Jmtz Media

Jmtz Media "Jmmusic Media - Tanzania Media Platform Based on Entertanment News (Music update) and Interviews u Promote your music through my website and wide your market

01/05/2024
HT Yanga 1 - 0 Tabora
01/05/2024

HT Yanga 1 - 0 Tabora

Yanga 1 - 0 Tabora
01/05/2024

Yanga 1 - 0 Tabora

FT Namungo 2 - 2 Simba
30/04/2024

FT Namungo 2 - 2 Simba


Namungo 1 - 2 Simba
30/04/2024

Namungo 1 - 2 Simba


Namungo 1 - 1 Simba
30/04/2024

Namungo 1 - 1 Simba


Numungo 0 - 1 Simba
30/04/2024

Numungo 0 - 1 Simba


Taarifa rasmi kutoka wekundu wa Msimbazi Mabingwa kombe la Muungano
28/04/2024

Taarifa rasmi kutoka wekundu wa Msimbazi Mabingwa kombe la Muungano

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoa...
26/04/2024

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.

Full Time JKT Tanzania 0 - 0 Yanga
24/04/2024

Full Time JKT Tanzania 0 - 0 Yanga

HT Jkt Tanzania 0 - 0 Yanga
24/04/2024

HT Jkt Tanzania 0 - 0 Yanga

“Leo Young Africans SC tumeingia ushirika na Shirika la Ndege la Air Tanzania ambapo tutaitangaza biashara ya  Ushirika ...
24/04/2024

“Leo Young Africans SC tumeingia ushirika na Shirika la Ndege la Air Tanzania ambapo tutaitangaza biashara ya Ushirika huu unahusisha punguzo la bei kwenye safari zetu ambazo tutafanya na shirika hili. Hatuwezi kuona huduma ya Air Tanzania inafanyika bila sisi kuitangaza. Kufanya hivyo ni kuunga mkono juhudi za Serikali yetu” Rais wa Young Africans SC Eng.Hersi Said

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Lazaro Kilahala kuwas...
24/04/2024

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Lazaro Kilahala kuwasilisha majina ya Mameneja wa Kanda na Mikoa wa TEMESA ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi ili waweze kuchukuliwa hatua.

Bashungwa ametoa agizo hilo Aprili 22, 2024 jijini Dodoma kufuatia kupokea malalamiko mara kwa mara kuhusu huduma zinazotolewa na TEMESA ikwemo huduma ya Kivuko cha MV. Tanga Mkoani Tanga ambapo amemuagiza Katibu Mkuu kuingilia kati kubaini changamoto zinazokwamisha kivuko hicho.

“Mambo mengi ya kiutendaji yanaletwa kwa Waziri na Katibu Mkuu wakati Watendaji mpo na tumewaamini kusimamia Taasisi zenu, hasa jambo hili lipo TEMESA. Mtendaji Mkuu k**a kuna mapungufu ya wasaidizi wako bora uje kwa Katibu Mkuu useme huyu atufahi aondoke kuliko kukaa nao maana hatimaye litakuangukia wewe”, amesema Bashungwa.

Bashungwa amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Balozi Mhandisi Aisha Amour kuangalia namna bora ya usimamizi wa TEMESA katika huduma ya vivuko nchini ili kuleta manufaa na uboreshaji wa huduma za usafiri na usafirishaji ziimarike.

Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa bado TEMESA inaendelea kuwa na mikwamo na kutotekeleza majukumu yake kwa uharaka pindi tatizo linapogundulika katika Vivuko na hivyo kupelekea kuzorota kwa huduma hiyo katika baadhi ya maeneo.

Watuhumiwa watatu wamefikishwa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani Pwani jana tarehe 22 Aprili, 2024  wakikabiliwa na...
23/04/2024

Watuhumiwa watatu wamefikishwa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani Pwani jana tarehe 22 Aprili, 2024 wakikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya Methemphetamine Kilogramu 424.84 pamoja na He**in Hydrochloride gramu 158.24 kinyume cha kifungu cha 15 (1) (a) na cha (3) (i) cha Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Sura ya 95 k**a illivyorejewa 2019.

Washtakiwa hao ni Rajabu Kisambwanda (42) mkazi wa Kerege Matumbi, Bakari Said (39) Mkazi wa Kunduchi Mtongani na Hillary Rhite (35) Mkazi wa Kunduchi Sodike.

Wakisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Joyce Mkhoi na Wakili wa Serikali, Agness Ndanzi, alidai mahak**ani hapo kuwa, washtakiwa hao watatu walikutwa wakisafirisha dawa hizo za kulevya mnamo tarehe 10 Aprili, 2024 eneo la Zinga wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani .

Wakili Ndazi aliendelea kuieleza Mahak**a kuwa, katika tukio lingine, tarehe hiyohiyo mshtakiwa Bakari Said (39) Mkazi wa Kunduchi Mtongani alikutwa akisafirisha dawa za kulevya aina ya He**in hydrochloride yenye uzito wa gramu 158.24.

Hata hivyo washtakiwa wote watatu hawakuruhusiwa kujibu chochote kwani Mahak**a hiyo haina Mamlaka ya kisheria kusikiliza shauri hilo na watafikishwa tena mahak**ani kwa ajili ya kutajwa tarehe 7 mwezi Mei, 2024.

Katika tukio lingine, watuhumiwa wengine tisa (9) wamefikishwa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu jana tarehe 22 Aprili, 2024 wakikabiliwa na mashtaka ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya he**in na methamphetamine zenye uzito wa kilogramu 332.

Akisoma mashtaka yao mbele ya mahak**a hiyo, wakili wa serikali Batilda Mushi amewataja washtakiwa hao kuwa ni Ally Ally (28), Bilali Hafidhi (31), Mohamed Hamisi (47), Idrisa Mbona (33), Rashid Rashid (24), Shabenga Shabenga (24), Dunia Mkambilah (52), M***a Hussein (35) na Hamis Omary (25).
Amesema, katika shtaka la kwanza, tarehe 16 Aprili, 2024 karibu na hotel ya white sands wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, washtakiwa walikutwa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Methamphetamine kiasi cha kilgramu 100.83.

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limewahakikishia Watanzania kwamba safari za treni ya umeme zitakapoanza rasmi mwezi July...
23/04/2024

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limewahakikishia Watanzania kwamba safari za treni ya umeme zitakapoanza rasmi mwezi July mwaka huu abiria watatumia saa tatu tu kutoka Dar es salaam hadi Dodoma ambapo jana wakati wa safari ya kwanza ya majaribio treni hiyo imetumia saa nne kutoka Dar hadi Ddooma ambapo iliondoka saa 10 kasoro jioni na kufika Dodoma saa 1 usiku.

Akiongea na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano - TRC, Jamila Mbarouk amesema “Dares salaam hadi Dodoma kwa safari hii ya kwanza ya majaribio tumetumia masaa manne lakini baada majaribio kukamilika tutatembea masaa matatu kwa kuwa tutakuwa na vituo lakini k**a tukitembea one way bila kusimama kwenye vituo tunafika chini ya masaa matatu”

Itakumbukwa safari ya mwisho ya majaribio kutoka Dar es salaam hadi Morogoro treni hiyo ilitumia muda chini ya masaa mawili ambapo Jamila alisema “Safari hii tumetumia muda chini ya masaa mawili, kila siku tunavyoendelea kufanya majaribio ya miundombinu kwa lengo la kuangalia mifumo ya umeme na ufanisi wa uendeshaji umeme, niwahakikishie Watanzania kwamba tutatumia muda uleule tuliowaahidi wa dk 90 Dar - Morogoro na masaa matatu Dar - Ddooma”

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA OPARESHENI ZA ULINZI WA AMANI WA UMO...
23/04/2024

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA OPARESHENI ZA ULINZI WA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Stergomena Lawrence Tax, April 22, 2024 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Idara ya Oparesheni za Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa, Bwana, Jean Pierre Lacroix, katika ofisi ndogo za Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, jijini Dar-es-salaaam

Bwana Jean Lacroix aliyeambatana na Meja Jenerali Cheryl Pearce ambaye ni Naibu Mshauri Mkuu wa Masuala ya Ulinzi wa Amani katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa alimueleza Waziri wa Ulinzi na JKT utayari wa Umoja wa Mataifa kushirikiana na Tanzania na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za Kiusalama na Amani katika maeneo mbalimbali ambayo Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania linashiriki. Bwana Lacroix aliishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake wa kutafuta na kuleta Amani katika sehemu mbalimbali duniani. Mkuu huyo wa idara Ulinzi wa Amani ya Umoja wa Mataifa alimuhakikishia Waziri Tax pamoja na Tanzania kwa ujumla utayari wa Umoja wa Mataifa kuendelea kushirikiana na Tanzania.

Naye Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, alimshukuru Mkuu huyo wa Idara ya Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa kwa kutambua mchango wa Tanzania katika Ulinzi wa Amani duniani na alimhakikisha utayari wa Tanzania kuendelea kushirikiana na Umoja wa Mataifa katika kuhakikisha Amani inapatikana katika maeneo ambayo Umoja wa Mataifa na Tanzania wanashiriki juhudi za kupata Amani ya kudumu.
Viongozi wengine waandamizi toka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa waliokuwa pamoja na Waziri wa Ulinzi na JKT katika mazungumzo hayo ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kijeshi Wizara ya Ulinzi na JKT, Rear Admiral Michael Mumanga, na Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Amani Tanzania, Brigedia Jenerali George Itang’are.

Address

Ubungo
Dar Es Salaam
40204

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jmtz Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jmtz Media:

Share