Jua na Junior

Jua na Junior Do you know? Je wajua? Motto: Know what you don't know
Kauli mbiu: Jua usichokijua

Ni ukurasa rasmi wa chombo cha habari cha mtandaoni kiitwacho Junior MedTech Tanzania Limited kwa ajili ya kuwajuza watu mambo ambayo wengi wetu hatufahamu.

Je Wajua?Muonekano halisi wa VVU?Kumekuwepo kusambaa kwa taarifa na picha za upotoshaji inayosemekana ni muonekano wa ki...
02/01/2026

Je Wajua?

Muonekano halisi wa VVU?

Kumekuwepo kusambaa kwa taarifa na picha za upotoshaji inayosemekana ni muonekano wa kirusi cha UKIMWI (VVU) aliyevutwa kwa hadubini ya umeme (electronic microscope), jambo ambalo si kweli.

Picha hiyo inayosambaa k**a ionekanavyo kwenye picha sio VVU bali ni kiumbe mkubwa ambaye anaonekana kwa macho ya kawaida bila ya kutumia hadubini, kiumbe huyo ni kiwavi(lavar) mwenye miba anaitwa SPIKY CATERPILLAR, ni kiluwiluwi k**a wengine ambao ni miongoni mwa hatua za ukuaji wanazopitia wadudu(insects) mbalimbali k**a vile vipepeo, nondo n.k.

Viwavi hawa huwa na mwili uliozungukwa na miba, nywele ngumu au vinyweleo vyenye ncha kali zenye sumu katika sehemu mbalimbali ambavyo huwasaidia kujilinda na maadui mbalimbali na sumu hiyo huweza kusababisha muwasho, maumivu, uvimbe, vipele au mzio(allergy) kwa atakaegusa au kuchomwa na miba hizo.

Na picha ya pili unayoiona ndiyo picha iliyothibitishwa na wataalam husika kuwa inafanana zaidi na VVU.

31/12/2025
Je Wajua?Kwanini baadhi ya watu Uingereza huitwa SIR au DAME?.Tumeona baadhi ya waingereza wakiitwa "Sir" mwanzo wa maji...
26/12/2025

Je Wajua?
Kwanini baadhi ya watu Uingereza huitwa SIR au DAME?.

Tumeona baadhi ya waingereza wakiitwa "Sir" mwanzo wa majina yao mfano SIR ALEX FERGUSON na wengine kuitwa "Dame", sasa hii hapa sababu ya wao kuitwa hivyo;

"Sir" ni cheo ambacho hupewa wanaume na "Dame" ni cheo kinacholingana na SIR ila hiki hupewa wanawake ambavyo hutolewa na Mfalme au Malkia wa Uingereza (U.K) kwa watu waliotoa mchango mkubwa kwa taifa au kufanya mambo makubwa kwa taifa au mambo ya kipekee ambayo yatampa heshima kwa taifa.

Vyeo hivi hutolewa kwa raia wa Uingereza pekee lakini pia kuna cheo kinacholingana na SIR na DAME kwa ajili ya kupewa watu wa nje ya Uingereza yaani wageni ambapo huitwa KBE, DBE, GCMG, GCB n.k mwishoni mwa majina yao na ni kosa kumuita Sir mtu asiyekuwa Muingereza labda iwapo atachukua uraia wa uingereza.

Na kisheria jina hili linatumika kwenye aidha unapoitwa majina yote mawili au matatu yaani jina lako, jina la baba na jina la mwisho au ukoo kwa mfano SIR ALEX FERGUSON, Lakini pia linaweza kutumika kwenye jina moja la kwanza la muhusika tu kwa mfano SIR ALEX lakini cheo hiki haitakiwi kuitwa na jina la mwisho pekee au la kati pekee wala la kati na la mwisho kwa mfano ni makosa kuita SIR FERGUSON.

Baadhi ya waingereza waliopewa cheo hicho ni:

SIR ALEX FERGUSON
SIR LEWIS HAMILTON
SIR TIM BERNERS-LEE
SIR ELTON JOHN
SIR DAVID ATTENBOROUGH

Baadhi ya wageni wasio waingereza waliopewa cheo kinacholingana na SIR na DAME ni;

Nelson Mandela GCMG (Afrika Kusini)
Bill Gates KBE (Marekani)
Melinda Gates DBE (Marekani)
Desmond Tutu KBE (Afrika Kusini)
Angela Merkel GCMG (aliyekuwa Kansela wa Ujerumani)
Angelina Jolie GCMG (Marekani)
Steven Spielberg KBE (Marekani)
Bono KBE (Ireland)
Pelé KBE (Brazil)
Ronald Reagan GCB (aliyekuwa rais wa Marekani)
George Bush GCB (aliyekuwa rais wa Marekani)
Dwight Eisenhower GCB (aliyekuwa rais wa Marekani)
N.k.

Baadhi ya wanawake wa Uingereza waliopewa cheo cha Dame ni;

DAME JUDI DENCH
DAME MAGGIE SMITH
DAME HELLEN MIRREN
DAME VIVIENNE WESTWOOD
DAME ZAHA HADID
DAME JESSICA ENNIS-HILL
DAME KELLY HOLMES
DAME SARAH GILBERT
N.k.

Je Wajua?.Ukisearch google maneno yafuatayo yatatokea maajabu?Ukiingia google ukasearch maneno yafuatayo itatokea jambo ...
24/12/2025

Je Wajua?.
Ukisearch google maneno yafuatayo yatatokea maajabu?
Ukiingia google ukasearch maneno yafuatayo itatokea jambo lisilokuwa la kawaida kiasi unaweza ukajua ni tatizo la kimtandao au maajabu yasio kawaida lakini ukweli ni kwamba,

Google wanayo feature iitwayo "Google Easter Eggs" kwa ajili ya kuweka mvuto, kufurahisha na kuwashangaza watumiaji wake iwapo wakisearch baadhi ya maneno kwa kuwaonyesha jambo lisilotegemewa kuonekana kwenye kurasa ya google na pengine kuwapa michezo (games) la kucheza ukiwa hapo hapo google.

Baadhi ya maneno ambayo ukisearch wakati wowote google utaona maajabu ni;
"67" Ukiingia google ukasearch namba "67" utaona ukurasa wote wa google ukicheza k**a vile kuna hitilafu ya kiufundi au maajabu.

"Wizard of Oz" ukisearch maneno hayo utaona viatu vyekundu upande wa kulia ukivigusa viatu hivyo utaona mabadiliko yasio ya kawaida kuyaona google na ukurasa utabadilika na utasikia sauti isiyo ya kawaida na alama ya viatu itatoka na itakaa alama ya kimbunga na yenyewe ukiigusa pia itabadilika na kurudi kawaida na ile alama ya viatu itarudi, na itajirudia hivyo ukigusa tena na tena.

"Askew" ukisearch neno hilo pia utaona ukurasa wote wa google umekaa upande yaani umepinda kidogo upande mmoja, jambo ambalo si kawaida kwenye ukurasa wa google.

"Do a barrel roll" pia ukisearch maneno hayo pia ukurasa wote wa google utazunguka kwa mzunguko wa nyuzi 360⁰ ambapo nayo ni feature isiyo ya kawaida kwa google.

Hivyo ukiona umefanya hvyo na yakatokea hayo jua kwamba hakuna madhara yoyote isipokuwa ni sehemu ya google kustaajabisha, kuvutia na kufurahisha watumiaji wake tu.

Je wajua?Fomula ya kutengeneza Coca-cola haijulikani na ni siri haijawahi kuvuja?Fomula nzima ya kutengeneza soda ya Coc...
21/12/2025

Je wajua?
Fomula ya kutengeneza Coca-cola haijulikani na ni siri haijawahi kuvuja?

Fomula nzima ya kutengeneza soda ya Coca-Cola haijulikani na watu wengine wowote duniani isipokuwa watu 2 tu ambao ni miongoni mwa wakurugenzi wakuu wa kampuni hiyo na hawajawahi kutajwa hata majina.

Majina ya wakurugenzi hao wanaojua fomula hiyo hayajawahi kutajwa na hayajulikani ni siri nzito na wao pekee ndo wanaruhusiwa kujua mchakato mzima wa kuchanganya ili kuipata Coca-cola halisi na hata wakihitaji kusafiri hawaruhusiwi kusafiri kwa usafiri mmoja yaani ndege moja au gari moja ili kuepuka ajali itakayosababisha vifo vya wote kwa wakati mmoja.

Fomula hiyo inayoitwa (Merchandise 7X) imeandikwa kwenye karatasi moja tu haijwahi kuandikwa sehemu nyingine au karatasi nyingine yoyote,
Kisha karatasi hiyo imehifadhiwa kwenye chumba maalum kiitwacho THE VAULT kilichopo kwenye makumbusho yao yaitwayo (The World of Coca-Cola) huko Atlanta nchini Marekani.

Katika chumba hicho chenye ulinzi mkali wakurugenzi wawili tu ndo wanaruhusiwa na ndo wana uwezo wa kuingia kwenye chumba hicho chenye ulinzi mkali wa geti kubwa lenye lock ya kisasa na ngumu na lenye chuma kizito, alama za vidole (Fingerprints/ Biometric) lakini pia kuna vifaa vya kugundua mwendo iwapo mtu ataingia kengele itagonga kwa sauti kubwa na pia kuna walinzi wanaolinda eneo hilo.

Fomula hiyo inalindwa na kufichwa kwa sababu kadhaa ikiwepo kuzuia wengine wasijue jinsi ya kutengeneza soda halisi ya Coca-Cola kwa ajili ya ushindani wa kibiashara, thamani ya brand yao kuwa kubwa zaidi, siri za masoko, siri za haki miliki na siri za biashara kwa ujumla.

Na mpaka sasa hakuna kampuni yoyote iliyowahi kutengeneza soda iliyofanana na Coca-Cola kwa asilimia 100 badala yake hufananishwa kwa baadhi ya vitu tu na siri yao ya fomula haijawahi kuvuja ijapokuwa kuna baadhi ya taarifa kadhaa zilisambazwa na baadhi ya mashirika na taasisi kuwa wameipata fomula hiyo lakini wenyewe Coca-Cola walizikana fomula hizo kuwa sio sahihi.

Je wajua?Ukweli kuhusu WARNER BROS kununuliwa na NETFLIX.Taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusu Warner Bros imenunuliwa ...
10/12/2025

Je wajua?
Ukweli kuhusu WARNER BROS kununuliwa na NETFLIX.

Taarifa zinazosambaa mitandaoni kuhusu Warner Bros imenunuliwa na Netflix, wengine wamefika mbali zaidi na kuanza kugawa baadhi ya vitu mbalimbali walivyonunua.

Ukweli ni kwamba Warner Bros wameingia makubaliano na Netflix ya kuinunua kampuni hiyo kwa dau la $82.7 Billions kwa makubaliano kadhaa ikiwepo kusubiri mpaka Warner watakapofanikiwa kuigawa kampuni yake ya Discovery Global inayomiliki mitandao ya kebo k**a CNN, TNT na TBS ambapo inakadiriwa mauzo hayo huenda yatafanyika ifikapo mwisho wa mwaka 2026 au mwanzoni mwa mwaka 2027 na mauziano hayo yatahusisha Warner Bros Studio, HBO na HBO MAX pekee lakini haitohusisha CNN, TNT, TBS na vituo vya TV.

Lakini licha ya makubaliano hayo kupita na kutangazwa kampuni ya SKYDANCE (PARAMOUNT) imeongeza dau kubwa zaidi la kuinunua Warner Bros. Discovery kwa ujumla yaani kuanzia studio, Discovery Global, HBO, HBO Max na Vituo vya TV vyote kwa ujumla kwa dau la $108.4 Billions, hivyo inawezekana Warner Bros ikaghairi wakati wowote dili la kuiuza kampuni hiyo kwa Netflix.

Je Wajua?.Simba wa MGM walitumika watu 8 mpaka sasa?Logo ya kampuni ya uandaaji wa filamu duniani ya Metro-Goldwin Mayer...
23/11/2025

Je Wajua?.

Simba wa MGM walitumika watu 8 mpaka sasa?

Logo ya kampuni ya uandaaji wa filamu duniani ya Metro-Goldwin Mayer (MGM) ambayo kwa sasa inaitwa (AMAZON MGM) ina picha mjongeo ya simba akiwa ananguruma aitwae (Leo The Lion)

Simba aliyetumika kwenye logo hiyo ilitengenezwa kwa kutumia watu 8 mpaka sasa kwa nyakati tofauti tofauti na simba mmoja wapo wa 9 ni wa kutengeneza.

1. SLATS (1924–1928): Huyu alikuwa simba wa kwanza. Alitumika kwenye filamu za kimya (silent films) na hakuunguruma (alikuwa anatizama tu).

2. JACKIE (1928–1956):

Huyu ndiye aliyekuwa simba wa kwanza kuunguruma. Ungurumo wake ulirekodiwa kupitia gramafoni na kutumika kwenye filamu za sauti (talkies) za mwanzo. Yeye ndiye alijulikana sana kwa miaka mingi.

3. NUMA (1927-1928)

Alitumika kwenye majaribio ya logo za filamu za mwanzo za rangi (Technicolor).

4. TELLY (1928–1932) na

5. COFFEE (1932–1935): Walitumika kwa majaribio ya filamu za rangi za mwanzo (two-strip color).

6. TANNER (1934–1956): Huyu alitumika sana kwenye filamu zote za rangi za Technicolor hadi katikati ya miaka ya 1950.

7. GEORGE (1956–1957): Alitumika kwa muda mfupi tu.

8. LEO (1957–Hadi Sasa): Huyu ndiye simba ambaye ametumika kwa muda mrefu zaidi na ndiye anayeonekana kwenye filamu nyingi za MGM hadi leo. Jina lake la utani la "Leo" ndilo limetumika kwa simba wote kwa ujumla.

9. CGI Leo (2021–Hadi Sasa): Tangu mwaka 2021, MGM imeanza kutumia toleo la simba huyu aliyetengenezwa kwa kompyuta (CGI), ingawa bado anafanana na Leo wa asili.

Kwa kifupi, simba maarufu na anayejulikana sana leo anaitwa Leo.

Je wajua?Kuna ziwa ambalo huwezi kuzama ukiingia hata kwa ukitaka kwa hiari yako?.Nchini Misri maeneo ya jangwa la magha...
07/11/2025

Je wajua?
Kuna ziwa ambalo huwezi kuzama ukiingia hata kwa ukitaka kwa hiari yako?.

Nchini Misri maeneo ya jangwa la magharibi mwa misri (Western Egypt Desert) kuna maziwa yaitwayo Ziwa la chumvi la Siwa (Siwa salt Lakes) yaliyopo kwenye jangwa hilo ambayo huvutia watu kwa tabia yake ya ajabu ya kukufanya binadamu isizame kwenye maji ya maziwa hayo iwapo ukiingia hata k**a unataka uzame makusudi.

Ukiingia kwenye maji ya maziwa hayo utaelea tu bila ya kuzama na hutokea hivyo kwa sababu ladhaa k**a k**a vile kanuni za akimedesi (Archimedes principle), msongamano mkubwa wa maji uliopo katika eneo dogo la ziwa, na sababu nyingine yenye nguvu zaidi ni kwasababu ya wingi wa chumvi katika maji hayo,

Kwa kawaida maji ya bahari huwa na chumvi kiasi cha 3.5% lakini maji ya maziwa hayo huwa na chumvi kiasi cha 30% hivyo husababisha uzito mkubwa wa maji zaidi ya maji ya bahari na kuzidi zaidi yaa uzito wa mwili wa binadamu kiasi unaweza kukufanya uelee bila ya kuzama.

Je wajua?Alama ya nyoka aliyeizunguka fimbo kwenye nembo za sekta ya afya?Kuna nembo mbili ambazo hutumika kwenye nembo ...
15/10/2025

Je wajua?
Alama ya nyoka aliyeizunguka fimbo kwenye nembo za sekta ya afya?
Kuna nembo mbili ambazo hutumika kwenye nembo za hospitali na sekta nyingine za afya na watu wengi hawafahamu mahusiano yaliyopo kati ya alama hizo na afya.
Alama hizo zinamaanisha ni alama za k**a inavyoaminika kuwa ni miungu ya kigiriki ambao wanaitwa Asclepius na Hermes.
Asclepius inaaminika kuwa ni mungu wa kigiriki ambae alikuwa akitumia fimbo iliyozungukwa na nyoka iitwayo (Rod of Asclepius), inasadikika Asclepius ni mtoto wa Apollo na Coronis na inasadikika alikuwa ni mungu wa kuzaliwa upya, matibabu, madawa n.k, na hii inaaminika kuwa ndiyo alama sahihi kutumika kwenye sekta ya afya ikisimama k**a alama ya uponyaji kutoka kwamungu huyo Asclepius.
Hermes inaaminika pia kuwa ni mungu wa kigiriki ambae alikuwa akitumia fimbo yenye mbawa mbili na iliyozungukwa na nyoka wawili wakiitazama fimbo, inaaminika kuwa ni mtoto wa Zeus na Maia na inasadikika alikuwa ni mungu wa biashara, utajiri, amani, rutuba, safari, lugha n.k, na nembo hii ni nembo ambayo inasadikika inatumika kimakosa kwenye sekta ya afya ikilinganishwa na ile ya Asclepius ambaye ndiye mungu wa afya.

Je wajua?,Si kweli kwamba wazo pekee la biashara ni lile unalolijua tu.Ni kweli kwamba wazo la biashara ambalo unalijua ...
17/08/2025

Je wajua?,
Si kweli kwamba wazo pekee la biashara ni lile unalolijua tu.
Ni kweli kwamba wazo la biashara ambalo unalijua yaani ushawahi kufanya biashara hiyo ni zuri zaidi ya usiyoyajua lakini si wazo zuri pekee,
Watu wengi huamini na huaminisha wengine kwamba biashara ya kufanya ni ile unayoijua tu na ukifanya biashara usiyoijua utafirisika, jambo ambalo si kweli, kwa kawaida biashara yoyote iwe unaijua ama huijui inakuwa na sababu za kufirisika na sio kuijua na kutoijua pekee ndio sababu,
Ukiwa unataka kufanya biashara kwa wazo la biashara ambalo hujawahi kufanya inawezekana kwa asilimia sawa na ukifanya unayoijua iwapo utafuata taratibu nzuri za kuzuia hasara kwa sababu yoyote ile.
Hivyo tuachane na dhana potofu ya kushindwa kufanya biashara fulani kwa sababu tu huijui, hujawahi kuifanya biashara hiyo badala yake pesa ambayo ilibidi ufanye biashara hiyo inapotea kwenye matumizi mengine.

Mitandao ya Junior MedTech International imebadili jina na nembo (logo), sasa ni InterMedTech Group na nembo mpya k**a i...
11/07/2025

Mitandao ya Junior MedTech International imebadili jina na nembo (logo), sasa ni InterMedTech Group na nembo mpya k**a inavyoonekana kwenye picha.

Je Wajua?.Mama wa Jack Chan aitwae Lee lee Chan alikuwa mfanyabiashara za madawa ya kulevya na k**ali alipokutana na bab...
11/07/2025

Je Wajua?.

Mama wa Jack Chan aitwae Lee lee Chan alikuwa mfanyabiashara za madawa ya kulevya na k**ali alipokutana na baba yake Jack Chan aitwae Charles Chan ambaye alikuwa mpelelezi wa polisi, mzee Charles aliingia kwenye mapenzi na Lee wakati wa majukumu yake ya kumpeleleza kuhusu biashara haramu alizokuwa akifanya Lee.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255768612251

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jua na Junior posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jua na Junior:

Share

Category