Bongotzfm

Bongotzfm Bongofmtz

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeandaa kambi maalum ya matibabu ya kisasa ya upasuaji wa kuondoa mawe kwenye f...
16/01/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeandaa kambi maalum ya matibabu ya kisasa ya upasuaji wa kuondoa mawe kwenye figo kwa wagonjwa wenye changamoto hiyo kwa kutumia njia ya kisasa ya mionzi ya laser, ambapo kambi hiyo itafanyika kuanza tarehe 21-23 januari, 2026.

Daktari Bingwa wa Upasuaji Mfumo wa Mkojo Dkt. Hamis Isaka ameeleza kuwa kutokana na huitaji wa huduma hiyo kwa watu wengi, hospitali imeamua kufanya matibabu hayo ili kuhakikisha wananchi wananufaika na uwekezaji mkubwa uliyofanywa na Serikali katika sekta ya afya .

Amefafanua kuwa huduma ya kuvunja mawe kwenye figo kwa kutumia mionzi ya Lesar ni matibabu ambayo humsaidia mgonjwa kupata maumivu kidogo ,kutokuwa na kovu wala kukatwa ambapo mgonjwa atakaa wodini kwa muda mchache takribani siku moja hadi mbili.

Kwa mujibu wa Dkt. Isaka, huduma hiyo inahusisha wagonjwa wenye mawe kwenye figo madogo hadi ya kati, wagonjwa ambao dawa hazikusaidia, wanaoogopa upasuaji mkubwa, wagonjwa wenye uzito mkubwa au matatizo ya damu na wanaopata mawe ya figo mara kwa mara.

Aidha , Dkt. Isaka ameeleza namna ya kuzuia mtu kupata mawe kwenye figo ni pamoja na kunywa maji mengi angalau lita 3 kwa siku, kupunguza matumizi ya chumvi nyingi, kupunguza nyama nyekundu kupita kiasi, kula matunda na mbogamboga, kufanya mazoezi na kufanya uchunguzi wa mara kwa mara.

Miongoni mwa mechi ngumu zenye uzito wa ushindani ni Wagosi wa Kaya Coastal Union wanapokutana na waoka Mikate Azam Fc. ...
16/01/2026

Miongoni mwa mechi ngumu zenye uzito wa ushindani ni Wagosi wa Kaya Coastal Union wanapokutana na waoka Mikate Azam Fc.

Mechi hii haijawahi kuwa nyepesi ni ukuta wa Lameck Lawi juu kuna Abdul Suleiman Sopu wanaingia kuwakabili waajili wao wa zamani pale Azam Complex.

Je? ni Coastal Union ya Muhamed Muya ama Azam Fc ya Florent Ibenge itakayo ondoka na alama tatu ?

Sikiliza mchezo huu kupitia BONGO FM 🎤kipaza kitakuwa chini ya Issa Suleiman mchambuzi wa matukio ni Thomas Ng’itu.

✍️

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 16, 2026 ameongoza kikao cha kimkakati na Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makati...
16/01/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 16, 2026 ameongoza kikao cha kimkakati na Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu wa kisekta, Ofisini kwake, Mlimwa Jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, viongozi hao wamejadili kuhusu changamoto za biashara kati ya Tanzania na Zambia

Wizara zilizohudhuria kikao hicho ni pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera Bunge na Uratibu), Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Wizara ya Fedha, Wizara ya Nishati, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Pia, kikao hicho kilihudhuriwa na Wakuu wa Mikoa ya Katavi, Songwe na Rukwa.

16/01/2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda, ametoa siku 10 kwa Mkandarasi anayejenga shule ya sekondari Nela wilayani Kwimba, kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya Madarasa 8 pamoja na matundu ya choo 16 ili wanafunzi waanze kusoma.

Ametoa agizo hilo wakati akiwa katika ziara ya kukagua miundombinu inayojengwa kwa gharama ya zaidi ya Milioni 267 na mkandarasi Mairo Group of Companies ambapo amebaini ucheleweshaji wa mradi huo wa shule.

Mtanda amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kufanya tathmini ya kazi zilizofanyika mpaka sasa na kuhakikisha anampatia mzabuni mwenye uwezo wa kukamilisha ujenzi uliobaki kupitia fedha ambazo bado mkandarasi huyo hajalipwa.

Halikadhalika, ameiagiza Ofisi ya Takukuru wilayani humo, kufuatilia mwenendo wa zabuni ya ujenzi huo na idara ya manunuzi kwa ujumla na kumpatia taarifa.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda anatarajiwa kuwasilisha ujumbe maalumu kutoka kwa Rais ...
16/01/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda anatarajiwa kuwasilisha ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe wa kuthibitisha dhamira ya Tanzania kuwa moja ya nchi mwenyeji wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika
(AFCON) 2027.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Januari 16, 2026 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam, saa chache kabla ya kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya ujumbe huo, Mhe. Makonda amesema kuwa, hatua hiyo ni matokeo ya juhudi kubwa za Serikali katika kuimarisha sekta ya michezo hususan miundombinu ya viwanja, usafiri, malazi na maandalizi ya kiufundi yanayokidhi viwango vya kimataifa.

Ameongeza kuwa, Tanzania kuwa mwenyeji wa AFCON 2027 itakuwa ni fursa adhimu ya kutangaza sekta ya utalii, kuimarisha diplomasia ya michezo, pamoja na kukuza uchumi kupitia ajira na biashara zitakazotokana na mashindano hayo.

Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanza maandalizi ya kulifanya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuwa mwekezaji mk...
16/01/2026

Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanza maandalizi ya kulifanya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuwa mwekezaji mkubwa katika uchimbaji wa madini nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuongeza tija na mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa Taifa.

Hayo yamesemwa leo Januari 16 na Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde, wakati wa kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.

Waziri Mavunde amesema STAMICO tayari imenunua mitambo mikubwa ya kisasa itakayoliwezesha kufanya uchimbaji wa kiwango kikubwa, hatua itakayolifanya Shirika hilo kushiriki moja kwa moja katika miradi mikubwa ya madini kwa viwango vinavyolingana na migodi mikubwa iliyopo nchini.

Ameeleza kuwa Serikali inalenga kuijenga STAMICO kuwa mdau muhimu katika mnyororo mzima wa sekta ya madini ili kuongeza manufaa kwa Taifa na kuhakikisha Watanzania wananufaika zaidi na rasilimali za madini.

Akizungumza kuhusu mchango wa sekta ya madini, Waziri Mavunde amesema mafanikio yaliyopatikana yanatokana na uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse, amesema Shirika hilo linaendelea kuimarika kutokana na uwekezaji wa Serikali, kuimarishwa kwa uongozi na usimamizi wa karibu.

Naye Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo, amesema Tume ilivuka lengo la makusanyo kwa asilimia 108 mwaka 2024/25, na kwa mwaka wa fedha 2025/26 tayari imekusanya asilimia 56 ya lengo la Shilingi trilioni 1.2 hadi Desemba 2025.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, ameipongeza Wizara ya Madini kwa usimamizi mzuri wa sekta hiyo na kuahidi ushirikiano endelevu wa Kamati katika kufanikisha mipango ya maendeleo ya sekta ya madini kwa manufaa ya Taifa.

16/01/2026

Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameitaka mammlaka ya viwanja vya ndege kusimamia kwa umakini matumizi ya jengo hili kuhakikisha linatunzwa ipasavyo na kudumisha viwango na ubora wake.

Amesema Serikali inaendelea kuimarisha sekta ya uchukuzi kwa kutambua kuwa ufanisi na ubora wa huduma katika sekta hiyo huliweka Taifa katika nafasi nzuri ya ushindani wa kibiashara Kimataifa na pia huongeza mapato ya fedha za kigeni na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika Pato la Taifa.

Vilevile, amesema Serikali itaendelea kuboresha miundombinu na huduma mbalimbali katika viwanja vya ndege, pamoja na kuimarisha usafiri wa barabara, reli na majini, ili kuhakikisha sekta ya uchukuzi inaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.

Ameyasema hayo wakati wa uzinduzi rasmi wa jengo la viongozi mashuhuri la uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam leo Januari 16, 2026.



Add a comment…

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imejizatiti kuhakiki...
16/01/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali imejizatiti kuhakikisha Sekta ya Uchukuzi inaimarika ili kuliweka Taifa kwenye nafasi nzuri ya ushindani wa kibiashara, kuongeza mapato ya fedha za kigeni na kukuza mchango wa sekta hiyo katika pato la Taifa.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa uzinduzi wa Jengo la Viongozi Mashuhuri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Amesema pamoja na ujenzi wa jengo hilo, Serikali ya Awamu ya Sita imejipanga kikamilifu kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kisekta k**a ilivyoainishwa katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050, Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo ya Taifa na Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (2025).

Makamu wa Rais amesisitiza kwamba, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu na huduma mbalimbali katika Viwanja vya Ndege, huduma za usafiri wa barabara, usafiri majini na usafiri kwa njia ya reli.

Halikadhalika amesema, Serikali itaendelea na uboreshaji wa huduma za Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) kwa lengo kuboresha usafiri wa ndani, kuunganisha Tanzania na nchi nyingine, kupunguza gharama za usafirishaji na kuimarisha uchumi wa Tanzania na biashara za kimataifa.

Vilevile, Makamu wa Rais amesema ili kuboresha huduma za usafiri na usafirishaji, Serikali imedhamiria kuunganisha huduma za Sekta ya Uchukuzi, k**a vile uunganishaji wa huduma za Viwanja vya Ndege, usafiri wa barabara, maji na reli. Mathalan, mradi wa kimkakati unaoendelea wa ujenzi wa barabara za Mwendokasi (BRT) kati ya eneo la Posta na Gongo la Mboto utaunganishwa na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere ili kurahisisha huduma za usafiri katika jiji la Dar es Salaam.

Hali kadhalika, hatua za utekelezaji zinaendelea ili kuhakikisha huduma za reli zinaunganishwa na viwanja vya Ndege vya kimataifa, hususan Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato na Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro.

JESHI la Polisi mkoani Mbeya linamshikilia mkazi wa kijiji cha Madundasi kilichopo wilayani Mbarali, Doto Lubongeja kwa ...
16/01/2026

JESHI la Polisi mkoani Mbeya linamshikilia mkazi wa kijiji cha Madundasi kilichopo wilayani Mbarali, Doto Lubongeja kwa tuhuma za mauaji ya watoto watatu wa familia moja kwa kuwanyonga na kamba shingoni.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya,Wilbert Siwa, amewataja watoto waliouawa ni Petro Amosi(8), Samu Amosi(6) na Nkamba Amosi(4) wote wakazi wa Kijiji cha Madundasi.

Amesema tukio hilo lilitokea jana Januari 15, 2026 kijijini hapo, ambapo mtuhumiwa aliua watoto hao baada ya kuwakuta peke yao wakichunga ng’ombe jirani na nyumbani kwao.

Amesema baada ya kutekeleza mauaji hayo aliiba ng’ombe 15 kisha kuziswaga na kuzificha nyumbani kwa mjomba wake aitwaye Masoda Kulwa, anayeishi Kijiji cha Madundasi B na kuanza kutafuta mteja, ambapo aliuza ng’ombe hao na kupata fedha Sh milioni 5.1

Alisema kufuatia tukio hilo, pilisi walianza msako mkali na kufanikiwa kumk**ata Doto Lubongeja pamoja na Masoda Kulwa, ambaye walishirikiana kuuza ng’ombe hao.

Klabu ya Simba imemtambulisha Kocha mpya Msaidizi Kristopher Bergman Katika benchi lao la ufundi kwa ajili na kusaidiana...
16/01/2026

Klabu ya Simba imemtambulisha Kocha mpya Msaidizi Kristopher Bergman Katika benchi lao la ufundi kwa ajili na kusaidiana Kocha Mkuu Steve Barker kukinoa kikosi cha Simba.

Bergman raia wa Afrika Kusini ambaye amecheza soka nchini humo, anakuja Tanzania kwa ajili ya kuendeleza gurudumu la kuinoa Simba akiwa na Kocha Steve Barker.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu, akisalimiana na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani n...
16/01/2026

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu, akisalimiana na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani na Mbunge wa Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa 28 wa Maspika na Wenyeviti wa Bunge wa Jumuiya ya Madola leo tarehe 15 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Samvidhan Sadan, Bungeni Jijini New Delhi nchini India.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongotzfm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bongotzfm:

Share

Category