choicefm_tz

choicefm_tz Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from choicefm_tz, Radio Station, Dodoma.

Kutoka kwenye ukurasa wa instagramu wa Mbunge mstaafu wa Nzega Vijijini, Dkt. Hamis Kigwangalla, ameandika maneno haya."...
31/05/2026

Kutoka kwenye ukurasa wa instagramu wa Mbunge mstaafu wa Nzega Vijijini, Dkt. Hamis Kigwangalla, ameandika maneno haya.

"Siasa ni muhimu sana.

Lakini taifa haliwezi kujengwa kwa siasa peke yake.

Taifa hujengwa na watu wanaolima, wanaozalisha, wanaowekeza, na Siasa ni muhimu sana.

Lakini taifa haliwezi kujengwa kwa siasa peke yake.

Taifa hujengwa na watu wanaolima, wanaozalisha, wanaowekeza, na wanaofungua biashara zinazotengeneza ajira halisi.

Wiki hii nimekuwa Kapunga Rice Project kusimamia mavuno ya mpunga katika moja ya miradi yetu.

Kila ninapokuwa mashambani ninaamini zaidi kuwa Tanzania ina uwezo mkubwa sana wa kuwa taifa tajiri - tukiamua kuwekeza kwa nguvu katika uzalishaji, teknolojia ya kilimo, viwanda vya kuongeza thamani ya mazao yetu, na masoko.

Nchi haiwezi kuwa na uchumi mkubwa ikiwa tunazalisha malighafi pekee bila kujenga biashara na mifumo inayounganisha shamba na chakula mezani.

Ndiyo maana pamoja na kilimo, tunaendelea pia kuwekeza kwenye biashara za chakula na value addition kupitia miradi k**a Kigwangalla’s Farm: Steaks & More. Ndoto ni kuwa na chain ya hizi outlets!

Nimepitia nyakati tofauti katika uongozi wa umma, nimejifunza mengi, ila jambo moja muhimu ni kuwa:

Mijadala ya mitandaoni hupita. Lakini kazi hubaki.

Uchumi wa taifa hujengwa na kazi. Na heshima ya taifa pia hujengwa na kazi.

Tuendelee kujenga.

Kazi iendelee kuongea."

Wapiga Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge ...
31/05/2026

Wapiga Kura 222,218 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki kwenye uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Isimani lililopo Halamashauri ya Wilaya ya Iringa Mkoani Iringa na Kata 12 za Tanzania Bara.
------
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Mei 31, 2026 Mkoani Iringa wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Juni 01, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 628 vya Kupigia Kura vitatumika.
--------
“wapiga kura 89,753 wapo kwenye Jimbo la Ismani na wapiga kura 132,465 wapo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo na vituo 277 vipo kwenye Jimbo la Ismani na vituo 351 vipo kwenye kata 12 zitakazofanya uchaguzi mdogo.,”amesema Jaji Mwambegele.
--------
Aidha, amesema Katika Uchaguzi huu, jumla ya wagombea 108 kutoka katika vyama vya siasa 17 wanawania nafasi wazi ya ubunge na udiwani katika maeneo niliyoyataja.
------
“Jimbo la Ismani lina wagombea 17 wa nafasi ya Ubunge ambapo kati ya wagombea hao wagombea nane (08) sawa na asilimia 47.06 ni wanaume na wagombea tisa (09) sawa na asilimia 52.94 ni wanawake. Kata 12 zinazofanya uchaguzi mdogo wa udiwani zina jumla ya wagombea 91 ambapo kati ya hao wagombea 61 sawa na asilimia 67.03 ni wanaume na wagombea 30 sawa na asilimia 32.97 ni wanawake.” alisema Jaji Mwambegele.
------
“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Juni 01, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.
----
Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.
-----
Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, k**a wapiga kura bado wapo

Picha ya pre season kwa ajili ya msimu ujao 2026/2027 imevuja, kiungo fundi wa boli "Khalid Aucho" amerejea Yanga...
31/05/2026

Picha ya pre season kwa ajili ya msimu ujao 2026/2027 imevuja, kiungo fundi wa boli "Khalid Aucho" amerejea Yanga...

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza watumishi waliohusishwa na ubadhirifu wa zaidi ya shilingi milioni 500 katik...
30/05/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza watumishi waliohusishwa na ubadhirifu wa zaidi ya shilingi milioni 500 katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni watafutwe popote walipo, wak**atwe na kuchukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu huku fedha hizo zikirejeshwa serikalini.
----------
"Wamechota fedha za wananchi. Watafutwe hata ambao walishahamishwa, popote walipo wak**atwe, wawekwe ndani na fedha za Serikali zirudi. Hii si fedha ya mtu binafsi, ni fedha ya wananchi," alisema Dkt. Mwigulu.
--------
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo leo Jumamosi Mei 30, 2026 alipozungumza na wananchi wa Wilaya ya Manyoni katika Viwanja vya Tambukareli mkoani Singida akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.
---------
Alisema taarifa alizopokea zinaonesha kuwa jumla ya zaidi ya shilingi milioni 501 zilichotwa kutoka akaunti mbalimbali za halmashauri ikiwemo Akaunti ya Maendeleo (zaidi ya shilingi milioni 213), Akaunti ya Amana (zaidi ya shilingi milioni 259) na Akaunti ya Mapato ya Ndani (zaidi ya shilingi milioni 42), jambo ambalo haliwezi kuvumiliwa na Serikali.
---------
Waziri Mkuu aliwataja watumishi wanaodaiwa kuhusika katika ubadhirifu huo kuwa ni aliyekuwa Mweka Hazina wa Halmashauri hiyo Mwakapala, ambaye kwa sasa amehamishiwa mkoani Songwe, Mhasibu wa Mapato Edward Kilungu na Eliamini Maliki.
--------
Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida (RPC) kuhakikisha watumishi hao wanatafutwa, wanak**atwa na kuwekwa mahabusu hadi fedha za Serikali zitakapopatikana.
-------
"Mweka Hazina Mwakapala arudishwe, Edward Kilungu na Eliamini Maliki watafutwe. Wak**atwe, wawekwe ndani na wasitoke mpaka fedha ya Serikali irudi," alisema Dkt. Mwigulu.
-------
Aidha, Waziri Mkuu alimuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kuhakikisha watumishi wote waliohusika wanasimamishwa kazi mara moja huku taratibu za kinidhamu na kisheria zikiendelea.

Wabunge wakiwa Bungeni Jijini Dodoma kwa kushiriki kikao cha thelathini na tisa, mkutano wa tatu, Bunge la kumi na tatu ...
29/05/2026

Wabunge wakiwa Bungeni Jijini Dodoma kwa kushiriki kikao cha thelathini na tisa, mkutano wa tatu, Bunge la kumi na tatu leo Mei 29.2026.
--------
Mkutano wa tatu wa Bunge ni mahususi kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa bajeti za wizara zote kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wa makadirio ya mapato na matumizi ya serikali kwa huuwa fedha.

Serikali imeeleza dhamira yake ya kumaliza kabisa changamoto za huduma za mawasiliano nchini ifikapo mwaka 2030 kupitia ...
25/05/2026

Serikali imeeleza dhamira yake ya kumaliza kabisa changamoto za huduma za mawasiliano nchini ifikapo mwaka 2030 kupitia Mpango Mkakati wa Miaka Mitano wa 2025–2030 unaotekelezwa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
----------
Kauli hiyo imetolewa leo Mei 25, 2026, Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Dkt. Switbert Zacharia Mk**a (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Korogwe Vijijini, Mhe. Timotheo Paul Mnzava, kuhusu lini Serikali itatatua changamoto ya ukosefu wa huduma za mawasiliano ya simu katika Kata ya Kalalani.
---------
Naibu Waziri Mk**a amesema Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) tayari imefanya tathmini ya hali ya mawasiliano katika vijiji vya Mtoni Bombo na Kalalani. Amesema kijiji cha Mtoni Bombo kimebainika kuwa na changamoto kubwa ya huduma za mawasiliano, huku kijiji cha Kalalani, licha ya kuwa na minara miwili inayohudumiwa na kampuni tatu za simu, bado kinakabiliwa na changamoto ya huduma duni kutokana na ukubwa wa eneo hilo na shughuli nyingi za kiuchumi, ikiwemo uchimbaji wa madini.
--------
Aidha, Serikali kupitia UCSAF imeahidi kujumuisha vijiji vya Mtoni Bombo na Kalalani katika bajeti ya ujenzi wa minara ya mawasiliano kwa mwaka wa fedha 2026/2027 ili kuboresha huduma kwa wananchi.
-------
Akijibu swali la nyongeza kuhusu kuharakishwa kwa utatuzi wa changamoto hiyo, Mhe. Dkt. Mk**a ameielekeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufanya tathmini ya kina ya huduma za mawasiliano katika kata hiyo, sambamba na kuwataka watoa huduma za simu kuongeza nguvu ya minara iliyopo ili kuboresha upatikanaji wa huduma za mawasiliano.

"Nimefikiri na kutafakari kwa muda mrefu baada ya matukio ya ukiukwaji wa haki, utu na dhuluma dhidi ya uhai wa binadamu...
24/05/2026

"Nimefikiri na kutafakari kwa muda mrefu baada ya matukio ya ukiukwaji wa haki, utu na dhuluma dhidi ya uhai wa binadamu yaliyotokea tarehe 29 Oktoba 2025. Siwezi kuendelea kuishi katika huzuni na ukimya tena.

Kwa dhamira yangu binafsi, leo nimejiondoa rasmi kutoka CCM na kurejea CHADEMA kwa kufuata taratibu zote za CHADEMA.

Kwa Watanzania wote, na wanachama wa CHADEMA wale walioumizwa au kukatishwa tamaa na msimamo wangu wa awali, naomba radhi kwa dhati pale nilipokuwa kinyume na matarajio yetu ya pamoja katika safari ya kutafuta haki, utu na demokrasia ya kweli.

Naam, binadamu hukosea, lakini dhamira inapozinduka ni wajibu kusimama upande unaouona kuwa wa kweli na wa haki.

Asanteni Sana."

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, leo Mei 22, 202...
23/05/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, leo Mei 22, 2026 jijini Arusha ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Mawaziri kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
-----------
Mkutano huo ni hatua muhimu ya maandalizi ya Bajeti ya Jumuiya hiyo kabla ya kuwasilishwa katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kwa ajili ya kujadiliwa na kuidhinishwa kabla ya Juni 30, 2026.
----------
Katika mkutano huo, Mhe. Ridhiwani Kikwete aliambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki, Cde. James Millya; Naibu Waziri wa Fedha Cde.
----------
Mshamu Ali Munde; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu M***a; pamoja na maafisa wengine waandamizi wa Serikali.
---------
Aidha, katika Mkutano huo wamejadili mipango ya kibajeti ya Taasisi mbalimbali ikiwemo Mahak**a ya Haki ya Afrika Mashariki, Bunge la Afrika Mashariki, Taasisi ya Bonde la Ziwa Victoria na Nyenginezo.

Mchezaji wa zamani wa klabu ya  Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza (Kitasa) Rio Ferdinand, amewasili katika...
20/05/2026

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza (Kitasa) Rio Ferdinand, amewasili katika viunga vya Bunge Jijini Dodoma akiwa sambamba na mwenyeji wake Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda (MB), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) pamoja na baadhi ya Wabunge la Tanzania.
-----------
Ujio wa Rio Tanzania ukiwa ni kuchechemuwa mbio za kuelekea kwenye AFCON 2027 pamoja na kuitangaza Tanzania kupitia michezo na Utalii kwa kutembeea hifadhi taifa ya Serengeti.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho (Mb), akiwa anawasilisha hotuba ya bajeti ya maka...
19/05/2026

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho (Mb), akiwa anawasilisha hotuba ya bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2026/2027 amesema katika mwaka wa Fedha 2026/2027, Serikali inatarajia kutenga fedha kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Maendeleo jumla ya Shilingi 4,286,489,324,427.00 ambapo kati ya fedha hizo, Shilingi 3,859,955,671,427.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida, na Shilingi 426,533,653,000.00 ni kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo.
-----------
Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, amesema kati ya Fedha hizo, NGOME linatarajia kutengewa Shilingi 3,198,126,934,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 54,867,636,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo. Fungu 39 - JKT linatarajia kutengewa Shilingi 626,273,760,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 19,929,926,000.00 kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo.

Address

Dodoma
255

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when choicefm_tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category