07/06/2026
Zaidi ya waathirika 500 wamethibitishwa kuugua maradhi ya Ebola katika mlipuko unaoendelea kuenea katika Afrika ya Kati, kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa Juni 6, huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu ukubwa unaoongezeka wa janga hilo.
Katika taarifa ya kila siku kuhusu hali ya mlipuko huo, WHO imeripoti watu 452 kuugua maradhi hayo na vifo 82, katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ambako mlipuko huo ulitangazwa wiki tatu zilizopita.
Nchini Uganda, shirika hilo limeripoti watu 19 kuugua maradhi hayo, vikiwemo vifo viwili.
Maafisa wa Afya wameonya kuwa bila hatua madhubuti za afya ya umma, mlipuko wa sasa unaweza kufikia kiwango cha janga la Ebola la Afrika Magharibi la mwaka 2014, ambalo liliua Zaidi ya watu 11,000.
✍️ Alinda Kato