UFM Radio TZ

UFM Radio TZ UFM is the leading radio station in Tanzania which is Part of Azam Media Ltd, a company owned by the

Rais wa Kenya William Ruto ameunda jopo la pamoja linaloshirikisha idara na mashirika mbalimbali ili kupiga jeki vita dh...
20/08/2025

Rais wa Kenya William Ruto ameunda jopo la pamoja linaloshirikisha idara na mashirika mbalimbali ili kupiga jeki vita dhidi ya ufisadi nchini humo.

Jopo kazi hilo linahusisha asasi na tume kumi zitakazofanya kazi pamoja kukomesha ufisadi nchini Kenya ili kuunda mustakabali mpya wa kukomesha vitendo vya rushwa.

Rais ruto ambaye amesafiri kuelekea Japan, amesema kuwa vita dhidi ya wizi na ufujaji wa mali ya umma sasa vitakuwa na adhabu kali na ya kesi za ufisadi kutatuliwa kwa haraka zaidi.


Ajali ya basi magharibi mwa Afghanistan imeua watu 73, wakiwemo watoto 17, wengi wao wakiwa kwenye basi lililokuwa limew...
20/08/2025

Ajali ya basi magharibi mwa Afghanistan imeua watu 73, wakiwemo watoto 17, wengi wao wakiwa kwenye basi lililokuwa limewabeba wahamiaji wa Afghanistan waliofukuzwa kutoka Iran.

Mkurugenzi wa habari na utamaduni wa Taliban huko Herat Ahmadullah Mottaqi amesema basi hilo lililokuwa likielekea Kabul lilishika moto jana usiku baada ya kugongana na lori na pikipiki katika mkoa wa Herat.

Katika miezi ya hivi karibuni Iran imeongeza kasi ya kuwafukuza wahamiaji wa Afghanistan wasio na vibali ambao wamekimbia migogoro katika nchi yao.

Meli iliyobeba shehena ya chakula imetia nanga kwenye bandari ya Israel ya Ashdod ikiwa ni sehemu ya juhudi za hivi kari...
20/08/2025

Meli iliyobeba shehena ya chakula imetia nanga kwenye bandari ya Israel ya Ashdod ikiwa ni sehemu ya juhudi za hivi karibuni kabisa za kushughulikia hali mbaya ya kiutu kwenye Ukanda wa Gaza.

Meli hiyo inayopeperusha bendera ya Panama iliondoka Cyprus Jumatatu ikiwa na tani 1,200 za tambi, mchele, lishe ya watoto na vyakula vingine vya kusindikwa.

Shehena hiyo ya misaada itaaanza kusambazwa leo kwenye Ukanda wa Gaza eneo ambako mashirika ya Umoja wa Mataifa yanasema ukosefu wa chakula umefikia kiwango kisicho mithili.

Msaada huo umewasili siku moja baada ya kundi la Hamas kuridhia pendekezo jipya la kusitisha vita lililotolewa na wapatanishi wa nchi za kiarabu.

19/08/2025

Mwili mmoja wa fundi mchimbaji aliyekuwa amenasa kwenye kifusi kufuatia kuporomoka kwa mgodi umepatikana huku wachimbaji wengine 17 wakiendelea kutafutwa.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita amesema kuwa juhudi za uokoaji zinaendelea ili kuhakiksha kila aliye chini ya ardhi anatolewa.

Imeandaliwa na Kasisi Kosta

Mhariri | ✍

Wakati umefika kwa Tanzania kuandika historia kubwa.....Wakati umefika kwa nyota wanaokipiga ndani ya Tanzania kuonesha ...
19/08/2025

Wakati umefika kwa Tanzania kuandika historia kubwa.....

Wakati umefika kwa nyota wanaokipiga ndani ya Tanzania kuonesha ukubwa wao mbele ya timu kubwa Afrika.....

Wakati umefika kwa Mzize, Nado, Fei toto, Zimbwe, Muda, Kagoma, Kapombe, Bacca, Job na wengineo kuitikisa Afrika....

Wakati umefika kwa Tanzania kuisaka nusu fainali ya CHAN kwa mara ya kwanza kupitia mgongo wa timu kubwa Afrika, Morocco.

Ngoma inapigwa Benjamin Mkapa Stadium, Ijumaa hii Agosti 22 kuanzia saa 2:00 usiku na kuruka mbashara kwa viwango vya HD kupitia Azam Sports 1 HD.

Lipia sasa Kisimbuzi chako uwe sehemu ya rekodi hii itakayoishi miaka, kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama mchezo huu.

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron amependekeza kuwa mazungumzo kati ya Rais wa Urusi Vladmir Putin na Rais wa Ukraine, V...
19/08/2025

Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron amependekeza kuwa mazungumzo kati ya Rais wa Urusi Vladmir Putin na Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky yafanyike mjini Geneva, Uswisi.

Akizungumza leo na kituo cha habari cha Ufaransa, LCI, Macron ametangaza kuwa mkutano wa kilele kati ya viongozi wa Urusi na Ukraine utafanyika Ulaya.

Macron ameyasema hayo baada ya Rais wa Marekani Donald Trump, kufanya mazungumzo na viongozi wa Ulaya, Jumuiya ya Kujihami ya NATO na Zelensky mjini Washington jana.

19/08/2025

Serikali imetoa shilingi bilioni 600 kwaajili ya miradi ya reli ya kiwango cha kisasa ya SGR na reli ya MGR.

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Shiwa, ametoa kauli hiyo wakati wa ziara ya bodi ya Wakurugenzi wa TRC, kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa SGR sambamba na MGR kati ya Kigoma-Tabora na Tabora- Mwanza.

Mhandisi Shiwa, amesema reli ya MGR ina mtandao wa jumla ya km 2,700 ambao ukifanyiwa ukarabati mkubwa unaoendelea sasa utaleta matokeo chanya kwenye sekta ya usafirishaji kwa njia ya reli nchini.


19/08/2025


Wengi wanapopanda ghorofani kwenye majengo mbalimbali hupenda kutumia kile wanachokiita 'lift' lakini bila kujua kuwa si kiswahili fasaha.

Chukua hii kwamba neno 'lift' kwa lugha ya kiswahili ni 'Kambarau'

Msikilize mswahili hapa.

Usiache kusikiliza kuanzia saa 6 mchana kila Ijumaa.


Baraza la Amani na Usalama la Jumuiya ya Afrika limetaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuanza taratibu wa kuondo...
19/08/2025

Baraza la Amani na Usalama la Jumuiya ya Afrika limetaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuanza taratibu wa kuondoa marufuku ya silaha kwa Sudan Kusini ili kusaidia nchi hiyo kushughulikia changamoto zake za usalama.

Kituo cha Eye Radio kimesema baraza hilo limeeleza hatua hiyo itawezesha Sudan Kusini kudumisha umoja na nguvukazi muhimu.

Baraza hilo pia limeelezea wasiwasi juu ya kuzorota kwa hali ya kibinadamu nchini humo, vurugu kati ya jamii, ukosefu mkubwa wa usalama wa chakula, uhamishaji wa ndani na ufikiaji mdogo wa misaada ya kibinadamu katika maeneo yaliyoathirika na vita.

Ile michuano ya kujiandaa na msimu mpya wa soka kwa timu za Afrika mashariki   inaanza leo jijini Kigali, nchini Rwanda....
19/08/2025

Ile michuano ya kujiandaa na msimu mpya wa soka kwa timu za Afrika mashariki inaanza leo jijini Kigali, nchini Rwanda.

Matajiri wa Chamazi, Azam FC chini ya Kocha Florent Ibenge watakuwa wanatest silaha zao kwa mara ya kwanza kwa kucheza na Police FC.

Mechi hii itapigwa saa 11:00 jioni, na kuruka mbashara kupitia AzamSports4HD.

Saa 2:00 usiku, wenyeji APR watakuwa wanacheza na AS Kigali.

Mechi hii itaruka mbashara AzamSports3HD

Kwa kifurushi cha shilingi 28,000 unatazama michezo hii.

19/08/2025

“Uwe umefia nyumbani au hospitali, unapaswa kupata kifo cha Kifo” Sehemu ya maneno ya Hakimu Mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Temeke Mhangwa Dotto akizungumza kwenye kipindi cha

Cc


19/08/2025

“Uhitaji wa kutangaza kwenye gazeti la serikali ndio ulioondoa…ni lazima mirathi itangazwe” Sehemu ya maneno ya Hakimu Mkazi mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Temeke Mhangwa Dotto

Cc


Address

1 Mandela Road
Dar Es Salaam
12301

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UFM Radio TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to UFM Radio TZ:

Share

Category