Boresha Radio

Boresha Radio Online Platform for Non Mainstream Art and Educational Programs • • Gusa Website boresha.live Sikiliza Boresha Radio

09/06/2026

Kijana mdogo mwenye maono makubwa. 🎶

Wakati wengine wanasubiri fursa, Godlove Williams ameamua kuzitengeneza. Kupitia Youth Music Academy, anaendelea kufungua milango kwa vijana wenye ndoto za muziki kwa kuwapa mafunzo, mentorship na jukwaa la kuonyesha vipaji vyao.

Kwa Godlove, muziki si kipaji pekee bali ni taaluma inayohitaji kujifunza, kujituma na kuwekeza kwenye maarifa. Ndiyo maana anaamini kuwa kila kijana mwenye ndoto ana nafasi ya kufanikiwa ikiwa atapata mwongozo sahihi.

YoungVisionary BoreshaRadio

09/06/2026

🎶 Muziki si kipaji pekee, muziki ni taaluma. Unahitaji nidhamu, maarifa, ubunifu na kujifunza kila siku ili kufikia mafanikio. Kipaji kinaweza kukufungulia mlango, lakini taaluma ndiyo inayokufanya ubaki kwenye mchezo. 🎤

09/06/2026

"Unawezaje kuokoka ukiwa bado kijana?" Hilo ndilo swali ambalo wengi walimuuliza Pastor Robijoe alipofanya maamuzi ya kumtumikia Mungu akiwa katika ujana wake.

Katika Kijana Smart Show, anashiriki safari yake, changamoto alizokutana nazo, na kwa nini baadhi ya watu huamini kuwa ujana na wokovu haviendi pamoja.

09/06/2026

Walisema haiwezekani kijana kuokoka na kumtumikia Mungu." Lakini Pastor Robijoe alichagua kusimama kwenye maamuzi yake.
Usikose simulizi yake ya kuvutia kwenye Kijana Smart Show.

09/06/2026

MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI: Maono ya Mzee Mkapa Yanasongeshwa Mbele!

​Katika kuelekea miaka 6 ya kumbukizi ya kifo cha Hayati Benjamin William Mkapa na miaka 20 ya taasisi yake, wawakilishi wa wametushirikisha jinsi wanavyopambana kutokomeza virusi vya UKIMWI (VVU) nchini.

​Kama alivyokuwa Mzee Mkapa—kinara wa kwanza kuweka wazi vita hii kitaifa—taasisi yake leo hii inaendelea kupigana bega kwa bega na jamii kupitia:

Kusogeza Huduma: Kupunguza maambukizi mapya, hasa kwa vijana na makundi maalum maeneo ya pembezoni.

Kuimarisha Mifumo: Kuhakikisha upatikanaji wa dawa (ARVs) na huduma za unasihi na upimaji wa hiari.

Kutokomeza Unyanyapaa: Kuwajengea wananchi uelewa ili kila mtu apate haki na huduma za afya bila ubaguzi.

​Urithi wa Mzee Mkapa hauishii kwenye maneno, unaishi kwa vitendo vya kuokoa maisha!

​ Tanzania StudioInterviews

08/06/2026

Kuelekea kumbukizi ya miaka 6 ya kifo cha Hayati Benjamin Mkapa na miaka 20 ya Taasisi yake, wawakilishi kutoka wamefika studio na kufunguka jinsi wanavyotatua changamoto za vijana kufikia huduma za afya.

​Ukosefu wa rasilimali fedha umekuwa kikwazo kikubwa kwa vijana wengi. Ili kuondoa ukuta huo, Mkapa Foundation inakwenda nao sawa kupitia afua mbili kubwa:

1️⃣ Bima za Afya: Kuhamasisha na kuwashawishi vijana kujiunga na mifuko ya bima ya afya (NHIF na CHF) ili wapate matibabu bila vikwazo vya fedha mfukoni.

2️⃣ Uwezeshaji wa Kiuchumi: Kuwajengea uwezo wa kujitafutia kipato ili wamudu gharama za afya na kujikwamua kimaisha.

​Hivi ndivyo maono ya Mzee Mkapa yanavyoishi—kwa kusikiliza jamii na kuwapa suluhisho endelevu! 🇹🇿

​ UrithiWaMkapa Tanzania

🎙️ LIVE on Boresha Radio!This Sunday kutoka saa 10 jioni hadi 11 jioni, usikose mahojiano maalum na Mch. Robijoe Adriano...
06/06/2026

🎙️ LIVE on Boresha Radio!

This Sunday kutoka saa 10 jioni hadi 11 jioni, usikose mahojiano maalum na Mch. Robijoe Adriano akizungumza kuhusu masuala muhimu ya maisha, imani na maendeleo ya jamii.

📻 Jiunge nasi kupitia Boresha Radio na uwe sehemu ya mazungumzo haya yenye kujenga na kuhamasisha.

RadioTalk DarEsSalaam Tanzania Inspiration CommunityDevelopment

Kuelekea kumbukizi ya miaka 6 tangu kututoka kwa Mwasisi na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa...
06/06/2026

Kuelekea kumbukizi ya miaka 6 tangu kututoka kwa Mwasisi na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, tulikuwa na wenyeji wetu hapa studio kutoka .

​Wawakilishi hawa wametushirikisha namna Taasisi hiyo inavyoendelea kuyaishi maono ya Mzee Mkapa kwa vitendo—hususan kupitia miradi mikubwa ya afya inayotafuta na kunufaisha makundi maalum (wanawake, vijana, na wenye ulemavu) maeneo ya pembezoni.

​Miaka 6 bila yeye, lakini urithi wake wa utumishi bado unagusa mamilioni ya Watanzania. 🇹🇿

​ AfyaKwaWote StudioInterviews

06/06/2026

Miaka 20 ya utumishi uliotukuka na wenye maana kwa Watanzania!

​Kufikisha miaka 20 ya kuendeleza maono ya Hayati Benjamin William Mkapa ni ushahidi wa uongozi thabiti na dhamira ya kugusa maisha. Hadi sasa, tumegusa maisha ya watu milioni 33.2 na kuleta mabadiliko ya kudumu. Hii safari inaendelea!

Address

Mbezi Beach
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Boresha Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Boresha Radio:

Share