Upendo MEDIA

Upendo MEDIA Upendo Media inamiliki Upendo Fm Radio 107.7, Gazeti la Upendo na Upendo Televisheni, "Amani kwa w
(1)

Ikiwa leo ni siku ya kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa jambo gani unakumbuka wakati wa msiba wake?Wahenga tujuane kweny...
14/10/2023

Ikiwa leo ni siku ya kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa jambo gani unakumbuka wakati wa msiba wake?

Wahenga tujuane kwenye 'comment'

Admin nimesali Jumuiya ya Maduka Sita ya KKKT, DMP, Mtaa wa Mwanalugali.Tukutane kwenye 'Comment' watoto wa Mungu.
14/10/2023

Admin nimesali Jumuiya ya Maduka Sita ya KKKT, DMP, Mtaa wa Mwanalugali.

Tukutane kwenye 'Comment' watoto wa Mungu.

Katika kuadhimisha Siku ya Viwango Duniani, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wadau na wananchi kushiriki vye...
13/10/2023

Katika kuadhimisha Siku ya Viwango Duniani, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wadau na wananchi kushiriki vyema katika
uandaaji wa viwango ili kwa pamoja tuweze kuandaa viwango vinavyotekelezeka.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Oktoba 13,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Viwango Bw.Yona Afrika amesema kuna umuhimu mkubwa wa wadau kushiriki katika uandaaji wa viwango kwani viwango vinasaidia
uzalishaji wa bidhaa bora nchini na kuweza masoko makubwa ndani na nje ya nchi.

Aidha amesema kuwa viwango vinasaidia kupunguza gharama pamoja na kukuongezea wateja kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema suala la uandaaji wa viwango linahusisha wadau wote wa uzalishaji wa bidhaa na sio la Shirika la Viwango pekee.

Siku ya Viwango Duniani huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 14 kila mwaka.

WanaNjombe mpo tayari kutupokea wageni wenu?Kuanzia Lupila, Mbalache, Tandala, Bulongwa, Mang'oto, Luwumbu na Ipepo mjia...
13/10/2023

WanaNjombe mpo tayari kutupokea wageni wenu?

Kuanzia Lupila, Mbalache, Tandala, Bulongwa, Mang'oto, Luwumbu na Ipepo mjiandae tunakuja.

Ndugu zetu mliojibu hapa ni Mwanga mjipigie makofi..
13/10/2023

Ndugu zetu mliojibu hapa ni Mwanga mjipigie makofi..

13/10/2023
Baadhi ya matukio ya ugeni wa Watumishi kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani (ELCA) Sinodi ya Kaskazini mwa M...
13/10/2023

Baadhi ya matukio ya ugeni wa Watumishi kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani (ELCA) Sinodi ya Kaskazini mwa Maziwa Makuu (Michigan) ukiongozwa na Msaidizi wa Askofu wa Sinodi hiyo, Mchg. James Duehring walipotembelea vituo mbalimbali vya Dayosisi ya Mashariki na Pwani ikiwemo Upendo Media leo Oktoba 13, 2023.

Mbali na Wageni hao kutoka Marekani pia Dayosisi ya Mashariki na Pwani imetembelewa na wageni kutokea Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Hamburg, Ujerumani.

NAIBU Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Biteko amesema adhma ya serikali ya Awamu ya Sit...
13/10/2023

NAIBU Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Biteko amesema adhma ya serikali ya Awamu ya Sita ni kufikisha umeme katika kila kitongoji kabla ya uchaguzi wa 2025.
Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati akiwasha umeme kwenye Kijiji cha Ndalibo, Kata ya Mtanana Wilaya ya Kongwa sambamba na kuzindua kisima cha maji ambacho kitakuwa kikitumia umeme kwa manufaa ya wananchi wa eneo hilo.

Dkt.Biteko amesema kuwa Mhe. Rais Dkt. Samia anapambana usiku na mchana kuhakikisha umeme unapatikana na kuinua hali za maisha ya wananchi waliopo vijijini kwani umeme sio anasa bali ni jambo la muhimu kwa sasa.

“Katika sekta ya umeme tutafanya kila kupeleka umeme katika kila kitongoji kupeleka umeme katika kila eneo kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025 katika uongozi huu wa serikali ya Awamu ya Sita umeme sio anasa bali ni jambo la lazima.”amesema Dkt.Biteko

Habari kamili https://www.upendomedianetwork.co.tz/habari-kamili.php?nid=162

Kutokana na changamoto zilizokuwepo katika matamasha na hafla nyingi za Muziki wa Injili leo atakuwepo Adolph Nzwalla mt...
13/10/2023

Kutokana na changamoto zilizokuwepo katika matamasha na hafla nyingi za Muziki wa Injili leo atakuwepo Adolph Nzwalla mtaalamu kwenye uandaaji wa matamasha ya muziki kwa ajili ya kutoa ushauri.

TOPIC: NINI KIFANYIKE KUBORESHA EVENTS ZA GOSPEL
Mada; Nini kifanyike kuboresha matamasha 'Events' za muziki wa Injili na mada nyingine nyingi..

Ewe mtoto wa Yesu usikose !!!

UTEUZI.
12/10/2023

UTEUZI.

Wale waliotembea sehemu nyingi tukutane kwenye 'comment'..
12/10/2023

Wale waliotembea sehemu nyingi tukutane kwenye 'comment'..

Serikali imesimamisha leseni zote Nchi nzima za Kampuni ya Nadoyoo Mineral Trading kufuatia kukamatwa kwa mmoja wa wahus...
12/10/2023

Serikali imesimamisha leseni zote Nchi nzima za Kampuni ya Nadoyoo Mineral Trading kufuatia kukamatwa kwa mmoja wa wahusika wa Kampuni hiyo akitorosha dhahabu takribani kilo 4.3 zenye thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 562,288,207.

Hayo yamesemwa Usiku wa kuamkia leo Oktoba 11, 2023  na Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde  alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari Wilayani Kahama baada ya kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo "Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan haitakubali kuona watu wachache wanajihusisha na vitendo hivi viovu vya kutorosha madini. Nataka niwaambie, tutachukua hatua kali dhidi ya yeyote tutakayemkamata akijihusisha na utoroshaji wa madini” amesema Mh. Mavunde.

“Ninapoingia Wizara ya Madini mwezi mmoja uliopita nilisema, ukitaka kufahamu sura yangu nyingine basi jaribu kutorosha madini. Sasa basi, kuanzia leo mtu yeyote atayekamatwa kwa kosa la kutorosha madini, tutakwenda kusimamisha leseni zake zote Nchi nzima wakati tukisubiri hukumu ya vuombo vya sheria, na iwapo mahakama itabaini mhusika ana hatia, tutakwenda kuchukua hatua kali ikiwemo kufuta kabisa leseni zote na kuhakikisha hatajihusisha tena na biashara ya madini nchini” aliongeza Mhe. Mavunde.

Sambamba na hilo, Mhe. Mavunde alitoa wito kwa wafanyabiashara wa madini kuwa wazalendo kwa kufuata taratibu zilizopo na kulipa tozo, ada na kodi mbalimbali ili kuiwezesha Serikali kupata mapato na kuendelea kuimarisha huduma kwa wananchi ikiwemo ujenzi wa barabara, umeme, afya na elimu.

Pia, Mheshimiwa Mavunde alionesha utayari wa kutenga siku na kukaa pamoja na wafanyabiashara wa madini ili kwa pamoja wamweleze hasa ni nini wanadhani inaweza kuwa ni changamoto kubwa inayopelekea baadhi yao kufikia hatua ya kujihusisha na vitendo vya utoroshaji madini, hatua ambayo anaamini itasaidia Serikali kuchukua njia sahihi kushughulikia suala hilo.

Vilevile, Mheshimiwa Mavunde alieleza bayana kuwa pamoja na hatua kali
za kisheria kuchukuliwa dhidi ya watoroshaji wa madini, pia madini
yote yatakayokamatwa yatahifadhiwa na Serikali.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Upendo MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Upendo MEDIA:

Share