Dawasa

Dawasa Karibu katika ukursa rasmi wa Dawasa. Youtube TV Channel
https://youtube.com/channel/UCCVyHKIvUwDFG1tUyWhd7fQ

21/12/2025
18/12/2025

ONGEZEKO LA WINGI WA MAJI MTO RUVU, SASA MAMBO SAFI

Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu imeendelea kufuatilia hali ya na mwenendo wa wingi wa maji katika Mto Ruvu ambapo kwa mujibu wa takwimu zinaonesha kuna Ongezeko kubwa la maji kutokana na mvua zilizonyesha katika maeneo mbalimbali ya mto huo.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Bonde la Wami/Ruvu Bw. Nickson Lutenda alipokuwa katika ukaguzi wa vyanzo vyote vya maji vinavyotiririsha maji yake katika Mto Ruvu na kubainisha ya kuwa kwa sasa hali ya mto Ruvu inazidi kuimarika huku wingi wa maji ukiongezeka na kuendelea kutoa wito kwa watanzania kuendelea kuwa watulivu katika kipindi hichi cha mpito kwani wataalamu wako kazini kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya majisafi na salama inarejea k**a ilivyokuwa awali

13/12/2025

Uimarishaji wa huduma ya kupata maji kwa Ndoo inaendelea kuimarishwa kupitia KIZIMBA CHA MAJI MABWEPANDE katika eneo la BUNJU B- KIHOZILE njia panda ya kwenda Uwanja wa Simba Mo-Arena. Maji yanapatikana, wakazi wa maeneo hayo wanaendelelea kunufaika kwa kupata huduma.

Tunaendelea na jitihada za kuimarisha huduma na kuhakikisha wakazi wa maeneo hayo na ya jirani wanaendelea kunufaika na Kizimba hicho.

Kwa changamoto za huduma tupigie 181 (Bure)

kuimarisha huduma

13/12/2025

Maboresho ya KIZIMBA CHA MAJI katika eneo la WAZO KONTENA yamekamilika na huduma inaendelea kuimarika. Maji yameanza kutoka na wakazi wa maeneo hayo nufaika wameanza kupata huduma.

Tunaendelea na jitihada za kuimarisha huduma na kuhakikisha wakazi wanaohudumiwa na Kizimba hicho wanaendelea kunufaika.

Kwa changamoto za huduma tupigie 181 (Bure)

kuimarisha huduma

11/12/2025

Hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi kutoka katika BUNJU MALOLO imeendelea kuimarika. Maji yameanza kutoka na wakazi wa maeneo nufaika wameanza kupata huduma.

Maeneo yafuatayo yameanza kunufaika;
Kinondo kwa Muha, Kinondo Mwendokasi, Mbopo Loliondo na Kibesa.

Tunaendelea na jitihada za kuimarisha huduma na kuhakikisha maeneo yote yanayohudumiwa na Tanki hilo yananufaika.

Kwa changamoto za huduma tupigie 181 (Bure)

kuimarisha huduma

11/12/2025

Hali ya upatikanaji wa huduma ya majisafi kutoka katika TANKI LA KIMARA imeendelea kuimarika. Maji yameanza kutoka na wakazi wa maeneo nufaika wameanza kupata huduma.

Maeneo yafuatayo yameanza kunufaika;
Kilungule Kampendeza chini, Kilungule B; Kilaba Road, Kilungule Darajani kwa Mgongo Fimbo, Kilungule Kings Street, Msikiti mpya Baruti, Ubungo Kibo; Mizino Street na Kwa Mama Mzungu Baruti.

Tunaendelea na jitihada za kuimarisha huduma na kuhakikisha maeneo yote yanayohudumiwa na Tanki hilo yananufaika.

kuimarisha huduma

10/12/2025

Ndugu wateja ambao leo tumepeleka huduma ya Maji , je mmepata Maji k**a tulivyowatangazia awali? Tunaomba mrejesho ili tuboreshe zaidi

Address

Maji House Building, Ubungo University Road
Dar Es Salaam
P.O.BOX1573

Opening Hours

Monday 07:00 - 18:00
Tuesday 07:00 - 18:00
Wednesday 07:00 - 18:00
Thursday 07:00 - 18:00
Friday 07:00 - 18:00
Saturday 07:00 - 13:00

Telephone

0800110064

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawasa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dawasa:

Share