Upendo MEDIA

Upendo MEDIA Upendo Media inamiliki Upendo Fm Radio 107.7, Gazeti la Upendo na Upendo Televisheni, "Amani kwa w

Ikiwa leo ni siku ya kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa jambo gani unakumbuka wakati wa msiba wake?Wahenga tujuane kweny...
14/10/2023

Ikiwa leo ni siku ya kuadhimisha kifo cha Baba wa Taifa jambo gani unakumbuka wakati wa msiba wake?

Wahenga tujuane kwenye 'comment'

Admin nimesali Jumuiya ya Maduka Sita ya KKKT, DMP, Mtaa wa Mwanalugali.Tukutane kwenye 'Comment' watoto wa Mungu.
14/10/2023

Admin nimesali Jumuiya ya Maduka Sita ya KKKT, DMP, Mtaa wa Mwanalugali.

Tukutane kwenye 'Comment' watoto wa Mungu.

Katika kuadhimisha Siku ya Viwango Duniani, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wadau na wananchi kushiriki vye...
13/10/2023

Katika kuadhimisha Siku ya Viwango Duniani, Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wadau na wananchi kushiriki vyema katika
uandaaji wa viwango ili kwa pamoja tuweze kuandaa viwango vinavyotekelezeka.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Oktoba 13,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Viwango Bw.Yona Afrika amesema kuna umuhimu mkubwa wa wadau kushiriki katika uandaaji wa viwango kwani viwango vinasaidia
uzalishaji wa bidhaa bora nchini na kuweza masoko makubwa ndani na nje ya nchi.

Aidha amesema kuwa viwango vinasaidia kupunguza gharama pamoja na kukuongezea wateja kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema suala la uandaaji wa viwango linahusisha wadau wote wa uzalishaji wa bidhaa na sio la Shirika la Viwango pekee.

Siku ya Viwango Duniani huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 14 kila mwaka.

WanaNjombe mpo tayari kutupokea wageni wenu?Kuanzia Lupila, Mbalache, Tandala, Bulongwa, Mang'oto, Luwumbu na Ipepo mjia...
13/10/2023

WanaNjombe mpo tayari kutupokea wageni wenu?

Kuanzia Lupila, Mbalache, Tandala, Bulongwa, Mang'oto, Luwumbu na Ipepo mjiandae tunakuja.

Ndugu zetu mliojibu hapa ni Mwanga mjipigie makofi..
13/10/2023

Ndugu zetu mliojibu hapa ni Mwanga mjipigie makofi..

13/10/2023
Baadhi ya matukio ya ugeni wa Watumishi kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani (ELCA) Sinodi ya Kaskazini mwa M...
13/10/2023

Baadhi ya matukio ya ugeni wa Watumishi kutoka Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Marekani (ELCA) Sinodi ya Kaskazini mwa Maziwa Makuu (Michigan) ukiongozwa na Msaidizi wa Askofu wa Sinodi hiyo, Mchg. James Duehring walipotembelea vituo mbalimbali vya Dayosisi ya Mashariki na Pwani ikiwemo Upendo Media leo Oktoba 13, 2023.

Mbali na Wageni hao kutoka Marekani pia Dayosisi ya Mashariki na Pwani imetembelewa na wageni kutokea Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Hamburg, Ujerumani.

NAIBU Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Biteko amesema adhma ya serikali ya Awamu ya Sit...
13/10/2023

NAIBU Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Biteko amesema adhma ya serikali ya Awamu ya Sita ni kufikisha umeme katika kila kitongoji kabla ya uchaguzi wa 2025.
Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati akiwasha umeme kwenye Kijiji cha Ndalibo, Kata ya Mtanana Wilaya ya Kongwa sambamba na kuzindua kisima cha maji ambacho kitakuwa kikitumia umeme kwa manufaa ya wananchi wa eneo hilo.

Dkt.Biteko amesema kuwa Mhe. Rais Dkt. Samia anapambana usiku na mchana kuhakikisha umeme unapatikana na kuinua hali za maisha ya wananchi waliopo vijijini kwani umeme sio anasa bali ni jambo la muhimu kwa sasa.

“Katika sekta ya umeme tutafanya kila kupeleka umeme katika kila kitongoji kupeleka umeme katika kila eneo kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025 katika uongozi huu wa serikali ya Awamu ya Sita umeme sio anasa bali ni jambo la lazima.”amesema Dkt.Biteko

Habari kamili https://www.upendomedianetwork.co.tz/habari-kamili.php?nid=162

Kutokana na changamoto zilizokuwepo katika matamasha na hafla nyingi za Muziki wa Injili leo atakuwepo Adolph Nzwalla mt...
13/10/2023

Kutokana na changamoto zilizokuwepo katika matamasha na hafla nyingi za Muziki wa Injili leo atakuwepo Adolph Nzwalla mtaalamu kwenye uandaaji wa matamasha ya muziki kwa ajili ya kutoa ushauri.

TOPIC: NINI KIFANYIKE KUBORESHA EVENTS ZA GOSPEL
Mada; Nini kifanyike kuboresha matamasha 'Events' za muziki wa Injili na mada nyingine nyingi..

Ewe mtoto wa Yesu usikose !!!

UTEUZI.
12/10/2023

UTEUZI.

Wale waliotembea sehemu nyingi tukutane kwenye 'comment'..
12/10/2023

Wale waliotembea sehemu nyingi tukutane kwenye 'comment'..

Serikali imesimamisha leseni zote Nchi nzima za Kampuni ya Nadoyoo Mineral Trading kufuatia kuk**atwa kwa mmoja wa wahus...
12/10/2023

Serikali imesimamisha leseni zote Nchi nzima za Kampuni ya Nadoyoo Mineral Trading kufuatia kuk**atwa kwa mmoja wa wahusika wa Kampuni hiyo akitorosha dhahabu takribani kilo 4.3 zenye thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 562,288,207.

Hayo yamesemwa Usiku wa kuamkia leo Oktoba 11, 2023  na Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Mavunde  alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari Wilayani Kahama baada ya kuk**atwa kwa mfanyabiashara huyo "Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan haitakubali kuona watu wachache wanajihusisha na vitendo hivi viovu vya kutorosha madini. Nataka niwaambie, tutachukua hatua kali dhidi ya yeyote tutakayemk**ata akijihusisha na utoroshaji wa madini” amesema Mh. Mavunde.

“Ninapoingia Wizara ya Madini mwezi mmoja uliopita nilisema, ukitaka kufahamu sura yangu nyingine basi jaribu kutorosha madini. Sasa basi, kuanzia leo mtu yeyote atayek**atwa kwa kosa la kutorosha madini, tutakwenda kusimamisha leseni zake zote Nchi nzima wakati tukisubiri hukumu ya vuombo vya sheria, na iwapo mahak**a itabaini mhusika ana hatia, tutakwenda kuchukua hatua kali ikiwemo kufuta kabisa leseni zote na kuhakikisha hatajihusisha tena na biashara ya madini nchini” aliongeza Mhe. Mavunde.

Sambamba na hilo, Mhe. Mavunde alitoa wito kwa wafanyabiashara wa madini kuwa wazalendo kwa kufuata taratibu zilizopo na kulipa tozo, ada na kodi mbalimbali ili kuiwezesha Serikali kupata mapato na kuendelea kuimarisha huduma kwa wananchi ikiwemo ujenzi wa barabara, umeme, afya na elimu.

Pia, Mheshimiwa Mavunde alionesha utayari wa kutenga siku na kukaa pamoja na wafanyabiashara wa madini ili kwa pamoja wamweleze hasa ni nini wanadhani inaweza kuwa ni changamoto kubwa inayopelekea baadhi yao kufikia hatua ya kujihusisha na vitendo vya utoroshaji madini, hatua ambayo anaamini itasaidia Serikali kuchukua njia sahihi kushughulikia suala hilo.

Vilevile, Mheshimiwa Mavunde alieleza bayana kuwa pamoja na hatua kali
za kisheria kuchukuliwa dhidi ya watoroshaji wa madini, pia madini
yote yatakayok**atwa yatahifadhiwa na Serikali.

Katika kuboresha Huduma za afya nchini   Serikali kupitia Wizara yaAfya imejenga wodi maalum za uangalizi wa watoto njit...
12/10/2023

Katika kuboresha Huduma za afya nchini  Serikali kupitia Wizara ya
Afya imejenga wodi maalum za uangalizi wa watoto njiti 128 na kwa mwaka huu imepanga  kujenga wodi nyingine 100 ili kuhakikisha vifo vya watoto wachanga vinapungua na kuisha kabisa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Kwanza la Afya ya Mtoto Tanzania  na mkutano wa 24 wa Madaktari Bingwa wa Watoto Tanzania unaoendelea jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema kuwa Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika uangalizi wa watoto njiti lengo likiwa ni kuwapatia huduma bora na
uangalizi maalum mpaka watakapofikia uzito unaostahili.

“Uwekezaji huu ni pamoja na kuwa na madaktari Bingwa wa watoto
(Madaktari wa Mama Samia), kuboresha miundombinu katika Hospitali zote zenye wodi ya uangalizi maalum kwa watoto njiti ( NICU)”. Amesema Dkt. Mollel.

Dkt. Mollel amesema serikali imeamua kuwekeza katika eneo hilo kwani mtoto kuanzia anapozaliwa mpaka kutimiza miaka 18 anahitaji uangalizi wa karibu ili kupata ustawi mzuri na kuwa na taifa la kesho imara.

Aidha, ametoa wito kwa Madaktari Bingwa wa Watoto nchini kuendelea kufanya kazi nzuri ya kuwahudumia watoto wanaozaliwa kabla ya siku na wale wanaozaliwa kawaida kwani wote wanahitaji uangalizi wa karibu katika ukuaji, “Kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu tunawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayofanya ya kuhakikisha mnapunguza vifo vya watoto wachanga nchini, na kwa mantiki hiyo niwahakikishie kuwa tutakuwa bega kwa bega na nyie ili kuhakikisha mnatekeleza majukumu yenu kwa ufasaha”. Amesema Dkt. Mollel.

Kwa upande wake Mshauri Mkuu Mwandamizi wa Sera na mipango kutoka USAID Tanzania, Jema Bisimba amesema kuwa hivi karibuni watazindua programu ya USAID Tuwajali watoto yenye lengo la kusaidia watoto wanaoishi na virusu vya UKIMWI kuanzia miaka sifuri hadi miaka 17 kwa kuwawezesha Huduma zote zinazohusu mambo ya watoto.

Bisimba amesema kwa kupitia programu hiyo watasaidia Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Afya kufikia lengo la kumaliza maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa watoto fufikia 2030


Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT na Askofu wa Dayosisi a Kaskazini Dakta,  Fredrick Shoo  amesema k...
11/10/2023

Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT na Askofu wa Dayosisi a Kaskazini Dakta, Fredrick Shoo amesema kuwa umoja na ushirikiano ni jambo la msingi katika kujenga mwili wa Kristo Katika Kanisa.

Askofu Shoo amesema hayo wakati alipokuwa akifungua mkutano Mkuu wa 16 wa Jimbo Hai Dayosisi ya Kaskazini iliyofanyika jimboni hapo mkoani Kilimanjaro.
Amesema kuwa ndani ya mwili wa Kristo Kuna vipawa na karama nyingi ambavyo vikitumika kwa umoja bila ubinafsi vitaleta ufanisi katika utendaji wa kazi sharikani na kanisa kwa ujumla.

Amewataka watumishi kwa vipawa vyao kutumika kwa uaminifukwa kuhubiri neno la kweli na maombi ili kujenga mwili wa Kristo na kufanya Kanisa kuwa mahali salama penye amani na utulivu.
Kwa upande wake Katibu wa Dayosisi ya Kaskazini Injinia Zebedayo Moshi amewataka viongozi mbalimbali wa Jimbo kuwa na umoja, kunia mamoja, kufanya kazi kwa pamoja na kuweka ubinafsi pembeni.

Alipwa Milion 400 kwa kukaa jela miaka 30 kimakosaMwanaume mmoja nchini Marekani amejikuta akibubujikwa na machozi ya fu...
11/10/2023

Alipwa Milion 400 kwa kukaa jela miaka 30 kimakosa

Mwanaume mmoja nchini Marekani amejikuta akibubujikwa na machozi ya furaha yasiyo na mfano baada ya Mahak**a kuthibitisha hana hatia  na kutakiwa kuachiwa huru 

Perry Lott mpaka anatangaziwa uhuru wake alikuwa ameshatumikia   miaka zaidi ya 30 jela ambapo alikutwa na hatia na kuhukumiwa kwenda jela mnamo 1987, Lott aliachiwa kwa mara ya kwanza mnamo 2018 baada ya vipimo vya awali kuonesha hakuwa mhusika kwenye tukio la ubakaji japo aliyekuwa Jaji wa Mahak**a ya Jimbo la Oklahoma wakati huo Paul Smith alieleza kuwa uchunguzi ungeendelea hivyo Lott aishi kwa masharti yaliyowekwa na Mahak**a mpaka pale majibu rasmi ya vipimo vitakapotolewa.

Mnamo Oktoba 10, 2023 Mahak**a hiyo imejiridhisha kuwa Lott hakuwa na hatia ya shtaka la ubakaji ambapo Jaji wa Mahak**a hiyo,Steven Kessinger aliamuru  aachiliwe huru na kutakiwa kulipwa Milioni 438 k**a fidia ya kutumikia kifungo kimakosa.

Punde baada ya kuachiwa Lott alisema alikuwa na imani tokea siku ya kwanza kufungwa jela kuwa siku moja ukweli utagundulika na anamshukuru Mungu kwa kufanikisha hilo.

Picha za Matukio ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa K**e yaliyofanyika katika viwanja vya  Kanisa Kuu Bungo...
11/10/2023

Picha za Matukio ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa K**e yaliyofanyika katika viwanja vya Kanisa Kuu Bungo, KKKT Dayosisi ya Morogoro.

Mgeni rasmi akiwa ni Sheikh wa Mkoa wa Morogoro, Twaha Salum Kilango pamoja na Mwenyeji wake Mgeni Maalumu Baba Askofu Jacob Mameo wa KKKT Dayosisi ya Morogoro.

Mkurugenzi Mtendaji wa Upendo Media Network, Neng'ida Johanes (Kulia) akikabidhiwa Leseni ya kurusha matangazo ya FM kwa...
11/10/2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Upendo Media Network, Neng'ida Johanes (Kulia) akikabidhiwa Leseni ya kurusha matangazo ya FM kwa mikoa 20 na Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) Kanda ya Mashariki, Nobert Makonda wakati makabidhiano ya Leseni iliyofanyika leo Oktoba 11, 2023 katika ofisi za Kanda.

Aidha Makonda ameipongeza Upendo Media kwa kuzidi kupiga hatua huku akieleza kuwa ni furaha kwa TCRA kuona vyombo vya habari vikizidi kupiga hatua zaidi.

Baadhi ya Matukio ya kuelekea siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika leo Oktoba 11, 2023  Morogoro ikiongozwa na KKKT.
11/10/2023

Baadhi ya Matukio ya kuelekea siku ya Mtoto wa Afrika inayofanyika leo Oktoba 11, 2023 Morogoro ikiongozwa na KKKT.

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Upendo MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Upendo MEDIA:

Share

Amani Kwa Wote

Ungana nasi ili uwe wa kwanza kupata habari za kiroho, kitaifa na kimataifa #UpendoRadio107.7 #UpendoTV #UpendoGazeti #UpendoMedia