Njaro Media

Njaro Media Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Njaro Media, Media/News Company, S. L. P 2528, Dodoma.

Main Official page for | | Based on Sport | Entertainment

NJARO TV
WakaliwaUpdates
Tunazungumza Michezo na Burudani

SUBSCRIBE YOUTUBE YA NJARO MEDIA

06/09/2025

Msanii maarufu wa filamu, Rose Ndauka, amethibitisha kupitia ukurasa wake wa Instagram kwamba yeye na familia yake wamepata ajali ya gari.

Kupitia ujumbe wake, Rose Ndauka ameeleza kuwa licha ya tukio hilo, wote wako salama na amemshukuru Mungu kwa ulinzi wake. Pia amewashukuru mashabiki wake kwa maombi na upendo wao katika kipindi hiki kigumu.

Hata hivyo, hajafafanua chanzo cha ajali wala eneo ilipotokea, lakini amesisitiza kuwa hali yao ni shwari.


06/09/2025

Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, amemtaka kiongozi wa Urusi, Vladimir Putin, kufika Kyiv kwa mazungumzo ya kumaliza vita vinavyoendelea kati ya mataifa hayo mawili. Kauli hii imekuja baada ya Putin kupendekeza mkutano ufanyike Moscow, pendekezo ambalo Zelensky amelipinga vikali.

Katika mahojiano na ABC News, Zelensky alisema hawezi kukubali mwaliko wa kwenda Moscow wakati taifa lake linaendelea kushambuliwa na makombora ya Urusi kila siku.

> “Siwezi kwenda katika mji mkuu wa gaidi wakati nchi yangu inapigwa makombora. Ikiwa anataka mazungumzo, aje Kyiv,” alisema Zelensky.

Kwa upande wake, Putin kupitia hotuba yake katika Kongamano la Kiuchumi la Mashariki mjini Vladivostok, alisema hana mpango wa kusafiri kwenda Ukraine, lakini yuko tayari kukutana na Zelensky huko Moscow chini ya masharti ya usalama yatakayoandaliwa na Urusi.

Hata hivyo, wachambuzi wa kimataifa wameeleza kuwa mwaliko huo wa Putin unaweza kuwa ni mkakati wa kisiasa wa kumshawishi Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye amekuwa akisisitiza viongozi hao wawili wakae meza moja ili kumaliza vita.

Hali hii inaonyesha kuwa matumaini ya kufanyika kwa mazungumzo ya amani bado yako mashakani, huku vita vikiendelea kuvuruga maisha ya raia wa Ukraine na kuzua taharuki katika jamii ya kimataifa.


06/09/2025

Jeshi la Israel leo (Jumamosi) limeeleza kuwa wakaazi wa Jiji la Gaza wanapaswa kuondoka na kuelekea maeneo ya kusini, huku vikosi vyake vikiendeleza mashambulizi katika sehemu kubwa ya mji huo.

Taarifa ya msemaji wa jeshi hilo, Avichay Adraee, imetolewa kupitia mtandao wa X (zamani Twitter) ikiwataka wakaazi hao kuelekea Khan Younis, eneo la pwani lililoko kusini mwa Gaza, na kuwahakikishia kuwa watapatiwa huduma muhimu k**a chakula, makazi na matibabu.

Jeshi la Israel limedai kuwa kwa sasa linadhibiti karibu asilimia 75 ya Gaza, huku likiendelea na operesheni katika vitongoji vya mji wa Gaza ambavyo vimekuwa uwanja wa mapigano makali kwa wiki kadhaa. Siku ya Alhamisi, jeshi hilo lilitangaza kuwa linamiliki takribani nusu ya jiji hilo.

Hata hivyo, baadhi ya wakaazi wameripotiwa kukataa kuhamishwa, wakisema wamechoshwa na mizunguko ya kuhamia sehemu moja hadi nyingine tangu vita vilipoanza.

Taarifa kutoka mamlaka ya afya ya Gaza zinaeleza kuwa zaidi ya watu 64,000 wamepoteza maisha tangu mapigano hayo kuanza, huku maeneo makubwa ya Gaza yakiwa yameharibiwa vibaya na wakaazi wake wakikabiliana na hali ngumu ya kibinadamu.

Wakati huo huo, hatua ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuidhinisha operesheni ya kuteka mji wa Gaza kinyume na mapendekezo ya baadhi ya mak**anda wa kijeshi, imeendelea kuongeza mvutano na kuiacha Israel ikikabiliwa na upinzani wa kidiplomasia kutoka kwa baadhi ya washirika wake wa karibu.


06/09/2025

Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watu 18, akiwemo Katibu wa Uenezi wa Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Taifa, Felius Festo Kinimi, kwa madai ya kukusanyika kinyume cha sheria na kupanga vurugu.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ya Jeshi la Polisi iliyotolewa leo, Septemba 6, 2025, tukio hilo lilitokea eneo la Sambarai, Kibosho, wilayani Moshi. Polisi wamesema kuwa watuhumiwa hao walikuwa wakifuatiliwa kwa muda, na ushahidi dhidi yao umeanza kukusanywa. Baada ya mahojiano, hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa.

Vilevile, Jeshi la Polisi limetoa onyo kali kwa watu au makundi yanayopanga njama za kuchochea vurugu na kuhatarisha amani ya nchi, hasa kipindi hiki ambacho taifa linakaribia Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Kwa upande wa CHADEMA, chama hicho kimethibitisha kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa Katibu Mwenezi wa BAVICHA na wenzake walizuiwa na Polisi wakiwa njiani kuelekea Kibosho kwa ajili ya kumtembelea bibi wa Deusdedith Soka, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Mashujaa ya chama hicho, yanayotarajiwa kufikia kilele chake kesho Septemba 7, 2025.


06/09/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa tukio la kupatwa kwa Mwezi litatokea kesho, Jumapili tarehe 7 Septemba 2025. Hili ni tukio adimu ambapo Dunia inapita kati ya Jua na Mwezi, na kivuli chake kufunika uso wa Mwezi, hali ambayo hutokea pale sayari hizi tatu zinapolingana katika mstari mmoja.

Kwa mujibu wa TMA, tukio hili litakuwa la kupatwa kwa Mwezi kwa sehemu na kikamilifu na litaonekana katika mabara ya Ulaya, Asia, Australia na sehemu kubwa ya Afrika. Tanzania pia itashuhudia tukio hili kuanzia jioni baada ya jua kuzama.

Ratiba ya tukio kwa saa za Tanzania ni k**a ifuatavyo:

Kupatwa kwa sehemu: Kuanzia saa jioni hadi saa 2:29 usiku.

Kupatwa kikamilifu: Saa 2:30 usiku hadi saa 3:52 usiku.

Kupatwa sehemu tena: Saa 3:53 usiku hadi saa 5:55 usiku.

Kwa ujumla, tukio hili litadumu kwa takribani masaa sita.

Wataalamu wa hali ya hewa wanasema kuwa tukio hili lina uhusiano wa moja kwa moja na mzunguko wa mwezi ambao huathiri hali ya kupwa na kujaa kwa maji baharini. Ingawa kutakuwa na ongezeko la kina cha maji, hakuna athari kubwa zinazotarajiwa.

Hali ya hewa inatarajiwa kuwa na mawingu kiasi, jambo linalotoa nafasi nzuri kwa wananchi kushuhudia tukio hili kwa macho bila kifaa maalumu.

Njaro TV itakuletea taarifa zote za moja kwa moja kuhusu tukio hili.


05/09/2025

Mtag mchuchu wako hapa


05/09/2025

Hili goma la unalipa asilimia ngapi?


05/09/2025

Utani wa na 😁😄😄


05/09/2025

Hii hapa nyingine ya na Ishu ya BONGE LA DADA NA TID kwenye Show ya Mbosso iliyofanyika 💥💥 | ISHU YA DIAMOND KUWAAMBIA WATU WAFANYE KAZI

katema cheche nyingine nyingi sana 😄😄😄

Kaa karibu na YouTube ya . Muda wowote tutawawekea hii!

SUBSCRIBE | TURN ON NOTIFICATION ili usiikose hii


05/09/2025

Mwanasoka nyota wa Brazil, Neymar Jr, amejikuta kwenye tukio lisilo la kawaida baada ya tajiri mmoja kijana kuamua kumtaja k**a mrithi wa mali zake.

Bilionea huyo, mwenye umri wa miaka 31 na ambaye bado hajatajwa hadharani, ameandika rasmi kuwa anataka Neymar awe warithi wake wa mali zinazokadiriwa kufikia zaidi ya Dola za Kimarekani bilioni moja (sawa na takribani shilingi trilioni 2.5 za Kitanzania).

Kwa mujibu wa taarifa, sababu kubwa iliyomfanya bilionea huyo kumchagua Neymar ni msimamo wake wa kimaisha na upendo wa dhati kwa baba yake mzazi. Tajiri huyo alisema kitendo cha Neymar kuthamini na kumjali baba yake kinamkumbusha uhusiano aliokuwa nao na marehemu baba yake.

Inadaiwa pia kuwa bilionea huyo hana mke wala watoto, jambo lililochangia uamuzi wake wa kumchagua Neymar k**a mrithi.


05/09/2025

MRITHI WA DIAMOND NAYEYE ANASISITIZA WATU WAFANYE KAZI.

Anaungana na kauli za


Msanii wa muziki wa  bongofleva  ambaye kwa sasa anatamba na Extended Playlist (EP) ya   amefanikiwa kufikisha jumla ya ...
05/09/2025

Msanii wa muziki wa bongofleva ambaye kwa sasa anatamba na Extended Playlist (EP) ya amefanikiwa kufikisha jumla ya streams milioni 100 kwenye mtandao wa

anakuwa ni msanii wa 5 kwa Afrika nzima kufikisha streams 100M kwenye mtandao wa

Wasanii wengine wenye streams zaidi ya 100m streams ni k**a ;

Asake kutoka Nigeria ana Zaidi ya 2 bilioni
Seyi Vibez kutoka Nigeria ana Karibu 1.9 bilioni
Burna Boy kutoka Nigeria ana Karibu 1.5 bilioni
Omah Lay kutoka Nigeria ana Zaidi ya 1 bilioni

Hongera Sana Mshedede kutoka Tanzania 🇹🇿


Address

S. L. P 2528
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njaro Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njaro Media:

Share