Dawasa

Dawasa Karibu katika ukursa rasmi wa Dawasa. Youtube TV Channel
https://youtube.com/channel/UCCVyHKIvUwDFG1tUyWhd7fQ

11/05/2026
Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Mathew Kundo amesisitiza juu ya umuhimu wa Wizara ya Maji kushirikiana na Sekta binafsi nc...
10/05/2026

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Mathew Kundo amesisitiza juu ya umuhimu wa Wizara ya Maji kushirikiana na Sekta binafsi nchini kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kufanikisha malengo ya Serikali ya utoaji wa huduma ya majisafi kwa wananchi wote kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030.

Hayo ameyasema wakati wa ufunguzi wa kongamano lililoandaliwa na Kituo cha Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC)lenye lengo la kujadili nafasi ya ubia katika maendeleo ya Sekta ya maji nchini.

Kongamano hilo limeshirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo katika kujadili hali ya uboreshaji wa huduma ya maji ambapo Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)ilikuwa mojawapo ya washiriki katika kongamano hilo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo Mhandisi Kundo amesema ushiriki wa Sekta Binafsi ni muhimu katika kufanikisha malengo ya Wizara ya Maji ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma endelevu ya majisafi na salama.

“Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tayari imeandaa Mkakati wa Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi (Private Sector Investment Strategy) utakaowezesha kuongeza uwekezaji, ubunifu na ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maji nchini,” amesema Mhandisi Kundo.

Ameongeza kuwa ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi utaongeza uwezo wa kifedha na kitaalamu katika kuimarisha huduma kwa wananchi na utasaidia kutekelezwa kwa Dira ya 2050 ambayo inaelekeza kuitumia Sekta Binafsi k**a mhimili wa kuendesha uchumi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Miradi na Uwekezaji, Mhandisi Ramadhan Mtindasi amesema tayari DAWASA imefanya Ubia na Sekta binafsi haswa katika kudhibiti upotevu wa maji, ambapo juhudi hizo zimesaidia kupunguza kiwango cha upotevu wa maji Katika Kanda ya Kinondoni.

“Ni ukweli usiopingika kuwa tunakaribisha wawekezaji katika juhudi zetu za kusambaza Maji pamoja na kudhibiti upotevu wa Maji, tayari tumeshaanza Kwa Kinondoni na sasa tunawakaribisha wawekezaji kwani tayari tunayo miradi ya kimkakati inayohitaji uwekezaji ikiwemo Mradi wa maji Rufiji,” amesema Mhandisi Mtindasi.

Kupitia ushiriki wake katika kongamano hilo, DAWASA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) imekamilisha zoezi la upimaji wa wingi wa maji katika kisima kipya ch...
08/05/2026

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) imekamilisha zoezi la upimaji wa wingi wa maji katika kisima kipya cha Kisukuru eneo la Viwanja vya Benki ambapo kimethibitika kuwa na uwezo wa kuzalisha takribani Lita 144,000 kwa siku.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msimamizi wa mradi Mhandisi Phylemon Ojode amesema upimaji wa kisima hicho umeonesha kisima kina uwezo wa kuzalisha lita 6,000 kwa saa ambazo ni sawa na lita 144,000 za maji kwa siku zitakazotumika kuimarisha nguvu katika maeneo ya Kisukuru, Mianzini na Kihimbwa kwa matumizi ya wananchi pamoja na shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi.

“Tumekamilisha zoezi la majaribio ya pampu ambalo kitaalam ni mahususi kwa ajili ya kupima uwezo wa uzalishaji wa kisima hiki ambacho kwa sasa tumefahamu kina uwezo wa kuzalisha Lita 144,000, zitakazotumika kuimarisha Usambazaji wa Maji kwa wakazi wa Kisukuru, Mianzini na Kihimbwa,” amesema Mhandisi Ojode.

Aidha, Mhandisi Ojode ameeleza kuwa kwa sasa hatua inayoendelea ni kupima ubora wa maji ambapo DAWASA inafanya vipimo zaidi vyenye lengo la kuhakikisha maji hayo yanakuwa salama kwa matumizi ya binadamu.

Mwenyekiti wa Mtaa Kisukuru, Ndugu John Masele ametoa rai kwa DAWASA kuhakikisha inakamilisha taratibu zote kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika na kisima hicho ambacho kitarahisisha utekelezaji wa shughuli zao za kila siku.

Mradi wa uchimbaji kisima hicho ni sehemu ya jitihada za kuboresha huduma ya maji katika maeneo mbalimbali ndani ya eneo la kihuduma la DAWASA, ambapo Serikali imeendelea kuwekeza katika miradi ya maji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya uhakika.

Address

Maji House Building, Ubungo University Road
Dar Es Salaam
P.O.BOX1573

Opening Hours

Monday 07:00 - 18:00
Tuesday 07:00 - 18:00
Wednesday 07:00 - 18:00
Thursday 07:00 - 18:00
Friday 07:00 - 18:00
Saturday 07:00 - 13:00

Telephone

0800110064

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dawasa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share