04/05/2018
Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani:
Mengi yanapita, yamezungumzwa na kimsingi yanagusa tasnia ya vyombo vya habari katika kipindi cha muongo mmoja unaoelekea mwisho. Ndani yake kuna mazuri mengi yasiyopewa fursa na mabaya mengi yanayopigiwa kelele. Yapo yanayopewa fursa kubwa kwenye kurasa za mwanzo za magazeti ya Tanzania na yale ya nje. Tukiacha yote haya hili limezidi au kutiwa chumvi au kupuuzwa, au kutelekezwa! Eti wanahabari wanafanya kazi kwa uoga, wanatishwa, wanak**atwa, wanayanyaswa, wanauawa, wanatekwa na kupotea katika mazingira ya kutatanisha katika Tanzania hii hii ya leo! Kwanini kuituhumu Serikali? Kwa nini kuwatuhumu watu wasioonekana? Je siyo kazi ya wanahabari kufanya uchunguzi? Kwanini wanaibebesha Serikali jukumu la kuwak**ata wahalifu ambao hawajulikani? Hayo na maswali mengine mengi yaliuteka ukumbi wa mikutano wa Morena Hoteli Jijini Dodoma katika siku mbili za Mei 2 na 3 zilizowakutanisha wanahabari na wadau wa sekta hiyo nchi nzima katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani. Walioshiriki ni pamoja na taasisi za wahisani ikiwemo Friedrick Ebert Stiftung (FES), Shirika la Elimu na Sayansi la Umoja wa Matifa (UNESCO), Irish Aid, UN Tanzania, Jumuiya ya Ulaya (EU) na Serikali ya Tanzania. Mashirika mengine yaliyoshiriki ni MISA-Tanzania, MCT, TMF, TAMWA, MOAT, UNIC Dar Es Salaam, TEF, ARUPA, UTPC, Jamii Forum na Dodoma Media College. Walikuwepo pia wazee maarufu maarufu k**a Veterans wa fani ya Uandishi wa Habari. Shughuli hii ilifunguliwa rasmi na Spika wa Bunge la Tanzania -Mh Job Ndugai na kufungwa ramsi na Dr Harrison Mwakyembe, Waziri wa Habari, Utamaduni, Michazo na Sanaa. Kati ya mengi yaliyopewa kipaumbele ni haki za binadamu, haki za watoto na wanawake, maslahi ya wanahabari (mishahara mizuri inayotolewa kwa wakati, bima ya afya, bima ya ajali, pensheni na mazingira bora ya kufanya kazi na kuhakikishiwa vitendea kazi). ARUPA iliibuka na jambo moja kubwa kuwa kila mwandishi awe mlinzi wake mwenyewe. Hakuna habari kubwa kuliko maisha ya mwandishi. Mwandishi azingatie maadili na taaluma yake ili kuepukana na hatari zisizo za lazima. Kauli mbiu:Kudhibiti Utawala: habari, Haki na Kuzingatia Utawala bora wa Kisheria. Kwa habari zaidi soma Twitter Tag: WorldPressFreedomDAY Soma pia: https://www.youtube.comwatch?v=-MP6fBO0&feature=youtu.be Angalia pia: https://www.youtube.com/watch?v=fDrp-UJ2bfo