ujao.



Polisi nchini Kenya imesema imemk**ata mwanaharakati mashuhuri anaetetea haki za binaadamu nchini humo Boniface Mwangi n...
21/07/2025

Polisi nchini Kenya imesema imemk**ata mwanaharakati mashuhuri anaetetea haki za binaadamu nchini humo Boniface Mwangi na imepanga kumfikisha mahak**ani hii leo kwa madai ya kuchochea vitendo vya kigaidi.

Idara ya upelelezi nchini Kenya, DCI imesema katika mtandao wake wa X kwamba maafisa wake wamemk**ata Mwangi nyumbani kwake katika kaunti ya Machakos na kupata mabomu mawili ya kutoa machozi, mkanda wa risasi, simu mbili za mkononi, kompyuta na vitabu kadhaa vya kutunza kumbukumbu.

Kando na madai ya ugaidi, Mwangi pia anapaswa kusimamishwa kizimbani kujibu makosa ya kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Mataifa hayo matatu yanayojulikana k**a E3, yanatarajia kufanya mazungumzo na Iran baada ya kutoa onyo kwa Jamhuri hiyo ...
21/07/2025

Mataifa hayo matatu yanayojulikana k**a E3, yanatarajia kufanya mazungumzo na Iran baada ya kutoa onyo kwa Jamhuri hiyo ya kiislamu kwamba huenda, vikwazo vya kiuchumi dhidi yake vikarejeshwa iwapo haitaingia katika majadiliano hayo.

Shirika moja la habari nchini Iran limesema taifa hilo limekubali kuingia katika majadiliano na mataifa hayo matatu ya Magharibi na kwamba bado tarehe rasmi na mahala pa kukutana havijaamuliwa.

Hapo kabla, Iran na Marekani zilifanya duru kadhaa za mazungumzo juu ya mpango huo wa nyuklia wa Iran kupitia wapatanishi wa Oman kabla Israel kuanzisha mashambulio yake ya siku 12 nchini Iran yaliyoanza Juni 13.



Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada Randeep Sarai amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku Tatu na anatarajiw...
21/07/2025

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada Randeep Sarai amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku Tatu na anatarajiwa kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Canada katika miji ya Dar es Salaam, Dodoma, na Zanzibar.

Katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Sarai alipokewa na Waziri wa Afya Jenista Mhagama, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Said Shaib M***a na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wala Afrika Mashariki Balozi Swahiba Mndeme na Balozi wa Canada nchini Emily Burns.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share