TAG Online TV

TAG Online TV Today in Church | Interview | Documentary | Talk Show | Bishop Speech | Gospel | Teaching | Reels | Qoutes | Gospel Tour | Worship Events.

🔥 IBADA HII ITAKUWA MUBASHARA KUTOKEA DODOMA! 🔥Kuanzia saa 1:30 usiku ya leo, ibada hii itakuwa mubashara kutoka hapa Do...
18/08/2026

🔥 IBADA HII ITAKUWA MUBASHARA KUTOKEA DODOMA! 🔥

Kuanzia saa 1:30 usiku ya leo, ibada hii itakuwa mubashara kutoka hapa Dodoma. 🙏

Usikose kushuhudia kile ambacho Mungu amekiandaa!

👉 Nenda kwenye YouTube channel yetu, bonyeza Subscribe, kisha jiandae kuungana nasi na kuhudumiwa na Mungu kupitia ibada hii.

Usikose! Mungu akubariki. 🔥🙏

ASSEMBLIES OF GOD GHANA KUELEKEA BARAZA KUU LA 32Msimamizi Mkuu wa Assemblies of God Ghana, Mchungaji Stephen Wengam, an...
18/08/2026

ASSEMBLIES OF GOD GHANA KUELEKEA BARAZA KUU LA 32

Msimamizi Mkuu wa Assemblies of God Ghana, Mchungaji Stephen Wengam, anatarajiwa kuliongoza Baraza Kuu la 32 la Assemblies of God Ghana, ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili.

Baraza hilo linatarajiwa kuanza kesho, huku maandalizi ya kuhakikisha linafanyika kwa mafanikio yakiwa yamekamilika kwa kiasi kikubwa.

Baadhi ya wajumbe tayari wamewasili na wameanza zoezi la usajili, huku maandalizi mengine yakiendelea katika eneo la mkutano.

Mchungaji Stephen Wengam — Msimamizi Mkuu na Mwenyeji wa Baraza Kuu la 32 la Assemblies of God Ghana.

18/08/2026



CREW:

Mungu amefanya jambo jingine kubwa kwa kanisa lake.
18/08/2026

Mungu amefanya jambo jingine kubwa kwa kanisa lake.

18/08/2026

MIKATE MAALUM YA MEZA YA BWANA SASA YAZALISHWA NA RPH

Mikate maalum kwa ajili ya Meza ya Bwana (Sakramenti), inayozalishwa na kitengo cha Printing RPH (Revival Printing House) chini ya Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), imewekwa rasmi wakfu na Askofu Mkuu wa TAG, Askofu Barnabas W. Mtokambali.

Hatua hii inaifanya TAG kuanza rasmi kuzalisha mikate hiyo kupitia kiwanda chake, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kanisa katika kujenga uwezo wa ndani na kuwa na mifumo yake ya uzalishaji.

Ni hatua nyingine ya maendeleo na uwekezaji ndani ya TAG. Utukufu wote ni wa Mungu! 🙏

18/08/2026

ASKOFU MTOKAMBALI AWATAKA WAJUMBE KULIOMBEA TAIFA

Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God (TAG), Barnabas Mtokambali, amewataka wajumbe wa Mkutano Mkuu kuliombea taifa ili liendelee kuwa na amani, haki, umoja na utulivu.

Akizungumza katika siku ya kwanza ya Mkutano Mkuu unaoendelea Makao Makuu ya TAG, Miyuji jijini Dodoma, Askofu Mtokambali amesisitiza umuhimu wa kanisa kuendelea kusimama katika maombi kwa ajili ya taifa.

Aidha, amewataka wajumbe kutokutazama sana walikotoka, bali kuelekeza nguvu zao katika yale yaliyo mbele yao na katika kusudi ambalo Mungu ameliweka mbele ya kanisa.

“Tusitazame tulikotoka, bali tuangalie tunakoelekea.” 🙏🇹🇿

18/08/2026

ASKOFU MKUU ATOA WITO WA UMOJA NA UNYENYEKEVU NDANI YA KANISA

Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God, Barnabas Mtokambali, amehimiza umuhimu wa umoja ndani ya kanisa pamoja na kuwa na moyo wa unyenyekevu katika hotuba yake aliyoitoa leo, ikiwa ni siku ya kwanza ya Mkutano Mkuu wa TAG.

Mkutano huo umeanza mapema leo katika Makao Makuu ya Tanzania Assemblies of God (TAG), Miyuji jijini Dodoma, ndani ya Central Bible College (CBC).

Katika hotuba yake, Askofu Mkuu amesisitiza kwamba umoja na unyenyekevu ni misingi muhimu katika kujenga kanisa lenye nguvu, lenye mshikamano na linaloweza kutimiza kwa ufanisi wito na kusudi ambalo Mungu amelipatia.

Mkutano Mkuu umeanza rasmi—na ujumbe wa siku ya kwanza ni: TUDUMISHE UMOJA, TUISHI KWA UNYENYEKEVU. 🙏🔥

 CREW:
18/08/2026



CREW:

18/08/2026

Ni takribani miezi mitatu sasa tangu General Superintendent wa Assemblies of God, Ghana, Rev. Stephen Yenusum Wengam, akiambatana na Regional Superintendent wa Assemblies of God, Greater Accra East Region, Rev. Andrews N. Awintia, wazindue rasmi ofisi mpya na ya kisasa ya kanda hiyo.

Tazama jengo hili la kuvutia pamoja na mpangilio mzuri wa ofisi zake kwa ndani. Ni picha inayodhihirisha namna ambavyo Assemblies of God inavyoendelea kuchukua sura mpya katika maeneo mbalimbali duniani, hasa katika kipindi hiki ambacho kuna muamko mkubwa wa maendeleo ya kanisa barani Afrika.

Kanisa linakua si kwa idadi ya waamini pekee, bali pia katika miundombinu, uwekezaji, mifumo ya uongozi na mazingira ya utendaji. Hii ni sehemu ya picha kubwa ya kile kinachoendelea ndani ya Assemblies of God katika bara la Afrika na duniani kwa ujumla.

Hata Tanzania, miaka kadhaa iliyopita, kulikuwa na maono ya kuanzisha mji wa Tanzania Assemblies of God, ambao kwa mujibu wa maono hayo unatarajiwa kuwa na ofisi za kanisa pamoja na mlima mkubwa wa maombi, ambao ungekuwa sehemu ya kipekee ya ibada na maombi kwa watu kutoka Tanzania na mataifa mbalimbali.

Ukiachilia mbali hayo, pia tunaweza kuona uwekezaji katika ofisi za kisasa zinazotumiwa na kanisa, ikiwemo mazingira ya CBC hapa Miyuji, yanayoonyesha namna miundombinu inavyoweza kwenda sambamba na ukuaji wa huduma na elimu ya Biblia.

Kwa kweli, ukiyaangalia yote haya kwa pamoja, unaanza kuona picha kubwa ya Assemblies of God duniani—kanisa linalojenga, linawekeza, linapanua mifumo yake na kutumia kila fursa iliyopo ili kuendeleza kazi ya Injili.

Maono makubwa yanahitaji miundombinu mikubwa. Na kanisa linapowekeza katika mazingira ya huduma, elimu, uongozi na maombi, linakuwa linaandaa msingi wa kizazi kijacho.

Hili ni zaidi ya jengo; ni picha ya maono yanapogeuka kuwa uhalisia.

Kanisa la Assemblies of God Philipine wako kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuelekea kwenye Kongamano la Ishara na Maa...
18/08/2026

Kanisa la Assemblies of God Philipine wako kwenye maandalizi ya mwisho mwisho kuelekea kwenye Kongamano la Ishara na Maajabu (Signs & Wonders Conference) la mwaka 2026 ikiwa ni sehemu ya mkutano wao mkuu wa kanisa hilo.

📅 Agosti 25–28, 2026
📍 Word of Hope Church Central

Address

Mbwanga
Dodoma
41000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAG Online TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share