Njaro Media

Njaro Media Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Njaro Media, Media/News Company, Dodoma.

Main Official page for | | Based on Sport | Entertainment

NJARO TV
WakaliwaUpdates
Tunazungumza Michezo na Burudani

SUBSCRIBE YOUTUBE YA NJARO MEDIA

27/07/2025

Katika ajali ya kusikitisha iliyotokea leo kwenye eneo la mteremko wa Mbembel, kati ya Nzovwe na Lyunga jijini Mbeya, lori lenye namba za usajili T 576 CAK pamoja na tela namba T 121 CAY, lililokuwa limebeba shehena ya mbolea limehusika kwenye ajali baada ya kushindwa kuhimili mfumo wa breki.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Ofisa Oparesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Mbeya, Gervas Fungamali, lori hilo liliteleza kwenye mteremko na kugonga magari kadhaa madogo, yakiwemo mabasi mawili ya abiria. Ajali hiyo imesababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine kadhaa.

Fungamali amesema kuwa kikosi cha uokoaji kiliweza kuutoa mwili wa marehemu kutoka eneo la tukio na kuwaokoa majeruhi, ambao idadi yao kamili itatangazwa baada ya taratibu za uhakiki kukamilika.

Tukio hili linaongeza wito kwa madereva na wamiliki wa magari makubwa kuhakikisha magari yao yanakuwa na mifumo bora ya breki, hasa wanapopita kwenye maeneo yenye miinuko mikali k**a ya Mbeya.


27/07/2025

Rais wa Kenya, Mheshimiwa William Ruto, amewahakikishia Wakenya kuwa mpango wa elimu bila malipo kwa shule za msingi na sekondari za umma utaendelea kutekelezwa k**a kawaida, licha ya sintofahamu iliyozuka hivi karibuni kuhusu uwezo wa serikali kugharamia mpango huo.

Akizungumza katika hafla ya kitaifa jijini Nairobi, Rais Ruto alisema kuwa elimu ni msingi wa maendeleo ya taifa na hakuna mwanafunzi anayepaswa kunyimwa haki ya kupata elimu kwa sababu ya changamoto za kifedha.

Kauli ya Rais Ruto imekuja kufuatia taharuki iliyotanda miongoni mwa wananchi baada ya Waziri wa Fedha, Bw. John Mbadi, kueleza kuwa hali ya kiuchumi ya taifa kwa sasa haitoshelezi kuendeleza mpango huo bila maboresho ya kibajeti. Tamko hilo lilisababisha maoni mseto kutoka kwa wananchi na viongozi wa kisiasa, wakihofia kusitishwa kwa elimu bila malipo.

“Serikali yangu imejikita katika kuwahudumia wananchi, na elimu ni kipaumbele cha kwanza. Tutahakikisha fedha zinapatikana ili wanafunzi waendelee kupata elimu bora bila malipo,” alisema Rais Ruto.

Serikali ya Kenya imekuwa ikiendesha mpango wa elimu bila malipo kwa zaidi ya miaka 20 sasa, ikiwa ni juhudi za kuhakikisha watoto wote wanapata fursa sawa ya kujifunza bila kubaguliwa kutokana na hali ya kipato.

Wazazi na walimu wametolea wito wa kuwepo kwa uwazi na maelezo ya kina kutoka kwa serikali ili kufafanua hatma ya mpango huo, huku wengi wakifurahia kauli ya Rais k**a faraja kwa familia zenye kipato cha chini.


27/07/2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeweka historia kwa kuandaa utaratibu utakaowawezesha wafungwa na mahabusu kushiriki katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu. Hii ni hatua ya kihistoria inayolenga kuhakikisha ushirikishwaji wa makundi yote ya kijamii katika mchakato wa kidemokrasia.

Akizungumza katika mkutano uliohusisha viongozi wa vyama vya siasa kuhusu maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, Mkurugenzi wa INEC, Ramadhani Kailima, alisema tume imefanikiwa kuandikisha wapiga kura katika vituo 140 vya magereza vilivyopo Tanzania Bara na vituo 10 vya vyuo vya mafunzo visiwani Zanzibar.

“Tumeimeweka mazingira rafiki kwa wafungwa na mahabusu kushiriki uchaguzi kwa mara ya kwanza nchini, ikiwa ni utekelezaji wa marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi ya Mwaka 2024, hasa vifungu vinavyohusu haki ya wapiga kura walioko katika mazingira ya kifungo kisichozidi miezi sita,” alifafanua Kailima.

Katika kuhakikisha haki ya kila raia inazingatiwa, tume imeandaa utaratibu maalum utakaowawezesha kundi hili muhimu kushiriki kikamilifu katika siku ya uchaguzi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amepongeza hatua hiyo ya INEC, akisema ni hatua kubwa katika kuimarisha demokrasia nchini. Aliongeza kuwa, kwa mara ya kwanza, vyama vya siasa vitapatiwa orodha ya wapiga kura wa nchi nzima kabla ya kuanza kampeni—a mbayo awali haikuwepo.

“Ni jambo la kupongezwa kuona haki za msingi za wafungwa zikizingatiwa na pia kuona uwazi unaongezeka katika mchakato wa uchaguzi,” alisema Prof. Lipumba.

Hatua hii ya INEC inaashiria mabadiliko chanya katika kuimarisha ushirikishwaji wa makundi mbalimbali ya jamii na kuendeleza misingi ya demokrasia jumuishi.


27/07/2025

Ndege ya Shirika la American Airlines, yenye nambari ya safari 3023, ilikumbwa na hitilafu ya magurudumu wakati ikijiandaa kuruka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Denver, Marekani. Ndege hiyo ilikuwa ikielekea Miami.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, ndani ya ndege hiyo kulikuwa na jumla ya abiria 173 pamoja na wahudumu 6 wa ndege. Wote waliokolewa salama licha ya tukio hilo kusababisha hofu kwa muda mfupi. Taarifa zinaeleza kuwa mtu mmoja alipata jeraha dogo na alihudumiwa mara moja.

Maafisa wa usalama wa anga wanaendelea kufanya uchunguzi kubaini chanzo halisi cha hitilafu hiyo ya kiufundi.


27/07/2025

Klabu ya Singida Black Stars imethibitisha rasmi kuagana na mshambuliaji wao hatari kutoka Ghana, Jonathan Sowah, ambaye sasa amejiunga na mabingwa wa kihistoria wa soka nchini, Simba SC.

Kupitia taarifa yao kwa umma, Singida BS imeeleza kuwa uhamisho huo umefanyika kwa misingi ya makubaliano maalum yaliyofikiwa kati ya pande zote mbili, yakihusisha pia ushirikiano wa karibu kati ya Mlezi wa Singida Black Stars na Rais wa Heshima wa Simba SC.

“Tunawataarifu mashabiki wetu na wadau wa soka kuwa tumeridhia kwa moyo mmoja mchezaji wetu Jonathan Sowah kujiunga rasmi na Simba SC kwa mkataba wa kudumu,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Aidha, klabu hiyo imemshukuru Sowah kwa mchango wake mkubwa alipokuwa akilitumikia kikosi cha Singida BS na kumtakia kila la heri katika safari yake mpya ndani ya klabu ya Simba SC.

Ujio wa Sowah unatajwa kuwa ni sehemu ya mipango ya Simba SC kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa mashindano ya ndani na kimataifa.


27/07/2025

Mahak**a ya Kijeshi nchini DRC imefungua mash*taka mazito dhidi ya Rais mstaafu Joseph Kabila, huku akituhumiwa kwa makosa ya uhaini, mauaji ya makusudi, mateso, na kusaidia kundi la waasi wa M23/AFC linalodhibiti maeneo mashariki mwa nchi hiyo.

Kabila, ambaye aliongoza taifa hilo kuanzia mwaka 2001 kufuatia kuuawa kwa baba yake Laurent-Désiré Kabila, hadi alipoachia madaraka mwaka 2019, anadaiwa kushiriki kwa njia ya siri katika kulisaidia kundi hilo la waasi lililoteka mji wa Goma mwezi Januari 2025.

Taarifa kutoka Mahak**a ya Kijeshi zinaeleza kuwa mash*taka hayo yamefunguliwa bila uwepo wake mahak**ani, jambo linaloibua maswali kuhusu mustakabali wake wa kisiasa na usalama wake binafsi.

Inaelezwa kuwa kurejea kwake Goma mwezi Mei mwaka huu — mji unaokaliwa kwa sasa na waasi wa M23 — kumezua hisia kali kutoka kwa Serikali ya Rais Félix Tshisekedi, ambaye anamtuhumu Kabila kuwa mhusika mkuu katika kuendeleza ushawishi wa kundi hilo.

Hadi sasa, Joseph Kabila hajatoa tamko lolote rasmi kuhusu tuhuma hizo zinazotishia kusababisha mtafaruku mkubwa wa kisiasa na kiusalama ndani ya taifa hilo lenye historia ya migogoro ya muda mrefu.


27/07/2025

Mpenzi wa msanii maarufu wa Bongo Fleva, Ibraah, Hafsa Massudi, amefunguka kwa hisia kupitia ukurasa wake wa Instagram kuhusu safari yao ya ndoa na ujio wa mtoto wao wa kwanza, akieleza jinsi walivyobarikiwa katika hatua hiyo muhimu ya maisha.

Katika ujumbe wake wa kuvutia, Hafsa alieleza kuwa baada ya kuwa pamoja kwa muda, Ibraah alimchumbia rasmi, naye akakubali kwa moyo mmoja. Walifunga ndoa mbele ya wazazi wao na kwa baraka za Mwenyezi Mungu, ambapo mara baada ya ndoa hiyo walipewa zawadi ya ujauzito wa mtoto wao wa kwanza.

"Baada ya kuwa pamoja kwa muda, ulipendekeza ndoa nami nikasema NDIO... Tulifunga ndoa mbele ya wazazi wetu na mbele ya Mwenyezi Mungu. Tazama Mwenyezi Mungu alivyo, ametubariki moja kwa moja na ujauzito baada ya Nikkah yetu… Tumebaki kumsubiri mtoto wetu," aliandika Hafsa kwa furaha, akimshukuru mumewe kwa upendo na uaminifu.

Ujumbe huo uliambatana na hashtag , ikiwa ni ishara ya matarajio ya familia yao kukamilika mwaka huu.

Wafuasi na mashabiki wa Ibraah wamelipokea tangazo hilo kwa pongezi nyingi mitandaoni, wakimtakia kila la heri katika safari ya kuwa mzazi.


27/07/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limemk**ata kijana anayetuhumiwa kwa matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha, Alex Thobias (23), maarufu kwa jina la Sanchez, mkulima na mkazi wa Mahita, Chamwino, Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, mtuhumiwa huyo alikuwa akisakwa kwa muda mrefu kutokana na kuhusishwa na matukio mbalimbali ya uhalifu, ikiwemo uporaji wa pikipiki. Mnamo Julai 26, 2025, majira ya asubuhi, alik**atwa akiwa amejificha kwenye nyumba ya mpenzi wake, Halima Bakari, mkazi wa Chamwino, baada ya kudaiwa kupora pikipiki eneo la Msamvu usiku wa Julai 25, 2025.

Polisi walifanikiwa kumfuatilia mtuhumiwa huyo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi waliotoa ushirikiano. Hata hivyo, baada ya kubaini amezingirwa na askari waliokuwa wamejihami, Alex alijaribu kutoroka kwa kuruka ukuta lakini alipigwa risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.

Mtuhumiwa alikimbizwa hospitalini kutokana na kuvuja damu nyingi lakini alifariki dunia alipofikishwa hospitali.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa vijana kujiepusha na vitendo vya kihalifu na badala yake kujituma katika kazi halali ili kujipatia kipato.


26/07/2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza rasmi kuwa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kwa mwaka 2025 utafanyika Jumatano ya Oktoba 29, 2025. Tangazo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu wa Mahak**a ya Rufani, Jacobs Mwambegele, leo Julai 26, 2025 katika mkutano uliofanyika jijini Dodoma.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Jaji Mwambegele alibainisha kuwa mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za uteuzi kwa wagombea wa nafasi ya urais na makamu wa rais utaanza rasmi Agosti 9 na kukamilika Agosti 27, 2025.

Uchaguzi huu utahusisha nafasi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano pamoja na madiwani kwa upande wa Tanzania Bara.

Tume imetoa wito kwa vyama vya siasa, wagombea na wananchi kwa ujumla kuheshimu ratiba iliyowekwa na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zote zitakazotolewa katika kipindi chote cha uchaguzi.

Kwa sasa, maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea ikiwa ni pamoja na uhakiki wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, utoaji wa elimu kwa umma kuhusu haki na wajibu wa wapiga kura, pamoja na maandalizi ya vifaa na rasilimali za uchaguzi.


26/07/2025

Katibu Mkuu wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu, amesema kuwa hadi sasa bado haijajulikana k**a Mwenyekiti wa chama hicho, Hashim Rungwe, atagombea tena urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 27, 2025, jijini Dodoma, mara baada ya uzinduzi wa ratiba rasmi ya Uchaguzi Mkuu, Mwalimu alieleza kuwa mchakato wa ndani ya chama unaendelea, na kwamba kwa sasa hawezi kutoa uhakika juu ya k**a Rungwe ataendelea kuwania nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa nchi kupitia tiketi ya CHAUMMA.

Salum Mwalimu aliongeza kuwa ndani ya saa 72 zijazo, chama kitaweka wazi ratiba rasmi ya mchakato wa uteuzi wa wagombea kwa nafasi mbalimbali kuelekea uchaguzi huo, ikiwa ni hatua ya kuhakikisha maandalizi ya kidemokrasia yanafanyika kwa uwazi na kufuata katiba ya chama.


26/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirika la Fedha na Ujenzi la Korea (Korea Infrastructure Finance Corporation - K-Finco), Dkt. Eun-Jae Lee, pamoja na ujumbe wake katika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodo


26/07/2025

Aliyekuwa Kocha Msaidizi na Mkurugenzi wa Ufundi wa Klabu ya Yanga SC, Abdulhamid Moalin, hatakuwa sehemu ya benchi la ufundi la mabingwa hao wa Ligi Kuu ya NBC kwa msimu wa 2024/26. Hii inafuatia kumalizika kwa mkataba wake na klabu hiyo, pamoja na uamuzi wake binafsi wa kutoendelea.

Moalin, ambaye alijiunga na Yanga akitokea KMC katikati ya msimu uliopita, amewasilisha rasmi uamuzi wake kwa uongozi wa Yanga wa kutosaini mkataba mpya. Uongozi wa Yanga umekubali ombi hilo, hasa baada ya Kocha Mkuu mpya, Romain Folz, kueleza nia ya kuwa na benchi lake la ufundi binafsi kwa msimu ujao.

Kwa mujibu wa taarifa, Moalin pamoja na aliyekuwa mchambuzi wa video wa Yanga, wanatarajiwa kujiunga na aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Sead Ramovic, katika klabu ya CR Belouizdad ya Algeria.

Endelea kufuatilia kwa taarifa zaidi kuhusu usajili, mabadiliko ya benchi la ufundi na maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.


Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njaro Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Njaro Media:

Share