Bongotzfm

Bongotzfm Bongofmtz

04/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema dunia ipo katika kipindi cha mabadiliko makubwa ya kiteknolojia yanayofungua fursa mpya kwa vijana, akiwataka kuwa tayari kujifunza na kuendana na kasi ya maendeleo hayo ili wasibaki nyuma.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo jijini Moscow, Urusi, mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Uzamivu na Peoples’ Friendship University of Russia (RUDN), ambapo alisisitiza kuwa maendeleo ya teknolojia k**a Akili Mnemba (AI), sayansi za mashine na maroboti yanaibadilisha dunia kwa kasi kubwa.

Amesema hakuna taifa linalotaka kubaki nyuma katika mapinduzi hayo ya kiteknolojia, huku akibainisha kuwa mafanikio yatapatikana kwa wale watakaokuwa tayari kujifunza, kuendana na mabadiliko na kutumia fursa zinazojitokeza.

Katika hotuba yake iliyopokelewa kwa makofi kutoka kwa washiriki wa hafla hiyo, Rais Samia alieleza kuwa elimu imeendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo duniani, ikichochea mabadiliko katika familia, jamii na taifa kwa ujumla.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Sayansi na Elimu ya Juu wa Urusi, Konstantin Mogilevsky, ambaye alimpongeza Rais Samia kwa mchango wake katika kuimarisha sekta ya elimu nchini Tanzania.

Chuo Kikuu cha RUDN kina historia ya muda mrefu ya ushirikiano na Tanzania, ambapo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1960 kimesomesha zaidi ya Watanzania 1,100, huku wanafunzi wengine 72 kutoka Tanzania wakiendelea na masomo yao katika ngazi mbalimbali chuoni hapo.
Kwa kutunukiwa heshima hiyo, Rais Samia anaungana na viongozi wengine wa Afrika waliowahi kutambuliwa na chuo hicho, akiwemo Sam Nujoma, Thabo Mbeki na Olusegun Obasanjo.

04/06/2026

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesifu mchango wa Chuo Kikuu cha Urafiki cha Watu wa Urusi (RUDN) katika ukombozi wa nchi za Afrika akisema kimesadifu maono ya viongozi wa zama za ukombozi wa Bara la Afrika.

Rais Samia ameyasema hayo jijini Moscow, Urusi wakati wa tukio la kutunukiwa kwake Shahada ya Heshima ya Uzamivu (Honoris Causa) na chuo hicho kutokana na uongozi uliotukuka na mchango wake katika maendeleo ya taifa.

“Jina la Patrice Lumumba ambalo chuo hiki kilipewa kilisadifu jukumu kubwa ambalo mwanamapinduzi huyo wa Afrika na viongozi wenzake wa Afrika waliona k**a wajibu mkubwa wa uongozi.

“Kwamba elimu inatakiwa isiwe tu kuingia darasani bali ni mlango wa ukombozi, utu, maendeleo na uhusiano wa kuheshimiana. Historia ya chuo hicho imesadifu maono yao na kwa hakika heshima waliyonipa ni kubwa” alisema.

RUDN imekuwa na mahusiano ya muda mrefu na Tanzania, kikiwa kimesomesha zaidi ya Watanzania 1,100 tangu kianzishwe mwaka 1960 iliyopita na sasa wanafunzi wa Kitanzania 72 wanapata mafunzo katika ngazi mbalimbali chuoni hapo.

Rais Samia anakuwa Rais wa karibuni zaidi kupewa heshima hiyo na chuo hicho, huku marais wengine sita wakiwa wamewahi kupewa tuzo hiyo. Baadhi ya marais hao ni Sam Nujoma wa Namibia, Thabo Mbeki wa Afrika Kusini na Olesegun Obasanjo wa Nigeria.

Vyuo vikuu vingine saba ambavyo vimewahi kumtunukia Rais Samia shahada za namna hiyo ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Jawahral Nehru nchini India, Chuo Kikuu cha Ankara nchini Uturuki, Nasarawa nchini Nigeria, Chuo Kikuu cha Anga cha Korea Kusini, Chuo Kikuu cha Mzumbe na Chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA).

Rais Samia yuko nchini Urusi katika ziara ya kitaifa iliyoanza jana na itahitimishwa kesho baada ya kuhudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Uchumi wa St. Peterburg.

04/06/2026

USIYOYAJUA KUHUSU KABILA LA KIMAASAI

04/06/2026

Unazijua salamu za Kimaasai ?

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo nchini (STPU) limewapongeza na kutoa...
04/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo nchini (STPU) limewapongeza na kutoa zawadi kwa Wakaguzi na Askari 14 waliofanya vizuri zaidi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa mwaka 2025.

Akizungumza katika tukio hilo leo Juni 04, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Justine Masejo amewapongeza Wakaguzi na Askari hao kwa kuonesha nidhamu na kufanya kazi kwa weledi kwa kipindi husika.

Pamoja na pongezi hizo, pia amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa uongozi wao na juhudi wanazoendelea kuzifanya katika kuboresha ustawi wa Askari pamoja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi ndani ya Jeshi la Polisi.

Amesema utaratibu wa kutambua na kuwapongeza Askari nidhamu na uadilifu huku akisisitiza kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ambayo inaweza kuathiri maadili ya kazi na taswira ya Jeshi la Polisi mbele ya jamii.

Kwa upande wake, Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Simon Pasua amesema Askari wengi ndani ya Jeshi hilo wanaendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii na weledi mkubwa, lakini waliopatiwa zawadi ni wale waliojitokeza zaidi kwa utendaji bora katika kipindi husika.
.....................

04/06/2026

Sikiliza Kipindi cha kila siku Jumatatu-Ijumaa Kuanzia saa 5:00-8:00 mchana hapa Bongo fm.
Tufuatilie pia Kupitia YOUTUBE chaneli yetu Bongo FM kwa vipindi mbalimbali.



💻

04/06/2026

Ebu tuambie ni kweli wasanii waliotoka WCB wamekuwa wanafiki baada ya kutoka katika lebo hiyo?

Sikiliza Kipindi cha kila siku Jumatatu-Ijumaa Kuanzia saa 5:00-8:00 mchana hapa Bongo fm.
Tufuatilie pia Kupitia YOUTUBE chaneli yetu Bongo FM kwa vipindi mbalimbali.



💻

04/06/2026

MAISHA YA BUNGENI: Leo tunataka kujua, ugumu wa kazi ya ubunge.

Kutana na mic 🎤 ya Bongo FM Bungeni ikiwa kwenye mikono ya kuyasaka majibu kutoka kwa Wabunge wenyewe.

Wewe unaaminije?

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongotzfm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bongotzfm:

Share

Category