15/05/2026
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa China inataka Mlango wa Bahari wa Hormuz ubaki wazi kutokana na umuhimu wake katika usafirishaji wa mafuta duniani.
Trump amesema China inanunua kiasi kikubwa cha mafuta kupitia eneo hilo, hivyo ina maslahi ya kuona shughuli za usafirishaji zikiendelea bila vikwazo. Aidha, amedai kuwa Rais wa China Xi Jinping ameonyesha utayari wa kusaidia kufanikisha makubaliano ya kuhakikisha mlango huo unaendelea kuwa wazi.
“Yeyote anayenunua kiasi hicho cha mafuta ana uhusiano fulani nao, lakini alisema angependa kusaidia endapo ataweza,” amesema Trump akizungumzia msimamo wa China kuhusu eneo hilo muhimu la biashara ya mafuta.
Trump pia amesisitiza kuwa Marekani na China zina mtazamo unaofanana kuhusu suala la Iran na umuhimu wa kulinda utulivu katika eneo la Ghuba.