Boresha Radio

Boresha Radio Online Platform for Non Mainstream Art and Educational Programs • • Gusa Website boresha.live Sikiliza Boresha Radio

New year, new stories, new sounds. Thank you for being part of our creative journey. Let’s keep inspiring together in 20...
01/01/2026

New year, new stories, new sounds. Thank you for being part of our creative journey. Let’s keep inspiring together in 2026.

Happy Boxing Day to all our amazing followers and valued clients. Thank you for your continued support—wishing you relax...
26/12/2025

Happy Boxing Day to all our amazing followers and valued clients. Thank you for your continued support—wishing you relaxation, joy, and good moments with loved ones.

As we celebrate the birth of Jesus, we join hands with the world in spreading love, peace, and joy. May this season fill...
24/12/2025

As we celebrate the birth of Jesus, we join hands with the world in spreading love, peace, and joy. May this season fill your hearts with cherished moments and abundant blessings. Thank you to all our followers and clients. 🎄✨

Merry Christmas and a Happy New Year!

Tunapoadhimisha miaka 64 ya Uhuru, tuendelee kulijenga taifa letu kwa umoja, amani na bidii.Heri ya Siku ya Uhuru, Watan...
09/12/2025

Tunapoadhimisha miaka 64 ya Uhuru, tuendelee kulijenga taifa letu kwa umoja, amani na bidii.
Heri ya Siku ya Uhuru, Watanzania! 🇹🇿✨

TAARIFA KWA UMMA 🇹🇿Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewasilisha ujumbe wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan k...
08/12/2025

TAARIFA KWA UMMA 🇹🇿
Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amewasilisha ujumbe wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuelekea Desemba 09, 2025 – Maadhimisho ya Miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania 🇹🇿.
Amesema siku hiyo ni ya mapumziko, wananchi wanashauriwa kutulia nyumbani, isipokuwa wale wenye majukumu ya kikazi.

🇹🇿

MCHEZAJI WA LIGI YA ISRAEL AKAMATWA KWA TUHUMA ZA DAWA ZA KULEVYAPolisi wa Israel wametangaza leo Ijumaa kuwa wamefaniki...
05/12/2025

MCHEZAJI WA LIGI YA ISRAEL AKAMATWA KWA TUHUMA ZA DAWA ZA KULEVYA

Polisi wa Israel wametangaza leo Ijumaa kuwa wamefanikiwa kuwak**ata wanandoa wanaoishi Afula, kaskazini mwa nchi, kwa tuhuma za kumiliki na kusambaza dawa za kulevya kali, baada ya uchunguzi wa siri uliofanyika kwa muda.

Cha kushangaza zaidi ni kwamba mmoja wa watuhumiwa ni mchezaji wa mpira wa miguu anayeshiriki Ligi ya Taifa ya Israel, jambo lililozua mjadala mkubwa katika dunia ya michezo.

Watuhumiwa hao walik**atwa Alhamisi usiku baada ya polisi kufanya upekuzi kwenye gari la mchezaji huyo, ambapo walikuta aina mbalimbali za dawa za kulevya zilizokuwa zimepangwa tayari kwa ajili ya kusambazwa. Wakati huohuo, polisi waliokuwa karibu na makazi yao walimk**ata mwanamke wa tatu, aliyekutwa akiondoka ndani ya jengo hilo akiwa na kiasi kikubwa cha dawa mikononi mwake.

Mchezaji huyo na mpenzi wake, wenye umri wa miaka 29 na 34, waliwekwa mahabusu na leo wanatarajiwa kufikishwa katika Mahak**a ya Mwanzo ya Nof HaGalil, ambako polisi wataomba waongezewe muda wa kushikiliwa ili uchunguzi uendelee.

Kwa sasa, maafisa wa usalama wanaendelea kuchunguza mtandao mzima wa biashara hiyo haramu pamoja na nafasi ya kila mtuhumiwa katika mtandao huo.


KENYA YAPOKEA UJUMBE MKUBWA WA IFC 2026Rais William Ruto ametangaza kuwa Kenya itapokea ujumbe wa ngazi ya juu kutoka In...
05/12/2025

KENYA YAPOKEA UJUMBE MKUBWA WA IFC 2026

Rais William Ruto ametangaza kuwa Kenya itapokea ujumbe wa ngazi ya juu kutoka International Finance Corporation (IFC) mapema mwakani, kwa ajili ya kuimarisha ufadhili wa miradi mikubwa ya miundombinu na nishati.

Mazungumzo yatahusisha:
Ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa JKIA
Miradi ya nishati jadidifu (jotoardhi, maji, upepo)
Barabara, bandari na umeme

Ruto amesema hatua hii inaonesha imani ya wawekezaji binafsi katika uchumi wa Kenya.

Rais wa Rwanda, Paul Kagame, amesema kuwa makubaliano ya amani yaliyosainiwa na Rais wa DR Congo, Félix Tshisekedi, yana...
05/12/2025

Rais wa Rwanda, Paul Kagame, amesema kuwa makubaliano ya amani yaliyosainiwa na Rais wa DR Congo, Félix Tshisekedi, yana kila kitu kinachohitajika ili kumaliza kabisa mgogoro wa muda mrefu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Kagame amesema kuwa jukumu la utekelezaji sasa liko mikononi mwa waliotia saini mkataba huo pamoja na viongozi wa Afrika:

“Makubaliano haya yana yote yanayohitajika kumaliza mgogoro huu mara moja na kwa wote. Ikiwa yatashindikana, lawama haitakuwa kwa Rais Trump bali kwetu sisi wenyewe. Ni jukumu letu sisi Waafrika kushirikiana na washirika wetu kujenga, kuimarisha na kupanua amani.”

Ameongeza kuwa njia ya utekelezaji haitakuwa rahisi:

“Kutakuwa na changamoto njiani, kupanda na kushuka.”

🇷🇼 Hata hivyo, amesisitiza dhamira ya Rwanda:

“Lengo letu kuu daima limekuwa kulinda usalama wa nchi yetu baada ya kupitia maumivu mengi. Sasa tunataka kusonga mbele tukiwa na matumaini ya mustakabali salama na wenye ustawi.”

Rais wa Marekani Donald Trump leo Washington DC amekutana na Rais wa DR Congo Félix Tshisekedi pamoja na Rais wa Rwanda ...
04/12/2025

Rais wa Marekani Donald Trump leo Washington DC amekutana na Rais wa DR Congo Félix Tshisekedi pamoja na Rais wa Rwanda Paul Kagame, kwa ajili ya kuidhinisha makubaliano ya amani yanayolenga kumaliza mgogoro wa muda mrefu mashariki mwa RD Congo.

Makubaliano haya yanatarajiwa kuwa suluhisho rasmi la kumaliza vita vya zaidi ya miaka 30, hususan dhidi ya waasi wa M23, ambao wanadaiwa kuungwa mkono na Rwanda.

Hata hivyo, wakati viongozi hawa wakikutana kwa ajili ya amani, mapigano bado yanaendelea katika mkoa wa Kivu yakusini , hali inayozua maswali kuhusu utekelezaji halisi wa makubaliano hayo.

Dunia sasa inatazama kwa karibu kuona k**a mkutano huu wa kihistoria utaleta amani ya kweli au utaishia kuwa makubaliano ya karatasi tu.


Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ametangaza leo uteuzi wa Jenerali Roman Gofman kuwa Mkurugenzi mpya wa Mossad...
04/12/2025

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ametangaza leo uteuzi wa Jenerali Roman Gofman kuwa Mkurugenzi mpya wa Mossad, shirika la ujasusi wa nje la taifa hilo.

Jenerali Gofman, ambaye kwa sasa ni Katibu wa Kijeshi wa Waziri Mkuu, atachukua nafasi ya David Barnea, ambaye anamaliza muda wake wa miaka mitano Juni 2026. Uteuzi huu unatarajiwa kuthibitishwa leo na k**ati maalum ya uteuzi wa viongozi wakuu wa serikali.

Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya Waziri Mkuu, uteuzi wake wakati wa vita umeonesha:
Uwezo mkubwa wa kiutendaji
Ubunifu na ujasiri
Uelewa mpana wa adui
Usiri wa hali ya juu
Uratibu wa karibu na vyombo vyote vya ulinzi na ujasusi, ikiwemo Mossad

Imeelezwa pia kuwa mwanzoni mwa vita, Jenerali Gofman alikimbilia mstari wa mbele Gaza kupambana ana kwa ana na wapiganaji wa Hamas, ambapo alijeruhiwa vibaya.

Netanyahu amesema kuwa Gofman ndiye mtu anayefaa zaidi kuiongoza Mossad, na akamtakia kila la heri katika jukumu hilo muhimu, akisema:
“Mafanikio yake ni mafanikio yetu.”

Leo ni leo! STRONG JOINT inakuletea  fursa ya kipekee ya kufahamu mengi kuhusu tukio lao kubwa la charity, SANAA CHARITY...
04/12/2025

Leo ni leo! STRONG JOINT inakuletea fursa ya kipekee ya kufahamu mengi kuhusu tukio lao kubwa la charity, SANAA CHARITY EVENT 2025 | SEASON07!
Tazama au Sikiliza interview maalum je wawakilishi wa kundi hili la vijana wenye moyo wa kusaidia Watakuletea nini? Maelezo kamili kuhusu maandalizi, malengo ya msimu huu wa 7, na jinsi unavyoweza kushiriki kufanya mabadiliko chanya kwa watoto.
Usisahau kufatili kipindi cha Leo




Host🎙️: Limmy_ip

Guest🗣️: Strong Joint

🎧 Tusikilize kila siku Jumatatu-Ijumaa
🕗 Saa 3:00Pm hadi 5:00Pm
📱Kupitia Online Radio Platforms - Tafuta Boresha Radio

# Season07

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amefutia mashtaka na kumwachia huru mfanyabiashara wa vipodozi Jenifer Jovin (26) maarufu N...
03/12/2025

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) amefutia mashtaka na kumwachia huru mfanyabiashara wa vipodozi Jenifer Jovin (26) maarufu Niffer na Mika Lucas Chavala, waliokuwa na kesi ya uhaini.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Desemba 3, 2025 na Hakimu Mkazi Mkuu, Aaron Lyamuya, baada wakili wa Serikali, Titus Aron kuileleza Mahak**a hiyo kuwa DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa hao wawili.

DPP amewafutia kesi hiyo ya uchunguzi namba 26388/ 2025 chini ya kifungu namba 92(1) cha Sheria ya Makosa ya Jinai, Sura ya 20 ilivyofanya marejeo mwaka 2023.

“Mahak**a inakubaliana na ombi la upande wa Jamhuri k**a lilivyowasilishwa, hivyo inawaachua huru washtakiwa hawa wawili,” amesema Hakimu Lyamuya.

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Boresha Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Boresha Radio:

Share