Njaro Media

Njaro Media Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Njaro Media, Media/News Company, S. L. P 2528, Dodoma.

Main Official page for | | Based on Sport | Entertainment

NJARO TV
WakaliwaUpdates
Tunazungumza Michezo na Burudani

SUBSCRIBE YOUTUBE YA NJARO MEDIA

12/11/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu 38 raia wa Ethiopia, wote wakiwa wanaume, kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Benjamini Kuzaga, watuhumiwa hao walik**atwa Novemba 11, 2025, katika pori la ranchi ya Matebete lililopo kijiji cha Igumbilo Shamba, Kata ya Chimala, Wilaya ya Mbarali.

Watuhumiwa hao walikuwa wakisafiri kwa gari aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T.953 DJF, mali ya Stanslaus Mazengo, ambaye ndiye anayetajwa kuwaongoza.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Mazengo alikiri kuwa alikuwa akiwapeleka wahamiaji hao kufichwa katika nyumba ya Jackline Malya, mkazi wa Chimala, kwa lengo la kuwaandalia safari ya kwenda Afrika Kusini kwa njia za kificho.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limewataka wananchi kuacha tamaa ya fedha na kuepuka kushiriki vitendo vya kuwawezesha raia wa kigeni kuingia au kupita nchini kinyume cha sheria, na badala yake wawashauri kufuata taratibu rasmi kupitia mamlaka husika ili kuepuka hatua kali za kisheria.


12/11/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, ameitaka Mahak**a kumaliza kwa haraka kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, akisema kwamba Lissu amekaa mahabusu kwa muda mrefu wa zaidi ya miezi saba bila kesi yake kumalizika.

Aidha, Heche alibainisha kuwa CHADEMA imetuma mawakili wake kote nchini kwa ajili ya kutoa msaada wa kisheria kwa wanachama na wananchi waliok**atwa katika kipindi cha uchaguzi kutokana na kesi mbalimbali .

Alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za chama hicho kuhakikisha kila mwananchi anapata haki ya kisheria bila ubaguzi.


12/11/2025

Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, imeahirishwa hadi pale Msajili wa Mahak**a Kuu atakapoweka ratiba mpya ya uendeshaji wake, baada ya maombi mapya kuwasilishwa mahak**ani.

Lissu aliwasilisha hoja mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Dunstan Ndunguru, akipinga matumizi ya chumba maalum cha mashahidi waliolindwa (protected witnesses), akidai chumba hicho hakizingatii masharti ya kisheria.

Kwa mujibu wa hoja zake, Lissu alieleza kuwa hakuna agizo lolote la mahak**a linalomtaka shahidi kulala au kufichwa ndani ya "kiboksi", na kwamba mashahidi waliopewa ulinzi wanapaswa kutoa ushahidi wao ndani ya kizimba cha kawaida, sehemu ambayo Jaji pekee anaweza kuwaona.

Lissu alifafanua kuwa mfumo uliopo sasa unampa Jaji ugumu wa kumwona shahidi wakati kesi ikiendelea, hali ambayo anaamini inavuruga uwazi wa mwenendo wa mashauri. Aliongeza kuwa sheria inayotumika kulinda mashahidi haina nguvu kisheria kwa sababu haijachapishwa kwenye gazeti la serikali k**a inavyotakiwa na utaratibu wa kisheria.

Aidha, Lissu aliikumbusha mahak**a juu ya agizo lililowahi kutolewa na Jaji Mtembwa, likitaka majaji wanaosimamia kesi zinazohusu mashahidi wa siri kupewa majina ya mashahidi hao kabla ya usikilizaji kuanza. Alisema jambo hilo halikufanyika katika kesi yake, jambo analodai linaweka upande wa Jamhuri katika nafasi ya kujua mashahidi pekee.

Hoja nyingine aliyowasilisha ni kwamba iwapo upande wa Jamhuri ungehitaji kutumia kizimba maalum kwa mashahidi waliolindwa, ulipaswa kuomba kibali rasmi cha mahak**a, jambo ambalo halikufanyika.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Wakili wa Serikali Mkuu Nassoro Katuga aliomba muda zaidi wa kuandaa majibu ya kina kwa hoja zilizowasilishwa na upande wa utetezi, akibainisha kuwa hoja hizo zinahitaji majibu ya kisheria na utafiti wa kina.

Baada ya maombi hayo, jopo la majaji liliahirisha kesi hiyo hadi Msajili wa Mahak**a atakapopanga tarehe mpya ya kuendelea na usikilizaji.


12/11/2025

Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amekabidhiwa rasmi wadhifa wa Waziri Mkuu baada ya kuteuliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na kisha kula kiapo cha uaminifu na uzalendo mbele ya Spika wa Bunge, Mhe. M***a Zungu. Katika kiapo chake, Dkt. Gwajima ameahidi kutoa huduma bora kwa taifa na kuhakikisha masilahi ya wananchi yanatimizwa.

Tangu kuanza kazi yake ya ubunge mwaka 2020, Dkt. Gwajima amehudumu katika wizara muhimu za maendeleo ya jamii. Awali aliiongoza Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (2020–2022), kisha akaendelea katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum (2022–2025). Uzoefu huu wa kina katika nyanja za kijamii unamuwezesha kuiongoza serikali kwa ufanisi katika wadhifa wake mpya.


12/11/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Zungu, ameitaja kesho Alhamisi kuwa siku muhimu ambapo kikao cha tatu cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge kitafanyika. Kikao hiki ni muhimu kwa sababu kitahusisha:

1. Kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu

2. Uchaguzi na kiapo cha Naibu Spika

Spika Zungu amewaagiza wabunge wote kuwepo mapema, saa tatu kasoro dakika 10, na kila mmoja awe kwenye kiti chake tayari kwa shughuli za kikao.

Hii ni hatua ya kihistoria katika mchakato wa utendaji wa Bunge, kwani uteuzi wa Waziri Mkuu na kiapo cha Naibu Spika ni msingi wa uongozi wa Bunge na serikali.


12/11/2025

Klabu ya Rayon Sports FC kutoka Rwanda imeorodheshwa miongoni mwa zaidi ya vilabu 150 vya Afrika vilivyofungiwa kufanya usajili kwa madirisha matatu na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), kutokana na kushindwa kutekeleza maamuzi ya migogoro ya kimkataba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Novemba 11, 2025, vilabu hivyo vimeadhibiwa kwa kukiuka taratibu za kimkataba, ikiwemo kukatisha mikataba bila sababu halali au kushindwa kutimiza wajibu wa kifedha kwa wachezaji na wafanyakazi wa zamani.

Rayon Sports ilijikuta katika orodha hiyo baada ya kukabiliwa na kesi mbili za kinidhamu mwezi Oktoba 2025. Kesi ya kwanza iliwasilishwa na kocha raia wa Brazil, Roberto Oliveira Gonçalves do Carmo, maarufu k**a Robertinho, aliyedai kufukuzwa kazi kinyume cha utaratibu na kutolipwa haki zake.

FIFA iliiamuru Rayon Sports kumlipa Robertinho kiasi cha Dola 22,500 (sawa na zaidi ya milioni 30 za Kitanzania), lakini klabu hiyo ilishindwa kufanya hivyo, jambo lililopelekea kufungiwa usajili wa madirisha matatu mfululizo.

Aidha, klabu hiyo inakabiliwa pia na kesi nyingine iliyowasilishwa na mshambuliaji kutoka Guinea-Bissau, Adulai Jalo, ambaye anadai stahiki zake.

Mbali na Rayon Sports, vilabu vingine vya Afrika vilivyopigwa marufuku na FIFA ni pamoja na Nyasa Bullets, KenGold SC, Township Rollers, AS Arta Solar7, Coton Sport de Garoua, TS Galaxy, Pretoria Callies, Welkite Kenema FC, SCCM, Ismaily SC, Zamalek, Enyimba FC, na Club Sportif Sfaxien.


12/11/2025

Waamuzi wawili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Amina Kyando kutoka Morogoro (mwamuzi wa kati) na Abdalah Bakenga kutoka Kigoma (mwamuzi msaidizi namba mbili), wameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kwa mizunguko mitano kutokana na makosa ya kiufundi kwenye mchezo wa Ligi Kuu kati ya Pamba Jiji FC na Singida Black Stars.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Bodi ya Ligi, waamuzi hao walishindwa kutafsiri kwa usahihi sheria za mpira wa miguu, ikiwemo tukio la kipa wa Singida Black Stars kudaka mpira akiwa nje ya eneo la penati, bila kuchukua hatua yoyote ya kinidhamu.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mbali na kosa hilo, waamuzi hao pia walionekana kutetereka na kutojiamini katika kutoa maamuzi sahihi wakati wa mchezo huo, ambao ulimalizika kwa matokeo ya sare ya 1-1 kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.


12/11/2025

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amefikishwa katika Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, kwa ajili ya kuendelea na usikilizwaji wa kesi yake ya uhaini.

Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea leo ambapo mashahidi wa upande wa mashtaka wanatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wao mbele ya Jaji anayesikiliza shauri hilo.

Ikumbukwe kuwa Jumatatu, Novemba 10, 2025, mahak**a ilielezwa kuwa Lissu hakufika mahak**ani kutokana na sababu za kiusalama, jambo lililopelekea kuahirishwa kwa shauri hilo hadi leo.


12/11/2025

Mkazi wa Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Elipidius Balthazar, amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kosa la ubakaji kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Mahak**a ya Wilaya ya Muleba, mshtakiwa alitenda kosa hilo mnamo Septemba 19, 2025, katika Kijiji cha Kabirizi, Wilaya ya Muleba, ambapo alimbaka mwanamke (jina limehifadhiwa) kinyume na kifungu cha sheria cha Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 k**a ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Baada ya tukio hilo, mshtakiwa alik**atwa na Jeshi la Polisi na kufikishwa Mahak**ani Oktoba 1, 2025 ambapo mashahidi kadhaa walitoa ushahidi uliothibitisha kosa hilo.

Hukumu hiyo imesomwa Novemba 10, 2025, mbele ya Mheshimiwa Hakimu Lilian Mwambeleko, ambaye alisema ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka ulikuwa thabiti na ulithibitisha bila shaka kuwa mshtakiwa ndiye aliyetekeleza kosa hilo.

Hakimu Mwambeleko alieleza kuwa adhabu hiyo imelenga kutoa fundisho kwa watu wengine wenye tabia k**a hiyo, sambamba na kutoa haki kwa waathirika wa vitendo vya ukatili wa kijinsia.


12/11/2025

Mke wa Rais wa kwanza wa Gabon, Sylvia Bongo, na mwanawe Noureddin Bongo Valentin, wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia katika kesi ya ufisadi mkubwa iliyokuwa ikisikilizwa jijini Libreville.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa Jumanne usiku, hukumu hiyo imetolewa bila wawili hao kuwepo mahak**ani. Mahak**a imewaamuru pia kulipa faini ya milioni 100 za CFA Francs (sawa na takriban pauni 135,000) k**a fidia ya uharibifu wa fedha za umma.

Aidha, Noureddin Bongo amepewa adhabu ya ziada ya kulipa CFA Francs trilioni 1.201, sawa na dola bilioni 1.6, k**a sehemu ya marejesho ya fedha zilizopotea katika serikali ya Gabon.

Sylvia na Noureddin ni miongoni mwa wanafamilia wa aliyekuwa Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba, waliok**atwa baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyomuondoa madarakani mwaka 2023, ambapo jeshi liliahidi kupambana na rushwa na uporaji wa mali za umma.


12/11/2025

Kocha maarufu wa soka duniani, Jose Mourinho, ameingia lawamani baada ya kudaiwa kuondoka bila kulipa bili ya hoteli yenye thamani ya pauni 656,000 (sawa na takribani shilingi bilioni 2.1 za Kitanzania) alipokuwa akiishi katika hoteli ya kifahari ya nyota tano mjini Istanbul, Uturuki.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uturuki, Mourinho alikaa katika Hoteli ya Four Seasons kando ya mto Bosphorus kwa muda wa miezi 16 akiwa kocha wa klabu ya Fenerbahce, kabla ya kufukuzwa kazi baada ya mechi sita tu mwanzoni mwa msimu wa 2025/26.

Kocha huyo Mreno mwenye umri wa miaka 62 alijiunga na Fenerbahce mwezi Juni 2024, muda mfupi baada ya kuachana na klabu ya Roma ya Italia, akiwa na matarajio makubwa ya kuipa mafanikio klabu hiyo ya Uturuki.

Hata hivyo, baada ya kufutwa kazi, taarifa zinasema Mourinho aliacha deni kubwa la hoteli hiyo ya kifahari, yenye huduma za spa, mabwawa ya kuogelea, na ukumbi wa mazoezi wa kisasa. Bado haijathibitishwa k**a klabu ya Fenerbahce au Mourinho mwenyewe atawajibika kulipa bili hiyo.

Inaelezwa kuwa Mourinho alipokea malipo ya kuondoka ya pauni milioni 7.7 kutoka Fenerbahce, jambo linaloibua maswali kuhusu kwa nini bado bili hiyo haijalipwa.

Tukio hili linakumbusha matukio ya awali ya maisha yake ya ukocha, hasa wakati akiwa Manchester United, ambapo aliishi kwa zaidi ya siku 895 katika Hoteli ya The Lowry jijini Manchester, na kujikusanyia bili ya zaidi ya pauni 537,000 bila kununua au kukodisha nyumba yoyote.


12/11/2025

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, ametoa pole kwa walipakodi, watumishi wa TRA na Watanzania wote walioathirika kutokana na changamoto zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 29, 2025.

Akiwa katika ziara ya kikazi kwenye mikoa ya kikodi Ilala na Kariakoo, CG Mwenda alizungumza na walipakodi pamoja na watumishi wa mamlaka hiyo, ambapo alisisitiza dhamira ya TRA kuendelea kutoa huduma bora, kuwajali walipakodi na kushughulikia changamoto wanazokutana nazo.

Amesema licha ya athari zilizowapata baadhi ya watumishi na uharibifu wa mali katika ofisi za TRA, mamlaka itaendelea kufanya kazi kwa weledi na kujituma ili kuhakikisha huduma kwa walipakodi haziathiriki.

“Sisi TRA kipaumbele chetu ni walipakodi na biashara zao. Tunataka kuhakikisha wako salama na biashara zao zinaendelea kukua. Natoa pole kwa wote waliopata changamoto na ninaahidi kuwa tutaendelea kuwa karibu nao na kuwasaidia kwa mujibu wa sheria,” alisema CG Mwenda.

Ameongeza kuwa katika maeneo ambayo ofisi za TRA zilipata changamoto, huduma zimeanza kutolewa k**a kawaida na walipakodi wamejulishwa kuhusu utaratibu wa kupata huduma hizo.

Kwa upande wake, Bw. Salim Virani, mmoja wa walipakodi kutoka Kariakoo jijini Dar es Salaam, alisema wamekuwa wakiridhishwa na huduma zinazotolewa na TRA na kupongeza uongozi huo kwa kujali wateja wake.


Address

S. L. P 2528
Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njaro Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njaro Media:

Share