30/04/2026
Mchambuzi wa soka nchini, Jemedari Said, amemshushia rungu mwamuzi wa kati, Dickens Mimisa Nyagrowa, kufuatia uchezeshaji wake katika mchezo wa dabi ya Muungano uliopigwa visiwani Zanzibar.
Jemedari ameeleza kutoridhishwa kwake na kiwango cha mwamuzi huyo, akidai kuwa ameshindwa kusimamia sheria za mchezo kwa ujasiri na badala yake amechezesha kwa "uoga wa lawama." Kwa mujibu wa Jemedari, licha ya nia njema ya ZFF, Dickens Mimisa ameonekana kuwa "kawaida sana" na ameshindwa hata kutoa kadi za njano kwenye madhambi ya wazi, jambo ambalo amedai ni kuwadhalilisha waamuzi wengine ambao wangeweza kufanya kazi bora zaidi.
βKatika ukosoaji wake huo mzito kupitia ukurasa wake wa kijamii, Jemedari Said aliandika:
β"Nia ya ZFF kumleta ilikuwa njema kabisa, lakini huyu Refa wa MUONGO hana lolote, tena 'TAPELI' kabisa. Muoga wa lawama k**a vile kwao ni Mikindani Mtwara, faulu nyingi sana ameogopa kutoa hata kadi za njano. Kwa uchezeshaji huu waamuzi wetu tumewadharau bure kabisa, binafsi sina cha kumpongeza kwa 90 minutes."
βYapi maoni yako?
Follow the BONGO SOURCE channel on WhatsApp:
ππ https://whatsapp.com/channel/0029Vb6u2Xu7tkjHaNMwcQ44