Bongotzfm

Bongotzfm Bongofmtz

21/07/2025

FLYOVER IKO KWA HEWA MUDA HUU!!!!!!!! NA WAPO MJENGONI MUDA HUU KUHAKIKISHA JIONI YAKO INAKAA POA, IKUMBATIE BONGO FM.

21/07/2025

SHINDA KADRI UWEZAVYO MSHUA ANATOA MILIONI 10 KILA SIKU

Sikiliza Kipindi cha kila siku Jumatatu-Ijumaa Kuanzia saa 5:00-8:00 mchana hapa Bongo fm.
Tufuatilie pia Kupitia YOUTUBE chaneli yetu Bongo FM kwa vipindi mbalimbali.




🎥📝 .dvj.sady

Ndege ya Air India aina ya Airbus A320 iliyokuwa ikitokea Kochi kuelekea Mumbai imeteleza kidogo nje ya njia ya kurukia ...
21/07/2025

Ndege ya Air India aina ya Airbus A320 iliyokuwa ikitokea Kochi kuelekea Mumbai imeteleza kidogo nje ya njia ya kurukia ndege (runway) ilipokuwa ikitua leo Julai 21 asubuhi, wakati mvua kubwa ikinyesha katika uwanja wa ndege wa Mumbai.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Uwanja wa Ndege wa Mumbai imeeleza kuwa, ndege hiyo iliweza kurudi kwenye njia kuu haraka bila abiria na wahudumu wa ndege kudhurika.

Msemaji wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chhatrapati Shivaji Maharaj (CSMIA), Mumbai, amesema kuwa sehemu ya barabara ya kurukia ndege ambapo tukio hilo lilitokea imeharibika na sasa njia nyingine ya kurukia ndege ndiyo inatumika kwa safari nyinginezo.



21/07/2025

NA WAMEPATA WALICHOKITAKA

Sikiliza Kipindi cha kila siku Jumatatu-Ijumaa Kuanzia saa 5:00-8:00 mchana hapa Bongo fm.
Tufuatilie pia Kupitia YOUTUBE chaneli yetu Bongo FM kwa vipindi mbalimbali.




🎥📝 .dvj.sady

21/07/2025

BILLNASS AMEJITAKIA MWENYEWE K**A SIO MIPANGO

Sikiliza Kipindi cha kila siku Jumatatu-Ijumaa Kuanzia saa 5:00-8:00 mchana hapa Bongo fm.
Tufuatilie pia Kupitia YOUTUBE chaneli yetu Bongo FM kwa vipindi mbalimbali.




🎥📝 .dvj.sady

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa tamko rasmi kwa umma kikilaani vikali kuenea kwa taarifa za uongo na upotoshaji unaofa...
21/07/2025

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa tamko rasmi kwa umma kikilaani vikali kuenea kwa taarifa za uongo na upotoshaji unaofanywa na watu wenye nia ovu, hasa katika mitandao ya kijamii, kwa lengo la kuzua taharuki na kuchafua jina la chama hicho.

Kupitia taarifa iliyosainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Gabriel Makalla leo Julai 21, chama hicho kimeanzisha utaratibu mpya wa matumizi ya nembo maalum ya QR Code ili kurahisisha uthibitishaji wa taarifa zinazotolewa na CCM.

Kwa mujibu wa Makalla, msomaji wa taarifa yoyote inayodaiwa kutoka CCM ataweza kuithibitisha kwa ku-scan QR Code hiyo, ambayo itampeleka moja kwa moja kwenye chanzo rasmi cha taarifa husika kutoka tovuti au kurasa za mitandao ya kijamii za chama.

Makalla amesema kuwa lengo la mfumo huu wa uthibitishaji ni kusaidia wananchi wote kuweza kujiridhisha k**a taarifa fulani imetolewa rasmi na CCM au la, kwa kutumia teknolojia rahisi ya QR Code.



"Tumeamka Ili tuchanganyikiwe maana unasikia Simba haina hela ya kusajili ndio maana inakosa Wachezaji halafu baada ya m...
21/07/2025

"Tumeamka Ili tuchanganyikiwe maana unasikia Simba haina hela ya kusajili ndio maana inakosa Wachezaji halafu baada ya muda unasikia tena Simba imekamilisha mazungumzo ya kumsajili Mchezaji fulani sasa sijui huyo mchezaji tunamlipa Figo"

"Poleni ndugu zangu Wana Simba kwa kuchanganywa, taarifa sahihi za na uhakika utazipata kupitia Majukwaa rasmi ya klabu yetu zinaanzia kwenye Simba App na kusambaa kwenye majukwaa yetu mengine" Ameandika Msemaji wa Simba sc Ahmed Ally.

Una Maoni gani?

21/07/2025

Mazungumzo na Mchumi, Ally Mkimo kuhusu Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 - 2050........
Usikose kusikiliza kipindi cha 'Power Bank' kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, saa 3: 00 Asubuhi - 5: 00 Asubuhi. Anakuwepo & .

Producer:

Rais wa Marekani Donald Trump ameadhimisha miezi sita tangu aanze muhula wake wa pili madarakani, akisema kuwa kipindi h...
21/07/2025

Rais wa Marekani Donald Trump ameadhimisha miezi sita tangu aanze muhula wake wa pili madarakani, akisema kuwa kipindi hicho kifupi kimekuwa miongoni mwa vipindi muhimu zaidi kwa urais katika historia ya taifa hilo huku likiwa taifa linaloheshimika zaidi duniani.

Kupitia ujumbe aliouandika jana Julai 20, kwenye mtandao wa kijamii, Trump amesema kuwa utawala wake umefanikiwa kufanya mambo makubwa, ikiwemo kumaliza vita vingi ambavyo havikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Marekani, isipokuwa kupitia biashara au urafiki wa kimataifa.

"Leo ni kumbukizi ya miezi sita tangu nianze muhula wangu wa pili k**a Rais. Kipindi hiki kinatajwa kuwa miongoni mwa vipindi muhimu zaidi kwa rais yeyote kuwahi kuwa madarakani. Kwa kifupi, tumefanikisha mambo mengi mazuri na makubwa — ikiwemo kumaliza vita vingi ambavyo havikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Marekani, isipokuwa kupitia biashara au, kwa baadhi ya matukio, urafiki.

"Miezi sita si muda mrefu, lakini tumefanikiwa kuifufua nchi kubwa k**a Marekani. “Mwaka mmoja uliopita, nchi yetu ilikuwa k**a imekufa — bila matumaini yoyote ya kupona. Leo, Marekani ni nchi ‘ya moto’ zaidi na yenye heshima kubwa duniani.” Heri ya kumbukumbu ya miezi sita!" ameandika Trump.



21/07/2025

Je, unaijua tofauti kati ya Bajeti Kuu ya Serikali na Dira ya Taifa ya Maendeleo? Huyu hapa Mchumi, Ally Mkimo anaeleza.
.......
Usikose kusikiliza kipindi cha 'Power Bank' kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, saa 3: 00 Asubuhi - 5: 00 Asubuhi. Anakuwepo & .

Producer:

KENYA IMEKULA NYOYA MASHINDANO YA CECAFATimu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars) imejiondoa kwenye mashindano mafupi yana...
21/07/2025

KENYA IMEKULA NYOYA MASHINDANO YA CECAFA

Timu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars) imejiondoa kwenye mashindano mafupi yanayojumuisha timu nne, yaani Tanzania, Kenya, Uganda na Senegal.

Mashindano haya yaliandaliwa Kwa kushirikiana na ukanda mzima wa CECAFA, awali ilitakiwa ziwe timu nne ikiwemo timu ya taifa ya CONGO BRAZA VILLE ambayo wiki Moja kabla ya mashindano hayo kuanza ilijiondoa kutokana na kupata changamoto ya kusafiri.

Na baada ya timu hiyo kujiondoa, timu ya taifa ya Senegal iliongezwa kuziba nafasi hiyo, lakini Cha ajabu Kenya nao wamejiondoa kwenye michuano hiyo mifupi ambapo leo walitakiwa kucheza na timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) majira ya saa 9:00 Alasiri.

Timu hiyo imelazimika kuanza safari ya kurejea nchini kwao Kenya kuendelea na maandalizi ya CHAN ambayo itaanza tarehe 02/08/2025, hatua hii imekuja mara baada ya kocha mkuu wa timu hiyo Benni McCrthy kutoridhishwa na mazingira ya mashindano hayo.



21/07/2025

RASHFORD NI CHAGUO NAMBA TATU KWA FC BARCELONA -

Sikiliza Bao la Kila siku Jumatatu - Ijumaa kuanzia saa 12:00 Asubuhi Mpaka saa 3:00 Asubuhi, tufuatilie kwenye Mitandao ya Kijamii, Instagram, Facebook, TikTok, na Youtube pia tusikilize kupitia Radio Box na Radio Garden tafuta Bongo FM.

PROUDLY SPONSORED BY



🖥

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongotzfm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bongotzfm:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share