Bongotzfm

Bongotzfm Bongofmtz

25/09/2025

YANGA HII APEWE NABI BALAA FOLZ UWEZO MDOGO -

Sikiliza Bao la Kila siku Jumatatu - Ijumaa kuanzia saa 12:00 Asubuhi Mpaka saa 3:00 Asubuhi, tufuatilie kwenye Mitandao ya Kijamii, Instagram, Facebook, TikTok, na Youtube pia tusikilize kupitia Radio Box na Radio Garden tafuta Bongo FM.

PROUDLY SPONSORED BY



🖥

25/09/2025

BILA KUSAIDIWA FOLZ MECHI YA DERBY ANGEPASUKA -

Sikiliza Bao la Kila siku Jumatatu - Ijumaa kuanzia saa 12:00 Asubuhi Mpaka saa 3:00 Asubuhi, tufuatilie kwenye Mitandao ya Kijamii, Instagram, Facebook, TikTok, na Youtube pia tusikilize kupitia Radio Box na Radio Garden tafuta Bongo FM.

PROUDLY SPONSORED BY



🖥

25/09/2025

ROMAIN FOLZ AKIPOTEZA MECHI MOJA TU KAZI NGUMU -

Sikiliza Bao la Kila siku Jumatatu - Ijumaa kuanzia saa 12:00 Asubuhi Mpaka saa 3:00 Asubuhi, tufuatilie kwenye Mitandao ya Kijamii, Instagram, Facebook, TikTok, na Youtube pia tusikilize kupitia Radio Box na Radio Garden tafuta Bongo FM.

PROUDLY SPONSORED BY



🖥

Mwimbaji nyota wa kimataifa, Rihanna, ametangaza kwa furaha kubwa ujio wa mwanawe wa tatu kupitia chapisho la kupendeza ...
25/09/2025

Mwimbaji nyota wa kimataifa, Rihanna, ametangaza kwa furaha kubwa ujio wa mwanawe wa tatu kupitia chapisho la kupendeza katika ukurasa wake rasmi wa Instagram. Katika picha hiyo ya kipekee, Rihanna ameonekana akiwa na tabasamu la furaha huku akimkumbatia mtoto mchanga kwa upendo, akifichua jina lake kuwa Rocki Irish Mayers, aliyezaliwa rasmi tarehe 13 Septemba 2025.

Mtoto huyu ni baraka mpya kwa Rihanna na mchumba wake, rapa maarufu A$AP Rocky, ambao tayari ni wazazi wa wavulana wawili: RZA Athelston Mayers, aliyezaliwa Mei 2022, Riot Rose Mayers, aliyezaliwa Agosti 2023.

Kwa sasa, familia hii pendwa imebarikiwa kuwa na watoto watatu, na ujio wa Rocki unaongeza furaha na upendo ndani ya familia hiyo maarufu duniani. Rihanna na A$AP Rocky wameendelea kuvutia mashabiki si tu kwa mafanikio yao ya kisanaa, bali pia kwa jinsi wanavyolea watoto wao kwa upendo, mshik**ano, na faragha licha ya kuwa katika macho ya umma.

Imeelezwa kuwa mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mgombea urais wa Jamh...
24/09/2025

Imeelezwa kuwa mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania kupitia CCM, yameridhisha mioyo ya watanzania wengi hivyo anastahili kuchaguliwa tena.

Akihutubia wakazi wa Mufindi leo Septemba 24, Mgombea mwenza wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kipindi chote cha kampeni watanzania wameahidi kukipatia chama hicho ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa Oktoba 29.

"Hayo ndiyo yanayofanya watanzania waseme 'Rais Samia yeye ndiye anatudai sisi' kwa sababu watu wanapima kazi anazofanya. Mimi na wenzangu tumepita katika mikoa 13, mikoa yote tuliyopita wamesema wao ndio watakaoongoza kwa kura za Dkt. Samia," ameeleza Dkt. Nchimbi.

Akianza kwa kueleza mipango iliyopo kwenye Ilani ya CCM 2025 - 2030 kwa Mufindi, Dkt. Nchimbi amesema hospitali ya wilaya itaboreshwa kwa kuongezewa majengo, vitendea kazi pamoja na wataalamu wa afya. "Lakini vilevile tunakwenda kujenga vituo vya afya vitano na zahanati mpya nane," amesema.

Kuhusu sekta ya elimu, Mufindi patajengwa shule mpya nne za sekondari, shule saba za msingi pamoja na ujenzi wa madarasa 264 kwa shule za msingi za zamani, ujenzi wa nyumba 34 za walimu.

Dkt. Nchimbi amebainisha kuwa katika kilimo kutakuwa na ongezeko la ruzuku ya mbolea na mbegu, kujengwa kwa vituo vipya viwili vya kukusanyia na kuuza maziwa. "Tunakwenda pia kuanzisha mashamba darasa kwa ajili ya wakulima, wafugaji na wavuvi ili wanapofanya shughuli za kilimo na uvuvi wafanye kitaalamu na kupata tija zaidi," ameeleza Dkt. Nchimbi.

Kadhalika, Dkt. Nchimbi ameahidi kumaliza kabisa changamoto ya umeme Mufindi kwani licha ya kazi kubwa iliyofanyika, CCM hakijaridhika na hivyo kitajenga mradi wa Nyalawa wa usambazaji wa umeme.

24/09/2025
24/09/2025

Msimamo ni uleule wa TZEE NI SISI,SISI NI TEZEE wnataka mabadiliko Tanzania.

24/09/2025

Saa chache kabla ya Tume ya Uchaguzi ya Malawi kutangaza matokeo, Rais Lazarus Chakwera, ambaye alikuwa akigombea kuendelea kwa awamu nyingine, amekubali kumpongeza mpinzani wake, Peter Mutharika, kwa ushindi mkubwa.

Kupitia hotuba aliyoitoa leo Septemba 24, Rais Chakwera amempongeza Mutharika ambaye ameshinda kwa kupata takribani asilimia 66 ya kura, huku yeye akipata asilimia 24 pekee katika majumuisho ya awali jambo alilosema limemsukuma kutoa pongezi.

"Ninatambua wengi wenu mlioniunga mkono katika uchaguzi huu, hatua hii itawavunja moyo sana. Lakini nataka mfahamu kuwa siku zote nitakuwa mwenye shukrani kwa kuniamini na kuniunga mkono. Na ninafahamu kwa wengi wenu mliopiga kura, matokeo haya ni ishara utashi wenu wa kubadili serikali kwa hivyo kitu sahihi pekee ni mimi kukubali matokeo kwa kukubali utashi wenu k**a wananchi pamoja na kuiheshimu Katiba ya nchi yetu," amesema Rais Chakwera.

Pamoja na kukiri huko, Rais Chakwera amewapongeza wananchi wote wa Malawi kwa kudumisha mshik**ano na utulivu katika kipindi chote cha uchaguzi huku akiahidi makabidhiano ya amani.

Ushindi wa Peter Mutharika wa Democratic Progressive Party (DPP) unamrejesha tena katika nafasi ya urais kwani alihudumu k**a rais wa awamu ya tano kuanzia mwaka 2014 - 2020.

💻

24/09/2025

AMLIPE KIBIASHARA KAFANYA KOSA - HAJA

Unasikiliza Fleva kutokea maeneo gani?
Tufuatilie kupitia Mitandao yetu ya kijamii na Youtube.

Hosts:

24/09/2025

Wakati Chama Cha Mapinduzi kikitumia kaulimbiu 'Kazi na Utu, Tunasonga Mbele' Kada chama hicho, Mch. Peter Msigwa amefafanua maana yake.

Akihutubia leo Septemba 24 kwenye mkutano wa kampeni Mji wa Makambako kabla ya Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuhutubia wananchi waliohudhuria, Msigwa amesema kaulimbiu hiyo inachochewa na upendo wa Chama Cha Mapinduzi kwa Watanzania.

Msigwa amesema vikao vyote vya CCM vimejikita katika kujadili maendeleo yanayojali utu wa Mtanzania, jambo linalokitofautisha na vyama vingine vya siasa nchini.

24/09/2025

HARMONIZE HAWEZI MUZIKI BILA DIAMOND?-HAJA

Unasikiliza Fleva kutokea maeneo gani?
Tufuatilie kupitia Mitandao yetu ya kijamii na Youtube.

Hosts:

Mgombea mwenza wa Urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameeleza kuwa iwapo chama hi...
24/09/2025

Mgombea mwenza wa Urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, ameeleza kuwa iwapo chama hicho kitapata ridhaa ya kuendelea kuongoza serikali kitatenga maeneo ya wakulima na wafugaji ili kuondoa migogoro ya ardhi.

Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo leo Septemba wakati akiendelea na mikutano ya kampeni katika Mji wa Makambako, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

"Ilani ya CCM inataka tuhakikishe kwamba kuna mipango bora ya ardhi, ambvayo inawezesha makundi mbalimbali wananufaika nayo, wafugaji waweze kulima vizuri na wakulima walime vizuri bila maingiliano. Hayo tunakwenda kuyatekeleza katika miaka mitano ijayo," ameahidi Dkt. Nchimbi .

Akieleza kuhusu mipango ya chama kuwaelekea wafanyabiashara Dkt. Nchimbi amesema serikali ijayo itaweka sera rafiki za kodi ili waweze kulipa kodi za hiari na wajisifie kuchangia ujenzi wa nchi, mkakati utakaoenda sambamba na kujenga soko na stendi ya kisasa.

"Ilani ya CCM imesema wana Makambako ni wafanyabiashara na sisi tumeamua kwamba tunaenda kujenga soko la kisasa Makambako ndani ya miaka mitano. Lakini vilevile inasema namna Makambako ilivyo kiungo cha maeneo mbalimbali nchini, sisi tunakwenda kujenga stendi ya kisasa," amesema Dkt. Nchimbi.

Katika sekta ya afya, Dkt. Nchimbi amesema kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wakazi wa Jimbo hilo, CCM kitajenga vituo viwili vya afya, zahanati mpya tatu pamoja na kuboresha hospitali ya Makambako ili iweze kutoa huduma kwa viwango vya hali ya juu.

Akieleza mipango kwenye sekta ya elimu amesema pamoja na kujenga shule mpya, kutafanyika upanuzi kwenye shule za zamani kwa kuongeza madarasa 41. Kadhalika amesema mpango ni kuhakikisha katika kila wananchi 100, 95 wawe na uhakika wa maji safi na salama.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongotzfm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Bongotzfm:

Share

Category