Njaro Media

Njaro Media Ukurasa Rasmi wa kutoka Tanzania. Kwa habari za ukweli kuhusu
Jamii | Serikali | Siasa | Michezo | Burudani | Uchumi
!

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa China inataka Mlango wa Bahari wa Hormuz ubaki wazi kutokana na umuhimu wake ...
15/05/2026

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa China inataka Mlango wa Bahari wa Hormuz ubaki wazi kutokana na umuhimu wake katika usafirishaji wa mafuta duniani.

Trump amesema China inanunua kiasi kikubwa cha mafuta kupitia eneo hilo, hivyo ina maslahi ya kuona shughuli za usafirishaji zikiendelea bila vikwazo. Aidha, amedai kuwa Rais wa China Xi Jinping ameonyesha utayari wa kusaidia kufanikisha makubaliano ya kuhakikisha mlango huo unaendelea kuwa wazi.

“Yeyote anayenunua kiasi hicho cha mafuta ana uhusiano fulani nao, lakini alisema angependa kusaidia endapo ataweza,” amesema Trump akizungumzia msimamo wa China kuhusu eneo hilo muhimu la biashara ya mafuta.

Trump pia amesisitiza kuwa Marekani na China zina mtazamo unaofanana kuhusu suala la Iran na umuhimu wa kulinda utulivu katika eneo la Ghuba.


Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji Mchungaji wa Kanisa la Habari Njema, Kasese Gervas Bi...
14/05/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji Mchungaji wa Kanisa la Habari Njema, Kasese Gervas Bilalo (47), kwa tuhuma za kumuua mke wake, Martha Faustine (45).

Tukio hilo limebainika Mei 12, 2026 majira ya saa 6:00 mchana katika Kijiji cha Nyarututu, Kata ya Bwanga, Wilaya ya Chato mkoani Geita, ambapo marehemu alikutwa amefariki ndani ya nyumba yao katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi limebaini kuwa yalitengenezwa ili yaonekane k**a tukio la kujinyonga.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, mtuhumiwa anadaiwa kumvizia mkewe akiwa amelala kisha kumkaba shingoni kwa kutumia kamba ya katani kabla ya kumning’iniza juu ya kenchi ili kuficha ukweli wa tukio hilo.

Taarifa zinaeleza kuwa chanzo cha tukio hilo ni migogoro ya kifamilia iliyotokana na marehemu kumtuhumu mumewe kuwa na mahusiano ya nje ya ndoa yao, hali iliyokuwa ikisababisha ugomvi wa mara kwa mara ndani ya familia hiyo.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato kwa ajili ya uchunguzi zaidi, huku taratibu za kisheria zikiendelea ili mtuhumiwa afikishwe mahak**ani..


Fulltime
14/05/2026

Fulltime

Tanzania na Kenya zimekubaliana kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya njia za umeme zinazounganisha gridi za n...
14/05/2026

Tanzania na Kenya zimekubaliana kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya njia za umeme zinazounganisha gridi za nchi hizo mbili pamoja na kuboresha mifumo ya usafirishaji wa umeme ili kuimarisha usalama wa nishati, kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme na kukuza biashara ya umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughulikia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Mafuta wa Kenya, Bw. Alex Wachira, jijini Nairobi nchini Kenya.

Mazungumzo hayo yalijikita katika kuimarisha ushirikiano katika sekta ndogo ya umeme na nishati jadidifu, hususan biashara ya umeme, utekelezaji wa miradi ya uunganishaji wa gridi za umeme pamoja na maboresho ya mifumo ya usafirishaji na usambazaji wa umeme kati ya Tanzania na Kenya.

Viongozi hao pia walijadili hatua mbalimbali za kuimarisha biashara ya umeme katika ukanda wa Afrika Mashariki kupitia Umoja wa Soko la Pamoja la Kuuziana Umeme na Kuimarisha Mifumo ya Gridi (EAPP).

Aidha, makatibu wakuu hao wamesisitiza umuhimu wa kuongeza wigo wa njia za usafirishaji wa umeme zitakazounganisha nchi hizo mbili kupitia maeneo ya Namanga, Lungalunga, Loitoktok pamoja na Isibania/Sirari.


Mashabiki wa hip hop na utamaduni wa sneaker wamepokea habari kubwa baada ya kuthibitishwa kuwa kampuni ya Reebok pamoja...
14/05/2026

Mashabiki wa hip hop na utamaduni wa sneaker wamepokea habari kubwa baada ya kuthibitishwa kuwa kampuni ya Reebok pamoja na rapa 50 Cent wanatarajia kurudisha rasmi viatu maarufu vya G-Unit mwaka huu, zaidi ya miaka 20 tangu vilipotikisa dunia ya fashion na muziki.

Taarifa hizo zilianza kusambaa baada ya mwanachama wa G-Unit, Tony Yayo kuthibitisha kurejea kwa sneakers hizo kupitia podcast ya The Real Report. Baadaye, vyombo mbalimbali vya sneaker culture vilieleza kuwa Reebok tayari imeanza maandalizi ya kuzindua tena viatu hivyo ndani ya mwaka 2026.

Viatu vya G-Unit vilianza kutolewa mwaka 2003 wakati 50 Cent akiwa kileleni mwa mafanikio yake kupitia album yake maarufu Get Rich or Die Tryin'. Ushirikiano huo uliifanya G-Unit kuwa moja ya brand kubwa zaidi ndani ya sneaker culture ya hip hop, huku Reebok ikivuna mafanikio makubwa ya mauzo kutokana na ushawishi wa 50 Cent kwenye muziki na mitaani.

Ripoti za Sneaker News zinaeleza kuwa viatu hivyo vinatarajiwa kurejea mwezi Julai mwaka huu, ingawa Reebok bado haijatoa tarehe rasmi ya uzinduzi wala picha kamili za collection mpya.

Wadau wengi wa fashion wanaamini kurejea kwa G-Unit sneakers kunachochewa na kurudi kwa trend za miaka ya 2000 ambazo zimeanza kutawala tena kwenye muziki, mavazi na lifestyle ya kizazi cha sasa.

Kwa mashabiki wengi wa hip hop wa miaka ya 2000, kurejea kwa sneakers hizo kunaonekana k**a kurudi kwa enzi ya dhahabu ya muziki wa rap na fashion ya streetwear iliyotawala kipindi hicho.


14/05/2026

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA amezitaka taasisi za elimu nchini kutowazuia wanafunzi kufanya mitihani kwa sababu ya kushindwa kulipa ada za masomo.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kuongeza fedha za mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu pamoja na vyuo vya kati ili wanafunzi wengi zaidi waweze kunufaika na mikopo hiyo.

Dkt. Mwigulu ameyasema hayo leo Alhamisi Mei 14, 2026, Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Latifa Khamis Juwakali, ambaye alitaka kujua mkakati wa Serikali kuhusu wanafunzi wanaozuiwa kufanya mitihani kutokana na kutolipa ada.


Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema kuwa waasi wa M23 kwa kushirikiana na Jeshi la Rwanda...
14/05/2026

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema kuwa waasi wa M23 kwa kushirikiana na Jeshi la Rwanda walifanya mauaji, unyanyasaji wa kingono pamoja na utekaji nyara dhidi ya raia katika mji wa Uvira, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwishoni mwa mwaka 2025 na mwanzoni mwa 2026.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, raia 53 wakiwemo watoto sita waliuawa ndani ya kipindi cha mwezi mmoja ambao waasi hao walikuwa wakidhibiti eneo hilo. Uchunguzi wa shirika hilo umejumuisha ushuhuda wa manusura waliodai kuwaona wanajeshi waliovalia sare za Rwanda wakifanya ukatili dhidi ya raia.

Wachunguzi pia walibaini uwepo wa makaburi matatu ya halaiki huku visa vya watu kutoweka na ukatili wa kingono vikidaiwa kuongezeka katika kipindi hicho.

Maelfu ya wakazi walilazimika kukimbia Uvira baada ya M23 kuuteka mji huo. Waasi hao baadaye waliondoka kufuatia shinikizo la kidiplomasia kutoka mataifa ya Magharibi ikiwemo Marekani lililosaidia kufanikisha makubaliano ya amani.

Hata hivyo, licha ya makubaliano hayo, M23 bado inaendelea kudhibiti baadhi ya maeneo mashariki mwa Congo huku mapigano yakiendelea katika maeneo mbalimbali.


Fulltime
13/05/2026

Fulltime



13/05/2026

: SIMULIZI YA KUIBIWA CAMERA NA SIMU KISA KAZI ALIYOIPATA DAR ES SALAAM. -

Kocha raia wa Ureno, Jose Mourinho yuko katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kurejea kuinoa Real Madrid, miaka 13 baa...
13/05/2026

Kocha raia wa Ureno, Jose Mourinho yuko katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kurejea kuinoa Real Madrid, miaka 13 baada ya kuondoka kwake katika dimba la Santiago Bernabéu Stadium.

Mourinho mwenye umri wa miaka 63 ametajwa kuwa chaguo kuu la klabu hiyo kwa nafasi ya ukocha, huku akiwa mgombea pekee ambaye kwa sasa anaendelea na mazungumzo rasmi na uongozi wa Real Madrid.

Iwapo makubaliano yatafikiwa, Mourinho atamrithi Álvaro Arbeloa ambaye alichukua mikoba ya ukocha mwezi Januari baada ya kuondoka kwa Xabi Alonso.

Ripoti zinaeleza kuwa Rais wa Real Madrid, Florentino Pérez alianza kufikiria uwezekano wa Mourinho kurejea siku mbili baada ya kuondoka kwa Xabi Alonso, kupitia mawasiliano ya awali na wawakilishi wa kocha huyo wa Ureno.


Address

S. L. P 2528
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njaro Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njaro Media:

Share