25/07/2025
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa ufafanuzi kuhusu uamuzi wa kufanya mkutano mkuu wa dharura kwa njia ya mtandao, baada ya kuibuka maswali juu ya uhalali wa hatua hiyo kikatiba.
Makalla amezungumza hayo na waandishi wa habari leo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Ndugu Amos Makalla, amesema kuwa hatua hiyo imezingatia kikamilifu masharti ya Katiba ya chama hicho, ambayo inaruhusu matumizi ya mifumo ya kidijitali katika uendeshaji wa mikutano.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mkutano huo unatarajiwa kufanyika kesho, Julai 26, 2025, kuanzia saa 4:00 asubuhi. Utaunganisha viongozi wakuu na wajumbe kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar kupitia mfumo wa mtandao, ambapo ajenda kuu itakuwa kujadili na kupitisha mabadiliko ya Katiba ya chama.
Hatua hii ya CCM inatajwa k**a mojawapo ya maboresho katika matumizi ya teknolojia kuhakikisha uwazi, ushirikishwaji, na ufanisi katika shughuli za chama.
Gusa link hii kujiunga nasi katika group letu upate taarifa mbalimbali...
👇👇👇👇👇👇👇👇👇
https://chat.whatsapp.com/ByXMhbek7M8AZlz9sTpVte