Dawasa

Dawasa Karibu katika ukursa rasmi wa Dawasa. Youtube TV Channel
https://youtube.com/channel/UCCVyHKIvUwDFG1tUyWhd7fQ

Takribani wakazi 1,200 wa mtaa wa King's, Kata ya Kimara wamehakikishiwa huduma ya majisafi, salama na toshelevu mara ba...
23/10/2025

Takribani wakazi 1,200 wa mtaa wa King's, Kata ya Kimara wamehakikishiwa huduma ya majisafi, salama na toshelevu mara baada ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA), kutekeleza mradi wa uboreshaji huduma katika mtaa huo.

Mradi wa maji mtaa wa King's -Kimara unakwenda kunufaisha wakazi wa maeneo ya King's, Lami Makopo, pamoja na Makaburini maeneo yanayopatikana Kata ya Kimara, Wilayani Ubungo.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa DAWASA Mkoa wa Kihuduma Makongo, Mhandisi Boniphace Philemon amesema umuhimu wa mradi huo kwa wakazi hao na hali ya huduma itakavyokuwa baada ya kukamilika kwake.

"Mtaa huu wa King's ulikuwa unapata maji kwa kiwango kidogo sana na hata kipindi cha mgao muda mwingine maji hayakuwafikia, kukamilika kwake kutafanya wakazi hawa kupata maji kwa siku 5 ndani ya wiki kutoka siku 3 za awali," amesema Mhandisi Boniphace.

Mhandisi Boniphace amesema mradi huu wa maboresho ya huduma unajumuisha uchimbaji na ulazaji wa bomba za inchi 6 na 4 kwa umbali wa Kilomita 2.5 ambapo hadi sasa bomba zimekwishalazwa kwa umbali wa kilomita 1.2 na ifikapo mwanzoni mwa Novemba 2025 mradi huu utakuwa umekamilika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa mtaa wa Kilungule B, Ndugu Hilary Dimoso ameishukuru DAWASA kwakutekeleza mradi huu kwani eneo la Kings na maeneo jirani yalipata changamoto kwa kipindi kirefu.

"Huduma hii kwetu inakwenda kuwa mkombozi, tunafurahishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi kwani wakazi wa hapa walishindwa kufanya shughuli zao za kimaendeleo lakini pia kutumia gharama kubwa kununua maji.

Sasa tumepata tumaini na maeneo yote maji yalipokuwa yanasumbua huduma inakwenda kuimarika," amesema Dimoso.

23/10/2025
Jumla ya wakazi 600 watanufaika na maboresho makubwa ya huduma ya maji mtaa wa Mburahati NHC, kata ya Mburahati, Wilaya ...
23/10/2025

Jumla ya wakazi 600 watanufaika na maboresho makubwa ya huduma ya maji mtaa wa Mburahati NHC, kata ya Mburahati, Wilaya ya Ubungo.

Ni baada ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuanza utekelezaji wa mradi wa maji Mburahati kwa mroso wenye lengo la kuhudumia wakazi wa eneo hilo kutokana na kupata changamoto ya huduma ya maji kwa muda mrefu.

Mradi wa maji Mburahati kwa mroso unaogharimu kiasi cha Shilingi Milioni 5, utahudumia maeneo ya Mburahati NHC, Udzungwa, Tegemeo, Ruaha na Katavi na kuwapatia huduma bora ya majisafi na salama kwa wananchi.

Akizungumza utekelezaji wa mradi huo, Mhandisi wa Miradi mkoa wa kihuduma Magomeni, Mhandisi Bertha Ambangile amesema mradi huo ambao chanzo chake ni kisima cha maji kwa mroso utasaidia kutoa huduma ya majisafi kwa wakazi wa eneo hilo ambao walipata changamoto ya maji kwa muda mrefu.

"Mradi utaenda kusaidia kupunguza changamoto ya maji kwa wakazi wa Mburahati NHC na maeneo mengine ya jirani, chanzo chake ni kutoka kwenye kisima cha maji cha kwa mroso," amesema Mhandisi Ambangile.

Mhandisi Ambangile amesema kazi inayoendelea kwa sasa ni kusambaza bomba za inchi 2 kwa umbali wa mita 300 na ujenzi wa vizimba vitano (5) vya kuchota maji.

Kisima cha maji kwa Mroso kina uwezo wa kuzalisha maji lita za ujazo 15,840 kwa saa 1 na kufika lita 380,160 kwa saa 24 (siku moja).

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mburahati NHC, Ndugu Raphael Mteka ameipongeza DAWASA kwa kutekeleza mradi huu ukizingatia wingi wa wakazi katika eneo hili wana uhitaji wa huduma ya maji.

"Naishukuru sana DAWASA kazi kubwa wanayoifanya ili kuhakikisha wananchi wa eneo hili wanapata huduma ya maji, kwa sasa tuna imani baada ya kuona kasi ya utekelezaji wa mradi huu ambao unakwenda kumaliza kabisa changamoto ya maji hapa mtaani," amesema Ndugu Mteka.

Ndugu Sharifa Kipaumbele, mkazi wa mtaa wa Tegemeo ameishukuru DAWASA kwa kusikia kilio chao cha muda mrefu kwa kukosa maji na sasa wana matumaini ya kupata huduma.

"DAWASA mnatusaidia sana kwa hii changamoto ya maji sasa mnaenda kumtua mama ndoo ya maji kichwani," amesema Ndugu Kipaumbele.

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa Kihuduma Magomeni imeendelea na zoezi l...
17/10/2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa Kihuduma Magomeni imeendelea na zoezi la utoaji wa vifaa vya maunganisho mapya ya huduma ya majisafi kwa wananchi wa maeneo ya Manzese, Tandale hadi Sinza ili waweze kunufaika na jitihada za Serikali za kuhakikisha wamepata huduma ya majisafi.

Akizungumza wakati wa zoezi la ugawaji vifaa vya maunganisho mpya, Mhandisi wa Miradi mkoa wa kihuduma Magomeni, Mhandisi Bertha Ambangile amesema zaidi ya wateja 25 wataanza kunufaika na huduma ya maji mara baada ya kukamilika kwa zoezi la maunganisho.

"Tunaamini wateja 25 waliopokea vifaa vya maunganisho mpya ya maji wataenda kunufaika na huduma hiyo baada ya kuwaunganisha huduma ya majisafi," amesema Mhandisi Ambangile.

Sambamba na zoezi la utoaji wa vifaa hivyo, DAWASA Magomeni imetoa elimu kwa wateja hao wapya kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji, matumizi sahihi ya maji, njia rasmi ya kimawasiliano, malipo ya ankara na huduma nyingine zitolewazo na Mamlaka.

Kwa upande wake, mkazi wa Ubungo NHC, Ndugu Rehema Mwakyambiki ameishukuru DAWASA kwa kufanikisha kuwaunganisha na huduma ya majisafi mara baada ya kupokea vifaa vya maunganisho.

"Naishukuru sana DAWASA kwa hatua hii kubwa kwa kufanikisha kupata vifaa vya maunganisho na sasa tunaenda kuunganishiwa huduma ili tuweze kunufaika na huduma ya majisafi," amesema Ndugu Mwakyambiki.

Zaidi ya wateja wapya 25 wa maeneo ya Manzese, Tandale, Sinza, Magomeni na Kigogo wataanza kunufaika na huduma ya majisafi baada ya kukamilika kwa zoezi la maunganisho.

Mamlaka inawasisitiza wananchi wanaohitaji kuunganishiwa huduma ya majisafi kuwasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 181 (Bila malipo) au 0735 451 862 DAWASA Magomeni.

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imetoa elimu ya umuhimu wa maji na utunzaji miundombinu...
16/10/2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imetoa elimu ya umuhimu wa maji na utunzaji miundombinu ya maji kwa wanafunzi wa klabu ya mazingira shule ya sekondari Kibasila, Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es salaam.

Lengo la elimu hii ilikuwa ni kuwaelemisha wanafunzi umuhimu wa maji na utunzaji wa miundombinu ya maji ili waweze kuwa mabalozi wazuri wa huduma hii muhimu katika jamii.

Akizungumza wakati wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa shule hiyo, Afisa Mawasiliano kutoka DAWASA, Ndugu Prisca Makenya amesema maji ni rasilimali muhimu ambayo inahitajika kwa viumbe hai ikiwepo binadamu, mimea na wanyama, hivyo kuna ulazima wa kuyatunza na kuhakikisha yanalindwa ili yaweze kufaa kwa matumizi ya kila siku.

"Utunzaji miundombinu ya maji ni muhimu kwani unapunguza gharama zinazojitokeza wakati wa uharibifu, unasaidia upatikanaji majisafi na ya uhakika.

Miundombinu ya maji inayotumiwa na DAWASA ni pamoja na mitambo ya uzalishaji na Uzalishaji maji, mabomba, pumpu za kusukuma maji, dira za maji na viungio vyake," amesema Ndugu Makenya.

Ndugu Makenya amesema klabu za mazingira mashuleni zimeanzishwa kwa lengo la kuwajengea vijana uwezo katika masuala ya maji na usafi wa mazingira ili wanafunzi hao wakawe chachu na mabalozi wa mabadiliko kwa jamii wanazotoka.

Wanafunzi wamejifunza njia mbalimbali ovu zinazofanywa na wanachi wasiowaaminifu kwenye miundombinu ya DAWASA ikiwa ni pamoja na kukata mabomba, wizi wa mita za maji, kurudisha usomwaji wa mita nyuma.

Kwa upande wake, Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kibasila, Emmanuel Sedekia ameishukuru Mamlaka kwa kutoa elimu hii muhimu kwa wanafunzi wa shule hiyo inayowajengea uelewa wa namma nzuri ya kutunza miundombinu ya maji na hatua za kuchukua punde wanapoona wananchi wasio waaminifu wanaoharibu miundombinu.

Amewataka wanafunzi waliopatiwa elimu hiyo kuwa mabalozi wazuri wa huduma za maji katika jamii yao.

Mwanafunzi, Mashiri Bozuga aliyepata elimu hiyo, ameishukuru Mamlaka kwa kuwaelimisha na kuwasaidia kujua umuhimu wa utunzaji wa miundombinu ya maji na hatua za kuchukua pindi wanapoona uharibifu unapotokea, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa DAWASA kupitia namba 181 ya huduma kwa wateja.

"Kwa niaba ya wenzangu, tunaahidi tutakuwa mabalozi wazuri kwa jamii kuhakikisha tunalinda miundombinu ya maji kwa manufaa ya vizazi vijavyo," amesema Buzuga.

Klabu ya Mazingira Shule ya Kibasila ni moja ya klabu 11 za mazingira ambazo Mamlaka inazisimamia katika Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani ili kuwajengea uwezo wa kutambua shughuli mbalimbali za Mamlaka kuhusu majisafi na usafi wa mazingira na kwenda kuwa mabalozi wazuri katika jamii.

Viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameendelea na zoezi la ufuatili...
15/10/2025

Viongozi waandamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) wameendelea na zoezi la ufuatiliaji uimarikaji wa huduma ya Maji baada ya maboresho yaliyofanywa katika mfumo wa usambazaji maji.

Katika Wilaya ya Ilala, Mwakilishi wa Afisa Mtendaji Mkuu, Mhandisi Lydia Ndibalema amesema kuwa kwa sasa huduma ya maji inaendelea kuimarika katika maeneo ya *Saranga, Msitu wa Nyuki na Kisungu*, hali iliyokuwa tofauti na hapo awali ambapo kulikuwa na changamoto za upatikanaji wa maji.

“Kwa sasa maji yanapatikana mara kwa mara, tunapokea maoni chanya kutoka kwa wateja wetu, hii ni matokeo ya kazi kubwa inayofanywa na DAWASA kuhakikisha kila kaya inapokea huduma bora. Timu zetu ziko maeneo mbalimbali kuhakikisha huduma inaendelea kuimarika” alisema Mhandisi Ndibalema.

Mwenyekiti wa mtaa wa Saranga, Leonard Mbangile ameipongeza DAWASA kwa kuendesha zoezi la ufuatiliaji wa huduma ya maji pamoja na kupokea maoni ya wateja wao huku akitoa rai kwa DAWASA kuwafikia wateja wengi zaidi

"Zoezi hili ni tumaini kwa wananchi kwani DAWASA wameonesha kujali, kwa sasa huduma inaendelea kuimarika katika maeneo mbalimbali ndani ya mtaa wangu.Nitoe rai DAWASA kufikia wateja wengi zaidi ili kuhakikisha huduma inakuwa bora." amesema ndugu Mbangile

Sehemu ya Watendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imepita katika maeneo ya Buza na...
14/10/2025

Sehemu ya Watendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imepita katika maeneo ya Buza na Vituka kuangalia hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Wameshuhudia uimarikaji wa huduma katika maeneo ya Makaburi ya City, Amani, Lumo, Kwa Gude na Ikizu pamoja na Mtongani kwa eneo la Vituka ambayo awali yalikuwa na changamoto ya huduma.

Akizungumza wakati wa zoezi la ufuatiliaji wa huduma ya maji katika maeneo hayo, Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani DAWASA, CPA (T), Rosemary Lyamuya amesema kwa sasa huduma imerejea na maji yanapatikana muda mrefu na kwa presha kubwa.

"Siku chache zilizopita kulikuwa na changamoto ya maji lakini kwa sasa huduma imeimarishwa na maji yanapatikana na wananchi wanafurahia huduma," amesema Lyamuya.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Sigara, Ndugu Joseph Temba ameishukuru DAWASA kwa jitihada kubwa zinazoendelea kuimarisha huduma ya maji katika eneo lake.

"Hali ya maji imeanza kurudi vizuri. Tulikuwa na changamoto katika siku zilizopita lakini sasa maji yamefika na presha inaridhisha tunawashukuru DAWASA kwa kurejesha huduma hii muhimu," amesema Mwenyekiti Temba.

Kwa upande wa mkazi wa Makaburi ya City, Ndugu Tausi Abdulaziz ameishukuru Mamlaka kwa kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha huduma ya maji wanaipata kwa uhakika kila mara.

Mamlaka inatoa wito kwa wananchi wanaopata changamoto za kihuduma kuwasiliana na DAWASA 181 (Bila Malipo) au 0735 202 121 (WhatsApp tu).

Address

Maji House Building, Ubungo University Road
Dar Es Salaam
P.O.BOX1573

Opening Hours

Monday 07:00 - 18:00
Tuesday 07:00 - 18:00
Wednesday 07:00 - 18:00
Thursday 07:00 - 18:00
Friday 07:00 - 18:00
Saturday 07:00 - 13:00

Telephone

0800110064

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawasa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dawasa:

Share