Dawasa

Dawasa Karibu katika ukursa rasmi wa Dawasa. Youtube TV Channel
https://youtube.com/channel/UCCVyHKIvUwDFG1tUyWhd7fQ

21/07/2025
Ifikapo Mwaka 2050 huduma ya Majisafi na salama kuwafikia Watanzania wote.Dira ya awali (2000-2025) ililenga kuwa watu w...
20/07/2025

Ifikapo Mwaka 2050 huduma ya Majisafi na salama kuwafikia Watanzania wote.

Dira ya awali (2000-2025) ililenga kuwa watu waishio vijijini wanapata Majisafi kutoka asilimia 50 Mwaka 2000 hadi kufikia asilimia 85 Mwaka 2025 na watu waishio mjini wanapata maji kutoka asilimia 50 Mwaka 2000 kufikia asilimia 95 ifikapo Mwaka 2025.

Mpaka Desemba 2022 , 77% ya watu waishio vijijini walipata huduma ya Majisafi na salama na 88% wakazi wa mjini walikuwa wamefikiwa na huduma ya maji.

Serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan upatikanaji wa maji mijini umeongezeka kutoka asilimia 84 hadi asilimia 91.6 na vijijini kutoka asilimia 70.1 hadi asilimia 85

Wakati Rais Samia anaingia madarakani, huduma ya Maji ilikuwa imefika kwa Vijiji 5,258, hadi kufika mwaka 2025 vijiji 10,779 vilikuwa vimefikishiwa huduma ya Maji sawa na ongezeko la vijiji 5,521.

Kutokana na mwenendo huo upatikanaji wa maji unatarajiwa kufikia asilimia 100 ifikapo mwaka 2050.

WAKAZI KIN'GAZI WACHANGAMKIA MAUNGANISHO YA MAJI๐Ÿ“ Kin'gazi A, Dar es SalaamWatendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa ...
16/07/2025

WAKAZI KIN'GAZI WACHANGAMKIA MAUNGANISHO YA MAJI

๐Ÿ“ Kin'gazi A, Dar es Salaam

Watendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya mtaa Kin'gazi A, Kata ya Kwembe, Wilaya ya Ubungo wamegawa vifaa vya maunganisho mapya ya maji kwa wananchi mbalimbali.

Lengo ni kuwezesha wananchi kuunganishwa moja kwa moja na mtandao wa majisafi wa mradi mkubwa wa kimkakati wa Usambazaji Maji Dar es Salaam ya Kusini (Bangulo) ambao umekamilika kwa gharama ya Shilingi 36.9 bilioni.

Vifaa ambavyo vimetolewa ni pamoja na mabomba, koki, dira za maji na vifaa vya usalama vya kuunganisha maji majumbani.

Meneja wa DAWASA โ€“ Kinyerezi, ndugu Roberts Mugabe amesema zoezi hilo linalenga kuhakikisha wananchi wanaanza kupata huduma ya majisafi kwa urahisi na kwa wakati ambapo wateja 130 tayari wamekabidhiwa vifaa vya maunganisho mapya na zoezi la kuunganisha huduma linaendelea.

โ€œMradi huu wa Bangulo umeleta mabadiliko makubwa kwa maeneo ya Kusini mwa Jiji la Dar es Salaam. Tunataka wananchi waanze kuona matokeo chanya kwa vitendo, na ndiyo maana tumeanza kugawa vifaa ili kuharakisha maunganisho ya maji,โ€ amesema ndugu Roberts.

Ndugu Roberts ameongeza zoezi la maunganisho ni endelevu kwani hadi sasa mkoa wa kihuduma umepokea maombi takribani 400 ambapo hadi sasa tayari wateja 130 wamekabidhiwa kwa ajili ya kuunganishwa huku taratibu zikiendelea kwa ajili ya waliobaki na wanaoendelea kuwasilisha maombi.

Kaimu Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kin'gazi A, ndugu James Frank ameishukuru DAWASA na Wizara ya Maji kwa kuwaleta wananchi wake kwenye mstari wa mbele wa maendeleo, akibainisha kuwa maji ni kichocheo kikubwa cha afya na ustawi wa jamii.

"Kwa hili DAWASA inastahili pongezi kwa kusogeza huduma kwa wananchi, nitoe rai kwa wananchi kuendelea kufika ofisini kuomba huduma kwani sisi tuko kwa ajili ya kuwahudimia," ameeleza ndugu James.

Mkazi wa Kin'gazi A, Jolicia Ngowi ameipongeza DAWASA kwa kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumtua mama ndoo kichwani.

"Tumehangaika na changamoto ya upatikanaji wa maji kwa muda mrefu ambapo ilitulazimu kununua maji kwa bei ghali au kuchota sehemu zisizo salama. Niwapongeze DAWASA kwani sasa napata maji baada ya kukamilisha taratibu ndani ya muda mfupi," amesema ndugu Jolicia.

Mradi wa usambazaji maji Dar es Salaam ya kusini (Bangulo) ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati kitaifa inayotekelezwa kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa huduma ya majisafi kwa wananchi. Mradi huu unalenga kunufaisha majimbo matano ya uchaguzi ya Ukonga, Segerea, Ubungo, Ilala na Ubungo ambapo takribani wananchi 450,000 watanufaika na mradi huu.

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa Kihuduma Kawe imetekeleza kazi ya udhib...
15/07/2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa Kihuduma Kawe imetekeleza kazi ya udhibiti wa upotevu wa maji katika eneo la Baraza la Mitihani, Mbezi Juu.

Kazi hii imehusisha kubadilisha kipande cha bomba kilichoathirika katika bomba la usambazaji maji lenye ukubwa wa kipenyo cha inchi 6 katika eneo hilo.

Kukamilika kwa kazi hii kuataimarisha na kurejesha Huduma ya maji kwa wakazi wa Mtaa wa Seni, Mtaa wa Msafiri, Ndumbwi, Baraza la mitihani, Mbezi juu Kati, Vose hotel, Mtaa wa Mgogo, Kanisa la Sabato Twiga street na Power Nyati Udhibiti wa Upotevu wa maji ni moja kati ya vipaumbele muhimu vya Mamlaka katika kuhakikisha inatoa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

๐Ÿ“Dar es Salaam, Matosa Changamoto za upatikanaji wa maji, wizi wa mita, madeni na ulinzi wa miundombinu zimewakutanisha ...
12/07/2025

๐Ÿ“Dar es Salaam, Matosa

Changamoto za upatikanaji wa maji, wizi wa mita, madeni na ulinzi wa miundombinu zimewakutanisha wajumbe wa serikali ya mtaa Matosa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) ili kuzitafutia suluhu.

Uamuzi huo wa DAWASA kupitia Mkoa wa Kihuduma Makongo ni kuitikia wito wa Waziri wa Maji, Jumaa Aweso aliyewataka kuwasikiliza wananchi juu ya kero za maji maeneo mbalimbali na kuzitatua haraha.

Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo, Ndugu Amani Magoma na kuhudhuriwa na maafisa kutoka DAWASA pamoja na wawakilishi wa wananchi.

Lengo kuu la kikao hiki ilikuwa ni kutoa fursa kwa wananchi kupitia wajumbe wao kueleza kero, changamoto na mapendekezo kuhusu huduma ya maji ili kuyapatia suluhisho la pamoja.

Akizungumza katika kikao hicho, Magoma amesema:"Wananchi wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu huduma ya maji, hasa maeneo ambayo hayafikiwi na mtandao wa maji, tnashukuru sana DAWASA kwa kujitokeza kuwasikiliza wananchi wetu pamoja na kuanza kutekeleza mradi wa kusogeza mtandao wa Matosa.โ€

Katika kikao hicho, wajumbe wameeleza kuwepo kwa maeneo kadhaa ambayo bado yanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma ya majisafi huku wakisisitiza umuhimu wa kuhakikisha upatikanaji wa maji unaboreshwa kwa usawa na kwa wakati.

Kwa upande wake, Afisa Huduma kwa Wateja, Ndugu Christopher Sika alisema:"Tumejipanga kuhakikisha kila mteja anapata huduma bora. Tunaendelea kuboresha mifumo yetu ya kupokea taarifa kwa wakati, lakini pia Mamlaka inaendelea na utekeleza wa mradi wa kusogeza huduma kwa wananchi eneo la Matosa, hivyo tuwaondoe shaka wananchi ambao bado hawajafikiwa na huduma.โ€

Masuala ya ulinzi wa miundombinu ya maji yalijitokeza pia, ambapo wananchi wamehimizwa kushirikiana na Mamlaka katika kulinda mabomba, matenki na vifaa vingine vya DAWASA ili kuhakikisha huduma inaendelea bila vikwazo.

Vilevile, kikao kimegusia suala la madeni ya maji, ambapo Mamlaka ilihamasisha wananchi kuhakikisha wanalipa madeni yao kwa wakati ili kuiwezesha mamlaka kuendelea kutoa huduma bora na kuwekeza zaidi katika miundombinu ya maji.

DAWASA imesisitiza kuwa itaendelea kuwa karibu na wananchi kwa kusikiliza na kutatua changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha kila kaya inapata huduma ya majisafi na salama kwa maendeleo ya jamii na afya ya umma.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 07:00 - 18:00
Tuesday 07:00 - 18:00
Wednesday 07:00 - 18:00
Thursday 07:00 - 18:00
Friday 07:00 - 18:00
Saturday 07:00 - 13:00

Telephone

0800110064

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawasa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dawasa:

Share